Rais Kikwete na safari za nje

Rais Kikwete na safari za nje

..kwa hiyo anataka kutuambia hizo pesa tulizopewa na US za millenium challenge ni kwa sababu ya safari alizofanya,kweli nimeamini huyu jamaa kalewa cheo na anatuona wote vilaza,si bora angekaa kimya tuu kuliko kuja explaination ya kipumbavu kama hii.
 
Halafu watu watasema huyu anafaa kuwa President wa baadae.MMh?
Membe kama una akili na kweli Foreign Minister basi utakuwa unaelewa ya Kwamba Safari nyingi alizio fanya Mbeki zilikuwa za Usuluhishi na za Mambo ya Kiuchumi alialikwa ili kuwakilisha Africa basing on the fact that SA uchumi wao ni mkubwa hivyo wanaweza kuinfluence certain decision huku Africa na wanapokutana na Big Power. Otherwise unaweza ku-list hizo Safari zake za kwenda kuomba Investment? Mfano wa safari alizo alikwa ni Kama ule Mkutano wa G8 ujerumani? au Huo Mkutano wa Ureno na other economic Forum. Sio kwenda NASDAQ.
 
Waziri Membe, leo ametetea safari za rais Kikwete, nje ya nchi akisema zina umuhimu na manufaa makubwa sana kwa taifa letu. Akizungumza na waandishi wa habari katika hoteli ya Neptune, Zanzibar leo, alisema kuwa wale wanaomlaumu rais laiti wangejua faida ya hizo safari wasingesema sana na kumlaumu sana rais bila sababu za msingi.

Wamefikia hadi hatua ya kumuita Vasco da Gama, hii ni heshima kubwa sana, kwani huko Ureno kuna majumba mpaka mitaa yenye hilo jina, na mimi Membe ningeitwa hivyo ningefurahi sana, alisema waziri Membe.

Mwaka jana Rais Kikwete, alisafiri mara 17 nje ya nchi kulinganisha na Mbeki wa Afrika Kusini, aliyesafiri mara 21. Bila ya kupata rais wa kuhangaika, nchi haiwezi kuendelea. Alikwenda US kutafuta na kupewa dola 698 millioni na karibuni mtaona matunda yake. Wengine mnasema eti akienda huko Us haonani hata na rais wa huko, sio lazima amuone rais Bush, akienda huko. Anapoenda huko nje, huwa anaenda kuhemea, kutatua migogoro, kimsingi huwa anposafiri huwa ni kwa sababu ya jambo zito sana na sio kutaliii kama wapinzani wengi wanavyosema.

Wuuuuui!!!!!!!!

Matokeo ya kuwa na viongozi vilaza. Yaani kuwa na rais anayekwenda nje kuombaomba ndiyo mafanikio. Je anataka kusema kuwa Kikwete anashindana na Mbeki kwenda nje?
 
Mmmmh kazi tunayo.Huyo nae ni WAZIRI.

Sasa mbona hakusema kuwa na uchumi wa Africa Kusini ni sawasawa na wa Tanzania.Kazi tunayo
 
Huyu jamaa alikuwa serious kwenda kufanya research na kuja kulinganisha safari za Mbeki na Kikwete?
MAwaaziri wetu wangekuwa na huu moyo wa kujituma kwenye mambo ya maana na maendeleo tungekuwa mbali sana sasa hivi. PRIORITY ZA VIONGOZI WETU NI ZERO
 
1. Dola 698m mbona kuna nchi nyingi tu hupata hii pesa ya MC tangu mda mrefu??? Hii ni sera ya Marekani kusaidia nchi maskini asafiri JK US au laa!! Msumbiji wamepata tena pesa nyingi relative to their population ukiangalia na Tz- what is so special with Tanzania? Membe aache Kuwadanyanya Watz!

2. What business deals signed by JK during his 17 trips? Yaani alienda nje kulilia misaada wakati ndani akina Balali wanapora 133 bn? Kwa nini asikae home akaziba kapu linalovuja???
Hii syndome ya misaada inaturudisha nyuma.. yaani we are so proud kuwa tumepata msaada mkubwa.. ni aibu???

3. Kibaki hajasafiri sana 2007- licha ya matatizo end of year- je uchumi wa Kenya haukufanya vizuri kuliko wa Tanzania?? Yet budget ya Kenya haitegemei wafadhili- pesa ije au isije wao ni poa tu!

Membe his arguements are so weak!!!!
 
nadhani kumlinganisha Rais wa SA na wa Tanzania pia ni sawa na kulinganisha ndimu na mapapai.. si amlinganishe JK na Museveni, Kagame, Kibaki, na hawa majirani zetu... Hivi Karume alisafiri mara ngapi nje ya nchi.
 
For anybody who understand the history of plunder and pillage pioneered by Vasco Da Gama, for a Tanzanian to aspire to carry that name, a foreign affairs minister no less, it is an outrage.

I don't understand why such insensitive comments are left unchecked, where is the press? This guy should be crucified in the press just for this comment,Kikwete's travels aside.I would devote an entire column exposing how empty he needs to be upstairs to have said that.
 
Halafu watu watasema huyu anafaa kuwa President wa baadae.MMh?
Membe kama una akili na kweli Foreign Minister basi utakuwa unaelewa ya Kwamba Safari nyingi alizio fanya Mbeki zilikuwa za Usuluhishi na za Mambo ya Kiuchumi alialikwa ili kuwakilisha Africa basing on the fact that SA uchumi wao ni mkubwa hivyo wanaweza kuinfluence certain decision huku Africa na wanapokutana na Big Power. Otherwise unaweza ku-list hizo Safari zake za kwenda kuomba Investment? Mfano wa safari alizo alikwa ni Kama ule Mkutano wa G8 ujerumani? au Huo Mkutano wa Ureno na other economic Forum. Sio kwenda NASDAQ.

Umesahau ile ya kwenda kwenye onyesho la Boys II Men, kupitia Madrid kwenye uwanja wa Real Madrid(Safari ya kuialika timu hii iliishia wapi?)etc
 
I am trying to google this story for a source verification to no avail.

Mzee ES, anybody, source please so we can do the needful.
 
Utani pembeni, nyingi ya safari hizi zingeweza kufanywa na Waziri wa Mambo ya Nje au Mabalozi wetu walio kwenye nchi husika. Kama kuna mikakati na mipango mizuri, itajiuza tu, hauhitaji mtu kusafiri kwenda ughaibuni kuipigia debe. Ni wakati sasa Rais ajikite katika masuala yanayohusu uchumi na kero za wananchi.
 
I am trying to google this story for a source verification to no avail.

Mzee ES, anybody, source please so we can do the needful.

Jaribu ku google "Mbeki and foreign travels" nimeona several Mbeki Travels if those are what you are interested in.
 
Uchumi wa SA siyo tegemezi na nchi yenyewe si omba omba, wasafiripo wanasafiri kwa midege yao mikubwa na gharama zao wenyewe.
Sisi Bajeti ya nchi ina kifungu cha msaada wa wahisani lakini Rais wetu Kiguu na njia kana kwamba alilelewa kwa supu ya usafiri(makanyagio) wa kuku wa kienyeji.
Mbeki hasafiri kwenda kuomba fedha anasafiri kwenda kutanua msuri wa uchumi wa South Africa.
Huyu Fala pamoja na kuishi kwake Marekani muda mrefu na kukata shule akili yake bado ni finyu, kibaya zaidi anatamani sifa ambazo ni matusi kwa mila za Kiafrika. Kuitwa Vasco Da gama siyo sifa labda kama wewe utaifa wako ni wa Ureno, nje ya hapo Vasco ni Jambazi mkubwa.
Membe kibantu ni mapembe, kama mapembe ya ng'ombe. Inawezekana huyu jamaa akili yake ni sawa na pembe za mbuzi ndo maana anaona sifa kuitwa Jambazi Vasco.
 
Kwa average ya siku 5 kwa trip kwa hizo trip 17 ni total of 85 days out of the country (I am sure ni zaidi ya 5 maana kuna ile alikuja states nadhani for some 3 gd wks. Sasa huyu "Rahisi" anayekuwa nje ya nchi robo nzima ya mwaka na nchi ikiendelea kumasikinika inaingia akilini kweli? Membe angekuwa smart atengeneze jedwali lenye trip, gharama zilizotumika, faida tuliyopata au tutakayopata. Nadhani kwa hilo asingekuwa hata na haja ya kutoa hotuba.
 
KWELI TUNA WAZIRI WA MAMBO YA NJE MZURI!!! Anafanya mpaka research za Rais wengine wamefanya nini, naomba mawaziri wengine muige mfano huu!
 
Huyu jamaa alikuwa serious kwenda kufanya research na kuja kulinganisha safari za Mbeki na Kikwete?
MAwaaziri wetu wangekuwa na huu moyo wa kujituma kwenye mambo ya maana na maendeleo tungekuwa mbali sana sasa hivi. PRIORITY ZA VIONGOZI WETU NI ZERO

FD,

sisi wenyewe wananchi ndio tuliona deal kujadili safari za Rais, sasa jamaa anawajibu wananchi wake, nayo hamtaki!

Jamii yetu ya Kitanzania ina matatizo sasa, yenyewe haina priority...sasa what is safari 17 za nje kwa Rais!!!

Simply hatuendelei kwanza kwa sababu ili nchi iiendelee inahitaji.

1. Watu
2. Ardhi
3. Uongozi bora
4. Siasa safi...


Tatizo ni kwamba yote yanaanza kuharibiwa na Watu... hatuna watu Tanzania... (Watu sio) idadi tu, tunahitaji watu walioelimka...ambao ni wacheche mno kwa sasa...

Ndani ya watu walioelimika,,, utabata viongozi bora... na ndani ya viongozi bora watatengeneza siasa safi!!!

Sasa badala ya kuvalia njuga mambo mengine ati mumeona la safari tu... well tumelaaniwa!!!
 
Ili nchi iendelee inahitaji
Watu na Ardhi tu.

Siasa safi na uongozi bora ni Derived quantities zitokanazo na watu.

Ardhi na Watu ni Fundamental Quantities ambazo ndo msingi wa maendeleo.

Derived quantinties za Ardhi ni Misitu, maji, hewa nk kwa nini nazo zisijumrishwe kwenye hiyo list?

Ili tuendelee tunahitaji watu na Ardhi tu.

Kwamba ili wawe watu ni lazima waelimike hiyo si statement ya kweli.

Watu ni watu wana shule hawana bado ni watu.

Ni kweli Fundamental quantity ya watu ndo yenye matatizo na si kweli kwamba tatizo ni elimu.
Tatizo ni Vision.
Elimu tulio nayo watanzania wengi inatosha kutupa maendeleo, ila wengi tumekosa Vision kwenye dulu za maendeleo.

Vision ni kujenga na kuiona taswira ya kijacho baadaye na uwezo wa kukitafsiri leo katika lugha nyepesi ili wengine pia waone uonacho.
 
So far this story is unverified, did Membe say so? Who reported that? Source pleeeeeease!
 
Back
Top Bottom