The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

bubu ,point of clarification,

simu 2000 ltd si private compony ni kampuni ya serikali iliyoundwa na sheria ya bunge,kusimamia na kuuza na kugawa mali za kampuni iliyosambaratishwa na kutenganishwa ya TANZANIA POSTS AND TELECOMMUNICATIONS na kupata TANZANIA POSTS na TANZANIA TELLECOMMUNICATION COMPONY LTD...SO HAPO JENGA UPYA hoja ili uonyeshe kuwa kwanza huyo mkurugenzi wa simu 2000 ,hana sifa ya kukalia ofisi[maana kuwa shemeji ya rais haina maana usiteuliwe kama una sifa]...pili onyesha ufisadi .kwa kifupi kuna hoja nzuri tu hapa za kujibu.
 
sijui hapa maada ni ipi rushwa? biashara? au kutojua tunaongea nini? adabu kwa viongozi.

siku zote waswahili tunakasumba ya kusoma kwa ajili ya kujibu mtihani, na ninahisi ndio wengi tuliopo.

Kwanza kitendo cha kumuongelea kiongozi wako kama kijiko cha jibini ni dharau tosha juu ya wewe mwenyewe, maana raisi aliwekwa au anawekwa na wewe pale.

Na nina hisi kuwa watu wengi hatujui rushwa maana yake ni nini, sidhani katika wote hapa ndani ya forum hakuna asiyetoa au kupokea rushwa kwa kivyovyote.

tunapozungumzia rada. Ni chombo kinachosaidia mambo mengi ya kiusalama na mengine mengi na ninahisi kwa bei yeyote ile ilikuwa ni halali kuipata hiyo rada, sasa tukumbuke kuwa ile ni shida ya serikali ambayo ni sisi wenyewe kwajili ya usalama wetu wenyewe na mambo mengine.

na tukumbuke kuwa inabidi kununuliwa sio kuchukua tu. sasa kama kuna mtu au mfanyabiashara alikuwa anajua bei ya rada na akakaa kimya bila kusema huo ni ujinga wa hali ya juu, na tukumbuke kuwa penye biashara kuna wafanyabiashara wa aina tatu, mwenye mali, mtu wa kati na dalali. sasa kama utaenda dukani kwa ajili ya kununua kifaa fulani na ukakuta dalali, atakupa bei ya juu, na pale utakapoenda ukakuta mtu wa kati atakupa bei ya juu, ila kama ukienda dukani na kukuta mwenye duka na mali ni yake atakuuzia kwa makubaliano mtakayokubaliana. na stakabadhi utapata.

Sasa nashangaa wanaopiga kelele kuhusu rada, sijui warudishe hela na maneno mengi tangu lini umenunua kitu kupitia mtu wa kati dalali na mwenye mali na kupata kifaa chako ukaenda kumdai dalali na mtu wa kati.

Tujifunze kutokana na makosa sasa. na tukumbuke nchi hujengwa na mwanachi, tuache kuongea sana. fanyeni kazi kwa bidii na kusoma kwa ajili ya kunufaika wewe mwenyewe na nchi yako sio kusoma kwa ajili kujibia mtihani na kuonekana umefaulu kumbe hakuna kitu, sasa kuna wasomi wangapi lakini hakuna walichofanya zaidi ya kuuza nyumba ili waweke heshima bar?
 
maana yake kuwe na malengo, vitendo, na kufikia lengo.
tuache kuchanganya siasa na uongozi, siasa na maisha, siasa na uhandisi na siasa na fizikia.

nidhamu ndio kila kitu katika kujenga taifa, unaposema kiongozi yule hafai maana yake na wewe hufai, kwanini? kumbuka wewe ndiye uliyemuweka pale

hii ndio mzee (yes sir) lazima iwepo kutokana na kutojikinga toka mapema,

mfano unapanda daladala imejaa sana tena sehemu isiyo kituoni, bahati mbaya daladala hiyo ikapata ajali nakuumiza watu wengi, utaona sasa walewaliokuwa ndani ya ile daladala wanaanza ndio tena alijaza sana, sasa kwanini ulipanda au kwanini hukukataa asiongeze watu, ukiona shida imekuja lawama nyingi, nadhani kidogo naeleweka
 
Mikataba imekuwa siri.Na wanaoielewa wanafichiana siri ya uharibifu wao au wanajua na wao wanahusika.Mpaka tutakapoweza kusema hapana ndiyo tutakapo heshimika na kufanya mambo ya kuiletea Nchi maendeleo ya kweli na wananchi wote tukafaidika.
 
Na nina hisi kuwa watu wengi hatujui rushwa maana yake ni nini, sidhani katika wote hapa ndani ya forum hakuna asiyetoa au kupokea rushwa kwa kivyovyote.

tunapozungumzia rada. Ni chombo kinachosaidia mambo mengi ya kiusalama na mengine mengi na ninahisi kwa bei yeyote ile ilikuwa ni halali kuipata hiyo rada, sasa tukumbuke kuwa ile ni shida ya serikali ambayo ni sisi wenyewe kwajili ya usalama wetu wenyewe na mambo mengine.
Kwa kifupi hoja yako inaelekea kwenye kuunga mkono upokeaji wa rushwa kwa kauli kuwa hakuna mtu kwenye forum hii ambaye hapokei rushwa (hisia tu) na wewe ukiwa mojawapo. Vile vile, kwa kuwa tunahitaji rada, basi tuinunue kwa bei yoyote ile. Unayoyasema ndivyo unavyofanya katika maisha yako ya kila siku? Ajabu!!
 
Mujydebubyz,
Haya maneno unasema kwa akili zakoa ama ndivyo unavyofikiria kuwa.
Yaani rada tumeinunua bila risiti? kiasi kwamba unaanza kufananisha na ununuzi wa shati mtaa wa Kongo.
Vipi na kwa taarifa yako huku Ulaya kuna vitu hununuliwa na kuridishwa madukani maadam kuna guarantee fulani.
Mbona uantuletea siasa za Kikomunist hapa kwani huyo rais ndio hasemwi akikosea kitu?
Mshikaji tafuta uwanja (mada) size yako haya maji marefu sana kwako!
 
Habari Wanaforum leo niemkuja na hii habari ambapo Rais Kikwete amtetea Mkapa, Kabla hatujapata habari kamili, picha hiyo ni updates ya ziara ya Kikwete kutoka kwa mtandao wa vijana 'wetu' wa KikweteShein.com au JakayaKikwete.com :-

Jakaya_Kikwete_2_121.jpg

The President of the European Commission,Mr Jose Manuel Barroso welcomes President Jakaya Mrisho Kikwete to the EU Headquarters in Brussels Belgium this morning.The two leaders later held a press conference in which the EU President pledge continued cooperation with tha Tanzanian government Praising President Kikwete's insights on various challenges facing Tanzania.On his part President Kikwete pledged continued cooperation with the commission on implementing various joint development programmes. (Picha na Maro, Freddy) (Source JakayaKikwete.com)

Back to the topic:- Habari kutoka kwa mwandishi wa Rais kutoka huko Ubelgiji

SAKATA LA RADA... JK: Hakuna sababu Mkapa kujitetea

Kutoka gazeti 'letu' la Uhuru
Na Maura Mwingira, Brussels,Ubelgiji inasema


RAIS Jakaya Kikwete amesema haoni sababu ya Rais mstaafu Benjamin Mkapa, kusimama hadharani na kuzungumzia suala la ununuzi wa rada.

Kauli hiyo ya Rais Kikwete ilitokana na swali aliloulizwa na mmoja wa Watanzania wanaoishi mjini hapa, Abubakar Hiza, ambaye alitaka ufafanuzi kuhusu uchunguzi unaoendelea wa ununuzi wa rada na alitaka Rais mstaafu Mkapa, atoe tamko na aseme kwa uwazi na ukweli mambo yalikuwaje.

"Hivi mnataka mzee Mkapa atoe sauti, sauti kuhusu jambo gani? Mnataka aseme, aseme nini, naona tumwache mzee wa watu," alisema Rais Kikwete.

Aliyasema hayo alipokuwa akisalimiana na Watanzania wanaoishi Brussels, Ubelgiji, baada ya kuwasili kwa ziara ya kikazi ya siku mbili ambayo madhumuni yake ni kuonana na kuzungumza na Rais wa Jumuia ya Ulaya, Kamishna wa Maendeleo na Misaada ya Kibinadamu na Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Fedha katika Serikali ya Ubelgiji.

Alifafanua kuwa suala la uchunguzi wa ununuzi wa rada linafanywa na Serikali ya Uingereza, kupitia kitengo chake maalum, kwa kile kinachoamini kulikuwa na tuhuma za rushwa kati ya vongozi wa kampuni ya 'BEA System' na wakala aliyehusika na ununuzi wa rada.

Alisema Serikali ya Tanzania ilichofanya ni kutoa ushirikiano kwa taasisi hiyo, pale ilipoomba kuja nchini na kumhoji wakala huyo.

"Uingereza haituchunguzi sisi, wanaichunguza kampuni yao na viongozi wa kampuni hiyo, tena kampuni ya serikali, wanachunguzana wao kwa wao, kuona kama kuna tuhuma zozote za rushwa, na sisi tulitoa ushirikiano wote," alisema Kikwete.

Aliongeza kuwa suala hilo linaihusu Tanzania na serikali imelifikisha mikononi mwa Taasisi ya Kuchunguza Rushwa (PCB) ili nao wachunguze na kujua ukweli na kisha kutoa taarifa.

"Ikionekana wametudhulumu tutaona namna ya kufurukuta ndiyo maana tunashirikiana nao, matumaini yetu ni kwamba watatupatia taarifa ya nini kimetokea, lakini kwa kuwa tuna maslahi nalo na sisi tumewataka PCB walitazame suala hilo," alifafanua.

Aliongeza kuwa siyo uuzwaji wa rada kwa Tanzania pekee yake unachunguzwa, bali hata Afrika ya Kusini, Saudi Arabia nako kampuni hiyo inatuhumiwa kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Akijibu swali kuhusu kupanda kwa bei ya umeme na athari zake kwa mwananchi, hifadhi ya mazingira na suala la Net Group kushindwa kazi ya menejimenti, Rais Kikwete alisema upandaji wa bei ya umeme ulikuwa ni wa lazima kutokana na gharama za uzalishaji.

Alifafanua kuwa TANESCO ilitaka umeme huo upande kwa asilimia 25 lakini serikali ilikataa na kuruhusu asilimia hiyo sita ambayo alisema siyo kiwango kibaya sana, kulinganisha na asilimia 25 kwa kuwa hakuna njia mbadala.
Koraniga Mkora, alitaka serikali kuangalia upya ada ya sh. 770,000 wanayolipa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuwa ni kubwa mno nakupendekeza ipunguzwe ili wanafunzi wengi wapate elimu hiyo na taifa kujipatia wataalamu wa kutosha.

Akijibu hoja hiyo na ile ya kutaka wakuu wa mikoa wapigiwe kura na wananchi badala ya kuteuliwa na cheo cha mkuu wa wilaya kifutwe, Rais alisema uendeshaji wa serikali kokote duniani upo katika mifumo miwili.

Aliitaja mifumo hiyo kuwa ni viongozi wa kuteuliwa na wale wa kupigiwa kura, mifumo ambayo ndiyo inayotumiwa na serikali ya Tanzania.

Alisema tofauti na madiwani au wabunge, wakuu wa mikoa na wilaya ni wawakilishi wa serikali katika maeneo yao, hivyo watateuliwa na serikali badala ya kupigiwa kura na wananchi na kuwa cheo cha mkuu wa wilaya hakiwezi kufutwa.

Kuhusu ada ya sh. 770,000, alisema hiyo siyo ada kamili waliyotakiwa watoe kwa kuwa serikali imefidia sehemu iliyobaki.

Alisema serikali haiwezi kupunguza ada hiyo kwa sababu imeshafanya mengi ya kutosha katika kusaidia wanafunzi.

Katika hatua nyingine, Shila Malegesi, aliitaka serikali kutoharakisha katika uundwaji wa Shirikisho la Afrika Mashariki, kwa kile alichosema kuwapo tofauti kubwa na za msingi kati ya Tanzania na wana jumuiya wengine.

Alisema asingependa kuwapo kwa shirikisho hilo na kuwa: "Uundwaji wa shirikisho ni suala nyeti, Watanzania ni wastaarabu sana kuliko hao tunaotaka kuungana nao. Serikali yetu lazima ilipe umuhimu wa pekee kabla ya kufikia uamuzi."

"Hivi sasa tu serikali haitoi upendeleo kwa Wazalendo, tunashuhudia wageni wakipata ajira, kwa nini tusifanye kama wenzetu wa Ulaya ambao mtu wa nje hapati kazi kirahisi," alisema Malegesi.

Malegesi pia alilalamika kwamba tovuti ambayo wananchi wameshauriwa kupeleka maoni yao kuhusu shirikisho lao, haipatikani kwa urahisi na hivyo kufanya maoni yao kutowafikia walenga na kuchapishwa kwenye vyombo vya habari.

Akijibu hoja hiyo, Rais Kikwete alisema serikali itayashughulikia kwa ukamilifu maoni yote yatakayotolewa na wananchi na kutafakari mwelekeo muafaka wa uundaji wa shirikisho na aliwataka wananchi kutoogopa kuwasilisha maoni au hisia zao.

Watanzania hao, walimpongeza Rais Kikwete kwa hatua mbalimbali anazochukua katika kuwatumikia wananchi, kupambana na vitendo vya rushwa, ujambazi, elimu na uboreshaji wa mishahara ya watumishi wa umma na kuwa sasa wafanyakazi serikalini wanajivunia kufanya kazi serikalini.

Rais Kikwete aliwahimiza Watanzania hao kutosahau nyumbani kwa kuchangia maendeleo ya nchi yao na familia zao, kuheshimu sheria za nchi wanazoishi na kutojihusisha na vitendo vya uhalifu
 
Adelina: Mwanangu anateseka mwaka wa tatu sasa

Na Festo Polea

KAMA kuna siku ambayo itabaki kuwa katika kumbukumbu ya Adelina Luhungu ni Novemba 10, 2003. Hiyo ni siku ambayo iliandika historia mpya ya matatizo anayokabiliana nayo leo ambayo yamebadili kwa kiwango kikubwa mustakabali wa maisha yake. Awali, kama ilivyo kwa wazazi wengine, siku hiyo ilitarajiwa kuwa ya kumbukumbu njema yenye stahili ya kusherehekewa kila mwaka kwani ndiyo aliyojifungua mtoto wake, Neema John katika Hospitali ya Taifa Muhimbili. Tangu alipojifungua mtoto huyo hadi leo amekuwa akihangaika naye kutokana na matatizo makubwa ya kiafya ambayo yanamlazimu kusaka kwa kiwango cha chini kabisa kiasi cha Sh 94,000 kila mwezi kuhudumia vinginevyo maisha ya mwanae huyo yanakuwa hatarini. Simulizi ya chanzo cha matatizo ya mama huyo ambaye anasema kwamba hana kipato cha kumwezesha kukabiliana na mahitaji yake na ya mtoto wake kila mwezi ilianzia katika Hospitali ya Wilaya ya Ilala ya Amana. Anasema baada ya kupata uchungu, alikwenda hospitalini hapo ambako hakupata huduma ya haraka. “Kutokana na kukaa sana na maumivu nikihangaika kwenye benchi mtoto wangu alishuka kutoka kwenye nyonga nikajitahidi kujizuia na kupiga kelele kwa na uchungu lakini haikusaidia kitu kwani mtoto alikuwa mkubwa (kilo nne na gramu 900), kupita uwezo wangu kwani kipindi hicho nilikuwa na umri mdogo wa miaka 20,” anasema. Kutokana na kucheleweshwa huko, alilazimika kukimbizwa Muhimbili ambako anasema kwamba madaktari walimweleza kwamba mtoto wake huyo asingeweza kupona kwa kuwa alikuwa amekandamizwa na nyonga kiasi cha kuathiri ubongo wake. "Wengine walinieleza kwamba kupona kwa mtoto wangu kutatokana tu na uwezo wa Mungu..."

Alipofikishwa Muhimbili alikimbizwa katika chumba cha operesheni ya moja kwa moja... "Alipozaliwa siku ya kwanza hakulia na madokta (madaktari) wakasema kuwa hana fahamu. Walimwekea mipira ya hewa ya oksijeni kwa siku 30 hapo hali yake ikawa ikirudi taratibu na kuendelea na mazoezi. Hali ya mtoto wake iliendelea kuimarika japo kidogo huku akiendelea na mazoezi Muhimbili. Wakati wote huo kilichokuwa kikimsononesha ni maradhi ya mwanae na kuwaza jinsi gani angeweza kupata tiba zaidi ili naye awe kama watoto wengine. Mawazo ya wapi atapata fedha za kumhudumia kama ilivyo sasa hayakuwapo kwani mumewe, John Msewe, alikuwa hai na alikuwa amebeba jukumu hilo kikamilifu. Lakini Januari, mwaka jana alipatwa na janga jingine kubwa ambalo halina tofauti katika kumbukumbu kama lile la Novemba 10, 2003. Mumewe huyo tegemeo, alifariki dunia ghafla katika ajali. Basi la Coaster alilokuwa ameabiri lilizama katika Mto Wami, eneo la Dakawa, Morogoro. Tangu siku hiyo hadi leo, maisha yake yamekuwa magumu, yaliyojaa mashaka, dhiki na kila aina ya masahibu. Mama mwenye nyumba aliyekuwa akiwategemea katika malipo ya kodi, sasa amegeuka kuwa mfadhili na tegemeo lake kuu. Baada ya kushindwa kumudu kulipa gharama za chumba katika nyumba hiyo huko Ukonga Majumba Sita, mama huyo aliamua kutoa jiko lake na kumpa hifadhi, sehemu ambayo anasema kwamba ndiko anakojihifadhi. “Sasa naishi kwa kuchangiwa na wana jumuiya ya Mtakatifu Getruda Ukonga, maeneo ya Karakata. Inanichangia fedha za kuweza kupata chakula lakini nayo inachoka kwani michango kwa kila siku inashindikana. Hali inazidi kuwa mbaya. “Tangu afariki mtu niliyekuwa nikimtegemea kwa kila hali, maisha yangu sasa yamekuwa magumu mno kwani mtoto ndiyo ana matatizo nami sina kazi wala biashara yoyote," anasema na kuongeza: "Hivyo nikalazimika kuuza vitu vyote vya ndani ili aweze kupata fedha za chakula.” Anasema shemeji yake aliyebaki ni mdogo kwake ambaye naye hana uwezo wa kumsaidia kwani yupo na wazazi wake akiendelea kuwasaidia huko mkoani Morogoro. Hivi sasa licha ya kufuta ndoto za kumtafutia mtoto wake huyo matibabu zaidi, hata nauli ya kumpeleka Muhimbili kila wakati kufanya mazoezi ni tatizo kubwa. Kwa sasa mtoto huyo anapatiwa huduma ya mazoezi katika kitengo cha CCBRT, na Muhimbili.

“Mazoezi ya siku moja kwa mtoto hayamsaidii ipasavyo. Naomba watu wenye uwezo wanisaidie kupata vifaa ili niweze kumfanyia mazoezi nyumbani. Anavitaja vifaa hivyo kuwa ni kiti cha kumsaidia kuwa na uwezo wa kukaa, kiti cha matairi, kifaa cha kukakamaza shingo na uti wa mgongo na kifaa cha kumsaidia kutembea. Anasema baada ya kuangaika kwa kipindi kirefu, alikwenda katika vituo vya televisheni kuomba msaada. Anasema alipata msaada ambao hata hivyo masharti yake yalimshinda kwani anasimulia kuwa walijitokeza watu waliojitambulisha kuwa ni walokole na kumtaka aokoke ili wamwombee lakini kwa kuwa hakuwa na imani hiyo, aliamua kuomba msaada kwingineko. Huko nako alikumbana na masahibu mengi, alikumbana na baadhi ya wanaume wakware ambao badala ya kumpatia msaada wa kibinadamu, walimtaka kimapenzi kwanza. Hakuwa na nafasi ya kukata tamaa, aliendelea kuomba misaada na wasamaria wachache walijitokeza akiwemo Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba na kumsaidia fedha za kununulia dawa ambazo anasema zimekwisha. Mara nyingi wengi wetu tumezoea kukimbilia vijijini tulikosaliwa mara maisha yanapokuwa magumu, lakini hali ni tofauti kwa Adelina. Kwanza hajui mzazi wake alipo baada ya kuambiwa kwamba alikwisha hama kwao Peramiho, Songea. Lakini hata kama angekuwa Peramiho, asingeweza kumudu kumsaidia kutokana na hali yake kwani hana kipato kikubwa licha ya kukabiliwa na ulemavu wa macho. “Mama alifariki mwaka 2001 na baba ni kipofu. Baada ya kifo cha mama alipata mke mwingine na akahamisha makazi hivyo sijui alipo hata maisha yake sijui. Sasa kama yupo hai au vipi, nikienda Songea nitakaa kwa nani!” anasema Adelina kwa majonzi. Anasema baada ya kifo cha mama yake baba yake alianza kuumwa kichwa kwa muda mrefu macho yake yakawa yanatoa machozi hali iliyoendelea kwa muda kabla ya kumpotezea kabisa uoni wake. Aliondoka vipi Songea? Anasema alitambulishwa kwa mama mmoja anayemkumbuka kwa jina moja tu la Getruda kwamba ni ndugu ya mama yake katika ukoo hivyo akawa akimwita mama mdogo. Anasema mama huyo alimchukua kutoka Songea na kumpeleka Morogoro kwa ahadi ya kumsomesha lakini badala yake aliishia kufanya kazi na baadaye akamtafutia mume. Adelina anasema mama huyo na jirani yake walipanga mbinu za kumuoza akiwa bado na umri wa miaka 14 na kipindi hicho anasema alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa uvimbe wa shingo. Anasema walimhadaa kwamba wanampeleka kufanyiwa operesheni kumbe walikuwa wakimpeleka kwa mwanaume aliyekuwa na umri wa miaka 48! "Badala ya kupelekwa hospitali nilifikishwa katika chumba cha mwanamume lakini hatukumkuta na walimtaka amsubiri 'daktari' na kuwa angerudi siku yoyote kumpatia huduma. Baada ya wiki kadhaa mwanamume huyo 'daktari' alirejea lakini badala ya kumpatia tiba alimlazimisha kufanya naye tendo la ndoa huku akimtisha kuwa atamka panga.

“Kutokana na vitisho vya mwanamume huyo niliyelazimishwa kuolewa naye niliogopa, akanitenda nilipata maumivu makali,” anasema kwa machungu. Mama yake Adelina hakuwa na familia kubwa, walizaliwa wawili tu, yeye na kaka yake (mjomba wake Adelina), ambaye anasema hakuwahi kumwona kwani alifariki hajazaliwa. Anasema katika familia yao walizaliwa watatu, kaka yake yupo Malinyi, Morogoro ana familia na watoto watatu na dada yake yupo Mang’ula huko huko Morogoro naye ameolewa na ana familia ya watoto saba. Kutokana na kutokuwa na uwezo kifedha, ndugu zake hao humsaidia kipindi cha mavuno tu kwa kumpelekea mavuno waliyolima lakini sio fedha. Anasema hivi sasa mtoto wake Neema anaonyesha dalili za kupata fahamu kwani Januari 29 mwaka huu alipatwa maradhi ya kifua na alipompeleka hospitali alichomwa sindano na kulia kwa nguvu jambo ambalo awali halikuwa likimtokea. Anakumbuka kauli ya madaktari kwamba mtoto wake anaweza kurudi katika hali ya kawaida taratibu kama ataweza kufanyishwa mazoezi mara kwa mara. “Ninachoomba kwa sasa nipate sehemu ya kulala yenye uhakika, nipate dawa za kumwezesha mwanagu apate uwezo wa kawaida na vifaa ili apate mazoezi ya kila siku,” alisema Adelina.
 
jamani someni kwanza kabla hamjaposti.. mada hiyo inapostiwa mara tatu leo hapa.. (angalia mada ya "Suala la Rada"....
 
Kwa maoni yangu Mkapa ana maswali mengi ya kujibu. Maswali yenyewe ni kama yafuatayo.

1.Nani aliyemteua huyo mdosi aliyelipwa bilioni 12 kuwa gent wa ununuzi wa Rada na ndege ya Rais? Je zabuni zilitangazwa kwenye gazeti gani?

2. Kampuni ya shemeji yako Simu 2000 ndiyo iliyowaleta Net group Problems ili waendeshe Tanesco, je zabuni iliyowapa ushindi hao simu 2000 ilitangazwa wapi na makampuni gani mengine yaliyoshiriki?

3. Kampuni ya shemeji yako simu 2000 ndiyo iliyopewa usimamizi wa uuzaji mali mbali mbali za TTCL, je makampuni gani mengine yaliyoshiriki kwenye zabuni hiyo?

Viongozi wa Tanzania mna haja ya kujifunza kwamba nyinyi sio malaika au miungu watu kwamba hamfanyi makosa. Mnawaambia wabunge na wanachi wawakosoe pale ambapo mmekosea, lakini ni wagumu mno kukubali makosa yenu. Mfano ni kasheshe ya kiwanja cha Rose Garden ambapo bwana magufuli hakubali kama amefanya makosa alipopindisha maamuzi yaliyofanywa na madiwani.

Mkapa una maswali ya kujibu mengi tu, kama wewe ni muwazi na mkweli basi huna haja ya kuogopa kukaa masaa mawili au hata zaidi kujibu maswali yote kuhusiana na awamu yako.

~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*




Mkapa asisakamwe kwa rada - Kikwete
Titus Kaguo, Brussels
HabariLeo; Friday,February 23, 2007 @00:07

RAIS Jakaya Kikwete amesema haoni sababu ya Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin William Mkapa kusimama hadharani na kuzungumzia ununuzi wa rada inayotumika Tanzania ambao unadaiwa umegubikwa na harufu ya rushwa.

Kauli hiyo ya Rais Kikwete ilitokana na swali aliloulizwa katika mkutano na Watanzania wanaoishi Ubelgiji kuhusu uchunguzi unaoendeshwa na Serikali ya Uingereza juu ya ununuzi wa rada na pendekezo kwamba Rais mstaafu Benjamin Mkapa atoe tamko kuhusu kilichotokea.

Rada hiyo ilinunuliwa mwaka 2000 kwa gharama ya dola za Marekani milioni 40 kutoka kwa kampuni ya BAE ya Uingereza, huku yakiwapo madai kuwa gharama hiyo ilikuwa ya juu kwa asilimia kama 30 na kwamba dalali wa ununuzi huo alilipwa kiasi kikubwa cha fedha ambazo ziliwekwa kwenye akaunti ya benki moja ya Uswisi.

“Hivi mnataka Mzee Mkapa atoe sauti, sauti kuhusu jambo gani? Mnataka aseme, aseme nini? Mimi naona tumwache mzee wa watu,” alisema Rais.

Alikuwa akisalimiana na Watanzania wanaoishi Brussels, Ubelgiji, baada ya kuwasili kwa ziara ya kikazi ya siku mbili ambayo madhumuni yake ni kuonana na kuzungumza na viongozi wa Jumuiya ya Ulaya na wa Serikali ya Ubelgiji.

Rais alisema kwamba suala la uchunguzi wa ununuzi wa rada linafanywa na Serikali ya Uingereza kupitia kitengo chake maalumu, kwa kile tunachoamini kwamba kulikuwa na tuhuma za rushwa kati ya viongozi wa kampuni ya BAE System na wakala aliyehusika na ununuzi wa rada hiyo.

Alieleza kwamba ilichofanya Serikali ya Tanzania ni kutoa ushirikiano na taasisi hiyo ilipoomba kuja nchini na kumfanyia mahojiano wakala huyo.

“Uingereza haituchunguzi sisi. Wanaichunguza kampuni yao na viongozi wa kampuni hiyo tena kampuni ya serikali, wanachunguzana wao kwa wao, kuona kama kuna tuhuma zozote za rushwa, na sisi tulitoa ushirikiano wote,” alisema. Alisema kwa kuwa suala hilo linaihusu Tanzania, serikali imelifikisha mikononi mwa PCB ili nao wachunguze na kujua ukweli na kutoa taarifa yake serikalini.

“Ikionekana wametudhulumu tutaona namna ya kufurukuta ndiyo maana tunashirikiana nao. Matumaini yetu ni kwamba watatupatia taarifa ya nini kimetokea, lakini kwa kuwa tuna maslahi nalo na sisi tumewataka PCB walitazame suala hilo,” alisema.

Akijibu swali kuhusu kupanda kwa bei ya umeme na athari zake kwa mwananchi wa kawaida na hifadhi ya mazingira, alisema upandaji bei ya umeme ulikuwa wa lazima kutokana na gharama za uzalishaji. Rais alisema kuwa awali Tanesco ilitaka umeme huo upande kwa asilimia 25 lakini serikali ilikataa na kuruhusu asilimia hiyo sita aliyosema si kiwango kibaya kwa kuwa hakuna njia mbadala.

Watanzania hao walimpongeza Rais Kikwete kwa hatua mbalimbali anazochukua katika kuwatumikia wananchi, kupambana na vitendo vya rushwa, ujambazi, elimu na uboreshaji wa mishahara ya watumishi wa umma. Walisema hivi sasa wafanyakazi serikalini wanajivunia kufanya kazi serikalini.
 
Mkandara,
kuwa na watu kama Mujy ndani ya system zetu ni disaster!!!
Hebu jaribu ku-imagine, huyo Mujy ndio yuko mezani (ndani ya system) ku-review mikataba ili ashauri wakuu wake..............duuuhh!!, sasa huyu Mujy ndio typical situation ya watu wengi waliopo kule.........., alimradi mkono waenda kinywani ati.........
 
hii thread nadhani ilikuwepo, na mie niliiweka ikatolewa hivyo usishangae ukaona na hii pia inatolewa ! Lakini sikulaumu maana kama thread ikiwa na replies nyinyi mno kupita kiasi thread nzima inakuwa inaboa "boring", na hivyo members wengine huona uvivu kusoma thread yoote na hivyo wengine hata huamua kufungua topic bila ya kujua kwamba hiyo topic ilishawekwa katika thread nyingine. Ni hoja tu !!!!!

"Wenyewe" humu JF watakupigia kelele wewe Babu Ataka Kusema shauri yako........lol
 
KadaMpinzani,

Ndugu yangu sio kama wawepo huko akina Mujy!

Ukweli ni kwamba hawa jamaa ndio wameshika nafasi hizo.. yaani viongozi kibao serikalini wameshika nafasi hawana wanalo fahamu kabisa kuhusu nchi hizi. Kuna mmoja nilibishana nae kuhusu Richmond akanambia ati ana hakika hiyo kampuni ndiyo ina supply Umeme -Houston na Dallas!..
 
Tahariri from Daima

KAMA kuna jambo linalogusa hisia za Watanzania wengi kwa sasa, ni madai ya kuwepo kwa rushwa katika ununuzi wa rada, uliofanywa na Serikali ya Awamu ya Tatu.

Sisi wa Tanzania Daima, tunaamini kuwa jambo hili linawapa presha wananchi, viongozi, na hasa wale waliohusika na mpango wa kununua rada hiyo. Tunazo sababu za kuamini kuwa, madai ya kuwepo kwa mianya ya rushwa katika ununuzi wa rada yanawapa presha Watanzania.

Wakati serikali ya awamu ya tatu inatangaza uamuzi wake wa kununua rada hiyo aghali sana, Watanzania wengi walikuwa katika hali ngumu kiuchumi, na baadhi yao waliilalamikia hatua hiyo ya serikali. Walitaka mpango huo usitishwe au ubatilishwe, inunuliwe rada nyingine yenye ubora unaostahili kwa nchi yetu na isiyokuwa na gharama kubwa. Kilio hicho, hakikusikilizwa, viongozi walisisitiza kuwa ni lazima rada hiyo inunuliwe. Walitoa sababu kadhaa, baadhi ya sababu hizo ni kuwa, ina umuhimu mkubwa kwa taifa na ubora wake ni wa uhakika.

Pamoja na viongozi hao, mkuu wa nchi wa wakati huo, Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, akiwa ziarani nchi za nje, naye alikipuuza kilio cha wananchi wake kuhusu kusitishwa kwa mpango wa kununuliwa rada. Alisisitiza kuwa ni lazima inunuliwe kwa ajili ya maslahi ya taifa. Na ili kuwaondoa wasiwasi waliokuwa nao Watanzania na watu wengine duniani kuhusu kununuliwa kwa rada hiyo, Mkapa aliutangazia umma kuwa, katu mpango wa ununuzi wa rada haukuwa na chembe, wala harufu ya rushwa.

Kwa shingo upande, wapinzani wa mpango huo walikaa kimya, kwa sababu hakukuwa na jinsi ya kuliepusha taifa na matumizi makubwa ya fedha kama ilivyokuwa imekusudiwa na wakubwa, Mkapa akiwa kinara wao. Tunaamini kabisa kwamba, kutekelezwa kwa mpango huu kulipandisha presha za Watanzania wengi ambao walilazimika kukabiliana na makali ya uchumi kwa namna moja au nyingine. Sababu nyingine inayowapa ‘presha’ wananchi na viongozi, ni kuibuka kwa madai ya kuwepo kwa rushwa katika ununuzi wa rada hiyo.

Ni wazi wananchi wengi sasa wako roho juu, presha zimewapanda, wanataka kujua ni viongozi au watu gani waliohusika na ununuzi huo wa rada ambao sasa unadaiwa kuwa ulitekelezwa kwa mbinu chafu. Kwa viongozi, hasa wale walioguswa na mpango huu, nao tunaamini presha iko juu, wana wasiwasi kama uchunguzi unaofanywa na makachero wa Serikali ya Uingereza utawagusa au la.

Lakini presha kubwa zaidi kwa Watanzania katika sakata hili kwa sasa, inasababishwa na Rais Jakaya Kikwete. Tunasema hivi kwa sababu imekuwa vigumu kumuelewa kama ana nia ya dhati ya kuruhusu ukweli uchukue nafasi yake katika kashfa hii. Kinachotusukuma kusema hivi ni kauli zake, tangu kuibuka kwa tuhuma hizi. Anaonekana wazi kuwa hayuko tayari kuona baadhi ya watu waliohusika na suala hilo, hata kama wanahusika wakiwajibishwa ama kuchukuliwa hatua nyingine stahili.

Hatumuhukumu Rais Kikwete, lakini tunashawishika kuamini hivyo kutokana na kauli yake ya hivi karibuni aliyoitoa akiwa nchini Ubelgiji kuwa, Rais Mkapa aachwe, asibughudhiwe kuhusu suala hilo. Tunamuomba rais atuelewe kuwa, kauli zake za kuwakingia kifua wote wanaodhaniwa kuwa walihusika kwa namna moja au nyingine katika ununuzi wa rada hiyo, zinawatia presha Watanzania.

Na ili presha hii isiwepo, tunamuomba aache kuwachukulia wengine mizigo yao. Aache kila mmoja abebe mzigo kuhusu sakata hili la rada.
 
JK is one those thieves sasa unategemea nini ? Ulitegemea kweli rushwa na uharamia mwingine nupungue kwa kuwa JK is now the Prez ? Jamani tumefikwa na makubwa CCM wanatumaliza huku tunacheka .
 
Lunyungu,

Tuhuma nzito! DO YOU HAVE A PROOF? That can help otherwise mzee badili maandishi kidogo.

Hope nimeeleweka.
 
kama wizara ambayo alikuwa naiongoza kabla ya kupata uraisi ilikumbwa na ubadhirifu mkubwa wa fedha.sasa tumempa nchi,ambayo inawizara kibao hapa tutegemee nini kama siyo aliyosema lunyungu
 
Katibu Tarafa,
Well said. Tusidanganywe na nice smiles na uungwana.
 
Back
Top Bottom