Taratibu za kufuata ili kumiliki Silaha ya Moto Tanzania

Tengeneza Manati haina mlolongo ...joke..

Ngoj waje wataalamu mi Mwenyew Nipate elimu
 
Kumiliki silaha yoyote mkuu kisheria ni utumwa sana kwa nchi kama tz yaani process na maisha yako na condition za kucomply na maisha ya ukaguzi hautotofautiana na mtu mwenye kesi ya jinai the way utakuwa unaripoti mara kwa mara polisi.
Nakushauri uachane nayo mkuu boresha ulinzi unaotumia sasa basi.
 
Mchakato huanza kwa kuinunua kutoka Duka la Silaha na kwa hapa Dsm yapo Mawili tu Moja pale Pembeni mwa Diamond Jubilee na Lingine Pembeni mwa TRA ya karibu na Station!

Ukinunua unapewa risiti bila ya Silaha husika na unapewa Muda wa Miezi Sita kufuatilia vibali

Mchakato wa Vibali unaanzia Serikali ya Mtaa Mpaka kwa Mkuu wa Wilaya ambako Kamati ya Ulinzi na Usalama itaketi na kukujadili na ukishathibitishwa ndio itaenda kwa Jeshi la Polisi na ukishathibitishwa unapewa Document ya Umiliki ambayo ndio utaitumia kuonesha Kwny Duka la Silaha ili upewe Silaha yako.

Zipo aina mbalimbali za Silaha kutegemea Kiwango ha Pesa yako na uhodari na uzoefu wako wa kujenga Shabaha kwa kuwa kuna zingine Zina hitaji uzoefu

Ushauri wangu kwako Kama huna strong reasons usihangaike kuimiliki kwa kuwa baada ya Muda Mfupi hugeuka kuwa Mzigo na inaweza hata ikapelekea kukupeleka Gerezani!

Mie Nina cha kwangu cha Miaka Mingi kiasi lakin kwa Mazingira yangu naanza kuhisi Mzigo na hasa kadri umri unavyoyoyoma maana Siku hizi Silaha yenyewe ndio bidhaa inayotafutwa na Wahalifu wakupore wakati zamani wakagundua una Silaha ya Moto ndio wanakulalia Mbali ( Mchakato wa Maombi huanzia Serikali ya Mtaani kwako ambapo Wajumbe wengi ni Watu wa Vijiweni hivyo ukianza tu Mchakato Mtaa Mzima unajua)

Ukinunua na ukakosa Vibali Basi wanakurudishia Fedha yako kwa kukata kiasi kidogo sana cha charge ya usumbufu!

Zile Nzuri bei yake inaanzia 2Million-4.5 Million kutegemea aina. Wataalam ( Mie ni User sio Mtaalam) wanasema kwa Mazingira yetu za Turkey na Italy ni more njema zaid
 
Nenda kwenye maduka ya Tanganyika Arms yaliyo mkoani kwako au kama uko Dar unaweza kwenda kununua pale makao makuu ya jeshi Upanga.

Hapo watakutajia aina mbalimbali na kukupa uzishike na kuzikagua.

Kama kuna ambayo utaipenda unatakiwa kulipia full amount lakini huchukui silaha.

Baada ya hapo wanakupa fomu 1in 4 copies, ambayo utaenda nayo Serikali ya mtaa wako, Kamati ya usalama wa mtaa itakaa na kukujadili kama unastahili kupewa kibali na kama wameridhika Watasaini na kuzifoward hizo fomu katika Kamati ya Usalama ya Wilaya ambapo watazipitia na kukujadili tena na kama wameridhika na maelezo yako watazifoward katika Kamati ya Usalama ya mkoani na wao watakaa na kukuuta watakujadili tena na wataridhika basi na wao watazipeleka Central Police Station.

Kila Stage itakapopitia copy moja ya hizo fomu hubaki huko kwa kumbukumbu. Vile vile Uzito mkubwa uko katika mapendekezo ya kamati ya Usalama ya Mtaa na Wilaya, Zikipita stage hiyo na taifani hakuna shida kwa sababu hawakufahamu.

Baada ya fomu kufika CPS wao watakuita na kama wameridhika na recommendation za ngazi zote watatoa idhini ya wewe kwenda kuchukua hiyo silaha yako uliyoilipia, Pamoja na kutabu cha silaha hiyo ambapo kitatumika wakati wa ukaguzi wa Silaha unaofanyika kila mwaka.

Process nzima kuanzia ulipolipia hadi kukabidhiwa silaha kuna wengine imewachukua zaidi ya mwaka na wengine hata miezi 2 inategemeana na kujulikana kwako.

ANGALIZO: Bastola ni silaha ya kuua mtu siyo silaha ya kupewa kila mtu awe anaimiliki na ajibebe mfukoni kwenda nayo kwenye baa kutishia watu, hivyo Huko kwenye kuomba kibali si kila aombaye hupata. Labda silaha za kuwindia tu.

Nimeandika kadri zijuavyo, hivyo wataalamu wengine wataongezea. Kama kuna sehemu nimekosea nisahihishwe.


Ubarikiwe mkuu
 
Nenda kwenye maduka ya Tanganyika Arms yaliyo mkoani kwako au kama uko Dar unaweza kwenda kununua pale makao makuu ya jeshi Upanga.

Hapo watakutajia aina mbalimbali na kukupa uzishike na kuzikagua.

Kama kuna ambayo utaipenda unatakiwa kulipia full amount lakini huchukui silaha.

Baada ya hapo wanakupa fomu 1in 4 copies, ambayo utaenda nayo Serikali ya mtaa wako, Kamati ya usalama wa mtaa itakaa na kukujadili kama unastahili kupewa kibali na kama wameridhika Watasaini na kuzifoward hizo fomu katika Kamati ya Usalama ya Wilaya ambapo watazipitia na kukujadili tena na kama wameridhika na maelezo yako watazifoward katika Kamati ya Usalama ya mkoani na wao watakaa na kukuuta watakujadili tena na wataridhika basi na wao watazipeleka Central Police Station.

Kila Stage itakapopitia copy moja ya hizo fomu hubaki huko kwa kumbukumbu. Vile vile Uzito mkubwa uko katika mapendekezo ya kamati ya Usalama ya Mtaa na Wilaya, Zikipita stage hiyo na taifani hakuna shida kwa sababu hawakufahamu.

Baada ya fomu kufika CPS wao watakuita na kama wameridhika na recommendation za ngazi zote watatoa idhini ya wewe kwenda kuchukua hiyo silaha yako uliyoilipia, Pamoja na kutabu cha silaha hiyo ambapo kitatumika wakati wa ukaguzi wa Silaha unaofanyika kila mwaka.

Process nzima kuanzia ulipolipia hadi kukabidhiwa silaha kuna wengine imewachukua zaidi ya mwaka na wengine hata miezi 2 inategemeana na kujulikana kwako.

ANGALIZO: Bastola ni silaha ya kuua mtu siyo silaha ya kupewa kila mtu awe anaimiliki na ajibebe mfukoni kwenda nayo kwenye baa kutishia watu, hivyo Huko kwenye kuomba kibali si kila aombaye hupata. Labda silaha za kuwindia t
Nimeandika kadri zijuavyo, hivyo wataalamu wengine wataongezea. Kama kuna sehemu nimekosea nisahihishwe.

Ikiwa sijui kuitumia,nafundishwa?
 
Usihangaike kote huko njoo nikupeleke mpaka mwa congo mpaka AK47 zinapatikana unabadilishana na wale jamaa magunia matatu ya mahindi wanakupa mashine angalizo ukikamatwa na vijana wa Magufuli utaisoma namba kwa kiyunani
 
Ni mara chache sana wenye kumiliki silaha zimewasaidia, sana sana zimewaongezea matatizo, na wengi wamezitumia kujiua na kuuwa wapendwa wao, na wengi zaidi wameporwa, wengi pia wanapenda kutishia tishia tu watu na kupiga hewani hovyo. Aliyeitumia silaha yake kwa ufasaha ni yule bibi wa bagamoyo tu.
 
Ni mara chache sana wenye kumiliki silaha zimewasaidia, sana sana zimewaongezea matatizo, na wengi wamezitumia kujiua na kuuwa wapendwa wao, na wengi zaidi wameporwa, wengi pia wanapenda kutishia tishia tu watu na kupiga hewani hovyo. Aliyeitumia silaha yake kwa ufasaha ni yule bibi wa bagamoyo tu.
Alifanyaje mkuu?
 
Kwanza jitathimini mwenyewe unajazba? Kama jibu ni ndio nakushauri usijaribu kununua itakua rahisi kuchukua maamuzi magumu.
 
Za asubuhi wanaJF. N siku nyingine tena mapambano yanaendelea. Tunapambana.

Nataka kumiliki bastola kisheria kwa ajili ya ulinzi binafsi kutokana na nature ya shughuli yangu.

1. Je, taratibu zake zikoje?

2. Gharama za kununua bastola zikoje?

3. Ipi bastola nzuri?

4. Kuilipia kwa mwaka ni TZS ngapi?

5. Mchakato mpaka unaimiliki unachukua muda gani?

6.Criteria au vigezo vya kuimiliki vikoje?

Naombeni mawazo yenu wakuu.

Asanteni.
Ila kumbuka kuwa makini nayo Siku wife ukimzingua.asije akakutwanga nayo
 
Back
Top Bottom