Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,805
- 11,964
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Mwinyi amemteua Maalim Seif Shariff Hamad, kuwa Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar kuanzia leo Disemba 06, 2020.
=====
Taarifa kwa vyombo vya Habari
Kwa kuzingatia matakwa ya Kifungu cha 9(3) cha Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984,kinachosema kwamba “Muundo wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar utakuwa na Umoja wa Kitaifa na utendaji wa kazi zake utafanywa katika utaratibu utakaohakikisha kuendelezwa kwa umoja nchini na lengo la kufikia demokrasia”.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt.Hussein Ali Mwinyi amemteua Mheshimiwa Maalim Seif Sharif Hamad kuwa Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.
Uteuzi huo umeanza leo tarehe 6 Disemba, 2020