Maelezo yenu yana double standards, angalia Tariff 1 na Tariff 4, wewe unasema mtumiaji wa kiwango cha chini anakuwa tariff 1 Na wa Juu anakuwa Tariff 4 ,which is which



HIZI NDIO SABABU ZINAZOKUFANYA ULIPIE UMEME KWA GHARAMA KUBWA.

Unaweza kushangaa kuona wengine wakinunua Umeme wa 9,150 Wanapata Unit 75 wew ukinunua Umeme wa 10,000 unapata Unit 28.1

Iko hivi Watumiaji wadogo wa Umeme ambao kwa mwezi Matumizi yao hayazidi Unit 75 Wapo Tarrif D1(4) Na wanauziwa Unit moja kwa Sh.122,

Wakati watumiaji waliowengi wako Tarrif T1 hawa Unit moja wanauziwa Sh.kati ya sh.356.45 Kama sikosei

Maana yake mtumiaji aliyeko Tarrif D1(4) Ananunua Unit 41 Kwa sh 5,000
Wakati walioko Tarrif T1 Wananunua Unit 14 kwa sh.5000

NAWEZAJE KUA MIONGONI MWA WATUMIAJI WADOGO WA UMEME YAANI (TARIFF D1)

Kama ni nyumba yakupanga na mko wengi ni ngumu kidogo. Kwanza unatakiwa Kupunguza Matumizi Ya Umeme Yasiyo ya Lazima
Pili nunua Vifaa vyenye Wats ndogo vitu kama taa,Tv,Friji,Pasi n.k

Tuchukulie mfano wa Taa zenye Wats 40 nje zikiwa nne na za Wats 18 kwa ndani zikawa Taa 8 nyumba yako nzima itakua na jumla ya Taa 12 Ambazo zitakua na Jumla ya Wats 304
Lakini ukinunua Taa zenye Wats ndogo (Energy Saver) Japo bei yake iko juu ukilinganisha na Taa zenye Wats kubwa Kwa mfano huu huu ukanunua Taa zenye Wats 5 kila moja za nje Nne na taa 8 za ndani zenye Wats 3 kila moja
Jumla ya taa 12 zitakua na Jumla ya Wats 44 tu.

Maana yake utakua umepunguza jumla ya Wats 250 upande wa Taa tu lakini idadi ya Taa imeendelea kua ni ile ile. Mtu mwenye taa moja ya Wats 40 akiwasha nawew ukawa taa zote 12 Matumizi yenu yatakua hayana tofauti kubwa
Mwisho kabisha matumizi yako ya Umeme yakiwa chini ya Unit 75 kwa miezi mitatu mpaka Sita Mfululizo unatakiwa kuandika Barua unaiadress kwa Meneja wa TANESCO wa Ofisi uliyoko Karibu nayo Kuomba kubadilishiwa Kutoka Tarrif 1 kwenda Tarrif 4.

Siku ukitumia Zaidi ya Unit 75 kwa mwezi utarudishwa Tariff 1.

Kwa swali lolote ushauri kuhusu matumizi bora ya umeme
Usisite kuwasiliana nami

MR ELETRIC
0674656694
allanshaolin12@gmail.com
Tunashukuru sana mpendwa.mteja wetu.tunaomba maswala.yanayohusu TANESCO yaje kwetu moja kwa moja kwa ufafanuzi aidha wateja wanaruhusiwa kutoa maoni
 
wakubwa hii nyumba nnayoishi tupo kwenye system ya matumizi makubwa.....bas kila week tunanunua umeme was elfu tano tano (unit 15)......yani inatucost tunashindwa hata kunyoosha nguo....

Nisaidie utaratibu kwa mtaalam yeyote aliepo humu ndani jamn.....hili swala ni mzigo
 
Any way nimeshapata majibu kwenye ile comment inayohusu maswala ya tarrif D1 nk.......

Sasa najiuliza kitu kimoja mnisaidie nyie tanesco.
Hivi kwa nin mnapokuwa mnatufungia raia hizi mita na maswala mengine ya umeme mnaamua kutuweka kwenye mfumo huu wa 5000(unit 14) moja kwa moja????

Hakuna mtanzania anaeweza kuafford gharama hzo za umeme....yn hayupo.....kwa kifupi mnakuwa tu mmeamua kutengeneza mfumo wa kutupiga hela and nothing else.

Sio fair........
 
wakubwa hii nyumba nnayoishi tupo kwenye system ya matumizi makubwa.....bas kila week tunanunua umeme was elfu tano tano (unit 15)......yani inatucost tunashindwa hata kunyoosha nguo....

Nisaidie utaratibu kwa mtaalam yeyote aliepo humu ndani jamn.....hili swala ni mzigo
Kwa maelezo yako mpo kundi sahihi la matumizi ya nyumbani cha msingi kila mmoja asimamie vizuri matumizi yake kwani sehemu za wapangaji huwa zina matatizo ya kila mmoja kujifanya hana matumizi makubwa lakini ukweli anaujua mwenyewe
 
Wakuu: Nina swali kuhusu mita za LUKU. Zipo mita za kuweka ukutani na za kwenye nguzo. Nini tofauti yake? Na je mita za LUKU za ukutani zimesitishwa au zinafungwa bado majumbani kwa sasa?
 
Tanga eneo la Kange Kasera kwanini hamtaki kutuwekea nguzo za umeme eneo la chini ya msikiti ile hali tupo wateja xaidi ya 40 na ambao tumeshafanya wiring na kuleta barua ofisi za Meneja mkoa zaid ya mara tatu tangu mwaka jana mwezi wa pili?
Sababu za kibajet mnazotupa haturidhiki nazo kwa kuwa maeneo mengiine mapya kabisa mnaweka nguzo na maombi wameleta nyuma yetu. Kamma ni kuchangia gharama za hizo nguzo basi tuweken sawa sisi wananchi tupo tayari tuchangishane mtuwekee nguzo ili tupeleke maombi ya kuingiziwa umeme
 
Tanga eneo la Kange Kasera kwanini hamtaki kutuwekea nguzo za umeme eneo la chini ya msikiti ile hali tupo wateja xaidi ya 40 na ambao tumeshafanya wiring na kuleta barua ofisi za Meneja mkoa zaid ya mara tatu tangu mwaka jana mwezi wa pili?
Sababu za kibajet mnazotupa haturidhiki nazo kwa kuwa maeneo mengiine mapya kabisa mnaweka nguzo na maombi wameleta nyuma yetu. Kamma ni kuchangia gharama za hizo nguzo basi tuweken sawa sisi wananchi tupo tayari tuchangishane mtuwekee nguzo ili tupeleke maombi ya kuingiziwa umeme
Tunaomba namba yako ya simu mpendwa.mteja wetu
 
Write your reply... kwa aliepata chuo cha ustawi wa jamii ngazi ya cheti
na anahitaj chumba karibu na chuo cha ustawi wa jamii bamaga anicheki pm
 
Tutakufungia umeme hauna haja ya kuwa na hofu wala kudhani tunahitaji chochote.hii ni haki yako na sisi ni wajibu wetu.upo kwenye orodha yetu
Mtanifungia umeme lini jamani mbona imekua ni kero sana!!!I? Nina miezi 3 tangu nilipie na muda kusubiri umekwisha kila siku hakuna sababu za msingi. Wengine wamefungiwa kwa haraka na tulikuwa pamoja kwenye malipo mpaka ufuatiliaji nimuone nani; na mimi nitoe kidogo nipate huduma. Maana haya ni mazingira ya RUSHWA. TANESCO Makao Makuu nimeomba namba zenu hamtaki kunipa shida Ni nini jamani. Tanesco Kigamboni wanatesa wao huwajali wenye uwezo kipesa na mamlaka. Sisi walala hoi kila siku huambiwa nguzo, mara mita na waya hamna. Wakiona wamezidiwa hukimbilia magari mabovu ya kusambaza nguzo. Nifanye nini jamani.
 
Hadi muda huu nipo Tanesco nataka nilipie service line, hadi sasa mtandao hakuna tangu saa tano asubuhi tatizo nini?
 
Huduma zenu za matandao ni hovyo nipo Tanesco nimepoteza muda kusubiria matandao nipewe risiti nikalipe bank lakini mtandao hakuna. Mbona kwenye mitandao ya simu kuna mtandao ninyi mna shida gani na mkongo wa taifa, mmevurugwa nini?
 
Back
Top Bottom