The Rise and Fall of Augustine Lyatonga Mrema

Mkuu jmushi1,

1.Tukianza na mapambano dhidi ya ufisadi, hebu nitajie kimojawapo tu ya mafanikio ya Augostine Lyatonga Mrema.
2. Tukirudi kwenye harakati za mageuzi nitajie angalau moja alilolifanya A. L. Mrema kufanikisha hayo mageuzi.

Mimi nimesema nina makovu ya marungu ya polisi dhidi ya wanamageuzi kati ya 1991 mpaka 1994 wakiongozwa na Mrema. Wakati Mrema anadandia hiyo meli, mageuzi yalishapatikana na vyama vya kumsetiri asibaki uchi alipoihama CCM vilishakuwapo. Na hapa naomba usiingize ukabila kwa sababu ni njia ya kukosa hoja.

Alipokuwa mbunge alipigania maslahi ya wanyonge na pia mazao ya biashara kama kahawa nk.
Alipokuwa waziri wa mambo ya ndani pia alisolve matatizo mengi sana ya ujambazi na kwa kweli majambazi walijuwa Mrema si wa kuchezewa.
Issue za mirathi, haki za wanawake nk. Alishapata pia kuwa waziri wa vijana kama sijakosea...Naomba kuwa corrected.
Alikuwa akisimamisha shilingi kila mara ilipobidi na hakuwa na damu ya kifisadi hilo lilimfanya kuonekana mwana ccm wa tofauti sana na ndio maana hata akapewa uwaziri na mwinyi.
Wapi nimeingiza ukabila na wapi nimekosa hoja?
 
Mushi,

Unaweza kuwa na kumbukumbu nzuri ya 'mazuri' aliyoyafanya Mrema. Naomba unikumbushe zile Dhahabu za kina Naoushad Mohamed walizokamatwa nazo pale Airport ishu ile iliishia wapi? Maana tuliambiwa Mrema aliwaambia wale Watuhumiwa wamfuate Kiraracha na baada ya hapo hatukusikia tena zaidi ya kwaona kina Mohamed wakipeta Mitaani! Nakubaliana Mrema alifanya mengi makubwa katika serikali ile ya awamu ya pili lakini naye HAKUWA msafi sana...... alikuwa ni Mzee wa Madili yule kwa sasa angeitwa FISADI.

Mimi bado naamini Mrema aliondoka CCM sio kwa kutumwa kama wengi wanavyotaka tuamini. Mrema aliondoka CCM kwa HASIRA baada ya kujua JAMAA wamempiga chini kugombea Urais (ambao aliona hakuna mtu wa kumzuia kwa Umaarufu aliokuwa nao wakati ule) baada ya kuweka kipengele cha Digrii kwenye katiba ya CCM kwa wagombea Urais! Alipoona hivyo ndipo alipoamua kuwa Mzee wa Mabomu kila kukicha anapasua Bomu! Ndipo Rais Mwinyi akamvua Uwaziri kama alivyosema yeye mwenyewe kwa kukosa 'collective responsibility'

Kwa siasa za Tanzania SITASHANGAA kusikia Mrema karudi CCM kwani wapo wengi walisharudi huko! Yuko wapo Lamwai? Yuko wapi Ngawaiya? Yuko wapi Njelu Kasaka? Yuko wapi Ndembela Ngunangwa, yuko wapi Stephen Wassira, ukiacha wale 'wapuuzi' wengine kama kina Hizaa Tambwe na kina Msabaha! Kwa siasa za Tanzania kuwa Mpinzani inahitaji 'msuli' wa nguvu! Wapo viongozi wakubwa kabisa wa Serikali walishatamka hadharani kwamba ukiwa mfanyabiashara ukitaka kufanikiwa ni lazima uwe shabiki/mkereketwa/mwanachama wa CCM. Inawezekana kabisa kwa sasa Mrema anapita kwenye kipindi kigumu cha maisha! Ukizingatia Chama chake hakina au kinaweza kuwa kinapata ruzuku kidogo sana kutoka serikalini. Sidhani kama TLP ina vyanzo vingine vya fedha ili KIJIENDESHE ikiwemo kuwalipa mishahara watendaji wake. NJAA kwa kawaida huwa haina ADABU! Mrema kwa sasa ana NJAA! Kwa njaa yake aliyonayo ni rahisi sana kutumiwa na MAFISADI ili ikifika jioni wawe wamekamilisha malengo yao! Na yeye angalau awe AMESHIBA! Tusubiri tuone maneno aliyoyasema yule Muheshimiwa kuhusu Mrema si ya KUPUUZWA ila tusubiri tu!

Nawakilisha

Nakubaliana na wewe kiasi kikubwa isipokuwa kwenye highlights...Hiyo pointi ya njaa ni pointi ninayotakiwa kuitumia mimi na si wale wanaompinga Mrema.
Kama kweli ana njaa basi si kwasababu hakutaka kujisihibisha mwenyewe...Ni mtu shupavu. Kama unazungumzia njaa ya chakula then hayo ni madharau kwasababu sidhani kama Mrema ana njaa ya chakula. Kwanza ni diabetic na hivyo mlo wake ni wa kuangaliwa...Labda ulimaanisha pesa...Sasa kama ni pesa si alizikimbia za ufisadi ccm?
Mrema akirudi ccm ni kwakuwa watanzania walio wengi hususan wa upinzani wamemkosea fadhila.
 
Augustine Mrema kuwagawa CHADEMA na CUF na kuibukia CCM



Na kiongozi mmoja wa NCCR alithibitisha kuwa fedha za kampeni walikuwa wakichukua kutoka kwa Makamba.


Sasa baada ya NCCR kuonekana imechafuka sana, sasa umepangwa mkakati mwingine wa kuitumia TLP PM

Paparazi muwazi, nasikitika kwamba umejitumbukiza katika kazi iliyolaaniwa ya uchonganishi na uenezi wa uongo, nakushauri uiache maana uongo asili yake ni kuzimu na baba wa uongo ni ibilisi mwenyewe.
Aidha upaparazi wako unazidi kukosa viwango, pole sana.
 
Paparazi muwazi, nasikitika kwamba umejitumbukiza katika kazi iliyolaaniwa ya uchonganishi na uenezi wa uongo, nakushauri uiache maana uongo asili yake ni kuzimu na baba wa uongo ni ibilisi mwenyewe.
Aidha upaparazi wako unazidi kukosa viwango, pole sana.

waridi, na wewe mbona hujamwaga hapa zile issue?
 
Jmushi,
Inawezekana kabisa mimi siijui historia ya Tanzania kama unavyodai.Lakini naomba ukubaliane na mimi kuwa ukisema kuwa Mrema halikuwa hawapi watu aliowaita yeye jina la waharifu wamfuate kwake huko kiraracha inaonyesha ni jinsi gani unavyoijua hitoria ya Tanzania.

Sijui vizuri mambo ya uhalifu na intelligencia unayodai wewe unaifahamu kwa kiasi gani.Naomba usichanganye mambo tafadhali.Wakati wa ujambazi kipindi cha Mrema na wakati wa ujambazi wa mchana kweupe mara tu JK alipoingia madarakani.Ni vitu viwili tofauti kabisa.kimsingi Mrema alionyesha kiwango kidogo sana cha kuimudu wizara ya Mambo ya ndani ukilinganisha na wote waliowahi kushika wizara hiyo.Mrema alikuwa bingwa wa kukurupuka.HUWEZI NA NASISITIZA HUWEZI kukurupuka wakati wa ujambazi kama ule na kuanzisha sungusungu isiyo na kichwa wala miguu.Tuliona sungu sungu ikiishia kuwatesa raia wasio na hatia kwa vile wote waliokuwa wanalinda sungusungu hawakuwa na ama taaluma ya Ulinzi au mbinu za kiupelelezi.Wapi na wapi utamlinda jambazi wa SMG acha gobore kwa fimbo ya mpera????
Jiulize unafikiri mrema angekuwa waziri kipindi kile majambazi wanaiba hela za NMB pale ubungo kweupe angefanya nini.Si angesema hadi mashule yafungwe na wote tuwe walinzi wa sungu sungu na wanafunzi wa shule??

Ni kipindi hichohicho cha Mrema akiwa Waziri Mambo ya ndani ndo nilikona wanawake/kina mama wanaenda kushitaki kwake juu ya matatizo ya ndoa zao.Je unataka kuniambia yeye alikuwa ndo ustawi wa Jamii????Ina maana hakuona mahakama??Na bado kina baba walipatiwa shida na huyu bwana kisa Waziri maarufu mrema kasema.Ukiwa waziri kuna mipaka yako kiutendaji.Siyo kukurupuka tu na kushughulikia kila kitu.Namjua Mrema zaidi ya unavyoweza kuhisi.Ungekuwa na simu yake ningekwambia umpigie simu na umuulizie jina langu kama utataka niku-PM na umwambie mwaka 1995 tulimsaidia vipi yeye na Kamara Kasupya pale Dodoma.Lakini baada ya kumuona kuwa ni "ZIGO" niliachana nae mara moja.

Mrema ni mkurupukaji,mpenda sifa,hasiye shaurika na hasiye na mbinu wala strategy zozote zile.Kama unakumbuka unaweza kunambia kwenye mdahalo wa wagombea Urais 1995 alifanya madudu gani mbali na kuonyesha jamii ana hasira na uchu wa madaraka kiasi gani.Mrema huyu alikuwa anashauriwa na kuongozwa na wanamipango wa NCCR ili aseme nini kwenye makongamano lakini yeye kila mara alikuwa anakuja na mahadithi yake yasiyo na kichwa wala miguu kitu kilichomfanya ashindwe vibaya sana kwenye uchaguzi.Alihamia NCCR kikiwa na nguvu na akatoka kikiwa hakina nguvu.Kila anakoenda ni matatizo tuu kwa hoja dhaifu utasema aliandamwa na CCM,wewe unataka CCM wafanye nini??Wamwachie tu bila kumdhibiti??unajua siasa kweli wewe??Mbona Mbowe anaandamwa na CCM na hao kina Mtikila lakini Chadema kiasi inazidi kung'aa???Unafikiri mrema angekuwa ndo ZITTO wakati anasimamishwa ubunge ingekuwaje,si angefia hukohuko kabisa?? Lakini mbona dogo zitto mbali na kuandamwa lakini anafanya vizuri????

Mimi kwangu Mrema plus Mtikila ni sawa na uji na mgonjwa hasiye na meno.
Avache
 
Jmushi,
Inawezekana kabisa mimi siijui historia ya Tanzania kama unavyodai.Lakini naomba ukubaliane na mimi kuwa ukisema kuwa Mrema halikuwa hawapi watu aliowaita yeye jina la waharifu wamfuate kwake huko kiraracha inaonyesha ni jinsi gani unavyoijua hitoria ya Tanzania.

Sijui vizuri mambo ya uhalifu na intelligencia unayodai wewe unaifahamu kwa kiasi gani.Naomba usichanganye mambo tafadhali.Wakati wa ujambazi kipindi cha Mrema na wakati wa ujambazi wa mchana kweupe mara tu JK alipoingia madarakani.Ni vitu viwili tofauti kabisa.kimsingi Mrema alionyesha kiwango kidogo sana cha kuimudu wizara ya Mambo ya ndani ukilinganisha na wote waliowahi kushika wizara hiyo.Mrema alikuwa bingwa wa kukurupuka.HUWEZI NA NASISITIZA HUWEZI kukurupuka wakati wa ujambazi kama ule na kuanzisha sungusungu isiyo na kichwa wala miguu.Tuliona sungu sungu ikiishia kuwatesa raia wasio na hatia kwa vile wote waliokuwa wanalinda sungusungu hawakuwa na ama taaluma ya Ulinzi au mbinu za kiupelelezi.Wapi na wapi utamlinda jambazi wa SMG acha gobore kwa fimbo ya mpera????
Jiulize unafikiri mrema angekuwa waziri kipindi kile majambazi wanaiba hela za NMB pale ubungo kweupe angefanya nini.Si angesema hadi mashule yafungwe na wote tuwe walinzi wa sungu sungu na wanafunzi wa shule??

Ni kipindi hichohicho cha Mrema akiwa Waziri Mambo ya ndani ndo nilikona wanawake/kina mama wanaenda kushitaki kwake juu ya matatizo ya ndoa zao.Je unataka kuniambia yeye alikuwa ndo ustawi wa Jamii????Ina maana hakuona mahakama??Na bado kina baba walipatiwa shida na huyu bwana kisa Waziri maarufu mrema kasema.Ukiwa waziri kuna mipaka yako kiutendaji.Siyo kukurupuka tu na kushughulikia kila kitu.Namjua Mrema zaidi ya unavyoweza kuhisi.Ungekuwa na simu yake ningekwambia umpigie simu na umuulizie jina langu kama utataka niku-PM na umwambie mwaka 1995 tulimsaidia vipi yeye na Kamara Kasupya pale Dodoma.Lakini baada ya kumuona kuwa ni "ZIGO" niliachana nae mara moja.

Mrema ni mkurupukaji,mpenda sifa,hasiye shaurika na hasiye na mbinu wala strategy zozote zile.Kama unakumbuka unaweza kunambia kwenye mdahalo wa wagombea Urais 1995 alifanya madudu gani mbali na kuonyesha jamii ana hasira na uchu wa madaraka kiasi gani.Mrema huyu alikuwa anashauriwa na kuongozwa na wanamipango wa NCCR ili aseme nini kwenye makongamano lakini yeye kila mara alikuwa anakuja na mahadithi yake yasiyo na kichwa wala miguu kitu kilichomfanya ashindwe vibaya sana kwenye uchaguzi.Alihamia NCCR kikiwa na nguvu na akatoka kikiwa hakina nguvu.Kila anakoenda ni matatizo tuu kwa hoja dhaifu utasema aliandamwa na CCM,wewe unataka CCM wafanye nini??Wamwachie tu bila kumdhibiti??unajua siasa kweli wewe??Mbona Mbowe anaandamwa na CCM na hao kina Mtikila lakini Chadema kiasi inazidi kung'aa???Unafikiri mrema angekuwa ndo ZITTO wakati anasimamishwa ubunge ingekuwaje,si angefia hukohuko kabisa?? Lakini mbona dogo zitto mbali na kuandamwa lakini anafanya vizuri????

Mimi kwangu Mrema plus Mtikila ni sawa na uji na mgonjwa hasiye na meno.
Avache

Majita,

Wakati wengi wamesimuliwa tu mambo ya Mrema na mrema-fanatics, wengine tuliyashuhudia and we have the scars to prove it. Kama mtu anakataa kukubali amri za Mrema za siku saba za kumfuata Kiraracha, huyo ana lake (or was too young to fathom what was happening).
 
Maneno hayo mekundu yameandikwa na Masatu, Ingekuwa ni jioni ningedhani mvinyo unaharibu macho yangu,lakini muda huu nabakia kuguna tuu. Mhh!!

Utaguna sana, sadly Mrema unaemjua wewe ni huyu wa TLP ungesumbuka kidogo kutaka kujua utumishi wako wa huko nyuma usingeguna.

Nakutakia kila la hei kwenye miguno yako
 
Jmushi,
Inawezekana kabisa mimi siijui historia ya Tanzania kama unavyodai.Lakini naomba ukubaliane na mimi kuwa ukisema kuwa Mrema halikuwa hawapi watu aliowaita yeye jina la waharifu wamfuate kwake huko kiraracha inaonyesha ni jinsi gani unavyoijua hitoria ya Tanzania.

Sijui vizuri mambo ya uhalifu na intelligencia unayodai wewe unaifahamu kwa kiasi gani.Naomba usichanganye mambo tafadhali.Wakati wa ujambazi kipindi cha Mrema na wakati wa ujambazi wa mchana kweupe mara tu JK alipoingia madarakani.Ni vitu viwili tofauti kabisa.kimsingi Mrema alionyesha kiwango kidogo sana cha kuimudu wizara ya Mambo ya ndani ukilinganisha na wote waliowahi kushika wizara hiyo.Mrema alikuwa bingwa wa kukurupuka.HUWEZI NA NASISITIZA HUWEZI kukurupuka wakati wa ujambazi kama ule na kuanzisha sungusungu isiyo na kichwa wala miguu.Tuliona sungu sungu ikiishia kuwatesa raia wasio na hatia kwa vile wote waliokuwa wanalinda sungusungu hawakuwa na ama taaluma ya Ulinzi au mbinu za kiupelelezi.Wapi na wapi utamlinda jambazi wa SMG acha gobore kwa fimbo ya mpera????
Jiulize unafikiri mrema angekuwa waziri kipindi kile majambazi wanaiba hela za NMB pale ubungo kweupe angefanya nini.Si angesema hadi mashule yafungwe na wote tuwe walinzi wa sungu sungu na wanafunzi wa shule??

Ni kipindi hichohicho cha Mrema akiwa Waziri Mambo ya ndani ndo nilikona wanawake/kina mama wanaenda kushitaki kwake juu ya matatizo ya ndoa zao.Je unataka kuniambia yeye alikuwa ndo ustawi wa Jamii????Ina maana hakuona mahakama??Na bado kina baba walipatiwa shida na huyu bwana kisa Waziri maarufu mrema kasema.Ukiwa waziri kuna mipaka yako kiutendaji.Siyo kukurupuka tu na kushughulikia kila kitu.Namjua Mrema zaidi ya unavyoweza kuhisi.Ungekuwa na simu yake ningekwambia umpigie simu na umuulizie jina langu kama utataka niku-PM na umwambie mwaka 1995 tulimsaidia vipi yeye na Kamara Kasupya pale Dodoma.Lakini baada ya kumuona kuwa ni "ZIGO" niliachana nae mara moja.

Mrema ni mkurupukaji,mpenda sifa,hasiye shaurika na hasiye na mbinu wala strategy zozote zile.Kama unakumbuka unaweza kunambia kwenye mdahalo wa wagombea Urais 1995 alifanya madudu gani mbali na kuonyesha jamii ana hasira na uchu wa madaraka kiasi gani.Mrema huyu alikuwa anashauriwa na kuongozwa na wanamipango wa NCCR ili aseme nini kwenye makongamano lakini yeye kila mara alikuwa anakuja na mahadithi yake yasiyo na kichwa wala miguu kitu kilichomfanya ashindwe vibaya sana kwenye uchaguzi.Alihamia NCCR kikiwa na nguvu na akatoka kikiwa hakina nguvu.Kila anakoenda ni matatizo tuu kwa hoja dhaifu utasema aliandamwa na CCM,wewe unataka CCM wafanye nini??Wamwachie tu bila kumdhibiti??unajua siasa kweli wewe??Mbona Mbowe anaandamwa na CCM na hao kina Mtikila lakini Chadema kiasi inazidi kung'aa???Unafikiri mrema angekuwa ndo ZITTO wakati anasimamishwa ubunge ingekuwaje,si angefia hukohuko kabisa?? Lakini mbona dogo zitto mbali na kuandamwa lakini anafanya vizuri????

Mimi kwangu Mrema plus Mtikila ni sawa na uji na mgonjwa hasiye na meno.
Avache

Majita watu wenye chuki na Mrema wanazungumza mambo yale yale waliyokuwa wakizungumza kabla hata hajajitowa ccm...Maneno ya kudai kuwa alikuwa akiingilia wizara za watu wengine nk.
Umeshindwa kujibu kuhusu kina Mahita na ujambazi kupanda mara baada ya Mkapa kumtunukia Mahita kwa kumdhibiti Mrema.
Mahita mwenyewe alikuwa akitowa orders wakati akiwa nyumbani kwake na bukta tu na kuzungumza maneno ya kikabila na kumtukana Mrema na kutowa amri kuwa alimwe mabomu ya machozi.
Mag3 unazungumzia makovu...Kuna makovu pia wakati wa Mrema kudhitiwa na wafuasi wake.
Siwezi kushangazwa kabisa kuwa Mrema alikuwa tishio kubwa sana na siwezi kumfananisha na wanasiasa wengine wa upinzani ambao hata hawajawahi kushika nyadhifa za serikalini kama yeye.

Unapomfananisha na kina Zitto na Mbowe na huku ukijuwa kuwa huyu mtu ana historia ndefu zaidi ya wanamapinduzi hao.

Kila mmoja ana nafasi yake lakini mifano yako hainiingii akilini kabisa kutokana na relevance....Kwa mfano huwezi kujuwa kama hao uliowataja wange react vipi kwenye nafasi ambazo Mrema alishawahi kupitia.
Mimi sio fanatic wa Mrema kama anavyodai Mag3....Ila tuwe na logic...Sina maslahi hapa.
Mtikila unamfananisha na Mrema huo ndio ninaosema ni ushabiki...Hivi unataka tuweke rekodi za utumishi kwa umma hapa halafu tufanye comparison?

Ama unataka kumfananisha tumbili na binadamu simply because they sometimes have the same instincts? Ndio maana nikakwambia usilete ushabiki eti kwa kufananisha wanasiasa hao wawili maana sasa nataka unieleze wewe kuwa ni nani unayemuona kuwa ni perfect kisiasa halafu na mimi nikutolee vijimifano vya kuwafananisha na wanasiasa wengine uchwara kutokana na kauli za kisiasa.
 
Majita watu wenye chuki na Mrema wanazungumza mambo yale yale waliyokuwa wakizungumza kabla hata hajajitowa ccm...Maneno ya kudai kuwa alikuwa akiingilai wizara za watu wengine nk.
Umeshindwa kujibu kuhusu kina Mahita na ujambazi kupanda mara baada ya Mkapa kumtunukia Mahita kwa kumdhibiti Mrema.
Mahita mwenyewe alikuwa akitowa orders wakati akiwa nyumbani kwake na bukta tu na kuzungumza maneno ya kikabila na kumtukana Mrema na kutowa amri kuwa alimwe mabomu ya machozi.Mag3 unazungumzia makovu...Kuna makovu pia wakati wa Mrema kudhitiwa na wafuasi wake.
Siwezi kushangazwa kabisa kuwa Mrema alikuwa tishio kubwa sana na siwezi kumfananisha na wanasiasa wengine wa ipinzani ambao hata hawajawahi kushika nyadhifa za serikalini kama yeye.

Unapomfananisha na kina Zitto na Mbowe na huku ukijuwa kuwa huyu mtu ana historia ndefu zaidi ya wanamapinduzi hao.

Kila mmoja ana nafasi yake lakini mifano yako hainiingii akilini kabisa kutokana na relevance....Kwa mfano huwezi kujuwa kama hao uliowataja wange react vipi kwenye nafasi ambazo Mrema alishawahi kupitia.
Mimi sio fanatic wa Mrema kama anavyodai Mag3....Ila tuwe na logic...Sina maslahi hapa.
Mtikila unamfananisha na Mrema huo ndio ninaosema ni ushabiki...Hivi unataka tuweke rekodi za utumishi kwa umma hapa halafu tufanye comparison?

Ama unataka kumfananisha tumbili na binadamu simply because they sometimes have the same instincts? Ndio maana nikakwambia usilete ushabili eti kwa kufananisha wanasiasa hao wawili maana sasa nataka unieleze wewe kuwa ni nani unayemuona kuwa ni perfect kisiasa halafu na mimi nikutolee vijimifano vya kuwafananisha na wanasiasa wengine uchwara kutokana na kauli za kisiasa.

Mkuu Jmushi,
Labda sasa tukubaliane tuu kuwa tunataka kubishana.Yaani hapo ulipoandika habari za Mahita ndo SIJAKUELEWA KABISA na umenishangaza kweli kweli kusikia madai hayo ya uzushi.Kaka inaonekana hata riot hujui inafanywaje na hao maaskari.Labda nikusaidie tuu kuwa,askari polisi wakienda kwenye riot ama tuseme kutuliza fujo huwa kunakuwepo makamanda.Utaona kuna askari waliobeba bunduki za risasi za moto,mabomu ya machozi.virungu,machela nk pia utaona kama wana magari ya maji nk.Utaona pia kunakuwa na mwingine ana kipaza sauti.So inaanza kwa huyo mwenye kipaza sauti kuwaamuru watu watawanyike ama sivyo nguvu itatumika.Atatangaza na hilo li tarumbeta lake mara tatu,wakikataa inatoka amri ya kamanda kuwaagiza askari wa virungu,wakishindwa anaamuru wa mambomu ya machozi wakishindwa maji ya kuwasha wakishindwa mlolongo unaendelea.
Sasa kaka hebu nambie kati ya hao ni wapi mahita alionekana akiwa na bukta na kuamru askari wampige mrema?????Wewe unasema eti akiwa nyumbani anatoa amri????hivi kweli ni wewe au umepitiwa???Tunajua protokali ya kijeshi ilivyo ndo maana huwa tunamhusisha mahita na mabomu aliyopigwa mrema moshi.Lakini kwa statement yako hiyo sina la kuongeza bali kusema tu kuwa labda unataka uwe ubishi tuu humu tujaze idadi za threads.

Labda nikukumbushe kuwa kipolisi mkoani wote wanatii kwa RPC,weka mastafu kisha njoo RCO,kisha njoo kwa vikosi as FFU,trafic nk baada ya hapo shuka wilayani kwa OCD na OC CID hadi OCS.Narudia tena wote wanatii kwa RPC sasa kaka siku nyingine njoo na utetezi wa kina kuliko kudanganya watu kuwa mahita alitoa amri na bukta za kumpiga Mrema akiwa nyumbani.

Narudia kusema kuwa Mrema na Mtikila wanafanana sana.Kufanana kwao ni katika nyanja zifuatazo:-Wote ni watu wa kupenda sifa,wote ni wakurupukaji,wote hawashauriki,wote wanapenda umaarufu,wote ni watu wa kulipa visasi,wote ni watu wenye hasira,wote ni watu wanaoganga njaa,wote wanapenda kuona upepo kisiasa unaenda vipi na kulalia huko,wote hawana dira,wote wana uchu wa madaraka na wote unaweza kuongeza zingine.

Tofauti yao ni moja tu kuwa Mrema aliwahi kuwa kiongozi wa Serikali wakati mtikila hajawahi.THATS IT.
 
Mkuu Jmushi,
Labda sasa tukubaliane tuu kuwa tunataka kubishana.Yaani hapo ulipoandika habari za Mahita ndo SIJAKUELEWA KABISA na umenishangaza kweli kweli kusikia madai hayo ya uzushi.Kaka inaonekana hata riot hujui inafanywaje na hao maaskari.Labda nikusaidie tuu kuwa,askari polisi wakienda kwenye riot ama tuseme kutuliza fujo huwa kunakuwepo makamanda.Utaona kuna askari waliobeba bunduki za risasi za moto,mabomu ya machozi.virungu,machela nk pia utaona kama wana magari ya maji nk.Utaona pia kunakuwa na mwingine ana kipaza sauti.So inaanza kwa huyo mwenye kipaza sauti kuwaamuru watu watawanyike ama sivyo nguvu itatumika.Atatangaza na hilo li tarumbeta lake mara tatu,wakikataa inatoka amri ya kamanda kuwaagiza askari wa virungu,wakishindwa anaamuru wa mambomu ya machozi wakishindwa maji ya kuwasha wakishindwa mlolongo unaendelea.
Sasa kaka hebu nambie kati ya hao ni wapi mahita alionekana akiwa na bukta na kuamru askari wampige mrema?????Wewe unasema eti akiwa nyumbani anatoa amri????hivi kweli ni wewe au umepitiwa???Tunajua protokali ya kijeshi ilivyo ndo maana huwa tunamhusisha mahita na mabomu aliyopigwa mrema moshi.Lakini kwa statement yako hiyo sina la kuongeza bali kusema tu kuwa labda unataka uwe ubishi tuu humu tujaze idadi za threads.

Labda nikukumbushe kuwa kipolisi mkoani wote wanatii kwa RPC,weka mastafu kisha njoo RCO,kisha njoo kwa vikosi as FFU,trafic nk baada ya hapo shuka wilayani kwa OCD na OC CID hadi OCS.Narudia tena wote wanatii kwa RPC sasa kaka siku nyingine njoo na utetezi wa kina kuliko kudanganya watu kuwa mahita alitoa amri na bukta za kumpiga Mrema akiwa nyumbani.

Narudia kusema kuwa Mrema na Mtikila wanafanana sana.Kufanana kwao ni katika nyanja zifuatazo:-Wote ni watu wa kupenda sifa,wote ni wakurupukaji,wote hawashauriki,wote wanapenda umaarufu,wote ni watu wa kulipa visasi,wote ni watu wenye hasira,wote ni watu wanaoganga njaa,wote wanapenda kuona upepo kisiasa unaenda vipi na kulalia huko,wote hawana dira,wote wana uchu wa madaraka na wote unaweza kuongeza zingine.

Tofauti yao ni moja tu kuwa Mrema aliwahi kuwa kiongozi wa Serikali wakati mtikila hajawahi.THATS IT.

Mrema ana historia ya kupigania maslahi ya walalahoi toka akiwa chama tawala...Nani anajuwa mtafanya nini nyie mkipewa nchi?
Kama mpinzani mwenzenu mnapinga kuliko hata fisadi mwenyewe nyie ni watu wa kuaminika kweli?

Kumfananisha na Mtikila na kukomalia kichwa kwenye pointi hiyo ni dalili za wazi za chuki miongoni mwa wanasiasa wa upinzani.

Halafu unasema eti tofauti ya Mrema na Mtikila ni simply kuwa mmoja kafanya kazi serikalini na mwingine hakufanya....Halafu umeishia hapo na conclusion kuwa yule ambaye hakufanya kazi serikalini ni sawa na yule aliyefanya kazi serikalini na kusolve matatizo ta wananchi na kusimama kinyume na mwenendo mchafu wa kifisadi.

Unafananisha watu ambao wameupiga ufisadi ndani ya ngome ya ufisadi na wameonyesha hilo kwa vitendo bila woga wa kufa kisiasa.
Nani asiyejuwa kila mwana ccm mwenye kutaka kujiunga na upinzani anatumia kigezo cha Mrema kama kisingizio?

Nani anayetaka kuja kukosewa fadhila kama ilivyo sasa...Wanaona ni bora wakae tu humo ndani na wafuate flow almuradi mkono unaenda kinywani na mambo ni safi.

Kama upinzani ndio kuna watu kama nyie basi hakuna upinzani.
Kuhusu hilo la Mahita ni ukweli na inaonyesha huujui...So habari ndiyo hiyo...Unajifanya hujui kuwa polisi kama hao wako juu ya sheria hapo bongo..Kwa taarifa yako Mahita wakati huo alikuwa anaishi mahali ambapo ni njia yangu ya kila siku kwenda shule primary pale Kibo....Na baadhi ya marafiki zangu walikuwa wanishi jirani yake tu na wakati mwingine tunatembea tu hadi kwao wakati wa kwenda nyumbani....Na wakati mwingine Mahita utamkuta yuko nje na bukta akipiga tizi la hapa na pale na mawasiliano kama kawaida.

Wewe unajaribu kunielezea utaratibu wanaoufuata wanausalama hao wakati wa kudeal na riot...Kama hujui kuwa Mrema alikabidhiwa kwa Mahita then kuna issue ambazo hauzitilii maanani kutokana na kuwa umeshaamuwa kuwa Mrema ni mtu mbaya na hafai.

Kama ulivyodai kuwa umeshawahi kukutana naye nk..Inawezekana wewe ni mwanasiasa..So sishangazwi....Siwezi kushangazwa kwasababu umesema ana uchu wa madaraka...Ni kina nani hao huko upinzani wasiokuwa na uchu wa madaraka? NI neno "Uchu" ndio linalokushtuwa?
Nani asiyetaka kwenda ikulu huko upinzani kwa style ambayo tunaweza kusema ni uchu?
Ama unataka kusema wanataka madaraka lakini hawayatamani?

Mtikila aliyechukuwa pesa za Rostam unasema Mrema na yeye ana njaa? Sifa? what is sifa? Mwanasiasa gani asiyependa sifa...Ebu acha utani bana.
 
Upinzani siyo lazima tukubalianae na nyendo za Mrema.
Na siyo kweli kwamba wale ambao hawakufanya kazi serikalini huwezi kuwafananisha na waliofanya kazi serikalini.
 
Upinzani siyo lazima tukubalianae na nyendo za Mrema.
Na siyo kweli kwamba wale ambao hawakufanya kazi serikalini huwezi kuwafananisha na waliofanya kazi serikalini.

Sijasema ni lazima mkubaliane na Mrema...Nachosema hapa ni kuwa sikubaliana na sifa mbovu mnazomvika na kudai eti apumzike na huku mkimfananisha na mpinzani mwenzenu Mtikila.

Huwezi kufafanisha watu ambao wameshawafanyia kazi wananchi ama kwa maana nyingine kutatuwa matatizo yao na watu ambao hawajawahi kuwa na nafasi ambazo ni za utumishi wa umma kwasababu nafasi hizo zina opportunity ya kuweza kuwa fisadi...Sasa Mtikila mwenyewe hajapata nafasi hiyo lakini keshakula vya mafisadi....Jambo usilolijuwa ni kama usiku wa kiza.

Na hakuna mpinzani unayemuona ni bora ameshakuwa kwenye nafasi kama hiyo hili tuone angewatumikiaje wananchi zaidi tu ya maneno kuwa watafanya kazi nzuri.
 
Wanabodi,

Je, mimi nikisema kwa uhakika kwamba nimewahi kupeleka fedha kwa Mrema (akiwa waziri wa mambo ya ndani) kwa ajili ya magari ya mafuta yakiyokuwa yamekamatwa wakidai kuwa mafuta hayo yalikuwa ya magendo! - haikuwa kweli isipokuwa baadhi ya taratibu zilizotakiwa hazikufanyika..

Hakuwa msafi kama mnavyofikiria ila naweza kukubali alijaribu sana kutetea masikini mahala wanapolalamika tena mwanzoni aliposhika madaraka baadaye akajiunga naye kundi la majambazi.

Kifupi Mrema ni mbabaishaji tu, kiongozi hawezi kuwa kinyonga leo mzuri kesho mambo yakimwendea vibaya nyumbani anapokea rushwa...
 
Sijasema ni lazima mkubaliane na Mrema...Nachosema hapa ni kuwa sikubaliana na sifa mbovu mnazomvika na kudai eti apumzike na huku mkimfananisha na mpinzani mwenzenu Mtikila.
Huwezi kufafanisha watu ambao wameshawafanyia kazi wananchi ama kwa maana nyingine kutatuwa matatizo yao na watu ambao hawajawahi kuwa na nafasi ambazo ni za utumishi wa umma kwasababu nafasi hizo zina opportunity ya kuweza kuwa fisadi...Sasa Mtikila mwenyewe hajapata nafasi hiyo lakini keshakula vya mafisadi....Jambo usilolijuwa ni kama usiku wa kiza.
Na hakuna mpinzani unayemuona ni bora ameshakuwa kwenye nafasi kama hiyo hili tuone angewatumikiaje wananchi zaidi tu ya maneno kuwa watafanya kazi nzuri.

Maalimu Seif Hamad wa Chama Cha Wananchi,
 
Wanaqbodi,
Je, mimi nikisema kwa uhakika kwamba nimewahi kupeleka fedha kwa Mrema (akiwa waziri wa mambo ya ndani) kwa ajili ya magari ya mafuta yakiyokuwa yamekamatwa wakidai kuwa mafuta hayo yalikuwa ya magendo! - haikuwa kweli isipokuwa baadhi ya taratibu zilizotakiwa hazikufanyika..
Hakuwa msafi kama mnavyofikiria ila naweza kukubali alijaribu sana kutetea masikini mahala wanapolalamika tena mwanzoni aliposhika madaraka baadaye akajiunga naye kundi la majambazi.
Kifupi Mrema ni mbabaishaji tu, kiongozi hawezi kuwa kinyonga leo mzuri kesho mambo yakimwendea vibaya nyumbani anapokea rushwa...
Kweli kabisa Mkandara.
Unakumbuka zile pesa alichangisha pale Jangwani kuwa ni nauli ya kwenda kumuona Mandela na Malkia Elizabeth kuishtaki serikali ya Tanzania kwa matendo mabaya?
Unakumbuka nini kiliendelea baada ya hapo? Ni kwenda Marangu kula Christmas. Mrema ana katabia ka ukigeugeu na ubabaishaji. Huo ndio ukweli
 
Hakuna aliyetowa sababu nzito kwamba Mrema hafai...Ndugu Mkandara na yeye anazungumzia rushwa aliyompa Mrema..Hii kali.

Mwenye kusema kuna wanasiasa wasafi kwa asilimia mia moja basi ana ota njozi ya mchana....Mtu anayepigwa vita na ccm na mafisadi pamoja na wapinzani wenye uchu ambao wanataka ku capitalize kutokana na upepo wa kisiasa kuhusiana na ufisadi huku wakisahau historia ambayo ni kama muongo mmoja uliopita basi kuna matatizo katika bongo zetu sisi watanzania na ndio maana hata ccm wana abuse power kwasababu sisi ni wavivu kufikiri na wepesi kusahau.

Kuna wanaosema alijiunga na kundi la majambazi..Hapo naomba ufafanuzi kwasababu majambazi tunayajuwa.

Inasikitisha sana...Kuna listi ya wauza madawa ambayo hadi leo Rais mliyemchaguwa kaikalia...Yani maovu ambayo yameshafanyika na wanasiasa ambao wako madarakani hadi sasa ni makubwa na yasiyothimilika...Hata hivyo chuki mbaya dhidi ya Lyatonga imesababisha mashetani kuonekana watu wema na malaika.

Mwingine anakuja na pointi eti alichangangisha pesa jangwani na kuzipeleka Marangu....Ama kweli kuna watu wana rhuksa ya kula na wana bahati kwani wanastahili kula tu no wonder kuna wazee wa vijisenti, EPA, Kagoda, Meremeta nk....Kaazi kweli kweli...Inanikumbushia ile nyiombo ya Dk Remmy kuwa hata nguruwe wakila mazao basi ni yeye tu analalamikiwa...

Watu wavivu na magoi goi pia wanamwogopa Mrema..Kwasababu aliwa empower hata watu wa chini na mabosi waliambiwa wasichelewe kazini na wakifanya hivyo wafanyakazi walitakiwa kuchukuwa hatuwa.

Hakuna jinsi ya kudeal na matatizo tuliyonayo waafrika na watanzania kwa ujumla kama hatutatilia mkazo kwenye matatizo yetu sugu...
Watu wanataka laini laini tuuu! Wengi wetu tunataka mafanikio lakini ni ubinafsi na njia za mikato na uvivu...Na ndio maana rushwa imeota mizizi na Taifa kwa ujumla limeoza kiutendaji na kiufanisi kwaababu nobody cares.

Na viongozi tulionao naona wamekumbatia ule usemi wa ukila na kipofu usimshike mkono...Ni wazi jamii yetu ina matatizo na kama viongozi hawako dedicated kujaribu kuikombowa jamii..Basi watakuja na kupita tu huku historia ikiendelea kuandikwa...Lakini kama kweli wana nia nzuri, basi matendo yao yatakuwa wazi na watalitumikia Taifa bila kujali kama watafanikisha malengo yote...Kwamba viongozi wazuri ni wale ambao ni dedicated na wanafanya part yao huku wakiomba Mungu kuwa viongozi wajao wataendeleza pale walipoachia.

Kwetu ni tofauti sana tu...Nobody cares na viongozi wetu waliopita washasema hayo na Mkapa mwenyewe alishasema kuwa Watanzania hawasaidiki na ni wavivu wa kufikiri...Mambo mengi sasa yanaanza kumake sense in one way or another...

Na ndio maana siasa, unazi wa vyama,ubinafsi na tamaa za madaraka vimetake over ufanisi wa kiuchumi na kijamii huku sera zikiwa ni ufisadi....Sio siri ufisadi ulipata baraka mara baada ya Mrema kuzuliwa mambo na kuchafuliwa kisiasa na kufanywa aonekane kama hamnazo.

Tanzania ni nchi masikini na kwa wengi ulaji ni siasa...No wonder wanasiasa wengine wanafanya kila wawezalo kuwachafua wanasiasa wengine.

Kuna aliyesema kuhusu Seif Sharif..Ndugu yangu huyu na yeye si alisema watu waache tamaa za madaraka na wawapishe wengine..?

Imagine ingekuwa ni Mrema ambaye kuna watu wanasema wakati wake umepita..Na mimi nikitumia vigezo hivyo hivyo si ninaweza kusema wakati wa Hamad umepita?

Mimi naamini kwamba wanamapinduzi hao wako kwenye harakati za ukombozi na uhuru kwa mtanzania...Therefore harakati hizo zitaendelea na kaburi ndio mwisho wake unless ukombozi umekamilika.

Nani anayetaka kusema kuwa vita ya ukombozi ina kupitwa na wakati?

Namshauri Mrema aendeleze vita ya ukombozi na kifo ndiyo kiwe kikomo.
 
Mkulu Mushi,

Respect bro, sina uhakika na hoja zako nyingi kwenye hii thread lakini I sure respect your attitude ya kutetea what you believe to be ukweli na kuwa na msimamo,

wanasema Sharpton sio kiongozi hodari, lakini heshima yake inatokana na misimamo yake imara isiyoyumba.

Keep it up!
 
TLP chasambaratika mkoani Kilimanjaro

Na Victor Kwayu, PST Moshi

Zaidi ya viongozi na wanachama 100 wa Tanzania Labour Party (TLP) mkoani Kilimanjaro wakiongozwa na Mwenyekiti wao mkoani hapa, Rose Masuruali wamekihama chama hicho na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Akizungumza na viongozi wa kata mbalimbali za Kirua Vunjo, Masuruali alisema amefikia uamuzi wa kuihama TLP baada ya kubaini mapungufu kadhaa ya uongozi ndani yake.


Alisema TLP pamoja na viongozi wake wa ngazi za juu akiwemo Mwenyekiti wake, Augustine Mrema, wamekosa mwelekeo ikiwa ni pamoja na kutokuwa na sera mbadala za kumkomboa Mtanzania.


"Chama chetu (TLP) kimekosa mwelekeo, viongozi wa ngazi za juu wamekosa dira na ndio maana hatuna hata mbunge wala diwani, chama kimefilisika kisiasa na badala yake yamebakia majungu yanayosababisha kukigawa, sasa tumeamka," alisema Mwenyekiti huyo ambaye kabla ya kuukwa Uenyekiti wa mkoa alikuwa Mwenyekiti wa Wanawake Kata ya Kirua Vunjo.


Wanachama na viongozi wa kata waliokihama chama hicho na kujiunga na
CHADEMA ni waliotoka katika vijiji vya Nganjoni, Mrumeni, Kireuwo pamoja na kijiji cha Mero ambao kwa pamoja walipitisha azimio la kukihama cha hicho.

Naye Mwenyekiti wa TLP Kata ya Kirua Vunjo, Joseph Assey alisema kutokana na Mwenyekiti wa chama hicho, Augustine Mrema kuonekana kukosa sera mbadala, wameamua kukihama chama hicho na kujiungana na
CHADEMA katika kupambana na vita vya mafisadi sanjari na zoezi la kuwasakama mafisadi la Operesheni Sangara linaondelea Kanda ya Ziwa.

Alisema kimsingi
CHADEMA imeonyesha nia ya dhati ya kupambana na viongozi wasio waadilifu na kwa msingi huo wameona chama pekee kinachoweza kuing'oa CCM madarakani ni CHADEMA pekee.

"Operesheni Sangara imeitikisa nchi, viongozi na mafisadi ndani ya serikali matumbo joto ...kuingia kwetu
CHADEMA kutasaidia kuonyesha nia ya dhati ya kuendelea na mapambano dhidi ya mafisadi na viongozi wasio makini, lengo ni kumkomboa mwananchi na lindi la umasikini," alisema Assey.

Naye Katibu Mwenezi wa
CHADEMA Manispaa ya Moshi, Augustine Makelele alisema kundi la wanachama hao pamoja na viongozi wa TLP kuamua kujiunga na chama hicho, limedhihirisha ni namna gani chama hicho kinavyokubalika hivi sasa.

Alisema kwa msingi huo, chama hicho kimeazimia kuhakikisha kinahamishia zoezi la Operesheni Sangara katika Mkoa wa Kilimanjaro ikiwa ni pamoja na kuhamasisha wananchi kuhakikisha wanajiunga na chama hicho ambacho alikiita kama chama chenye mwelekeo wa kumtetea mnyonge dhidi ya vita ya umasikini wa kipato.


Alisema kutokana na TLP kuonyesha udhaifu kiutendaji ikiwa ni pamoja na kukosa sera ya kweli, wanachama kadhaa wa vyama kadhaa vya siasa mkoani Kilimanjaro wamekuwa wakituma maombi kadhaa ya kujiunga na chama hicho.


"Tumekuwa tukipokea maombi mengi kutoka kwa wanachama wa vyama vya siasa kikiwemo chama tawala cha CCM ...kutaka kujiunga na chama chetu, sera na mwelekeo wa CHADEMA umekuwa ukikubalika na kuwa na mvuto mkubwa, hivyo tunawakaribisha kwa mikono miwili," alisema Makelele.


Aidha, alisema viongozi na wanachama hao waliojiunga na chama hicho wakitokea TLP, watakabidhiwa kadi rasmi na Mwenyekiti wa chama hicho kitaifa, Freeman Mbowe hivi karibuni mjini hapa.


SOURCE: Nipashe
 
Back
Top Bottom