Paul Makonda Ameingia Mitini, hatahudhuria Power breakfast ya Clouds FM

Paul Makonda Ameingia Mitini, hatahudhuria Power breakfast ya Clouds FM

Swali la kujiuliza ,,,,huyo PAUL CHRISTIAN KISHITE wa Tabora FM,anatumia vyeti gani kwa sasa?
 
Hana la kusema maana ukweli unajulikana, lies has got it ends!
 
Awesome indeed...
Kufoji vyeti sio criminal offence...wala haihusiani na utendaji wa mkuu wetu wa mkoa aliyetukuka...
Nami nasema afoji tu, ikibidi hata cheti cha ndoa.
Mkuki kwa nguruwe.,ni muda sasa wakutuambia Yale Ben SAA kumi aliyoongea ni kweli au laa kuhusu thesis zenu na kama mange kimambo anayozua ni kweli au laa!! Sisi tulio foji vyeti mmetutumbua makazini na kupoteza stahiki zetu .,ninyi sasa ni zamu yenu kutumbuka.
Mtangazaji wa Clouds FM, Paul James amethibitisha kuwa Paul Makonda hatafika katika kipindi za Power breakfast (PB) Makonda alitarajiwa kujibu tuhuma za kununua cheti za Kidato cha nne.

Makonda amesema amepata dharura ya majukumu ya kiserikali.

Kutokana na kubanwa majukumu ya kiserikali Mh. Paul Makonda kwa leo hataweza kujibu tuhuma zinazomkabili hadi hapo siku nyingine itakapotangazwa tena.

Wewe ndio uiombe radhi kwa kuiamini radio ya wasanii
 
Binadamu wanafiki sana Jana baada ya PM kuitikia wito mkasema weeeeeeee kuwa ameitikia wito wa clouds na alipuuzia wito wa mahakama

Kaamua sasa kuwasikiliza Kwa maana ya kutokwenda mmeanza tena kulia lia ni sawa na wakati ule akiwataja wauza madawa mnalalamika asipo wataja mnalalamika

Ni ngumu sana kuwaelewa nyie watu kama ilivyo ngumu kumuelewa mwanamke
Tuambie wewe nani? Au popo.
 
Kibonde alipowaponda wanafunzi wa elimu ya juu kuhusu mikopo wanavyoitumia, haikuchukua hata siku 3 matokeo yake yakawekwa hadharani. Wadukuzi ina maana sasa hivi hawapo kumdukua huyu bwana mkubwa kwa taarifa anazotuhumiwa? Najaribu kutafakari kwa sauti tu
 
Ivi makunda atoke hadharani aje ajibu tuhuma anaejiita mage! siku hiyo nitamdharau sana.

Kwani aliyekuambia kuwa hili suala la Yeye kuwa na Cheti siyo chake limeanzishwa na Mange ni nani? Kwa taarifa yako tu kuwa Watu wenye Kazi / Shughuli zao walishawahi hata kupinga tu kuteuliwa Kwake ila nguvu ya ( wa Kunyumba ) iliwashinda na Jamaa akateuliwa. Ni vyema siku zingine kama haupo detailed juu ya mambo fulani uwe tu unatulia na kuacha WANAMUME waweke mambo hadharani.
 
nilijiandaa kumuuliza maswali mawili mazito........bahati yake kaingia mitini.
 
Nachotaka kujua Ndalichako matamko yameisha au hizi kelele hazisikii? Mwenye email au number za simu za huyu waziri tafadhali mtuwekee hapa tumfuate inbox direct.

Mkuu, nina hakika wameshaangalia taarifa zote tunazozisema hapa na wanaujua ukweli. I am just thinking, haiwezekani watu wa NECTA wakawa wanasoma maoni yote haya huku tukizungumzia majina ambayo wao wana taarifa zote wasioangalie. Tatizo ni watu kuwa waoga kupita kiasi, hasa wakishagundua kwamba taarifa zinazosemwa ni za kweli. Ni nani anaweza kumfunga paka .....? Usisahau msimsmo wa ovyo wa wanachama wa chama kile, maslahi ya chama chao ni muhimu sana kuliko maslahi ya taifa letu. Kwa hiyo kitu chochote kinachoonekana kuwa na madhara kwa chama chao, hakiwezi kuwekwa wazi kwa umma.
 
Mkuki kwa nguruwe.,ni muda sasa wakutuambia Yale Ben SAA kumi aliyoongea ni kweli au laa kuhusu thesis zenu na kama mange kimambo anayozua ni kweli au laa!! Sisi tulio foji vyeti mmetutumbua makazini na kupoteza stahiki zetu .,ninyi sasa ni zamu yenu kutumbuka.
Ungekuwa unajua kusoma katikati ya mistari ungeelewa nilichomaanisha... nadhani tumetofautiana uelewa hasa kwa hizi lugha za mafumbo.
 
Kupata dharura kwa binadamu kupo wala sio suala LA kukimbia
 
Back
Top Bottom