Lunyungu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2006
- 8,873
- 1,919
Posted Date::5/8/2008
Chenge: Siwezi kujiua niache visenti vyangu
* Atamba akiwahutubia wananchi wa Bariadi
* Vigogo wa CCM Mwanza, Shinyanga wamsindikiza
* Mkuu wa Wilaya aongoza mapokezi mjini
* Makada Bariadi wapinga tamko la UVCCM Tanga
Frederick Katulanda, Bariadi
LICHA ya aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge kuwaomba radhi Watanzania kwa kudai kuwa Sh1.2bilioni anazodaiwa kuzificha katika Kisiwa cha Jersey ni vijisenti, jana alirudia tena usemi huo wakati akihutubia mamia ya wakazi wa Bariadi mjini.
Chenge aliwaambia wananchi waliofika kumsikiliza kuwa hawezi kunywa sumu na kuacha vijisenti vyake nyuma.
"Mnyantuzu, kamwe siwezi kunywa sumu ili nife na kuacha vijisenti vyangu nyuma..." alisema Chenge.
Akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara mjini Bariadi jana, Chenge alisema kuwa amesikitishwa sana kuzushiwa kuwa amefariki dunia na kusema kwamba hawezi kujiua na kuviacha vijisenti vyake.
Akizungumza kwa Lugha ya Kisukuma Chenge alisema: "Bhadugu bhane wakayomba niachile olwa sumu, bhadugu Mnyantuzu ong'wa sumu, oleka vijisenti byakwe?". Alikuwa ana maanisha kuwa, akiwa kama Msukuma Mnyantuzu hawezi kufa kwa kujiua na kuacha vijisenti vyake.
Wakati Chenge akirejea kutoka safari ya China, alisema kwamba amesikia kuna watu wanalalamikia vijisenti na alipobanwa na waandishi wa habari kuwa bilioni moja ni vijisenti, alisema kwamba kila mtu ana viwango vyake.
Mara baada ya kutoa matamshi hayo, watu mbalimbali wakiwamo wanasiasa walijitokeza kulaani matamshi hayo na kumtaka aeleze alivyopata hizo fedha, ikiwa ni pamoja na kuachia madaraka ya uwaziri.
Baada ya hali hiyo kuwa tete, Chenge kupitia vyombo vya habari aliomba msamaha Watanzania kwamba, kwa Wasukuma vijisenti ni neno la kawaida na kwamba yeye si mjuzi wa Kiswahili kama ilivyo kwa Wazaramo.
Pamoja na hayo, mamia ya wananchi wa Wilaya ya Bariadi wakiwamo viongozi wa CCM, walijitokeza kumpokea Chenge ambaye alihutubia mkutano wa hadhara mjini humo.
Akisoma risala ya chama, Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Bariadi, Masunga Lyabuyenze alisema wao kama wana-CCM na viongozi wa chama, wanapinga na kulaani tamko la kikao cha Baraza la Vijana wa CCM Mkoa wa Tanga kuwa waliokumbwa na tuhuma za ufisadi waachie ngazi.
Alidai tamko hilo lilipaswa kungoja uchunguzi ukamilike kwanza kwa vile Chenge anatuhumiwa tu na kwamba hazijathibitika kama ni kweli.
Katika hatua nyingine, viongozi waandamizi wa CCM wa mikoa ya Mwanza na Shinyanga jana waliongoza maandamano na mapokezi 'ya kishindo' ya Chenge ambaye alirejea kwa mara ya kwanza jimboni kwake Bariadi Magharibi, baada ya kulazimika kujiuzulu kwa kashfa ya kujilimbikizia fedha za kigeni dola milioni moja (Sh1.2bilioni) huko Uingereza zinazodaiwa kuhusika na malipo ya rada.
Viongozi walioshiriki katika maandamano yaliyoanzia Mwanza hadi Bariadi ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza,Clement Mabina na makada mbalimbali wa mkoa huo, na alipofika Bariadi alipokelewa na Mwenyekiti wa Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja.
Mbali na viongozi wa chama, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Baraka Konisaga aliongoza magari kutoka Bariadi kwenda kumpokea Chenge na msafara wake kutoka Mwanza.
Safari ya Chenge kujisafisha ilianzia jijini Mwanza juzi jioni, ambako mara baada ya kupokelewa alipelekwa katika ofisi ya CCM mkoa na kusaini kitabu cha wageni.
Akimkaribisha Mwanza Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza, Rajabu Kundya alisema mapokezi hayo kwao yamekuwa na maana mbili, ya kwanza ikiwa ni pole kutokana na misukosuko hiyo na pili ikiwa ni kumpongeza kwa ujasiri ambao aliuchukua kuamua kujiuzulu kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma kufanyika.
Chenge aliondoka jijini Mwanza asubihi ambako msafara wake ulipokelewa wilayani Magu katika ofisi ya CCM kwa magari 22 yakiwemo mabasi madogo matano, malori aina ya fuso saba na gari ndogo pamoja na pikipiki kumi ambazo ziliandaliwa na Mabina.
Hata hivyo, idadi ya magari iliongezeka katika mji mdogo wa Ramadi ambako timu ya wafanyabiashara wa Bariadi mjini wanaodaiwa kumuunga mkono Chenge walipofika kumpokea wakiwa na malori mengine sita na magari zaidi ya 15 wakiongozwa na Konisaga.
Akizungumza katika Vijiji vya Dutwa na Sapiwi akiwa njiani kuelekea Bariadi mjini, Chenge alisema baada ya kujiuzulu uwaziri na baadhi ya watu wa Dar es Salaam wamekuwa wakimsakama wakidai kuwa hafai kuwa mbunge.
Hata hivyo, alisema uamuzi wa kutofaa ama kufaa wanajua wananchi wa Bariadi ambao ndiyo wapiga kura wake.
"Mimi ninaamini niko safi, tungoje uchunguzi, lakini kuna watu Dar wanapiga kelele eti sifai kuwa mbunge, jamani kama sifai kuwa mbunge mnaojua sifai ni ninyi wananchi wa Bariadi wala siyo wao, lakini maandiko matakatifu yanasema mpende binadamu mwenzako, wao wamenizushia Chenge (kajiua kwa sumu) wamepata faida gani,"
alihoji.
Alisema kuwa lengo la safari yake si kujisafisha bali kuhimiza maendeleo na kuwaahidi wananchi wa Bariadi Magharibi kuwa, ahadi zake ziko pale pale ikiwemo ile ya kujenga barabara ya Shinyanga kwenda Musoma kupitia Bariadi, hadi Ramadi wilayani Magu kwa kiwango cha lami ambayo alidai inaendelea kushughulikiwa.
Chenge alijiuzulu uwaziri wa Miundombinu kuhusiana na kuficha Sh1.2 bilioni katika Kisiwa cha Jersey ambazo zinachunguzwa na Taasisi ya Kuchunguza Makosa Makubwa ya Jinai ya Uingereza (SFO) ili kubaini kama zina uhusiano na rushwa kwenye mchakato wa ununuzi wa rada.
Chenge: Siwezi kujiua niache visenti vyangu
* Atamba akiwahutubia wananchi wa Bariadi
* Vigogo wa CCM Mwanza, Shinyanga wamsindikiza
* Mkuu wa Wilaya aongoza mapokezi mjini
* Makada Bariadi wapinga tamko la UVCCM Tanga
Frederick Katulanda, Bariadi
LICHA ya aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge kuwaomba radhi Watanzania kwa kudai kuwa Sh1.2bilioni anazodaiwa kuzificha katika Kisiwa cha Jersey ni vijisenti, jana alirudia tena usemi huo wakati akihutubia mamia ya wakazi wa Bariadi mjini.
Chenge aliwaambia wananchi waliofika kumsikiliza kuwa hawezi kunywa sumu na kuacha vijisenti vyake nyuma.
"Mnyantuzu, kamwe siwezi kunywa sumu ili nife na kuacha vijisenti vyangu nyuma..." alisema Chenge.
Akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara mjini Bariadi jana, Chenge alisema kuwa amesikitishwa sana kuzushiwa kuwa amefariki dunia na kusema kwamba hawezi kujiua na kuviacha vijisenti vyake.
Akizungumza kwa Lugha ya Kisukuma Chenge alisema: "Bhadugu bhane wakayomba niachile olwa sumu, bhadugu Mnyantuzu ong'wa sumu, oleka vijisenti byakwe?". Alikuwa ana maanisha kuwa, akiwa kama Msukuma Mnyantuzu hawezi kufa kwa kujiua na kuacha vijisenti vyake.
Wakati Chenge akirejea kutoka safari ya China, alisema kwamba amesikia kuna watu wanalalamikia vijisenti na alipobanwa na waandishi wa habari kuwa bilioni moja ni vijisenti, alisema kwamba kila mtu ana viwango vyake.
Mara baada ya kutoa matamshi hayo, watu mbalimbali wakiwamo wanasiasa walijitokeza kulaani matamshi hayo na kumtaka aeleze alivyopata hizo fedha, ikiwa ni pamoja na kuachia madaraka ya uwaziri.
Baada ya hali hiyo kuwa tete, Chenge kupitia vyombo vya habari aliomba msamaha Watanzania kwamba, kwa Wasukuma vijisenti ni neno la kawaida na kwamba yeye si mjuzi wa Kiswahili kama ilivyo kwa Wazaramo.
Pamoja na hayo, mamia ya wananchi wa Wilaya ya Bariadi wakiwamo viongozi wa CCM, walijitokeza kumpokea Chenge ambaye alihutubia mkutano wa hadhara mjini humo.
Akisoma risala ya chama, Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Bariadi, Masunga Lyabuyenze alisema wao kama wana-CCM na viongozi wa chama, wanapinga na kulaani tamko la kikao cha Baraza la Vijana wa CCM Mkoa wa Tanga kuwa waliokumbwa na tuhuma za ufisadi waachie ngazi.
Alidai tamko hilo lilipaswa kungoja uchunguzi ukamilike kwanza kwa vile Chenge anatuhumiwa tu na kwamba hazijathibitika kama ni kweli.
Katika hatua nyingine, viongozi waandamizi wa CCM wa mikoa ya Mwanza na Shinyanga jana waliongoza maandamano na mapokezi 'ya kishindo' ya Chenge ambaye alirejea kwa mara ya kwanza jimboni kwake Bariadi Magharibi, baada ya kulazimika kujiuzulu kwa kashfa ya kujilimbikizia fedha za kigeni dola milioni moja (Sh1.2bilioni) huko Uingereza zinazodaiwa kuhusika na malipo ya rada.
Viongozi walioshiriki katika maandamano yaliyoanzia Mwanza hadi Bariadi ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza,Clement Mabina na makada mbalimbali wa mkoa huo, na alipofika Bariadi alipokelewa na Mwenyekiti wa Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja.
Mbali na viongozi wa chama, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Baraka Konisaga aliongoza magari kutoka Bariadi kwenda kumpokea Chenge na msafara wake kutoka Mwanza.
Safari ya Chenge kujisafisha ilianzia jijini Mwanza juzi jioni, ambako mara baada ya kupokelewa alipelekwa katika ofisi ya CCM mkoa na kusaini kitabu cha wageni.
Akimkaribisha Mwanza Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza, Rajabu Kundya alisema mapokezi hayo kwao yamekuwa na maana mbili, ya kwanza ikiwa ni pole kutokana na misukosuko hiyo na pili ikiwa ni kumpongeza kwa ujasiri ambao aliuchukua kuamua kujiuzulu kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma kufanyika.
Chenge aliondoka jijini Mwanza asubihi ambako msafara wake ulipokelewa wilayani Magu katika ofisi ya CCM kwa magari 22 yakiwemo mabasi madogo matano, malori aina ya fuso saba na gari ndogo pamoja na pikipiki kumi ambazo ziliandaliwa na Mabina.
Hata hivyo, idadi ya magari iliongezeka katika mji mdogo wa Ramadi ambako timu ya wafanyabiashara wa Bariadi mjini wanaodaiwa kumuunga mkono Chenge walipofika kumpokea wakiwa na malori mengine sita na magari zaidi ya 15 wakiongozwa na Konisaga.
Akizungumza katika Vijiji vya Dutwa na Sapiwi akiwa njiani kuelekea Bariadi mjini, Chenge alisema baada ya kujiuzulu uwaziri na baadhi ya watu wa Dar es Salaam wamekuwa wakimsakama wakidai kuwa hafai kuwa mbunge.
Hata hivyo, alisema uamuzi wa kutofaa ama kufaa wanajua wananchi wa Bariadi ambao ndiyo wapiga kura wake.
"Mimi ninaamini niko safi, tungoje uchunguzi, lakini kuna watu Dar wanapiga kelele eti sifai kuwa mbunge, jamani kama sifai kuwa mbunge mnaojua sifai ni ninyi wananchi wa Bariadi wala siyo wao, lakini maandiko matakatifu yanasema mpende binadamu mwenzako, wao wamenizushia Chenge (kajiua kwa sumu) wamepata faida gani,"
alihoji.
Alisema kuwa lengo la safari yake si kujisafisha bali kuhimiza maendeleo na kuwaahidi wananchi wa Bariadi Magharibi kuwa, ahadi zake ziko pale pale ikiwemo ile ya kujenga barabara ya Shinyanga kwenda Musoma kupitia Bariadi, hadi Ramadi wilayani Magu kwa kiwango cha lami ambayo alidai inaendelea kushughulikiwa.
Chenge alijiuzulu uwaziri wa Miundombinu kuhusiana na kuficha Sh1.2 bilioni katika Kisiwa cha Jersey ambazo zinachunguzwa na Taasisi ya Kuchunguza Makosa Makubwa ya Jinai ya Uingereza (SFO) ili kubaini kama zina uhusiano na rushwa kwenye mchakato wa ununuzi wa rada.