Rais Kikwete na safari za nje

Rais Kikwete na safari za nje

Hivi watu wanaamini Membe katamka "Vasco Da Gama" kwa authority gani inayotoa hiyo habari?

Mkuu kubali tu uliweka habari bila source na watu makini wakaomba source,

Mkuu naomba kurudia, ule mchezo wa kuwapa urais bure hautatokea tena, kwako labda hayo maneno hapo juu ni maneno ya mtu anyedai source, lakini kwangu ni ya mkereketwa wa Membe, umeomba source umepewa bado umeendelea kudai tu hata ulipokumbushwa na Mtanzania, kuwa tayari umepewa soource sasa unataka nini,

hiyo ndio tabia yako siku zote mkuu toka ulipokuwa TTJ/Kulikoni, na siku zote hukosi neno Mzee Es huwa haambiwi ukweli hapa, toka siku ya kwanza ulipoingia hii JF hili neno chini huwa halikosi mdomoni mwako mkuu,

Au Mkuu FMES yuko beyond kuulizwa source?

Mkuu hatujabadilika, bado mambo ni yale yale, waziri wako au mgombea wako ndio huyu ameanza kujionyesha wazi kuwa hana uwezo mkubwa wa kufikiri, sijawahi mkuu kuandika bila sources na wewe binafsi unajua maana toka uanze kudai sources huwa unapewa, mara ya mwisho ulitaka nikupe maana ya ubabe wa Mkapa kwenye vikao vya CC, nikakuwekea, sasa sijui ulifikiri nini this time kwamba utafanikiwa kuharibu huu mjadala on the behalf ya mgombea wako?

Mambo bado ni yale yale tu mkuu hayajabadilika, hukuwa na nia ya kuomba osurce isipokuwa ulitaka kuharibu mjadala, ninakuomba uuache hiyo tabia mkuu.

Pundit,

FMES amekuambia ametoa gazeti la Mtanzania na katoa na toleo namba, labda utuambie humuamini mzee ES au utuambie kwamba mzee ES anadanganya, vinginevyo sijui unatafuta source gani tena?

Hiyo habari imesemwa na Membe huko Zanzibar ambako yuko kwenye mkutano na maofisa wa wizara yake pamoja na mabalozi
 
Unajua kuna watu humu walifurahishwa na uteuzi wa Membe...wakammwagia misifa kibaaaooo...ooh eti jamaa kicha..sijui kasoma Johns Hopkins or one of those prestigious Universities....na blah blah nyingine nyingi tu. Sasa nashangaa watu wanamkandia....

Mkuu Nyani,

Heshima mbele, unajua kuwa waliofurahishwa walikuwa ni wale wale wapambe wake kutoka London, you know for a fact kwamba sikuwa one of them kwa sababu siku zote huwa nina tatiozo na wanasiasa wanaotumia mbinu chafu ambazo ni extreme kama alizotumia huyu Membe, na Mtandao mzima kupata power, ni mbinu ambazo huwa ni empty kwa sababu in the process huwa zinazuiya nafasi ya wananchi kuwajua vizuri watengeneza uchafu, ndio maana sasa wakianza kuongea tunpata ukweli kuwa hawana uwezo, hata tungetoa source ngapi ukweli ni wazi kuwa hawana uwezo!!
 
Membe sound like maembe mabovu. You cant compare apples and oranges. Tanzania and South Africa is total different, from their economic stand point, to life expectency.

Hivi Jakaya akisikia habari kama hii, wont he get tampeted to flip his cabinet? This is a mess, and we do expect him to represent us on other nations? I wounder why JK decides to be president and foreign minister at the same time. Because his representative is full of 000 in his brain.


Mr Membe! Can someone tell me his biography?
 
Kwa hiyo Vasco Da Gama akisariri huenda kupitisha bakuli? Why as a country are we so proud kuwa omba omba? Hand outs?? Je ndo msingi wa maendeleo? Leo almost 50 years tumekuwa matonya.. nchi imepiga maendeleo yapi?

Mimi swala la safari za umatonya.. zinanitia kichefuchefu!

Tunahitaji safari za kufanya mikataba ya kibiashara and may be trips za mediation over conflicts!
 
Kama Rais ndiyo huyo unategemea atakuwa na mawaziri wa namna gani. Maji hufuata mkondo!!!
 
Kwa hiyo Vasco Da Gama akisariri huenda kupitisha bakuli? Why as a country are we so proud kuwa omba omba? Hand outs?? Je ndo msingi wa maendeleo? Leo almost 50 years tumekuwa matonya.. nchi imepiga maendeleo yapi?

Mimi swala la safari za umatonya.. zinanitia kichefuchefu!

Tunahitaji safari za kufanya mikataba ya kibiashara and may be trips za mediation over conflicts!

Mzalendohalisi,

Watanzania walio wengi tumekuwa wazembe wa kufikiri, tumenyweshwa mwarobaini wa kuamini misaada kuliko kujitegemea.

Pamoja na elimu tosha ya Nyerere kuhusu kujitegemea, wamekuja wajanja ambao wanawaambia wananchi kwamba wao wanaweza kuondoa mawazo yao kwa kuwa ombaomba.

Ukienda wilayani siku hizi kujaribu kuwaelemisha wananchi mbinu za kuendeleza maisha yao, wao wanaona unapoteza muda, wanataka uwape shilingi
elfu moja moja, wanywe Mkomboti.

Sasa hata baraza la mawaziri limepata hako kaugonjwa, wao ni omba omba, wakingaji wakubwa wa bakuli, lakini wakifika nyumbani ni matanuzi tu. Hakuna cha kufikiria miradi ya maendeleo, kwanini wasumbuke wakati wanaweza kwenda Ulaya na Marekani kuomba misaada?

Ndio maana Membe anaona kuwa Vasco Da Gama ni sifa. Anasahau kwamba japo wote ni Watembezi lakini malengo ya Vasco Da Gama yalikuwa tofauti kabisa na malengo ya JK.
 
Wakuu JF, tunahitaji kuwa-expose wale wote wanaotaka kugombea urais, ambao tayari wameanzisha kambi tayari. Uzuri na ubaya wao lazima uanikwe, uwezo wao na uwezo wao mdogo lazima uwekwe hapa JF,

Ngoja niwapeni siri ya wale wote wanaojitayarisha kugombea urais, wamegundua mchezo mpya mchafu sana, huwa wanayawahi na kuyanunua usiku kabla ya asubuhi kuanza kuuzwa magazeti yenye kashfa zao, na ndicho kilichowaponza kina Kubenea, kwani mafisadi walichelewa kuyawahi yale magazeti wakaishia kuwamwagia tindikali,

Ndio maana kuna wanaoshangaa kuwa nimeyapata wapi magazeti yenye habari ya uozo wa rais wao mtarajiwa, maana walidhani wameyanunua yote, sasa labda waje watumwagie acid na huku JF, majuzi wameshindwa kwa sababu kitendo cha yule kijana kilikuwa co-ordinated na some higher powers tunajua tayari,

Ninatoa wito kwa wakuu wote hapa wenye uchungu na taifa letu, ukipata gazeti lenye uozo wa mafisadi usilichukulie for granted huenda ndilo la mwisho, tayari wameyanunua yote mengine, liweke ili uje uweke dataz hapa,

So far:-

1. Mama Mongella

2. Membe

two down, more to go kwa wagombea urais hatutawaogopa tutawaweka tu hapa, ili wananchi waamue kusuka ua kunyoa, lakini wananchi tumechoka na viongozi magoi goi, tena hasa wanaotuharibia jina la vijana!
 
Hebu wacha tuone hapa .
Raia mwema iko mtandaoni , Kubenea hayuko mtandaoni, Tanzania Daima iko mtandaoni, This day na Kulikoni sijui kam wako mtandaoni .Walio bakia hawana habari ni wapambe do we need to worry ? Hebu niweke sawa Mzee Es .Wanaweza kununua ili watanzania wasisome maana pia hawana access ya mtandao sawa . Nimekupata mkuu .
 
Lets be realistic on Membe's claim. You can not compare Mbeki and Kikwete on anything.

Mbeki has enough capital to have a super jet and visit any country he wants. SA is not a third world country, it is not a begger like Matonya.

What we should do is compare Kikwete with a president who has same economical numbers and see who among the two is either wasting money or making efforts to generate money.

How can we justifty global trotting to sek aid and loans while we can not even manage our national reserves?
 
Rev. Kishoka,
How can we justifty global trotting to sek aid and loans while we can not even manage our national reserves?

Chukua tano mkuu...right on the money!

Hivi hawa viongozi hukosa maswali kama haya akilini mwao kabla hawajaropoka?...
 
Mkandara si wao bali ni kulewa madaraka na kiburi kwamba hata wakisema nothing will happen . Membe ana kiburi sana even from hims look anabwabwaja tu .
 
Sasa hii site imefika pabaya maana tunajadili ushabiki kuliko maslahi ya nchi. Tunatakiwa tutumie hii site kuelimishana badala ya ushabiki wa kitoto. Kasome budget na uangalie pesa inatoka wapi nenda kwenye website ya Tanzania na tafuta hiyo information. Huwezi kushinda unaandika vitu ambavyo hufahamu wakati unaweza kwenda kwenye website ya taifa na kujua data kwa undani, huu ni ushabiki na ni aibu sana hii site imegeuka kuwa kichekesho namna hii.
 
Sasa hii site imefika pabaya maana tunajadili ushabiki kuliko maslahi ya nchi. Tunatakiwa tutumie hii site kuelimishana badala ya ushabiki wa kitoto. Kasome budget na uangalie pesa inatoka wapi nenda kwenye website ya Tanzania na tafuta hiyo information. Huwezi kushinda unaandika vitu ambavyo hufahamu wakati unaweza kwenda kwenye website ya taifa na kujua data kwa undani, huu ni ushabiki na ni aibu sana hii site imegeuka kuwa kichekesho namna hii.

Acha zako hakuna ushabiki wa kitoto hapa.
Hizo data za serikali ya SISIEMU hata mapisto yule kichaa anaweza andika zina taabu gani wakati hasisemi ukweli?
Wewe wadhani kwa vile tunaongea maneno yasiyo panda kichani mwako basi tu vichekesho?

Huwezi kuwabana SISIEMU na serikali yao kwa kusoma taarifa zao rasmi.Unawabana kwa kuibua uoza wao ambao hauko kwenye taarifa rasmi yeyote hapa duniani.

Kamati ya Fedha ya bunge ilipitia taarifa ya ukaguzi wa BOT ikasema mahesabu yote ni safi. Leo hii tunajua ni Uongo na Wizi
Wewe waweza simama kwa miguu yako miwili leo na kutuambia tukasome taarifa hiyo kwa sababu ina usahihi 100%

Acha zako wewe.
 
Naona tuko nyuma kidogo au safari hiii ya DAVOS kaamua kuchimoa kwani ishaiva na wenzie tayari washafika huko na wanaonanan na ma bankers wao kule ZURICH kabla ya kwenda DAVOS. Kuna possiblity kubwa kuwa hahitaji suti tena kwani mara ya mwisho najua alinunuliwa suti 300 kule PARIS na naona siku hizi kaamua kuvaa ma PARKA tuu akiwa Bongo

r-DAVOS-large.jpg
 
huu ni ushabiki na ni aibu sana hii site imegeuka kuwa kichekesho namna hii.


Mkuu huwa htupendi hoja za nguvu hapa, Jf haijakukosea kitu mkuu kama ni aibu au kuwa kichekesho basi labda wewe ndiye unakuwa the one, maana hizo website zako za taifa je zina onyesha hela zilizoibiwa kule BOT? Wafanyakazi wa serikali sasa hivi hawapti mshara ontime wanasubiri hadi two to three months je hiii nayo ipo kwenye hiyo website zako za taifa?

Comeon bro, usitumie hoja za nguvu hapa halafu unaitukana JF znima kwa sababu tu ya ushabiki wako, heshimu wengine mkuu kama wanavyokuheshimu wewe, kama huna hoja waache wenye nazo waseme lakini usilazimishe wote tufikiri kama wewe, people worked so hard kuifikisha hii forum ilipo mkuu na wewe ukaweka mawazo yako yakasikika, wape heshima kwa kuweka hoja badala ya viroja!

Wengi kama wewe huko nyuma wameishia kuchekesha hapa JF, na wakaiacha vile vile ilivyo ikiendelea kumkoma nyani!
 
Ngoja, nadhani naijua ratiba ya Mzee: ni hii hapa chini. Safari ndogo ndogo za kwenda Kenya, Uganda na nchi jirani sikuzijumuisha.

January 1 -15: Tanzania
January 15 - 22: Netherlands
Januray 23 - 28: Germany
January 29 - February 12: Tanzania
February 13- February 27 : USA
february 28- March 7: Tanzania
march 8- March 16 : UK
March 17- March 30: Nordic Countries
April 1- April 5: Tanzania
April 6- April 17: Brazil
april 18- April 20: venezuela
April 21- may 1: Tanzania
may 2- May 10: Japan
May 11- May 17 Singapore
may 18- June 1: Australia
June 2 - june 7: New Zealand
June 8 - June 16 - Hawaii
june 17 - June 25 - Canada
June 26 - June 30 - South Africa
June 30- July 10 - Tanzania
July 10-July 20 - China
july 21- July 25 - India
July 26 - August 2 - UAE
August 2- August 9 - Tanzania
August 10- August 15 - Seychelles
August 16- August 18 - Mauritus
August 19 - August 22- Madagascar
August 22 - August 27 - South Africa
August 28- Sept 10 - Tanzania
Sept 11- Sept 17 - USA
Sept 18 - Sept 25 - Canada
Sept 26 - Sept 30 - Greenland (at last)
oct 1 - Oct 5 - Denmark
Oct 6 - Oct 15 - Belgium and France
oct 15- Nov 1 - Italy, Spain and Switzerland
Nov 2- Nov 5 - Tanzania
Nov 6- Nov 14- Korea
Nov 15- Nov 30 - USA
Dec 1- Dec 30; Tanzania

Jamani Kichuguu ulikuwa unatupiga mafiksi! Mbona Jk yupo bado nchini, hiyo safari ya Ujerumani na Uholanzi mbona haikuwepo? Jamani tupeni data za uhakika! Au BoT imevuruga mipango?
 
Sasa hii site imefika pabaya maana tunajadili ushabiki kuliko maslahi ya nchi .. unaweza kwenda kwenye website ya taifa na kujua data kwa undani, huu ni ushabiki na ni aibu sana hii site imegeuka kuwa kichekesho namna hii.

Mheshimiwa Kamundu,

Naomba kwa heshima na taadhima usome tena hayo uliyoyaandika, hasa hayo niliyoyanukuu hapo juu halafu jiulize haya maswali

1. Je ushabiki ni nini; ni pale unapoelezwa linalokuhusu halafu ukakosa la kujitetea kwa vile wewe binafsi umejifungia kwenye kisanduku kilicho jaa mawazao yako mwenyewe. Hence huamini kuwa kuna sense beyound your sphere of thinking.

2. Hiyo website ya taifa unayoizungumzia na hizo data zilizomo zina uhakika upi wakati tunachozungumzia ni upuuzi na pumba zinazotolewa na "viongozi" wetu.

3. Linalochekesha zaidi ni lipi - Membe kutamani kuitwa Vasco Dagama au Meghji kutoa kisingizio cha kudanganywa au sisi kuyaweka wazai hayo unayo yaona kuwa ni ushabiki. Ndugu yangu hivu uko dunia ya ngapi?

Ningependa kunukuu yafuatayo ambayo ni makala yaliyopo kwenye gazeti la Rai, tolea la tarehe 24/01/2008:


Sitaki kuamini kwamba kila mtu anaweza kuwa waziri katika nchi hii, lakini kwa hoja ya Waziri Meghji, ambaye ni miongoni mwa mawaziri wazoefu katika baraza letu, inatosha kabisa kutia shaka kwamba kumbe yeyote anaweza kuteuliwa kuwa waziri, kama uwaziri unamaanisha kuwapo kwa mtu tu ambaye atasaini lolote atakaloambiwa na anaowaamini.

Na huyo mwandishi naye ni shabiki? ( sijui wa nani)


Hivi ni Mtanzania gani anaweza kuyaamini maneno ya Meghji, kwamba gavana ana uelewa mkubwa wa uendeshaji wa nchi kuliko yeye waziri ambaye ni sehemu ya Serikali? Yeye ni mjumbe wa baraza la mawaziri ambalo ndilo lenye mamlaka ya uendeshaji wa nchi. Ingekuwa Ballali kamdanganya Meghji katika mambo mengine ya kibinfasi, kwa vyovyote lisingekuwa jambo la kushangaza, lakini haingii akilini kuwa gavana wa BoT mwenye udhibiti mkubwa wa Serikali, anaweza kumdanganya bosi wake, Waziri wa Fedha, mwenye mtandao mkubwa wa washauri wa taaluma mbalimbali nyuma yake, kiasi cha kuidhinisha malipo makubwa ya fedha za nchi kwa mipango ya kifisadi.

Mtu waye yote amabaye anaweza kusoma na kuandika hawezi akabisha kuwa hilo lisemwalo is unthinkable. Mind you Membe na Meghji a said to be very close to JK (kwa kujikomba I am told) Sasa make you own conclusion which will be obviously - ushabiki. Ingawa mimi naona ni kuwa upeo mdogo kiutendaji.


Kudanganywa, hata kama ni kweli kulitokea, hakuwezi kuwa utetezi mbele ya kadhia kubwa kama ya BoT, hata mbele ya sheria! Tukirudisha kumbukumbu zetu nyuma kidogo katika utawala wa awamu ya tatu, tutaikuta kadhia nyingine ya rushwa ya viwanda vya minofu ya samaki kule Mwanza.

Haya ushabiki mwingine according to you, kwa vile waziri alikuwa Meghji huyo huyo.

Ulimwengu kulizunguka jua wewe utasema ushabiki, kwa vile unacho kiona ni jua kutokea mashariki hadi magharibi na usiku ukija utasema jua limezimika, na ukiambiwa othewise utasema ushabiki tuu huo !
 
Back
Top Bottom