Ukitaka kujua data zina anguka hapa .Mguse Malecela utamjua ES na Prof akiguswa utamjua Mtanzania .Yangu macho tuendelee
Kwi kwi kwi.....
Mwenzako Kibaki "amekuwa rais" kwa mara nyingine tena akiwa na miaka 76 sembuse 68 ya Mwandosya? vipi Jongo la zimbabwe mpaka leo anapeta tu na miaka 82!
Duh!!! na wewe umetoa mpya . Kwa hiyo wewe kwako JK na mizunguko yake ni sawa kwako ?
Lakini wakuu hebu tuweni wakweli na nafsi zetu, wewe ungekuwa katika nafasi ya Bernard Membe ungesema nini kuhusu safari za bosi wako?
Eeeeh bwana wee, wewe kiboko haswaaaa! yaani hakuna jibu kama hilo maanake kutokana na uvumbuzi wote wa Vasco Da Gama na misafara yake, Portugal ndio bado nchi maskini kuliko zote Europe!Nisingesema rais wetu kuitwa Vasco Da Gama ni sifa kubwa
Kwi kwi kwi.....
Mwenzako Kibaki "amekuwa rais" kwa mara nyingine tena akiwa na miaka 76 sembuse 68 ya Mwandosya? vipi Jongo la zimbabwe mpaka leo anapeta tu na miaka 82!
Mwandosya akitaka kuwa rais na akaamua kufight na kufanya ufisadi kidogo apate mapesa kibao anaweza kuwa rais Afrika bila kujali umri wake.
Maombi yetu kuwa Kina Mkumbo watakuwa wamefikisha miaka 40 sijui 35 ya kisheria ya kuwaruhusu wagombee uraisi. Otherwise, nchi inakatisha tamaa hiyo we acha tu.
MWK, Comrade Robert Mugabe, KCB ana miaka 83.
LOL
So far this story is unverified, did Membe say so? Who reported that? Source pleeeeeease!
Mkuu Pundit,
Heshima mbele, source ya hii topic ni gazeti la:-
.Mtanzania
.Toleo # 4271, ISSN 0856-5678
.Jumamosi, Januari 19, 2008, (Page # 1&2).
Now my point kuiweka hapa ilikuwa kuwafahamisha wananchi wote hapa JF, kuwa tunaposema viongozi wetu wanaishi nasi hapa huwa tunasema ukweli, maana jina hilo la Vasco da Gama, originally alipewa hapa JF, sasa kufikia waziri wetu wa nje wa Jamhuri, kulisema wazi tena hadaharani ni clear kuwa hata mkulu analijua, na believe me kwamba ni lazima limepunguza safari kama kumi zisizokuwa na sababu ambazo angezifanya bila ya sisi JF kuwepo na kumpa hilo jina,
Kwa hiyo kwa wale wanaofikiria hapa JF ni mahali pa kubuzi buzi na ku-hang out tu labda wanahitaji ku-think twice, maana huu ni ushahidi tosha kuwa tuko nao hapa, sasa tuwekeni vitu vya kweli, kuhusu aliyoyasema, kwa kweli inatia uchungu badala ya kusikitisha, I mean a State foreign minister? Yaani kazi ya huyu mkuuu si sawa na iliyokuwa kazi ya Kissinger? Can you imagine Kissinger kusema huo utumbo? Yaaani ile vurugu yote ya kuwachafua wagombea urais kina Salim, it was all about this kind of thinking? Halafu nasikia na yeye anataka urais pia?
Mungu Ibariki Tanzania!
Kuna nini CCM kinachowabadilisha watu? Huyu muungwana wanadai alivyokuwa Canada alikuwa muadilifu alafu unakumbuka ile issue ya Hassy Kitine, few years later anakuja na huu utumbo. Tanzania tuna safari ndefu
Kumbe kuchafuana kwenye kampeni za uchaguzi, na kuongoza ni vitu viwili tofauti?
Ndiyo kwanza anaendelea kupasha misuli moto tayari kwa kuingia kwenye kinyang'anyiro cha urais hapo mwezi March. Huyu Mzee nadhani anataka kufia madarakani. Hivi hao wana ZANU PF hawana watu wengine wenye uwezo wa kuongoza nchi zaidi ya Mugabe? Huu ufisadi ni balaa kubwa sana, najua anachoogopa ni kwamba je akiachia ngazi mrithi wake ataendelea kulinda ufisadi wake?
Lakini wakuu hebu tuweni wakweli na nafsi zetu, wewe ungekuwa katika nafasi ya Bernard Membe ungesema nini kuhusu safari za bosi wako?
Naona nilipunguza mwaka mmoja ili kumfanya aonekane kijana.... ila kweli huwezi kuamini the guy anataka tena kugombea kwa miaka mingine mitano!
Mkuu FMES, heshima mbele mkuu, hata mi nilipoona ametaja ilo jina al-maaruf hapa barazani, nikaamini maneno waliyosema kuwa hata Muungwana huwa anapitia hapa mkuu, so baraza hili limekuwa na impact kuliko hata baadi ya magazeti, na hili nishalisema(ga) hapa Mkuu!
Na kuhusu kuchafuana na kuongoza, mkuu unadhani kuna hata mmoja anayetaka kutuongoza mkuu! ni kuwa literally hatuna viongozi! ama wangekuwepo, sasa hivi Tanzania ingekuwa paradiso..tuna maliasili, na kila kitu!
In fact tuna kesi ya kumjibu Muumba, as kwa nini mkuu, hadi leo watu ni masikini kwenye nchi iliyojaa maziwa na asali!
Uongozi mkuu! uongozi!