Rais Kikwete na safari za nje

Rais Kikwete na safari za nje

Mzee ES,

Vipi mkuu mbona unataka kutuua wenzako? Nimecheka hii mpaka mbavu zinauma.

Looh! kweli serikali ya JK ina watu, maana hata mwanangu wa miaka 10 si ajabu angepata sababu kubwa zaidi ya kumtetea boss wake kuliko huyu jamaa.

Hivi mnaomjua Membe, uwezo wake ukoje? Inaelekea ni mbabaishaji mno, maana hii ya leo ni babu kubwa!

Mungu niokoe niache kucheka maana hii ya Membe kali!
 
Nimefurahi kuona hata waziri nafikiri hata kikwete mwenyewe anajua kuwa ni Vasco da Gama. Ingawa kama walivyo vilaza hawakujiuliza undani na maana ya neno hilo. Kwa rais kuitwa hivyo sio jambo la kushangilia. Kama waziri anatamka hadharani kuwa ni heshima kubwa kuitwa hivyo ina maana hata rais kalikubali jina hilo. sasa kama analishangilia hivyo that means neno kujitegemea ni NDOTO ya mwenda wazimu. kwani membe kasema Rais anaenda kuhemea!!! kwa mbwembwe waziri anasema Rais kaenda kuhemea!! ameleta pesa!! mtaona matunda ya safari. Ni mawazo ya ujima. ni mawazo finyu sana. Ina maana strategy za serikali ni kuombaomba. Vasco da Gama bin Matonya. Kwa mtaji huo si halali kumfukuza matonya Dar es salaam kwa ajili ya kuomba msaada. Maana serikali ya kikwete ni serikali ombaomba. tena wanajisifia. I DONT BELIEVE THIS! is a ashame kuendekeza umatonya. je hao watoa misaada wakikataa?? je masharti gani wanatoa au ni freeeeeee!! Eee Mungu iokeoe Tanzania.

Anathubutu kulinganisha safari za Mbeki wa South Africa. je Uchumi wa RSA ni sawa na Uchumi wa Tanzania? stupid comparison.mwisho watajilinganisha na USA!!
 
Uchumi wa SA siyo tegemezi na nchi yenyewe si omba omba, wasafiripo wanasafiri kwa midege yao mikubwa na gharama zao wenyewe.
Sisi Bajeti ya nchi ina kifungu cha msaada wa wahisani lakini Rais wetu Kiguu na njia kana kwamba alilelewa kwa supu ya usafiri(makanyagio) wa kuku wa kienyeji.
Mbeki hasafiri kwenda kuomba fedha anasafiri kwenda kutanua msuri wa uchumi wa South Africa.
Huyu Fala pamoja na kuishi kwake Marekani muda mrefu na kukata shule akili yake bado ni finyu, kibaya zaidi anatamani sifa ambazo ni matusi kwa mila za Kiafrika. Kuitwa Vasco Da gama siyo sifa labda kama wewe utaifa wako ni wa Ureno, nje ya hapo Vasco ni Jambazi mkubwa.
Membe kibantu ni mapembe, kama mapembe ya ng'ombe. Inawezekana huyu jamaa akili yake ni sawa na pembe za mbuzi ndo maana anaona sifa kuitwa Jambazi Vasco.

Mkuu,
Heshima yako,hapo nimecheka sana.

Ila hatuna mawaziri ni Hewa wote,tunae waziri mmoja tu Prof.Mwandosya. Hizi type Za akina MRamba na Membe ni Usaliti mkubwa kwa watanzania.Kama huyo Mramba labda asigombee Ubunge miaka ijayo,huyu watanzania wenye uzalendo ni kuungana kuhakikisha harudi bungeni.Manake kuna siku nae alisema "Watu wasifikirie eti,Rais akiwa nje anaenda kunywa kahawa na maandazi tu"

Kama election inayokija mramba atarudi Bungeni basi ni pigo kubwa kwa Watanzania.Huyu Membe nae ni mzigo kwetu
 
Without a veifiable source it is hard to take the claim that Membe said the reported, especially the Vasco Da Gama part in the reported light seriously.

I was getting ready to machete him with the mighty pen but the lack of a verifiable source of the news (googling is not producing any matches) put a restrain on any reasonable attack.

Without a verifiable source, one is bound to doubt Membe uttered the reported comments at all.
 
Hahahahaha...tutalalamika weeee...come 2010...JK anashinda ki-tsunami akiwaacha wengine wanapiga vigelegele na wengine midomo wazi. Halafu watu tukisema Waafrika ndivyo tulivyo tunashambuliwa. So far, incompetence waliyoionyesha (Kikwete regime) if it were someplace else it would have been a wrap for them. Oh well....
 
..Raisi ni mwanachama wa CCM, vilevile amekuwa waziri wa mambo ya nje miaka 10, sasa anakwenda kujitambulisha Ulaya na Marekani kwa kitu gani kipya?

..Membe atueleze ni sera ipi ya ndani au nje iliyobadilika kiasi cha kulazimisha Kikwete aende "kujitambulisha" Ulaya na Marekani.

..Fedha za msaada toka Marekani zimepatikana kutokana na juhudi za serikali ya Mkapa. Fedha hizo zina mchakato wa muda mrefu sana. Membe anaongopa anapodai kwamba zimepatikana kutokana na safari ya Kikwete Marekani.

..Mwisho, si busara kujilinganisha na kushindana na Afrika Kusini hata ktk mambo ambayo hayana faida kwetu.

..Membe kam ni mkweli atueleze ni lini Raisi Mbeki amekwenda ulay a kutembelea viwanja na timu za mpira[real madrid].
 
Karibuni atakuja kumlinganisha Jk na safari zake na Marehemu Yasiri Arafat...
 
Ila hatuna mawaziri ni Hewa wote,tunae waziri mmoja tu Prof.Mwandosya.

By the way kila nikimkumbuka huyu mpendwa wako... Nakumbuka kifo cha TTCL!

Ndio naanza kujua kumbe nchi hii na wananchi wake mafisadi pia... Ahsante somo lingine!!!
 
By the way kila nikimkumbuka huyu mpendwa wako... Nakumbuka kifo cha TTCL!

Ndio aanza kujua kumbe nchi hii na wananchi wake mafisadi pia... Ahsante somo lingine!!!

Una maana gani ya kuua TTCL?

Kwani Mwandosya alikuwa Mkuu wa TTCL? just curios
 
Una maana gani ya kuua TTCL?

Kwani Mwandosya alikuwa Mkuu wa TTCL? just curios


Thanks for asking, TTCL haikuuzwa na TTCL Management kwa MCI/MSI iliuzwa na serikali chini ya Mh... mpendwa rudi nyuma ni story ndefu... lakini ukiwauliza wafanyakazi wa TTCL watakueleza yaliyojiri vizuri zaidi.
 
Thanks for asking, TTCL haikuuzwa na TTCL Management kwa MCI/MSI iliuzwa na serikali chini ya Mh... mpendwa rudi nyuma ni story ndefu... lakini ukiwauliza wafanyakazi wa TTCL watakueleza yaliyojiri vizuri zaidi.

Come on now,

Mgalagaze huyo Mwandosya usimpe breki.
Mimi nakutengea bonge la pasi za Jason Kidd na wewe unashindwa kudanki kama Vince Carter na kummaliza kabisa Mheshimiwa!

Unaniangusha sasa!
 
Thanks for asking, TTCL haikuuzwa na TTCL Management kwa MCI/MSI iliuzwa na serikali chini ya Mh... mpendwa rudi nyuma ni story ndefu... lakini ukiwauliza wafanyakazi wa TTCL watakueleza yaliyojiri vizuri zaidi.

Kasheshe,

Unarudia mambo yale yale ambayo yamejadiliwa hapa kwa nguvu zote. TTCL haikuuzwa wakati wa prof. Mwandosya.

Prof. Mwandosya alichaguliwa kuwa mbunge na kuwa waziri wakati TTCL tayari imeuzwa.

Yeye alienda tu kupambana na migogoro ambayo ilitokana na kuuzwa kwa TTCL, kama kupunguzwa wafanyakazi nk. na ndio maana kuna watu wanamuunganisha prof. Mwandosya na TTCL.

Makubaliano ya mwisho kuhusu kuuzwa kwa TTCL yalifanywa tarehe 07/12/2000 wakati ambapo sijui hata kama Prof. Mwandosya alikuwa amechaguliwa kuwa waziri.

Matatizo yote yaliyotokana na uuzaji mbaya wa TTCL, yeye Prof. ndio alikumbana nayo na matokeo yake baadhi ya watu wanaamini yeye ndiye alihusika kuuza TTCL, jambo ambalo sio kweli.

Ukitaka facts zaidi sema na utapewa, lakini nafikiri ni kumuonea prof. kusema yeye alihusika kwenye kuuzwa kwa TTCL. Kama una facts tofauti na tulizo nazo wengine basi lete.
 
Lakini mbona kuna kimemo kilipatikana na kuonyesha Prof. anasomeshewa binti yake huko south africa na walioinunua TTCL
 
Kasheshe,

Unarudia mambo yale yale ambayo yamejadiliwa hapa kwa nguvu zote. TTCL haikuuzwa wakati wa prof. Mwandosya.

Prof. Mwandosya alichaguliwa kuwa mbunge na kuwa waziri wakati TTCL tayari imeuzwa.

Yeye alienda tu kupambana na migogoro ambayo ilitokana na kuuzwa kwa TTCL, kama kupunguzwa wafanyakazi nk. na ndio maana kuna watu wanamuunganisha prof. Mwandosya na TTCL.

Makubaliano ya mwisho kuhusu kuuzwa kwa TTCL yalifanywa tarehe 07/12/2000 wakati ambapo sijui hata kama Prof. Mwandosya alikuwa amechaguliwa kuwa waziri.

Matatizo yote yaliyotokana na uuzaji mbaya wa TTCL, yeye Prof. ndio alikumbana nayo na matokeo yake baadhi ya watu wanaamini yeye ndiye alihusika kuuza TTCL, jambo ambalo sio kweli.

Ukitaka facts zaidi sema na utapewa, lakini nafikiri ni kumuonea prof. kusema yeye alihusika kwenye kuuzwa kwa TTCL. Kama una facts tofauti na tulizo nazo wengine basi lete.

Hii ndio JF, watu wamejaa data hadi inatisha.
Asante Mtanzania. Ila huu ushindani wa Membe, Mwandosya na Lowasa kwenye ugombea urais wa ccm naona umeanza mapema kuliko ilivyo kawaida.

Mpinzani kama mimi nachukua popcorn na Bozz sound system kusikiliza muziki.
 
Without a veifiable source it is hard to take the claim that Membe said the reported, especially the Vasco Da Gama part in the reported light seriously.

I was getting ready to machete him with the mighty pen but the lack of a verifiable source of the news (googling is not producing any matches) put a restrain on any reasonable attack.

Without a verifiable source, one is bound to doubt Membe uttered the reported comments at all.

I agree with you on this one. Source is important...then you could comment with all certainty, authority, freedom and confidence. Otherwise, let us only continue to write here.
 
Lakini mbona kuna kimemo kilipatikana na kuonyesha Prof. anasomeshewa binti yake huko south africa na walioinunua TTCL

Nurujamii,

Soma hii link http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=5271&page=7

Unaweza kuanzia huo ukurasa au soma kila kitu toka mwanzoni.

Hapo utagundua pumba na mchele. Simtetei prof. Mwandosya kuhusu suala la mwanawe kuchukua internship ya MSI ila haiji kichwani kuunganisha hiyo
scholarship na kuuzwa kwa TTCL.

TTCL iliuzwa kabla hata yeye hajapata hiyo kazi, sasa baada ya miaka miwili ndio aje achukue rushwa ili kuwasaidia makaburu kununua kampuni ambayo tayari walishainunua?

Kosa la Prof. Mwandosya kwenye case ya mwanawe ni lile la kumruhusu mwanawe
kukubali hiyo internship ya dola 2000 ambazo hata yeye angeweza kuzitoa. Yeye alikuwa waziri wa wizara ambayo MSI walikuwa ni wahusika, hivyo tunaweza kusema kuna conflict of interest hapo.

Lakini kulingana na Prof. Mwandosya hata hakujua kwamba huyo mtoto kapewa hiyo internship na MSI mpaka magazeti yalivyoandika. Yeye anasema aligharamia gharama zote za hiyo internship. Huenda mtoto alichukua pesa huku na huku.
 
Hii ndio JF, watu wamejaa data hadi inatisha.
Asante Mtanzania. Ila huu ushindani wa Membe, Mwandosya na Lowasa kwenye ugombea urais wa ccm naona umeanza mapema kuliko ilivyo kawaida.

Mpinzani kama mimi nachukua popcorn na Bozz sound system kusikiliza muziki.

Mwafrika wa Kike,

Mimi naona wote kati ya hao hawafai. Prof. atakuwa amezeeka, nafikiri atakuwa na miaka 68. Hao wawili tumewaona, uwezo wao duni sana. Wanachofahamu ni ufisadi.

Labda nchi ipate vijana ambao wana mawazo mapya. Huenda upinzani utakuwa na nguvu na tunaweza kupata rais toka upinzani.
 
Mwafrika wa Kike,

Mimi naona wote kati ya hao hawafai. Prof. atakuwa amezeeka, nafikiri atakuwa na miaka 68. Hao wawili tumewaona, uwezo wao duni sana. Wanachofahamu ni ufisadi.

Labda nchi ipate vijana ambao wana mawazo mapya. Huenda upinzani utakuwa na nguvu na tunaweza kupata rais toka upinzani.

Kwi kwi kwi.....

Mwenzako Kibaki "amekuwa rais" kwa mara nyingine tena akiwa na miaka 76 sembuse 68 ya Mwandosya? vipi Jongo la zimbabwe mpaka leo anapeta tu na miaka 82!

Mwandosya akitaka kuwa rais na akaamua kufight na kufanya ufisadi kidogo apate mapesa kibao anaweza kuwa rais Afrika bila kujali umri wake.

Maombi yetu kuwa Kina Mkumbo watakuwa wamefikisha miaka 40 sijui 35 ya kisheria ya kuwaruhusu wagombee uraisi. Otherwise, nchi inakatisha tamaa hiyo we acha tu.
 
Mwenzako Kibaki "amekuwa rais" kwa mara nyingine tena akiwa na miaka 76 sembuse 68 ya Mwandosya? vipi Jongo la zimbabwe mpaka leo anapeta tu na miaka 82!

Ndiyo kwanza anaendelea kupasha misuli moto tayari kwa kuingia kwenye kinyang'anyiro cha urais hapo mwezi March. Huyu Mzee nadhani anataka kufia madarakani. Hivi hao wana ZANU PF hawana watu wengine wenye uwezo wa kuongoza nchi zaidi ya Mugabe? Huu ufisadi ni balaa kubwa sana, najua anachoogopa ni kwamba je akiachia ngazi mrithi wake ataendelea kulinda ufisadi wake?
 
Back
Top Bottom