Wanawake Kufuata Jeneza Na Kumswalia Maiti



Alhidaaya.com





Swali:



Je inafaa kwa mwanamke kufuatia jeneze hadi misikiti na kumswaliya maiti? Jazaakumullahu kheiran





Jibu:



AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.



Inachukiza kwa wanawake kufuata jeneza kwa kauli ya Ummu 'Atwiyyah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa tulikatazwa kufuata jeneza na haikufanywa ni Shariy’ah kwetu sisi [Muslim].



Kumswalia maiti mwanamke anaruhusiwa naye kujiunga katika Swaalah ya Janaazah.

Ingia katika kiungo kifuatacho upate maelezo zaidi muhimu yanayohusu mas-ala haya:



Wanawake Wanayopasa Kufanya Wakati Wa Jeneza Linapotoka



Na Allaah Anajua zaidi
 
UJUMBE WA LEO :

Biblia inatufahamisha tena kuwa kumbe anayefaa kuwa na mke mmoja ni askofu kumaanisha asiyekuwa askofu anaweza kuwa na zaidi ya mmoja. Hebu tusome: "Basi, askofu anapaswa kuwa mtu asiye na lawama; anapaswa awe na mke mmoja tu, awe mwenye kiasi, nidhamu na utaratibu" (1 Timotheo 3: 2). Hatujui kwa nini maaskofu wa Kikatoliki hawaruhusiwi kuoa kabisa?


Mwengine anayefaa kuwa na mke mmoja ni mzee wa Kanisa kama tunavyoarifiwa: "Mzee wa Kanisa anapaswa kuwa mtu asiye na hatia; aliye na mke mmoja tu, na watoto wake wanapaswa kuwa waumini" (Tito 1: 6).
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب النهي عن البخل والشح

061-Mlango Wa Kukatazwa Ubakhili na Uchoyo



Alhidaaya.com





قَالَ الله تَعَالَى:

وَأَمَّا مَن بَخِلَ وَاسْتَغْنَىٰ ﴿٨﴾ وَكَذَّبَ بِالْحُسْنَىٰ ﴿٩﴾ فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْعُسْرَىٰ ﴿١٠﴾ وَمَا يُغْنِي عَنْهُ مَالُهُ إِذَا تَرَدَّىٰ ﴿١١﴾

Ama yule afanyaye ubakhili na akajiona amejitosheleza. Na akakadhibisha Al-Husnaa (anayowajibika kuyasadiki). Na Tutamuwepesishia kwa yaliyo magumu. Na itamsaidia nini mali yake atakapoporomoka kuangamia (motoni). [Al-Layl: 8-11]



وَمَن يُوقَ شُحَّ نَفْسِهِ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ﴿١٦﴾

Na yeyote anayeepushwa na ubakhili na tamaa ya uchu wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufaulu. [At-Taghaabun: 16]







Hadiyth – 1

وعن جابر رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( اتَّقُوا الظُّلْمَ ؛ فَإِنَّ الظُّلْمَ ظُلُمَاتٌ يَوْمَ القِيَامَةِ . وَاتَّقُوا الشُّحَّ ؛ فَإنَّ الشُّحَّ أهْلَكَ مَنْ كَانَ قَبْلَكُمْ ، حَمَلَهُمْ عَلَى أنْ سَفَكُوا دِمَاءهُمْ وَاسْتَحَلُّوا مَحَارِمَهُمْ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ogopeni dhuluma, kwani dhuluma, ni giza kwa mwenye kuifanya Siku ya Qiyaamah. Na ogopeni (tahadharini) na ubakhili, kwani ubakhili ndio uliowaangamiza waliokuwa kabla yenu. Huu (ubakhili) uliwapelekea wao kumwaga damu na kuhalalisha vilivyo haramu." [Muslim]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب الإيثار والمواساة

062-Mlango Wa Kupendelea Wengine na Kusaidiana



Alhidaaya.com



قَالَ الله تَعَالَى:

وَيُؤْثِرُونَ عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ وَلَوْ كَانَ بِهِمْ خَصَاصَةٌ ۚ ﴿٩﴾

Na wanawapendelea kuliko nafsi zao japokuwa wao wenyewe wanahitaji. [Al-Hashr: 9]



وَيُطْعِمُونَ الطَّعَامَ عَلَىٰ حُبِّهِ مِسْكِينًا وَيَتِيمًا وَأَسِيرًا﴿٨﴾

Na wanalisha chakula, juu ya kukipenda kwake, masikini na mayatima na mateka. [Al-Insaan: 8]







Hadiyth – 1

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : جَاءَ رَجُلٌ إِلَى النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ : إنِّي مَجْهُودٌ، فَأرسَلَ إِلَى بَعْضِ نِسَائِهِ ، فَقالت : وَالَّذي بَعَثَكَ بِالحَقِّ مَا عِنْدِي إِلاَّ مَاءٌ، ثُمَّ أرْسَلَ إِلَى أُخْرَى ، فَقَالَتْ مِثلَ ذَلِكَ ، حَتَّى قُلْنَ كُلُّهُنَّ مِثلَ ذَلِكَ : لا وَالَّذِي بَعَثَكَ بالحَقِّ مَا عِنْدِي إِلاَّ مَاءٌ . فَقَالَ النبي صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ يُضيفُ هَذَا اللَّيْلَةَ ؟ )) فَقَالَ رَجُلٌ مِنَ الأنْصَارِ : أنَا يَا رسولَ الله ، فَانْطَلَقَ بِهِ إِلَى رَحْلِهِ ، فَقَالَ لامْرَأَتِهِ : أكرِمِي ضَيْفَ رسول الله صلى الله عليه وسلم .

وفي روايةٍ قَالَ لامْرَأَتِهِ : هَلْ عِنْدَكِ شَيْءٌ ؟ فقَالَتْ : لاَ ، إِلاَّ قُوتَ صِبيَانِي . قَالَ: فَعَلِّليهم بِشَيْءٍ وَإذَا أرَادُوا العَشَاءَ فَنَوِّمِيهمْ ، وَإِذَا دَخَلَ ضَيْفُنَا فَأطْفِئي السِّرَاجَ ، وَأريهِ أنَّا نَأكُلُ . فَقَعَدُوا وَأكَلَ الضَّيْفُ وَبَاتَا طَاوِيَيْنِ ، فَلَمَّا أصْبَحَ غَدَا عَلَى النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ : (( لَقَدْ عَجبَ الله مِنْ صَنِيعِكُمَا بِضَيْفِكُمَا اللَّيْلَةَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: "Alikuja mtu kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na akamwambia: "Mimi nina njaa." Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akatuma kwa mmoja wa wakeze, Alimjibu: "Naapa kwa aliyekutuma kwa haki sina chochote isipokuwa maji." Kisha akamtuma kwa mwingine, akasema mfano wake: "Naapa kwa aliyekutuma kwa haki sina isipokuwa maji." Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akauliza: "Nani atamkirimu huyu usiku wa leo?", Akasema mtu katika Answaari: "Mimi Ee Rasuli wa Allaah." Akaenda naye nyumbani kwake, akamwambia mkewe: "Mkirimu mgeni wa Rasuli wa Allaah(Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)."

Na katika riwaayah: alimwambia: "Je, una chochote?" Akasema: "La, isipokuwa chakula cha watoto." Akasema: Washughulishe na vitu, wakitaka chakula walalishe. Na anapoingia mgeni wetu zima koroboi, na muonyeshe kuwa tunakula. Wakakaa, na mgeni akala, Wao wakalala na njaa. Kulipo pambazuka alikwenda kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na akamwambia: "Hakika Allaah ameshangazwa kwa kitendo chenu cha usiku kwa mgeni wenu." [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 2

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( طَعَامُ الاثْنَيْنِ كَافِي الثَّلاَثَةِ ، وَطَعَامُ الثَّلاَثَةِ كَافِي الأربَعَةِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

وفي رواية لمسلمٍ عن جابر رضي الله عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( طَعَامُ الوَاحِدِ يَكْفِي الاثْنَيْنِ ، وَطَعَامُ الاثْنَيْنِ يَكْفِي الأَرْبَعَةَ ، وَطَعَامُ الأَرْبَعَة يَكْفِي الثَّمَانِية ))

Na imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Chakula cha wawili kinatosha watatu, na chakula cha watatu kinatosha wanne." [Al-Bukhaariy, Muslim na At-Tirmidhiy]

Na katika riwaayah ya Muslim kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Chakula cha mmoja kinatosha wawili, na chakula cha wawili kinatosha wanne, na chaula cha wanne kinatosha wanane."





Hadiyth – 3

وعن أَبي سعيد الخدري رضي الله عنه ، قَالَ : بَيْنَمَا نَحْنُ فِي سَفَرٍ مَعَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم إذْ جَاءَ رَجُلٌ عَلَى رَاحِلَةٍ لَهُ ، فَجَعَلَ يَصرِفُ بَصَرَهُ يَميناً وَشِمَالاً ، فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ كَانَ مَعَهُ فَضْلُ ظَهْرٍ فَليَعُدْ بِهِ عَلَى مَنْ لا ظَهرَ لَهُ ، وَمَنْ كَانَ لَهُ فَضْلٌ مِنْ زَادٍ ، فَلْيَعُدْ بِهِ عَلَى مَنْ لا زَادَ لَهُ )) فَذَكَرَ مِنْ أصْنَافِ المالِ مَا ذكر حَتَّى رَأيْنَا أنَّهُ لاَ حَقَّ لأحَدٍ مِنَّا في فَضْلٍ . رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Sa'iyd Al-Khudhriy(Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Tulipokuwa katika safari pamoja na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mara akaja mtu akiwa amepanda kipandio chake na huku anatizama kuliani na kushotoni kwake. Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): 'Yeyote ambaye ana kipando cha ziada (mnyama wa kupanda) basi ampatie (kama swadaqah) asiyekuwa nao; na yoyote mwenye ziada ya chakula basi atoe swadaqah kwa asiyekuwa nacho.' Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaendelea kutaja aina tofauti ya mali mpaka tukadhania kuwa hapana haki ya mmoja wetu kuwa na ziada ya chochote." [Muslim]





Hadiyth – 4

وعن سهل بن سعدٍ رضي الله عنه : أنَّ أمْرَأةً جَاءَتْ إِلَى رسول الله صلى الله عليه وسلم بِبُرْدَةٍ مَنْسُوجَةٍ ، فَقَالَتْ : نَسَجْتُها بِيَدَيَّ لأَكْسُوكَهَا ، فَأَخَذَهَا النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم مُحْتَاجاً إِلَيْهَا ، فَخَرَجَ إِلَيْنَا وَإنَّهَا إزَارُهُ ، فَقَالَ فُلانٌ : اكْسُنِيهَا مَا أحْسَنَهَا ! فَقَالَ : (( نَعَمْ )) فَجَلَسَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم في المَجْلِسُ ، ثُمَّ رَجَعَ فَطَواهَا ، ثُمَّ أرْسَلَ بِهَا إِلَيْهِ : فَقَالَ لَهُ الْقَومُ : مَا أحْسَنْتَ ! لَبِسَهَا النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم مُحتَاجَاً إِلَيْهَا ، ثُمَّ سَألْتَهُ وَعَلِمْتَ أنَّهُ لا يَرُدُّ سَائِلاً ، فَقَالَ : إنّي وَاللهِ مَا سَألْتُهُ لألْبِسَهَا ، إنَّمَا سَألْتُهُ لِتَكُونَ كَفنِي . قَالَ سَهْلٌ : فَكَانَتْ كَفَنَهُ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Sahl bin Sa'd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa mwanamke alimjia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na shuka iliyofumwa akasema: "Nimeifuma kwa mikono yangu ili nikuvalishe." Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaichukua kwani alikuwa anaihitaji, aliivaa kama izari yake (kikoi). Mtu akasema: "Nipe mimi kwani ni kizuri sana." Akasema: "Ndio." Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akakaa katika kikao, aliingia ndani, akakikunja na kumpelekea. Watu wakamwambia: "Hukufanya vizuri kwani Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikivaa kwa kuwa anakihitaji nawe ukamuomba akupati huku ukijua kuwa yeye hamrudishi mtupu mwenye kumuomba." Akasema: "Wa-Allaahi mimi sikumuomba ili nikivae, bali nimemuomba ili iwe sanda yangu." Akasema Sahl: "Hiyo ndiyo iliyokuwa sanda yake." [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 5

وعن أَبي موسى رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ الأشْعَرِيِّينَ إِذَا أرْمَلُوا في الغَزْوِ ، أَوْ قَلَّ طَعَامُ عِيَالِهِمْ بالمَديِنَةِ ، جَمَعُوا مَا كَانَ عِنْدَهُمْ في ثَوْبٍ وَاحِدٍ ، ثُمَّ اقْتَسَمُوهُ بَيْنَهُمْ في إنَاءٍ وَاحدٍ بالسَّوِيَّةِ فَهُمْ مِنِّي وَأنَا مِنْهُمْ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Muwsaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Al'Ash'ariyy wanapoenda vitani au chakula cha ukoo kikipungua Madiynah, wana jumuisha walivyonavyo katika nguo moja, kisha wanagawana baina yao sawasawa katika chombo kimoja. Hivyo wao ni pamoja na mimi, nami ni pamoja na wao." [Al-Bukhaariy na Muslim]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب التنافس في أمور الآخرة والاستكثار مما يتبرك بِهِ

063-Mlango Wa Kushindana Katika Mambo Yanayohusu Aakhera na Kutaka Vitu vya Baraka



Alhidaaya.com





قَالَ الله تَعَالَى:

وَفِي ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ الْمُتَنَافِسُونَ ﴿٢٦﴾

Mwisho wake ni miski. Na katika hayo basi washindane wenye kushindana …[Al-Mutwaffifiyn: 26]









Hadiyth – 1

وعن سَهْلِ بن سَعدٍ رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم أُتِيَ بِشَرابٍ ، فَشَرِبَ مِنْهُ وَعَنْ يَمِينِهِ غُلاَمٌ ، وَعَنْ يَسَارِهِ الأشْيَاخُ ، فَقَالَ لِلغُلاَمِ : (( أتَأذَنُ لِي أنْ أُعْطِيَ هؤُلاء ؟ )) فَقَالَ الغُلامُ : لاَ وَاللهِ يَا رسولَ الله ، لا أُوْثِرُ بِنَصِيبـي مِنْكَ أحَداً . فَتَلَّهُ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم في يَدِهِ . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kutoka kwa Sahl bin Sa'd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliletewa kinywaji, naye akanywa kidogo. Kulikuwa na kijana upande wake wa kulia na wazee upande wake wa kushoto. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia yule kijana: "Je, utanipatia idhini niwapatie hawa (yaani wazee)?' Akasema yule kijana: "Ee Rasuli wa Allaah! Naapa kwa Allaah kuwa simpatii nafasi hiyo yeyeote baada yako." Hivyo, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimpatia kinywaji kilichobaki." [Al-Bukhaariy na Muslim]







Hadiyth – 2

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( بَيْنَا أيُّوبُ عَلَيْهِ السَّلام يَغْتَسِلُ عُرْيَاناً ، فَخَرَّ عَلَيْهِ جَرَادٌ مِنْ ذَهَبٍ ، فَجَعَلَ أيُّوبُ يَحْثِي في ثَوْبِهِ ، فَنَادَاهُ رَبُّهُ عز وجل : يَا أيُّوبُ ، ألَمْ أكُنْ أغْنَيتكَ عَمَّا تَرَى ؟! قَالَ : بَلَى وَعِزَّتِكَ وَلَكِنْ لاَ غِنى بي عن بَرَكَتِكَ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wakati Nabiy Ayyub ('Alayhis Salaam) alikuwa akioga uchi, mara nzige wa dhahabu akadondoka juu yake. Alijaribu kumshika kwa nguo yake, Allaah ('Azza wa Jalla) akamwita: 'Ee Ayyuwb!, Je sikuwa mwenye kukutosha wewe kama uonavyo?' Akasema: Ndio! lakini mimi sitosheki na baraka zako." [Al-Bukhaariy]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب فضل الغَنِيّ الشاكر وهو من أخذ المال من وجهه وصرفه في وجوهه المأمور بِهَا

064-Mlango wa Ubora wa Tajiri Mwenye Kushukuru na Kuchuma Mali na Halali na Kuitumia kwa Njia Iliyoamriwa



Alhidaaya.com





قَالَ الله تَعَالَى:



فَأَمَّا مَنْ أَعْطَىٰ وَاتَّقَىٰ ﴿٥﴾ وَصَدَّقَ بِالْحُسْنَىٰ ﴿٦﴾ فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْيُسْرَىٰ ﴿٧﴾

Basi yule anayetoa (mali) na akamcha Allaah. Na akasadikisha Al-Husnaa (jazaa na laa ilaaha illa Allaah). Basi Tutamuwepesishia kwa yaliyo mepesi [Al-Layl: 5-7]



وَسَيُجَنَّبُهَا الْأَتْقَى ﴿١٧﴾ الَّذِي يُؤْتِي مَالَهُ يَتَزَكَّىٰ ﴿١٨﴾ وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُ مِن نِّعْمَةٍ تُجْزَىٰ ﴿١٩﴾ إِلَّا ابْتِغَاءَ وَجْهِ رَبِّهِ الْأَعْلَىٰ ﴿٢٠﴾ وَلَسَوْفَ يَرْضَىٰ ﴿٢١﴾

Na ataepushwa nao mwenye taqwa kabisa. Ambaye anatoa mali yake kujitakasa. Na hali hakuna mmoja yeyote aliyemfanyia fadhila yoyote hata amlipe. Isipokuwa kutaka Wajihi wa Rabb wake Aliyetukuka. Na bila shaka atakuja kuridhika. [Al-Layl: 17-21]



إِن تُبْدُوا الصَّدَقَاتِ فَنِعِمَّا هِيَ ۖ وَإِن تُخْفُوهَا وَتُؤْتُوهَا الْفُقَرَاءَ فَهُوَ خَيْرٌ لَّكُمْ ۚ وَيُكَفِّرُ عَنكُم مِّن سَيِّئَاتِكُمْ ۗ وَاللَّـهُ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرٌ ﴿٢٧١﴾

Mkidhihirisha swadaqah basi ni vizuri hivyo, na mkizificha na kuwapa mafakiri, basi hilo ni khayr kwenu. Na Atakufutieni katika maovu yenu. Na Allaah kwa yale myatendayo, ni Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika. [Al-Baqarah: 271]





لَن تَنَالُوا الْبِرَّ حَتَّىٰ تُنفِقُوا مِمَّا تُحِبُّونَ ۚ وَمَا تُنفِقُوا مِن شَيْءٍ فَإِنَّ اللَّـهَ بِهِ عَلِيمٌ ﴿٩٢﴾

Hamtoweza kuufikia wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda. Na kitu chochote mnachotoa basi hakika Allaah kwacho ni Mjuzi. [Aal-'Imraan: 92]









Hadiyth – 1

وعن عبدِ الله بن مسعود رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( لاَ حَسَدَ إِلاَّ في اثْنَتَيْنِ : رَجُلٌ آتَاهُ اللهُ مَالاً ، فَسَلَّطَهُ عَلَى هَلَكَتِهِ فِي الحَقِّ ، وَرَجُلٌ آتَاهُ اللهُ حِكْمَةً فَهُوَ يَقضِي بِهَا وَيُعَلِّمُهَا )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hapana kuoneana wivu ila kwa mambo mawili: Mtu aliyepewa na Allaah mali na akawa akaitumia katika njia ya haki (kujikurubisha na Allaah pamoja na kutii) na mtu ambaye amepatiwa na Allaah hekima, naye anahukumu watu kwayo na kuifundisha." [Al-Bukhaariy na Muslim]







Hadiyth – 2

وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لاَ حَسَدَ إِلاَّ في اثْنَتَيْنِ : رَجُلٌ آتَاهُ اللهُ القُرْآنَ ، فَهُوَ يَقُومُ بِهِ آنَاءَ اللَّيْلِ وَآنَاءَ النَّهَارِ ، وَرَجُلٌ آتَاهُ مَالاً ، فَهُوَ يُنْفِقُهُ آنَاءَ اللَّيْلِ وَآنَاءَ النَّهَارِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Na imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hapana hasad (wivu) ila kwa watu wawili: Mtu ambaye amepatiwa Quraan na Allaah, naye akawa amesimama imara nayo kwa kuisoma na kuitekeleza maamrisho yake mchana na usiku; na mwengine ni yule aliyepatiwa mali na Allaah, naye akawa anaitoa (swadaqah) mchana na usiku." [Al-Bukhaariy na Muslim]







Hadiyth – 3

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ فُقَراءَ المُهَاجِرينَ أتَوْا رسول الله صلى الله عليه وسلم ، فَقَالُوا : ذَهَبَ أهْلُ الدُّثُورِ بِالدَّرَجَاتِ العُلَى ، وَالنَّعِيم المُقيم ، فَقَالَ : (( وَمَا ذَاك ؟)) فَقَالوا : يُصَلُّونَ كَمَا نُصَلِّي ، وَيَصُومُونَ كَمَا نَصُومُ ، وَيَتَصَدَّقُونَ وَلاَ نَتَصَدَّقُ ، وَيَعْتِقُونَ وَلاَ نَعْتِقُ ، فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( أفَلا أُعَلِّمُكُمْ شَيْئاً تُدْرِكُونَ بِهِ مَنْ سَبَقَكُمْ ، وَتَسْبِقُونَ بِهِ مَنْ بَعْدَكُمْ ، وَلاَ يَكُونُ أحَدٌ أفْضَلَ مِنْكُمْ إِلاَّ مَنْ صَنَعَ مِثْلَ مَا صَنَعْتُمْ ؟ )) قالوا : بَلَى يَا رسول الله ، قَالَ : (( تُسَبِّحُونَ وَتُكَبِّرُونَ وَتَحْمِدُونَ ، دُبُرَ كُلِّ صَلاَةٍ ثَلاثاً وَثَلاثِينَ مَرَّةً )) فَرَجَعَ فُقَرَاء المُهَاجِرِينَ إِلَى رسول الله صلى الله عليه وسلم ، فقالوا : سَمِعَ إخْوَانُنَا أهلُ الأمْوالِ بِمَا فَعَلْنَا ، فَفَعَلُوا مِثلَهُ ؟ فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( ذَلِكَ فَضْلُ اللهِ يُؤْتِيهِ مَنْ يَشَاءُ )) متفقٌ عَلَيْهِ ، وَهَذا لفظ رواية مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba mafakiri wa Muhaajirina walikuja kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumwambia: "Wenye mali nyingi wamenyakuwa daraja za juu na neema za daima." Akasema: "Na inakuwa vipi hilo?" Wakasema: "Wao wanaswali kama tunavyoswali, wanafunga kam tunavyofunga, wanatoa swadaqah nasi hatutoi, wanaacha watumwa wala hatuachi." Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Je niwafundishe kitu mtawafikia nacho waliowapiteni, na mtawashinda wa baada yenu, wala hakuna bora kuliko nyinyi ila atakayefanya mnavyofanya?" Wakasema: "Ndio ee Rasuli wa Allaah." Akasema: "Msabihini Allaah, Muhimidini Allaah na leteni takbiri baada ya kila Swalaah mara thelathini na tatu." Walirudi tena mafakiri wa Muhaajirina kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakasema: 'Ndugu zetu wenye mali wamesikia tunayofanya, wakafanya mfano wake?" Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Hiyo ni fadhila ya Allaah anampa amtakaye." [Al-Bukhaariy na Muslim, na hii ni lafdhi ya riwaayah ya Muslim]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب ذكر الموت وقصر الأمل

065-Mlango wa Kukumbuka Mauti na Kupunguza Matarajio



Alhidaaya.com





قَالَ الله تَعَالَى:

كُلُّ نَفْسٍ ذَائِقَةُ الْمَوْتِ ۗ وَإِنَّمَا تُوَفَّوْنَ أُجُورَكُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ۖ فَمَن زُحْزِحَ عَنِ النَّارِ وَأُدْخِلَ الْجَنَّةَ فَقَدْ فَازَ ۗ وَمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا إِلَّا مَتَاعُ الْغُرُورِ ﴿١٨٥﴾

Kila nafsi itaonja mauti. Na hakika mtalipwa kikamilifu ujira wenu Siku ya Qiyaamah. Basi atakayewekwa mbali na moto na akaingizwa Jannah kwa yakini amefuzu. Na uhai wa dunia si lolote ila ni starehe ya udanganyifu. [Aal-'Imraan: 185]



وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ مَّاذَا تَكْسِبُ غَدًا ۖ وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ بِأَيِّ أَرْضٍ تَمُوتُ ۚ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ ﴿٣٤﴾

Na nafsi yoyote haijui nini itachuma kesho, na nafsi yoyote haijui itafia katika ardhi gani [Luqmaan: 34]





فَإِذَا جَاءَ أَجَلُهُمْ لَا يَسْتَأْخِرُونَ سَاعَةً ۖ وَلَا يَسْتَقْدِمُونَ ﴿٣٤﴾

Basi utakapofika muda wao huo, hawatataakhari wala hawatatangulia saa. [Al-A'raaf: 34]





يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُلْهِكُمْ أَمْوَالُكُمْ وَلَا أَوْلَادُكُمْ عَن ذِكْرِ اللَّـهِ ۚ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْخَاسِرُونَ﴿٩﴾

Enyi walioamini! Zisikupurukusheni mali zenu na wala watoto wenu mkaacha kumdhukuru Allaah. Na yeyote atakayefanya hivyo basi hao ndio waliokhasirika.



وَأَنفِقُوا مِن مَّا رَزَقْنَاكُم مِّن قَبْلِ أَن يَأْتِيَ أَحَدَكُمُ الْمَوْتُ فَيَقُولَ رَبِّ لَوْلَا أَخَّرْتَنِي إِلَىٰ أَجَلٍ قَرِيبٍ فَأَصَّدَّقَ وَأَكُن مِّنَ الصَّالِحِينَ﴿١٠﴾

Na toeni katika yale Tuliyokuruzukuni kabla hayajamfikia mmoja wenu mauti akasema: Rabb wangu! Lau Ungeliniakhirisha mpaka muda wa karibu hivi, basi ningetoa swadaqah na ningelikuwa miongoni mwa Swalihina.



وَلَن يُؤَخِّرَ اللَّـهُ نَفْسًا إِذَا جَاءَ أَجَلُهَا ۚ وَاللَّـهُ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ﴿١١﴾

Lakini Allaah Haiakhirishi kamwe nafsi yeyote inapokuja ajali yake na Allaah ni Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika kwa yale myatendayo. [Al-Munaafiquwn: 9-11]



حَتَّىٰ إِذَا جَاءَ أَحَدَهُمُ الْمَوْتُ قَالَ رَبِّ ارْجِعُونِ ﴿٩٩﴾

Mpaka itakapomfikia mmoja wao mauti, atasema: Rabb wangu! Nirejeshe (duniani).



لَعَلِّي أَعْمَلُ صَالِحًا فِيمَا تَرَكْتُ ۚ كَلَّا ۚ إِنَّهَا كَلِمَةٌ هُوَ قَائِلُهَا ۖ وَمِن وَرَائِهِم بَرْزَخٌ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ ﴿١٠٠﴾

Ili nikatende mema katika yale niliyoyaacha. (Ataambiwa) Laa hasha! Hakika hilo ni neno alisemaye yeye tu. Na nyuma yao kuna barzakh mpaka Siku watakayofufuliwa.



فَإِذَا نُفِخَ فِي الصُّورِ فَلَا أَنسَابَ بَيْنَهُمْ يَوْمَئِذٍ وَلَا يَتَسَاءَلُونَ ﴿١٠١﴾

Basi itakapopulizwa baragumu, hakutokuwa na unasaba baina yao Siku hiyo, na wala hawatoulizana.



فَمَن ثَقُلَتْ مَوَازِينُهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ ﴿١٠٢﴾

Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, hao ndio wenye kufaulu.



وَمَنْ خَفَّتْ مَوَازِينُهُ فَأُولَـٰئِكَ الَّذِينَ خَسِرُوا أَنفُسَهُمْ فِي جَهَنَّمَ خَالِدُونَ ﴿١٠٣﴾

Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu, basi hao ni ambao wamekhasirika nafsi zao; katika Jahannam ni wenye kudumu.



تَلْفَحُ وُجُوهَهُمُ النَّارُ وَهُمْ فِيهَا كَالِحُونَ ﴿١٠٤﴾

Moto utababua nyuso zao; nao humo watakuwa ni wenye midomo iliyosinyaa na kuvutika mbali na meno.



أَلَمْ تَكُنْ آيَاتِي تُتْلَىٰ عَلَيْكُمْ فَكُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ ﴿١٠٥﴾

(Wataambiwa): Je, hazikuwa Aayaat Zangu zinasomwa kwenu na nyinyi mkawa mnazikadhibisha?



إِلَى قَوْله تَعَالَى :



قَالَ كَمْ لَبِثْتُمْ فِي الْأَرْضِ عَدَدَ سِنِينَ ﴿١١٢﴾

(Allaah) Atasema: Muda gani mlikaa katika ardhi kwa idadi ya miaka?



قَالُوا لَبِثْنَا يَوْمًا أَوْ بَعْضَ يَوْمٍ فَاسْأَلِ الْعَادِّينَ ﴿١١٣﴾

Watasema: Tumekaa siku au sehemu tu ya siku. Basi waulize wanaohesabu.



قَالَ إِن لَّبِثْتُمْ إِلَّا قَلِيلًا ۖ لَّوْ أَنَّكُمْ كُنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿١١٤﴾

(Allaah) Atasema: Hamkukaa (huko duniani) isipokuwa kidogo tu, lau mngelikuwa mnajua.



أَفَحَسِبْتُمْ أَنَّمَا خَلَقْنَاكُمْ عَبَثًا وَأَنَّكُمْ إِلَيْنَا لَا تُرْجَعُونَ ﴿١١٥﴾

Je, mlidhania kwamba Sisi Tulikuumbeni bila kusudio mcheze tu na kwamba nyinyi Kwetu hamtorejeshwa? [Al-Muuminuwn: 99-115]





أَلَمْ يَأْنِ لِلَّذِينَ آمَنُوا أَن تَخْشَعَ قُلُوبُهُمْ لِذِكْرِ اللَّـهِ وَمَا نَزَلَ مِنَ الْحَقِّ وَلَا يَكُونُوا كَالَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلُ فَطَالَ عَلَيْهِمُ الْأَمَدُ فَقَسَتْ قُلُوبُهُمْ ۖ وَكَثِيرٌ مِّنْهُمْ فَاسِقُونَ ﴿١٦﴾

Je, haujafika wakati kwa walioamini kwamba zinyenyekee nyoyo zao kwa kumdhukuru Allaah na yale yaliyoteremka ya haki, na wala wasiwe kama wale waliopewa Kitabu kabla, ukawatawilikia muda, kisha zikawa ngumu nyoyo zao? Na wengi miongoni mwao ni mafasiki. [Al-Hadiyd: 16]







Hadiyth – 1

وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : أخذ رسول الله صلى الله عليه وسلم بِمِنْكَبي ، فَقَالَ : (( كُنْ في الدُّنْيَا كَأَنَّكَ غَرِيبٌ أَوْ عَابِرُ سَبِيلٍ )) . وَكَانَ ابْنُ عُمَرَ رضي الله عنهما ، يقول : إِذَا أمْسَيْتَ فَلاَ تَنْتَظِرِ الصَّبَاحَ ، وَإِذَا أصْبَحتَ فَلاَ تَنْتَظِرِ المَسَاءَ ، وَخُذْ مِنْ صِحَّتِكَ لِمَرَضِكَ ، وَمِنْ حَيَاتِكَ لِمَوْتِكَ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) akisema: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaau 'alayhi wa aalihi wa sallam) alishika mabega yangu akasema: 'kuwa duniani kana kwamba ni mgeni au mpita njia.' Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) alikuwa akisema: 'Na ukichelewa usingoje asubuhi, na unapopambazuka usingoje jioni. Na chukua uzima wako kwa ajili ya maradhi yako. Na chukua uhai wako kabla ya mauti yako." [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 2

وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَا حَقُّ امْرِئٍ مُسْلِمٍ ، لَهُ شَيْءٌ يُوصِي فِيهِ ، يَبيتُ لَيْلَتَيْنِ إِلاَّ وَوَصِيَّتُهُ مَكْتُوبَةٌ عِنْدَهُ )) متفقٌ عَلَيْهِ ، هَذَا لفظ البخاري .

وفي روايةٍ لمسلمٍ : (( يَبِيتُ ثَلاَثَ لَيَالٍ )) قَالَ ابن عمر : مَا مَرَّتْ عَلَيَّ لَيْلَةٌ مُنْذُ سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم قَالَ ذَلِكَ إِلاَّ وَعِنْدِي وَصِيَّتِي .

Na imepokewa kutoka kwa 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Haifai kwa Muislamu ambaye ana kitu cha kuusia (kitu ambacho kinaweza kurithiwa na warithi wake) kulala masiku mawili ila tayari ameandika usia wake." [Al-Bukhaariy na Muslim, hii ni lafdhi ya Al-Bukhaariy]

Na katika riwaayah ya Muslim: "Analala masiku matatu." Amesema Ibn 'Umar: "Haijapita kwangu usiku mmoja baada ya kusikia maneno haya kutoka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) isipokuwa nina usia wangu."





Hadiyth – 3

وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : خَطَّ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم خُطُوطاً ، فَقَالَ : (( هَذَا الإنْسَانُ ، وَهَذَا أجَلُهُ ، فَبَيْنَمَا هُوَ كَذَلِكَ إذْ جَاءَ الخَطُّ الأَقْرَبُ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwake Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Alichora Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mistari mingi akasema: Huyu ni mwanadamu na 'Msitari huu ni ajali yake. Akiwa hivyo anajiwa na msitari wa karibu" (yaani mauti)." [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 4

وعن ابن مسعود رضي الله عنه ، قَالَ : خَطَّ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم خَطّاً مُرَبَّعاً ، وَخَطَّ خَطّاً في الوَسَطِ خَارِجَاً مِنْهُ ، وَخَطَّ خُطَطاً صِغَاراً إِلَى هَذَا الَّذِي في الْوَسَطِ مِنْ جَانِبهِ الَّذِي في الوَسَط ، فَقَالَ : (( هَذَا الإنْسَانُ ، وَهذَا أجَلُهُ مُحيطاً بِهِ – أَوْ قَدْ أحَاطَ بِهِ – وَهذَا الَّذِي هُوَ خَارِجٌ أمَلُهُ ، وَهذِهِ الْخُطَطُ الصِّغَارُ الأَعْرَاضُ ، فَإنْ أخْطَأَهُ هَذَا ، نَهَشَهُ هَذَا ، وَإنْ أخْطَأَهُ هَذَا ، نَهَشَهُ هَذَا )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alichora hati ya mraba, akachora msitari katikati nje yake. Akachora mistari midogo kuelekea huu wa kati toka upande wake ambao uko katikati. Akasema: 'Huyu ni mwanadamu, na hii ni ajali yake imemzunguka, au imeshamkuta. Na huu ulio nje ni matarajio yake, hii mistari midogo ni mitihani, Unapomkosa huu basi anapatwa na huu; unapomkosa huu anakutwa na huu." [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( بَادِرُوا بِالأعْمَالِ سَبْعاً ، هَلْ تَنْتَظِرُونَ إِلاَّ فَقْراً مُنْسِياً ، أَوْ غِنَىً مُطْغِياً ، أَوْ مَرَضَاً مُفْسداً ، أَوْ هَرَماً مُفَنِّداً ، أَوْ مَوْتَاً مُجْهِزاً ، أَوْ الدَّجّالَ ، فَشَرُّ غَائِبٍ يُنْتَظَرُ ، أَوْ السَّاعَةَ وَالسَّاعَةُ أدْهَى وَأمَرُّ ؟! )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu). Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Harakisheni kufanya amali, kabla ya mambo saba: Je, mnangojea ufakiri unaosahaulisha, au utajiri unaopoteza, au maradhi yenye kuharibu siha, au uzee unaoharibu akili, au mauti ya ghafla, au kuja kwa Dajjaal naye ni shari iliyojificha inayongojewa, au Qiyaamah ni tukio gumu na chungu." [At-Tirmidhiy, ambaye alisema ni Hadiyth Hasan].





Hadiyth – 6

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( أكْثِرُوا ذِكْرَ هَاذِمِ اللَّذَّاتِ )) يَعْنِي : المَوْتَ . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameseam: "Zidisheni kukumbuka kiondoa ladha" (yaani umauti)." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan].





Hadiyth – 7

وعن أُبَيِّ بن كعبٍ رضي الله عنه : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم إِذَا ذَهَبَ ثُلُثُ اللَّيْلِ قَامَ ، فَقَالَ : (( يَا أَيُّهَا النَّاسُ ، اذْكُرُوا اللهَ ، جَاءتِ الرَّاجِفَةُ ، تَتْبَعُهَا الرَّادِفَةُ ، جَاءَ المَوْتُ بِمَا فِيهِ ، جَاءَ المَوْتُ بِمَا فِيهِ )) قُلْتُ : يَا رسول الله ، إنِّي أُكْثِرُ الصَّلاَةَ عَلَيْكَ ، فَكَمْ أجْعَلُ لَكَ مِنْ صَلاَتِي ؟ فَقَالَ : (( مَا شِئْتَ )) قُلْتُ : الرُّبُع ، قَالَ : (( مَا شِئْتَ ، فَإنْ زِدْتَ فَهُوَ خَيْرٌ لَكَ )) قُلْتُ : فَالنِّصْف ؟ قَالَ : (( مَا شِئْتَ ، فَإنْ زِدْتَ فَهُوَ خَيْرٌ لَكَ )) قُلْتُ : فالثُّلُثَيْنِ ؟ قَالَ : (( مَا شِئْتَ ، فَإنْ زِدْتَ فَهُوَ خَيْرٌ لَكَ )) قُلْتُ : أجعَلُ لَكَ صَلاَتِي كُلَّهَا ؟ قَالَ : (( إذاً تُكْفى هَمَّكَ ، وَيُغْفَر لَكَ ذَنْبكَ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Ubayy bin Ka'b (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa akiamka thuluthi ya mwisho ya usiku na kusema: "Enyi watu! Mtajeni Allaah! Tetemeko limekuja, likifuatiwa na raa-di, mauti yamekuja na yalio ndani yake." Nikamuuliza: "Ee Rasuli wa Allaah! Mimi nimeongeza kukuswalia. Je, nikutengee kiasi gani kwenye Swalaah yangu?" Akasema: "Unavyotaka." NIkasema: "Je, robo?" Akasema: "Unavyo penda na ukizidisha ni bora kwako." Nikasema: "Je, nusu?" Akasema: "Unavyo penda na ukizidisha ni bora kwako." Nikasema: "Je, thuluthi mbili (2/3)?" Akasema: "Unavyo penda na ukizidisha ni bora kwako." Nikasema: "Je, nijaalie swalaah yangu ni yako?" Akasema: "Basi utatoshwa hamu yako, na kufutiwa dhambi yako." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan].
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب استحباب زيارة القبور للرجال وما يقوله الزائر

066-Mlango Wa Kupendeza Kuzuru Makaburi kwa Wanaume na Anachosema Mwenye Kuzuru



Alhidaaya.com







Hadiyth – 1

عن بُرَيْدَة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( كُنْتُ نَهَيْتُكُمْ عن زِيَارَةِ القُبُورِ فَزُوروها )) رواه مسلم .

وفي رواية : (( فَمَنْ أرَادَ أنْ يَزُورَ القُبُورَ فَلْيَزُرْ ؛ فإنَّهَا تُذَكِّرُنَا الآخِرَةَ )) .

Imepokewa kutoka kwa Buraydah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nilikuwa nimekukatazeni kuzuru makaburi, sasa yazuruni." [Muslim]

Na katika riwaayah: "Yeyote anayetaka kuzuru makaburi basi ayazuru; kwani (huko kuzuru makaburi) kutawakumbusha Aakherah."





Hadiyth – 2

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم - كلَّما كَانَ لَيْلَتُهَا مِنْ رسول الله صلى الله عليه وسلم - يَخْرُجُ مِنْ آخِرِ اللَّيْلِ إِلَى البَقِيعِ ، فَيقولُ : (( السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ دَارَ قَوْمٍ مُؤْمِنِينَ ، وَأتَاكُمْ مَا تُوعَدُونَ ، غَداً مُؤَجَّلْونَ ، وَإنَّا إنْ شَاءَ اللهُ بِكُمْ لاَحِقُونَ ، اللَّهُمَّ اغْفِرْ لأهْلِ بَقِيعِ الغَرْقَدِ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiyah Allaahu 'anhaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kila inapokuwa zamu yake, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), alikuwa anatoka mwisho wa usiku kuelekea Baqii' na anasema: "Amani juu yenu Waumini wa nyumba hii, Yamekujieni mlioahidiwa, Mmetangulizwa wakatimaalumu. Na hakika sisi akitaka Allaah tutakutana nanyi. Ee Mola wangu wasamehe watu wa Al'Baqi'i Al-Gharqad, (yenye michongoma)." [Muslim]





Hadiyth – 3

وعن بريدة رضي الله عنه ، قَالَ : كَانَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم يُعَلِّمُهُمْ إِذَا خَرَجُوا إِلَى المَقَابِرِ أنْ يَقُولَ قَائِلُهُمْ : (( السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ أهلَ الدِّيَارِ مِنَ المُؤْمِنينَ وَالمُسلمينَ ، وَإنَّا إنْ شَاءَ اللهُ بِكُمْ للاَحِقونَ ، أسْألُ اللهَ لَنَا وَلَكُمُ العَافِيَةَ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Buraydah (Radhwiya Allahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiwafundisha dua wakitoka kwenda makaburini asema mmoja wao: "Amani juu yenu watu wa nyumba hizi miongoni mwa Waumini na Waislamu. Na hakika sisi akitaka Allaah tutakutana nanyi, Tunamuomba Allaah sisi na nyinyi afya." [Muslim]







Hadiyth – 4

وعن ابن عباسٍ رضي الله عنهما ، قَالَ : مرَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم بِقُبورٍ بالمدِينَةِ فَأقْبَلَ عَلَيْهِمْ بِوَجْهِهِ ، فَقَالَ : (( السَّلامُ عَلَيْكُمْ يَا أهْلَ القُبُورِ ، يَغْفِرُ اللهُ لَنَا وَلَكُمْ ، أنْتُمْ سَلَفُنَا وَنَحنُ بالأثَرِ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Na imepokewa kutoka kwa bn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipita katika makaburi ya Madiynah akayakabili kwa uso wake na kusema: "Amani iwashukie enyi watu wa makaburi. Allaah atusamehe sisi na nyinyi. Nyinyi mumetutangulia nasi tunawafuatia." [At-Tirmidhiy, na kasema ni Hadiyth Hasan].
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



بابُ كراهة تمنّي الموت بسبب ضُرّ نزل بِهِ وَلاَ بأس بِهِ لخوف الفتنة في الدين

067-Mlango Wa Karaha ya Kutamani Umauti Kwa Sababu ya Dhara Iliyomkumba na Haina Tatizo Ikiwa Anahofia Fitna Katika Dini



Alhidaaya.com









Hadiyth – 1

عن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لا يَتَمَنَّ أحَدُكُمُ المَوْتَ ، إمَّا مُحْسِناً فَلَعَلَّهُ يَزْدَادُ ، وَإمَّا مُسِيئاً فَلَعَلَّهُ يَسْتَعْتِبُ )) متفقٌ عَلَيْهِ ، وهذا لفظ البخاري .

وفي رواية لمسلم عن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لاَ يَتَمَنَّ أَحَدُكُمُ المَوْتَ ، وَلاَ يَدْعُ بِهِ مِنْ قَبْلِ أنْ يَأتِيَهُ ؛ إنَّهُ إِذَا مَاتَ انْقَطَعَ عَمَلُهُ ، وَإنَّهُ لاَ يَزِيدُ المُؤْمِنَ عُمُرُهُ إِلاَّ خَيْراً )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Asitamani mmoja wenu mauti kwani kama kama ni mtu mwema huenda akazidisha amali njema. Na ama akiwa ni mtu muovu (mwenye kufanya madhambi) huenda akatubia (na kutadaraki yalioyopita)." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad, na hii ni lafdhi ya Al-Bukhaariy]

Katika riwaayah ya Muslim kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Asitamani mmoja wenu umauti wala asiwe ni mwenye kujiombea kabla hayajamfikia, kwani akiaga dunia amali yake yote hukatika. Na kwa hakika umri wa Muumini hauongezeki ila huleta kheri zaidi."





Hadiyth – 2

وعن أنسٍ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( لاَ يَتَمَنَّيَنَّ أحَدُكُمُ المَوْتَ لِضُرٍّ أصَابَهُ ، فَإنْ كَانَ لاَ بُدَّ فَاعِلاً ، فَلْيَقُلْ : اللَّهُمَّ أحْيِني مَا كَانَتِ الحَيَاةُ خَيْراً لي ، وَتَوَفَّنِي إِذَا كَانَت الوَفَاةُ خَيراً لي )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwake Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Asitamani mmoja wenu mauti kwa sababu ya madhara yaliyomsibu. Ikiwa hapana budi mpaka atamani basi aseme: 'Ee Mola wangu nipe uhai ikiwa una kheri na mimi na unifishe ikiwa kuaga dunia kwangu ni kheri kwangu." [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 3

وعن قيسِ بن أَبي حازم ، قَالَ : دَخَلْنَا عَلَى خَبَّاب بن الأرَتِّ رضي الله عنه نَعُودُهُ وَقَدِ اكْتَوَى سَبْعَ كَيَّاتٍ ، فَقَالَ : إنَّ أَصْحَابَنَا الَّذِينَ سَلَفُوا مَضَوْا ، وَلَمْ تَنْقُصْهُمُ الدُّنْيَا ، وَإنَّا أصَبْنَا مَا لاَ نَجِدُ لَهُ مَوْضِعاً إِلاَّ التُّرَابَ وَلولا أنَّ النبي صلى الله عليه وسلم نَهَانَا أنْ نَدْعُوَ بالمَوْتِ لَدَعَوْتُ بِهِ . ثُمَّ أتَيْنَاهُ مَرَّةً أُخْرَى وَهُوَ يَبْنِي حَائِطاً لَهُ ، فَقَالَ : إنَّ المُسْلِمَ لَيُؤْجَرُ فِي كُلِّ شَيْءٍ يُنْفِقُهُ إِلاَّ فِي شَيْءٍ يَجْعَلُهُ في هَذَا التُّرَابِ . متفقٌ عَلَيْهِ ، وهذا لفظ رواية البخاري

Imepokewa kutoka kwake Qays bin Abu Haazim amesema: Tulimtembelea Khabbaab bin Al-Aratt (Radhwiya Allaahu 'anhu) alipokuwa mgonjwa. Mishipa yake ya damu ilikuwa imefunguliwa mahali saba. Alituambia: "Hakika sahibu zetu waliotangulia wamepita, Dunia haikuwapunguza. Kwa hakika sisi tumepata ambayo hayan mahali isipokuwa udongo. Na lau sio Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kutukataza kuomba mauti ningeyaomba." Kisha tulimzuru mara nyingine tukamkuta anajenga ukuta wake, akasema: "Hakika Muislaamu analipwa kwa kila kitu anachotoa isipokuwa kitu anachokijalia katika huu udongo." [Al-Bukhaariy na Muslim, na hii ni lafdhi ya Al-Bukhaariy]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب الورع وترك الشبهات

068-Mlango Wa Kujichunga na Kuacha Mambo Yenye Shaka



Alhidaaya.com





قَالَ الله تَعَالَى

وَتَحْسَبُونَهُ هَيِّنًا وَهُوَ عِندَ اللَّـهِ عَظِيمٌ ﴿١٥﴾

Na mnalidhania ni jambo jepesi; na hali hili mbele ya Allaah ni kubwa mno. [An-Nuwr: 15]

إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ ﴿١٤﴾

Hakika Rabb wako bila shaka Yu tayari Awavizia. [Al-Fajr: 14]







Hadiyth – 1

وعن النعمان بن بشيرٍ رضي الله عنهما ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( إنَّ الحَلاَلَ بَيِّنٌ ، وَإنَّ الحَرامَ بَيِّنٌ ، وَبَيْنَهُمَا مُشْتَبَهَاتٌ لاَ يَعْلَمُهُنَّ كَثيرٌ مِنَ النَّاسِ ، فَمَنِ اتَّقَى الشُّبُهَاتِ ، اسْتَبْرَأَ لِدِينهِ وَعِرْضِهِ ، وَمَنْ وَقَعَ فِي الشُّبُهَاتِ وَقَعَ في الحَرَامِ ، كَالرَّاعِي يَرْعَى حَوْلَ الحِمَى يُوشِكُ أنْ يَرْتَعَ فِيهِ ، ألاَ وَإنَّ لكُلّ مَلِكٍ حِمَىً ، ألاَ وَإنَّ حِمَى اللهِ مَحَارِمُهُ ، ألاَ وَإنَّ فِي الجَسَدِ مُضْغَةً إِذَا صَلَحَت صَلَحَ الْجَسَدُ كُلُّهُ ، وَإِذَا فَسَدَتْ فَسَدَ الْجَسَدُ كُلُّهُ ، ألاَ وَهِيَ القَلْبُ )) متفقٌ عَلَيْهِ ، وروياه مِنْ طرقٍ بِألفَاظٍ متقاربةٍ .

Imepokewa kutoka kwa An-Nu'maan bin Bashiyr (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakika halali iko wazi na haramu iko wazi; na baina ya vitu hivi viwili kuna mambo yenye shaka, watu wengi hawayajui. Basi mwenye kuepuka mambo yenye shaka, hakika amehifadhi Dini yake na heshima yake. Na mwenye kuingia kwenye mambo ya shaka ameingia kwenye haramu, kama mchunga anayechunga pambizoni mwa mpaka anachelea kulisha humo, jueni, hakika kila mfalme ana mpaka, na jueni kuwa hakika mwili kuna kinofu, kikitengemaa utatengemaa mwili wote, kikiharibika utaharibika mwili wote, jueni kuwa huo ni moyo." [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 2

وعن أنسٍ رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم وَجَدَ تَمْرَةً فِي الطَّرِيقِ ، فَقَالَ : (( لَوْلاَ أنِّي أخَافُ أنْ تَكُونَ مِنَ الصَّدَقَة لأَكَلْتُهَا )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwake Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliona tende njiani, akasema: "Lau kama mimi sikuhofia kuwa hii tende ni ya swadaqah ningeila." [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 3

وعن النَّواسِ بن سمعان رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( البِرُّ : حُسْنُ الخُلُقِ، وَالإِثْمُ : مَا حَاكَ فِي نَفْسِكَ ، وَكَرِهْتَ أنْ يَطَّلِعَ عَلَيْهِ النَّاسُ )) رواه مسلم.

Imepokewa kutoka kwa An-Nawwaas bin Sam'aan ya kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema: "Kutenda wema ni tabia nzuri, na kitendo kiovu ni chenye kukukera katika nafsi yako na ukachukia watu wakuone nacho." [Muslim]





Hadiyth – 4

وعن وَابِصَةَ بن مَعبدٍ رضي الله عنه ، قَالَ: أتَيْتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ: (( جئتَ تَسْألُ عَنِ البِرِّ ؟ )) قُلْتُ : نَعَمْ ، فَقَالَ : (( اسْتَفْتِ قَلْبَكَ ، البرُّ : مَا اطْمَأنَّت إِلَيْهِ النَّفسُ ، وَاطْمأنَّ إِلَيْهِ القَلْبُ ، وَالإثْمُ : مَا حَاكَ في النَّفْسِ ، وَتَرَدَّدَ فِي الصَّدْرِ ، وَإنْ أفْتَاكَ النَّاسُ وَأفْتُوكَ )) حديث حسن ، رواه أحمد والدَّارمِيُّ في مُسْنَدَيْهِمَا .

Imepokewa kutoka kwake Waabiswah bin Ma'bad (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba nilikuja kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), naye akaniuliza: "Je, umekuja kuuliza juu ya kutenda wema?" Nikamwambia: "Ndio." Akasema: "Ushauri moyo wako. Kutenda wema ni kufanya lenye kutuliza nafsi, na ukatulia moyo; na kitendo kiovu ni chenye kukera kwenye nafsi na kutaradadi kifuani hata kama wamekutolea fatwa watu (kuwa chafaa)." [Hadiyth Hasan, imepokewa katika Musnadi mbili: Ahmad bin Hambal na Ad-Daarimiyy]





Hadiyth – 5

وعن أَبي سِرْوَعَةَ عُقبَةَ بنِ الحارِثِ رضي الله عنه : أنَّهُ تَزَوَّجَ ابنَةً لأبي إهَابِ بن عزيزٍ ، فَأتَتْهُ امْرَأةٌ ، فَقَالَتْ : إنّي قَدْ أرضَعْتُ عُقْبَةَ وَالَّتِي قَدْ تَزَوَّجَ بِهَا . فَقَالَ لَهَا عُقْبَةُ : مَا أعْلَمُ أنَّك أرضَعْتِنِي وَلاَ أخْبَرْتِني ، فَرَكِبَ إِلَى رسول الله صلى الله عليه وسلم بِالمَدِينَةِ ، فَسَأَلَهُ : فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( كَيْفَ ؟ وَقَد قِيلَ )) فَفَارَقَهَا عُقْبَةُ وَنَكَحَتْ زَوْجاً غَيْرَهُ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abu Sirwa'ah 'Uqbah bin Al-Haarith (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba alimuoa bint wa Abu Wahaab bin 'Aziyz, akaja kwake mwanamke alliyemwambia: "Hakika mimi nimemnyesha 'Uqbah na mkewe." 'Uqbah akamwambia: "Sijui kama wewe umeninyonyesha wala hujanijulisha hilo." Akafunga safari kuelekea Madiyah kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na alipofika alimuuliza (kuhusu jambo hilo). Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia: "Vipi, na tayari ushaelezwa?" 'Uqbah alimuacha mkewe huyo na kuoa mwanamke mwengine." [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 6

وعن الحسن بن علي رضي الله عنهما ، قَالَ : حَفِظتُ من رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( دَعْ مَا يريبُكَ إِلَى ما لاَ يَرِيبُكَ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa Al-Hasan bin 'Ali (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa alisema: "Nimehifadhi kutoka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Acha lenye kukutia shaka kwa lisilokutia shaka." [At-Tirmidhiy, na akasema kuwa ni Hadiyth Hasan]





Hadiyth – 7

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : كَانَ لأبي بَكر الصديق رضي الله عنه غُلاَمٌ يُخْرِجُ لَهُ الخَرَاجَ ، وَكَانَ أَبُو بَكْرٍ يَأكُلُ مِنْ خَرَاجِهِ ، فَجَاءَ يَوْماً بِشَيءٍ ، فَأكَلَ مِنْهُ أَبُو بَكْرٍ ، فَقَالَ لَهُ الغُلامُ : تَدْرِي مَا هَذَا ؟ فَقَالَ أَبُو بكر : وَمَا هُوَ ؟ قَالَ : كُنْتُ تَكَهَّنْتُ لإنْسَانٍ في الجَاهِلِيَّةِ وَمَا أُحْسِنُ الكَهَانَةَ ، إِلاَّ أنّي خَدَعْتُهُ ، فَلَقِيَنِي ، فَأعْطَانِي لِذلِكَ ، هَذَا الَّذِي أكَلْتَ مِنْهُ ، فَأدْخَلَ أَبُو بَكْرٍ يَدَهُ فَقَاءَ كُلَّ شَيْءٍ فِي بَطْنِهِ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Abu Bakr As-Swiddiyq (Radhwiya Allaahu 'anhu)alikuwa na kijana aliyekuwa akimtolea mapato. Abu Bakr alikuwa akila humo. Akaja siku moja na kitu na Abu Bakr akala. Kijana Akamwambia: "Unajua nini hiki?" Akasema Abu Bakr: "Ni nini hicho?" Akasema: "Nilimfanyia uchawi mtu katika jahiliyyah (ujinga) na sikujua uchawi ila nilimhadaa. Alikutana nami na kunipa kitu hicho ambacho umekula." Abu Bakr alitia mkono wake kwenye mdomo na kutapika chote kilichokuwa ndani ya tumbo lake." [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 8

وعن نافِع : أن عُمَرَ بن الخَطّاب رضي الله عنه كَانَ فَرَضَ لِلمُهَاجِرينَ الأَوَّلِينَ أرْبَعَةَ الآفٍ وَفَرَضَ لابْنِهِ ثَلاَثَة آلافٍ وَخَمْسَمئَةٍ ، فَقيلَ لَهُ : هُوَ مِنَ المُهَاجِرينَ فَلِمَ نَقَصْتَهُ ؟ فَقَالَ : إنَّمَا هَاجَرَ بِهِ أبُوهُ . يقول : لَيْسَ هُوَ كَمَنْ هَاجَرَ بِنَفْسِهِ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Naafi' kwamba 'Umar bin Al-Khattaab (Radhwiya Allaahu 'anhu) alikuwa anawapatia Muhaajiriyn wa mwanzo elfu arobaini na akawa anampatia mtoto wake elfu tatu na mia tano. Akaambiwa: "Yeye pia ni miongoni mwa Muhaajiriyn kwa nini unampunguzia kiwango chake?" Akawaambia: "Hakika yeye alihama na babake, hivyo hawi sawa na yule aliyehama pake yake." [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 9

وعن عَطِيَّةَ بن عُروة السَّعْدِيِّ الصحابيِّ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( لاَ يَبْلُغُ الْعَبدُ أنْ يَكُونَ منَ المُتَّقِينَ حَتَّى يَدَعَ مَا لاَ بَأسَ بِهِ ، حَذَراً مِمَّا بِهِ بَأسٌ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa 'Atiyyah bin 'Urwah As-Sa'adiy amabaye ni Swahaaba (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakuna mja atakayefika daraja ya uchamngu mpaka aache yale mambo yasiyo na tatizo lolote kama tahadhari kwa yale yenye madhara." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

باب استحباب العزلة عند فساد الناس والزمان

069-Mlango Wa Kupendekeza Kujitenga Wakati wa Uharibifu na Ufisadi au Hofu ya Fitnah Katika Dini au Kujiingiza Katika Haramu na Shaka





Alhidaaya.com



قَالَ الله تَعَالَى:

فَفِرُّوا إِلَى اللَّـهِ ۖ إِنِّي لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ ﴿٥٠﴾

Basi kimbilieni kwa Allaah, hakika mimi kwenu ni mwonyaji bayana kutoka Kwake. [Adh-Dhaariyaat: 50]





Hadiyth – 1

وعن سعد بن أَبي وقاص رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( إنَّ الله يُحِبُّ الْعَبْدَ التَّقِيَّ الغَنِيّ الْخَفِيَّ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Sa'd bin Abu Waqqaas (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakika Allaah anampenda mja mchamngu mwenye utajiri wa nafsi na asiyejionesha." [Muslim]





Hadiyth – 2

وعن أَبي سعيد الخدري رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رَجُلٌ : أيُّ النَّاسِ أفْضَلُ يَا رسولَ الله ؟ قَالَ : (( مُؤْمِنٌ مُجَاهِدٌ بِنَفْسِهِ وَمَالِهِ في سَبيلِ اللهِ )) قَالَ : ثُمَّ مَنْ ؟ قَالَ : (( ثُمَّ رَجُلٌ مُعْتَزِلٌ فِي شِعْبٍ مِنَ الشِّعَابِ يَعْبُدُ رَبَّهُ )) . وفي رواية : (( يَتَّقِي اللهَ ، وَيَدَعُ النَّاسَ مِنْ شَرِّهِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Mtu alisema: "Ee Rasuli wa Allaah! Mtu gani bora zaidi?" Akasema: "Muumini anayepigana kwa nafsi yake na mali yake katika njia ya Allaah." Akasema: "Kisha ni nani?" Akasema: "Kisha mtu aliyejitenga katika bonde miongoni mwa mabonde akimuabudu Rabb wake." Katika riwaayah: "Anamcha Allaah na kuacha watu na shari yake (kutowaudhi)." [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 3

وعن أَبي سعيد الخدري رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( يُوشِكُ أنْ يَكُونَ خَيْرَ مَالِ المُسْلِمِ غَنَمٌ يَتَّبعُ بِهَا شَعَفَ الجِبَالِ ، وَمَواقعَ الْقَطْر يَفِرُّ بِدينِهِ مِنَ الفِتَنِ )) رواه البخاري .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wakati upo karibu ambapo mali bora ya Muislamu itakuwa ni mbuzi wengi ambao atakwenda nao juu ya jabali au sehemu ya mvua ili kuilinda Dini yake kutokana na fitna." [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 4

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَا بَعَثَ اللهُ نَبِيّاً إِلاَّ رَعَى الْغَنَمَ )) فَقَالَ أصْحَابُهُ : وأنْتَ ؟ قَالَ : (( نَعَمْ ، كُنْتُ أرْعَاهَا عَلَى قَرَارِيطَ لأَهْلِ مَكَّةَ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Allaah hakutuma Nabiy, ila Nabiy huyu alichunga mbuzi." Swahaabah wakauliza: "Hata wewe?" Akasema: "Ndio nilikuwa nikichunga kwa watu wa Makkah na nikilipwa Qaraarit (kipimo maalum cha dhahabu chenye wizani wa 1/24 ya dinari)." [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم ، أنَّه قَالَ : (( مِنْ خَيْرِ مَعَاشِ النَّاسِ لهم رَجُلٌ مُمْسِكٌ عِنَانَ فَرَسِهِ في سَبيلِ الله، يَطيرُ عَلَى مَتْنِهِ كُلَّمَا سَمِعَ هَيْعَةً أَوْ فَزعَةً ، طَارَ عَلَيْهِ يَبْتَغِي القَتْلَ ، أَوْ المَوْتَ مَظَانَّه ، أَوْ رَجُلٌ فِي غُنَيمَةٍ في رَأسِ شَعَفَةٍ مِنْ هذِهِ الشَّعَفِ ، أَوْ بَطنِ وَادٍ مِنْ هذِهِ الأَوْدِيَةِ ، يُقِيمُ الصَّلاَةَ ، وَيُؤتِي الزَّكَاةَ ، وَيَعْبُدُ رَبَّهُ حَتَّى يأتِيَهُ اليَقِينُ ، لَيْسَ مِنَ النَّاسِ إِلاَّ فِي خَيْرٍ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Maisha yaliyo bora miongoni mwa watu ni mtu kushika hatamu za farasi katika njia ya Allaah. Anampanda kwenye mgongo wake na kuruka nae (kwenda haraka) pindi tu anaposikia sauti ya vita (kuwa vipo tayari) au mfano wake wa fazaa. Anakimbilia sehemu hiyo akiwa tayari kupigana au kwa yule mtu anayejitenga na mbuzi wake wachanga juu ya mlima miongoni mwa hii milima au akawa anaishi kati ya moja ya mabonde. Na hapo anasimamisha Swalaah na kutoa Zakaah na kutekeleza 'Ibadah ya Rabb wake mpaka yatakapomfikia yeye umauti na wala haingilii maisha ya watu ila kwa kutaka kheri." [Muslim]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب فضل الاختلاط بالناس وحضور جُمَعِهم وجماعاتهم ،

ومشاهد الخير ، ومجالس الذكر معهم ، وعيادة مريضهم ، وحضور

جنائزهم ، ومواساة محتاجهم ، وإرشاد جاهلهم ، وغير ذلك من

مصالحهم لمن قدر عَلَى الأمر بالمعروف والنهي عن المنكر ، وقمع

نفسه عن الإيذاء وصبر عَلَى الأذى

070-Mlango Wa Fadhila za Kutangamana na Watu, Kuhudhuria Mikusanyiko yao, Kushuhudia Kheri, Kushiriki Katika Vikao Vya Dhikri Pamoja nao, Kutembelea Wagonjwa, Kuhudhuria Jeneza Zao, Kukidhi Haja za Masikini Miongoni Mwao, Kuwaongoza Wajinga Wao na Mengineyo Katika Maslahi yao na Mwenye Kuweza au Kuamrisha Mema na Kukataza Mabaya na Kutoa Katika Nafsi Yake Uchafu na Kusubiri Maudhi na Shida.





Alhidaaya.com





اعْلم أنَّ الاختلاط بالنَّاسِ عَلَى الوجهِ الَّذِي ذَكَرْتُهُ هُوَ المختارُ الَّذِي كَانَ عَلَيْهِ رسول الله صلى الله عليه وسلم وسائر الأنبياء صلواتُ اللهِ وسلامه عَلَيْهِمْ ، وكذلك الخُلفاءُ الرَّاشدون ، ومن بعدَهُم مِنَ الصَّحَابَةِ وَالتَّابِعِينَ ، ومن بَعدَهُم من عُلَماءِ المُسلمين وأَخْيَارِهم ، وَهُوَ مَذْهَبُ أكثَرِ التَّابِعينَ وَمَنْ بَعدَهُمْ ، وبه قَالَ الشافعيُّ وأحمدُ وأكثَرُ الفقهاءِ رضي اللهُ عنهم أجمعين. قَالَ اللهُ تَعَالَى: ( وَتَعَاوَنُوا عَلَى البِرِّ وَالتَّقْوَى ) [ المائدة : 20 ] والآيات في معنى مَا ذكرته كثيرة معلومة .

Jua ya kwamba kutangamana na watu kwa njia niliyoitaja ndio yenye kupendeza. Ndio njia iliyokuwa ikifuatwa na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Manabii wote na hivyo hivyo Makhalifa waongofu na waliokuja baada yao miongoni mwa Swahaabah na Taabi'iyna. Na pia hiyo ilikuwa ndio sifa ya waliokuja baada yao miongoni mwa wanavyuoni Waislaamu na wabora wao. Na hii ndiyo madhehebu ya Taabi'iyna wengi na wala waliokuja baada yao. Na kwayo ndio amesema Ash-Shaafi'iy, na Ahmad na Mafakih wengi. Amesema Allaah Ta'aalaa: "Na shirikianeni katika wema na taqwa." [Al-Maaidah: 2]. Na kuna ayah nyingi katika mlango huu.
 
UJUMBE WA LEO:

Na imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hapana hasad (wivu) ila kwa watu wawili: Mtu ambaye amepatiwa Quraan na Allaah, naye akawa amesimama imara nayo kwa kuisoma na kuitekeleza maamrisho yake mchana na usiku; na mwengine ni yule aliyepatiwa mali na Allaah, naye akawa anaitoa (swadaqah) mchana na usiku." [Al-Bukhaariy na Muslim
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب التواضع وخفض الجناح للمؤمنين

071-Mlango Wa Unyenyekevu na Kuinamisha Bawa Waumini



Alhidaaya.com



قَالَ الله تَعَالَى:

وَاخْفِضْ جَنَاحَكَ لِمَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿٢١٥﴾

Na inamisha ubawa wako kwa anayekufuata miongoni mwa Waumini. [Ash-Shu'araa: 215]



يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا مَن يَرْتَدَّ مِنكُمْ عَن دِينِهِ فَسَوْفَ يَأْتِي اللَّـهُ بِقَوْمٍ يُحِبُّهُمْ وَيُحِبُّونَهُ أَذِلَّةٍ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ أَعِزَّةٍ عَلَى الْكَافِرِينَ ﴿٥٤﴾

Enyi walioamini! Yeyote atakayeritadi miongoni mwenu kutoka Dini yake, basi Allaah Ataleta watu (badala yao) Atakaowapenda nao watampenda; wanyenyekevu kwa Waumini, washupavu juu ya makafiri.[Al-Maaidah: 54]



يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّا خَلَقْنَاكُم مِّن ذَكَرٍ وَأُنثَىٰ وَجَعَلْنَاكُمْ شُعُوبًا وَقَبَائِلَ لِتَعَارَفُوا ۚ إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّـهِ أَتْقَاكُمْ ۚ ﴿١٣﴾

Enyi watu! Hakika Sisi Tumekuumbeni kutokana namwanamme na mwanamke, na Tukakujaalieni mataifa na makabila ili mtambuane. Hakika aliye na hadhi zaidi miongoni mwenu mbele ya Allaah ni mwenye taqwa zaidi kati yenu. [Al-Hujuraat: 13]



فَلَا تُزَكُّوا أَنفُسَكُمْ ۖ هُوَ أَعْلَمُ بِمَنِ اتَّقَىٰ ﴿٣٢﴾

Basi msizitakase nafsi zenu. Yeye Anamjua zaidi aliyekuwa na taqwa. [An-Najm: 32]



وَنَادَىٰ أَصْحَابُ الْأَعْرَافِ رِجَالًا يَعْرِفُونَهُم بِسِيمَاهُمْ قَالُوا مَا أَغْنَىٰ عَنكُمْ جَمْعُكُمْ وَمَا كُنتُمْ تَسْتَكْبِرُونَ ﴿٤٨﴾ أَهَـٰؤُلَاءِ الَّذِينَ أَقْسَمْتُمْ لَا يَنَالُهُمُ اللَّـهُ بِرَحْمَةٍ ۚ ادْخُلُوا الْجَنَّةَ لَا خَوْفٌ عَلَيْكُمْ وَلَا أَنتُمْ تَحْزَنُونَ ﴿٤٩﴾

Na watu wa Al-A’raaf watawaita watu (wa motoni) wanaowatambua kwa alama zao, watasema: Hakukufaeni kujumuika kwenu (duniani) na vile mlivyokuwa mkitakabari. Je, hawa si wale ambao mliapa kwamba Allaah hatowafikishia kwa rahmah yoyote ile? (Leo wanaambiwa) Ingieni Jannah! Hakuna khofu juu yenu na wala nyinyi hamtohuzunika. [Al-A'raaf: 48-49]





Hadiyth – 1

وعن عِيَاضِ بنِ حمارٍ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ الله أوْحَى إِلَيَّ أنْ تَوَاضَعُوا حَتَّى لاَ يَفْخَرَ أحَدٌ عَلَى أحَدٍ ، وَلاَ يَبْغِي أحَدٌ عَلَى أحَدٍ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Iyaadh bin Himaar (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah amenifunulia Wahyi kuwa nyenyekeeni hadi yoyote asijifakhiri mtu juu ya mwingine, wala yoyote asimfanye uadui mwingine." [Muslim]





Hadiyth – 2

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( مَا نَقَصَتْ صَدَقَةٌ مِنْ مَالٍ،وَمَا زادَ اللهُ عَبْداً بعَفْوٍ إِلاَّ عِزّاً، وَمَا تَوَاضَعَ أحَدٌ للهِ إِلاَّ رَفَعَهُ اللهُ (عزّ وجلّ) )) رواه مسلم.

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Swadaqah haipunguzi mali; na Allaah anamuongezea utukufu mwenye kusamehe. Na hanyenyekei yoyote kwa ajili ya Allaah ('Azza wa Jalla) isipokuwa Allaah humnyanyua." [Muslim]





Hadiyth – 3

وعن أنس رضي الله عنه : أنَّهُ مَرَّ عَلَى صبيَانٍ ، فَسَلَّمَ عَلَيْهِمْ ، وقال : كَانَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم يفعله . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa alipita mbele ya watoto na akawasalimia. Na hapo akasema: "Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) alikuwa akifanya hivyo." [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 4

وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : إن كَانَتِ الأَمَةُ مِنْ إمَاءِ المَدينَةِ لَتَأْخُذُ بِيَدِ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، فَتَنْطَلِقُ بِهِ حَيْثُ شَاءتْ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa alisema: "Kijakazi miongoni mwa vijakazi wa Madiynah alikuwa anaweza kuushika mkono wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na akawa anakwenda naye popote anapotaka ili amweleze shida yake." [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 5

وعن الأَسْوَدِ بن يَزيدَ ، قَالَ : سُئِلَتْ عائشةُ رضي الله عنها مَا كَانَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم يَصْنَعُ فِي بَيْتِهِ ؟ قالت : كَانَ يَكُون في مِهْنَةِ أهْلِهِ – يعني : خِدمَة أهلِه – فإذا حَضَرَتِ الصَّلاَةُ ، خَرَجَ إِلَى الصَّلاَةِ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Al-Aswad bin Yaziyd ambaye amesema, 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) aliulizwa: "Je, Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akifanya nini nyumbani?" Alisema: :Alikuwa akiwahudumikia na kuwasaidia watu wake wa nyumbani, lakini wakatika wa Swalaah unapofika alikuwa akitoka kwenda kuswali." [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 6

وعن أَبي رِفَاعَةَ تَميم بن أُسَيْدٍ رضي الله عنه ، قَالَ : انْتَهَيْتُ إِلَى رَسولِ الله صلى الله عليه وسلم وَهُوَ يخطب ، فقلت : يَا رسول الله ، رَجُلٌ غَريبٌ جَاءَ يَسْألُ عن دِينهِ لا يَدْرِي مَا دِينُهُ ؟ فَأقْبَلَ عَليَّ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، وتَرَكَ خُطْبَتَهُ حَتَّى انْتَهَى إلَيَّ ، فَأُتِيَ بِكُرْسيٍّ ، فَقَعَدَ عَلَيْهِ ، وَجَعَلَ يُعَلِّمُنِي مِمَّا عَلَّمَهُ اللهُ ، ثُمَّ أَتَى خُطْبَتَهُ فَأتَمَّ آخِرَهَا . رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Rifaa'ah Tamim bin Usayd (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: "Nilifika kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiwa anakhutubu, nami nikamuuliza: 'Ee Rasuli wa Allaah! Mtu mgeni amekuja kuuliza kuhusu Dini yake kwani yeye hajui chochote kuhusu Dini yake?' Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alinikabili na akaja kwangu. Aliletewa kiti, akakikalia. Akawa ananifundisha aliyofundishwa na Allaah. Kisha alijia hutuba yake akaitimiza." [Muslim]





Hadiyth – 7

وعن أنس رضي الله عنه : أن رسول الله صلى الله عليه وسلم كَانَ إِذَا أكَلَ طَعَاماً ، لَعِقَ أصَابِعَهُ الثَّلاَثَ . قَالَ : وقال : (( إِذَا سَقَطَتْ لُقْمَةُ أَحَدِكُمْ فَلْيُمِط عنها الأَذى ، وليَأكُلْها وَلاَ يَدَعْها لِلشَّيْطان )) وأمرَ أن تُسلَتَ القَصْعَةُ ، قَالَ : (( فإنَّكُمْ لاَ تَدْرُونَ في أيِّ طَعَامِكُمُ البَرَكَة )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akilamba vidole vyake vitatu baada ya kumaliza kula. Amesema Anas kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Tonge la mmoja wenu likianguka basi aondoe uchafu ulioingia na kisha alile na wala asimwachie shetani." Na pia ameamuru kufuta kabisa sahani (aliyolia mmoja wenu) na akasema: "Hakika nyinyi hamujui ni chakula chenu kipi kina baraka." [Muslim]





Hadiyth – 8

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَا بَعَثَ الله نَبِيّاً إِلاَّ رَعَى الغَنَمَ )) قَالَ أصْحَابُهُ : وَأنْتَ ؟ فَقَالَ : (( نَعَمْ ، كُنْتُ أرْعَاهَا عَلَى قَرَارِيطَ لأَهْلِ مَكَّةَ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Allaah hakutuma Nabiy, ila Nabiy huyo alichunga mbuzi." Wakasema Swahaaba zake: "Hata wewe?" Akasema: "Ndio, nilikuwa nikichunga kwa watu wa Makkah na nikilipwa Qaraarit." [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 9

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لَوْ دُعِيتُ إِلَى كُراعٍ أَوْ ذِرَاعٍ لأَجَبْتُ ، ولو أُهْدِيَ إِلَيَّ ذراعٌ أَوْ كُراعٌ لَقَبِلْتُ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Lau ningealikwa kwa chakula cha muundi au bega ningeitikia na lau ningepatiwa zawadi ya muundi au bega ningekubali (ningepokea)." [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 10

وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : كَانَتْ ناقةُ رسول الله صلى الله عليه وسلم العضْبَاءُ لاَ تُسْبَقُ ، أَوْ لاَ تَكَادُ تُسْبَقُ ، فَجَاءَ أعْرَابيٌّ عَلَى قَعودٍ لَهُ ، فَسَبَقَهَا ، فَشَقَّ ذَلِكَ عَلَى الْمُسْلِمِينَ حَتَّى عَرَفَهُ ، فَقَالَ : (( حَقٌّ عَلَى اللهِ أنْ لاَ يَرْتَفِعَ شَيْءٌ مِنَ الدُّنْيَا إِلاَّ وَضَعَهُ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Ngamia wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiitwa 'Adhbaa', naye hakuwa akimruhusu ngamia yeyote amshinde. Wakati mmoja alikuja bedui aliyekuwa na ngamia mchanga aliyempita ngamia wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Jambo hilo lilikuwa gumu sana kwa Waislamu mpaka Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akatambua hilo. Akasema: "Ni haki kwa Allaah kukutojikweza chochote duniani ila atakishusha." [Al-Bukhaariy]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب تحريم الكبر والإعجاب

072-Mlango Wa Kuharamishwa Kibri na Kujiona



Alhidaaya.com



قَالَ الله تَعَالَى:

تِلْكَ الدَّارُ الْآخِرَةُ نَجْعَلُهَا لِلَّذِينَ لَا يُرِيدُونَ عُلُوًّا فِي الْأَرْضِ وَلَا فَسَادًا ۚ وَالْعَاقِبَةُ لِلْمُتَّقِينَ ﴿٨٣﴾

Hiyo ni nyumba ya Aakhirah, Tunaijaalia kwa wale wasiotaka kujitukuza katika ardhi na wala ufisadi. Na hatima njema ni kwa wenye taqwa. [Al-Qaswasw: 83]



وَلَا تَمْشِ فِي الْأَرْضِ مَرَحًا ۖ ﴿٣٧﴾

Na wala usitembee katika ardhi kwa majivuno. [Al-Israa: 37]



وَلَا تُصَعِّرْ خَدَّكَ لِلنَّاسِ وَلَا تَمْشِ فِي الْأَرْضِ مَرَحًا ۖ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ كُلَّ مُخْتَالٍ فَخُورٍ ﴿١٨﴾

Na wala usiwageuzie watu uso wako kwa kiburi, na wala usitembee katika ardhi kwa maringo, hakika Allaah Hampendi kila mwenye kujivuna mwenye kujifakharisha. [Luqmaan: 18]



إِنَّ قَارُونَ كَانَ مِن قَوْمِ مُوسَىٰ فَبَغَىٰ عَلَيْهِمْ ۖ وَآتَيْنَاهُ مِنَ الْكُنُوزِ مَا إِنَّ مَفَاتِحَهُ لَتَنُوءُ بِالْعُصْبَةِ أُولِي الْقُوَّةِ إِذْ قَالَ لَهُ قَوْمُهُ لَا تَفْرَحْ ۖ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ الْفَرِحِينَ ﴿٧٦﴾

Hakika Qaaruwn alikuwa miongoni mwa kaumu ya Muwsaa, lakini aliwafanyia uonevu kwa kutakabari. Na Tulimpa katika hazina ambazo funguo zake zinalemea kundi la watu wenye nguvu (kuzibeba). Walipomwambia watu wake: Usifurahi kwa kujigamba. Hakika Allaah Hapendi wanaofurahi kwa kujigamba. [Al-Qaswasw: 76]

إِلَى قَوْله تَعَالَى:

فَخَسَفْنَا بِهِ وَبِدَارِهِ الْأَرْضَ ﴿٨١﴾

Basi Tukamdidimiza yeye na nyumba yake ardhini [Al-Qaswasw: 81]





Hadiyth – 1

وعن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لاَ يَدْخُلُ الجَنَّةَ مَنْ كَانَ في قَلْبِهِ مِثْقَالُ ذَرَّة مِنْ كِبْرٍ ! )) فَقَالَ رَجُلٌ : إنَّ الرَّجُلَ يُحِبُّ أنْ يَكُونَ ثَوْبُهُ حَسَناً ، ونَعْلُهُ حَسَنَةً ؟ قَالَ : (( إنَّ اللهَ جَمِيلٌ يُحِبُّ الجَمَالَ ، الكِبْرُ : بَطَرُ الحَقِّ وَغَمْطُ النَّاسِ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Abdillah bin Mas'uuwd (Radhwiya Alaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaah 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hataingia Peponi yeyote ambae katika moyo wake kuna chembe ya kiburi." Akasema mtu mmoja: "Hakika mtu anapenda kuwa na nguo nzuri na viatu vizuri?" Akasema: "Hakika Allaah ni mzuri na anapenda vizuri. Kiburi ni kukataa haki kwa kujiona na kuyarudisha kwa mwenyewe na kuwaona watu wengine kuwa duni." [Muslim]





Hadiyth – 2

وعن سلمة بن الأكوع رضي الله عنه : أنّ رَجُلاً أكَلَ عِنْدَ رسول الله صلى الله عليه وسلم بشمالِهِ ، فَقَالَ : (( كُلْ بيَمِينِكَ )) قَالَ : لاَ أسْتَطِيعُ ! قَالَ : (( لا اسْتَطَعْتَ )) مَا مَنَعَهُ إِلاَّ الكِبْرُ . قَالَ : فما رفَعها إِلَى فِيهِ . رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Salamah bin Al-Akwa' (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: "Kuwa mtu mmoja alikula mbele ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa mkono wa kushoto. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akasema: 'Kula kwa wa kulia.' Akasema: 'Siwezi.' Akasema: 'Hutaweza.' Hakuna kilichomzuia kufuata agizo la Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) isipokuwa kibri, hivyo hakuweza tena kuunyanyua mdomoni mwake." [Muslim]





Hadiyth – 3

وعن حارثة بن وهْبٍ رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( ألا أُخْبِرُكُمْ بأهْلِ النَّار : كلُّ عُتُلٍ جَوّاظٍ مُسْتَكْبرٍ )) متفقٌ عَلَيْهِ ، وتقدم شرحه في بابِ ضعفةِ المسلمين .

Imepokewa kutoka kwa Haarithah bin Wahb (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Je, niwaeleze nyinyi kuhusu watu wa Peponi? Kila dhaifu na mwenye kudhoofishwa. Lau ataapa kwa Allaah, Allaah atamtekelezea. Je, siwapashi habari juu ya watu wa Motoni? Ni kila mkavu, safihi na mwenye kiburi." [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 4

وعن أَبي سعيد الخدري رضي الله عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( احْتَجّتِ الجَنَّةُ وَالنَّارُ ، فَقَالَت النَّارُ : فيَّ الْجَبَّارُونَ والمُتَكَبِّرُونَ . وقالتِ الجَنَّةُ : فيَّ ضُعفاءُ الناس ومساكينُهُم ، فقضى اللهُ بَينهُما : إنكِ الجنّةُ رَحْمَتِي أرْحَمُ بِك مَنْ أشَاءُ ، وَإنَّكِ النَّارُ عَذَابِي أُعَذِّبُ بِكِ مَنْ أشَاءُ ، وَلِكِلَيْكُمَا عَلَيَّ مِلْؤُهَا )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Pepo na Moto zilibishana. Moto ukasema: 'Ndani yangu watakaa majabari na wenye kiburi.' Na Pepo ikasema: 'Ndani yangu watakaa madhaifu miongoni mwa watu na masikini wao.' Allaah akaamua baina yao: 'Hakika yako wewe, Pepo ni Rehema Yangu ninamrehemu kwako nimtakaye. Na hakika yako wewe, Moto ni adhabu Yangu, ninawaadhibu kwako nimtakaye, Na ni juu Yangu kuwajaza nyote wawili." [Muslim]





Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لاَ يَنْظُرُ اللهُ يَوْمَ القِيَامَةِ إِلَى مَنْ جَرَّ إزَارَهُ بَطَراً )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Allaah hamwangalii siku ya Qiyaamah mwenye kuburuza kikoi chake kwa kiburi." [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 6

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( ثَلاَثَةٌ لاَ يُكَلِّمُهُمُ اللهُ يَوْمَ القِيَامَة ، وَلاَ يُزَكِّيهِمْ ، وَلاَ يَنْظُرُ إلَيْهِمْ ، وَلَهُمْ عَذَابٌ ألِيمٌ : شَيْخٌ زَانٍ ، وَمَلِكٌ كَذَّابٌ ، وَعَائِلٌ مُسْتَكْبِرٌ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Watu watatu Allaah hatazungumza nao Siku ya Qiyaamah wala hatawatakasa wala hatawaangalia: Mzee mzinifu, na mfalme mwongo na fakiri mwenye kiburi." [Muslim]





Hadiyth – 7

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( قَالَ الله (عزّ وجلّ) : العِزُّ إزَاري ، والكبرياءُ رِدائي ، فَمَنْ يُنَازِعُنِي في وَاحِدٍ منهما فَقَد عَذَّبْتُهُ )) رواه مسلم .


Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Amesema Allaah ('Azza wa Jalla): Utukufu ni kikoi Changu, na kiburi ni shuka Yangu, na atakayeshindana Nami katika moja wapo ya viwili hivi Nitamuadhibu." [Muslim]



Hadiyth – 8

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( بَيْنَمَا رَجُلٌ يَمشِي في حُلَّةٍ تُعْجِبُهُ نَفْسُهُ ، مُرَجِّلٌ رَأسَهُ ، يَخْتَالُ فِي مَشْيَتهِ ، إِذْ خَسَفَ اللهُ بِهِ ، فَهُوَ يَتَجَلْجَلُ في الأَرضِ إِلَى يَوْمِ القِيَامَةِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mtu akiwa anatembea katika pambo akijiona nafsini mwake. Nywele zake zimechanwa, anajivuna katika kutembe kwake. Allaah akamdidimiza ardhini, Yeye anadidimia ardhini hadi Siku ya Qiyaamah.' [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 9

وعن سَلَمةَ بنِ الأكْوَعِ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( لاَ يَزَالُ الرَّجُلُ يَذْهَبُ بِنَفْسِهِ حَتَّى يُكْتَبَ في الجبَّارِين ، فَيُصيبَهُ مَا أصَابَهُمْ )) رواه الترمذي ، وقال: (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Salamah bin Al-Akwa' (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anaendelea mtu kujitenga na watu na kuwa ni mwenye kiburi mpaka anaandikwa pamoja na wenye kiburi na hivyo kupatiwa adhabu sawa na wale wenye kiburi." [At-Tirmidhiy, na akasema hii ni Hadiyth Hasan]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب حسن الخلق

073-Mlango Wa Tabia Njema



Alhidaaya.com



قَالَ الله تَعَالَى:

وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ﴿٤﴾

Na hakika wewe uko juu ya kiwango adhimu cha tabia njema. [Al-Qalam: 4]



وَالْكَاظِمِينَ الْغَيْظَ وَالْعَافِينَ عَنِ النَّاسِ ۗ ﴿١٣٤﴾

Na wanazuia ghadhabu, na wenye kusamehe watu. [Aal-'Imraan: 134]





Hadiyth – 1

وعن أنس رضي الله عنه ، قال : كَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم أحْسَنَ النَّاس خُلُقاً . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa ni mwenye tabia nzuri kuliko watu wote." [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 2

وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : مَا مَسِسْتُ دِيبَاجاً وَلاَ حَرِيراً ألْيَنَ مِنْ كَفِّ رسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، وَلاَ شَمَمْتُ رَائِحَةً قَطُّ أطْيَبَ مِنْ رَائِحَةِ رسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، وَلَقَدْ خدمتُ رسول اللهِ صلى الله عليه وسلم عَشْرَ سنين ، فما قَالَ لي قَطُّ : أُفٍّ، وَلاَ قَالَ لِشَيءٍ فَعَلْتُهُ : لِمَ فَعَلْتَه ؟ وَلاَ لشَيءٍ لَمْ أفعله : ألاَ فَعَلْتَ كَذا ؟ متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Sijashika dibaji wala hariri laini zaidi kuliko kiganja cha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), wala sijasikia harufu nzuri kuliko harufu ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), hakika nilimtumikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) miaka kumi, hakuniambia kabisa: 'Ah.' Na wala hakuniambia kwa kitu nilichofanya kwa nini umefanya?, Wala kwa kitu ambacho sikufanya, lau ungefanya hivi?" [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 3

وعن الصعب بن جَثَّامَةَ رضي الله عنه ، قَالَ : أهديتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم حِمَاراً وَحْشِيّاً ، فَرَدَّهُ عَلَيَّ ، فَلَمَّا رأى مَا في وجهي ، قَالَ : (( إنّا لَمْ نَرُدَّهُ عَلَيْكَ إِلاَّ لأنّا حُرُمٌ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Swa'b bin Jathaamah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Nilimpatia hadiya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ya punda, naye akanirudishia. Alipoona alama ya sikitiko katika uso wangu, alisema: "Sijarudisha zawadi yako ila ni kwa sababu ya kuwa tumeshahirimia." [AL-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 4

وعن النَّوَاس بنِ سمعان رضي الله عنه ، قَالَ : سألتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم عن البِرِّ وَالإثم ، فَقَالَ : (( البِرُّ : حُسنُ الخُلقِ ، والإثمُ : مَا حاك في صدرِك ، وكَرِهْتَ أن يَطَّلِعَ عَلَيْهِ النَّاسُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa An-Nawwaas bin sam'aan (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nilimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu wema na dhambi akasema: "Wema ni tabia nzuri, na dhambi ni iliokera nafsini mwako na ukachukia watu kuiona." [Muslim]





Hadiyth – 5

عن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما ، قَالَ : لَمْ يكن رسولُ الله صلى الله عليه وسلم فَاحِشاً وَلاَ مُتَفَحِّشاً ، وكان يَقُولُ : (( إنَّ مِنْ خِيَارِكُمْ أحْسَنَكُمْ أخْلاَقاً )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Abdillah bin 'Amru bin Al-'aas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: "Hakuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni mwenye kuzungumza maneno machafu wala kuyasikiliza." Na alikuwa akisema: "Hakika aliye bora miongoni mwenu ni yule mwenye tabia nzuri." [Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy na Ahmad].





Hadiyth – 6

وعن أَبي الدرداءِ رضي الله عنه : أن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَا مِنْ شَيْءٍ أثْقَلُ في مِيزَانِ العبدِ المُؤْمِنِ يَوْمَ القِيَامَةِ مِنْ حُسْنِ الخُلُقِ ، وَإنَّ الله يُبْغِضُ الفَاحِشَ البَذِيَّ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Dardaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakuna kitu chochote kilicho kizito zaidi katika mizani ya Muumini Siku ya Qiyaamah kuliko tabia nzuri. Na hakika Allaah anamchukia mwenye kutoa maneno machafu na ya kishenzi." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh].





Hadiyth – 7

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : سُئِلَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم عَنْ أكثرِ مَا يُدْخِلُ النَّاسَ الْجَنَّةَ ؟ قَالَ : (( تَقْوَى اللهِ وَحُسنُ الخُلُقِ )) ، وَسُئِلَ عَنْ أكْثَرِ مَا يُدْخِلُ النَّاسَ النَّارَ، فَقَالَ : (( الفَمُ وَالفَرْجُ )) رواه الترمذي، وقال : (( حديث حسن صحيح )).

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Aliulizwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa mambo ambayo yatawaingiza watu wengi Peponi?" Akasema: "Uchaji wa Allaah na tabia nzuri." Na akaulizwa kuhusu mambo ambayo yatawaingiza wengi Motoni. Akasema: "Ulimi na sehemu za siri." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh].





Hadiyth – 8

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قال: قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم: (( أكْمَلُ المُؤمنينَ إيمَاناً أحسَنُهُمْ خُلُقاً، وَخِيَارُكُمْ خِيَارُكُمْ لِنِسَائِهِمْ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Muumini mkamilifu wa Iymaani ni mzuri wao wa tabia, na wabora wenu ni wabora wenu kwa wake zao." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]





Hadiyth – 9

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( إنَّ المُؤْمِنَ لَيُدْرِكُ بحُسْنِ خُلُقِه دَرَجَةَ الصَّائِمِ القَائِمِ )) رواه أَبُو داود .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakika Muumini anafikia kwa tabia nzuri daraja ya mfungaji mwenye kusimama usiku." [Abu Daawuud]





Hadiyth – 10

وعن أَبي أُمَامَة الباهِليِّ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( أنَا زَعِيمٌ ببَيتٍ في ربَض الجَنَّةِ لِمَنْ تَرَكَ المِرَاءَ ، وَإنْ كَانَ مُحِقّاً ، وَبِبَيْتٍ في وَسَطِ الجَنَّةِ لِمَنْ تَرَكَ الكَذِبَ ، وَإنْ كَانَ مَازِحاً ، وَبِبَيْتٍ في أعلَى الجَنَّةِ لِمَنْ حَسُنَ خُلُقُهُ )) . حديث صحيح ، رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .

Imepokewa kutoka kwa Abu Umamah Al-Baahiliy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mimi ni mdhamini wa nyumba ya chini Peponi kwa mwenye kuacha kujionesha japo ana haki. Na nyumba ya katikati ya Peponi, kwa mwenye kuacha uongo, japokuwa kwa kufanya mzaha. Na kwa nyumba iliyo sehemu ya juu kabisa Peponi kwa mwenye tabia nzuri." [Hadiyth Swahiyh, Abu Daawuud kwa Isnaad Swahiyh]





Hadiyth – 11

وعن جابر رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إنَّ مِنْ أحَبِّكُمْ إليَّ ، وَأقْرَبِكُمْ مِنِّي مَجْلِساً يَوْمَ القِيَامَةِ ، أحَاسِنَكُم أخْلاَقاً ، وَإنَّ أبْغَضَكُمْ إلَيَّ وَأبْعَدَكُمْ مِنِّي يَوْمَ القِيَامَةِ ، الثَّرْثَارُونَ وَالمُتَشَدِّقُونَ وَالمُتَفَيْهقُونَ )) قالوا : يَا رسول الله ، قَدْ عَلِمْنَا (( الثَّرْثَارُونَ وَالمُتَشَدِّقُونَ )) ، فمَا المُتَفَيْهقُونَ ؟ قَالَ : (( المُتَكَبِّرُونَ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika wapendwa wenu zaidi kwangu, na wakaribu wenu zaidi wa kukaa nami Siku Ya Qiyaamah, ni wazuri wenu zaidi wa tabia. Na wabughudhiwa wenu zaidi wenu zaidi kwangu Siku ya Qiyaamah ni wale ma-tharthar (wenye kuzungumza sana) na mutashaddiquun (wanaorefusha mazungumzo yao na wanazungumza kwa kujaza midomo yao kwa majisifu) na mutafayhiquun." Wakasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Hakika tunawajua ma-tharthar na mutashaddiquun lakini hawa mutafayhiquun ni kina nani?" Akasema: "Wenya kiburi." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب الحلم والأناة والرفق

074-Mlango Wa Upole, Umakini na Utaratibu



Alhidaaya.com



قَالَ الله تَعَالَى:

وَالْكَاظِمِينَ الْغَيْظَ وَالْعَافِينَ عَنِ النَّاسِ ۗ وَاللَّـهُ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ ﴿١٣٤﴾

Na wanazuia ghadhabu, na wenye kusamehe watu. Na Allaah Anapenda wafanyao ihsaan. [Aal-'Imraan: 136]



خُذِ الْعَفْوَ وَأْمُرْ بِالْعُرْفِ وَأَعْرِضْ عَنِ الْجَاهِلِينَ ﴿١٩٩﴾

Shikamana na usamehevu, na amrisha mema na jiepushe na majahili. [Al-A;raaf: 199]



وَلَا تَسْتَوِي الْحَسَنَةُ وَلَا السَّيِّئَةُ ۚ ادْفَعْ بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ فَإِذَا الَّذِي بَيْنَكَ وَبَيْنَهُ عَدَاوَةٌ كَأَنَّهُ وَلِيٌّ حَمِيمٌ﴿٣٤﴾

Na wala haulingani sawa wema na uovu. Lipiza (uovu) kwa ambalo ni zuri zaidi; tahamaki yule ambaye baina yako na baina yake kuna uadui, atakuwa kama ni rafiki mwandani.



وَمَا يُلَقَّاهَا إِلَّا الَّذِينَ صَبَرُوا وَمَا يُلَقَّاهَا إِلَّا ذُو حَظٍّ عَظِيمٍ﴿٣٥﴾

Na hapewi hayo isipokuwa wale waliovuta subira, na hapewi hayo isipokuwa mwenye fungu adhimu. [Fusw-swilat: 34 - 35]



وَلَمَن صَبَرَ وَغَفَرَ إِنَّ ذَٰلِكَ لَمِنْ عَزْمِ الْأُمُورِ﴿٤٣﴾

Na atakayevuta subira na akasamehe, hakika hilo bila shaka ni katika mambo ya kuazimiwa. [Ash-Shuwraa: 43]





Hadiyth – 1

وعن ابن عباس رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم لأَشَجِّ عَبْدِ القَيْسِ : (( إنَّ فيكَ خَصْلَتَيْنِ يُحِبُّهُمَا اللهُ : الْحِلْمُ وَالأنَاةُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) ameseam: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia Ashajj 'Abdil-Qays: "Hakika wewe una sifa mbili anazozipenda Allaah: Uvumilivu na uthabiti na kuacha haraka." [Muslim].





Hadiyth – 2

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ اللهَ رفيقٌ يُحِبُّ الرِّفْقَ فِي الأَمْرِ كُلِّه )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah ni Mpole na anapenda upole katika mambo yote." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]





Hadiyth – 3

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إنَّ اللهَ رَفِيقٌ يُحِبُّ الرِّفقَ ، وَيُعْطي عَلَى الرِّفق ، مَا لاَ يُعْطِي عَلَى العُنْفِ ، وَمَا لاَ يُعْطِي عَلَى مَا سِوَاهُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah ni Mpole, hivyo anapenda upole, na anatoa kwa upole asichotoa kwa ukali na wala kwa chengine chochote mbali na upole na ulaini." [Muslim]





Hadiyth – 4

وعن عائشة رضي الله عنها : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إنَّ الرِّفْقَ لاَ يَكُونُ في شَيْءٍ إِلاَّ زَانَهُ ، وَلاَ يُنْزَعُ مِنْ شَيْءٍ إِلاَّ شَانَهُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika upole unafanya kitu kiwe kizuri, na pindi upole unapoondolewa katika kitu chochote isipokuwa uzuri wake huondoka." [Muslim]





Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : بَال أعْرَابيٌّ في المسجدِ ، فَقَامَ النَّاسُ إِلَيْهِ لِيَقَعُوا فِيهِ ، فَقَالَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم : (( دَعُوهُ وَأرِيقُوا عَلَى بَوْلِهِ سَجْلاً مِنْ مَاءٍ ، أَوْ ذَنُوباً مِنْ مَاءٍ ، فَإنَّمَا بُعِثْتُمْ مُيَسِّرِينَ وَلَم تُبْعَثُوا مُعَسِّرِينَ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Bedui mmoja alikojoa Msikitini, watu wakamsimamia ili kumpiga, Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Muacheni na mwagieni ndoo ya maji juu ya mkojo wake. Hakika nyinyi mmetumwa kurahisisha, wala hamkutumwa kufanya uzito." [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 6

وعن أنس رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( يَسِّرُوا وَلاَ تُعَسِّرُوا ، وَبَشِّرُوا وَلاَ تُنَفِّرُوا )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Rahisisheni wala msiyafanye uzito, na toeni bishara wala msifukuze." [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 7

وعن جريرِ بنِ عبدِ اللهِ رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقولُ : (( مَنْ يُحْرَمِ الرِفْقَ ، يُحْرَمِ الخَيْرَ كلَّهُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Jariyr bin 'Abdillah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Anayeharimishiwa (kukosa) upole amekosa kheri zote." [Muslim].





Hadiyth – 8

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رَجُلاً قَالَ للنبيِّ صلى الله عليه وسلم : أوْصِني . قَالَ : (( لاَ تَغْضَبْ )) ، فَرَدَّدَ مِرَاراً ، قَالَ : (( لاَ تَغْضَبْ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba mtu mmoja alimwambia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Niusie." Akasema: "Usighadhibike." Akakariri mara nyingi. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akasema: "Usighadhibike." [Al-Bukhaariy].





Hadiyth – 9

وعن أَبي يعلى شَدَّاد بن أوسٍ رضي الله عنه ، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إنَّ الله كَتَبَ الإحْسَانَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ فَإذَا قَتَلْتُم فَأحْسِنُوا القِتْلَة ، وَإِذَا ذَبَحْتُمْ فَأحْسِنُوا الذِّبْحَةَ ، وَليُحِدَّ أَحَدُكُمْ شَفْرَتَه ، وَلْيُرِح ذَبِيحَتَهُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Ya'laa Shaddaad bin Aws (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah Ameamrisha Ihsaan (wema) kwa kila kitu. Kwa hivyo, mkiuwa uweni vizuri, na mkichinja chinjeni vizuri. Kila mmoja wenu akitie makali kisu chake, na akipunguzie uchungu kichinjwa chake." [Muslim].





Hadiyth – 10

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : مَا خُيِّرَ رسول الله صلى الله عليه وسلم بَيْنَ أمْرَيْنِ قَطُّ إِلاَّ أَخَذَ أيْسَرَهُمَا ، مَا لَمْ يَكُنْ إثماً ، فَإنْ كَانَ إثماً ، كَانَ أبْعَدَ النَّاسِ مِنْهُ . وَمَا انْتَقَمَ رسول الله صلى الله عليه وسلم لِنَفْسِهِ في شَيْءٍ قَطُّ ، إِلاَّ أن تُنْتَهَكَ حُرْمَةُ الله ، فَيَنْتَقِمَ للهِ تَعَالَى . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakupewa fursa ya kuchagua baina ya mambo mawili katu isipokuwa alichadua jepesi lao, madamu si dhambi, ikiwa ni dhambi huwa mbali nalo zaidi. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakulipiza kisasi kwa nafsi yake katika jambo lolote isipokuwa mipaka ya Allaah inapokiukwa, kwa hilo hulipiza kisasi kwa ajili ya Allaah Ta'aalaa." [Al-Bukhaariy na Muslim].







Hadiyth – 11

وعن ابن مسعود رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( ألا أخْبِرُكُمْ بِمَنْ يَحْرُمُ عَلَى النَّار ؟ أَوْ بِمَنْ تَحْرُمُ عَلَيْهِ النَّار ؟ تَحْرُمُ عَلَى كُلِّ قَرِيبٍ ، هَيّنٍ ، لَيِّنٍ ، سَهْلٍ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Niwajulishe nyinyi ambaye moto ni haramu kwake?. ni haramu kwa kila wa karibu, mwepesi, laini, mwepesi." [At-Tirmidhiy, na akasema ni hadiyth Hasan]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب العفو والإعراض عن الجاهلين

075-Mlango Wa Kusamehe na Kupuuza Wajinga



Alhidaaya.com



قَالَ الله تَعَالَى:

خُذِ الْعَفْوَ وَأْمُرْ بِالْعُرْفِ وَأَعْرِضْ عَنِ الْجَاهِلِينَ ﴿١٩٩﴾

Shikamana na usamehevu, na amrisha mema na jiepushe na majahili. [Al-A'raaf: 199]

فَاصْفَحِ الصَّفْحَ الْجَمِيلَ﴿٨٥﴾

Basi samehe msamaha mzuri. [Al-Hijr: 85]



وَلْيَعْفُوا وَلْيَصْفَحُوا ۗ أَلَا تُحِبُّونَ أَن يَغْفِرَ اللَّـهُ لَكُمْ ۗ ﴿٢٢﴾

Na wasamehe na waachilie mbali. Je, hampendi Allaah Akughufurieni? [An-Nuwr: 22]

وَالْعَافِينَ عَنِ النَّاسِ ۗ وَاللَّـهُ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ ﴿١٣٤﴾

Na wenye kusamehe watu. Na Allaah Anapenda wafanyao ihsaan. [Aal-'Imraan: 134]

وَلَمَن صَبَرَ وَغَفَرَ إِنَّ ذَٰلِكَ لَمِنْ عَزْمِ الْأُمُورِ﴿٤٣﴾

Na atakayevuta subira na akasamehe, hakika hilo bila shaka ni katika mambo ya kuazimiwa. [Ash-Shuwraa: 43]





Hadiyth – 1

وعن عائشة رضي الله عنها : أنها قالت للنبي صلى الله عليه وسلم : هَلْ أتَى عَلَيْكَ يَوْمٌ كَانَ أشَدَّ مِنْ يَوْمِ أُحُدٍ ؟ قَالَ : (( لَقَدْ لَقِيتُ مِنْ قَوْمِكِ ، وَكَانَ أشَدُّ مَا لَقيتُ مِنْهُمْ يَوْمَ الْعَقَبَةِ ، إذْ عَرَضْتُ نَفْسِي عَلَى ابْنِ عَبْدِ يَالِيْلَ بْنِ عَبْدِ كُلاَلٍ ، فَلَمْ يُجِبْني إِلَى مَا أرَدْتُ ، فَانْطَلَقْتُ وَأنا مَهْمُومٌ عَلَى وَجْهِي ، فَلَمْ أسْتَفِقْ إِلاَّ وأنَا بِقَرْنِ الثَّعَالِبِ ، فَرَفَعْتُ رَأْسِي ، وَإِذَا أنَا بِسَحَابَةٍ قَدْ أظَلَّتْنِي ، فَنَظَرْتُ فَإذَا فِيهَا جِبريلُ (عليه السلام) ، فَنَادَاني ، فَقَالَ : إنَّ الله تَعَالَى قَدْ سَمِعَ قَوْلَ قَوْمِكَ لَكَ ، وَمَا رَدُّوا عَلَيْكَ، وَقَد بَعَثَ إلَيْكَ مَلَكَ الجِبَالِ لِتَأْمُرَهُ بمَا شِئْتَ فِيهِمْ . فَنَادَانِي مَلَكُ الجِبَالِ ، فَسَلَّمَ عَلَيَّ ، ثُمَّ قَالَ : يَا مُحَمَّدُ إنَّ اللهَ قَدْ سَمِع قَوْلَ قَوْمِكَ لَكَ ، وَأنا مَلَكُ الجِبال ، وَقَدْ بَعَثَنِي رَبِّي إلَيْكَ لِتَأْمُرَنِي بِأَمْرِكَ ، فَمَا شِئْتَ ، إنْ شئْتَ أطْبَقْتُ عَلَيْهِمُ الأَخْشَبَيْنِ )) . فَقَالَ النبي صلى الله عليه وسلم : (( بَلْ أرْجُو أنْ يُخْرِجَ اللهُ مِنْ أصْلاَبِهِمْ مَنْ يَعْبُدُ اللهَ وَحْدَهُ لاَ يُشْرِكُ بِهِ شَيْئاً )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa alimuuliza Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Je umefikwa na siku ngumu zaidi kuliko siku ngumu zaidi kuliko siku ya Uhud?" Akasema: "Hakika nimekutana na watu wako, na ilikuwa ngumu zaidi kutoka kwao kuliko siku ya 'Aqabah, siku hiyo nilijipeleka kwa Ibn 'Adbil Yaaliil bin 'Abdi Kulaal, hakunijibu nililolitaka. Niliondoka nami nikiwa mzito juu ya uso wangu. Nilifarijika nilipofika Qarn Ath-Tha'alib, niliponyanyua kichwa changu na kuona kulikuwa na kiwingu kilichokuwa kimenifunika. Nilipotazama nikamuona Jibriyl ('Alayhis Salaam), aliita akisema: "Hakika Allaah Ta'aalaa amesikia kauli ya kaumu yako kwako, na walivyokujibu, Allaah Amekutumia Malaika wa jabali aliniita akanisalimia, kisha akasema: 'Ee Muhammad! Hakika Allaah amesikia kauli ya watu wako, na mimi ni Malaika wa majabali. Na hakika amenituma Mola wangu kwako uaiamuru amri yako; Utakacho, ukitaka nitawasaga na haya majabali mawili.' Akasemas Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): 'Bali napenda Allaah atoe katika migongo yao watakaomuabudu Allaah Peke Yake hawamshirikishi Yenye na chochote." [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 2

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : مَا ضَرَبَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم شَيْئاً قَطُّ بِيَدِهِ ، وَلاَ امْرَأةً وَلاَ خَادِماً ، إِلاَّ أنْ يُجَاهِدَ فِي سَبيلِ اللهِ ، وَمَا نِيلَ مِنْهُ شَيْءٌ قَطُّ فَيَنْتَقِمَ مِنْ صَاحِبِهِ ، إِلاَّ أن يُنْتَهَكَ شَيْءٌ مِنْ مَحَارِمِ اللهِ تَعَالَى ، فَيَنْتَقِمُ للهِ تَعَالَى . رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakupiga kitu chochote kwa mkono wake na wala hakumpiga mwanamke wala mjakazi isipokuwa anapopigana jihadi katika njia ya Allaah. Na hakulipiza kisasi kwa lolote alilofanyiwa yeye isipokuwa inapovukwa mipaka ya Allaah Ta'aalaa, hapo ndio alikuwa akilipiza kisasi." [Muslim]





Hadiyth – 3

وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : كُنْتُ أمشي مَعَ رسول الله صلى الله عليه وسلم وَعَلَيْهِ بُرْدٌ نَجْرَانيٌّ غَلِيظُ الحَاشِيَةِ ، فأدْرَكَهُ أعْرَابِيٌّ فَجَبذَهُ بِرِدَائِهِ جَبْذَةً شَديدةً ، فَنَظَرْتُ إِلَى صَفْحَةِ عَاتِقِ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، وَقَدْ أثَّرَتْ بِهَا حَاشِيَةُ الرِّدَاءِ مِنْ شِدَّةِ جَبْذَتِهِ ، ثُمَّ قَالَ : يَا مُحَمَّدُ ، مُر لِي مِنْ مَالِ اللهِ الَّذِي عِنْدَكَ . فَالتَفَتَ إِلَيْهِ ، فَضَحِكَ ثُمَّ أَمَرَ لَهُ بِعَطَاءٍ . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nilikuwa nikitembea pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiwa amevaa shuka la Najran lililokuwa na ugumu pembezoni mwake. Akamkuta njiani Mbedui amabaye alimshika na kumvuta kwa shuka lake hilo kwa nguvu. Nilipomwangalia Nabiy (Swalla allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika shingo yake akiwa ameathirika kwa ule ugumu wa pembezoni wa shuka lake kwa ile nguvu kubwa ya kuvutwa. Kisha alisema: 'Ee Muhammad! Toa amri nipatwe katika ile mali ya Allaah uliyokuwa nayo.' Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwangalia na kucheka, kisha akaamrisha apatiwe sehemu katika mali hiyo." [Al-Bukhaariy na Muslim].





Hadiyth – 4

وعن ابن مسعود رضي الله عنه ، قَالَ : كأني أنظر إِلَى رسول الله صلى الله عليه وسلم يَحْكِي نَبِيّاً مِنَ الأنبياءِ ، صَلَوَاتُ اللهِ وَسَلامُه عَلَيْهِمْ ، ضَرَبَهُ قَوْمُهُ فَأدْمَوْهُ ، وَهُوَ يَمْسَحُ الدَّمَ عَنْ وَجْهِهِ ، ويقول : (( اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِقَوْمِي ؛ فَإنَّهُمْ لاَ يَعْلَمُونَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Kana kwamba ninamwangalia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akimzungumzia Nabiy miongoni mwa Manabiy ambaye alipigwa na watu wake mpaka akawa anatoka damu; alipokuwa anaifuta hiyo damu usoni alikuwa anasema: "Ee Mola wangu wasamehe watu wangu kwani wao hawajui." [Al-Bukhaariy na Muslim].





Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لَيْسَ الشَّديدُ بِالصُّرَعَةِ ، إنَّمَا الشَّدِيدُ الَّذِي يَمْلِكُ نَفْسَهُ عِنْدَ الْغَضَبِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye nguvu ni yule amabye anamiliki nafsi yake anaposhikwa na ghadhabu." [Al-Bukhaariy na Muslim].
 
Baadhi ya post za zamani

BINADAMU ANAPONZWA NA MATUMAINI YA MUDA MREFU

Kila mwanadamu huwa na matumaini kwamba hakika yeye bado ana mda mrefu wa kuishi duniani,na kwamba uzima wake na afya yake nzuri ndio viashiria ambavyo humuaminisha kwamba yeye bado yupo yupo kwanza.

Ukitaka uamini hili ninalosema ebu msikie huyu mtu ikiwemo mimi na wewe mara tunapo sikia habari ya mtu fulani amekufa mara moja huanza kuuliza, vipi alikuwa anaumwa? Au amekufa kwa maradhi gani?

Hii yote inadhihirisha kwamba tunaamini wote wanao kufa basi lazima wawe wanaumwa kwanza au lazima wawe hawako vizuri kiafya hii ndio mitazamo yetu kwa wengi wetu.

Matokeo yake kwa sisi ambao alihamdulillah tumejaaliwa afya njema kwa mda huu huwa na matumaini makubwa sana ya kuishi mda mrefu, na matokeo yake tunashindwa kukumbuka kwamba ipo siku nasi tutakuwa marehemu watarajiwa na tutakutana na Mola wetu.

Matumaini ya kuishi mda mrefu hutufanya tuweze kuwadhulumu watu haki zao huenda labda kutokana na vyeo vyetu au connection zetu katika jamii, kutotenda haki kwa wanadamu wenzetu, kujilimbikizia mali zisizo halali ili tu tunufaishe matumbo yetu, kuchukua rushwa na mambo kama hayo.

Mtu mwerevu ni yule ambaye siku zote hukumbuka kuwa yeye ni mavumbi na hakika mavumbini atarejea, hivyo hana budi kujitengezea mazingira mazuri ya huko anakokwenda baada ya kifo chake,hakika huko atahojiwa kwa kila tendo alilolifanya hapa duniani.

Mwanadamu anarekodiwa kwa kila tendo na jambo analolifanya ima liwe kubwa au dogo,yote hayo yako katika kumbukumbu zake, mwanadamu huyu anakuwa salama tu pale anapokuwa amelala au pale anapokuwa hajazungumza chochote, au hajafanya tendo lolote, kwani Mwenyezi Mungu ametusamehe kwa yale ambayo yapo katika mawazo maadamu tu hatujayafanya.

Mfano naweza kuwaza kwamba nataka nikazini na fulani,kwakuwaza huku sitakuhukumiwa ila nikilitekeleza wazo langu kwa kuenda kuzini hapo sasa nitachukuliwa kumbukumbu zangu kwa matumizi ya baade huko akhera.

Mwanadamu atambue kuwa kila mtu ana malaika wawili ambao anaambatana nao katika maisha yake yote, mmoja yupo kuliana kwake huyu huandika mambo mema na yule wa kushoto huandika matendo mabaya ya mja huyu, ima umezungumza chochote au kuandika chochote au kufanya chochote basi kumbuka kumbukumbu zinahifadhiwa kwa matumizi ya baadae.

Acha kuwa na matumaini ya mda mrefu kwani hakika mwanadamu hujui mda wala saa ya kuondoka kwake,hakikisha unayatarisha makazi yako ya mbinguni mapema kabisa.
 
Baadhi ya post za zamani...

SIKU ZOTE HESABU BARAKA ZAKO

Kuna mwamba ambaye alipotea baharini akiwa safarini kwa mda wa mwezi mmoja,alipoulizwa ni kitu gani ambacho ulikihitaji sana wakati wa changamoto yako ya kupotea,alijibu ni maji na chakula

Naam,wakati mwingine huwezi jua baraka zako mpaka pale zinapokupotea,ndo unajua khe kumbe maji nayo baraka kubwa au chakula nacho kumbe ni baraka kubwa.

Tulio wengi wetu hatuhesabu baraka zetu ambazo tumejaaliwa na muumba wetu,huwa tunaangalia sana mambo ambayo huwa hatuna na kutamani tuwe nayo,na hii hupelekea kutozithamini baraka ambazo tunazo siku zote

Mfano mtu anapopata shida ya kupumua na kutumia gas ili aweze kusavaivi,hapo ndipo atakapo ona eeh kumbe kupumua nako ni baraka kubwa. Lakini akiwa mzima anaona kupumua kama jambo rahisi hivi na la mchezo mchezo lakini subiri shida hiyo impate ndio atajua hakika hiyo ni baraka kubwa mno.

Siku zote za maisha yetu tuzikumbuke baraka mbali mbali ambazo tumejaaliwa na mola wetu na tushukuru kwa kila jambo,usihuzunike kwa kukosa jambo fulani kwani tambua nawe una jambo ambalo wengine wanatamani wawe nalo.

Always remember to count baraka zako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…