Sitta kama binadamu wengine wote ana mapungufu yake, lakini hebu semeni ni kiongozi gani wa Tanzania ambaye amekuwa jasiri kusema ukweli kuhusu ufisadi na udhaifu wa serikali na upole usio kifani wa Mh Kikwete. Hamkumbuki ni huyu huyu Sitta, akimkaribisha Mh Kikwete kuhutubia bunge, alimuomba au alimwambia awe mkali kidogo ili wananchi warudishe imani na serikali. Ni chini ya huyu huyu Sitta, bunge au wabunge waliweza kuwa huru na kutoa siri nyingi za maovu. Na mpaka sasa anasimama kidete kutetea yaliyo ya kweli, sasa wale mnaoona Lowasa anaonewa, simameni mseme wapi anaonewa?
Ukweli ni kuwa wengi ndani ya CCM wanaogopa kuwa akishika mpini, watu kama Mkapa wankwenda mahakamani, na huyu mzee hataki kabisa kummsikia Sitta. Na CDM, nao wanajua Sitta akisimama, mpira utakuwa mgumu saana kwa kwa Dr Slaa. Huu ndo ukweli, wote wanajua CCM ikimuweka EL, basi Dr anapeta