Tanesco Nyamagana mnatuumiza wateja wenu tumelipia kuvuta umeme tangu mwezi wa kumi mwaka jana hadi leo ni chenga tu za hapa na pale....ohh nguzo hamna, nguzo hazijaja huku wengine wanafungiwa tabia mbaya.
 
Tanesco Kisarawe, sie wakazi wa Chanika zingiziwa tunahitaji umeme tulitafuta surveyor kaja kuhesabu nguzo zinazohitajika zimefika 15 amesema idadi hyo yapasa tupate mradi, awamu zote za Rea wametupita kama hawatuoni na nguzo zetu zikahamishwa kupelekwa Mvuti cc CCM tunawasubiri kwa hamu maana mliahidi tumchague Waitara mlete umeme .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nipo Tabora vijijini.Nimewapigia Tanesco mikoani (Regional Manager) siku ya 5 sasa hatuna umeme.Namba zangu 0787938347.Vitu vinaharibika kwenye Frizer jamani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunaomba namba yako ya simu tafadhali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mrad wa rea morogoro ifakara kata ya mbasa kuna baadh ya maeneo yamechimbwa mashimo hawajaweka nguzo ili hal sehem nyingine wanasambaza nyaya na kila tukimuuliza mkandaras anasema nguzo zimeisha na hana matumain ya kuleta hii imekaaje?
Tunaomba namba yako ya simu tafadhali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunaomba namba yako ya simu tufatilie tuhuma zako na kuchukua hatua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Moshi eneo la mjohoroni Shia hakuna umeme wiki sana. Simu ikipigwa majibu 'mafundi wanakuja sasa hivi' wiki sasa,,Kulikoniii
 
*FEBRUARI 16, 2019*

*SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)*

*TAARIFA YA MATENGENEZO YA MASHINE KITUO CHA KUFUA UMEME KWA GESI CHA UBUNGO II PAMOJA NA KITUO CHA SONGAS*

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu Wateja wake wa Dar es Salaam na Zanzibar kuwa kutokana na kufanya maboresho makubwa yanayohusisha matengenezo ya mashine 3 za kituo cha ubungo II moja baada ya nyingine, uwekaji wa transfoma kubwa la MVA 300 kwenye kituo cha kupoza umeme cha Ubungo ili kukiongezea uwezo na kwenda sambamba na ukuaji wa mahitaji ya jiji la Dar es Salaam kutakuwa na mapungufu ya upatikanaji wa huduma ya umeme kwa maeneo tajwa.

Aidha, Kampuni ya Songas itafanya matengenezo kinga katika mashine zake. Matengenezo hayo katika vituo vya Ubungo na Songas yataendelea kwa awamu na yanatarajiwa
kukamilika ifikapo mwezi Juni , 2019.

Wataalamu wetu kwa Kushirikiana na Mkandarasi Kampuni ya SIEMENS kutoka nchini Sweden wanaendelea na matengenezo ya mashine na ubadilishaji wa vipuri ili kuongeza ufanisi zaidi katika uendeshaji wa mitambo hii na kuimarisha hali ya upatikanaji umeme kwa Mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Zanzibar.

Huduma ya umeme haitakosekana kwa kipindi chote cha matengenezo ila kwa baadhi tu ya siku na nyakati.

Mashine hizo za Ubungo II na Songas zimeungwa katika mfumo wa usambazaji umeme wa msongo wa kilovolti 132 wa Dar es Salaam, Pwani na Zanzibar na hivyo kusababisha mapungufu katika maeneo tajwa.

Tutaendelea kutoa taarifa zaidi ya hali ya matengenezo inavyoendelea.

Ahsanteni kwa ushirikiano wenu.

Tafadhali usishike wala kukanyaga waya uliokatika au kuanguka.

Kituo cha miito ya simu 2194400 na 0768 985100

*Tunaomba radhi kwa usumbufu unakaojitokeza*

Tovuti: www.tanesco.co.tz,

*Mitandao ya kijamii*

Twitter, www.twitter.com/tanescoyetu,

Facebook https://www.facebook.com/tanescoyetultd/

*IMETOLEWA NA:*

OFISI YA UHUSIANO
TANESCO MAKAO MAKUU

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wilaya

Namba ya simu

Eneo

Tunaomba hizo taarifa kwa hatua zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku hizi wanatoa 10 tu ndugu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…