Yehoshafati
JF-Expert Member
- Apr 7, 2021
- 325
- 660
Halafu akiambiwa wale M23 ni askari wa Rwanda anasema si kweliKagame kasema, kama wale majeshi ya SADC wasingejishusha angewashushia kipigo kikali na kupukutisha wote!
Halafu akiambiwa wale M23 ni askari wa Rwanda anasema si kweliKagame kasema, kama wale majeshi ya SADC wasingejishusha angewashushia kipigo kikali na kupukutisha wote!
Jamaa sikiliza kwanza hiyo speech ya Kagame.Mkuu Rwanda is nothing to South Africa.
Tena South Africa usimtaje kabisa,hivi unajua kama South Africa ana wanasayansi wanaomsaidia Qatar kuunda silaha ikiwemo drones?
Kilichotokea Congo ni kwamba SADC hawakuenda na silaha zao nzito Bali waliitumia silaha za jeshi la Congo walizozikuta,pia wanajeshi wa Congo hawakuwa wazalendo kwa jeshi lao,makundi ya wapiganaji ya kiraia yalikua active kuliko jeshi la Congo.
Mind you Tanzania angeleta smerch Bm-30 Mlrs ama A-100 Mlrs na South Africa akaleta Air supremacy yake pale Congo na jeshi la Congo likawa active,Kagame jioni sana angepiga ukunga.
Sasa unazungumzia Congo iliyokuwa tayari ina internal stabilities? Na issue ya Congo sio kusema eti Kagame alikuwa anahusika mwenyewe 100%Logistic sio shida. Kagame na Kabarebe walimpindua Mobutu mwaka 1997 wakati DRC ilikuwa hivyo kwa miundo mbinu na kubwa kuliko Tanzania.
Israel impigwa mpaka imeomba ceasefire kupitia Trump hadi mamilion ya waisrael wameikimbia nchi yao ya ahadiUnajua uwezo wake? Israel yenye watu 8mln imempiga Iran yenye watu zaidi ya million 100 kwa siku 12 mpaka rais wao hajaonekana mpaka leo akiogopa kuuliwa🤣🤣🤣🤣
Siongelei Polisi wala usalama. Naongelea Jeshi la Wananchi wa Tanzania
View: https://youtu.be/wUu2W2Mk3k0
General Paul Kagame amezungumzia mgogoro wake na Congo. Moja ya vitu alivyovisema ni kwamba wale wote ambao wanaamini kwamba wanaweza kuitishia Kigali wakiwa mbali anao uwezo wa kuwafuata hukohuko makwao.
Akaendelea kusema kwamba, wale waliokuwa wanaiunga mkono serikali ya Congo, Rwanda iliwasamehe na kuwaacha wapite nchini Rwanda na kurudi makwao. Katika watu ambao waliruhusiwa kupita Rwanda ni pamoja na askari wa JWTZ ambao kuna video inaonesha wanasachiwa ili kurudi nyumbani.
Paul Kagame amesema, kama wale wanajeshi wangethubutu kutunisha misuli bila kusalimu amri basi wangeangamizwa wote. Tena kama kuna wengine wataendelea kufikiria kwamba wataitishia Rwanda basi watafuatwa hukohuko makwao.
Maneno ya Dikteta Paul Kagame yameanzia dakika ya 14 ya hii video niliyoambatanisha hapa. Ni ujumbe wa vitisho kwa mataifa ya SADC, ikiwemo Tanzania, Malawi na Afrika Kusini.
Kuna msemo husema hivi, "Usipokuwa makini, hata mbwa atakucheka"
Povu Ruksa, Karibu Sana......
View: https://youtu.be/wUu2W2Mk3k0
General Paul Kagame amezungumzia mgogoro wake na Congo. Moja ya vitu alivyovisema ni kwamba wale wote ambao wanaamini kwamba wanaweza kuitishia Kigali wakiwa mbali anao uwezo wa kuwafuata hukohuko makwao.
Akaendelea kusema kwamba, wale waliokuwa wanaiunga mkono serikali ya Congo, Rwanda iliwasamehe na kuwaacha wapite nchini Rwanda na kurudi makwao. Katika watu ambao waliruhusiwa kupita Rwanda ni pamoja na askari wa JWTZ ambao kuna video inaonesha wanasachiwa ili kurudi nyumbani.
Paul Kagame amesema, kama wale wanajeshi wangethubutu kutunisha misuli bila kusalimu amri basi wangeangamizwa wote. Tena kama kuna wengine wataendelea kufikiria kwamba wataitishia Rwanda basi watafuatwa hukohuko makwao.
Maneno ya Dikteta Paul Kagame yameanzia dakika ya 14 ya hii video niliyoambatanisha hapa. Ni ujumbe wa vitisho kwa mataifa ya SADC, ikiwemo Tanzania, Malawi na Afrika Kusini.
Kuna msemo husema hivi, "Usipokuwa makini, hata mbwa atakucheka"
Povu Ruksa, Karibu Sana......
sipo na jamaa wa Bungeni mkuu ila huyo Kagame hakuna kitu atagusa huku mazee ninaliamini sana Jeshi la Tanzania.
Upo serious kabisa kabisa...au macho siyo makavu!?Unajua uwezo wake? Israel yenye watu 8mln imempiga Iran yenye watu zaidi ya million 100 kwa siku 12 mpaka rais wao hajaonekana mpaka leo akiogopa kuuliwa🤣🤣🤣🤣
Imeamua kuachana nae au kawadhalilisha? Jeshi la kichawa linawezaje kupambana na watu wenye akili?Tanzania imeamua tu kwa makusudi kuachana na huyo Kagame tunayo mengi ya kwenye ilani za uchaguzi tunahangaika nayo.
Rwanda ni ndogo kuliko mkoa wa Tabora au Morogoro, pia hatuna watu wengi wenye hulka za kitutsi za kujikweza na kuwatazama walio wengi kwa mtazamo wa dharau na dhihaka, tulishatoka huko kitambo sana.
Watapigana hawa wenye nchi yao.Na vita ikianza wale migambo mstari wa mbele wanaokufaga wote wachaguane UVCCM kama wanavyopeana UDed na Udc
Huyu hana tofauti na ayatollah maneno mengi akipelekewa motonkidogo mbio mapangoni.Huyu nae anajikuta lord war wa east and central africa ngoja watamshangaza na asiamini.
Tena kasema kilometre 2000 kwa makusudi maana kutoka Kigali hadi Dodoma ni Kilometre 700-800 na Kigali hadi Dar ni Kilometre 1100-1400.Anasema wanaotishia Kigali wakiwa mbali kabla hawajaipiga Kigali watawafuata huko huko. Anasema RPF wanaweza kupigana 2000km kwa miguu!
My take, kusema watawafuata huko huko kabla hawajashambulia Kigali ni ujumbe kuwa wapo "huko" tayari wanasubiri amri tu! Tuwe makini hasa mamluki ndani ya vyombo.
Acha upuuzi wewe. So wanajeshi wa Tanzania waliouliwa walikuwa wanapigana na nani?Nina ndugu wapo huko kwa mwamvuli tofauti Moja wapo amerudi na jeshi la SAMIDRC,unamdanganya nani!?
Hakuna askari wa SADC hususan TZ aliyeingia front,askari wa DRC ndio walikua front,pia awamu hii sio TZ Wala South Africa ambao walikuja na silaha zao na ndio maana hata vita ilionekana ngumu kidogo.
Silaha walizozikuta ni duni huko Congo.
Nina ndugu wanajeshi mzeee usinidanganye.
Rwanda nchi ya kiboya sana, na haina uwezo wa kupambana na tz hata kwa dakika 5 tumewazid kila.idara katika medani vifaa vya kisasa
Idadi ya military personnel
Hakuna kitu hakuna kitu wanaweza fanya akitaka ajaribu aisiwe kama usa kuingea on
iniIla tuwe wa kweli , japo Rwanda itazidiwa au kushindwa lakini TPDF hivi sasa ipo weak katika historia ya hii nchi, very weak...
Mbinu za kivita duniani zimebadilika sana asee, vita ya Ukraine damage kubwa zinafanywa na drones, karibu asilimia 70...
Na jeshi la Rwanda wamejiingiza kwenye hizo drones, operators wa drones sio wanapasua matofali kwa kichwa, wao ni kama gamers tu, kama mtu anacheza playstation... vita imebadilika sana..
Hao jamaa kujiamini hivyo inabidi iwe wake up call, itakuwa hawajiamini bure... mnakwenda na Artillery guns/mabomu ya mizinga ya enzi za Kagera war, unatumiwa ki drone kidogo kinawalipua na silaha zenu zote...
Wakuu wa jeshi wana ongelea kuhusu vipenyo wanapewa madaraka ,uku bi kiremba ana cheka cheka kama jinga ana waza upinzani tu na TiSS wake.Vita vya sasa ni information na Rwanda ana information nyingi sana kuhusu Tanzania. Kuna wanajeshi JWTZ wanavujisha siri. Kuna wafanyakazi wengi wa wizarani ni wa Rwanda. Tanzania kutikiswa na Kabambe inawezekana kabisa mchana kweupe. Na wana advantage myavkuhonga pesa nyingi maana currency yao ipo juu.