Rais Dkt. Mwinyi amteua Maalim Seif kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar

Mbona hamueleweki wakikataa mnawaita vibaraka wa wazungu na sio wazalendo na wakikubali mnawaita wachumia tumbo.
Pongezi kwa CCM kwa ukomavu wa kisiasa, hongera ACT kwa kukubali kwamba maendeleo hayana chama.

Tuliwaasa sana ndugu zetu kwamba hakuna upinzani Tanzania ila kuna wachumia tumbo na vibaraka wakatukatalia, ila nadhani sasa wataelewa.

Mungu ibariki Tanzania
 
Huyu mzee ni ccm hajawahi kurudisha card mpaka leo, amewekwa kimkakati kuhadaa wazanzibari na alifanikiwa lakini saivi mwisho wake umefika ameonesha rangi yake halisi.
 
Zanzibar hamuhitaji siasa za kuuwana wala kuandamana, lakini wakati wa uchaguzi lazima muuwawe ili ccm wakae madarakani! Sasa sijui ni kuuana kupi unakuoongelea.

Ninachokiona mimi ni kujaribu kurudi kwenye siasa za maridhiano na utulivu ambazo zilikuwa na matunda mengi tuu. Wanyonge waliweza kuendelea na shughuli zao za kawaida na pia iliweka mazingira ya uchaguzi wa utulivu kwa uchaguzi ujao/2015.

Kukaa nje kutaendeleza purukushani na waznz wataishi kwa miaka 5 ijayo kwa mkiki bila ya sababu yoyote. Nadhani hii ni faida moja kubwa kuliko hizo nyengine.
 
After all nimesikiliza maoni ya wazanzibari wengi wanaunga mkono kuingia ndani ya serekali. Nadhani watakuwa wanafahamu na wameshaona hasara na faida zake kwa sasa.
 
Ninachokiona mimi ni kujaribu kurudi kwenye siasa za maridhiano na utulivu ambazo zilikuwa na matunda mengi tuu. Wanyonge waliweza kuendelea na shughuli zao za kawaida na pia iliweka mazingira ya uchaguzi wa utulivu kwa uchaguzi ujao/2015.

Kukaa nje kutaendeleza purukushani na waznz wataishi kwa miaka 5 ijayo kwa mkiki bila ya sababu yoyote. Nadhani hii ni faida moja kubwa kuliko hizo nyengine.

Kwahiyo kwa maneno marahisi ili wazanzibari washiishi kwa amani ni lazima ccm iwatale kwa shuruti?
 
Bado Lissu kurudi na kujakupewa kazi aliyoahidiwa. Salary Slip na wenzake watafute kabisa sehemu watakapoficha nyuso! Ha ha haaa!
===
Hongera watanzania mnaoishi Zanzibar kwa kuonyesha mfano wa kuigwa.
 
Kwahiyo kwa maneno marahisi ili wazanzibari washiishi kwa amani ni lazima ccm iwatale kwa shuruti?
Nope haina maana hio sheikh. Fikiria hivi ni sawa na kuwa jela halafu ukagoma kula wakati ukijua mlinzi wa magereza hajui hata maana ya haki za binadamu. Pengine anakuombea dua ufe apate aendelee na shughuli zake nyengine! Sasa ni kheri ule tuu huo ugali kama hauna sumu basi sawa na unavuta muda ukitarajia msaada na kudra za M.Mungu.

Hebu nitajie faida moja ya kugoma na kususa itakayopatikana ?
 
Zanzibar inaweza jikomboa si lazima kwa nguvu za ndani, pengine Allah kapanga mengine ambayo hatuyafahamu kwa sasa. Kwa mfano siasa za Tanganyika zikibalika tuu basi tushavuka, acha wanyonge waendelee na maisha bana. Kushiriki serekali kuna faida kubwa ya kuleta utulivu, mie naona ni wazo la kishujaa kabisa.

Naamini M.Seif kwa umri alionao hana shida yoyote au ulazima wowote ule wa kuwa makamu bali kwa dhati kabisa ametizama maslahi ya Zanzibar na watu wake kuliko yake mwenyewe binafsi.
 
Nope haina maana hio sheikh. Fikiria hivi ni sawa na kuwa jela halafu ukagoma kula wakati ukijua mlinzi wa magereza hajui hata maana ya haki za binadamu. Pengine anakuombea dua ufe apate aendelee na shughuli zake nyengine! Sasa ni kheri ule tuu huo ugali kama hauna sumu basi sawa na unavuta muda ukitarajia msaada na kudra za M.Mungu.

Hebu nitajie faida moja ya kugoma na kususa itakayopatikana ?

Kugoma na kususa ni kulazimisha haki kutendeka. Sasa unategemea upate haki kwa kushirikiana na anayepora haki yako, hapo utatoboa?
 
Kugoma na kususa ni kulazimisha haki kutendeka. Sasa unategemea upate haki kwa kushirikiana na anayepora haki yako, hapo utatoboa?
1995, 2015 ni mifano ya kugoma. Ilipatikana iyo haki ? Nadhani mazingira ya 2020 yalikuwa mabaya zaidi, bora tungeshiriki na kujaribu kujenga umoja toka 2015 hadi 2020 basi tungelikuwa wamoja na pengine kusingekuwa na hata nzi alieumizwa.
 
Kuna video au kesi ya jamaa aliepigwa risasi akichota mchanga tuu wala haandamani wala chochote. Huu ni mfano tuu kukuonesha kama kuna umuhimu wa kuepo kwa utulivu na kutokutoa nafasi kwa polisi kuanza mauaji yasio ya msingi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom