Habari ndugu mteja, ahsante kwa kuwasiliana nasi kupitia ukurasa huu na pole kwa changamoto hiyo, gharama hiyo ya shilingi 27,000 ni kwa wateja wetu wa vijijini wanao hudumiwa na mradi wa REA, kama eneo lako halipo chini ya mradi huo utalipia gharama za kawaida za kuunganishwa na huduma ya umeme, tunaomba kusisitia kuwa malipo yote ya TANESCO hufanyika kupitia control namba. ^HS
Gharama zipi sasa, tufafanulieni tujue
 
Hbari ndugu mteja asante kwa kuwasiliana nasi kupitia ukurasa huu na pole kwa changamoto hiyo, tafadhali tupatie taarifa zifuatazo kwa msaada zaidi,
Jina
Eneo
Namba ya simu
Tatizo
Mita namba
Kitu maarufu
TANESCO Huduma Kwa Wateja
SIMU: 0748 550000
WhatApp: 0758346869^OK
Nimezungumzia tatizo la eneo zima yaani kata nzima ya eneo hilo umeme unakatika yaani kila siku unakatika mpaka mara 4 ma hakuna taarifa naomba sana tuwe tunapata taarifa hapa wilaya ya kahama bulungwa mseki naomba sana
 
hello TANESCO
Matumizi yangu hayajawahi kuzidi unit 60 kwa mwezi kwa zaidi ya miaka mitatu sasa, kwa nini msinihamishiwe zero tariff?
Kama kweli mpo kuwasaidia wananchi wenye kipato cha chini; Kwa nini hadi karne ya 21 mumtake mteja masikini asafiri kuja ofisini kwenu kuomba zero Tarriff wakati mna data zote za mita?
Binafsi nafikiri kuna tatizo hapa kwani mtu akitumia unit nyingi hata kama amepta ugeni mwezi huo nasikia huwa mnambadilisha kwenda tarrif ya juu; inamaana mpo kukomoa na siokusaidia???

Kwa nini msiwe na utaratibu kuwa, mtu akitumia uniti za Chini kwa miezi sita mfululizo anahamishiwa zERO TARRIFF na akitumia unit za juu kwa zaidi ya miezi miwli (miezi mitatu mfululizo) anawekwa uniti za juu

Asante
 
Nimekwenda Ofisi za TANESCO Sengerema Mwanza kuuliza taratibu za kuunganishiwa umeme kwa umbali wa nguzo 1,nimeambiwa utaratibu umebadilika, siwezi kulipia hadi hapo utaratibu mpya utakapoanza. Kwa sasa TANESCO Sengerema wanashughulika na wateja waliolipia zamani na ndio nguzo zao zipo. Naomba kupata majibu au ushauri nifanye nini ili nilipie na nifungiwe umeme mapema?
Ndugu Mteja!

Tunashukuru kwa kuwasiliana na TANESCO Huduma kwa Wateja, Tunakujulisha kuwa sasa TANESCO imekurahisishia huduma ya wewe kuweze kufanya maombi ya kuunganishiwa umeme kwa kutumia mfumo bora wa Nikonekt popote ulipo na wakati wowote, Unaweza kufanya maombi kwa njia zifuatazo:

- Nikonekt.tanesco.co.tz

-Nikonekt App (Ipo Play store na Apple store)

- Kubofya *152*00#

-Kwenye ofisi za TANESCO



Kwa Maulizo au msaada wowote tafadhali wasiliana na kituo chetu cha huduma kwa wateja kwa

Simu;0748550000

WhatsApp: 0758346869^EB
 
Habari ya kazi TANESCO . Naomba kufanyiwa key change kwenye mita namba 37209700303. Nyumba ilikuwa inakaliwa na mtumishi wenu, sasa amehama na mita inatakiwa kufanyiwa key change kuja kwenye matumizi ya kawaida na mtumishi wenu kaondoka na unit zake nami nimebaki giza. Msaada jamani. Asante
 
Ndugu Mteja!

Tunashukuru kwa kuwasiliana na TANESCO Huduma kwa Wateja, Tunakujulisha kuwa sasa TANESCO imekurahisishia huduma ya wewe kuweze kufanya maombi ya kuunganishiwa umeme kwa kutumia mfumo bora wa Nikonekt popote ulipo na wakati wowote, Unaweza kufanya maombi kwa njia zifuatazo:

- Nikonekt.tanesco.co.tz

-Nikonekt App (Ipo Play store na Apple store)

- Kubofya *152*00#

-Kwenye ofisi za TANESCO



Kwa Maulizo au msaada wowote tafadhali wasiliana na kituo chetu cha huduma kwa wateja kwa

Simu;0748550000

WhatsApp: 0758346869^EB
Nimeshafanya online Application na kuprint fomu, na nikapita kwa fundi wiring, nilipopeleka TANESCO waliikataa fomu na kusema kwa sasa hawapokei wateja wapya hadi waishe wa zamani asee! inaboa sana
 
Napenda kutoa Shukrani zangu za Dhati na kuipongeza TANESCO. Nimekuwa mteja wenu miaka mingi lkn kwa Hili lililotokea WIKI HII ni kubwa. Jumanne tarehe 11/4/2023 nilijaza taarifa za Kuomba kufungiwa Umeme kwa njia ya Mtandao, mchoro ukawekwa. Tarehe 11/04/2023 hiyo hiyo akaja Saveya kukadiria. Tarehe 12/4/2023 nikatumiwa control namba nikalipa bill kwa 320,900/=. Leo tarehe 14/4/2023 asbh saa 3 nishafungiwa Umeme. Kiukweli nimeshangaa sana Utendajikazi huu wa mwendikasi TANESCO.
Nawashukuru sana Hongereni kwa kazi nzuri TANESCO.
acha unafiki
 
Habari ndugu mteja, ahsante kwa kuwasiliana nasi kupitia ukurasa huu na pole kwa changamoto hiyo, gharama hiyo ya shilingi 27,000 ni kwa wateja wetu wa vijijini wanao hudumiwa na mradi wa REA, kama eneo lako halipo chini ya mradi huo utalipia gharama za kawaida za kuunganishwa na huduma ya umeme, tunaomba kusisitia kuwa malipo yote ya TANESCO hufanyika kupitia control namba. ^HS
Asante kwa majibu mazuri
 
Habari. Bei ya kuunganisha umeme pembezoni mwa miji ambako ni sawa na kijijini ni shilingi ngapi? Maana ndugu yangu ameomba umeme hapo Igingilanyi Iringa mpakani na Nduli ambako watu wamehamia baada ya kuhamishwa na upanuzi wa uwanja wa ndege lakini amepewa bill ya malipo ya manispaa. Naomba ufafanuzi maana yeye alijua ni 27,000/= lakini kaletewa bill ya 360,960/= kiasi kwamba amekwama kulipa
Ndugu mteja asante kwa kuwasiliana nasi kupitia ukurasa huu na pole kwa changamoto, kwa wateja wa maeneo ya vijijini huwa wanapatiwa huduma kwa kiwango cha 27,000 endapo wapo kwenye mradi wa REA kama ni nje ya mradi basi watapaswa kulipia kulingana na viwango vya kupata huduma ya umeme vilivyo weka wa na shirika.^OK
 
37249129745 we tanesco samahani embu angalia hiyo mita ina deni au maana kila nikitia umeme wanasema haitoshi hela niko miono hapa chalinze
Ndugu mteja asante kwa kuwasiliana nasi kupitia ukurasa huu na pole kwa changamoto hiyo, mita hii ina deni la kodi ya jengo shilingi 12,000 nunua umeme wa zaidi ya kiasi hicho utapata huduma.^OK
 
Ndugu mteja asante kwa kuwasiliana nasi kupitia ukurasa huu na pole kwa changamoto hiyo, mita hii ina deni la kodi ya jengo shilingi 12,000 nunua umeme wa zaidi ya kiasi hicho utapata huduma.^OK
Hii Kode ya jengo mbona kama n Ile service charge mmeirudisha kijanja??
 
TANESCO Mtaa wa Raha/mchikichi na Muhonda kilichobaki ni kuunguza maduka ya watu maana kila baada ya dk 5 umeme unakatika na kurudi maana yake ni nn?

Kila siku mna matengenezo mtaa huu tuu maana kuna nyumba mbili kama sio tatu mtaa wa Raha /Muhonda lazima umeme ukatike muitwe

mbona mnawakwaza sana wananchi na wafanyabiashara wa mtaa huu?

Ifike mahali mutuonee huruma wafanyabiashara na wakaazi wa eneo hili tushachoka sasa
 
Habari ndugu mteja asante kwa kuwasiliana nasi kupitia ukurasa huu na pole kwa changamoto hiyo, tumepokea taarifa ya hitilafu maeneo hayo, wataalamu wetu wanafanya jitihada ili huduma irejee tunaomba radhi kwa adha zilizo jitokeza.^OK
 
Habari ndugu mteja asante kwa kuwasiliana nasi kupitia ukurasa huu na pole kwa changamoto hiyo, tumepokea taarifa ya hitilafu maeneo hayo, wataalamu wetu wanafanya jitihada ili huduma irejee tunaomba radhi kwa adha zilizo jitokeza.^OK
Haya,jmosi hii weekend hamjaona mda mwingine kukata umeme zaidi ya weekend,kweli?
Mimi niwashauri jambo,mnapokuwa mnadeal na issues maeneo ya nje ya mji muwe mnafanya katikati ya wiki siku kama za jtano,alhamisi au jnne,mojawapo.
Nje ya mji kunachangamka na kuwa bize weekends hivyo sio muda muafaka kufanya matengenezo yoyote yanayohusisha kukata umeme.Ni kinyume na mjini huko ambako jpili kunapoa.
Nimesoma tangazo lenu kuwa kuna mkandarasi wa treni ya kasi kuna shughuli anaifanya leo na kesho.
Hii sio sawa.Why weekend?
Kwanini isiwe katikati ya wiki ambapo matumizi ya umeme ni madogo na shughuli zetu nyingi zinapoa?
Umeme ni sensitive sana,hata hizo kazi ni bora zifanyike katikati ya wiki na usiku mwingi,mnatutia hasara sana.
 
Habari ndugu mteja asante kwa kuwasiliana na TANESCO huduma kwa wateja na pole kwa changamoto, huduma hiyo bado ipo, lakini inakuwa chini ya miradi ya REA ambao husambaza umeme kwenye vijiji mbalimbali, kwa walio nje ya miradi au walikosa fursa ya kupata huduma chini ya mradi watalipia bei za viwango vya kawaida vilivyowekwa na TANESCO, gharama halisi mteja atazipata baada ya surveyor kufika na kufanya tathmini kwenye eneo lake.^OK
 
Back
Top Bottom