Simulizi ya Vita: Mwanzo baada ya Mwisho by M.Kitua

mBONEASenior

Member
Feb 4, 2023
37
32
HABARI WANA JF.

SEHEMU YA 1

MWANZO BAADA YA MWISHO ....

Watu walikuwa wakifa, wengine wakikimbia, wengine wakijikuta kuna miguu mikubwa kama ile ya vunjachungu(parying mantis) ikitenganisha miili yao na wengine wakihangaika kupambana na wanyama ‘beasts’ wakubwa kuliko wao walio wazidi maumbile, wakiwachezea kama vile simba anavyochezea chakula baada ya kukiwinda.

“No! No! Hatuwezi kufa kirahisi hivi!” nilijesemea lakini hata nikisema hivyo hakuna litakalo badilika mbele yangu kwani hata mimi mwenyewe pamoja na Armor ‘ngao’ niliyokuwa nimevaa bado haikuweza kuulinda mkono wangu wa kushoto ambao ulikwapuliwa wakati nikipambana na Hellhound, mbwa mkubwa urefu wa kipimo cha mwanadamu, mwenye meno makali yenye sumu ambayo kwa sasa ilishaanza kusambaa mwilini.

Nchi nzima ilikuwa kwenye hali ya kukosa matumaini kwani baada ya tangazo la Onyo lililotolewa na serikali kabla hata ya GATE kufumuka ambalo lilikuwa juu ya uso wa dunia kufunika Afrika Mashariki yote, Gates ndogo ndogo zilikwisha lipuka na kuachia viumbe wote waliokuwa upande wa pili kumwagika. Hichi kitendo cha Gates (Mlango unaounganisha dunia yetu na dunia zingine) kufumuka ndicho wazungu walichokiita Gate Explosion na ndicho kilichoitokea dunia.

“Jayden!” Niliisikia sauti ikiliita jina langu ikija mbele yangu. Kiukweli hata kuona vizuri nilikua sioni tena kwa maana sumu ilikua imekwisha anza kufika mpaka kichwani.

“Lisa!” Niliita kinyonge baada ya kuona kabisa naishiwa nguvu mwilini. Upanga niliokuwa nimeushikilia wenye makali pande zote na kishikio kilichopambwa kwa dhahabu ambao sasa umejaa damu ya purple iliyotoka kwenye mwili wa jibwa hilo ndiyo uliokuwa ukinipa sapoti nisianguke na hapohapo Lisa aliyekuwa amevalia ngao yake iliyokua ikifunika mwili wake mzima na kumfanya aonekane kama malaika alinidaka.

“Usianguke, Jay! Ukianguka wewe na taifa zima linaanguka!” Alisema huku akiniegemesha chini pembeni na jengo ambalo lilisha kwisha angushwa chini likibaki kama gofu na hapo hapo akaanza kunipa matibabu.

“Hahaha! Sio kwamba wewe ndiyeutakayeanguka?” Nilisema kiutani hali ingawa nilikuwa sina nguvu. Nilijua kabisa kuwa Lisa alikuwa akijihisi vibaya kwa kuona namna nilivyo huku mkono wangu ukitiririsha damu pale uliponyofolewa.

Lisa alikuwa amebarikiwa nguvu ya “HOLY HEAL” ambayo ilikuwa ikimtenganisha na watu wengi sana duniani kwani ilimfanya awe na uwezo wa kuponyesha magonjwa, majeraha, hadi viungo vilivyokatwa na kufanya viote upya lakini kwa kulipia kitu.

“Hapana Lisa, usitumie Heal juu yangu! Wewe mwenyewe wajua sina system ya kunisaidia kuuimarisha mwili wangu kama walivyo Hunters wengine. Usipoteze nguvu zako kuni-heal.” Nilimwambia, nikijaribu kumkatisha tama asifanye alichokua anataka kuanza kufanya.

“Kwa hiyo kama huna system ndio nikuache? Kati ya hao hunters unaowasifia wakati huu wako wapi?” Aliuliza huku akinitazama kwa huruma. Macho yake mazuri yakilengwa na machozi.

Ni kweli HUNTERS ambao ndiyo wanaopaswa kupambana na MONSTERS wanaotoka kwenye gates walikua na system ambayo ilikua ikionekana kwao peke yao tu na hakuna mtu mwingine ambaye angeweza kuiona. System hii ilikua kulingana na maneno ya watu tofauti wanasema ni kama kajikioo kanakokuwepo mbele ya macho yako. Haka kajikioo kalikuwa kakitokea pale tu utakapo tamka maneno maalumu STATUS WINDOW, hivyo katajitokeza mbele ya macho yako na kukupatia ripoti nzima ya ukuaji wa mwili wako kiuwezo, kuanzia Agility (Spidi na wepesi wa mtu), Strength, Vitality, Mana, Health, Level aliyopo, na idadi ya skills alizokuwa nazo. Lakini kwangu mimi hata sikuwa nayo.

Sikujaliwa nayo hiyo system. Ni kama vile ilinitenga kwani hata baada ya kufanya taratibu zote ili niweze kuwa Hunter kama walivyo wengine bado sikuipata na niliishia kujijenga mwenyewe kuanzia kuongeza nguvu za mwili wangu hadi kutengeneza namna ya kuweza kuufanya mwili wangu uweze kubeba mana.

“Lisa usifanye hivyo!”

“Tulia, Jay! Tafadhali tulia kama ulivyo niku-heal! Embu angalia tu hapa tulipo. Unaona hunter yeyote aliye hai?” Alisema Lisa huku akinikazia macho ambayo yalionyesha kabisa kutokuwa na matumaini kwani ndiyo ulikuwa mwisho wa nchi yetu. “Kila mmoja wao amekwisha kufa, tumebaki sisi tu. Hunters wa guild yetu wako mbali na sisi na nina uhakika wao wenyewe wamebanwa kuja kutusaidia.”

Nyuma yake kulikuwa kumelala miili ya watu ambao walikuwa wamenyumbuliwa viungo vyao na kutenganishwa vichwa na viwiliwili vyao huku wengine wakiwa chali juu ya magari yaliyokuwa yameharibika kwa kutokana na vita vilivyokuwa vimefanyika kati yao na monsters kutoka Gate moja lililokuwa juu ya uso wa nchi. Lilikuwa kama duara kubwa jeusi lililofanya anga kutanda rangi ya damu hata jua lilikua limefunikwa na viumbe wakubwa kama ndege wakipaa angani jamii ya Wyvern ambao walikuwa kama nusu dragons. Jiji zima la Dar es Salaam lilikuwa likiuona mwisho wake kwani hakuna binadamu niliyemuona zaidi ya mimi na Lisa.

“Najua umekata tama kama mimi lakini, wewe ndiye kimbilio letu la mwisho kwa watu ambao bado wapo hai wamejificha kutokana na kwamba hawana uwezo wa kupambana.” Alisema Lisa huku akitazama macho yangu ambayo yalikuwa yakiona damu baada ya kovu nililolipata kichwani kutiririsha damu mpaka zikaingia machoni.

Ghafla alikamata sura yangu na kisha kunipiga busu la mdomoni ambalo sikulitegemea. Maumivu yote niliyokuwa nikiyahisi mwilini yalikata ghafla. Ni kama vile mawasiliano ya mwili yalipotea na kilichobaki kufanya kazi ulikua ulimi wangu peke yake. Mabusu yalikaa takribani dakika mbili huku tukiwa tumefumba macho lakini machozi yaliyokuwa yakitiririka kutoka kwenye uso wa Lisa yaliangukia mashavuni mwangu na mimi nikamtazama huku akiendelea kufurahia busu alilokua akinipa.

“Sijui kama hili litafanikiwa lakini ndiyo njia pekee ya mwisho niliyobakiwa nayo.” Alisema Lisa baada ya kutenganisha mdomo wake na wangu huku akianza kufuta machozi usoni mwake. Nilijihisi vibaya sana kwani hata nguvu nilizokuwa nazo za kunyanyua mkono wangu niliobakiwa nao ziliniisha.

“Umefanya nini Lisa!” niliongea kama mshangao lakini hakunijibu bali ghafla alianza kung’aa mngao kama ule wa jua ambao ulikua mkali sana hadi kunifanya nifumbe macho.

Punde sauti ya ngurumo ya kama vile monsters wote waliokuwa karibu waliuona ule mwanga aliokuwa akiutoa kwenye mwili wake. Nilijaribu kusimama ila nikashindwa na hata kuunyanyua upanga wangu sikuweza. Mwili ulikuwa umeishiwa nguvu kabisa. Kulikuwa hakuna matumaini. Mtikisiko wa ardhi ukaanza kuwa mkubwa kuashiria kabisa monsters wote walikuwa wakija kuelekea tulipo.

“Lisa!” niliita ili kumwambia akimbie angalau nife peke yangu kuliko kufa wote. “Lisa, run! Sina nguvu ya kunyanyuka kukimbia na wewe Lisa, please run uniache hapa, nitabuy time for you!” niliongea huku nikijitahidi kujisukuma hivyo hivyo mpaka nikaanguka kwenye magoti yake Lisa ambaye sasa alikuwa kama jua. Mwili wake mzima ulikuwa uking’aa mpaka kutoa joto kali. “Lisa!”

“Jay my dear! I love you.” Alisema Lisa huku akigeuza uso wake kuangalia uso wangu uliokuwa kwenye magoti yake tena huku akitabasamu. Sikujua alikua akitaka kufanya nini lakini nilijua kabisa kuwa ndiyo mwisho wangu kukutana na Mtanzania ambaye yawezekana kuwa wa mwisho kabisa nchini kuwa Hunter kwenye janga hili, tena mbaya zaidi moyo wangu ukaanza kuniuma kwani kitendo cha yeye kukiri mbele yangu kuwa ananipenda kilionyesha dhahiri kabisa kuwa alitamani kuendelea kuwepo lakini hakuwa na jinsi zaidi ya kufanya alichokuwa akitegemea kufanya baada ya kuufanya mwili kung’aa kiasi kile.

Monsters wote waliokuwa wakija kwetu walikua washafika na walipotuona tu pale pale wakaturukia. Haikuwa Hellhound, mbwa mwenye manyoya meusi kama giza au Ratkings, panya buku wakubwa size ya jogoo, au nyoka ambao wangeweza kutumeza tukiwa tumesimama, wote walikuwa wakitaka kuturukia na kutugombania.

“Ha!” Nilihema kwa nguvu nikijua kabisa ndo mwisho wetu na hamna ambaye angeweza kutusaidia kwa hali tuliyokuwa nayo! Hunters kutoka mabara mengine walishakwisha ombwa kuja kutoa msaada lakini hata kabla ya Gate kubwa ambalo lilikua juu ya Afrika Mashariki nzima kufumuka hakuna hata mmoja aliyejitokeza kutusaidia. Wote walitupuuzia tena kwa kejeli kabisa wakionyesha wazi wazi kuwa hawataisaidia nchi yoyote ile ya Afrika hasa nchi zilizopo Afrika Mashariki. Tulikuwa tumetengwa.

Ile tunakaribia kuraruliwa, mimi nikiwa nimeukumbatia mwili wa Lisa aliyekuwa aking’aa kama jua, mwili wake ghafla, uliganda kama barafu na punde ile ile, ukalipuka kama bomu la nuclear na kutawanyisha kila monster ambaye alikuwa karibu yetu ndani ya mile mbili nzima. Hadi majengo, magari na kila kitu kilichokuwa karibu yetu kilifutwa juu ya uso wa ardhi.

“Lisa?” Niliita kwa kuzinduka huku nikishangaa kuona niko peke yangu. Hakuwepo Lisa wala monster yeyote aliyebaki. Mwili wangu pale pale ukarudiwa na nguvu zilizokuwa zimenitoka. Mkono wangu wa kushoto uliokuwa umekwapuliwa ukiwa umeota mwingine mpya. Majeraha niliyokuwa nayo yote yakiwa yamepona.

“Is this why you said goodbye like that?” nilijiuliza nikiangalia mchanga kama majivu yaliyokuwa yamenisambaa nilipokuwa nimepiga magoti. “I am sorry Lisa! I am really sorry I wasn’t able to save you too!” nilijikuta machozi yakianza kunitiririka. Yalikuwa machozi yenye maumivu makali sana kwani nilianza kukumbuka kila mtu niliyempoteza ambaye alikuwa wa muhimu kwangu. Nilianza kulia kama mtoto mdogo tena kwa sauti kabisa bila ya kujali kuwa kunaweza kukawa na monsters karibu ambao hawakusafishwa na mlipuko uliotokea mimi nikiwa epicenter kabisa. Nililia sana.

“If only I was stronger!” nilijiambia huku nikihisi kama vile Mungu amenitenga mimi na nchi yangu kwani gate lililokuwa juu angani lilikuwa limeizunguka Tanzania nzima bila kuacha pande yoyote ila na kwenda hadi Sudan ya Kusini, na kuimeza Nusu ya Congo mashariki na nchi za Malawi na Mozambique.

‘ROOOOOAAAAAARRRRR!’

Ilikuwa ngurumo kubwa sana kiasi kwamba nadhani watu waliokuwa upande mwingine wa dunia wangeisikia. Ilikuwa sauti ya kutisha sana. Iliifanya ardhi kutikisika kama vile ilikuwa tetemeko la ardhi ambalo lingeifanya dunia kupasuka na kumeza kila kitu. Mgandamizo uliokuwa ukisababishwa na kiumbe kilichokuwa kikitaka kutoka kwenye geti lililokuwa angani likifunika jua ulikuwa sio wa kawaida. Ni kama vile gravity ilikuwa imezidishwa mara kumi. Majengo yaliyokuwa mbali na mimi yalikuwa yakiminywa chini kiasi kwamba yalikuwa yakibomoka na kuanguka.

Taratibu bonge la kichwa lilijitokeza kama kuchungulia upande wetu wa dunia. Lilikuwa bichwa likubwa jekundu kama damu, lenye uso kama wa mbwa, meno makubwa size ya ghorofa la Posta, na pua ambazo zinaweza kumeza mibuyu mitano bila shida. Hali ya hewa ilibadilika palepale na ngurumo kali zilikuwa zikisambaa pande zote za nchi na pale tu lilipotokea jicho lake la njano kama uji wa volcano, ardhi iliyumba jinsi navyo lilivyocheza. Ilikuwa ni hali ya kutisha sana.

Hasira zilianza kunibubujika ndani kwa ndani. Najua kabisa sio kwamba siku zingine zote zile sikuwa na hasira dhidi ya monsters waliokuwa wakifurika juu ya uso wa dunia, lakini kwa muda huo nilijihisi kabisa kukombwa na hasira za watu wote waliokufa nchini. Labda kwa mtu mwingine angehisi ilikua ni hisia tu lakini kwangu kwa muda huo haikua hisia ya hasira tu bali ilikua ni hisia za hasira za wafu wote waliokufa kwa sababu ya monsters na kunyimwa msaada na nchi ambazo zilikuwa na uwezo wa kutusaidia. Nilijihisi kama nimeshikwa mkono na watu wote hao waliokufa kwenye mikono ya monsters.

Nguvu zilinijaa. Kiwango changu cha Mana nilichokuwa nacho mwanzo kilifurika maradufu kana kwamba nilikuwa nahisi kama nina bahari ya mana ndani yangu isiyoweza kuisha.

“Siwezi ruhusu kiumbe kama hicho kushuka hapa duniani.” Nilijiambia kwa sauti nikilitazama likiumbe ambalo nilikuja kugundua lilikuwa ni dragon king kwani dragon wa kawaida alikuwa na size ya urefu wa ghorofa tatu za floor ishirini na ukubwa wa ghorofa saba ila hili hapa, jino lake peke yake lilikuwa na urefu wa ghorofa moja lenye floor ishirini.

Macho yangu yalituwa kwenye mpini wa panga langu ambalo lilikuwa limevunjwa vunjwa kutokana na mlipuko wa mwili wake Lisa. Niliiukota na baada tu ya kuugusa, pale pale likajitengeneza upanga wa mana ambao ulikua uking’aa sana. Ilikuwa mara yangu ya kwanza kufanikisha kitu kama hicho ambacho Hunters wale wenye manapool kubwa wajulikanao kama Rankers huweza tengeneza. Walilipa jina ya Mana Sword na ukubwa wake ulitegemea na kiwango cha mana mtu ambacho anacho.

“Lisa! Thank you very much. Najua ni wewe umeunganisha watu wote hao na kunipa nguvu kiasi hichi.” Taratibu nikaanza kupiga hatua huku macho yangu yakilitazama jicho la Dragon King lililokuwa likizunguka kama kukagua dunia na ngurumo ikitoka kwenye kinywa chake.

“I promise to enact revenge on every one of you na kuzilinda familia zenu zilizobaki hai. Nitawapatia tumaini.” Hasira niliyokuwa nayo ilijizidisha mara tano yake tena hadi kusababisha mmwili wangu wote kujawa na rangi ya njano kunizunguka.

Ili kuweza kufika angani lilipo geti linalo mruhusu Dragon King kujitokeza, ni lazima nifikie urefu wake hivyo njia rahisi ya kulifikia si nyingine zaidi ya kupanda ghorofa. Kwa uwezo niliojaliwa na Lisa na wengine wote waliotangulia nje ya uso wa dunia, kukimbia kwa spidi ya radi lilikuwa jambo dogo sana kwani nilijihisi mwepesi kupita kiasi. Nilihisi kabisa mwili wangu ukitengeneza radi ambayo ilianza kuichapa ardhi nilipokuwa nikikanyaga na ikitoa sauti ya kama radi zinazopiga makofi huku nikianza kuchochea mwendo kwani tayari lile dragon lilikwisha anza kutoa mkono nje na kuongeza ngurumo kabisa.



* New York City *


“Tuko hapa tukiwaletea taarifa live kabisa kutoka Tanzania ambapo SSS-Level Gate Explosion imetokea ndani ya siku mbili tu tokea geti kutengenezeka.” Ilikuwa sauti ya mtangazaji mzungu wa chombo cha BBC akiwa anatoa habari huku kamera zilizokuwa nyuma yake zikionyesha jinsi hali ilivyo huko Tanzania.

“Jesus Christ! Isn’t that the Dragon King that High Rankers have been evading from the gate in Holland?” Mmoja kati ya watu waliokuwa bar huko New York City alisema akiwa na wenzake wote wakiishangaa tv iliyokuwa imening’inizwa juu maeneo wanapohudumiwa na pub.

“Yeah! Ndio lenyewe! Isn’t the gate way bigger than how it was two days ago?” mwingine naye akatupia comment huku wote waliokuwemo humo ndani wakianza kujadili jinsi geti lilivyopanuka sana. Ilikuwa ni hali ya kutisha na kusikitisha sana.

Nje ya bar humo barabarani kwenye junction ambazo watu walikuwa wakivuka barabara magari yakiwa yamesimama wakitazama TV za matangazo zilizo kwenye magorofa zikionyesha habari hiyo hiyo na watu wakitoa macho yao kusikiliza utafikiri hawako nje barabarani.

“Hali sio shwari baada ya hii clip iliyoonyesha mlipuko katikati ya jiji la Dar es salaam na kusawazisha eneo lote ndani ya maili zaidi ya mbili. Mwana habari mwenzangu aliyekuwepo huko White House anasema kuwa serikali ya Marekani inakana kuhusika na mlipuko huo na wanakiri kutokutuma aina yoyote ile ya bomu la nyuklia hivyo kutia watu kwenye mshangao kuwa ni nini kilicholipuka.”

Mwana habari huyu sio kwamba labda alikuwa juu ya helikopta au ndege, la hasha, bali walikuwa wakitumia Drones zenye uwezo wa kutembea masafa makubwa huku zikiongozwa kwa remote ili kuongeza usalama wa wana habari na kutokuwatia kwenye matatizo.

“Russia pia nayo imekana kuhusika na swala hilo la mlipuko hivyo kusababisha sisi kuwa na theory kuwa yawezekana ikawa ni skill ya hunters wa Kitanzania wakipambana na monsters ambao wako chini.” Aliongea mwanahabari huyo huku televisheni ikionyesha sehemu ya mlipuko ulipotokea dakika kadhaa zilizopita.

“Oh God!” Ilisikika sauti za watu wakina mama na wakina baba humo New York wakishtuka kwa hofu baada ya kusikia ngurumo kali sana na kubwa ambayo ilitoka kwa Dragon King ambaye sasa amekwisha anza kutoa mkono nje.

“They are dead now!” ilisikika sauti ya mtu mwingine akisema huku akiitazama tv iliokuwa ghorofani ikilionyesha Dragon King likijitokeza na jicho lake. Dunia ilihisi kusimama.

Muda kidogo, watu kwenye chaneli zingine walianza kuziponda serikali za nchi kubwa kama Marekani na Russia, na kwenye mitandao ya kijamii wakaanza kuwaponda Rankers ambao walikuwa wakifahamika kwa uwezo wao mkubwa wa kimapigano huku wakisema kuwa wamewaacha watu Waafrika kupambana wenyewe wakati wanajua fika kabisa kuwa Afrika bado haina Hunters wenye uwezo wa kupambana na Dragon King.


* LONDON *


“I mean like seriously! Did you not hear them? The rankers intentionally refused to give aid to Africa and the American government diligently agreed with their thoughts without even begging them to go help!” alisema mtu mmoja kwenye simu ya mwanadada ambaye alikuwa amekaa kwenye treni ya mwendo kasi huko London ikielekea Mjini akitazama na waliopembeni yake.

“High Rankers? To me they just look like cowards afraid of giving help since they can’t defeat a dragon.” Alikuwa akisema huku akiwaponda sana High Rankers duniani kote na sio yeye peke yake, watu wengi kwenye treni walikuwa wakitazama watu kama hao huko Instagram jinsi wanavyo wakashifu high rankers ambao walikuwa wakijisifu kama walinzi wa dunia.

“Angalia jinsi nchi hiyo ya Tanzania ilivyopotea hata kwenye ramani ya satellite inaonyesha kabisa jinsi ilivyosawazishwa. Serikali za kiafrika ziliomba msaada kutoka Marekani, Ulaya na Urusi ili waweze kuwasaidia kupunguza maafa na kudili na monsters waliotoka kwenye mageti madogo madogo. Je, hizo nchi zilizo ombwa msaada ziliutoa huo msaada?”

“Nasikia pia waliombwa kusaidia kuwatoa raia na kuwahamisha kwa mbinu za usafirishaji mpaka nchi nyingine kabla ya mapambano dhidi ya monsters kutokea na wakanyimwa. Tena usafiri wa ndege kwa wale waliotaka kuhama nchi ulizuiliwa na nchi za nje, kumaanisha kuwa, nchi zote za Ulaya, marekani, urusi na bara la asia tumewatelekeza majirani zetu waafrika.”

Hili swala liliwagusa watu wengi sana duniani mpaka kusababisha maandamano kuomba serikali za nchi husika kuruhusu raia kutoka nchi za Afrika kuhamia kwa muda nchini mwao lakini maandamano yao hayakufanikiwa.


*WHITE HOUSE, WASHINGTON DC *



Watu walikuwa wamesimama na mabango yaliyoandikwa, “SAVE AFRICA” huku wakipiga kelele ikulu ya marekani, White house lakini waliishia kufukuzwa na kuambiwa wasubiri swala hilo linajadiliwa.

“We are sad to all American citizens with relatives from Africa for what is happening out there but as you can all see through media means, there is no way for any transport method capable to help the affected African countries where the SSS-Level Gate has appeared to reach them. Therefore we are sad to announce that the only means we have to help them is to pray for them that may God save them from this tranquil.”


Hiyo ilikuwa sauti ya Rais wa Marekani akihutubia wananchi wa Marekani ambao walikuwa wakitegemea akitoa maelezo ya msingi lakini maelezo aliyoyatoa yaliwafanya wananchi wake kupandwa na hasira na kuanza kumtupia mayai na vitu vingine huku akimaanisha kuwa kutokana na geti hilo basi wasingeliweza kusaidia nchi husika.



* UN Europian Branch, GENEVA *



“What about Rankers? Are you saying that they are not capable of going there to aid the remaining African Hunters?” alikuwa mmoja wa wananchi aliyehudhuria hotuba nyingine huko Ulaya iliyowekwa na UN.

“We- We- aaah- we….” Ni kigugumizi tu kilichosikika cha mhutubiaji ambacho kilionyesha wazi kabisa kuwa siyo kwamba hakuwa na majibu bali hao High Rankers wanao wazungumzia wako zao wanakula bata na hawana mpango wakuwasaidia Africa. Jambo hili lilileta kelele sana hadi kusababisha Muungano wa UN kutishiwa kutetereka maana hata shirika la Hunters – Hunters World Union, lilikuwa limeziba masikio yake ili lisiwasikilize wote wale wanaowaombea Waafrika kusaidiwa.

Mataifa kama Israel, Egypt na South Africa yalituma hunters wake lakini kwa bahati mbaya walibidi kurudi nchini kwao kwani hali ya nchini kwao pia zilikuwa tete kwani baada tu ya geti lililotokea Afrika mashariki kuonekana, mageti madogo madogo kwenye nchi zingine za Afrika yalianza kulipuka hivyo kusababisha msaada wa Waafrika kwa Waafrika kuwa mdogo na kusababisha vifo vya hunters wengi wa kiafrika. Bara zima la Afrika lilikuwa likiwaka moto.

Conspiracy theorists (wale watu wanaojua kutunga njama na kuzidadavulia) wakaanza kutoa theory zao juu ya swala ambalo liliwafanya watu wenye akili na huruma juu ya bara la Afrika kuanza kutilia mashaka mataifa yao.

“mageti makubwa kama hili la SSS-Class husababisha mageti mengine yanayoendana ki frequency kuanza nayo kukuwa na kusababisha kufurika hadi kupasuka. Hii ni kumaanisha kwamba, geti kama hili lililotokea lilipaswa kuathiri dunia nzima. Lakini cha ajabu ni nini? Linaathiri Afrika peke yake, na tena linaathiri hadi mageti ambayo hayaendani kifrequency, kitu ambacho hakiwezekani.”

Mpaka hapo tu, watu wengi duniani wakaanza kupata jibu moja. THIS MAY NOT BE A NATURAL OCCURANCE. Kumaanisha kuwa yote yale yanayotokea barani Afrika hayajatokea kiasili kama vile linavotokea tetemeko la ardhi, au kimbunga, au hata kunyesha mvua ambayo ni maswala yasiyokuwa ndani ya uwezo wa kibanadamu.

Hapa watu wakaanza kuwaogopa wanasiasa duniani kote, wakaanza kuhisi kama kweli yanayotokea Afrika yamesababishwa na mtu au kikundi cha watu, basi hao watu huenda wakawa wana uwezo wa ajabu, au ni hunters au hasa Wanasiasa. Macho ya dunia nzima yakaanza kuogopana.

Kitendo cha kuweza kusababisha geti kufumuka ni kitendo ambacho kinatakiwa kiwe cha kimungu, lakini ghafla watu wanaanza kusikia kuna mtu au watu ambao wanaweza kusababisha mageti kufumuka!? Watu wakaanza kuyumba kisawa sawa maana walianza kuogopa kwamba huyo mtu anaweza akaamua tu kuangamiza nchi Fulani na nchi hiyo ikafutwa juu ya uso wa dunia bila ya hata watu kujua na wakahisi ni hali ya kimungu kumbe ni mtu ameamuru kitu hicho kutokea kwa kusababisha mageti makubwa kufumuka.

Taarifa zote hizi zilikwisha sambaa hata kabla ya geti lililokuwa likisababisha nchi za Afrika mashariki kutokupata jua ndani ya siku mbili nzima kufumuka hivyo watu wengi walianza kuona kabisa, mtu ambaye amesababisha nchi kubwa kama Marekani kuwanyima ruhusa waweze kuhamia nchini mwao kwa muda ndiye amesababisha haya yote yakatokea na Jay hakuwa nyuma kitaarifa


One Day Ago –


* Tanzania, Dar es Salaam. The RESISTANCE GUILD HQ *

“So what? Doesn’t that mean all those countries are in cahoots with whoever that person is?” Alisema bwana mmoja mweusi hivi ambaye misuli yake ilijichora hadi nje ya armor aliyokuwa amevaa. Alikuwa mrefu kiasi na alikuwa mwenye hasira sana ila uwezo wake ulikuwa ni mkubwa sana hivyo kundi ambalo Jay na Lisa walikuwemo lilimchukua.

“Giedon, usiseme hivyo! Hiyo ni conspiracy tu!” Aliongea guild leader Danny, ambaye ndiye aliekuwa kiongozi kundi hili waliloliita The Resistance Guild. Lilikuwa ni kundi kubwa ingawa lilitengenezwa ndani ya mwaka mmoja lakini lilikua na hunters wa mataifa tofauti tofauti wakiwemo Wachina, Wajapani, hadi Wamerakani ambao waliamua kuishi Afrika wakiwa wameipanda kwa dhati kabisa.

“Danny yuko sahihi Giedon. Kumbuka sisi ndiyo wenye shida, sasa tukianza kuwahisi hadi tunaowaomba msaada vibaya basi hali yetu ya kusaidiwa itakuwa mbaya zaidi.” Alisikika mrembo mweupe pisi kali Lisa Mtanzania ambaye alikuwa ameegemeza kichwa chake kwenye mikono yake juu kwenye meza ambayo walikuwa wamekaa wanakikundi wenye nguvu kwenye kikao hichi waliokuwa kumi na tatu.

Sauti yake nyororo ilimfanya Giedon hata yeye pamoja na makelele yake yote ajishushe kidogo huku watu wakimwangalia mrembo huyu mwembamba ambaye armor yake ingawa ilikuwa imefunika mwili wake wote lakini iliufanya mwili wake uonekane hasa kifua chake kilichoshiba kana kwamba ukikiangalia unajiona kama utaogelea. Siye Giedon tu hata mimi mwenyewe sikua salama kwenye swala zima la kudoea doea kinachoonekana.

“But what if haya yote ni ya kweli?” Aliuliza mwanadada mwingine mrembo mweusi kiasi ambaye yeye armor aliyovaa haikumficha chochote. Kifua chake kilikua wazi kabisa, kikizibwa sehemu tu kidogo na ngao hiyo yenye mchanganyiko wa mistari ya chuma yenye nyekundu na nyeusi. Alikuwa akitambulika kama Joan The Berseker.

“Hata kama ni kweli, mnadhani mtaweza kwenda kupambana na mtu mwenye uwezo wa kusababisha Gate Explosion?” Aliongea Danny tena. Mjadala ulionekana kuwa mzito sana kwani hali ya wana kikundi haikuwa nzuri kwa sababu ya hofu na kuchoka pia kwani hata masaa si mengi wametoka kulifunga geti lililofumuka Kisiwani Unguja na kusababisha kisiwa kizima kuzama. Malumbano yalikuwa makali sana hata mimi na wanakikundi wengine ambao tulikuwa tumesimama pembeni kuwazunguka viongozi wetu waliokuwa wamekaa tuliona kabisa hakuna uwezekano wa sisi kufanikiwa kwenye hili ila sasa walikuwa wanatoka kwenye mada iliyokisababisha hichi kikao kikaliwe.

“So what should we do?” Ukimya ulitanda ghafla na majadiliano yakakata pale pale na wote wakanigeukia kunitazama. Ngao yangu iliyokuwa imechoka utafikiri imeokotwa ilisababisha watu kuniangalia kwa dharau.

“Sidhani mtu ambaye hana hata status window anaruhusiwa kuwepo kwenye hichi kikao.” Ilikua sauti yenye kebehi ya Joan huku akisababisha hadi watu wengine kuniangalia vibaya.

“Ivi unafanya nini humu ndani? Kwanza ulitakiwa usiwe hunter kabisa hata kama unayo mana na unaweza kuitumia. Kitendo cha wewe kutokuwa na System inayokuonyesha status window ilitakiwa iwe sababu moja kubwa ya kukufukuza kwenye guild.” Alikuwa ni Giedon zamu hii ambaye aliongea kama vile yeye ndiye mwenye mamlaka kwenye kundi zima.

“Giedon!” Aliita Lisa huku akionyesha hasira kwa Giedon na kuonyesha kunionea huruma mimi. Nisiseme uongo, nilijihisi vibaya sana Giedon alivyoongea hivyo lakini ulikuwa ukweli tena ukweli unaouma sana kwani ingawa nilikuwa na uwezo mkubwa wa kupambana lakini bado nilikuwa nikinyanyaswa sana ndani ya guild letu. Walikua wakiniona kama vile nimekosea njia kuwa Hunter, na nilitakiwa kuwa muuza supu ya pweza.

“Lisa usijali.” Nilisema huku nikisogea mbele ili watu wanione vizuri. “Kwa hiyo Guild Maste Danny, kwa sababu lengo letu sio kufanya upelelezi kujua kuwa ni kweli kuna mtu anafanya mageti kufumuka au la, unaonaje tukaweka strategy ya kupambana na mageti yote yaliyobaki nchini na nchi za jirani kabla geti kubwa kuliko yote linalotuzibia jua halijafumuka?”

Maneno yangu yaliwashangaza wengi kwani niliongea kijasiri sana utafikiri mimi ndo kiongozi sasa hata mimi mwenye nilijihisi kajasho kakiteremka mgongoni kwa jinsi Danny alivyonitazama na kuniona kama vile namtoa kwenye nafasi yake ya uongozi.

“Nakubaliana na Jayden! Point yake iko sahihi kabisa. Hatujaja hapa kudiscuss kuhusu Wamarekani wanaokataa kutusaidia wala Waingereza waliotunyima msaada.” Alisema Lisa na kwa sababu watu wengi walikuwa wakimkubali waliishia tu kuitikia kwa vichwa kwa lile alilosema.

“So, una strategy yoyote ya kutusaidia?” Aliniuliza Danny huku akiniangalia kwa kuashiria nirudi nyuma kidogo maana nimesimama karibu naye sana.

“Ipo moja tu ambayo itatutatulia matatizo mengi kwa wakati moja.” Nilisema huku nikikunja mikono na wote walianza kunitolea macho kusikiliza nitasema nini.

“Ongea basi we mshenzi acha kupoteza muda!” kwa hasira nilishangaa nikifokewa na Joan ambaye alipandisha miguu yake juu ya meza na kusababisha kijigauni alichokuwa amevaa kushuka na kuacha mapaja yake yote wazi. Ni kitendo cha yeye kupanua tu miguu kidogo na tungeona kilicho katikati ya miguu hiyo milaini ya maji ya kunde.

“Ehm!” ilinibidi nijikoholeshe ili macho ya watu yabadilishe mwelekeo na kuniangalia mimi niliyekuwa nimesimama katikati ya Danny na Lisa ambao walikuwa wakiiangalia ramani ya Afrika mashariki iliyojuu ya meza.

“What mostly depends on this strategy is speed!” Nilianza kuielezea strategy yangu huku viongozi wote wakiwa wametega masikio kunisikiliza hata Giedon na Joan walisogea karibu kuona ninachoonyesha kwenye ramani. Hapo hapo baada ya kikao kuisha tu wote wakaanza kufuata strategy niliyowaelekeza maana ilikuwa yenye mshiko hadi kukosa upinzani.

Strategy ilikuwa ikiwahitaji viongozi wale wenye spidi kuliko viongozi wote kwenda kutoka Dar es Salaam mpaka mpakani mwa Kenya na Tanzania na wengine mpaka mpakani mwa Mozambique na Tanzania kumaanisha Mtwara. Wakisha fika humo watapanga msitari viongozi wote kwenye usawa na bahari na kisha tutaanza kuizunguka Tanzania nzima kama vile tunaifagia.

Walio katikati wataenda kwa kuifinya nchi, yani kumaanisha wataingia ndani ya nchi kutoka Dar na kuingia Dodoma mpaka kufika mwisho wan chi mpkani mwa DRC na Tanzania na tutafunga geti lililoko Ziwa Tanganyika kwa kuwa ndilo kubwa kuliko yote. Tutatengeneza kama mshale tukipitia nchi nzima.

Ilikuwa strategy ngumu kwa kuitazama kwa haraka haraka lakini pale walipokuja kugundua kuwa Viongozi wenye spidi kushinda wote wanaweza kufika Kilimanjaro na Mtwara ndani ya nusu saa tena bila kutumia nguvu nyingi, swala likawa rahisi, ukijumlisha pia kuwa kuna Portal inayoiunganisha Miji mikubwa nchi nzima hivyo wale wanaotoka katikati kufika Dodoma mpaka Kigoma ilikuwa rahisi sana.

“Hatutawasaidia majirani zetu?” Aliuliza Danny huku watu wote wakionyesha umakini na kukubaliana na strategy yangu.

“Nadhani wao ndiyo wanaopaswa kutusaidia sisi kwa sababu ukiangalia eneo zima ambalo geti lililopo juu yetu…”

“Death Gate!” Aliongea bwana mmoja hivi mwenye shombe shombe hivi mwenye armor ya kijani tupu na nyeusi aliyeitwa Joses huku akitabasamu kwa kufurahi kupata jina la kuliita geti lililojuu ya vichwa vya madari ya nyumba zetu.

“Yes, The death gate! Eneo lote hilo limeimeza Tanzania nzima bila hata ya kuacha eneo kidogo la jua kupita na Tanzania ndiyo inayoonyesha kuwa na mageti mengi kuliko hata Kenya au Mozambie au hata Congo!” Nilimaliza kutoa maelezo na watu walikubaliana nayo.

Kazi nzima iliisha ndani ya masaa saba peke yake. Kumaanisha kuwa mageti yote yaliyokuwa yakikaribia idadi ya mageti hamsini na nne kila moja lilichukua takribani dakika nane na kusafiri kwenda geti lingine lilipo ilichukua dakika tano hadi sita.

Hapa mtu akikuambia kuwa Hunters walikuwa na uwezo wa ajabu usishangae kwa kuwa system walizokuwa nazo zilikuwa zikiwasaidia kufidia nguvu ambazo mwanadamu wa kawaida hakuwa nazo na hakuna mtu hata mmoja ambaye alibahatika kujua kuwa system hizi zimetokea wapi kwani mara tu baada ya mageti kuanza kutokea duniani miaka kumi na tano iliyopita, ndipo hizi system ambazo zilikuwa zikionekana kwa hunters peke yake zilipoanza kuonekana.

Watu wengine walianza kusema kuwa labda mageti ndiyo yanayosababisha watu kuwa na uwezo wa namna hiyo wa kupata system na wengine ambao theory yao ilipata mashiko zaidi ni waliosema kuwa, dunia ndiyo inayosababisha watu kupata hizo systems kwani ni namna ya kuwasaidia binadamu kuweza kuzishinda nguvu zinayoivamia dunia.

Hunters walikuwa wakipata nguvu nyingi sana pale wanapofanikiwa kuuwa monsters na kufunga mageti hivyo kupelekea mfumo mzima wa dunia kuzunguka kwa hunters kwani kama si wao kupata nguvu kupitia system basi dunia ingekuwa imeisha.

Strategy ilianza saa tisa kamili mchana na iliisha saa tatu za usiku pale ambapo tulikutana Dodoma kundi zima kwa ajili ya kujipongeza na kupumzika. Ingawa angani kulikuwa na geti, haikujalisha na watu waliendelea na shughuli zao za kawaida bila ya kujali wakiamini kabisa kuwa hata kama geti hilo litafumuka basi haitakuwa leo, hivyo ya leo yafanyike leo ikiwemo swala zima la kula bata.

Nilikuwa nimesimama zangu tu pembeni nikitazama jinsi viongozi na wanakukindi wenzangu wanavyokula zao bata bila ya kijali geti lililojuu ya vichwa vyao. Nilikua si mnywaji wa bia sana na sikuipendelea kwa kuwa ilikuwa ikinitia ukakasi hivyo nilikuwa nimesimama zangu pembeni nikiwa nawaangalia wanakikundi wakinywa bia utadhani wanakunywa maji hasa Giedon na Joan ndiyo walikuwa viongozi. Ukiwatazama wanavyoshikana shikana nina uhakika hata wewe ungedhani wapenzi maana walikuwa wakibebana kwenye mapaja kama vile wanabinuana. Sikumuona Lisa ingawa nilitamani hata naye angekuwa akifurahia hata kama hatujui kesho yake itakuwaje.

“Mbona umesimama peke yako?”

“Ah, Lisa! Za jioni hii?” Alinishtua sana kwani sikutegemea kumuona kabisa na kitendo cha yeye kuja kuniongelesha ndicho kilichonifanya nikamsalimia utadhani naenda kuomba kazi benki maana nilikakamaa ajabu.

“Hahaha! Acha hizo basi. Mbona umekakamaa utadhani uko jeshini? Kuwa tu kawaida tukiwa pamoja hivi.” Wow! Ndilo wazo lililokuja kichwani mwangu pale macho yangu yalipoanza kumkagua Lisa. Alikua amevaa kimini-jeans cheusi kilichoacha mapaja yake yote yaonekane na t-shirt ya Chelsea nyeupe huku akiwa ameshikilia chupa ya wine kubwa aina ya Soliera Rose na kuidubua kidogo kisha kuhema kwa msisimko baada ya kuinywa.

Ingawa ni usiku maeneo haya tuliyokuwepo ya mtaa wa Dodoma Mjini ila kwa uzuri aliokuwa nao Lisa na weupe wake nina uhakika ungeumwa moyo papo hapo.

“Hahaha! Jamani, unataka kumaanisha mimi ni mrembo kiasi hicho?” Alisema huku akianza kuona aibu kwani aliona kama vile ninaweza kumtoboa kwa namna macho yangu yanavyomshangaa.

“Si mrembo tu, ni mrembo kupindukia!” Ha!!!!!????? Nilijikuta nikishangaa kimya kimya kwani sikutegemea kama nitaweza kuongea hayo maneno kwa sauti, nilijua nimejiongelea akilini kumbe nimeyaropoka. Hata Lisa mwenyewe hakutegemea kwani aibu ilimzidi palepale. “Ah, sorry! Sorry! Namaanisha… Ah!” Yani hata maneno yakufanya hali iliyokuwepo ipungue yalikuwa hayaji kichwani.

“Asante!” Nini!!!????? Nilijikuta nikishangaa tena. Sikutegemea kwa mara nyingine tena kwamba mrembo kama huyu ambaye guild zima linamtamani hadi guild master mwenye anamtolea macho kuwa angeitikia na kunishukuru kwa kumwambia kuwa ni mrembo.

“Ah…Ah, Your wel-welcome! Hehehe!” Yani sio kwa ushamba niliokuwa nauonyesha mbele ya huyu mrembo, kwani hata aibu aliyokuwa akiionyesha pia ilikuwa ya kunifanya nianze kuwaza vitu ambavyo vilikuwa haviwezekani kama vile kujihisi labda huyu mtoto ananipenda. Yani hilo swala lilikuwa gumu sana.

Tuliendelea kupiga story kwa muda kidogo huku nikijaribu kuweka topic za kumtongoza lakini kwa aibu aliyokuwa akiiweka nilikuwa nikihisi labda ninamfanya asijihisi comfortable kuwa na mimi, lakini wakati tukipiga story kuna mtu alikuwa akiniangalia kwa macho makali kana kwamba hata nilihisi anaweza akaniua ila sikujua ni nani kwani sikumuona.

Baada ya lisaa na nusu tu watu wote wakawa wameenda kupumzika kwa kuwa kazi waliyoifanya leo ilikuwa kubwa san, hata kama walishirikiana na guilds ndogo ndogo lakini bado kazi ilikuwa ni nzito hivyo walikuwa wamechoka sana.


WIIIIIIWUUUUUUU WIIIIIIIWUUUUUUU WIIII….


Ilikuwa ni king’ora ambacho huwekwa kila sehemu ambayo ina makazi ya watu kuashiria kuwa kuna geti ambalo linafumuka na monsters watakuwa wakianza kutoka hivyo watu waende kwwenye maeneo yaliyoandaliwa ya kujifichia.

“Ugh! Kuna nini?” Alikuwa ni Joses huyo akishangaa ni kitu gani hicho kina sababisha kuamka wakati usingizi haujamtosha.

“The Death Gate! It’s the Death Gate!” Moja kati ya member wa kikundi alianza kupiga kelele ndani ya hoteli ambayo tulikodi kwa pamoja (jina la hoteli) na kusababisha hata wale ambao walikuwa wakipiga maji kusimamisha shughuli yao kwa muda na kuchungulia dirishani kwani walichokiona kilizitisha nafsi zao.

“MUNGU WANGU!” Ulikuwa ni mshangao wa watuambao walitoka nje kushuhudia kile kilichokuwa kikendelea angani kwani monsters walianza kumwagika bila ya kukoma kutoka angani.

Watu walianza kukimbiakimbia kama kuku waliochinjwa vichwa. Hunters waliokuwa wamekwisha amka walianza kuwasaidia watu kukimbilia kwenye safe zones ambazo zilikuwa zimekwisha andaliwa kwa ajili ya matukio kama haya lakini kazi yao iligeuka ngumu pale ambapo monsters walianza kumwagika juu ya vichwa vyao. Ukiona hali ambayo ilikuwepo naamini hata wewe mwenyewe ungekosa nguvu na ungehisi kama ndicho kile kiama kilichokuwa kikitabiriwa.

Mapanya makubwa kama kuku yalikuwa yakianguka kutoka juu mbinguni, mambwa marefu usawa wa kimo cha mwanadamu nayo vivyo hivyo na viumbe vingine vya ajabu vivyo hivyo. Ilikuwa ni mvua, mvua ya viumbe waliokuwa wakimwagwa kutoka juu na mengi ya lipotua chini yalirojeka kwani yalikuwa hayana namna yakupunguza kasi yaliyokuwa yakianguka nayo. Yalipasuka pasuka sana na ambayo yalibaki na ahueni ni viumbe ambavyo vilikuwa na mabawa kama Wyverns ambayo yalikuwa kama mijibwa ila yenye mabawa na mengine mengi.

Hali haikuwa shwari.

“Lisa! Lisa! Lisa yuko wapi?” Niliita kwa wasiwasi huku nikiuliza kile niliyekutana naye lakini hakuna ambaye alikuwa na majibu. Hivyo ikabidi nikimbilie chumba ambacho nilimsindikiza masaa machache yaliyopita kwenda kulala. Usishangae bwana nilinyimwa kitumbua kwa hiyo ilinibidi nirudi nikajilalie zangu ndiyo maana unaona nahangaika kumtafuta kwani kati ya watu wote ambao walikuwa wakinijali kwa dhati japo ya mimi kuwa mtu asiye na system, yeye alikuwa namba moja. Chumba chake niligonga ila hakikujibiwa hivyo niliuvunja mlango lakini hakuwemo ndani, na ile natoka tu nikakutana na Danny ambaye naye alikuwa anakuja kumwangalia.

“Lisa yuko wapi?” Aliniuliza kwa jazba sana na kunikwida kola ya armor niliyokuwa nimevaa huku watu wakitupigapiga vikumbo kwani walikuwa kwenye hemuhemu ya kuikimbia hoteli kuwahi safe zones. Kilichonishangaza ni kwanini guild master ananikwida wakati na mimi nimekuja kumtafuta Lisa kama yeye. “Nakuuliza tena Lisa yuko wapi?”

“Sijui yuko wapi Danny! Kwa nini unanishikilia hivi?” Nilimuuliza kwa sauti kali kwani niliona kama vile ananivunjia heshima hata kama yeye ni guild master.

“Wewe ndiye uliyeondoka naye jana kumaanisha kuwa ulikuja na ukalala naye!” The https://jamii.app/JFUserGuide????? Nilishangaa sana kwani niliona wivu uliokuwa ukimchoma huyu bwana na ndipo nilipogundua aliyekuwa akinitoboa mgongo kwa macho alikuwa ni yeye lakini nilimuelewa kwani kila mtu alikuwa akimtamani sana Lisa sio kwa uzuri na shepu aliyokuwa nayo.

“Brah! Aliyekuambia nimelala naye ni nani kwani?” Nilimuuliza Danny kwa hasira hadi akaanza kujishtukia na kulegeza mikono kwani sio kwa kunikwida kwa nguvu zake zote. “Mimi sijalala naye aisee, huyo aliyekuambia hivyo basi amekosea sana kwani mimi nilimsindikiza tu na kisha nikaenda kujilalia chumbani kwangu.”

Danny alijishtukia kweli kwani alitia aibu sana mbele yangu na baadhi ya guild members waliokuwa wakitupita kwenye hiyo korido ambayo ilikuwa floor ya tatu ya ghorofa ya hii hoteli.

“Kwa hiyo yuko wapi sasa!?” Aliniuliza baada ya kuniachia na kuanza kuniangalia kwa hasira.

“Mimi sijui ndiyo maana unaniona namtafuta!” Nilimjibu na hapo hapo nikaanza kuondoka. Sikujali kuwa alijihisi vibaya kwa kuwa sikumuonyesha heshima kama Guild master wala nini kwani nilishaanza kumuona kama vile mtu ambaye ameteswa na mapenzi naye hakunifuata bali alishika njia yake.

“Joan!” Niliita baada ya kufika chumba ambacho nilikuwa na uhakika kilikuwa cha Joan na bila hata kugonga mlango kwani hiyo hali iliyokuwa nje haikunihitaji kugonga mlango na nikauvamia hivyo hivyo ila sekunde chache tu nilijutia kutokugonga mlango hata kama ilikuwa ni situation iliyohitaji uharaka.

“For https://jamii.app/JFUserGuide’s sake, Guys!!!!” Niliita pale pale kwani macho yangu yalishuhudia kitu ambacho huaga naonaga xvideos peke yake na sijawahi kukiona live. Joan alikuwa akiendesha gari la mwamba huku mkongojo wa Giedon ukiwa ndani kama gia na walikuwa uchi wa unyama kabisa kitandani wakila uroda bila ya kujali yale yote yaliyokuwa yakiendelea huko nje.

“Oh, kumbe ni Jay, mshamba wa kijijini asiye na system!” alikuwa Joan huyo aliyeongea kwa kuniangalia huku macho yake yamelegea kwa raha alizokuwa anazipata huku matiti yake yakicheza cheza kila akiwa anapanda na kushuka kwenye bamia la mwamba Giedon.

“Oya vipi mwamba? Hujawahi ona mtu akiliwa kitumbua au?” Alikuwa Gideon huyo ambaye baada ya kusema hivyo alimshikilia Joan kiuno na kunyanyuka naye bila kutenganishana, mkongojo wake ukiwa bado ndani yake Joan ambaye alitoa kaukelele kamoja karaha hako hata Giedon mwenyewe akamtazama. “Vp tena Joan! Mbona sijawahi kusikia hako kamlio!?”

Haaaa!!!???? Inamaana siyo mara yenu ya kwanza kukunjana? Ndiyo maswali yaliyokuwa yakipita kichwani mwangu kwani badala ya wao kuachina na kuvaa kuondoka kwenye hoteli ambayo inatingishika kama vile muda wowote inaweza anguka, wao ndo kwanza wanawekana kwenye meza ambayo ilikua upande wa kulia wa kitanda na kuendelea kutiana.

“Joan, Lisa atakuwa wapi?” Niliuliza kwa haraka baada ya jengo zima kutingishika kwa nguvu na kunitoa kwenye mshangao wa hamu nilizokua naziona wakipeana Giedon na Joan, mabaunsa wa guild nzima.

“Asa unamuuliza Joan, yeye ndo yuko naye?” Alijibu Giedon kwa hasira na kugeuza shingo yake huku mikono yake ikiwa kwenye meza aliyokaa Joan naye Joan akimlamba Giedon shingo.

“Ni marafiki ndo mana namuuliza kwani Lisa hayupo chumbani kwake!” Nilisema huku nikiendelea kutizama shoo aliyokuwa akiipeleka Giedon.

“Ahn… Ah… Ah!” Joan alikuwa akiguna kwa raha maana alionekana kabisa kapiga mabao mengi sana hadi kuhema juu juu kiasi hicho. “Atakuwa kaenda kwa wazazi wake Dar! Ahn…. Ah bebi... Chomeka yote bebi!”

Kudadeki! Hawa watu vipi? Argh! Yani nikahisi kichwa kinaniuma kwa wakati mmoja baada ya kumsikia Joan akitoa miguno ya namna hiyo kwani taswira yake ya kibabe iliyokuwa kwenye kichwa changu ilifutika apo apo.

“Shit! Lisa!” Nikashtuka kutoka kwenye live shoo niliyokuwa naitazama na kuanza kuondoka baada ya kuambiwa nifunge mlango nyuma yangu. Hawa wakuda ni watu wa namna yake. Yaani watu huko nje wanatafunwa tafunwa na mamonsters size ya jengo zima wao wanakula uroda umu ndani, dah!

Anyway, akili yangu ilirudi na kukaa vizuri, nikaanza kufikiria shortcut nzuri ya kumfikia Lisa ni ipi maana nina uhakika kabisa bado hajafika Dar kwani hazijapita hata dakika kumi na ni usiku. Ingawa nio uhakika hakuna kinachoweza kumdhuru kwa uwezo aliokuwa nao kwani kwa level zinazotambulika kwenye Guild, Guild master Danny ni Level 390 na Lisa ni Level 401 kumaanisha Lisa akijumlisha nguvu zake zote na skills zote alizokuwa nazo kuanzia Heal, mpaka Spearmanship (Ujuzi wa kutumia mikuki) basi hata Danny hawezi kumgusa. Kwa kuwa mimi sina system hivyo hata kujua levyo yangu siwezi, viongozi walikadiria uwezo wangu nakusema nakaribia level 250 na ndiyo maana walinikubali kwenye kundi japokuwa sikuwa na system.

“Nina uhakika nikikatiza Morogoro nikanyosha na Kibaha nitamfikia!” Nilijiamini kwenye swala zima la kusoma ramani kwani nilikuwa nimeiweka kichwani. Iliniongezea kuaminiwa kwenye guild kwani nilikuwa najua nchi nzima kwa kichwa na nilikua nauhakika Lisa hakuwa na uwezo wa kujua anapoelekea kirahisi kwani alikuwa na wasiwasi juu ya wazazi wake lakini hapo ndipo nilipokosea.

Wakati The death Gate likianza kufumuka, muda ulikuwa saa tisa kuelekea saa kumi, na mpaka mimi nafika ilipokuwa nyumba ya kitajiri ya wazazi wake Lisa na kumkuta akiwa amesimama nje ya gofu hilo, ilikuwa saa kumi na vidakika. Nyumba ya wazazi wake ilikuwa imejawa na damu nyingi sana kutoka kwa viumbe vilivyokuwa kivianguka kutoka juu hadi kuipelekea kuvunjika kabisa hadi kubaki gofu lenye manyama ya viumbe kibao zilizochanganyika na mawe, bati na samani za nyumba hizo. Swala la wazazi wake kuwa hai lilikuwa ni ndoto tu kwani kutoka alipokuwepo aliona kabisa miili yao iliyokua imeminywa na paa lililowaangukia baada ya kiumbe mkubwa sana kuliko hata hellhound kuiangukia nyumba hiyo.

“Lisa.” Niliita huku nikimsogelea Lisa aliyekuwa ameanguka chini baada ya kuona kilichoko mbele yake. Nilijaribu kumshika lakini hakuonyesha utayari. Sijui ni nini lakini nilijihisi kumkumbatia hata kama atakataa na ndicho nilichofanya kwani alianza kunipigapiga kifuani kila nilipomgusa hadi akakubali na kuanza kulia kwa nguvu kama mtoto mchanga. Nilimkumbatia hivyo kwa muda mpaka pale maumivu yalipompungua na akatulia.

Muda tu baada ya Lisa kuacha kulia, viumbe waliokuwa wakimwagika kutoka kwenye lile geti lililokuwa juu ya vichwa vyote vya Afrika Mashariki, walipungua hadi wakaisha na hawakutoka viumbe wengine tena, lakini kilichofuata ni geti zima kuongezeka upana na muda huu lilikuwa kubwa kiasi kwamba Kenya na Uganda yote na Mozambique na Malawi hadi Zambia na sasa hivi nusu yaKongo ilikuwa imemezwa. Giza halikufucha ukuaji wa geti hili kwani lilikuwa limezungukwa na miale mikali ya purple na nyekundu na nyeusi ya kiza ikiwa ndiyo iliyo kiini cha geti hili hivyo ule mwanga uliokuwa ukitengenezwa na kona za geti hili la duara ziliangaza sana hadi kumeza anga za kimataifa za mpaka bahari ya Hindi.


GRRRRRR…..


Ilikuwa sauti iliyotoka katika mdomo wa kiumbe huyu Hellhound na kwa bahati mbaya sana hakuwa peke bali walikuwa kama kumi wakiaanza kutuzunguka kwani walivutiwa na haarufu ya damu kutoka kwenye miili iliyokatika hali ya utumbo na viungo vyote vya ndani kuonekana nje ya wazazi wake Lisa.

“Lisa! We need to leave this place!” Nilimwambia Lisa nikijaribu kumsihi anyanyuke tuondoke kabla Hellhounds hawajaanza kukusanyana katika mtaa huu wa Posta ambao ulikuwa na miili mingi sana iliyotapakaa na magari mengi sana yakiwa mengine yamelipuka na mengine yamegona na mengine yameachwa wazi na wenye magari hayo kukimbia baada ya mvua ya viumbe hao kuanza kunyesha.

“No! I am going to kill everything that is moving towards us!” Lisa alizungumza macho yake ghafla yakawa meupe kiasi cha mng’ao wa tochi na kwa kuwa alikuwa amekwisha vaa armor yake wala hakuhitaji kujali namna atavyowafanya hawa viumbe waliomuulia wazazi wake.

“Then, acha nikusaidie!” Nilimwambia huku ninyanyuka na kuuchomoa upanga wangu ambao ulikuwa mgongoni mwangu. Kilichofuata kilikua ni kitendo cha sekunde chache tu na panga langu lilikua likipita katikati ya miili ya hawa mbwa wakubwa saizi ya miili yetu na Lisa alikuwa akiyatandika ngumi na kwa kutumia skill Fist Burst ilikuwa tu ngumi zake zikigusana tu na hawa hellhounds walikuwa wakipasuka kama Maputo na maviungo yao yakimrukia mwili mzima.

Mapambano haya yalidumu hadi mchana kwani Lisa alikuwa kwenye hali ya mauaji muda wote. Alihama pale tulipokuwa baada ya kumalizana na viumbe wote walikuwa wakitufata na hakuridhika kwani hapo hapo akaanza kuwafuata hawa viumbe huko walipo kwenye maeneo mengine. Posta nzima na Mawasiliano ilikuwa ni uwanja wa mapigano kwani watu tuliokuwa tukipigana tulikuwa wawili tu na Lisa hakuwa akichoka kabisa. Najisifia kwa stamina lakini kwa trance aliyokuwa nayo Lisa kwa wakati huo, hata mimi nilijiona sina kitu.

Ingawa juwa lilikuwa limekwisha chomoza ila halikuonekana. Ilikuwa kama vile jua linatua kwani kote kulikuwa kwa njano kama hali ya jua la jioni likitua ilhali ilikuwa saa tatu kuelekea saa nne.



* NOW *



“Ah… hii ni live kutoka Tanzania, kwenye jiji lililobakia magofu la Dar es salaam. Tumepata ripoti kuna Hunter ambaye yupo anaelekea kupambana na Dragon King. However, we are still not getting a clear picture. We will be right back to bring you the live fight! Will, this hunter manage to defeat the Dragon king before its decent or will this be the end of the continent as we know it!?”

Ilikuwa ni sauti ya reporter wa Aljazeera ndiye aliyekuwa akitangaza huko nchini Pakistan, huku taifa zima na mataifa mengine mengi yakiwa yanamuombea bwana huyu wasiyemjua ambaye ameamua kupigana na dragon king mwenye size ya kuizidi Tanzania nzima kwa ujumla. Walikua wameshika tasbihi wakiswali kwa Mola amsaidie huyo hunter kwani walikuwa wanauhakika kabisa kuwa kiumbe huyo akifanikiwa kutua chini duniani na kukanyaga ardhi basi wao watakuwa wa kwanza kuangamia.

Nchi zote duniani zilikuwa zikisubiria vyombo vya habari virudishe matangazo ili vione kile kinachoendelea. Serikali ya Marekani pamoja na Hunters’ Association walishangazwa na taarifa za kwamba kuna mtu anaenda kupigana na The Dragon King, kwani waliamini hicho kitu hakiwezekani. Wao wenyewe wameogopa hatakusogea karibu sembuse mbongo tu fala mmoja huko anayejifanya shujaa! Ndiyo yaliyokuwa mawazo yao.

“Please dear Lord help him!” haya ni maombi ya waumini waliokusanyika huko Vatican kwa ajili ya kumuombea bwana huyo ambaye wamesikia dakika chache zilizopita kuwa ataanza pambano la kihistoria.


“VVVBOOOOOOOMMMMMMM!!!!!!”


Ni kishindo kikali sana cha ajabu kilichosikika kwenye TV za watu pale matangazo yaliporudi live. Hawakuamini walichokuwa wakiona. Kitendo cha upanga kugongana na mabaka ya dragon king kwani hiyo sauti ilikuwa kama vile mlipuko na pale pale watu wakamuona aliyekuwa akiweka maisha yake hatarini likupigana kuliokoa bara lake.

“Wow!” Mishangao ya watu wengi wa dunia waliokuwa wakilitazama pambano live kwenye runinga walikuwa wakitoa macho kwani bwana huyu alikuwa akitoa radi kwenye miguu na upanga wake ulikua ni wa ni wa kung’aa kiasi cha kuangaza mwili mzima.

Alipotea ghafla mbele ya kamera zilizokuwa zikimmulika na kitendo cha sekunde akatokea karibu kabisa na mabaka ya dragon yaliyokuwa magumu kama chuma chenye leya nne kwani hata dalili ya kukatika hayakuonyesha.

“There is no way he can leave a scratch on a dragon scale!” Kejeli zilianza za chini chini kwa wale waliokuwa wamejawa wivu kwani waliona kabisa jinsi mtu huyo alivyokuwa akitia juhudi kupambana na dragon king bila mafanikio.

“Dragons usually have a reverse scale, akilipata hilo basi kazi yake itakuwa imeisha!” walikuwa wakiongea wengine waliokuwa wakiona pambano huku wakipata moja baridi na kuendelea kutazama burudani live.

“You think that’s easy as you make it sound?” aliongea mwingine kwenye ile baa yetu ya mwanzo kule New York. “Finding a reverse scale on multitude of scales is not an easy feat to acheave so stop spouting shit and sit down and watch!” aliongea kwa jazba kweli hadi Yule wa kwanza kunena akaona kabisa jinsi watu walivyomwangalia kama vile kasema neon baya.

“I cant find the reverse scale!” nilijiambia huku macho yangu yakiiuzunguka shingo ya hili dragon ambalo mwili wangu wenyewe ulikuwa mdogo kulinganisha na scale yake moja. Lakini sikuacha kuendelea kugonganisha panga langu dhidi ya mabaka yote hayo kwenye mwili wake.

Ghafla joto likaanza kuongezeka. kuja kushtuka, dragon alikuwa anakusanya nguvu kwenye mdomo wake mkubwa ambao unaweza kuimeza Kilimanjaro nzima, napunde tu kampira kadogo kamoto kakaanza kuongezeka size hadi likawa bonge la pira la moto. Lilikuwa likubwa sana kana kwamba kama akiliiachia basi litaondoka na ardhi yote ya Tanzania na Kongo kwa mpigo.

“Oh my God! Is it annoyed and trying to shoot a fireball?” walikua wakiongea watu Paris wakiwa wamezishika simu zao na kutazama tukio zima.

“If that is released, the continent will split in half without a doubt.” Aliongea mwingine akionyesha hofu ya kitu kinachoweza kutokea kama lipira lote hilo la moto uliokandamizwa kwa pamoja likiachiwa.

“Stop it! Stop it! Stop it!” Zilikuwa ni kilele za watu duniani kote wakiongea kwa pamoja kwani walijua kabisa hilo lipira liloko mdomoni mwa dragon likiachiwa ndio utakuwa mwisho wa nusu ya bara la Afrika.

“AAAAARGH!” Nilitoa ukulele kukusanya nguvu zangu zote nilizokuwa nimebakiwa nazo kwani hii ndiyo ilikuwa nafasi yangu ya mwisho. Kama siwezi kuliumiza kwa nje basi nitaliumiza kwa ndani.

Nilikusanya nguvu zangu zote kwenye miguu yangu na kusababisha radi kubwa kutoka kwenye miguu yangu hadi kusababisha viatu na suruali ya armor niliyokuwa nimevaa kuharibika kabisa na kuchanika. Radi ilikuwa kubwa kiasi kwamba ilikuwa ikifika hadi chini kwenye udongo na kufanya majengo ambayo bado yalikuwa hayajaanguka kupigwa na radi hizo.

Na pale pale wakati the dragon king likiwa tayari kuutema mpira huo wa moto, nilipaa kwa uwezo wangu wote na kulichapa buti la kidevu mpaka kupelekea likameza lempira lililokuwa mdomoni mwake.


UWOOOOOOOOOOOOOO!!!!!!!!

Zilikuwa ni kelele za shangwe zilizosikika duniani kote. Sio wamarekani, waingereza, waarabu, wala wachina na wajapani. Wote walishangilia kwa pamoja walivoona nimefanikiwa kusababisha hilo dragon kushindwa kutema lipira hilo lililojaa moto.

“Haa… Haaa … haaa!” nilijikuta nikihema kwa nguvu sana huku nikiwa hewani nikielea nikilitazama jinsi koo la hili lidragon likiwaka moto ndani kwa ndani na pale pale nikajua kazi yangu imeisha. Nilifurahi kujua nimefanikiwa kuliua.

“No way!!!” ulikuwa mshangao wa Giedon ambaye alikuwa amesamama maili mbali kidogo na pale Jay alipokuwa akipambana. Hakuwa mwenywe. Alikuwepo Danny, Joan na wanaguild wengine wote ambao walikuwa bado wapo hai.

“Did he just do that?” Aliuliza kwa sauti huku wanaguild wakiwa wanashangaa tukio zima. Hawakuamini, Jay, ambaye hata System window hakuwa nayo kafanikiwa kulidhibiti Dragon King tena peke yake bila usaidizi. Midomo yao ilikuwa wazi.

Dunia nzima ilikuwa kwenye furaha sana, lakini kuna mtu mmoja ambaye hakuwa na furaha kwa kitendo alichokifanya Jay! Alionekana akipiga meza kwa nguvu hadi kuivunja na hatukujua ni nani! Kisha akaonyeshwa akiweka tabasamu mdomoni.

“Hey, is the gate supposed to do that?” Ilikuwa sauti ya bwana mmoja mtaani London akiwa anaangalia TV za kwenye ghorofa huku watu wengine wakiendelea kushangilia kwa kazi nzuri aliyoifanya bwana huyu. Na pale pale watu wakaanza kushtukia kitu ambacho hakijawahi tokea tokea mageti yanayounganisha dunia yetu na dunia nyingi zingine kwenye multiverse kutokea.
x
“Hey, the gate is reversing! Hurry up and send him a message to get away from there!” ilikuwa sauti za watu tofauti tofauti huko duniani awkipiga kelele kwamba hao watu wa vyombo vya habari na serikali wamwambie huyo bwana akimbie hapo alipokua, lakini wapi. Kulikua hakuna namna yoyote ile ya Jay kuweza kusikia sauti za watu walionyuma ya kamera ambazo zinamzunguka.

“Hey I think we should leave!” Aliongea Danny huku akianza kuwapa ishara wanaguild wengine kuanza kuondoka.

“Why? Are we not going to help him? The gate is reversing man!” aliongea Giedon. Ingawa huyu mwamba anaonekana kuwa ni mtu wa hasira na roho mbaya lakini sivyo. Ni mtu mwenye roho nzuri sana hasa pale kunapohusisha kusidia watu wengine.

“We can’t Giedon. It’s too late! Labda ashtukie mwenyewe lakini kwa umbali tuliopo hatuwezi kumfikia na kumsaidia!” aliongea Joan akionyesha masikitiko huku yeye na wengine wote wakianza kuondoka kwani walishaanza kuona jinsi geti lilivyoanza kuzunguka kurudi kinyume wakati lilikuwa likizunguka clockwise.

“But…!” Alisema Giedon lakini hata yeye alijua kabisa, akisogea karibu tu kidogo basi yeye na Jay wataenda na maji.

Kilikua ni kitu cha kusikitisha sana maana Jay alikuwa amekwisha ishiwa na nguvu na hadi kupelekea yeye kuzimia akiwa angani futi mia tatu juu hivyo yeye kujiokoa na hiyo gate reverse ilikuwa haiwezekani. Ghafla huku watu wakiwa kwenye masikitiko, mwili wa Jay ulipatwa na kitu kama mkono mkubwa mweupe uliotokea kwenye geti hilo ambalo tayari lilishalimeza dragon king ambaye amekwisha kata moto na kuingia ndani na Jay akiwa ameshikiliwa na mkono huo wa maajabu.

“What was that?” yalikuwa ni maswali ya watu wengi duniani walioshuhudia huo mkono wa maajabu uliobeba Jayden na kuingia naye humo ndani mwa hilo geti.


............................


“SYSTEM INITIATING”
"Mfumo unaanza"

“ALMIGHTY SYSTEM EMBEDDING”
"Mfumo unapachikwa!"

“ALMIGHTY SYSTEM EMBEDDED”
"Mfumo umepachimwa"

“ALMIGHTY SYSTEM SUCCESSFULLY INHERITED”
"Mfumo wa Almighty Umerithishwa kikamilifu!"

“SENDING HOST TO THE TURNING POINT OF TIME 15 YEARS TO THE PAST!”
"Mmiliki anarudishwa miaka 15 nyuma wakati wa mabadiliko ya muda!"

“HOST HAS ARRIVED TO THE TURNING POINT OF TIME 15 YEARS AGO!”
"Mmiliki amefika miaka 15 nyuma kabla ya mabadiliko ya muda!"

“GOODLUCK DEAR HOST!!!!!!!”
"Nakutakia safari njema mmiliki!"


“Argh! Mbona kuna mtu anaongea kwa nguvu ivo!” nilijikuta nikisema kwani hiyo sauti ilikuwa karibu kabisa na masikio yangu kama sio ndani kabisa.

HEEEEEEE!! Mbona nina sauti ya kitoto?

Haraka harak nilinyanyuka kutoka nilipokua nimelala. Nakumbuka kabisa ceiling board ya chumba change ndo ilikua ivo wakati nikiwa nasoma O level nikiwa bado naishi na wazazi wangu!

Kitu cha kwanza nilichokikimbilia kilikuwa ni kioo kilichokuwa ukutani karibu na mlango wangu wa kutoka kushuka sebuleni ambao nilikua napenda kuutundika nguo za Superman.

“The hell is this?” Nilishangaa sana kujiona kwenye kioo nikiwa kwenye mwili wangu mdogo hata vindevu sina nikiwa na kitambi tena kabisa.


“THE FUUUUUUCKKK!!!!”


NAOMBENI MAONI YENU KAMA ITAWAFURAHISHA, NIIENDELEZE KUITUNGA : )
MTUNZI: M.Kitua
SIMU: 0622-809-054

AHSANTENI....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom