The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

Umefanya a wild and wooly assumption kwamba walioko nje wanatokea TZ ya 'Ushuani.' Sio kweli. Wengi wanatoka Uswahilini na baadhi Vijijini. Na wengi wamekwenda nje ukubwani, kuanzia miaka ya 1990. Kwa hiyo wanaijua Bongo na maisha ya Uswekeni. Sijawahi kukutana na Mtanzania nje ambaye hajawahi kufika Kijijini wala Uswahilini, hata awe mtoto wa "Kishua."

Hiyo assumption sio sahihi.

Ni kweli assumption ya kuhani mkuu sio sahihi ,napenda kumthibitishia kwamba mie nipo nje hapa uingereza lakini kati ya tarehe 14 april na 4 may nilikuwa tanzania,mojawapo ya maeneo niliyotembelea kwa dar ni gongo la mboto,mikocheni ubungo,kimara,mbezi,posta na vilevile nikaondoka kwenda Iringa mjini,mafinga makambako,njombe,mgololo,na mwisho makete katika kijiji cha mwakauta karibu na hospitali ya bulongwa halafu nikarudi tena dar na badaye UK.Upo hapo Kuhani Mkuu?sio kwamba watu wa nje labda waliondoka miaka ya 80 au sijui 90 wanarudi sana home,wako update sana.Tunajua maisha ya kimji na swekeni.
 
Tanzania sasa hivi tunahitaji mtu mwenye guts ambaye anaweza kuamua kufanya jambo hata kama wanaoumia ni watu wake wa karibu sana au ndugu kwa sababu viongozi wote wameoza. Kikwete kama ameamua kuwa hivyo wananchi tuko nyuma yake kwa kuwa tunaoumia ni sisi.

Atawezaje kuwashughulikia wkt yeye mwenyewe alitwajwa kama fisadi...hivi fisadi anaweza kumshughulikia fisadi mwenzie??
 
Kuna mambo ya msingi sana ambayo Kuhani Mkuu ameyahoji ambayo kuna haja ya kuyajibu. Kwa mfano, mosi, Chenge yupo London kutoa ushahidi au kawa arrested? Pili, kulikuwa na haja kweli JK kutoa search warrant yeye mwenye personally, hakuna vyombo vingine vya kufanya hili? Tatu, ok, kama JK alitoa hiyo search warrant, ilikuwa ni lazima kweli aitoe kisirisiri, si Chenge alikuwa waziri wake, aliyemteua yeye mwenyewe bila shinikizo tena kinyume kabisa na maoni ya wananchi walio wengi, au JK alikuwa na anamuogopa Chenge? Sasa kwa nini amuogope? Hapa ndipo nami nakubaliana na Kuhani Mkuu kuwa bado kuna maswali mengi zaidi kuliko majibu.

Simplicity is the enemy of truth!

Mkuu Kitila,

Nakuelewa una maana gani lakini mambo ya TZ hayaendi na common sense. Hata hili tu
la JK kuruhusu Chenge apekuliwe ni hatua mbele.

Wengi tungefurahi kama mambo yangefanywa inavyotakiwa lakini kwa TZ tunayoijua ni kwamba bado tuko nyuma sana kwenye utawala bora.

Tungelikuwa na vyombo vya sheria vinavyofanya kazi zake wala haya tunayoyajadili hapa yasingelikuwa na maana.

Ila tu una amini polisi wa Tanzania wanaweza kwenda kum search waziri wa TZ bila JK kuwa na habari? Sio lazima yeye mwenyewe aweke sahihi kwenye search warrant lakini ni lazima atakuwa ametoa idhini kwa hilo tendo kufanyika.

Hili la Chenge ni hatua mbele hata kama bado ni ndogo.
 
habari za ndani kabisa ni kwamba chenge amemchagua wakili mmoja maarufu wa moshi ili amtetee wakati suala lake litakapofika katika mahakama za tanzania.

siwezi kumtaja kwa sasa kwa sababu za maadili ya kazi ila mambo yatakapoiva mtajulishwa.
Stay turned!!

Okay......maybe u shud change ur name sir,maana otherwise itaonekana ni umbea tu
 
Issue ya Chenge iko complicated kwa kiasi kikubwa na ndiyo maana inazaa maswali mengi ambayo majibu yake yanaweza kutofatiana kutokana na tofauti zetu katika reasoning.

Ninashawishika kukubali kwamba Chenge si shahidi tu, bali pia ana mashaka na yeye anaweza kuunganishwa kwenye mashitaka. Ataunganishwa namna gani hapo ndipo sipati picha kamili.

Magazeti ya hapa kwetu yaliongea na Mwanasheria wa Chenge ambaye yuko US na jamaa akatema cheche kwamba atamtetea Chenge kwa nguvu zote na akaonya kwamba kuna wana siasa wengi wataunganishwa kwenye hiyo kesi, haikuishia hapo alinyooshea vidole waliokuwa vigogo wa wizara za ulinzi na jkt na mawasiliano na uchukuzi akidai hao walikuwa na mkono kwenye issue ya radar. Sasa kama mtu ni shahidi tu, iweje aanze kusaka wakili na tena wa kutoka majuu ili amtetee. Shahidi gani ambaye huwa anatetewa na wakili? Chenge ni lawyer na anajua kilicho kwenye hilo sakata na ndiyo maana ana haha kusaka mawakili wa kumtetea. Halafu hapo hapo ujiulize huyu wakili wa mmarekani alipata wapi data kwamba kuna wana siasa wengine kwenye hilo sakata mpaka akitaja na wizara zilizohusika?

Kuna waliouliza kama JK anamuogopa Chenge au la, nadhani waliouliza hawakumbuki kwamba JK amekuwa akifanya kazi kwa kunawa mikono ili kuonyesha kwamba yeye hayumo. Mfano ni swala la Lowassa, alipotua Dar akiongea na wazee wa CCM alitamka kwamba yaliyompata Lowassa ni ajali ya kisiasa. Kwa maneno mengine hakuwa tayari kumtosa swahiba wake pamoja na kwamba alikuwa anajua kila kitu kwa kuwa aliwahi kuingilia hilo swala kipindi fulani na hatimaye akawabadilisha mawaziri. Kwanini kwenye kikao hicho cha wazee hakuongea kwamba Msabaha na Karamagi nao ilikuwa ni ajali ya kisiasa? Kuna watu ambao anajua kwamba akiwagusa yanaweza kuja mengine ambayo jamii haitakiwi kuyafahamu na hapo ndipo unapoanza kujiuliza kwanini anafanya mambo kichinichini? Wakati Lowassa anajiuzulu jamaa alikuwa Dodoma kapiga kambi kwa kisingizio cha kuongoza cabinet meeting. Yaliyotokea wote tunayajua na sasa ni historia na tunasubiri dvd/kideo kutoka kwa ES tujikumbushe. Mazingira hayo yanakuonyesha wazi kwamba JK huwa anafanya mambo yake kwa mazingira ya kujiweka mbali ili kuepuka lawama. Aidha kwa kuogopa waliomsaidia kuingia Ikulu ama kwa kuogopa wanaojua mabomu yake.

Utendaji kazi wa Jeshi la Polisi una walakini mkubwa sana, kwa hiyo sishangai ninaposikia kwamba Ikulu ilitoa go ahead ya kum-search Chenge. Hapa naomba niwakumbushe maneno ya Dr. Hoseah (DG wa PCCB) kuhusu tuhuma za Mkapa. Hoseah alisema wazi kwamba kama JK kasema Mkapa asichunguzwe basi PCCB haiwezi kwenda kinyume na agizo la rais ambaye ni boss wa Hoseah. Kwa maneno mengine hata IGP nae hawezi kutoa search warrant ya kum-search waziri bila ya kuwa na go ahead ya Ikulu. Nadhani hapa lugha ndiyo imetofautiana. Ikulu haiwezi kutoa search warrant ila IGP or whoever, anaweza kui-contact Ikulu na kuwajulisha kwamba kuna hiki na kile kinatakiwa kufanyika, je waidhinishe upekuaji? Ikulu ikisema NO, IGP hana nguvu ya kupingana nayo japo Jeshi la Polisi ndiyo lenye mamlaka ya kutoa vibali vya kupekua nyumba/ofisi wanayoituhumu kwa mambo fulani.

SFO walipokuja Tanzania, lazima serikali ya Tanzania ilikuwa inajua kinachoendelea na hivyo Ikulu ilikuwa inapewa updates ya kila kitu ili JK/Ikulu wajue kinachoendelea. Kwa hiyo swala la SFO kumtaka Chenge aende UK kwa ajili ya mahojiano zaidi inawezekana lina ukweli zaidi. Watu wakumbuke kwamba Chenge alipekuliwa na SFO na lazima waliondoka na vitu vingi ambavyo walienda kuvi-study na sasa wanahitaji clarification kutoka kwake. Kwa hiyo hoja kwamba ameenda kwa shida za kifamilia naona haina nguvu sana, labda tungejiuliza kwanini hiyo shida ya kifamilia igongane na issue ya SFO?

Mimi ninashawishika kuamini kwamba Chenge yuko UK kwa mwaliko wa SFO ili waweze ku-extract more info kwa ajili ya uchunguzi/upelelezi wao. Angekuwa Tanzania tungesema anaisaidia polisi (maana ya kuisaidia polisi ni pale wanapokuhoji ili uwape info za kuhusiana na uchunguzi wanaouhitaji na wakihisi kwamba wakikuachia unaweza kuharibu uchunguzi wao ndipo wanakulaza ndani mpaka wahakikishe info zote ulizozotoa wamezifanyia kazi ipasavyo na watuhumiwa wamewanasa na wamejiridhisha kwamba wewe hukuhisika na kwamba unabaki na jina safi la shahidi ili majambo yakienda mahakamani uweze kwenda kutoa ushahidi wako). Kwa hiyo kitendo cha Chenge kuwa chini ya ulinzi mkali wa SFO ni kwamba hawataki aharibu ushahidi, watamuweka chini ya ulinzi mpaka pale watakapokuwa wamekusanya info zote wanazotaka.
 
Mkuu,

Kwanza kabisa, Chenge hakujiuzulu kutokana na shinikizo la Waingereza. Tufuatilie vitu kwa makini jamani. Shinikizo la Kisiasa lilikuwa nyumbani.

Pia unasema Chenge yumo. Yumo wapi? Kwenye Uchunguzi? Umesikia wapi hilo? Si kuna article ya gazeti lao Waingereza imepostiwa humu, naomba uisome. Na ndefu kidogo (kama ukurasa mmoja ni mrefu) lakini vumilia uimalize kwa sababu ni muhimu kuelewa kinacho endelea. Chenge ni shahidi tu, hawezi kuwa chini ya ulinzi Churchil hotel.

Kuhusu Juridisction ya kum search Chenge, inawezekana alikubali kusachiwa kwa hiari. Ukikubali kwa hiari hawahitaji ku assert jurisdiction. Yeye sio target wa investigation hivyo sio hatari kuwakubalia wam search. "Dataz" zilisema Chenge alileta ubishi akaonyeshwa warrant ya Kikwete. Tukaswalisha hilo. Kikwete hawezi kutoa ruhusu kisiri siri Waziri wake asachiwe.

Halafu ni muhimu kukumbuka political atmospherics zilizo kuwa zinaendelea wakati huu. JK alikuwa ametoka kumteua Chenge dhidi ya shinikizo kubwa la Kisiasa lililotaka amtose. Kwa hiyo ni mtu wake. Angemgeuka vipi Waziri wake kwa kuruhusu search kisiri siri, Waziri ambae JK alikuwa tayari kulipa political price kumlinda?

Kwa hiyo Mkuu, tuna maswali mengi kuliko majibu. Tunauliza kwa sababu sisi sio MwanaHALISI na TanzaniaDAIMA. Tanzania hakuna Media, inabidi tutafute haya mambo na tuyachambue wenyewe tujue nini kinaendelea. Hakuna gazeti lililo mbana Waziri Simba atueleze uchunguzi wa UK unatuhusu nini sisi, au hela za Chenge zilizo patikana Benki za Bongo zilisachiwa na nani na kwa Jurisdiction gani. Hakuna kiumbe kwenye Press ya Bongo ameandika vitu hivyo. Not one. Zero! Zepo! Zilch! Lakini tutafika.

Ahsante Mkuu. Naomba usisahau, mwisho wa siku, letu moja. Ila, wanasema Uhuru unashamiri mawazo yakiwa na Uhasama. Na nadhani wote tumeleteana uhamasa wa mawazo ipasavyo. Baadae!

Kuhani,

Hiyo nukuu uliyotuletea ni ya chapisho la tarehe gani? Umesoma tarehe iliyoandiklwa hapo juu ukajiulilza leo hii ni siku ngapi zimepita na uwezekano gani kuwa sasa Chenge si shahidi tena bali ni mtuhumiwa?

Je Chenge alijiuzulu lini? na kwa nini?

Sasa hizo hapo juu ni data, twende kwenye assumed logic.

What if status yake kutokana na kuwa Waziri ilimfanya awe shahidi na sasa hivi makubaliano yalikuwa akisha achia ngazi kama waziri basi ni Ruksa kwa SFO kucheza naye makida makida na hata ile immunity ikaondolewa?

Naamini sheria za Uingereza ni sawa na za Tanzania. Mtoa Rushwa na Mpokea rushwa wote wako kundi moja. Sasa kama Chenge alipokea au anahifadhi fedha za Rushwa inayochunguzwa, kuna ugumu gani kwa yeye kubadilishwa nafasi kutoka kuwa shahidi kwenda kuwa mtuhumiwa?

Hivi FBI walipokuja Dar na kufanya msako wa waliolipua ubalozi mpaka wakamweka ndani Thomas Lyimo ilikuwa jurisdication na nchi ya nani?

Je ni kipi cha ajabu alichofanya Kikwete kumchagua tena Chenge ilhali ilijulikana wazi kuwa Chenge si mtu safi tangu awali (IPTL)? Ikiwa Kikwete aliamua kumfanya Lowassa kuwa Waziri Mkuu pamoja na pingamizi nyingi na kutumia fedha na kanuni za Chama ili Lowassa asimikwe na Bunge na kisha Lowassa aanguke kutokana na yale yale tuliyoyajua kabla ya kupewa cheo, kuna tofauti gani na Chenge na kujua tabia za Kikwete za kutokuwa makini?

Sasa hivi suala si FMES na KUhani au wana JF kamboi moja na JF Kambi nyingine, suala ni je kuna uwezekano gani kuwa jambo hili ni la kweli au si kweli?

Hivyo basi kwa kutumia Data, Logic na illogic sense tumung'unye what is happening. Tumeshaletewa kesi, tuichambue.
 
Mheshimiwa Rais nakuomba sana,
Naomba chenge Asulubiwe sana,
Najua tutajua wewe ni jasiri sana,


Mie naamaini kama kweli Ujasiri huu wa Muungwana kumuangamiza Chenge kautoa yeye na kama ni kwa manufaa ya nchi hii na siyo kisiasa,Basi Maneno ya Lowassa aliyoyasema bunegni yatatimia.

Kwani Pesa za TANGOLD zilifanya kampeni ya kumuweka nani madarakani??nani Mkurugenzi wake??Nahisi kama kuna Spinning kubwa kuhsu jambo flani.


mzee FMES,
I have gone deep inside in your story and it will make a history,Mwafrika wa kike,JK is going to be one term President????Yes You said and ithink it will happen then
 
"Utendaji kazi wa Jeshi la Polisi una walakini mkubwa sana, kwa hiyo sishangai ninaposikia kwamba Ikulu ilitoa go ahead ya kum-search Chenge. Hapa naomba niwakumbushe maneno ya Dr. Hoseah (DG wa PCCB) kuhusu tuhuma za Mkapa. Hoseah alisema wazi kwamba kama JK kasema Mkapa asichunguzwe basi PCCB haiwezi kwenda kinyume na agizo la rais ambaye ni boss wa Hoseah. Kwa maneno mengine hata IGP nae hawezi kutoa search warrant ya kum-search waziri bila ya kuwa na go ahead ya Ikulu. Nadhani hapa lugha ndiyo imetofautiana. Ikulu haiwezi kutoa search warrant ila IGP or whoever, anaweza kui-contact Ikulu na kuwajulisha kwamba kuna hiki na kile kinatakiwa kufanyika, je waidhinishe upekuaji? Ikulu ikisema NO, IGP hana nguvu ya kupingana nayo japo Jeshi la Polisi ndiyo lenye mamlaka ya kutoa vibali vya kupekua nyumba/ofisi wanayoituhumu kwa mambo fulani.

SFO walipokuja Tanzania, lazima serikali ya Tanzania ilikuwa inajua kinachoendelea na hivyo Ikulu ilikuwa inapewa updates ya kila kitu ili JK/Ikulu wajue kinachoendelea. Kwa hiyo swala la SFO kumtaka Chenge aende UK kwa ajili ya mahojiano zaidi inawezekana lina ukweli zaidi. Watu wakumbuke kwamba Chenge alipekuliwa na SFO na lazima waliondoka na vitu vingi ambavyo walienda kuvi-study na sasa wanahitaji clarification kutoka kwake. Kwa hiyo hoja kwamba ameenda kwa shida za kifamilia naona haina nguvu sana, labda tungejiuliza kwanini hiyo shida ya kifamilia igongane na issue ya SFO
?"

Mkuu uliyetoa statement hapo juu,
Labda kwa faida tu tujikumbushe juu ya utendaji kazi wa jeshi la polisi,ki mfumo mambo yote yanayotokea hapa nchini ambayo yanaripotiwa polisi(labda tu polisi wenyewe waamue kuficha) yanajulikana hadi ikulu kila siku kuanzia saa 12 jioni hadi saa mbili usiku.Kwa jeshi la polisi muda huu unaitwa briefing hours ambapo OCS anatoa taarifa kwa OCD,OCD anatoa taarifa kwa RPC kuhusu matukio yote au ripoti nzima ya kazi ya wilaya ya siku hiyo.Vivyo hivyo RPC kwa IGP na IGP anatoa ikulu kupitia idara ya usalama kitengo cha security ikulu,hivyo hadi kufikia saa 3 usiku Rais anakuwa amejua nini kimefanyika nchini kwake kwa siku nzima hiyo.Hivyo hata habari au request for search iwe imefikia kwa IGP au kokote kule lazima ajue,na sio lazima kama ulivyosema aanguke sahihi mwenyewe,it suffices yeye kusema au kuandika proceed.
 
Kuna mambo ya msingi sana ambayo Kuhani Mkuu ameyahoji ambayo kuna haja ya kuyajibu. Kwa mfano, mosi, Chenge yupo London kutoa ushahidi au kawa arrested? Pili, kulikuwa na haja kweli JK kutoa search warrant yeye mwenye personally, hakuna vyombo vingine vya kufanya hili? Tatu, ok, kama JK alitoa hiyo search warrant, ilikuwa ni lazima kweli aitoe kisirisiri, si Chenge alikuwa waziri wake, aliyemteua yeye mwenyewe bila shinikizo tena kinyume kabisa na maoni ya wananchi walio wengi, au JK alikuwa na anamuogopa Chenge? Sasa kwa nini amuogope? Hapa ndipo nami nakubaliana na Kuhani Mkuu kuwa bado kuna maswali mengi zaidi kuliko majibu.

Simplicity is the enemy of truth!


Mjomba Kitila,

Ukitumia neno search warrant, tutarudi kule kule kwa kudai je JK ana mamlaka gani kusaini search warrant.

Mimi logic yangu kutokana na hii habari ni hivi.

SFO na serikali yao walimtumia ujumbe JK na kumwambia, katika suala la Radar, uchunguzi wetu unaonyesha kuwa Chenge ni mtu muhimu sana, anaweza kuwa shahidi au mtuhumiwa. SSFO wakamwambia JK, tuna ushahidi mkubwa wa kuonyesha kuwa Chenge amehifadhi mshiko mkubwa ambao source yake ni hiyo kampuni ya Red Diamond na Vithlani ambao ndiyo wahusika wengine wa BAE scandal.

Ilikuwa ni jukumu la JK kukubali au kukataa kama Saudia Arabia walivyofanya kwa kukataa Prince Bandar asiendelee kuchunguzwa.

JK kakubali na hata kawapa barua ya Ikulu inayowapa kibali kufanya kazi nchini na hata kumpekua na kumfuatilia Chenge. Yawezekana alimpa amri Manumba au Mwema wasaini sasa hiyo "search warrant" ili kufuata taratibu za sheria. Hivyo Chenge alipofuatwa na kugongewa hodi, SFO walikuwa na "Search Warrant" na barua kutoka Ikulu.

Kwa nini JK kaamua kumtosa Chenge ambaye alikuwa ni waziri wake? Hapa swali ni gumu kwa Kikwete si kwetu. Uswahiba wa Kichama, Kiserikali na kufichiana siri ndio ulimfanya Kikwete ampe Chenge uwaziri alipounda ile timu ya American Footbal January 2006. Je kwa nini alimrudisha Chenge ambaye tayari alikuwa na tuhuma nzito ya IPTL? jiulize IPTL ilipoanza na ilipofanyika, JK alikuwa wapi na nani? Je mikataba ya madini na kuletwa kwa kina Sinclair kulifanywa na nani? Hata tukienda kwenye mambo ya EPA na ushindi wa Tsunami wa Kikwete au wa Chenge kwenye Halmashauri kuu, bado kuna common denominator ambayo zinawaunganisha (speculation)!

Hivyo yawezekana Chenge kufanywa waziri na Kikwete yalikuwa malipo ya fadhila na siri fulani, hata alipomchagua kwa mara ya pili mwezi Februari, ndiyo maana Chenge aliwaambia Watanzania wakamhoji JK kwa nini karudishwa madarakani.

Sasa hapa kuna wengine watasema ohh JK alikuwa anampigia time na kuvuta muda ili ajikaange mwenyewe kwa kuwa SFO walikuwa wameanza uchunguzi na m=kumfuata Kikwete. Wengine watasema, Kikwete ni naive sana kwa kupuuza mambo ambayo ni obvious mabovu. Sasa hapo chagua mwenyewe lipi lina make sense.

Ujeuri na tabia za viongozi wetu ndio umewafikisha waingie kwenye aibu kubwa kama hizi. Yawezekana Chenge alirudi Bariadi kama mtemi bila kujua kuwa sasa kwa kujiuzulu kwake ambako inawezekana ndiko JK alikuwa anasubiri ili SFO wafanye kweli, ndiko kulikukuwa chachu kwa yeye kubadilishwa kutoka kuwa Shahidi na sasa mazingira kuwa ni Mtuhumiwa.

Kwa nini JK yupo kimya na kujikausha kuachia SFO wafanye kazi hii na si Mwema na Manumba au Mwanyika? ni kwa kuwa wote walikuwa chungu kimoja na Chenge na SFO wamewasitiri JK na labda Mkapa kwa kuwa walikuwa maraisi (another logic speculation)!

Tanzania haitafanya uchunguzi dhidi ya Chenge mpaka CCM iondoke madarakani.
 
Kwa hiyo kitendo cha Chenge kuwa chini ya ulinzi mkali wa SFO ni kwamba hawataki aharibu ushahidi, watamuweka chini ya ulinzi mpaka pale watakapokuwa wamekusanya info zote wanazotaka.

Keil,

Umegusia kitu kimoja ambacho sasa macho yamenifunguka. Mnakumbuka kuwa BAE ndiyo inachunguzwa? na Chenge ni shahidi muhimu? je ni kazi gani kugundua kuwa kuna haja ya Chenge kuwekwa kwenye ulinzi mkali ili kulinda anachokijua hata kama kitakuja mdhuru yeye Chenge?

Je ikiwa BAE, Vithlani na Red Diamond au Chenge mwenyewe watataka "ushahidi" upotee au shahidi asiwepo kuna ugumu gani kwa SFO kumuweka kwenye ulinzi mkali?

Ikiwa wanene wa BAE wamewekwa ndani Houston Texas na FBI, hamuoni kuwa jambo hili ni kubwa sana?
 
Rev Kishoka,
Nimependa sana your logic na umeonyesha ni jinsi gani ulivyojaribu ku-make sense of this all. THe inference you make is actually very logical and it shows what a good analytical mind you have.
I believe that the data tunazopewa ni snapshot of things and it is up to us to connect the dots.
Hapa kuna ishu mbili:
1. Data: hapa FMES amefanya kazi kubwa ya kuweka data anazojua yeye. Kazileta kama alivyozipata (we assume). Hivyo nadhani ndiyo maana yuko offended tunapoanza kuhoji kusign warrant na vitu vingine. Yeye ameangalia pure data kama ilivyo, na kweli naona amehangaika kuweka anachokijua
2. Connecting the dots: analysts kama tunavyojua hulipwa pesa nyingi katika dunia ya kwanza yaani nchi zilizoendelea kwa kuwa data kama data haitoshi ni lazima ifanyiwe kazi. Sasa wapo wanaJF ambao ni analytical minded na wanaojaribu kutafuta logic and sense na wanaona kama kuna walakini mkubwa.
Nadhani kuna haja ya kujaribu kuangalia pande zote mbili bila emotions. FMES, kazi yako tumeikubali lakini tunaendelea kuichambua, kaka don't take it personally.
Personally, nafikiri kuwa SFO watakuwa wamefanya search yoyote ile kwa kushirikiana na wahusika hapa Bongo ambao nadhani itakuwa PCCB. Kwa hiyo ni lazima watumie mgongo wa PCCB na wanapofika kwene scene wanafanya wenyewe kazi lakini they have to collaborate apparently with local authorities. That would make more sense.
Chenge kwenda London pia inawezekana lakini I am sure that he was not threatened or under arrest kwa sababu lawyers wake wa US na wengine wangekuwa on the case. The most probable case ni kwamba he has made a deal with SFO na amewatosa wengine wengi.
So we have data (have to sort out exaggeration and innuendo) now we have to connect the dots.
 
HOngera Kikwete kwa kazi nzuri...

Hongera kwa kupigana na mafisadi hata kwa kutumia wageni. Inabidi sasa sifa zitolewe kwa maana kazi zimeanza kuonekana.

CCM tukiamua kufanya kazi tunafanya kweli na huu ni mwanzo tu.
Kidumu chama cha mapinduzi.
 
Rev.Kishoka, Kitila Mkumbo,

..huu uchunguzi unaihusu BAE na shughuli zao popote pale wanapo-operate. umeanzia huko kwa wakubwa, na kuteremka mpaka huku kwetu.

..Kikwete amelazimika tu kukubali Chenge achunguzwe, and he is now taking this issue one day at a time.

..Tanzania ni nchi masikini na Raisi wake hana ubavu wa kuchunguza kampuni za wakubwa kama hilo li BAE. Wakubwa nao wakimfuata Raisi wetu wakimwambia tuna shida na waziri wako fulani, basi Raisi wetu hana la kufanya zaidi ya ku-comply.

..Mimi siamini kabisa kama Kikwete ana nia na ujasiri wa kupambana na mafisadi. hapa nyumbani kulikuwa na manunguniko kuhusu ubinafsishaji wa shirika la posta na simu. malalamiko hayo yalikuwa yanamhusu mtoto wa Mramba. kitu cha ajabu kabisa Kikwete akampa madaraka Mramba kuunda tume ya ndani kumchunguza mwanawe. taarifa ya tume hiyo iko kapuni mpaka leo.

..nilitegemea wanafunzi wa HISTORIA mko hapa, na mtatukumbusha kuhusu maraisi wa kiafrika waliokuwa na ujasiri wa kupambana na rushwa kubwa-kubwa.

..labda niwakumbushe kisa za makachero wa Gen.Muhamad Buhari aliyepata kuwa Raisi wa Nigeria. makachero hao walimteka nyara Ummaru Dikko, waziri wa mafuta wa serikali ya Shehu Shaghari[aliyepinduliwa na Buhari], wakamdunga madawa ya kulevya na kumpakia kwenye diplomatic cargo.

..ndani ya sanduku alimotiwa ummaru dikko kulikuwa na kachero mwingine aliyekuwa akimuongezea dose ili asije kuamka kabla hajapakiwa kwenye ndege kwenda Nigeria kufunguliwa mashtaka.

..mpango huo ulikuwa aborted na scotland yard kwenye uwanja wa ndege heathrow. wasingekamatwa pale uwanja wa ndege Ummaru Dikko angekiona cha mtema kuni huko Lagos. Waingereza ndiyo waliomuokoa Ummaru Dikko.

..kisa hicho hapo juu ndicho kinachonifanya niamini kwamba Kikwete hana nia ya kupambana na rushwa. zaidi amepata nafasi ya Uraisi kwa msaada wa wala rushwa. tena kwa kampeni iliyodumu kwa miaka zaidi ya 10.

..vilevile huu uchunguzi umeshika kasi namna hii kwasababu wakubwa wameamua kuuvalia njuga. kama wangekuwa hawana interest nao basi wangeuhujumu kama walimvyomhujumu Gen.Muhamad Buhari alipotaka ku-deal na Ummaru Dikko aliyekula rushwa na makampuni ya mafuta ya UK.

NB:

..kuna wengine wanafikiri technicalities ni upuuzi. hawa wanataka mambo yaende ki-Mrema-Mrema.

..labda kuwakumbusha tu, yule IGP aliyekanyaga mwananchi na gari, alifutiwa kesi yake on technicalities.

..marehemu Abdulrahman Babu alikosa nafasi ya kuwa mgombea mwenza wa Mrema on technicalities.
 
Britain SFO mum on Chenge probe

2008-05-19 09:46:05
By Hannah Mwandoloma

Britain`s Serious Fraud Office (SFO), which has been probing the controversial 28 million pounds sterling (approx. 70bn/-) military radar system sale to the Tanzanian government, has said it is still too early to reveal any details.

The SFO Press Office told The Guardian over the weekend that investigations relating to the saga were going on but at the current stage, they were not ready to discuss the details of the investigation or its progress.

``The Serious Fraud Office investigation relating to a BAE Systems Plc contract with the government of Tanzania for an air radar system is ongoing. We regret but we cannot at this stage discuss the details of our investigation or its progress,`` the SFO Press Office said in a brief statement.

The office was responding to questions e-mailed by this reporter. The SFO was also asked when they expected to complete the probe and measures to be taken.

``We announce significant developments in our cases through a press release. These are mostly about the outcome of prosecutions. However, the opening of an investigation or the charging of suspects may be announced if it is thought to be in the public interest,`` the statement added.

Mid last month, the UK Guardian newspaper disclosed that more than $1m had been discovered by SFO in offshore bank accounts controlled by former Infrastructure Minister Andrew Chenge, fuelling allegations that some of the money originated from the 2002 radar deal.

SFO investigators, who had been scrutinising the multibillion air radar system deal, identified the money in Jersey accounts personally controlled by Chenge.

After the UK newspaper broke the news, the main question that dominated the public domain was how he was able to stash away more than $1m (over 1.2bn/-) in offshore bank accounts, given past and present government salary rates.

Chenge, who was reportedly to be in the UK over the weekend, has not disputed the money in his offshore bank accounts, but has strongly denied suggestions that he received corrupt payments from Britain`s BAE Systems, manufacturers of the controversial radar sold to the Tanzanian government.

He was quoted as saying he was only involved in minor aspects of the radar deal, which was promoted by other ministries and approved by the cabinet.

At the time the highly-dubious deal was negotiated and concluded, Chenge was serving as attorney general.

However, after much public pressure, he tendered a letter of resignation, which was accepted by President Jakaya Kikwete.

According to the SFO, approximately 65% of their cases have an international dimension and that national borders rarely prove to be barriers to determined fraudsters

SOURCE: Guardian
 
Mzee ES, mkuu nakuaminia kuhusu connection uliyoleta ya Rostam na Manji. Hapo kuna siri kubwa sana na nadhani umepata nyeti za EPA kuhusu hao wawili na jinsi walivyoleta kiburi na kuwadhalalisha viongozi wa kamati. Mpira wameurudisha kwa JK maana Manji kakubali portion tu ya sehemu ya fedha zilizochukuliwa na Rostam ndio atarudisha zingine anadai go to hell.
 
Rev Kishoka, JokaKuu, Susuviri, et al.

Mimi ni miongoni mwa watu ambao nimeheshimu kabisa mchango wa FMES wa kutuletea hizo dataz. Niachokataa ni kuwakemea wale wanaojaribu kuhoji zaidi kuhusu kukamatwa au kuitwa (whatever you want to call it) kwa Chenge huko London. La muhimu zaidi ambalo mimi nakataa ni kujaribu kuanza ku-spin hili na kumpa credit JK kwamba anapambana na rushwa au ufisadi au ujambazi wa mahela ya walipa kodi.

JK angekuwa jasiri na angekuwa angalau anauchukia ubadhirifu, ufisadi, rushwa na ujambazi wa hela za walipa kodi, achilia mbali kuwa na nia ya kupambana nao, asingethubutu kamwe kuwateua Chenge na Mramba kwenye cabinet yake. Kwa hiyo, kama alivyosema JokaKuu, kuruhusu uchunguzi wa Chenge ni kwamba afanyeje, inabidi tu ukizingatia kuwa yeye huwaita hawa majaa ya UK na US mabwana wakubwa! Kwa maneno mengine, JK wetu ni sehemu ya tatizo na wala sio sehemu ya majawabu ya matatizo ya ufisadi na uporaji wa fedha za walipa kodi.

Ndio maana lazima na ni muhimu sana tuendelee kuwasaidia wenzetu akina Masaka na wenzake wanaoshangilia na kumpa hongera JK kuzibuka pua, masikio na macho ili wapate kunusa, kusikia na hatimaye kuona hali halisi ya uozo wa chama chao ili waanze kuchukua hatua za kukiponya!

As I said earliera and I say it again, simplicity is the enemy of truth.
 
Wakuu worup! worup! worup!

Maneno ni kumkoma nyani bado tunazifuatilia kwa karibu dataz, more dataz, and more dataz......tutarudi soon stay tuned,

Now let me say this, sina muda na magoi goi wa kufikiri, wanaofikiri bongo ni majuu, bongo mambo yetu huwa tunafanya kibongo bongo tutaendelea kukupa the raw halafu uamue kusuka au kunyoa!

Tutarudi soooon stay tuned hatujamaliza maana we have more dataz than ever before, woooooooooooh!

I love JF!
 
Kitila Mkumbo,
Mkuu umesema mengi ya kweli kabisa maanake nasikia sifa kubwa ya Kikwete ni hiyo..USWAHILI..
Hata viongozi wote aliowaachisha madaraka ama wale waliojiuzuru aliwaambia kwa lugha ya kiungwana inabidi wajikate.. Sio nia yake isipokuwa wao ndio wamekipaka hivyo bora wajiuzuru kufunika kombe sisi watoto wa haramu tupite....
Kwa hiyo upo uwezekano mkubwa kuwa mambo yote haya yanatokea nje ya uwezo wake na kwa sababu hapendi kuharibu jina lake ama la chama huwapa lugha kama ile alopewa Lowassa, Karamagi Mama Meghji na wengine wote waliokwenda kulia mbele yake...
Kushindwa kwake kuongoza upelelezi toka siku zile alipoambiwa kuhusu sakata hili la BAE ni wazi alifahamu kilichokuwa kinaendelea isipokuwa sasa hivi maji yapo shingoni hawezi kuzuia uchunguzi unaofanywa na chombo cha UK ambacho kimepata baraka za Bunge.. Kikwete sio sawa na Watawala wa Saudia ambao huchukuliwa kama Miungu watu wa hapa duniani...naweza kusema wanaabudiwa badala ya kuheshimiwa!
Kama ingetokea Uingereza kutangaza kuwa rais wa Tanzania amezuia uchunguzi wa Chenge kuhusiana na Radar, mkuu swala hili lingefika mbali sana na pengine kuitenganisha CCM..
 
Wakuu worup! worup! worup!

Maneno ni kumkoma nyani bado tunazifuatilia kwa karibu dataz, more dataz, and more dataz......tutarudi soon stay tuned,

We aaaight! we aaaight! we aaaight!

Just get up in dere man, snatch that "dataz" knapsack, and ease out. Uwanja wa Fisi style. You know it. You be doin it the way it should be does.

Then pass that "dataz" down here same way you pass the buddha. Somebody trana steal our money. It aint funny man, we up on they necks and they kids!

Tell u what tho. We gon double check what's in that "dataz" knapsack fore be buy it!

Got to. Got to. You know how we do it!

We ready when you ready man. Be cool now, and remember to dust them fingerprints.
 
Back
Top Bottom