Serikali kutumia Tsh. Bilioni 190.57 kununua V8 mpya za Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Ujenzi wa Makazi na Utawala

Hayo mengine zuga tu mkuu,main chick hapo ni mandinga mapyaaaaa
Zuga ya nini wakati mchanganuo upo? Kama wanataka kuzuga si wanaweza wasisome hiyo section wakaruka tuu kwani Utajua?

Chukua vitabu vya Bajeti utaona magari ni kiasi gani, majengo ya Utawala kiasi gani,makazi ya Viongozi kiasi gani.Mbona Kila kitu Huwa kinawekwa wazi?

Wazuge Kwa sababu zipi za msingi? Gari ni kitendea kazi na Samia kayanunua kweli Kila taasisi ya Umma Kwa Sasa Haina shida sana za vitendea kazi kama Mwanzo
Screenshot_20240416-213850.jpg
 
Wewe bwege kweli. Sasa nani kakataa kuwa magari si vitendea kazi? Unakuja mbio umetoka msalani na kopo la kutawadhia lina maji kurukia hoja hata hujaielewa? Umbea.na ukilaza mbaya sana.
Mapovu ya upumbavu wako kaogeshee mkeo.

Ndio wamenunua na watanunua Kwa hiyo unatakaje sasa labda wewe kima.
 
Ni jambo la busara sana. Kuinua uchumi wa nchi. Mama abarikiwe sana. Ametuona kwa kweli. Magari mengi yalikuwa ni model iliyopita kwa kutununulia haya na hizi mvua kwa kweli ametutia moyo sana.

Miaka mingine 30 mbele aongezewe.

View attachment 2965685
Kwa kuonesha umuhimu wa hili, waziri wa fedha ni PM account ya bank kuu niwaongeze gari 9. Mnafanya kazi nzuri sana 😂
 
Hatuwezi kuendelea hata siku moja Kwa mipango mibovu kama hii ya kununua magari ya gharama wakati serikali imeshindwa kutekeleza majukumu yake mengi ya msingi mf; kurekebisha Miundo mbinu ya miji mikubwa, km Arusha, Dar nk. Nchi nyingi kwasasa zinabana matumizi na Kutafuta namna ya kuongeza mapato lakini Tz, tunaenda enda kama tumekatwa vichwa.
Matumizi mengi ya serikali yapo kwenye magari ya gharama na kuyahudumia.

Haya MaCCM yatakuwa yamerogwa na Wajapan. Hii siyo bure..... Yaani hata JPM na ukali wake wa kubanwa pesa bado kwenye maVEighty alitoa pesa.
 
190,570,000,000/113=Tshs.1,686,460,177 kwa kila Gari na huku NHIF kuwahudumia wadanganyika tu miyeyusho.

MAMA OYEEEEEEEEEEEEEEE.
CCM OYEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE.
Mbaya zaidi kuna watu hapo wameingiza zao mfukoni na wengine wanatamani huo ulaji na kutembelea hilo gari
 
Watu waliona na akili na wenye busara wakijitenga na kutoshiriki kufanya siasa, wasio na akili au hata busara watachukua nafasi. watu hawa wakishika mpini, watakacho panga au kuamua kitakuwa.... Ndio hali tuliyoifikia kwenye utawala na uongozi wa nchi hii. :oops:
 
Zuga ya nini wakati mchanganuo upo? Kama wanataka kuzuga si wanaweza wasisome hiyo section wakaruka tuu kwani Utajua?

Chukua vitabu vya Bajeti utaona magari ni kiasi gani, majengo ya Utawala kiasi gani,makazi ya Viongozi kiasi gani.Mbona Kila kitu Huwa kinawekwa wazi?

Wazuge Kwa sababu zipi za msingi? Gari ni kitendea kazi na Samia kayanunua kweli Kila taasisi ya Umma Kwa Sasa Haina shida sana za vitendea kazi kama Mwanzo View attachment 2965731
Sasa hadi vitabuni ni leo tena bloangu?
 
Basi wangetufikiria kidogo walimu...
Wangetupa hata boda boda!!
Ualimu nchi hii ni alama ya umaskini, uoga na ujinga , kwaio subiri muda wa uchaguzi upewe tsheti na kofia. Bodaboda itakubidi uungeunge mshahara wako wa nyanya.
 
Waziri wa TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa amesema katika mwaka 2024/25, TAMISEMI imepanga kutumia shilingi bilioni 190.57 kwa ajili ya ununuzi wa magari ya Viongozi wa Mikoa na Wilaya, kuendelea na ujenzi, ukarabati na ukamilishaji wa miundombinu ya Mikoa ikiwemo majengo ya utawala, Ikulu ndogo, makazi ya Viongozi na Watumshi wa Mikoa, Wilaya na Tarafa katika Mikoa 26.

Mchengerwa ametoa taarifa hiyo Bungeni Jijini Dodoma leo April 16,2024 wakati akitoa hotuba kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka 2024/202 ambapo amesema shughuli zitakazotekelezwa katika utawala bora ni pamoja na ununuzi wa magari 9 ya Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa katika Mikoa ya Katavi, Njombe, Iringa, Kigoma, Mwanza, Singida, Dar es Salaam na Manyara”

“Shughuli nyingine ni ununuzi wa magari 56 ya Wakuu wa Wilaya na 47 ya Wakurugenzi wa Halmashauri”
Ni mwendelezo wa matumizi mabaya serikalini...hakuna lugha nyingine.
 
Waziri wa TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa amesema katika mwaka 2024/25, TAMISEMI imepanga kutumia shilingi bilioni 190.57 kwa ajili ya ununuzi wa magari ya Viongozi wa Mikoa na Wilaya, kuendelea na ujenzi, ukarabati na ukamilishaji wa miundombinu ya Mikoa ikiwemo majengo ya utawala, Ikulu ndogo, makazi ya Viongozi na Watumshi wa Mikoa, Wilaya na Tarafa katika Mikoa 26.

Mchengerwa ametoa taarifa hiyo Bungeni Jijini Dodoma leo April 16,2024 wakati akitoa hotuba kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka 2024/202 ambapo amesema shughuli zitakazotekelezwa katika utawala bora ni pamoja na ununuzi wa magari 9 ya Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa katika Mikoa ya Katavi, Njombe, Iringa, Kigoma, Mwanza, Singida, Dar es Salaam na Manyara”

“Shughuli nyingine ni ununuzi wa magari 56 ya Wakuu wa Wilaya na 47 ya Wakurugenzi wa Halmashauri”
Brazil kwa kuuza soy beans pekee inaingiza Usd 35 billion..zaidi ya budget yetu nzima!
Mbona hatufikirii kukipa bust kilimo cha umwagiliaji ambacho kitaajir lots of pple na kupunguza umasikini,haya madude yananunuliwa kwa pesa mingi na pia maintanance yake ni kubwa mno, lets be real,namna hii tunachelewa!
 
Huku bima za afya NHIF zimefutwa,, TRUMP AJENGEWE SANAMU POPOTE.

AFRICA A SHIT HOLE
 
Halmashauri zinadaiwa hadi na wazee waliokwishastaafu miaka mitano iliyopita.

Wakurugenzi hawapeleki michango ya watumishi kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii kiasi wastaafu wengi wamelipwa pension pungufu hivyo bado wanasotea since 2019 huko.

Halafu watu wananunuliana magari tu na wanauziana wenyewe baadae kwa bei ya kashata.
 
Back
Top Bottom