Kwanza unatakiwa uwe na malengo! ni nini kilichompeleka mkeo Merekani wakati wewe unaishi Tanzania?
Kama ni ujana na ma-adventure, ntakuelewa.
Maisha ya Merekani ni tofauti na maisha ya kwetu. Unaweza ukapata kazi ukalipwa vizuri, lakini, Jee, fedha ndio kila kitu?
Hivi mkeo kuwa mbali nawe kwa sababu tu za kipato! huoni kuwa hapo kuna tatizo, anaweza akabamizwa huko na wewe ukabamiza huku! hapo kuna faida?
Kuna rafiki yangu, alimpeleka mkewe mkewe kutafuta maisha kama miaka kumi iliyopita, bahati nzuri au mbaya, yule dada sasa ana watoto wawili, wa nje ya ndoa.
Kuna sababu maalumu za kumpeleka mtu nje ya kwao. Kama kusoma au matibabu na hata maisha lakini, utazame maisha yako ya sasa na unategemea yepi huko uendako?
Kuna dada mmoja namjuwa alikwenda Merekani, kama miaka mitatu sasa, lakini huyu alikwenda na malengo. Aliondoka hapa ni muathirika wa HIV, kenda kule sasa anapata tiba namba moja. Wanawajali sana wenye maambukizi, matibabu ni first class kwa wenye virusi. Huyu halaumiki kwa kwenda huko. Si unajuwa hapa tunavyo nyanyapaa wagonjwa?
Kama unaenda popote pale, uwe na malengo! la sivyo, mrudishe mkeo muhangaike hapa bongo yetu, bado kuna opportunities nyingi sana. Usiwasikilize Chadema, watakupoteza.