Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,816
- 4,566
Polisi mjini Meru wanamtafuta mtu aliyesalimisha bunduki kanisani baada ya kutubu dhambi na kueleza kwamba ameokoka.
Kwa mujibu wa tovuti ya Taifa Leo imeandika kuwa jana Jumanne Februari 14, 2024 Polisi walipigwa na butwaa baada ya mchungaji Nathan Kirimi kufika katika Kituo cha Polisi cha Meru Central akiwa na bunduki aina ya AK47 na kueleza kwamba silaha hiyo ililetwa kanisani na muumini aliyekwenda kutubu dhambi.
Kamanda wa Polisi wa Kaunti ndogo ya Imenti Kaskazini, Ezekiel Chepkwony amesema wakati Mchungaji Kirimi wa Huduma ya Jesus Winner alipofika kituoni hapo akiwa na bunduki hiyo walipatwa na mshangao.
Mchungaji huyo aliandikisha maelezo Polisi ambapo alisema kuwa wakati wa ibada ya Jumapili, kundi la waumini walikwenda madhabahuni wakitaka kumpa Yesu maisha, kisha walipiga magoti, naye kuwaongoza maombi ya toba.
“Kwa mujibu wa maelezo ya mchungaji huyo, baada ya ibada, mwanamume mmoja alimfuata na kumweleza kwamba alikuwa na ushuhuda na alitaka kusalimisha silaha,” amesema Kamanda Chepkwony kwenye mahojiano na Taifa Leo.
Ofisa huyo wa Polisi amesema bunduki hiyo inaonekana ilikuwa imefichwa mahali kwa muda mrefu au kufukiwa ardhini kwa sababu ilikuwa na kutu.
Kwa mujibu wa tovuti ya Taifa Leo imeandika kuwa jana Jumanne Februari 14, 2024 Polisi walipigwa na butwaa baada ya mchungaji Nathan Kirimi kufika katika Kituo cha Polisi cha Meru Central akiwa na bunduki aina ya AK47 na kueleza kwamba silaha hiyo ililetwa kanisani na muumini aliyekwenda kutubu dhambi.
Kamanda wa Polisi wa Kaunti ndogo ya Imenti Kaskazini, Ezekiel Chepkwony amesema wakati Mchungaji Kirimi wa Huduma ya Jesus Winner alipofika kituoni hapo akiwa na bunduki hiyo walipatwa na mshangao.
Mchungaji huyo aliandikisha maelezo Polisi ambapo alisema kuwa wakati wa ibada ya Jumapili, kundi la waumini walikwenda madhabahuni wakitaka kumpa Yesu maisha, kisha walipiga magoti, naye kuwaongoza maombi ya toba.
“Kwa mujibu wa maelezo ya mchungaji huyo, baada ya ibada, mwanamume mmoja alimfuata na kumweleza kwamba alikuwa na ushuhuda na alitaka kusalimisha silaha,” amesema Kamanda Chepkwony kwenye mahojiano na Taifa Leo.
Ofisa huyo wa Polisi amesema bunduki hiyo inaonekana ilikuwa imefichwa mahali kwa muda mrefu au kufukiwa ardhini kwa sababu ilikuwa na kutu.