Rachel Dangwa yuko 'kwenye Mikono Salama'

Rachel Dangwa yuko 'kwenye Mikono Salama'

Acha ujinga wewe yule ni kiporo tu Interpol wakiamua saa yoyote watamkabidhi hapo Airport.
Kuna yule jamaa na mkewe waliua wakaiba huko South walikamatwa Arusha hujui?
Rusesabagina wa Hotel Rwanda alitamba sana huko US,Belgium na Europe yoote kwamba ni mwamba.
Alikamatwa kizembe tu na mpaka leo kala nyundo za kutosha hapo Rwanda.
Na yule mwanamke aliegombea urais akajipeleka mwenyewe kupiga campain kaliwa kichwa miaka 30.
Hiyo ni mifano tu.
Siku wakiamua Mange sekunde tu mtamuona hapo Dar.
US si mbinguni na wao wakimtaka mtu wao wanapewa anytime.
Yule mwizi mbona alikamatwa Dubai aliowaibia huko US wakampeleka kula nyundo kule
Intepol kwani ni muahalifu
 
Sumaye naye alifanya nini mstaafu wa watu? Mzee anaogeshwa matusi sambamba na Makonda. Binti anatukana hadi mkuu wa nchi matusi ya nguoni bila aibu. Si alisema hawatamkamata huko Tokyo hata wafanye nini, sasa imekuaje akamatwe kindezi hivyo?
 
Ninapotofautiana na baadhi yenu hapa wengi ni kiwango kikubwa cha Unafiki, Chuki na kuendeshwa na Mihemko tu. Sasa kama leo baada ya kujaa Mfumoni tumebadilika ghafla na kusema alikuwa Mgonjwa wa Akili (Mwehu) ilikuwa muda wote anafanya aliyokuwa akiyafanya na tukawa tunamuona Shujaa mpya wa Taifa kiasi kwamba tulikuwa hasa tunayaamini kwa 85% hadi 90% Uwongo wake aliokuwa akijua kuufanya uonekane ni wa kweli?

Ninajua msiopenda huu Ukweli mtakuja kwa Kufura na Mashambulizi juu yangu na Mimi ninawakaribisheni sana tu.
 
Ila dada alikuwa anaongea matusi ya kuudhi na kudhalilisha sana viongozi. Hata kama alikuwa anajitambulisha kama mpinzani, aliokuwa anaufanya sio upinzani, ni jinai na udhalilishaji.

Hakuna haja ya kutumia nguvu kupita kiasi, ashughulikiwe tu kwa mujibu wa sheria zetu inatosha. Atakuwa amepata haki yake na litakuwa fundisho kwa wengine.

Na mlalamikaji ni nani?
Nchi imekuwa ya kijinga sana...
Yaani kuna machawa wanachukizwa ovyo ovyo kama wana mimba changa za mabosi wao
 
Back
Top Bottom