Sitta alonga katika 'Dakika 45' ya ITV

Sitta alonga katika 'Dakika 45' ya ITV

jamani, kasema Jk ni fisadi no.1, walihonga hadi wabunge, bado ikashindikana, ndo walipoamua kumuengua kimtindo.
 
Naona waziri Sitta anatoa yaliyo moyoni kwake. Anaelezea alivyoshindwa uspika kwa kushindwa kulala mwanamme na kuamka mwanamke. Hicho ni kigezo kilichowekwa mahsusi kumuengua katika mbio za uspika!
 
Bado mnamuongelea Sitta ? Jamani ni kweli tumeishiwa kweli mada hapa JF hadi Sitta aje in betwee ?

Yupo on air kama kawaida yake ni kujisifia na kuongea kwa hisia. maelezo yake yanatoa hisia kuwa Mwakyembe kapewa sumu na Makinda kawekwa na mafisadi....loh!
 
Source: dakika 45.
Kasema mafisadi ambao wako tayari kumtoa roho ndio waliobadili utaratibu wa uchaguzi wa spika.
Anasema walishindwa kushindana naye kwenye box la kura wakaamua kuweka kigezo cha jinsia.
My take: kama JK aliridhia naye ni fisadi
offcourse
 
bado anaulilia uspika ndo maana hataki kutoka kwenye nyumba ya Spika, na huo ni ufisadi. Kama ana uchungu na nchi hii atoke CCM na aseme ukweli. Kuendelea kukaa katika serikali ya CCM na kusema hawampendi ni unafiki mkubwa. Mzee 6 nazidi kukudhalau kwani wote wa CCM ni gale gale tu
 
Kubenea kanunuliwa na mafisadi,TANZANIA DAIMA IMENUNULIWA NA MAFISADI,huyu ndiyo Sita!
 
'Chadema wametikisa ccm igunga', ,'ugumu wa maisha unasababishwa na kukosa uadilifu kwa viongoz',
 
Acha kupotosha, kamsifia JK hapa tena kasema atakijenga chama vizuri

Mnafiki anapozungumza read between the lines..... kampiga dongo JK aliposema kuwa mafisadi waliibuka na hoja ya kuwa spika atakuwa mwanamke this time, maana yake kamsema JK kwani ndiye aliyefanya maamuzi hayo. Kama alishauriwa na mafisadi ina maana kukubaliana na hoja za mafisadi basi na yeye ni fisadi! Huwa anamsifia JK kimtindo lkn msg sent....! huyu bwana mazungumzo yoteeeeeee ni hasira za uspika kudadadeki!
 
hakuna jipya hapo! Tumeshasoma mchezo zamani! Jasiri ni Dr slaa,hakumung'unya maneno,alitaja majina 11 kama yalivyo mpaka mwenye nchi!
 
Naamini kwa hapa alipofikia siku zake ccm zinahesabika! Jamaa hawatakaa kimya tena, ila tusubiri tuone. CDM tunaanza kujiandaa na uchaguzi maana jamaa lazima wamtose.
Kikwete atajifanya kafanya maamuzi magumu.
umeona eeeeeee anaichana ccm live na anaisifia cdm kidizaini
 
Back
Top Bottom