Israel: Raia 120,000 watuma maombi ya kumiliki silaha

Papasa

JF-Expert Member
Nov 2, 2018
1,947
4,131
8b8e1350-788d-11ee-b315-7d1db3f558c6.png


Hii vita haishi leo wala kesho sisi Waswahili tuendelee na kilimo mvua zimeshaanza.

=====

Tangu shambulio la Oktoba 7, ambapo zaidi ya watu 1,400 waliuawa na wanamgambo wa Hamas, zaidi ya maombi 120,000 mapya ya leseni ya silaha yamewasilishwa na raia wa Israel.

Harakati za kupata bunduki kihalali zinafanyika kote nchini. Masafa ya upigaji risasi yana shughuli nyingi na idadi isiyokuwa ya kawaida ya Waisraeli wanaotaka kuboresha ujuzi wao. Nje ya maduka ya bunduki, foleni kubwa za watu wanaosubiri kununua silaha yao ya kwanza inaongezeka.

Kufuatia tangazo la serikali ya Israel kwamba italegeza sheria zake za umiliki wa bunduki, wale ambao hawana rekodi ya uhalifu au matatizo ya kiafya, sasa wanaweza kupata leseni ya bunduki ndani ya wiki moja. Watu binafsi pia wataruhusiwa kumiliki hadi risasi 100, kutoka 50.

"Sasa, ni rahisi kupata bunduki, kwa sababu waliondoa vikwazo vyote" anasema Omri Shnaider, wakili mwenye umri wa miaka 41 kutoka Kibbutz nje kidogo ya mji wa Jerusalem.

Lakini Bw Schnaider licha ya kufurahia uamuzi wake, ana wasiwasi kuhusu athari za maelfu ya silaha zinazotolewa kwa raia.

"Kuna faida, lakini pia hasara. Tunaona kile kilichotokea Marekani. Sio uamuzi rahisi. Lakini hili ndilo ninahisi nahitaji kufanya, ili kuwafanya watu wa Israeli wajisikie salama."

Waziri wa Usalama wa Kitaifa wa Mrengo wa kulia Itamar Ben-Gvir, mtetezi wa muda mrefu wa umiliki wa bunduki za kibinafsi, amekuwa akizuru nchi akitoa maelfu ya silaha.

Alisema silaha hizo mpya ni maalum kwa ajili ya wale wanaoishi karibu na mpaka na Gaza au katika miji yenye mchanganyiko wa Wayahudi na Waarabu na kuzihimiza jumuiya hizo zote za Kiyahudi kuunda makundi ya usalama za raia.

Chanzo: BBC Swahili
 
Back
Top Bottom