Mbogela,
E bwana kacheze bahati nasibu, utashinda. Guess yako iko on point ile mbaya.
Siku ile Chenge alipotangazwa ana lawyer Mmarekani, aliyetishia kuibua masoo kwenye kesi ya Chenge, nikajiuliza, huyu lawyer amesajiliwa ku practice Bongo? Na kama amesajiliwa, Chenge atakujaje na lawyer wa kigeni mahakamani, lawyer anaeongea na mi accent ambayo majaji wanaweza wasimuelewe. I mean, Chenge is no dummy, itakuwaje awe na lawyer mzungu? Strategically inaweza kuwa sio move nzuri sababu majaji wanaweza kuona huyu mgeni anakuja hapa kutufundisha sheria zetu. Ana mpango gani hapa Chenge? (kwenye chess/draft lazima ufikirie adui anafikiria nini, halafu umpe benefit of assumption kwamba he is the most skilled strategist).
Mimi nikatafuta info za huyu lawyer mitandaoni nikapata namba ya simu. Kwa sababu hakuna mwandishi yeyote aliye uliza kama huyu Mmarekani amesajiliwa ku-practice Bongo, nikaona, u know what, we are not going to wait for a Press that does not exist.
Nikampigia lawyer wa Chenge Ohio. Nikaona nikimwambia mimi mwandishi wa habari jamaa naye ataleta u lawyer. Nikaamua kumtengeneza (if u know what I mean). Nikamwambia, nimekusikia jina lako kwenye Media hivi majuzi, nahitaji huduma yako. Kaniuliza we nani, nikampa mi ID ya kutengeneza. Shida yako, nikamwambia Baba yangu kakamatwa na Kesi ya Rushwa. Wapi, ye nani, nikamwambia alikuwa meneja Mkuu wa Kampuni ya Taifa ya Sigara, sasa hivi yuko dhamana. Mzungu hajui chochote kuhusu wakuu wa makampuni ya Bongo chochote ninachomwambia cha mbele. Alipo maliza maswali yake, nikaanza yakwangu. Nikamwambia, unaweza kumpresent babangu akasema, tutaangalia, mwambie anipigie simu. Unaweza ku-practice Bongo, umesajiliwa, akasema ndio, mimi ni Mmarekani peke yake ninaye weza ku-practice in the commonwealth. Sijui ana maana gani, manake kama ni nchi za commonwealth zote, basi nadhani hawezi kuwa peke yake.
Sasa cheki basi. Nikamuuliza, sasa utakuja Tanzania kumrepresent Babangu, akasema, well, tutaangalia kwa sababu nina ma partner Bongo. Na kama kawaida ya Wazungu wanapenda sana kuongea vitu ambavyo hawajaulizwa. Basi akaanza kutoa mi "dataz" (no pun). Akaendelea, "hivi ninavyoongea nimetoka kuwasiliana na "Nima Radi Makono" ameondoka sasa hivi kurudi Tanzania." (Na kweli wakati ule Mkono alikuwa USA, alitokea kwenye media reports siku chache earlier akikanusha madili yake ya BOT kwa njia ya simu kutoka USA.) Sikutaka kumbana sana kuhusu Mkono kwa sababu nilitaka kujifanya sijui kitu, wala simjui "Nima Radi Makono."
Akanirudisha kwenye kesi ya Babangu wa "Kampuni ya Taifa ya Sigara," nikamtengeneza tena. Halafu tukaagana, nikamwacha anasubiri simu.
Kwa hiyo Mkono ni partner wa lawyer wa Chenge Tanzania. Na huyu lawyer anasua sua kuja Bongo. Anahitaji sana ushauri huyu lawyer wa kigeni. Inawezekana kabisa Mkono anatoa ushauri. Ni partner.