Tresor Mandala
JF-Expert Member
- Aug 20, 2010
- 37,483
- 78,733
Hivi ukinunua silaha nje ya nchi unaweza kuisajiri/kuja nayo Tanzania?
Mkuu Si kila kitu tunaweza share hapa,kutokana na unyeti wake naomba ufike kwa mtu mwenye cheo cha msajili wa silaha pale polisi makao makuu ghorofa ya 5 utapata majibu yote.
hapana mkuu, just self defenceJamaa asubuhi asubuhi yote hii unaanza kuulizia upatikanaji wa bastola,vibaka walitikisa dirisha nini?
Nenda kwenye maduka ya Tanganyika Arms yaliyo mkoani kwako au kama uko Dar unaweza kwenda kununua pale makao makuu ya jeshi Upanga.
Hapo watakutajia aina mbalimbali na kukupa uzishike na kuzikagua.
Kama kuna ambayo utaipenda unatakiwa kulipia full amount lakini huchukui silaha.
Baada ya hapo wanakupa fomu 1in 4 copies, ambayo utaenda nayo Serikali ya mtaa wako, Kamati ya usalama wa mtaa itakaa na kukujadili kama unastahili kupewa kibali na kama wameridhika Watasaini na kuzifoward hizo fomu katika Kamati ya Usalama ya Wilaya ambapo watazipitia na kukujadili tena na kama wameridhika na maelezo yako watazifoward katika Kamati ya Usalama ya mkoani na wao watakaa na kukuuta watakujadili tena na wataridhika basi na wao watazipeleka Central Police Station.
Kila Stage itakapopitia copy moja ya hizo fomu hubaki huko kwa kumbukumbu. Vile vile Uzito mkubwa uko katika mapendekezo ya kamati ya Usalama ya Mtaa na Wilaya, Zikipita stage hiyo na taifani hakuna shida kwa sababu hawakufahamu.
Baada ya fomu kufika CPS wao watakuita na kama wameridhika na recommendation za ngazi zote watatoa idhini ya wewe kwenda kuchukua hiyo silaha yako uliyoilipia, Pamoja na kutabu cha silaha hiyo ambapo kitatumika wakati wa ukaguzi wa Silaha unaofanyika kila mwaka.
Process nzima kuanzia ulipolipia hadi kukabidhiwa silaha kuna wengine imewachukua zaidi ya mwaka na wengine hata miezi 2 inategemeana na kujulikana kwako.
ANGALIZO: Bastola ni silaha ya kuua mtu siyo silaha ya kupewa kila mtu awe anaimiliki na ajibebe mfukoni kwenda nayo kwenye baa kutishia watu, hivyo Huko kwenye kuomba kibali si kila aombaye hupata. Labda silaha za kuwindia tu.
Nimeandika kadri zijuavyo, hivyo wataalamu wengine wataongezea. Kama kuna sehemu nimekosea nisahihishwe.
Nenda kwenye maduka ya Tanganyika Arms yaliyo mkoani kwako au kama uko Dar unaweza kwenda kununua pale makao makuu ya jeshi Upanga.
Hapo watakutajia aina mbalimbali na kukupa uzishike na kuzikagua.
Kama kuna ambayo utaipenda unatakiwa kulipia full amount lakini huchukui silaha.
Baada ya hapo wanakupa fomu 1in 4 copies, ambayo utaenda nayo Serikali ya mtaa wako, Kamati ya usalama wa mtaa itakaa na kukujadili kama unastahili kupewa kibali na kama wameridhika Watasaini na kuzifoward hizo fomu katika Kamati ya Usalama ya Wilaya ambapo watazipitia na kukujadili tena na kama wameridhika na maelezo yako watazifoward katika Kamati ya Usalama ya mkoani na wao watakaa na kukuuta watakujadili tena na wataridhika basi na wao watazipeleka Central Police Station.
Kila Stage itakapopitia copy moja ya hizo fomu hubaki huko kwa kumbukumbu. Vile vile Uzito mkubwa uko katika mapendekezo ya kamati ya Usalama ya Mtaa na Wilaya, Zikipita stage hiyo na taifani hakuna shida kwa sababu hawakufahamu.
Baada ya fomu kufika CPS wao watakuita na kama wameridhika na recommendation za ngazi zote watatoa idhini ya wewe kwenda kuchukua hiyo silaha yako uliyoilipia, Pamoja na kutabu cha silaha hiyo ambapo kitatumika wakati wa ukaguzi wa Silaha unaofanyika kila mwaka.
Process nzima kuanzia ulipolipia hadi kukabidhiwa silaha kuna wengine imewachukua zaidi ya mwaka na wengine hata miezi 2 inategemeana na kujulikana kwako.
ANGALIZO: Bastola ni silaha ya kuua mtu siyo silaha ya kupewa kila mtu awe anaimiliki na ajibebe mfukoni kwenda nayo kwenye baa kutishia watu, hivyo Huko kwenye kuomba kibali si kila aombaye hupata. Labda silaha za kuwindia t
Nimeandika kadri zijuavyo, hivyo wataalamu wengine wataongezea. Kama kuna sehemu nimekosea nisahihishwe.
Ikiwa sijui kuitumia,nafundishwa?
Angalizo:ukinunua silaha utatumia muda mwingi kuilinda kuliko yenyewe kukulinda wewe
Alifanyaje mkuu?Ni mara chache sana wenye kumiliki silaha zimewasaidia, sana sana zimewaongezea matatizo, na wengi wamezitumia kujiua na kuuwa wapendwa wao, na wengi zaidi wameporwa, wengi pia wanapenda kutishia tishia tu watu na kupiga hewani hovyo. Aliyeitumia silaha yake kwa ufasaha ni yule bibi wa bagamoyo tu.
Ila kumbuka kuwa makini nayo Siku wife ukimzingua.asije akakutwanga nayoZa asubuhi wanaJF. N siku nyingine tena mapambano yanaendelea. Tunapambana.
Nataka kumiliki bastola kisheria kwa ajili ya ulinzi binafsi kutokana na nature ya shughuli yangu.
1. Je, taratibu zake zikoje?
2. Gharama za kununua bastola zikoje?
3. Ipi bastola nzuri?
4. Kuilipia kwa mwaka ni TZS ngapi?
5. Mchakato mpaka unaimiliki unachukua muda gani?
6.Criteria au vigezo vya kuimiliki vikoje?
Naombeni mawazo yenu wakuu.
Asanteni.