The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

Kwa mujibu wa kumbukumbu za shughuli za Bunge la Mamwinyi la Uingereza, ambako mjadala mzito uliibuka Jumanne wiki hii, Rais Mkapa alitetewa na aliyekuwa Waziri wa Masuala ya Maendeleo wa Uingereza, Bibi Clare Short

Akinukuliwa kwenye taarifa hizo za Bunge, Bibi Short alitoboa siri akisema mkataba wa awali ambao ndio baadaye uliokuja kuifanya Tanzania inunue rada kutoka kampuni ya BAE Systems ya Uingereza, ulisainiwa kabla Bw. Mkapa hajaingia madarakani, hivyo kuifanya Serikali yake kutokuwa na chaguo zaidi ya kuutekeleza

Kwa mujibu wa kumbukumbu hizo za Januari 30 mwaka huu, Bibi Short alikaririwa akisema: "Niliamua kupunguza kiasi cha mkopo tuliokuwa tumeiahidi Tanzania kwa kiasi cha pauni milioni 10 na nikaamua kwenda kuonana na Rais Mkapa, mtu ambaye ninamheshimu sana na aliyeifanyia mambo makubwa nchi yake.

"Akaniambia kwamba mkataba wa awali wa ununuzi wa rada, ulikuwa umeshasainiwa kabla yeye hajaingia madarakani, tayari malipo ya awali yalishatolewa na kulikuwa na kipengele kinachoibana Serikali kwamba ikiamua kujitoa katika mkataba huo, ingewajibika kulipa gharama kubwa," alisema Bibi Short.

Bibi Short aliliambia zaidi Bunge, kuwa baada ya kusikia kauli hiyo ya Rais Mkapa, aliona hakuna jinsi ya kuuzuia mkataba huo, zaidi ya kutumia sheria za Uingereza kuinyima leseni ya usafirishaji kampuni ya BAE.

Akijibu swali la mbunge, Bi. Susan Kramer, aliyeshangaa kusikia kuwa Rais Mkapa alikuwa na mawazo ya kuangalia namna ya kuachana na mkataba huo wa rada, wakati kuna taarifa nyingi kuwa Serikali hiyo ndiyo iliyokuwa ikilazimisha ununuzi huo, Bibi Short alieleza tatizo kuu lililomsibu Rais Mkapa.

Akizungumzia tatizo lililomfanya Rais Mkapa akose nguvu za kisiasa na kiushawishi, na hata kujenga msimamo wa kuepuka rada hiyo, Bibi Short aliliambia Bunge hilo kwamba "Rais Mkapa ni kiongozi maridhawa, Rais safi, lakini hakuwa na nguvu za kisiasa na alijikuta ameurithi mkataba huo.

"Kama Serikali ya Uingereza ingemsaidia kwa kuzuia utoaji wa leseni ya kusafirishwa kwa mtambo huo kwa kutumia kanuni ya 8 (inayozuia mauzo ya vifaa vya gharama kubwa kwa nchi maskini) ni wazi angekuwa mtu mwenye furaha, lakini mkataba ulikuwa na vifungu vya kulipa gharama kama angeuvunja."

Kwa mujibu wa Bibi Short, akimtetea zaidi Rais Mkapa, aliliambia Bunge kuwa kiongozi huyo alipoingia madarakani, mkataba wa awali kuelekea ununuzi wa rada, ulishalipiwa pauni milioni 5.

"Jambo la msingi kufahamu ni kuwa kwa wakati huo, Uingereza ndiyo ilikuwa na nguvu (ya kuweza kusaidia kuuzuia mkataba huo). Niliongea na Waziri Mkuu (Tony Blair), Waziri wa Fedha na pia Waziri wa Mambo ya Nje, Bw. Robin Cook. Mawaziri walikubaliana nami kwamba tuupinge mradi huo.

" Lakini baadaye kikaitishwa kikao cha ghafla cha mawaziri ambapo mawaziri wadogo walishinikizwa kuwa kwa lolote liwalo, waunge mkono uuzaji wa rada...na hapo ndipo tukabaini kuwa kumbe kulikuwa na mazungumzo ya siri ya kulisukuma mbele suala la rada. Wizara ya Ulinzi (ya Uingereza) iliridhia suala hilo."

Bibi Short alisema wakati Serikali ya Uingereza ndiyo iliyokuwa na uamuzi wa mwisho wa kuzisaidia fikra za ndani za Rais Mkapa, yenyewe ikawa ikisaidia kuhakikisha inaweka mazingira ambapo hata suala la leseni kama lisingetolewa, bado mkataba ungefikiwa mwisho kwa rada kupelekwa Tanzania.

"Kwa sababu hiyo, unaweza kusema kirahisi tu kwamba tusingeipa mkopo tena Tanzania kwa sababu kulikuwa na rushwa, lakini nchini humo kuna watu wengi maskini na wenye njaa. Mikopo ni kwa ajili yao. Kuna mtu mwingine aliyeiba pesa, kwa nini tuwaadhibu maskini kama vile wao ndio waliotenda maovu?" alihoji

Katika kikao hicho, Bibi Short akizungumza na kuonesha dhamira ya ndani zaidi ya Rais Mkapa, alithibitisha mbele ya Bunge hilo, kuwa kutokana na mtazamo wake wa ndani juu ya rada, ndiyo maana kiongozi huyo alifikia hatua, baadaye, akapitisha uamuzi wa kuzuia ununuzi wa awamu ya pili wa rada nyingine ambao mkataba wake haukuwa umesainiwa awali.

"Tufanye nini sasa? Hilo ndilo lililotutatiza. Rais Mkapa na mimi tulifikia makubaliano, kwamba kama alikuwa tayari kunihakikishia kwamba hataendelea na awamu ya pili ya ununuzi wa rada nyingine, tungeendelea kuipa misaada nchi yake.

"Nimekutana naye akiwa ameshaondoka madarakani na amenihakikishia kuwa ahadi hiyo inatimizwa. Ingawa alishindwa kuzuia mkataba wa kwanza, lakini angalau sasa fedha zaidi hazitapotezwa," alisema Bibi Short.

Aliliomba Bunge lisaidie jitihada na mtazamo wa Rais Mkapa wa kukataa Serikali ya Tanzania kuuziwa rada nyingine.

Kauli hii ya Bibi Short ni ya kwanza ya mtu aliyeufahamu kwa undani zaidi mtazamo wa Rais Mkapa kuhusu sakata la rada na akaamua kuuweka bayana.

Pia kauli hiyo inaweza kuonesha, kwa mara ya kwanza ni kwa nini Bibi Short na Rais Mkapa, hata baada ya kuonekana hadharani kuwa walitofautina juu ya ununuzi wa rada hiyo, lakini bado walibaki marafiki. Kumbe wote walikuwa wakiamini katika jambo moja adhimu; kwamba rada ilikuwa gharama zaidi kwa Watanzania

JAMANI SASA INAMAANISHA KWAMBA MWINYI NAYE ALISHAMEGA KAMISHENI YA MKATABA WA AWALI?
 
Mpigakura,

Claire ugomvi wake ni serikali ya Blair. Anataka kutoa lawama kwa Mkapa
ili nguvu kubwa aielekeze kwenye serikali ya Blair.

Kama ni hivyo mbona sehemu ya pili ya rada ambayo ilitakiwa tununue, hatujanunua na sijaona tukilipa chochote?

Watu wanatufanya wendawazimu kwa kutuletea ujinga mwingi.

JK anasema itabidi serikali ya Uingereza warudishe pesa, wakati kipindi kile maneno yake na yale ya rais wake ndio yalitumiwa na serikali ya Blair bungeni ili kuweza kupitisha hilo deal. Tuliambiwa wakati huo hiyo bei ya juu mno, mbona hakulalamika? Anajifanya sasa ndio anajua bei ilikuwa juu?

Ni ujinga tu ule ule ambao unatuingizia hasara kubwa.
 
mmemsikia clare short ,akiongea kwenye house of lords amesema mkapa hakuwa na namna ya kuukwepa mkataba wa rada kwa kuwa aslikuta rais aliyemtangulia [mzee mwinyi] alishasaini mkataba na kulipa downpayment ya 5 million pounds ,na kulikuwa na vipengele vinavyosema anayejitoa inabidi alipe fidia kubwa,,,so kikubwa alichotegemea kujitoa ni kama serikali ya uk ingewanyima BAE kibali cha kuuza kwa kigezo cha uhuru wa serikali ya uingereza kuingilia manunuzi ya silaha ya nchi masikini...jambo ambalo halikufanyika...sasa kumbe list ndefu MZEE MWINYI naye ndani..uzuri nayeye yupo labda akipenda atatoa ufafanuzi..
 
1. Threads za mada
Admin labda ungeunga habari/nyuzi?/threads za hii mada ya rada iwe moja badala ya kutawanyika huku na huko.

2. JK kupotoshwa au kuzembea?
Kuna mahali kasema "...(BAE) inamilikiwa kwa asilimia 100 na serikali ya Uingereza...". Labda akagundua amekosea, akasema "...serikali ina hisa kubwa humo..."


3. Mzee Mwinyi, BM au JK?

Mkataba ulisainiwa wakati wa Mwinyi wakati huo JK alikuwa Waziri wa Fedha au Nishati na Madini?

"Brutus Wilfrem Mkirene" alikuta paundi milioni 5 zishalipwa.
 
Serikali ya UK haikuwahi na haitaweza kuwahi kuuza Rada.JK anatufanay wajinga wakati anajua the whole issue kwamba ni kampuni ambayo iko UK na si Serikali ya UK . Sasa anaomba UK ipi warudishe pesa ? UK Serikali ama UK ile kampuni ya kuuza silaha ambayo serikali ina sema ina share na kutoa kibali cha kuuza silaha ?Tuwekane sawa hapa JK sisi si wajinga fanya usanii lakni ujue miaka hii ni mingine .

Issue Rada JK anahusika kwa 100%
 
NI KWELI.....tena yuko kwenye top 10 za washutumiwa watarajiwa wa....
 
( Makala hii imechapwa katika gazeti la Tanzania Daima leo Jumapili. Picha ya maktaba)

Na Maggid Mjengwa

TUMESIKIA wabunge wa Uingereza wakiongozwa na mbunge wa kujitegemea mwanamama Clare Short, wakiichachafya serikali ya Bw. Tony Blair juu ya sakata la nchi yetu kuuziwa rada ya bei juu na pia rushwa kutumika katika ununuzi huo.Soma zaidi na angalia picha; http://mjengwa.blogspot.com
 
We need time frame ya hii Radar issue. If Mkapa was not involved, meaning he came in an found the deal was already at the table, why it took 7 yers of his presidency for the Radar to be delivered? Who signed for Radar before Mkapa became Raisi? was it Ali Mwinyi, Jakaya Kikwete, Pholo Sarungi or who?
 
The government has issued a statement on the controversial purchase of radar that has been the subject of raging debate in both Tanzania and the UK.

Defence and National Service deputy minister Omar Mzee told the National Assembly here yesterday that nobody would be spared once implicated in what is widely believed to be a dubious deal involving the acquisition of the radar from Britain.

Echoing President Jakaya Kikwete`s recent remarks, Mzee declared that Tanzania would not hesitate to lodge appropriate claims against all parties behind a purchase that cost the nation billions of dollars.

President Kikwete told the nation that Tanzania could claim compensation from the British government if it was discovered that the purchase of the radar was involved fraud or corruption.

`The government is conducting investigations so as to establish the truth behind the actual cost of the radar received from Britain. Appropriate measures will be taken against all those found to be behind the suspected hiking of the radar�s price tag,` announced the deputy minister saying the government was monitoring the unfolding situation very closely.

He was answering a question from Parmukh Singh Hoogan (Kikwajuni), who demanded explanation on the monitoring of navy docking in Zanzibar and Dar es Salaam, which requires the use of security equipment similar to the radar currently under serious discussion.

The radar purchase controversy has prompted heated debate in the UK, with some MPs wondering why poor countries like Tanzania should go for such expensive technology.

Mzee told the House that military delegations from European and other countries have continued to visit Tanzania for many years under special arrangements, adding that the government would always communicate with the visitors ahead of time `to ensure that everything is in place`.

`Tanzania has received navy ships from France, Germany, India, Pakistan, Kenya and South Africa for the purpose of exchange of expertise, strengthen bilateral relations and for tourist purposes,` he explained.

SOURCE: Guardian
http://www.ippmedia.com/ipp/guardian/2007/02/06/83842.html
 
Wanabodi,

Katika hii sakata ya Rada kuna KUNDI moja ambalo lilihusika moja kwa moja lakini limesahaulika kabisa. Kundi hili ndilo lenye nguvu (kwa siasa za bongo) kuliko hata Rais wa Nchi...nadhani sasa ni wakati wa kuangalia upande mwingine wa hili saga...kundi hili ni Maofisa wa Juu wa Jeshi Letu...yes our beloved JWTZ. Hawa walihusika moja kwa moja maana kifaa hicho kilichonunuliwa kilikuwa ni cha KIJESHI.

Sasa wanabodi hebu jiulizeni...kama wanajeshi walisema wanaitaka hiyo Rada kwa Gharama yoyote unadhani kuna mwanasiasa angesema No...hakuna si Mwinyi, Mkapa wala aliyekuwa Waziri JK. Ni kundi hili ambao wana majumba ambayo wala hawaishi humo pale London...hao wanasiasa kwa HILI tunawaonea tu.

Ukitaka kujua nani alihusika upande wa JWTZ tafuteni majina ya maofisa wa jeshi wenye nyumba London...hapo ndio pazuri pa kuanzia...kazi kwenu.
 
Hahahahaaaaaa!
YeboYebo hapo umetumbua jipu. Una focus nzuri sana mzee**Kwa kweli hili kundi lilisahaulika kabisaaa! Lakini ina maana kwamba TPDF hawakujua kwamba hiyo rada walishkishwa? au ni mambo flani ya kamisheni.
 
Wanabodi,

Katika hii sakata ya Rada kuna KUNDI moja ambalo lilihusika moja kwa moja lakini limesahaulika kabisa. Kundi hili ndilo lenye nguvu (kwa siasa za bongo) kuliko hata Rais wa Nchi...nadhani sasa ni wakati wa kuangalia upande mwingine wa hili saga...kundi hili ni Maofisa wa Juu wa Jeshi Letu...yes our beloved JWTZ. Hawa walihusika moja kwa moja maana kifaa hicho kilichonunuliwa kilikuwa ni cha KIJESHI.

Sasa wanabodi hebu jiulizeni...kama wanajeshi walisema wanaitaka hiyo Rada kwa Gharama yoyote unadhani kuna mwanasiasa angesema No...hakuna si Mwinyi, Mkapa wala aliyekuwa Waziri JK. Ni kundi hili ambao wana majumba ambayo wala hawaishi humo pale London...hao wanasiasa kwa HILI tunawaonea tu.

Ukitaka kujua nani alihusika upande wa JWTZ tafuteni majina ya maofisa wa jeshi wenye nyumba London...hapo ndio pazuri pa kuanzia...kazi kwenu.

Yebo Yebo,
Unaweza ukawa na hoja nzuri sana, lakini Tanzania bado hatujafikia huko. Vyombo vyetu vya usalama ni watu wa "Yes Sir" zaidi kiasi kwamba hata masuala yao mengi yanaamuliwa na wanasiasa. Wanaweza kuwa na mivyeo mikubwa na majina makubwa lakini mbele ya wanasiasa sichochote kile.
Kitaalam wanaweza kushauri kitu gani kinahitajika lakini kushinikiza hawawezi kwa sababu viongozi wengi wa ngazi za juu jeshini ni watu wakujikomba mno kwa wanasiasa, labda kwa matumaini siku moja ka u-DC au ka u-RC kanaweza kuwangukia. Kwa ujumla wanajeshi ni watu wakuangushiwa ka kamisheni kadogo tu baada ya kuwasaidia wanasiasa kufanya vitu vyao.
 
Mkapa tunakuomba ujibi maswali yafuatayo:

1.Je tangu lini Mbunge wa Uingereza Mama Claire Short amekuwa msemaji wako?

2. Je ni lini na wapi uliwaambia wananchi wa Tanzani kwamba ulikuwa hukubaliani na wazo la kununua rada kwa sababu ilikuwa na bei kubwa mno na uwezo wa nchi yetu ulikuwa ni mdogo kuafford rada hiyo? Maana mama Claire Short amedai kwamba ulikuwa unapinga ununuzi wa rada hiyo, je ulikuwa unampaka mafuta ya mgongo wakati Watanzania unawaambia hadithi tofauti?

3. Je mkataba wa kununua rada hiyo ulisainiwa wakati wa uongozi wa Mwinyi au uongozi wako? Tunataka ushahidi wa maandishi ili tuone mkataba huo ulisainiwa tarehe gani, mwezi gani na mwaka gani?

4. Je huyo Muhindi aliyekuwa agent wa ununuzi wa rada pamoja na ndege alichaguliwa na nani kuwa agent wa manunuzi hayo? Kuna zabuni iliyotangazwa? kama ipo ilitangazwa lini na kwenye gazeti gani la Tanzania? Na akina nani ambao walikuwemo kwenye kamati iliyoamua mshindi wa zabuni hiyo?

5. Kampuni ya Simu 2000 ambayo ni ya shemeji yako na watoto wake ambao ni wakurugenzi katika kampuni hiyo, ndiyo iliyohusika na mkataba wa kuwaleta Net Group ili waendeshe Tanesco, je zabuni hiyo ilitangazwa lini na wapi? Na ni nani waliokuwemo katika kamati iliyoichagua Simu 2000 kama mshindi wa kutafuta kampuni ya kuendesha Tanesco? Na ni kiasi gani cha pesa kilicholipwa kwa Simu 2000 kwa kuwaleta Net Group?

6. Pia Simu 2000 ndiyo ilikabidhiwa uuzaji wa mali zilizokuwa za TTCL, baada ya shirika hilo kubinafsishwa zikiwemo nyumba, magari, furnitures za majumbani na maofisini n.k. Je inajulikana ni mali ya kiasi gani waliyokabidhiwa Simu 2000? Je zabuni ya kusimamia uuzaji wa mali hizo ilitangazwa lini na wapi? Na ni akina nani waliokuwemo kwenye kamati iliyoichagua Simu 2000 kama mshindi wa kusimamia uuzaji wa mali hizo.

Mheshimiwa Mkapa, awamu yako uliita awamu ya 'uwazi na ukweli'. Sasa hivi kuna kiwingu kizito kilichotanda miongoni mwa Watanzania wengi kuhusiana na maamuzi yako mbali mbali yakiwemo ya mikataba ya uchimbaji wa madini, ununuzi wa Rada na ndege, na kampuni ya Simu 2000 ambayo inamilikiwa na shemeji yako. Sasa tuonyeshe Watanzania uwazi na ukweli ulionao kwa kutwambia ukweli wa mambo kuhusiana na kiwingu kilichotanda. Kumbuka siku zote panapofuka moshi, hapakosi....

His Excellency, the ball is in your court and we're very anxious waiting to hear from you.
~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*

Deodatus Balile


LEO nimeamua niandike juu ya sakata la ununuzi wa rada. Nakumbuka niliandika makala nyingi na habari juu ya suala hii miaka ya 2003/2004. Nakumbuka pia, uamuzi wa kununua rada uliwasilishwa bungeni na serikali ya awamu ya tatu kwa ajili ya kupiga muhuri na kubariki uamuzi uliokwishachukuliwa.

Aliyekuwa Waziri wa Mashauriano ya Kimataifa wa hapa Uingereza, Claire Short, alitofautiana kwa kiwango kikubwa na serikali juu ya uamuzi wa kukubali kuiuzia Tanzania rada kutoka Kampuni ya BAE Systems. Mwanamama huyu alikuwa akisisitiza kuwa bei ya rada ilikuwa kubwa na kulikuwa na mchezo mchafu katika mchakato mzima.

Rada hiyo iliyoelezwa kununuliwa paundi milioni 28 sawa na sh bilioni 40 wakati huo, ilitetewa kwa kiasi kikubwa na Rais (mstaafu) Benjamin Mkapa. Sitaki kurejea katika historia, lakini kwa ufupi nimkumbushe tu, kuwa Mkapa na maswahiba wake walinichukia kwa kuandika habari hizo kwa kiasi kikubwa.

Yupo mmoja simtaji leo, alipata kutoa kauli hii: “Kwani huyu Balile anayemwandama Rais Mkapa ni nani? Ni lazima aendelee kufanya kazi na gazeti hili?” Naamini sasa hivi baada ya kusoma maneno haya amejikumbuka mheshimiwa huyu mwenye uraia wa kutiliwa shaka, iwapo kweli ana uchungu na nchi yetu.

Niliendelea kuandika makala zangu na uhusiano wangu na mheshimiwa huyu aliyekuwa na nguvu kubwa katika awamu ya tatu japo hakuwa na wadhifa wowote rasmi zaidi ya ushauri, hadi tulipolazimika kukabidhiana mikoba, nikaondoka na taaluma yangu, naye akabaki na gazeti lake!

Mkapa mara kadhaa alivishambulia vyombo vya habari kwa kuandika alizoziita habari za uzushi. Hakusita kutuita wajinga, wapuuzi, wavivu wa kufikiri. Haya na mengi yalitokea tulipoandika habari za rada, ununuzi wa ndege inayodaiwa ina mafua, ambayo Rais wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete, amekataa kuitumia nje ya nchi kwa kuwa ni ya ghali.

Leo imebainika kuwa ununuzi wa rada ulikuwa ‘mchoro’. Wapo wakubwa walipewa pande la sh bilioni 12 zikaingia kwenye akaunti ya Mtanzania huko Uswisi. Hapa Uingereza moto umewaka. Chama cha Upinzani cha Conservative, kimeibana Serikali ya Tony Blair, iseme iliruhusuje uuzaji wa rada hiyo. Rais Jakaya Kikwete, anasema waliohusika atawashughulikia vilivyo na atadai tofauti ya malipo kutoka Serikali ya Uingereza.

Short naye amekiunga mkono chama cha upinzani. Amekwenda mbali zaidi akasema hata Waziri Mkuu mtarajiwa, Golden Brown, naye alipinga uuzaji wa rada hiyo kwa nchi masikini kama Tanzania, lakini hakusikilizwa. Maelezo yaliyokuwa yakitolewa nisiyojua yana ukweli kiasi gani ni kuwa uwezo wa rada yenyewe unaishia Kibaha!

Kikosi cha Kupambana na Ulaghai (SFO) nchini hapa, kimemweleza Short na kumwonyesha nyaraka kuwa kulikuwapo na rushwa katika mauzo ya rada hiyo. Bunge la nchi hii wiki hii limehitimisha mjadala kwa kusema kuwa baadhi ya maofisa wa Tanzania walihongwa kupitisha ununuzi wa rada hiyo.

Kati ya mambo waliyokubaliana ni kuwashitaki wote waliohusika na ununuzi au uuzaji wa rada hiyo. Hii wanasema inalenga kulinda uchumi wa nchi changa kama Tanzania dhidi ya viongozi maharamia.

Napenda kuamini Rais Mkapa anajua mpango mzima wa ununuzi wa rada. Katika hili ana jukumu la kulieleza taifa letu mchango wake na hatua alizochukua katika ununuzi wa rada. Mkapa aliitetea rada hii, akisaidiwa na maswahiba wake waliojifanya mabingwa wa ushauri.

Sisemi ina uhusiano, lakini tunasubiri pia Mkapa atutangazie mali zake baada ya kuachia madaraka, sawa na alivyofanya alipoingia madarakani. Tunapaswa kuelezwa sisi kama Watanzania, Mkapa anaishi wapi, ana nyumba ngapi ndani na nje ya nchi kama zipo, na alizipataje.

Narudia, sisemi haya ninenayo yamethibitishwa, lakini ni wasiwasi uliotanda miongoni mwa Watanzania. Anao maswahiba waliokuwa makarani tu mitaani, lakini leo ni matajiri wa kutupwa. Hawa nao wanapaswa kutueleza waliupataje utajiri na kwa utaratibu upi.

Naomba nieleweke hapa. Napingana na dhana ya watu kuwa masikini katika taifa na wala sichukii utajiri, ila sipendi utajiri unaopatikana kwa njia haramu. Utajiri unaopatikana kwa kukausha mishipa ya maendeleo kwa taifa letu haufai.

Sitanii, Mkapa anawafahamu vizuri hawa Wazungu. Wanaposema watawashtaki wote waliohusika, hawatanii. Wanamaanisha watafanya hivyo. Kama amesahau awaulize jamaa za akina Jenerali Augusto Pinochet, Saddam Hussein na Slobodan Milosevic!

Najua waliohusika na sakata hili la rada na baadaye ndege, sasa matako yanalia mbwata. Mkapa hawezi kuwa salama naye. Hata kama si yeye, lakini ni utawala wake unaonyooshewa kidole. Ni vyema asimame sasa na kusema ukweli ilikuwaje, kipi anakijua na kipi hakijui.

Ukimya haumsaidii. Inakuwa ni sawa na kufukia chemchemi kwa mchanga ukidhani maji yataishia ardhini. Kamwe hilo halitokei, maji huendelea kujaa na kumeza magunia ya mchanga. Nashauri mheshimiwa huyu afungue kabrasha, aeleze akijuacho sasa, badala ya kusubiri kuitwa kizimbani.

Tukio hili la Mkapa na serikali yake, liwe fundisho kwa viongozi wa serikali za Afrika pia. Tabia yao ya kubeza vyombo vya habari ikome. Watukome kabisa kwani tuandikayo tunakuwa na data. Hakuna marefu yasiyokuwa na ncha. Kila tulipoandika masuala haya tuliitwa wazushi, sasa kiko wapi? Mkapa, sema usikike.

deobalile@yahoo.com au +447904159144.

Source: http://www.freemedia.co.tz/daima/2007/2/11/makala8.php
 
Maswali magumu ya Ndg Balile, Rais Mstaafu hatoweza (au atakwepa kwa makusudi) kuyajibu.Kwa mtazamo wangu kila kitu kimekwishakuwa wazi,wale walioondoka na baadhi ya Vinara ambao wapo madarakani leo wamehusika na sakata hili la RADA. Tusubiri tu taarifa ya wanaofanya uchunguzi wa kashfa nzima ya ununuzi wa Rada,Taarifa ipo tayari, na punde tu itakuwa wazi kwa vyombo vya habari.Ndg watanzania tuikubali Taarifa hiyo na sio kukubali maandamano yatakayoandaliwa na watawala kwa makusudi ya kuipinga Taarifa hiyo!.
 
Tangu huyu mama Short adai kuwa Mkapa hakuhusika katika ununuzi wa rada hiyo kweli nimeshindwa kuelewa mwenendo mzima wa swala hili. Wengi wetu pamoja na kuwa na kumbukumbu hafifu tunafahamu kabisa huyu mama alivyosimama kidete kwa madai mazito kuwa rushwa ilikuwa imetembea kwa viongozi waandamizi Tanzania. Wakati huo huo Mkapa naye alikuwa meshupaa kudai kuwa serikali itanunua tu rada hiyo, na yeyote anayedai kuwepo kwa rushwa alete ushahidi. Waziri wa mambo ya nje wakati huo bwana Kikwete naye akasikika akisema kuwa Tanzania ina haki ya kujiamulia nini nini inachokitaka kwa masilahi yake.

Sasa ghafla kugeuziwa kibao kuwa Mkapa hakuwa anataka ununuzi huo, na Kikwete kudai kuwa serikali ya Uingereza iliitapeli nchi maskini ya Tanzania ni kejeli kweli kweli. Sijui kama Mkapa amemuomba sana mama Short amsamehe kumhusisha kwenye sakata hilo na kuwa chini ya miguu yake ampitishie mbali kikombe hicho. Yaani sielewi kabisa.

Jambo moja liko wazi kuwa rushwa kweli ilitumika ya 30%; pesa za rushwa zilitolewa na kulipwa katika benki ya "USWISI' ambako ndiko wala rushwa na wauza madawa wanakotunzia hela zao.
 
Back
Top Bottom