kwani sitta ana kashfa zipi ukilinganisha na wengine? wote mnaomkosoa hamna sababu za msingi za ukosoaji wenu mnabaki kusema ni mnafiki mnafiki mnafiki! hamna hoja bali ni kuropoka tu.
Huyu sitta ndo alifanya watu walione bunge kuwa tamu, kwa kiasi kikubwa alijaribu sana kuwa unbiased,ishu nyingi za ufisadi zimeibukia bungeni alipokuwa spika,alijaribu sana kuweka wazi mijadala na wabunge wengi wakajenga confidence ya kusema bungeni maovu ya watendaji wa serikalini , unafikiri angekuwa msekwa ishu za richmond/dowans etc zingepata nafasi ya kujadiliwa bungeni? hata huyu mama wa sasa anapretend kuvaa viatu vya sitta lakini kuna ishu kadhaa kazificha kwenye 'underwear'! wabunge wangapi wametoa hoja zao na spika akawataka wathibitishe kwa maandishi na pindi walipoleta uthibitisho yule mama anaficha kwenye 'underwear' anapotezea moja kwa moja mpaka inasahaulika! mbunge Godbless Lema wa Arusha mjini alipotaka waziri mkuu awajibike kwa kusema uongo bungeni, mlisikia majibu ya mama na akamtaka alete maelezo na alipoleta akaficha kulekule 'kunako' na ndugu Lema alipohoji kwa mara nyingine alipotezewa, angekuwa sitta angeacha pinda ayakoge maji!