The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

Huu ni mwanzo wa mwisho wa wanasiasa wetu? huytu kaupata wapi ujasiri wa kuyasema haya ?JK watch out something is coming.
 
Jamco Za, hata watanzania mkijua mtafanya nini? Haya mambo kuna watanzania wengi tu walikuwa wanajua wanaumia roho, lakini hakuna cha kufanya.
Tatuna cha kufanya, mkiandamana kwa upole watawapeni hotuba nzuri, mkiandamana kwa fujo, mtapigwa mabomu, hebu niambie una mpango wa kufanya nini, hivyo ambavyo umeshajua?
 
Anamtishia nani huyo kama mbwai, mbwai tuu hakuna atakae acha kwenda mahakamani, kwa kifupi huyu jamaa anataka kucontrol nchi yetu, hizo siri au hayo mabomu ndo yatamuangamiza huyu mshenzi wake, kama alikuwa na siri na mbinu za vigogo kwanini asinge simama na kukemea ili kutetea maslahi ya nchi anasubiri kaumbuka ndo anatisha nyau, tena asicheze na nchi yetu kabisa, chenge nakutaadharisha usione watanzania wajinga, huna haja ya kusuburi mahakama kama kunasiri nzito unazijua na unajali taifa lako zimwage uwanjani, acha kelele
 
Huu ni mwanzo wa mwisho wa wanasiasa wetu? huytu kaupata wapi ujasiri wa kuyasema haya ?JK watch out something is coming.

Awatch out nini tena, hapa swala ni kuja mbele na kusema ukweli aombe msamaha arudishe na kuachia kiti na hu wito ni wote wanaohusika, tena ni bora waje mbele mapema kabla hawajaumbuliwa.... maana moto utawawakia
 
kwani wanasiasa ndio hao peke yao wakifa hao wanakuja wengine na wengine mimi yangu ni 2015 ubunge wa moshi vijijini
 
Jamco Za, hata watanzania mkijua mtafanya nini? Haya mambo kuna watanzania wengi tu walikuwa wanajua wanaumia roho, lakini hakuna cha kufanya.
Tatuna cha kufanya, mkiandamana kwa upole watawapeni hotuba nzuri, mkiandamana kwa fujo, mtapigwa mabomu, hebu niambie una mpango wa kufanya nini, hivyo ambavyo umeshajua?

Hawa wanasiasa wanaajiriwa na wananchi, then tutawashitaki kwa wananchi kama baadhi ya mambo yanavyopelekwa kwa wananchi na kutolewa maamuzi, sasa hivi wanazomewa kila kona imebaki kidogo hawa wananchi wakipata elimu ya uraia wataacha kuwapigia kura na watakuwa wamepigwa chini.
 
Jamco Za, hata watanzania mkijua mtafanya nini? Haya mambo kuna watanzania wengi tu walikuwa wanajua wanaumia roho, lakini hakuna cha kufanya.
Tatuna cha kufanya, mkiandamana kwa upole watawapeni hotuba nzuri, mkiandamana kwa fujo, mtapigwa mabomu, hebu niambie una mpango wa kufanya nini, hivyo ambavyo umeshajua?

Haika
Hapa unataka wananchi wanyamaze kimya wanavyoendelea kubebeshwa mizigo ya umasikini kwa ubadhirifu huu wa dhahiri wa mali zao au una maana gani?Huwa inafika wakati kufa na kuishi vyote ni sawasawa.Kama hamna mabadiliko ya dhati ya ktk kuendesha nchi hii,usitegemee wimbo wa kudumisha amani unaoimbwa kwenye majukwaa utadumu.God is watching from above.

Je Marekani pamoja na kumnyonga SADDAM wamefanikiwa na vifaru vyao kiitawala IRAK?

Je Marekani pamoja na kumwondoa Mura OMAR na Osama Afghanstani wamefanikiwa kuitawala?Nadhani una taarifa Rais waliyemweka juzi tu kaponea chupu chupu kulipuliwa.

Tena wasije wakadharau na kuajribu kuzima hizi kelele unazosikia za wa TZ na kuona ni wanyonge,hawawezi kuthubutu,siku zinakuja ambapo hata hawa viongozi kutembea hawatakuwa na uhuru hapa nchini.
 
kwani wanasiasa ndio hao peke yao wakifa hao wanakuja wengine na wengine mimi yangu ni 2015 ubunge wa moshi vijijini

Ndugu "shy" nimekuwa nafuaatilia hoja zako kwa muda nakuona mambo yako yako kupinga pinga tu, tena unatia kichefuchefu, ni mtu wa ovyo, watu hapa wanaongea hoja za msingi, za maendeleo wewe unaleta za kucheza.

Kama ni kiu yako ya ubunge si uende ukaanze kampeni kama MAFISADI wenzako. Naona hapa unapoteza mda tu. Nyambafu we!!!
 
Single D, mimi nakuuliza wewe, una mpango wa kufanya nini? Yaani baada ya kumaliza kupost huku kwny JF, au unawazo mtu fulani afanye nini, na utamsaidiaje?
 
Single D, mimi nakuuliza wewe, una mpango wa kufanya nini? Yaani baada ya kumaliza kupost huku kwny JF, au unawazo mtu fulani afanye nini, na utamsaidiaje?

Nadhani kama umenisoma vema umenijua dhamira yangu nini.
Mawazo yangu ni kwamba tusikae tukabweteka kuwa hawa mafisadi hawawezi kutikiswa na kitu chochote kwa kuwa ni CCM.
Ule wakati wa zidumu fikra sahihi za mwenyekiti wa CCM umepitwa na wakati.Hatuna haja ya kutiwa hofu.Wananchi sasa hivi wanaangalia uadilifu wa mtu ktk kuongoza si chama.Kilango,MWAKYEMBE,Kimaro aloyce n.k ni CCM lakini wananchi wengi wanawakubali kwa kuwa mchango wao unaonekana hali kadhalika ZITO,HAMAD,SLAA N.K pia wanakubalika kwa kuwa wanajua kilichowapeleka ndani ya mjengo
Ni kuhakikishie kuwa kura yangu 2010 haitaenda kwa fisadi na pia ndo dhamira halisi ya wapenda maendeleo ya Taifa hili
 
...hata watanzania mkijua mtafanya nini? Haya mambo kuna watanzania wengi tu walikuwa wanajua wanaumia roho, lakini hakuna cha kufanya.

Haika, usijishushe sana! Mengi ya mageuzi unayoyaona yanafanyika sasa yanatokana na kilio cha wanahabari na wananchi kwa ujumla wao. Hivyo usiwakatishe wanaJF ktk kupigania haki! Sauti hii ina nguvu sana.

Tatuna cha kufanya, mkiandamana kwa upole watawapeni hotuba nzuri, mkiandamana kwa fujo, mtapigwa mabomu, hebu niambie una mpango wa kufanya nini, hivyo ambavyo umeshajua?

Kuandamana ni njia moja lakini kura zetu ndio zinazoaawajiri viongozi na chama chama ktk kututumikia na kututumikia they must au OUT!
 
nakumbuka hivyo vitisho havina tofauti na kashi kashi za nduli Idi Amini Dadaa ,yaani jamaa anatisha ile mbaya ila hapa ni Tz na huko ni Ulaya uhuru wake unaweza ukapigwa fulustop.mambo ya kutishana yamepitwa na wakati ,ila kama ndio alivyojaaiwa kula feza ya fisadi basi asiiwache na mwisho atuachie jamaa tumpeleke jela yeye abaki akiambaa ambaa na feza aliyoipata huku akisema tanzania hakuna eshima mahakamani tunaamua tunavyotaka ,yaani iyo feza ya bahili ndio imepata uyo jamaa aikwapue kiulaini maana hata hizo simu anazodai anapiga kila siku atoi hata kajindururu zinatumika hivyo vijisenti vya Chenge,yaani feza inaliwa na wajanja.
 
Ndugu "shy" nimekuwa nafuaatilia hoja zako kwa muda nakuona mambo yako yako kupinga pinga tu, tena unatia kichefuchefu, ni mtu wa ovyo, watu hapa wanaongea hoja za msingi, za maendeleo wewe unaleta za kucheza.

Kama ni kiu yako ya ubunge si uende ukaanze kampeni kama MAFISADI wenzako. Naona hapa unapoteza mda tu. Nyambafu we!!!

I told you that this boy was a stinker mkasema nimechukia sana .Sasa huyu hapa .The boy was cool lakini tangia ale mateso ya akina Mike kabadilika na Mwalimue alisema ukila nyama ya mtu hutaacha .Yeye kesha lamba hataacha u snitch .

Wakili wa Chenge anatishia na ni hatari .Ama anaujue ukweli na akisema itakuwa mwisho wa aserikali ya CCM na JK ama anataka kuzima soo kumuokoa Vijisenti.Ila JK kama Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Tanzania naamini anaweza kusema wacha tuone na avuke mipaka na Chenge ashitakiwe tuone .Huyo Wakili anaweza pia kukataliwa kuingia Nchini kama si Mtanzania atafanya nini ?
 
Nguvu ya umma hatimaye inaanza kuchukua upper hand katika vita dhidi ya mafisadi. Mambo yanaanza kuunganika taratibu na wataanza kutajana mmoja baada ya mwingine na hapo ndio kutatokea mtikisiko mkubwa katika Taifa la Tanzania ambalo hatujawahi kuuona tangu tupate uhuru mwaka 1961.

Halafu tumsikie mtu tena aseme hadharani kwamba wahusika ni matajiri wakubwa hivyo kuwakamata kutasababisha nchi kulipuka. Maana kwa wenye mapenzi ya kweli kwa nchi yetu tunadhani kuwaacha watu hao waendelee kuwa huru ndiko kutasababisha nchi kulipuka.

Mungu ibariki Tanzania na Watu wake
 
hapo ndo tulipokuwa tunapasubiri siku nyingi sana. wacha wafunuane kwa ushahidi, ili sisi wananchi tupate mtelemko.

ila kwa mtazamo wangu naona hii ni janja ya kuitisha serikali isifunguwe mashtaka kwa chenge.

tatizo ni kuwa this is not btw mkapa and chenge anymore, kuna mzungu anahusika. na huyo labda umrubuni kwa kumgawia nchi nusu ndo afute kesi
 
hivi kwanini siku hizi kila kiongozi ikibainika kafanya maovu anatishia kutaja wengine? hi si tayari inadhihirisha kafanya? mi napendekeza kila afanyae hivi iwe "admission of guilt" na hao anaowataja walazimike kujitetea au wakinyamaza nao itambulike ni wahalifu pia
 
Anamtishia nani huyo kama mbwai, mbwai tuu hakuna atakae acha kwenda mahakamani, kwa kifupi huyu jamaa anataka kucontrol nchi yetu, hizo siri au hayo mabomu ndo yatamuangamiza huyu mshenzi wake, kama alikuwa na siri na mbinu za vigogo kwanini asinge simama na kukemea ili kutetea maslahi ya nchi anasubiri kaumbuka ndo anatisha nyau, tena asicheze na nchi yetu kabisa, chenge nakutaadharisha usione watanzania wajinga, huna haja ya kusuburi mahakama kama kunasiri nzito unazijua na unajali taifa lako zimwage uwanjani, acha kelele

Huo ndo ukweli mtupu anatishia ili Chenge asifikishwe mahakamani, atafute mbinu nnyingine hii ni ya kitoto sana.
 
Back
Top Bottom