Rais Kagame anailenga Tanzania katika ujumbe huu?

Rais Kagame anailenga Tanzania katika ujumbe huu?

rwanda-bayraktar-turkey-baykar.png

Rwanda hivi sasa wana process za kuanza kutumia stealth drones na zina AI..
Lets be careful... huyu mzee akiachiwa hivi pasipo kuchukua tahadhari, miaka 10/20 baadae tukikaa kifala tutashindwa hata kumgusa..
 
Ila tuwe wa kweli , japo Rwanda itazidiwa au kushindwa lakini TPDF hivi sasa ipo weak katika historia ya hii nchi, very weak...

Mbinu za kivita duniani zimebadilika sana asee, vita ya Ukraine damage kubwa zinafanywa na drones, karibu asilimia 70...

Na jeshi la Rwanda wamejiingiza kwenye hizo drones, operators wa drones sio wanapasua matofali kwa kichwa, wao ni kama gamers tu, kama mtu anacheza playstation... vita imebadilika sana..

Hao jamaa kujiamini hivyo inabidi iwe wake up call, itakuwa hawajiamini bure... mnakwenda na Artillery guns/mambomu ya mizinga ya enzi za Kagera war, unatumiwa ki drone kidogo kinawalipua na silaha zenu zote...
Vita vya sasa ni information na Rwanda ana information nyingi sana kuhusu Tanzania. Kuna wanajeshi JWTZ wanavujisha siri. Kuna wafanyakazi wengi wa wizarani ni wa Rwanda. Tanzania kutikiswa na Kagame inawezekana kabisa mchana kweupe. Na wana advantage ya kuhonga pesa nyingi maana currency yao ipo juu.
 
Hii kauli inaonyesha jinsi gani wamejipanga. Vyombo vya Ulinzi na Usalama viwe macho muda wote
Vita ya sasa ahitaji kuwa na macho,zana za kisasa,pk jeuri yote hiyo jamaa ana silaha za kisasa jeshi lake kalijenga kizalendo mno,kenya wanafikiria kununua iron dome kwa muisrael hapo,uganda ana sukhoi 27,sie tuna chengdu ya mwaka 60 sijui 😃,imefika muda na sisi tuongeze bajeti ya silaha,majirani zetu wa silaha nzito
 
Mimi nilisha wambia humu Rwanda anaweza kuitandika Tanzania wengine wakasema mimi ni mtusi eti 😆 😂
Mmmh hawezi aisee, kwanza logistic itakuwa ni changamoto kwao, sana sana waishia kuiteka kagera kwa muda, ila in the long run, tutawapiga kwa war of attrition sababu kwanza wao ni land locked country, na ndo utakuwa mwisho wa Kagame
 

View: https://youtu.be/wUu2W2Mk3k0

General Paul Kagame amezungumzia mgogoro wake na Congo. Moja ya vitu alivyovisema ni kwamba wale wote ambao wanaamini kwamba wanaweza kuitishia Kigali wakiwa mbali anao uwezo wa kuwafuata hukohuko makwao.

Akaendelea kusema kwamba, wale waliokuwa wanaiunga mkono serikali ya Congo, Rwanda iliwasamehe na kuwaacha wapite nchini Rwanda na kurudi makwao. Katika watu ambao waliruhusiwa kupita Rwanda ni pamoja na askari wa JWTZ ambao kuna video inaonesha wanasachiwa ili kurudi nyumbani.

Paul Kagame amesema, kama wale wanajeshi wangethubutu kutunisha misuli bila kusalimu amri basi wangeangamizwa wote. Tena kama kuna wengine wataendelea kufikiria kwamba wataitishia Rwanda basi watafuatwa hukohuko makwao.

Maneno ya Dikteta Paul Kagame yameanzia dakika ya 14 ya hii video niliyoambatanisha hapa. Ni ujumbe wa vitisho kwa mataifa ya SADC, ikiwemo Tanzania, Malawi na Afrika Kusini.

Kuna msemo husema hivi, "Usipokuwa makini, hata mbwa atakucheka"

Povu Ruksa, Karibu Sana......

Mshenzi Huwa anaongea shit akijua nchi imeconcentrate kwenye uchaguzi,anajua hakuna wa kumzingatia
 
Vita ya sasa ahitaji kuwa na macho,zana za kisasa,pk jeuri yote hiyo jamaa ana silaha za kisasa jeshi lake kalijenga kizalendo mno,kenya wanafikiria kununua iron dome kwa muisrael hapo,uganda ana sukhoi 27,sie tuna chengdu ya mwaka 60 sijui 😃,imefika muda na sisi tuongeze bajeti ya silaha,majirani zetu wa silaha nzito
Baelezee hiyo. Na sisi tuna upumbafu wa CCM ndio kabisaaa
 
Hii kauli inaonyesha jinsi gani wamejipanga. Vyombo vya Ulinzi na Usalama viwe macho muda wote
Vyombo gani na Ulinzi unavyovizungumzia wewe??.

Hawa Chawa wa CCM ambao Intelijensia Yao imejikita ni wapi alipo Gwajima, CHADEMA wanafanya nn??.


Hatuja Jeshi , huo ndio ukweli, huwezi kua na Jeshi la kichamachama ukategemea liwe Imada.

Kagame alikua kuliabisha sana JESHI la CCM.
 
Vita ya sasa ahitaji kuwa na macho,zana za kisasa,pk jeuri yote hiyo jamaa ana silaha za kisasa jeshi lake kalijenga kizalendo mno,kenya wanafikiria kununua iron dome kwa muisrael hapo,uganda ana sukhoi 27,sie tuna chengdu ya mwaka 60 sijui 😃,imefika muda na sisi tuongeze bajeti ya silaha,majirani zetu wa silaha nzito
Uko sahihi mkuu
 
Drone ni hela zako tu, ukiingia hapo China na bilioni 100 unazichukua za kutosha. So Rwanda kuzimiliki sio kwamba Tanzania ni dhaifu
Za Tanzania zipo wapi ? Hata tulitenga hio bajeti hakuna mtu mwenye uchungu na nchi. Watapiga cha juu na zitanunulia zisizo na uwezo. Nchi hizi hakuna mfanyakazi serikalini aliye na uzalendo. Wanashindana kununua magari 0 km kuhonga wanawake na kuongeza wake. Pesa zinapotea bora miaka ya nyuma watu waliiba na kufungua biashara. Leo hii wanaiba na kujenga Airbnb. Airbnb moja inaajiri maximum watu watatu. Uchumi unakua au unadidimia ?
 
Kuna watu watafurahia Tanzania kupigwa ili tupate serikali mpya itakayothamini kila mchango wa Kila mtanzania

Naona wako macho dhidi ya chadema tuuuu
Hivi itokee wanatangaza National Mobilization Kwa Watanzania wote kuanzia miaka 18, nani ataenda ??.

Yaan unategemea ,Mfuasi wa Gwajima, Au CHADEMA aende kupigania vita kwaajili ya Wanaccm??.

Wataenda wao, ni heri wanipige Risasi lkn sio kujifanya Mzalendo wa Kupambania Taifa langu ili hali vitani ni kwenda Kupambania Ugali wa CCM.
 
Uzuri kagame hua hatanii mwaka huu tunampa njia zote za kuwashugulikia yaani mumekalisha matako yenu makubwa na vitambi mkisubiri wananchi wawaunge mkono nyie wajinga kweli tuache kuiunga mkono Rwanda Ili iwatembezee kichapo tuwaunge mkono majizi safari hii mnalo hilo
Wewe ndio mjinga ambae umeshindwa kututoa sisi wenye vitambi umekaa unamsubiri Kagame aje kututoa we kweli punguani.
 
Nyie mmeinvest kwenye wizi na propaganda za kuwasifia wanasiasa lkn hiki kinchi kidogo masikini kinawatukana watu waliokizi maendeleo mpaka idadi ya watu mara mia.

Kuna siku East Afrika tutakuja kulia kisa kuifumbia macho hii migogoro ambayo inawakumba jirani zetu lkn hatuoneshi udhibiti zaidi ya kutegemea wageni wa ulaya watusaidie.

Nina imani hiki kinchi(Rwanda) hakifanyi mambo kwa kukurupuka wala kwa mihemko, bali ni uhalisia, pia nina uhakika kwa Rwanda ilipofika ina intelligence kubwa mpaka huku tusikofikiria, vile vile kina technologia ambazo baadhi yetu bado hatuna na hatuna mipango nazo kwa kujidanganya sisi taifa lenye amani

Ipo siku hii amani fake itawaliza watu na tutaumbuka vibaya sana, nguvu zetu tumeziwekeza ktk siasa chafu za kuuwana, kuchafuana na kupora mali za umma, lkn mambo ya msingi bado tuko nyuma.

Jeshi letu linaweza kuwa bora ktk uiamara wa kuwaandaa na kuwapa ukakamavu askari na wanajeshi lkn kwa technolojia hili tusidanganyane, technolojia haifichiki, bado tuko nyuma sana, nyuma saana.

Ushahidi mnao, kambi zetu si mnazijua? Maonesho ya siraha zetu si huwa tunayaona?, basi hata wakisema wanaficha baadhi ya siraha ushahidi mnao wenyewe kuwa Tanzania kitechnolojia bado tuko nyuma sana,
Tutafichwa vingine lakin nyenzo za kivita hasa ktk ulimwengu wa leo Tanzania bado hatujafika huko tumebaki ktk matumizi ya nyenzo za generation ya 3 huko ambayo ni outdated zingine zilitumika vita ya pili ya dunia na zingine kipindi cha akina Idd amin.

We need to improve, si tunajifunza vita za Ukraine+ Russia, Israel+ Iran kuwa vita vya sasa ni technolojia na kupunguza matumizi ya wanajeshi, yaani unapigwa nchini mwako kwa shambulio kubwa bila matumizi makubwa ya askari wa kijeshi, muda na fedha, na gharama za maandalizi ya plan.
 
Hiyo mikwara tu mkuu,kwa anayejua huyo hapati shida.
Kipindi cha Jakaya alipiga mikwara sana aisee,JAKAYA akampiga mkwara wa askari wa mpakani kwa paredi akaufyata.
Viazi wa ccm siku zote hoja zenu huwa ni nyepesi sana maana vichwa vyenu huwa mnafugia nywele tu.

Sasa kwa akili yako Rwanda ya kipindi cha JK(almost 10 years ago) utailinganisha na ya sasa hivi?

Haya, huyu amri jeshi mkuu(mama yenu anayejua kufuga machawa tu) utamlinganisha na amri jeshi mkuu wa wakati ule ambaye kwanza alikuwa ni mwanajeshi(Kikwete)...?

Mtu anayeiongoza wizara kipindi hiki(mwanamke ambaye hajui kushika hata darubini) utamlinganisha na aliyekuwa anaiongoza wakati ule(Hussein Mwinyi) ambaye ana taaluma ya mambo ya kisheji)

Hivi umewahi kufuatilia jinsi Rwanda walivyo modernize jeshi kwa hii miaka ya karibuni? Je, nyie kuna kipi mmefanya kwenye JWTZ hili kuendana na mabadiliko ya kidunia msiachwe nyuma?

Yaan kabisa umekaa hapa unaibeza Rwanda kwa hizi hoja dhaifu kwamba eti JK aliwapiga biti miaka ile wakanywea basi hawana uwezo wa kutufanya kitu?

Kweli sasa nimeamini nyie wabongo hasa mashabiki wa ccm ni maiti, wewe endelea kumshabikia samia huku ukimbeza Kagame wakati yule ni mtu mwenye akili kuliko nyie maccm yote
 
Za Tanzania zipo wapi ? Hata tulitenga hio bajeti hakuna mtu mwenye uchungu na nchi. Watapiga cha juu na zitanunulia zisizo na uwezo. Nchi hizi hakuna mfanyakazi serikalini aliye na uzalendo. Wanashindana kununua magari 0 km kuhonga wanawake na kuongeza wake. Pesa zinapotea bora miaka ya nyuma watu waliiba na kufungua biashara. Leo hii wanaiba na kujenga Airbnb. Airbnb moja inaajiri maximum watu watatu. Uchumi unakua au unadidimia ?
Namaanisha pamoja na hayo mapungufu, drone sio kitu cha kuringia kwa dunia ya sasa.

Hivi ujajua kuna ma engineers wa silaha kutoka Asian countries wapo wameajiriwa na nchi za ki Africa?

Sio issue kabisa hata kwenye drone, ukiwa na central command ukawaweka wachina 10 wanatosha kabisa kuipa joto Rwanda
 
Back
Top Bottom