The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

Hata hivyo, pamoja na kuandaliwa maandamano hayo, huenda yakageuka mwiba mchungu kwake kwa kuzomewa kwani eneo hilo ni ngome ya chama cha upinzani cha United Democratic (UDP).


Ama umemind kwasababu ya hiyo kauli hapo juu?
Kuna mtu ambaye hakuwahi kuwa CCM back in a day?
Ama wazazi etc etc!
Sijui kama yo're just taunting ama you're serious!
Lakini hata mimi bado nina uwezo wa kuisamehe CCM kama ikiweza kuleta mabadiko ya kweli na uwajibikaji!
Other than that naona unabakia kwenye ushabiki wa vyma ambao ni kama ule wa Simba na Yanga! Just ushabiki tu..!
Almradi ushinde ubishi na wala sio kutambua kuwa ushabiki sio mzuri kwenye issue nyeti!
 
chenge ni ccm kweli kweli au amezamia nakukuta dili nje nje!!! amekula sana pesa zetu chenge....yeye na wenzake ccm wote hawafai hata kutuambia kitu tuwasikilize......naomba ccm ipotee kabisa maana sio chama cha maendeleo kwetu watanzania,wamekalia dili na kutunyanyasa sisi watanzania kote kote tanzania,zanzibar,dar,mwanza,arusha,kote ni shida.....rais ajui nini cha kufanya!!! epa,kiwira,richmond,iptl....mengine siyajui yote ni feki bila kusahau rada ya chenge.mungu tuombee sisi watanzania tuwe wazalendo wa kweli kwa nchi yetu.
 
vijisenti naye...hana hata mshipa wa haya. Ingekuwa vema na haki akajiuzulu huo ubunge maana laiti angejua kuwa hao wanaoenda kumlaki wanaenda kumchora tuu hata asingesogea hapo. Labda waandishi waamue kufagilia hayo mapokezi, maana kunaweza kuwa na watu chini ya mia lkn ukaambiwa ni umati wa watu.
 
Jamani mnashangaa CHENGE, LOWASSA na wengine kujisafisha, kwanini?????????????? Mafisadi wote hupigiwa kelele kwa siku kadhaa, kisha kujisafisha kwa nia mbalimbali na mambo huisha.

kwani ya SUMAYE si yameisha mbali ya shilingi tirioni kadhaa zilizotangazwa ameweka kwenye akanti ukiacha mali alizonazo.

Mnakumbuka RPC alikutwa na shilingi billioni moja kwenye akaunti yake hapa bongo JK alipokuchukua tu madaraka, mbona anapeta tu
 
Ni vizuri kutokutabilika kwa sababu ukiwa unatabilika kiurahisi watu wanakuzoea hovyo hovyo....Lakini kama hutabiriki mtu atajiuliza mara mbili mbili kabla hajasema au kufanya kitu kwa vile hajui utachukuliaje...

Halafu Chenge si mwana CCM..? Kwa hiyo CCM hoyee...CCM milele

Kutabirika nilikokuwa nikizungumzia ni kule kuwa na Principle ama misimamo isiyoyumba!
Muulize mkuu Zitto atakupa darasa lake!
 
Na sie wananchi tunajidhalilisha, hiyo hadithi ya ufisadi hata ukiamua kumhadithia mbwa ataelewa kuwa vijisent, wakuvanga, mr clean fisadi wooote ni wezi. Lakini kwa kushabikia vyama hata maslahi yetu tunayaweka nyuma. Unaenda kumlaki mtu alikuibia ambaye kaja kwa ndege wakati wewe hata nauli ya basi tu ni ndoto na una mwaka hujatoka nje ya mji, kisa ukata. Watoto wako wanatembea bila viatu wakati watoto wa huyo tunayemtolea jasho kwa kumshangilia kwa wizi wake wanaishi nje ya nchi na wana elimu bora kabisa through pesa za wizi (alizokuibia).

Hawa hawa ndio watakaopewa elfu tano tano na kofia, na bia na nyama choma ili wampe kura uchaguzi ujao, sijui nani ataamsha hawa wananchi maskini ya Mungu!
 
Kama Chenge ataweza kuwaeleza wapiga kura wake wakamuelewa basi nitaogopa tanzania kama ukoma.

Jamani pamoja na kelele ni jumumu la walio na macho kuwakomboa vipofu. Ni jukumu la wale wenye uwezo wa kuona mbali kuwaelimisha wenzao.
 
kakindomaster,
Mfa maji haachi nini vile? Hawa mafisadi sasa wanatapatapa kuanzia kinara wao Lowassa, Karamagi na sasa Chenge. Kitu ambacho hawataki kukubali ni kwamba Watanzania wameshawashtukia. Wewe subiri uone mambo 2010.
 
vijisenti naye...hana hata mshipa wa haya. Ingekuwa vema na haki akajiuzulu huo ubunge maana laiti angejua kuwa hao wanaoenda kumlaki wanaenda kumchora tuu hata asingesogea hapo. Labda waandishi waamue kufagilia hayo mapokezi, maana kunaweza kuwa na watu chini ya mia lkn ukaambiwa ni umati wa watu.

Mafisadi wana haya mama? Si unamuona hata fisadi Mkapa alipotakiwa ajibu tuhuma dhidi yake akajibu, "Niacheni mimi nimesharetire kwenye siasa". Hawana haya wala hawajui vibaya, lakini tutapambana nao kila kona mpaka sheria iwatie adabu na wafilisiwe.
 
Sherehe hizi za Chenge za nini?

John Bwire Mei 7, 2008
Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo

WA kwanza alikuwa Edward Lowassa. Lakini baadhi yetu tulimwelewa. Ilikuwa ni taharuki tu ya joto la wakati huo.

Yeye alikuwa Mtanzania wa pili kujiuzulu uwaziri mkuu, baada ya Julius Nyerere mwaka 1962, japo sababu zao zinapishana sana. Kwa historia hiyo, baadhi wanaweza kufumbia macho mapokezi yake makubwa Monduli.

Lakini haya anayofanya Andrew Chenge, Waziri wa miundombinu aliyejiuzulu, hakika yanadhihirisha namna maadili yetu kama Watanzania yanavyozidi kuzama topeni.

Taarifa kutoka jimboni kwake, Bariadi Magharibi, zinasema kuwa wana CCM wa huko wameandaa sherehe na mapokezi ya ‘kufa mtu.’

Kwa mujibu wa Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Bariadi, Nasunga Lyabuyenze, wananchi wa Bariadi Magharibi “wameandaa mapokezi makubwa na ya kihistoria kwa mwanasiasa huyo (Chenge) licha ya tuhuma za ufisadi” zinazomkabili.

Tusingejali sana kama sherehe kubwa kama hii inayoandaliwa ingekuwa inahusiana na vitu kama vile Chenge kumtoa binti yake, au kumwoza kijana wake. Hakuna angejali kama sherehe hizo zingekuwa za siku yake ya kuzaliwa, ama za kuadhimisha kumbukumbu yoyote ya masuala yake, ama ya familia yake.

Lakini kumwandalia mapokezi kamambe kama hayo kiongozi anayekabiliwa na tuhuma za ufisadi na ambaye baada ya yeye mwenyewe kuzipima ameamua kujiuzulu, hakika si kitu cha kufurahisha hata kidogo kwa wananchi wowote makini.

Tumebaki na mshangao huku tukijiuliza maswali mengi. Ni nini ambacho wenzetu hawa wa Bariadi Magharibi wanakifurahia kutoka kwa Chenge ambacho walibakinacho moyoni hadi alipoandamwa na tuhuma za ufisadi na kujiuzulu? Je, mapokezi haya yana baraka za makao makuu ya CCM?

Vyovyote vile; huu ni utamaduni ambao wenzetu wa Bariadi wanataka kuuanzisha lakini ambao kwa ujumla wake hautasaidia kujenga nchi hii masikini ambayo imekuwa ikikwamishwa na vitendo visivyo na tija vya baadhi yetu, vinavyorudisha nyuma maendeleo. Toka lini tuhuma za ufisadi likawa ni jambo zuri la kufurahisha na kusherehekea?

Ni kweli kwamba Chenge anaheshimika sana jimboni kwake. Ni kweli pia kwamba kabla ya tuhuma dhidi yake kuanikwa, wengi walikuwa na imani naye kubwa. Ni kweli pia kwamba baada ya haya yote yaliyomfika anahitaji watu wa kumliwaza. Ni hulka ya binadamu. Nasi tunaielewa. Lakini ni kweli pia huku kunakoandaliwa na wanajimbo lake ni kumliwaza kwa aina yake kwenye tafsiri ya kuuenzi ufisadi.

Na wala Chenge si waziri wa kwanza kujiuzulu nchini. Majuzi tu hapa mawaziri wawili katika Baraza alilokuwamo walijiuzulu. Lakini hatujasikia Dk. Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi, ambao kwa macho ya umma wa kawaida, wana tuhuma kama za Chenge, wakitutangazia jinsi wapiga kura wao wanavyofurahia tuhuma zilizowafika hadi kuwandaalia mapokezi ya kishindo.

Na si hao tu. Tutashangaa kama Watanzania watakuwa wamesahau kwamba katika muda si mrefu uliopita, kina Dk. Juma Ngasongwa, Iddi Simba, Profesa Simon Mbilinyi, Dk. Hassy Kitine na Kilontsi Mporogomyi walijiuzulu kwa tuhuma mbalimbali, lakini hatukupata kusikia wakiandaliwa mapokezi ya kuwapongeza majimboni kwao.

Kwamba leo Chenge anataka kuonyeshwa kwamba amefanya jambo la kishujaa sana na hivyo kustahili mapokezi makubwa, ni utamaduni ambao haupaswi kuachwa ukue, na kwa hakika ni jambo linalodhihirisha ni jinsi gani CCM imekosa uongozi wenye busara katika jimbo hili.

Lakini pia, kwa kiasi fulani, inaonyesha ni namna gani CCM inashindwa kuongoza vyema wanachama wake na jumuiya zake.

Maana, haiwezekani jumuiya ya vijana ya chama hicho mkoa wa Tanga (UVCCM-Tanga) itoe tamko la kuwataka viongozi wa CCM wanaotuhumiwa kwa ufisadi wajiondoe madarakani halafu katika wiki hiyo hiyo, CCM wilaya ya Bariadi imwandalie mapokezi kamambe mmoja wa hao wanaotuhumiwa kwa ufisadi!

Ni dhahiri kuna mushkeli, na itashangaza kama uongozi wa juu wa CCM utashindwa kusoma maandishi ukutani na kuanza kuchukua hatua kudhibiti utamaduni huu wa kuuenzi ufisadi ambao unatutia aibu sote.
 
Hawa wasukuma wa bariadi magaharibi wanauelezea nini umma wa Tanzania?
Kwa ujinga na upuuzi huu wa kushabikia wezi,Kumbe ndo maana hata yule M kanada Williamsons aliwadanganya pale MWADUI akakusanya almas zote,wala hata hawakujua ni mawe ya thamani.

Chenge amechangia sehumu kubwa nchi hii kuwa maskini kwa kusaini mikataba mibovu leo wanajipanga barabarani kumpokea?tugasa!!!
 
Hawa wasukuma wa bariadi magaharibi wanauelezea nini umma wa Tanzania?
Kwa ujinga na upuuzi huu wa kushabikia wezi, Kumbe ndo maana hata yule Mkanada Williamsons aliwadanganya pale MWADUI akakusanya almas zote, wala hata hawakujua ni mawe ya thamani. Chenge amechangia sehumu kubwa nchi hii kuwa maskini kwa kusaini mikataba mibovu leo wanajipanga barabarani kumpokea?tugasa!!!

Wakati Williamson anaingia Usukumani watu walikuwa chini ya ukoloni wa Mwingereza na hawakuwa na elimu, mwamko wala uzalendo. Leo hii mwaka 2008, karne ya 21 na miaka 47 baada ya uhuru, siwaelewi Wasukuma hawa. Uuwiiiii. Natamani NG'WANAMALUNDI angefufuka awanyoshee kidole CHenge na mashabiki wake wa Bariadi Magharibi wakauke kama kuni. Madudu matupu, kudadeki!!!! kwi kwi kwi kwi !!!!!!
 
Sherehe hizi za Chenge za nini?

John Bwire Mei 7, 2008
Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo

WA kwanza alikuwa Edward Lowassa. Lakini baadhi yetu tulimwelewa. Ilikuwa ni taharuki tu ya joto la wakati huo.

Yeye alikuwa Mtanzania wa pili kujiuzulu uwaziri mkuu, baada ya Julius Nyerere mwaka 1962, japo sababu zao zinapishana sana. Kwa historia hiyo, baadhi wanaweza kufumbia macho mapokezi yake makubwa Monduli.

Lakini haya anayofanya Andrew Chenge, Waziri wa miundombinu aliyejiuzulu, hakika yanadhihirisha namna maadili yetu kama Watanzania yanavyozidi kuzama topeni.

Taarifa kutoka jimboni kwake, Bariadi Magharibi, zinasema kuwa wana CCM wa huko wameandaa sherehe na mapokezi ya ‘kufa mtu.’

Kwa mujibu wa Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Bariadi, Nasunga Lyabuyenze, wananchi wa Bariadi Magharibi “wameandaa mapokezi makubwa na ya kihistoria kwa mwanasiasa huyo (Chenge) licha ya tuhuma za ufisadi” zinazomkabili.

Tusingejali sana kama sherehe kubwa kama hii inayoandaliwa ingekuwa inahusiana na vitu kama vile Chenge kumtoa binti yake, au kumwoza kijana wake. Hakuna angejali kama sherehe hizo zingekuwa za siku yake ya kuzaliwa, ama za kuadhimisha kumbukumbu yoyote ya masuala yake, ama ya familia yake.

Lakini kumwandalia mapokezi kamambe kama hayo kiongozi anayekabiliwa na tuhuma za ufisadi na ambaye baada ya yeye mwenyewe kuzipima ameamua kujiuzulu, hakika si kitu cha kufurahisha hata kidogo kwa wananchi wowote makini.

Tumebaki na mshangao huku tukijiuliza maswali mengi. Ni nini ambacho wenzetu hawa wa Bariadi Magharibi wanakifurahia kutoka kwa Chenge ambacho walibakinacho moyoni hadi alipoandamwa na tuhuma za ufisadi na kujiuzulu? Je, mapokezi haya yana baraka za makao makuu ya CCM?

Vyovyote vile; huu ni utamaduni ambao wenzetu wa Bariadi wanataka kuuanzisha lakini ambao kwa ujumla wake hautasaidia kujenga nchi hii masikini ambayo imekuwa ikikwamishwa na vitendo visivyo na tija vya baadhi yetu, vinavyorudisha nyuma maendeleo. Toka lini tuhuma za ufisadi likawa ni jambo zuri la kufurahisha na kusherehekea?

Ni kweli kwamba Chenge anaheshimika sana jimboni kwake. Ni kweli pia kwamba kabla ya tuhuma dhidi yake kuanikwa, wengi walikuwa na imani naye kubwa. Ni kweli pia kwamba baada ya haya yote yaliyomfika anahitaji watu wa kumliwaza. Ni hulka ya binadamu. Nasi tunaielewa. Lakini ni kweli pia huku kunakoandaliwa na wanajimbo lake ni kumliwaza kwa aina yake kwenye tafsiri ya kuuenzi ufisadi.

Na wala Chenge si waziri wa kwanza kujiuzulu nchini. Majuzi tu hapa mawaziri wawili katika Baraza alilokuwamo walijiuzulu. Lakini hatujasikia Dk. Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi, ambao kwa macho ya umma wa kawaida, wana tuhuma kama za Chenge, wakitutangazia jinsi wapiga kura wao wanavyofurahia tuhuma zilizowafika hadi kuwandaalia mapokezi ya kishindo.

Na si hao tu. Tutashangaa kama Watanzania watakuwa wamesahau kwamba katika muda si mrefu uliopita, kina Dk. Juma Ngasongwa, Iddi Simba, Profesa Simon Mbilinyi, Dk. Hassy Kitine na Kilontsi Mporogomyi walijiuzulu kwa tuhuma mbalimbali, lakini hatukupata kusikia wakiandaliwa mapokezi ya kuwapongeza majimboni kwao.

Kwamba leo Chenge anataka kuonyeshwa kwamba amefanya jambo la kishujaa sana na hivyo kustahili mapokezi makubwa, ni utamaduni ambao haupaswi kuachwa ukue, na kwa hakika ni jambo linalodhihirisha ni jinsi gani CCM imekosa uongozi wenye busara katika jimbo hili.

Lakini pia, kwa kiasi fulani, inaonyesha ni namna gani CCM inashindwa kuongoza vyema wanachama wake na jumuiya zake.

Maana, haiwezekani jumuiya ya vijana ya chama hicho mkoa wa Tanga (UVCCM-Tanga) itoe tamko la kuwataka viongozi wa CCM wanaotuhumiwa kwa ufisadi wajiondoe madarakani halafu katika wiki hiyo hiyo, CCM wilaya ya Bariadi imwandalie mapokezi kamambe mmoja wa hao wanaotuhumiwa kwa ufisadi!

Ni dhahiri kuna mushkeli, na itashangaza kama uongozi wa juu wa CCM utashindwa kusoma maandishi ukutani na kuanza kuchukua hatua kudhibiti utamaduni huu wa kuuenzi ufisadi ambao unatutia aibu sote.

ITS A SHAME KWA WATU WENYE AKILI NA BUSARA KUMPOKEA KWA SHEREHE MTU WA AINA HII. ONA SPEECH YAKE NI MATUSI, ANAWAAMBIA HAWEZI KUJIUA AACHE VISENTI VYAKE, NA WASUKUMA WANAONA YUKO SAWA!!AU WALIMTUMA AKAJIKUSANYIE KWA MANUFAA YAKE NA NANI?? HUU NI UFINYU WA MAWAZO. SIAMINI KWA WATU WENYE KUFIKIRIA KWAMBA WANGESTAHILI HATA KUKAA NA HUYU FISADI MEZA MOJA. NINACHOKIONA HAPA, NI KWAMBA, HUENDA HAO VIONGOZI WALIOANDAA MAPOKEZI YAKE NI MAPANDIKIZI YAKE HIVYO WANALIPA FADHILA KAMA ILIVYO DESTURI YA WATAWALA WA CHUKUA CHAKO MAPEMA. WAPINZANI WAKIITISHA MAANDAMANO KUPINGA UOZO WA SERIKALI WANAAMBIWA HAKUNA ULINZI HIVYO HAIRUHUSIWI, BEN KAZOMEWA KIKOSI KIMEMWAGWA MTAANI, CHENGE KAENDAKUWATUKANA TENA WATANZANIA KUPITIA KWA WASUKUMA DOLA INAMPA TUFF!! WHAT THE HELL IS THIS???? HAPA NDIPO WANAHARAKATI TUNAPOFIKIA HATA KUMKOSEA MUNGU NA KUJUTA KUZALIWA TANZANIA. NINA IMANI THERE COMES A TIME TUTAJIKOMBOA KUTOKA KWA HAWA MAFISADI. KAMA SIO KWA NGUVU ZETU, BASI HATA KWA SALA ZETU NA MARAFIKI ZETU, TUTAKUWA HURU KAMA MUNGU ALIVYOWAHURUMIA WANA WA ISRAEL.
TUKESHE TUKIOMBA KWANI BADO KITAMBO KIDOGO.
 
Chenge: Nimezushiwa

na Jane Kajoki, Bariadi


MBUNGE wa Bariadi Magharibi aliyejiuzulu uwaziri hivi karibuni kwa kashfa ya kukutwa na fedha zinazohusishwa na ufisadi, Andrew Chenge amewataka wananchi wa jimbo lake kuendelea kumwamini kwa kuwa yeye ni mtu safi na asiye na hatia yoyote kwani tuhuma dhidi yake ni za kuzushwa.

Mbali ya hilo, Chenge alisema alifikia uamuzi wa kujiuzulu wadhifa wa Waziri wa Miundombinu zaidi ya wiki mbili zilizopita si kwa sababu ya kukiri makosa, bali ili kutoa fursa kwa taasisi zinazochunguza kashfa yake kufanya kazi yake kwa uwazi.

Chenge ambaye jana alihutubia mikutano ya hadhara katika maeneo ya Bariadi Mjini, Ramadi, Nyakabimbi na Kapiwi, alisema wakazi wa Dar es Salaam ndio ambao wamekuwa wakimuona kuwa mtu asiyefaa kutokana na kubebeshwa tuhuma zisizo za ukweli, ikiwa ni pamoja na kuzushiwa kifo.

“Dar es Salaam wanasema sifai labda kwa sababu ya sura yangu...Pamoja na watu wa Dar es Salaam kupiga kelele kuwa sifai, naamini sina hatia yoyote, na ndiyo maana nilijiuzulu. Ninyi wakazi wa jimboni kwangu ndio mnajua kama sifai au nafaa.

“Haya mambo yaliyotokea ni ajali ya kisiasa. Ni mambo ya kupikwa na watu, lakini kwa tuhuma hizi wacha tuwape nafasi waendelee na uchunguzi. Sitakiwi kuzungumzia hilo kwa sasa, nimekuja nyumbani kuhimiza shughuli za maendeleo katika jimbo letu katika nyanja zote za barabara, elimu, afya na maji,” alisema Chenge ambaye alivuta umati mkubwa wa wananchi waliokuwa wakimshangilia kila alipokuwa akihutubia.

Alisema pamoja na kujiuzulu uwaziri, aliahidi kuendelea kuwatumikia wananchi wa jimbo lake na akasema anaamini ifikapo mwaka 2010 atakuwa ametekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005-2010.

“Walio na ndoto za ubunge tukutane kwenye hoja za utekelezaji wa ilani mwaka 2010. Mmeona tulivyojenga shule za sekondari, barabara, mabwawa, visima, vituo vya afya vyote hivyo ni katika jimbo letu. Pamoja na habari ya kuzushiwa kifo, nawaomba mtulie, tushirikiane kwa kutembea kifua mbele kufanya kazi na kujiletea maendeleo,” alisema Chenge ambaye anatembelea jimbo lake kwa mara ya kwanza tangu ajiuzulu.

Akiwa katika Kijiji cha Dutwa alisema alitaja vijisenti si kwa nia ya kukejeli bali akiwa na mtazamo wa Kisukuma ambao wao wanapoongelea ng’ombe 100 kwa mfano wanasema ‘vijing’ombe’.

Hii ni mara ya pili kwa Chenge kuzungumzia kauli yake ya vijisenti ambayo kwa kiwango kikubwa ndiyo inayoonekana kuwa iliyokuza tuhuma alizokuwa akihusishwa nazo.

Kwa mara ya kwanza, Chenge alizungumzia kauli yake hiyo jijini Dar es Salaam wakati alipofanya mahojiano kwa njia ya simu na gazeti hili, ambapo aliwaomba radhi Watanzania ambao walikwazika au kuumizwa na kauli yake hiyo ya vijisenti.

Alisema halikuwa lengo lake kuwakera wananchi kwa kauli hiyo iliyozua mjadala kiasi cha baadhi ya makundi ya watu wa kada tofauti kutoa maoni yao wakimtaka Rais Jakaya Kikwete amwajibishe.

“Mimi siyo Mzaramo. Hiki ni Kiswahili. Sisi wengine kule Usukumani kusema vijimambo, au vijisenti, vijitoto hivi ni kawaida kwa desturi zetu...ndiyo maana napenda kusema wazi kwamba iwapo kuna Watanzania niliwaumiza kwa kauli ile niliyoitoa kwa nia njema kabisa na wala si kwa lengo la kuwakejeli, naomba radhi kwa hilo,” alisema Chenge wakati huo.

Tuhuma dhidi ya Chenge ziliandikwa kwa mara ya kwanza katika gazeti la The Guardian la nchini Uingereza likikariri taarifa kutoka Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa Makubwa ya Jinai ya nchini humo (SFO).

Gazeti hilo liliandika kuwa, uchunguzi wa SFO uligundua akaunti moja inayohusishwa na Chenge ikiwa na zaidi ya dola za Marekani milioni moja iliyopo kwenye kisiwa cha Jersey.

Gazeti hilo liliandika kwamba, SFO ilikuwa ikitarajia kuanza upya kufanya uchunguzi kuhusu fedha hizo ili kuangalia iwapo zilikuwa na uhusiano na zile zinazoaminika kuwa zilitolewa kwa njia ya rushwa wakati Tanzania iliponunua rada ya kijeshi kutoka nchini humo kwa paundi milioni 28 ambazo ni sawa na shilingi bilioni 70, mwaka 2002.

The Guardian katika habari yake hiyo liliripoti kuwa, taarifa hizo zinakuja ikiwa ni miaka mitatu sasa tangu Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru) kwa kushirikiana na SFO na taasisi za uchunguzi za Uswisi na Jersey zilipoanza kuchunguza kuhusu kashfa nzima ya ununuzi wa rada.

Gazeti hilo lilimkariri Waziri Chenge akikiri kwamba fedha hizo ni zake na akatumia fursa hiyo kukanusha kuwapo kwa uhusiano wowote kati ya fedha hizo na kashfa nzima ya ununuzi wa rada, uliofanywa wakati yeye akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

“Jambo la wazi linalotaka kuonekana hapa ni kwamba mimi nilipokea kwa lengo la kujinufaisha mwenyewe fedha za rushwa kutoka BAE. Huu ni uongo,” alisema Chenge.

Aidha, gazeti hilo lilimkariri Chenge akisema kuwa, wakati rada hiyo ilipokuwa ikinunuliwa yeye alihusika kwa kiwango kidogo sana katika mchakato mzima, kwani jambo hilo lilishughulikiwa na wizara nyingine na uamuzi ukaidhinishwa na Baraza la Mawaziri.

Mbali ya hilo, gazeti hilo lilimkariri mwanasheria wa Chenge anayeishi Cleveland, Ohio, nchini Marekani, J Lewis Madorsky, akikanusha kwa niaba ya mteja wake huyo, kuwapo kwa uhusiano wowote kati ya fedha zake na tuhuma zozote.

“Wakati tukitambua kuwa masuala hayo yalitokea muda mrefu uliopita, tunaweza tu tukathibitisha kuwa, tuhuma zozote za ukiukwaji wa sheria, ukiukwaji wa maadili, kutenda isivyo sawa na mambo mengine ya hivyo dhidi ya mteja wetu ni mambo ambayo kimsingi tunayakanusha kwa nguvu kubwa,” alisema mwanasheria huyo wa Chenge.

Hata hivyo, gazeti hilo liliandika uchunguzi huo dhidi ya Chenge unamfanya yeye kuwa tu shahidi muhimu, kwani wanaielenga zaidi BAE ambayo inadaiwa ilimlipa wakala mmoja wa Tanzania mamilioni ya fedha ili kujenga ushawishi wa rada iliyokuwa ikiiuza kununuliwa.

Wakala huyo ambaye amekuwa akitajwa kwa muda mrefu, na ambaye sasa anaaminika kukimbia nchini na kutafutwa na polisi wa kimataifa ni, Shailesh Vithlani

Source: Tanzania Daima


Ni kweli watu wa Dar es Salaam mnachukia Chenge kwa sabanu ya sura yake? ... ama kwa kutokujua kwake Kiswahili? ndiyo maana mnamwita fisadi..haya Kazi kwetu! Hayo ni maelezo ya Chenge, wala siyo yangu mimi
 
Kama tumefika mahali ambapo kiongozi mwenye mabilioni kwenye akaunti zake ndani na nje ya nchi hii maskini anasimama kwenye jukwaa bila aibu na kusema "nimeonewa", tumekwisha kama Taifa! Sasa tutegemee kila mfungwa akitoka jela kwa makosa ya wizi, ujambazi,uuaji, kubaka n.k. kupokewa na magari na pikipiki na kutangaza kuwa "ilikuwa ajali tu ya kibiashara"! Lazaros
 
Kama tumefika mahali ambapo kiongozi mwenye mabilioni kwenye akaunti zake ndani na nje ya nchi hii maskini anasimama kwenye jukwaa bila aibu na kusema "nimeonewa", tumekwisha kama Taifa! Sasa tutegemee kila mfungwa akitoka jela kwa makosa ya wizi, ujambazi,uuaji, kubaka n.k. kupokewa na magari na pikipiki na kutangaza kuwa "ilikuwa ajali tu ya kibiashara"! Lazaros

ILISHATOKE MY DEAR FRIEND!!!

KUNA BWANA MMOJA ALITOLEWA KWENYE KIFUNGO CHA MIKA 30 MKAZI WA ARUSHA, AMBAYE ALIHUKUMIWA KWA MAKOSA YA UJAMBAZI WA SILAHA. KUTOKANA NA INFLUENCE ALIYOKUWA NAYO KWA MAFISADI AMBAO TAYARI WAMEACHIA NGAZI, ILITUNGWA MIZENGWE AKATOLEWA KWA MAANDAMANO YA KUTISHA YA MAVX NA MSURURU WA WAHUNI WENZAKE. BAADA YA KUTOKA YUKO NJE YA NCHI NA SIDHANI KAMA ATATHUBUTU KURUDI BAADA YA JAMMA YAKE KUACHIA NGAZI. HII NDIYO TANZANIA BWANA. UKIWA NA KITU HUNA HATIA. NAOMBA USINILAZIMISHE KULIA.
 
ILISHATOKE MY DEAR FRIEND!!!

KUNA BWANA MMOJA ALITOLEWA KWENYE KIFUNGO CHA MIKA 30 MKAZI WA ARUSHA, AMBAYE ALIHUKUMIWA KWA MAKOSA YA UJAMBAZI WA SILAHA. KUTOKANA NA INFLUENCE ALIYOKUWA NAYO KWA MAFISADI AMBAO TAYARI WAMEACHIA NGAZI, ILITUNGWA MIZENGWE AKATOLEWA KWA MAANDAMANO YA KUTISHA YA MAVX NA MSURURU WA WAHUNI WENZAKE. BAADA YA KUTOKA YUKO NJE YA NCHI NA SIDHANI KAMA ATATHUBUTU KURUDI BAADA YA JAMMA YAKE KUACHIA NGAZI. HII NDIYO TANZANIA BWANA. UKIWA NA KITU HUNA HATIA. NAOMBA USINILAZIMISHE KULIA.

Anaitwa Justin Nyari.
 
Watanzania wenzangu nchi yetu hapa ndipo ilipofika, ili uwe mtukufu lazima uambatane na viteno vya kifisadi, ili watanzania wakudharau uwe mtu mwema na mtiifu na mwenye uchungu na nchi hii, ukiwa fisadi bwana kama Chenge huwezi kuwa na hatia sata siku moja, Tanzania imeshapelekwa kuzimu na wengi waliomo ndani yake wamekuwa ni mazezeta usiku kwao ni mchana na mchana kwao ni usiku, chini ya uongozi wa CCM, Chukua Chako Mapema na Chenge ameshafaulu kwa hilo. Poleni sana wale wenzangu na mimi iko siku moja itakua kweli
 
Back
Top Bottom