Operation Sangara: Chadema yajipanga Upya

Mchungaji,
Saa inakuja nayo ipo sasa ambapo sisiemu kwa sera zake za udini inakwenda kumalizwa. Unanielewa?
 
Operesheni Sangara yazoa kijiji cha Warioba







KAMPENI maalum inayoendeshwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), iliyopewa jina la Operesheni Sangara, jana ilizoa kijiji kizima cha Nyamuswa alikozaliwa kada wa CCM, Jaji Joseph Warioba.


Moto wa operesheni Sangara inayoendeshwa na Chadema kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa ulizoa watu takribani 1,500 wa Kijiji hicho cha Nyamuswa.


Operesheni hiyo huendeshwa kwa kufanya mikutano ya hadhara, ambayo Chadema inaielezea kuwa ni kwa ajili ya kuikomboa nchi kutoka mikononi mwa mafisadi.


Wakizungumza mara baada ya kukabidhiwa kadi za uanachama wa Chadema, baadhi ya wanachama hao wapya walisema wameamua kufanya hivyo baada ya kuchoshwa na ahadi hewa ambazo zimekuwa zikitolewa na CCM juu ya uboreshaji wa maisha ya wananchi walio wengi.


Christopher Matata, aliyekuwa kada wa CCM kwa muda mrefu, alisema licha ya utumishi wake uliotukuka ndani ya chama hicho, haoni mabadiliko yoyote ya kimaisha kwake binafsi na hata kwa jirani yake kama CCM ilivyoahidi wakati wa uchaguzi, hali inayoonyesha dhahiri kwamba chama hicho tawala hakina la maana kwa watu wake.


Wananchi hao walieleza kufikia maamuzi yao hayo kupitia mkutano wa hadhara katika kijiji cha Nyamuswa jana ambako Naibu Katibu Mkuu wa

Chadema, Zitto Kabwe alikuwa akihutubia. Walisema wamechukua hatua hiyo kukomesha uonevu dhidi yao.


Tukio hilo lilianzia majira ya saa 5:00 kwenye kijiji cha Nyakomogo na mamia ya watu waliojitokeza.


Hamasa zilizokuwa zikitokana na hotuba ya Zitto Kabwe na hasa kuhusiana na chanzo cha hali ngumu ya maisha kwa wananchi wengi, akiunganisha na matukio ya ufisadi, iliwachochea wanakijiji hao kujitokeza kurudisha kazi za CCM na kuchukua za Chadema.


Akizungumza katika mkutano huo, Zitto alisema katika operesheni yao hiyo ambayo pia inasimika mabalozi kila mtaa au kijiji wanachopita, zaidi ya wakazi 2,600 wa kijiji hicho walijisajili katika karatasi maalumu zilizoandaliwa na maafisa wa chama hicho na baadaye kukusanywa.


Zoezi la kusajili wanakijiji hao lilianza saa 5:00 na likaendelea hadi saa 12:00 jioni na ndipo takwimu hizo za wanakijiji waliopata kadi na wale waliojiandikisha lakini wakakosa na kuahidiwa kufikishiwa baadaye zitakapopatikana.


Akihutubia baadaye jioni kwenye mkutano wa hadhara katika eneo la stendi ya zamani mjini hapa, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe aliwataka Watanzania wote kwa pamoja kushikamana katika kudai haki yao inayoporwa kila siku na mafisadi waliojazana ndani ya CCM na serikali yake.


Ni kutokana na hilo Mbowe alisema kamwe chama chake hakitaacha kuipigia kelele serikali ya CCM inayoongozwa na Rais Jakaya Kikwete mpaka pale itakapoeleweka hatima ya Watanzania walio wengi, hata kama kitatishiwa na viongozi waandamizi wa serikali aliyoiita ya mafisadi hao.


Mwenyekiti huyo alisema kinachomfanya apige kelele ni ufujaji wa fedha unaofanywa na viongozi wa serikali ya CCM akisema inatafuna fedha za wananchi huku wenye mali walio wengi wakitaabika katika dimbwi la umasikini wenye kuandamana na kupanda kwa gharama za maisha zinazopanda kila kukicha.


Operesheni hiyo maalumu ina lengo la kuwahamasisha wananchi kujua haki na wajibu wao, sambamba na kufanya mabadiliko ya mfumo wa utawala.
 
Wakati mwingine huwa nafurahishwa sana na maneno yanayotumiwa na wanasiasa. Kwa kweli huyu aliyekuja na hii term ya operation sangara ninampa tano kwa creativity ya hali ya juu sana aliyoonesha.

operation sangara..... sangara.... inakumbusha mbali sana miaka ile ambayo serikali ya Mwinyi ilianza kupuuzia wanafunzi wa boarding school na kuishia kuwalisha ugali (sima) na maharage (changarawe) kwa mwaka mzima (hakuna mboga wala matunda). Hii ilileta msemo wa kimaramara - sima na vimol(r)o AKA sangara.

Sangara ilitumiwa kama alternative ya maharage (usiniambie kuwa maharage ni mboga).... kazi kweli kweli
 
Ukiona chama tawala kinafuata/kinaiga kitu kilichoanzishwa na chama cha upinzani, kwa hakika huu ndio mwanzo wa anguko la chama tawala. Ni ushahidi wa wazi wa kukosa mwelekeo au dira kwa CCM.

Wasomi walioko huko sisiemu hamkisaidii chama chenu? Au mpo huko kuganga njaa zenu tuu?
 
Ukiona chama tawala kinafuata/kinaiga kitu kilichoanzishwa na chama cha upinzani, kwa hakika huu ndio mwanzo wa anguko la chama tawala. Ni ushahidi wa wazi wa kukosa mwelekeo au dira kwa CCM.

Wasomi walioko huko sisiemu hamkisaidii chama chenu? Au mpo huko kuganga njaa zenu tuu?

Maneno matupu hayavunji mfupa.
 
Date::11/19/2008
Operesheni Sangara: yasaidia Chadema kuingia vijijini




Mwenyekiti wa CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe akihutubia wananchi.
Na Mussa Juma


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Oktoba 19 mwaka huu, kilizindua operesheni Sangara, katika mji wa Musoma mkoani Mara.


Operesheni hii ya Chadema, ilizinduliwa katika uwanja Mkendo na kuhudhuriwa na mamia ya wakazi wa mji wa Musoma na vitongoji vyake.


Wazo la kuanzishwa operesheni hiyo, lilipatikana mjini Mwanza mapema mwaka huu baada ya viongozi wa juu ya Chadema kufanya ziara na mkutano wa hadhara katika mkoa huo.


Mara baada ya mkutano huo, hoja zilitolewa za kuwapo matawi ya chama kila mahali, uwepo wa viongozi kuanzia ngazi za mabalozi na hivyo ili iwe rahisi kuendesha siasa zenye tija na ushindi siku zijazo.


“baada ya mawazo mengi kutokea ndipo tuliamua kuanzisha operesheni hii na mwanzo tulipanga izinduliwe mkoani Mwanza ila kutokana na historia ya kipekee ya mkoa wa Mara na ushindi ya kishindo tuliupata Tarime tuliona ni vyema kuanzia mkoa huu

huu,” anasema Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.


Chadema kimepanga kuitumia Operesheni hiyo katika mkoa wa Mwanza ili kuibua vuguvugu jipya la mageuzi hadi ngazi za vijiji likilenga kuhamasisha wananchi kuwa kitu kimoja na kutetea rasilimali na nchi na kupinga ufisadi.


Akizindua operesheni hiyo hivi karibuni, katika wilaya, kata na vijiji vya mkoa wa Mara, Mbowe anasema nchi inakwenda pabaya, hivyo Chadema wameona haiwezekanii kukaa kimya na kuacha mambo yaendee kuendeshwa kama ilivyo hivi sasa ndivyo sivyo.


“Ndugu zangu nchi yetu inakwenda pabaya…serikali ya CCM imeshindwa kuwapa Watanzania maisha bora na mafisadi ndio wanatamba hivyo lazima tuunganishe nguvu bila kujali itikadi, tukombowe nchi yetu,” anasema Mbowe.


Anasema lengo la operesheni sangara ni kupeleka madaraka kwa wananchi kuanzia ngazi za vijiji, hadi mikoani bila kusimama na kuwa kitu kimoja ili kuikomboa Tanzania kiuchumi.


Mbowe anasema, kushindwa kwa serikali ya CCM kuleta maisha bora licha ya kuwa nchi ina rasilimali za kutosha kunatokana na wasaidizi wa Rais Jakaya Kikwete kujali maslahi yao binafsi na kuacha taifa likiteketea.


“Sisi Chadema tumeamua kuja kwenu wananchi kuwaeleza nchi yenu inakwenda pabaya na

tutakuwa pamoja majumbani kwenu, katika vijiji vyenu hadi kieleweke,” anasema Mbowe.


Anasema nchi imejaa ufisadi hivyo matumaini ya watanzania kwa Rais Jakaya Kikwete ambaye aliingia madarakani kwa kura nyingi yametoweka kabisa.


“Ndugu zangu tusifanye tena makosa mwaka 2010 tushikamane tuiondowe CCM madarakani kwani chama hiki hakiwezi tena kuleta maendeleo kwa watanzania kwa sera zile zile,

watu wale wale eti kwa kauli mbiu ya ari mpya na nguvu mpya,” anasema Mbowe.


Katibu mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilbroad Slaa alikuwa akifafanua kitendo cha serikali kushindwa kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wa ufisadi mapema kuwa ni kasoro kubwa kwa serikali ya CCM.


Anasema pamoja za serikali ya Rais Jakaya Kikwete kutoa maagizo mbali mbali kuhusu ufisadi, lakini hadi sasa bado hali ni mbaya na ufisadi unaendelea.


“kuna ufisadi mkubwa katika nchi hii... hapa mkoani Mara kuna ufisadi wa Sh155 milioni katika mgodi wa Buhemba kupitia kampuni ya Meremeta inayomilikiwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ),” anaeleza Dk Slaa.


Dk Slaa anasema kuna tuhuma nyingi za ufisadi ambazo wamezitoa lakini wanashangaa serikali inashughulikia suala EPA pekee.


Dk Slaa anasema ni jukumu la wananchi kusimama kidete na kushinikiza mafisadi wote wachukuliwe hatua zinazostahili.


“Operesheni hii inalenga kuwapa changamoto kila mmoja wetu ajuwe wajibu wake…sisi sote ni Watanzania tuna haki sawa hakuna ambaye ana haki kubwa zaidi ya mwingine hivyo ni lazima sote tudai haki hizo bila kujali itikadi zetu,” anasema Dk Slaa.


Upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe, alikuwa akihimiza umoja kwa vijana bila kujali itikadi zao kwani wao ndio watapata shida miaka ijayo.


“CCM na viongozi wake wamechoka hata kwa mawazo hivyo ni jukumu letu sisi vijana kuungana

na kuwang’oa madarakani,” anasema Kabwe.


“Tuna rasilimali nyingi lakini hazitunufaishi Watanzania….tuna madini lukuki, wanyamapori, samaki na ardhi nzuri lakini vyote havitunufaishi kutokana na sera mbovu za CCM na serikali yake,” anasema Kabwe.

Kikubwa kilichopatikana katika operesheni hiyo ya Chadema ni kufanikiwa kufika hadi vijiji wakati huu kabla ya uchaguzi na hivyo kupata wafuasi.


Hali hii ni dhahiri itazidisha upinzani kwa chama tawala katika chaguzi zijazo kwani kwa miaka mingi vyama vya upinzani vimekuwa viking’ang’ania mijini pekee na vijijini kuiachia CCM kutamba.

 
Hakuna shaka kila mtu atakubali michango na pia harakati za chama hiki cha CHADEMA zimechangia kwa kiasi kikubwa kwa mafisadi wengi kutiwa ktk hati hati hata kama si dizaini ile ya akina Mramba lakini jamba jamba na tumbo joto
HONGERA CHADEMA
 
Safi sana CHADEMA, kujisimika vijijini ndilo jambo la msingi, hongereni kwa kulitambua hilo, ila sasa mnatakiwa muwe wabunifu zaidi pamoja na kuonyesha mapungufu ya CCM ambayo kwa sasa imestuka na kuanza viini macho?/sijui kweli? vya kujisafisha inabidi mueleze na kuwasomesha wana vijiji maengo ya chma chenu na mikakati ya kuwaondolea umasikini ulio wagubika kwa miaka kibao!

Wape na kuwaonyesha watu mwanzo wa matumaini.
 
Zitto amshutumu Waziri Malima kwa kumpinga Spika

Na Paulina David, Mwanza

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Kabwe, anamtetea Spika Samwel Sitta, kwa kusakamwa na Waziri Adam Malima.

NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Kabwe, amesema kuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Adamu Malima, hakupaswa kutoa kauli ya kumpinga Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Samwel Sitta, kuhusu uwazi kwenye mikataba ya madini.

Zitto, ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini alitoa kauli hiyo jana kwenye Viwanja vya Sahara, wakati akihutubia wananchi wa Jiji la Mwanza kwenye Operation Sangara.

Alisema Malima hakupaswa kumjibu wala kumpiga Spika Sitta kuhusu mikataba ya madini kuwekwa wazi na kupelekwa bungeni kwa ajili ya kujadiliwa na wabunge, kwa sababu inahusu rasimali ya taifa.

Alisema kauli ya Malima juu ya mikataba hiyo kuhusiana na mambo ya biashara haina mantiki yoyote, kwa sababu wawekezaji wanaokuja kuwekeza wanawekeza kwenye ardhi ya Watanzania na wanachochuma ni rasilimali ya yao, hivyo wanapaswa kuijua mikataba inayotiwa saini na Serikali.

Zitto alisema Malima hakupaswa kumjibu Spika kutokana na umri wake na nafasi ya uspika aliyonayo katika nchi hii na kusisitiza kwamba, kwa kauli yake ameonyesha kushindwa kumheshimu spika na muhimili muhimu nchini.

“Spika anaongoza wabunge zaidi ya 360 na bunge ndicho chombo cha kutunga sheria na kuisimamia serikali, hivyo kauli ya Wziri Malima inaonyesha jinsi asivyoli liheshimu bunge ambalo ni muhimili muhimu katika nchi hii,’ alisema na kuongeza:

“Hivi Malima ni nani katika nchi hii ambaye anaweza kupingana na kauli ya Spika ya kutaka mikataba ya madini inayotiwa saini na serikali kufanywa kwa uwazi na kupelekwa bungeni. Hivi jeuri hiyo ya kumjibu Spika ameitoa wapi?”

Alisema kuwa yeye binafsi anakubaliana na kazi kubwa inayofanywa na spika na anaiunga mkono, kwa sababu ameleta mabadiliko makubwa katika bunge hadi kufikia hatua ya Waziri Mkuu wa nchi kujiuzulu kutokana na kutowajibika.

Alisema kutokana na hali hiyo ni lazima suala la mikataba ya madini lifanyike kwa uwazi kwa sababu ni mali ya Watanzania, hivyo hakuna sababu ya kufanywa kwa siri.

Aidha, Zitto alisema kuwa inasikitisha kuona walimu wanalalamikia serikali kwa kushindwa kuwalipa madai mbalimbali yakiwemo malimbikizo ya mishahara, huku serikali ikisamahe mabilioni ya fedha kwa wawekezaji wanaomiliki kampuni mbalimbali za madini hapa nchini.

Alisema kutokana na hali hiyo, ni wazi kuwa serikali imeshindwa kusimamia ipasavyo rasilimali za nchi na kuwafanya watu kutoka nje kunufaika na utajiri wa nchi wakati Watanzania wakiendelea kuwa masikini.

“Ndugu zangu hakuna mtu anayekataa wawekezaji hata mimi nawakubali, lakini ambao hawalipi kodi na ambao wanaochukua rasilimali zetu bila ya taifa kupata chochote hawanafaida kwetu na hakuna sababu ya nchi kuwa na wawekezaji wa aina hii,” alisema Zitto.
 
Date::12/13/2008
Polisi wazuia Operesheni Sangara kuzinduliwa Mbeya
Na Brandy Nelson
Mwananchi

JESHI la Polisi wilayani Mbeya limekizuia Chama cha Demkokrasi na Maendeleo (CHADEMA) kufanya mkutano wa uzinduzi wa Operesheni Sangara mjini hapa leo kwa madai kuwa halielewi maana ya neno hilo.

Chadema ilizindua Operesheni Sangara, ikiwa ni mkakati ambao chama hicho kinauelezea kuwa ni wa kuikomboa nchi kutoka mikononi mwa mafisadi na ilizinduliwa katika siku ya kuadhimisha tarehe ya kutangazwa kwa orodha ya mafisadi wanaoitafuna nchi na ambao baadhi yao wamefikishwa mahakamani kujibu tuhuma za wizi wa fedha za umma.

Tayari operesheni hiyo imeshafanyika katika mikoa ya Kanda ya Ziwa baada ya kupata kibali cha Jeshi la Polisi, lakini chombo hicho cha dola wilayani Mbeya kimedai badi hakijaelewa dhana hiyo ya Operesheni Sangara, ikiwa ni siku chache baada ya katibu mkuu wa CCM, Yusuf Makamba kukiri kuwa mkakati huo wa Chadema ni sumu.

Barua iliyoandikwa na Jeshi la Polisi wilayani Mbeya yenye kumbukumbu namba MB/A.24/30.B/232 na iliyosainiwa na mkuu wa polisi wa wilaya, SP Msuya, inamuelekeza katibu wa chama hicho cha upinzani wilayani hapa asifanye mkutano huo kutokana na kutoelewa maana ya neno la "Oparasheni Sangara".

“Tumepokea taarifa yako ya kuhitaji kufanya mkutano wa hadhara Desemba 13, mwaka huu saa 8:00 mchana hadi saa 12:00 jioni kwenye viwanja vya Ruanda Nzovwe jijini Mbeya. Hata hivyo, tumeshindwa kuelewa madhumuni ya mkutano huo hasa kutokana na neno Oparesheni Sangara lililotumika ambalo hatulifahamu nini maana yake na nini malengo yake," inaeleza sehemu ya barua hiyo

Barua hiyo imeeleza kuwa kutokana na utata huo polisi imeshindwa kuelewa
ni vipi itajipanga kuandaa ulinzi wa mkutano huo na kwamba kutokana na mazingira hayo wanaelekeza kwamba mkutano huo usifanyike kwa tarehe hiyo hadi hapo watakapopata ufafanuzi wa maandishi wa maana ya neno Oparesheni Sangara ili waweze kufanya tathimini ya ulinzi kulingana na malengo ya oparasheni hiyo.


Akiotoa ufafanuzi wa Oparesheni Sangara, katibu wa Chadema wa hapa, Rehema Mgimwa alisema kuwa barua aliyoliandikia jeshi hilo ni kuomba kibali kwa ajili ya uzinduzi wa Oparesheni Sangara na kwamba oparesheni rasmi itaanza Desemba 17, 2008.

Alisema kuwa kwa ufafanuzi Oparesheni Sangara ni ziara maalum za kujenga Chadema, kuhamasisha uwajibikaji wa viongozi na kutetea rasilimali za taifa na kwamba neno Sangara ni jina la samaki ambalo linawasilisha azma ya chama kuweka mkazo wa kuhakikisha rasilimali za nchi zinawanufaisha Watanzania.

“Opareshen Sangara inakwenda sambamba na kuhamasisha wananchi kujiunga na Chadema na inasimamiwa na uongozi wa taifa na ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa Chadema wa mwaka 2006 mpaka 2010 wa kueneza chama na sera zake kwa umma na kuhamsisha mabadiliko kwa lengo kuweka tuamini jipya la demonkrasia maendeleo,” alieleza.

Aidha alisema kuwa Oparesheni hiyo inatarajia kuzinduliwa na viongozi wa taifa wa Chadema, wakiongozwa na mwenyekiti Freeman Mbowe.
 
CCM si kawaida kama republican wengine duniani tu. Mabavu kwa sana. No democracy and freedom granted by our constitution. BUT the end is very very close.
 
Huyo Mkuu wa polisi ni mwanasiasa tena inawezekana anakadi ya chama kwa siri na anajiandaa kugombea cheo fulani baada ya kustaafu upolisi. Lakini na hao Chadema kulikuwa na umuhimu gani kuandika maneno ya sangara kwenye barua yao? si wangeandika mkutano wa hadhara tu!
 
Mimi naona mkuu wa huyu wa polisi alikuwa sahihi kabisa kuzuia operation Sangara, kama barua aliyokuwa amepelekewa haikutoa ufafanuzi wa nini Operation Sangara. Hivyo sababu zilizotolewa na Mkuu huyu ni za msingi kabisa, kwani ni lazima apange ulinzi kulingana na aina ya operation. Nafikiri huyu ni moja ya watu ambao wanafanya kazi kwa kufikiri na siyo kwa mazoea. Hongera sana Bw. Msuya
 
Bado hakija haribika kitu,watapata mana na operation itaendelea ahaaaaaaaaaaa sijui kuna kimomo kilienda au ndio utendaji makini ati na shangaa kwa sababu viongozi hupelekewa magazeti ofisini yanayolipiwa na kodi zetu sasa sijuhi hawakuwahi kusoma hii operation sangara.Ok wapewew maana kwa barua kama walivyodai simple.
 
Maneno ya Makamba na Chiligati kwambva CCM ni Chama tawala kina kila kitu wanajivunia kutumia mabavu ila wakielezwa kwamba wao ni watawala hadi kwenye EPA na Kagoda wanawaka moto .Sasa wanasema nini na asubuhi wanatenda nini? Wamechelewesha tu hawataweza kuzuia na wanawapa wananchi moyo wa kujazana wakitoka hapo wanahamia kwenye kampeni za Ubunge kazi wanayo CCM .Hivi kweli kuna mwanadamu anaweza kuikinga mvua ikinyesha kwamba yote iilingie katika ndoo yake ya maji pekee ?
 
Back
Top Bottom