Msomi wa kiwango cha kimataifa wa Tanzania, Profesa Shivji ameshangazwa na kitendo cha wafanya biashara kuchaguliwa kuongoza taasisi za umma.

Shivji anasema sekta ya umma haiwezi kuchangamana na sekta binafsi.

Sisi wengine tumeshangazwa na uteuzi wa wafanya biashara na watu wenye maslahi binafsi kwenye bodi ya TANESCO. Yule mama Balozi ndie mwanzilishi mwenza wa kampuni ya Rex Attorneys ambao wanaiwakilisha Dowans na Symbion kwenye kesi ambazo TANESCO inashitakiwa na hayo makampuni halafu anateuliwa kuwa board member.

"Pamoja na kushirikiana na sekta binafsi, huwezi kuwaingiza wafanyabiashara jikoni wakupikie chakula cha umma!
Sekta ya umma na sekta binafsi hazilinganiki. Ni kweli huwezi kuendesha biashara kama idara ya serikali; pia ni kweli huwezi kuendesha serikali kama kitengo cha biashara."

Unaweza kusoma mwenyewe hapa.

View attachment 1954110


Uongozi wa nchi umeshapoteza 'legitimacy' kwa umma ni wazi bin dhahiri TANESCO tayrai imeshabinafsishwa kwa mlangoi wa nyuma. Hakuna mwananchi wa kawaida atakayeweza tena kupata huduma ya umeme kwa bei nafuu na kimsingi chama tawala kimekiuka mktaba na wananchi kupitia 'Ilani' ya uchaguzi 2020-2025.

Ni bayana kwa sasa migogoro ilikuwa inajitokeza kawa kutaka kukwamisha miradi na kuhujumu ulikuwa unafadhiliwa na uongozi uliojiweka kwa sasa na wananchi wataumia sana na hakuna mwanasiasa wa upinzani atajitokeza kuwasemea wananchi maana walikuwa pamoja kuhakikisha JPM hayupo na lengo walikamilisha hivyo hawana haja ya kupigania kero na shida zinazowakabili wananchi zaidi ya kuwaneemesha wafanyabiashara.

*Njia panda changua njia pana yenye kila kitu njiani dhid ya njia nyembamba yenye uhaba wa vitu vya anasa za kupita
 
Msomi wa kiwango cha kimataifa wa Tanzania, Profesa Shivji ameshangazwa na kitendo cha wafanya biashara kuchaguliwa kuongoza taasisi za umma.
Shivji anasema sekta ya umma haiwezi kuchangamana na sekta binafsi.
Sisi wengine tumeshangazwa na uteuzi wa wafanya biashara na watu wenye maslahi binafsi kwenye bodi ya TANESCO. Yule mama Balozi ndie mwanzilishi mwenza wa kampuni ya Rex Attorneys ambao wanaiwakilisha Dowans na Symbion kwenye kesi ambazo TANESCO inashitakiwa na hayo makampuni halafu anateuliwa kua board member.
Unaweza kusoma mwenyewe hapa.
C& P
JE NI HAKI MTU AMBAYE KAMPUNI YAKE INAISHITAKI TANESCO KUWA MJUMBE WA BOADI YA TANESCO,? WAANDISHI WA HABARI WASIWE VIPOFU,, WAFUKUE UKWELI
 
We unamchagua mpiga deal kama mwezi wa kwanza kuongoza wizara unategemea nini kama sio kupigwa
 
Naomba nielimishwe kidogo, hilo lipo katika katiba au ni mawazo binafsi ya Shivji? Yule Trump aliyekuwa Rais wa Marekani ana biashara dunia nzima, Vipi nchi iliathirika na ubiashara wake au ya kule nisiyahusishe na huku kwetu wenye nyeusi ngozi?

Mbowe ni mfanyabiashara na aliwahi kugombea uraisi, vipi km angepata Prof Shivji angekuja na maoni haya pia?!!
Akili umekosa ndio nachoweza kusema
 
Tatizo nilionalo mimi ni huko kuingiza watu ambao ama tayari wanasemwa semwa kwa kutilia shaka uadilifu wao au wale ambao kutokana na mgongano wa kimaslahi wanaweza kuleta ushawishi kwa bodi na menejimenti ili kupata upendeleo kwenye taasisi zao binafsi.

Wanazoziongoza lakini suala la shirika kujiendesha kibiashara mbona hata wakati wa Magufuli tuliambiwa shirika sasa linajiendesha kibiashara na kudaiwa kwamba sasa shirika halipokei tena ruzuku toka serikalini au ilikuwa changa la macho ili kumpamba mzee wa misifa?
Siku utasikia azam hawalipi bill za umeme ndio hapo tutapojua kuwa sisi ni washamba wa waarabu
 
You could be right. Tatizo kubwa la utendaji wa mashirika ya umma Tanzania halitokani sana na incompetence ya watendaji wala BOD. Bali ni viongozi wa kisiasa wenye hulka ya ufisadi. Power sekta imeteseka sana na hili. Ni juzi tu tumetoka “kufunika” suala la Tegeta Escrow (ambalo suspected top villains ndio hao hao). Ndio maana wamehakikisha hakuna kesi mahakamani. Zipo scandals nyingine zilivyofunikwa hivyo hivyo.

Hata uweke private sekta yote kwenye mgt na BOD ya TANESCO kama viongozi wa juu kisiasa wamelenga kufanya yao kama walivyofanya kupitia IPTL sahau habari ya ufanisi. Hapa, baadhi ya wateule kwenye hiyo BOD wanatia shaka mapema kwamba wana conflict of interest.

Labda pengine tusihangaike sana na hilo. Tupiganie kwanza katiba itakayodhibiti mikono ya wanasiasa kuingilia moja kwa moja shughuli za utendaji za mashirika ya umma na kutengeneza mazingira ya “state capture” ili kufanikisha ufisadi mkubwa.
Na katiba mpya unayoongelea wewe ni ipi?

Ya Kikwete(Bunge la katiba) au ya Warioba(katiba pendekezwa ya Warioba)?

Embu tuanzie hapo kwanza kuboresha mada.

Maana twaweza sema tunataka katiba mpya tukaishia kulishwa matapishi.
 
Naomba nielimishwe kidogo, hilo lipo katika katiba au ni mawazo binafsi ya Shivji? Yule Trump aliyekuwa Rais wa Marekani ana biashara dunia nzima, Vipi nchi iliathirika na ubiashara wake au ya kule nisiyahusishe na huku kwetu wenye nyeusi ngozi?

Mbowe ni mfanyabiashara na aliwahi kugombea uraisi, vipi km angepata Prof Shivji angekuja na maoni haya pia?!!
Mbona ilishawahi kutokea hapohapo Tanesco? Kuna Bosi mmoja make wake ndiye aliyekuwa anapewa Tender mbalimbali hapo kwenye Shirika. Na ilifanyiwa kazi. Hii inaitwa "Conflict of interest". Ni kosa kubwa. Ni sawa na Uhujumu uchumi.
 
Mbona ilishawahi kutokea hapohapo Tanesco? Kuna Bosi mmoja make wake ndiye aliyekuwa anapewa Tender mbalimbali hapo kwenye Shirika. Na ilifanyiwa kazi. Hii inaitwa "Conflict of interest". Ni kosa kubwa. Ni sawa na Uhujumu uchumi.
I mean "Mke wake"
 
Wewe pia hapa na ujinga wako! Balozi ana law firm ambayo inatetea kampuni zinazoishitaki Tanesco, huyo mama huoni kuwa katika Bodi ya tanesco si sahihi? Je, vetting imefanyika Sawa? Au kwa vile walimwajiri Ridiwani Kikwete wakati huo
Umemjibu vyema huyo oya oya
 
Msomi wa kiwango cha kimataifa wa Tanzania, Profesa Shivji ameshangazwa na kitendo cha wafanya biashara kuchaguliwa kuongoza taasisi za umma.

Shivji anasema sekta ya umma haiwezi kuchangamana na sekta binafsi.

Sisi wengine tumeshangazwa na uteuzi wa wafanya biashara na watu wenye maslahi binafsi kwenye bodi ya TANESCO. Yule mama Balozi ndie mwanzilishi mwenza wa kampuni ya Rex Attorneys ambao wanaiwakilisha Dowans na Symbion kwenye kesi ambazo TANESCO inashitakiwa na hayo makampuni halafu anateuliwa kuwa board member.

"Pamoja na kushirikiana na sekta binafsi, huwezi kuwaingiza wafanyabiashara jikoni wakupikie chakula cha umma!
Sekta ya umma na sekta binafsi hazilinganiki. Ni kweli huwezi kuendesha biashara kama idara ya serikali; pia ni kweli huwezi kuendesha serikali kama kitengo cha biashara."

Unaweza kusoma mwenyewe hapa.

View attachment 1954110



Kwanza tuweke wazi huyu mzee ni professor wa History si uchumi au biashara. Bodi anaweza akawekwa mtu yeyote mpaka pale tu ambako kuna maslahi binafsi.
 
Naomba nielimishwe kidogo, hilo lipo katika katiba au ni mawazo binafsi ya Shivji? Yule Trump aliyekuwa Rais wa Marekani ana biashara dunia nzima, Vipi nchi iliathirika na ubiashara wake au ya kule nisiyahusishe na huku kwetu wenye nyeusi ngozi?

Mbowe ni mfanyabiashara na aliwahi kugombea uraisi, vipi km angepata Prof Shivji angekuja na maoni haya pia?!!
Mkuu kwani hujui Trump ana kesi ya kukwepa kulipa kodi,alitumia cheo cha uraisi kukwepa kulipa kodi kibao na aliposhtukiwa akayaka ang'ang'anie madarakani ili apate kinga ya kutopelekwa mahakamani. Unapoteua mtu kama mtoto wa Bakhresa kwenye bodi ya Tanesco maana yake makampuni yake yaanzae kupata upendeleo maalumu,pia unapomteua aliyekuwa wakili wa kampuni za kitapeli zilizoinyonya Tanesco maana yake nini huyu February ni mpigaji wa juu kwa juu, sasa tunaona team ya wapigaji wakirudi kwa nguvu,Shivji yupo sahihi.
 
Back
Top Bottom