Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

kwa kila mwanasiasa wa tanzania anaetaka kuungwa mkono na wananchi wengi amekuwa akijitahidi kujionesha kuwa ni mfuasi wa rais wa kwanza wa tzania mwl nyerere. Anasifiwa kwa kila kitu lakini kwangu mimi simkubali kabisa mwl nyerere. Siamini kama alikuwa na kipaji cha uongozi. Alikuwa ni dikteta. Alifinya uhuru wa habari, aliwafunga wapinzani wake, alileta umasikini mkubwa kwa taifa na wananchi wa tzania. Si kwamba alikuwa anapendwa bali alikuwa anaongoza wananchi wengi wasiojua dunia inakwendaje"wajinga".

Huyo ndio nyerere. Kwa miwani yangu namuona kuwa ana mabaya mengi kuliko mazuri kama tunavyolazimishwa kuamini. Kutojilimbikizia mali au kutoa huduma za jamii bure si kigezo cha kutokuwa dikteta maana hata pinnochet, hitler na mussolin walikuwa wanatoa huduma za jamii bora na bure kabisa kwa watu wao.

nenda kusini nenda kaskazini, nenda magharibi nenda mashariki, hakuna kiongozi dikteta ambaye ameacha madaraka kwa hiyari, huku wananchi wake wakimlilia. Kama Nyerere angewaumiza wananchi wake wangemchukia na katu wasingemkumbuka kama ilivyo sasa. Kama angekuwa dikteta asingelipigania usawa, vita dhidi ya mafisadi, kupigania mgombea binafsi, Kuifafanua katiba kuwa ni kama vazi la kijana ambalo huwa linamtosha kwa kipindi fulani. Lakini baada ya muda fulani vazi hilo halimtoshi tena, linambana. Hivyo anahitaji vazi lingine.

nenda uendako hakuna kiongozi kama nyerere. Ambaye alikuwa anahangaishwa na umaskini wa watu wake.
 
Ni mtazamo tu!

Mtazamo chanya au hasi?

Watu wengi hawamjui Nyerere! Unahitaji mchanganuo wa facts ili kuhitimisha msimamo wako kuhusu Nyerere. Si kumtendea haki kumhukumu kwa kuangalia mambo aliyoshindwa peke yake. Ni vizuri kuchukua tahadhari za pande zote.
 
Kwa kila mwanasiasa wa Tanzania anaetaka kuungwa mkono na wananchi wengi amekuwa akijitahidi kujionesha kuwa ni mfuasi wa Rais wa kwanza wa Tzania Mwl Nyerere. Anasifiwa kwa kila kitu lakini kwangu mimi simkubali kabisa Mwl Nyerere. Siamini kama alikuwa na kipaji cha uongozi. Alikuwa ni dikteta. Alifinya uhuru wa habari, aliwafunga wapinzani wake, alileta umasikini mkubwa kwa taifa na wananchi wa Tzania. Si kwamba alikuwa anapendwa bali alikuwa anaongoza wananchi wengi wasiojua dunia inakwendaje"wajinga".

Huyo ndio Nyerere. Kwa miwani yangu namuona kuwa ana mabaya mengi kuliko mazuri kama tunavyolazimishwa kuamini. Kutojilimbikizia mali au kutoa huduma za jamii bure si kigezo cha kutokuwa dikteta maana hata Pinnochet, Hitler na Mussolin walikuwa wanatoa huduma za jamii bora na bure kabisa kwa watu wao.

Mimi nadhani alikuwa na kipaji cha uongozi na ndio maana hata baada ya kutoka madarakani aliweza kumsimamisha Mkapa na kumpigia kampeni mpaka akachaguliwa kuwa rais. Kumbuka ameyafanywa haya miaka kumi baadaya kuachia urais. Kuhusu masuala ya kuminya uhuru wa habari, kuwafunga wapinzani, na kuleta umaskini nakubaliana na wewe. Kuhusu kupendwa napingana na wewe huyu jamaa alikuwa anapendwa sana (charismatic). Na huu upendo wa watu kwa Nyerere haukutokana na ujinga kama unavyodai bali ulitokana na watu kukubaliana na mambo mazuri mengi aliyoyafanya.

Ninawajua watu wengi wasomi na wenye uelewa mzuri tu ambao hata hii leo wanamkumbuka kwa upendo Nyerere. Na jambo kubwa ni kuwa wengi wanakiri kuwa asingekuwa Nyerere kuleta sera za elimu bure na fursa ya kila mtu kusoma kutokana na uwezo wake wa akili (siyo pesa) basi wangeishia kubaki vijijini bila elimu. Na kila mtu anakubali kuwa wakati wa Nyerere kiwango cha elimu kilichouwa kikitolewa na shule za serikali kilikuwa ni cha juu kulinganisha na shule binafsi.
 
Ni kweli nyerere hakupigania uhuru bali alipewa tuu. Hata babaako kama angekuwa mstari wa mbele ktk chama angepewa huo uhuru. Kumbukeni kuwa kipindi hicho tulikuwa chini ya himaya ya waingereza baada ya mjerumani kushindwa ww2. Mkumbuke pia kuwa alikwenda UNO kwenye mkutano miaka ya 1958 akisindikizwa na baadhi ya wahindi (waliosponsor safari yake huko) . Maadhimio ya mkutano huo yalikuwa kwamba watanganyika wasubiri kidogo hadi 1961 ndo watapewa huo uhuru wanaodai. Kwa wale mtakaokumbuka, nyerere alipokuwa anarejea toka yuno akiwa eapot alikuwa ameshikilia bango lenye ujumbe wa kuwa "uhuru 1961'. Kwa hiyo ni kweli kabisa nyerere hakupigania uhuru. Kumbukeni kuwa wakati wa mkoloni kulikuwa na matabaka yaani wazungu(tabaka la juu) waasia(kati) na weusi(chini). Kwa maan hiyo waasia(wahindi) walikuwa wanaloby namna ambavyo watakuwa tabaka la juu na ndio maana walishadadia sana na kusupport move yote ya kuomba uhuru. Mtakubaliana na mimi kwamba wahindi ni wataalamu wa lobying.mtakubaliana na mimi pia kuwa katika wageni wote waliokuwapo enzi za ukoloni, ni wahindi pekee ndo hawakufukuzwa na ndo hadi sasa wako wanamiliki biashara nyingi na kuishi katika maeneo prime ya miji yetu mikubwa. Watu kama akina mtikira ndo maana walikuwa wanamchukia sana nyerere kwa kuwabeba "magabachori'
Kwa maana nyingine ni sawa na sasa ambapo matajiri (akina rostam na wengineo) wananyenyekewa kwa sababu ya kusupport chama. Hata enzi za mwalimu walikuwepo. Ninachoweza kusema ni kuwa Nyerere alikuwa na "stupidity innocense". Mkumbuke kuwa amepewa nchi akiwa a mere guy, hajui mambo ya uchumi,hana chochote yaani hakuwa na experience yoyote ya uongozi pamoja na kuwa kiongozi wa TAA na baadae Tanu. Ujinga na uppuuzi wake unakuja pale alipokuwa hataki ushauri toka kwa watu wataalamu kama akina mtei, kolimba nk. Mjue pia kuwa ndo maana uongozi wa Nyerere ulijaa viongozi ambao noi ma yes men/women. Yeyote aliyeonekana kuchallenge aliwekwa kizuizini au kupelekwa mbali mfano kuwa balozi.
Ukiangalia uchumi wa Tanganyika na baadae Tanzania utagundua kuwa wakoloni walituacha pazuri sana. Baada ya kupewa uhuru nyerere na wenzake walikuwa wakisherehekea tangu hiyo 61 hadi kuungana na zanzibar. Miaka yote hiyo no production at all. Kilichokuwa kinafanyika ni kuchukua kwenye hivyo viwanda. Kuja kutahamaki uchumi unaanza kuyumba na yeye kuja na arusha declaration(ujamaa na kujitegemea-african socialism) kama suluhisho la kurevive uchumi. Lakini kwa sababu ya mipango mibovu inashindwa. Come 1972 anakuja na villagilization anahamisha watu mahali ambapo walizoea kulima( kwa maana wanajua majira ya mwaka, udongo nk) na kupelekwa sehemu ngeni. Matokeo yake watanzania wakawa stranded. Hawajui cha kufanya. Unapita msimu wa kwanza na wapili kwani hawajui ni zao gani walime na majira hawayajui. Baati mbaya ukame unaikumba nchi miaka ya 1975 na kuleta disaster ya njaa. Kumbuka kuwa tangu 1972 uzalishaji wa chakula unayumba kwa sababu ya vilagisation, ukame unaikumba nchi, matokeo yake ni njaa. Kama mnakumbuka enzi za unga wa Yanga kama msaada toka marekani. 1978 vita ya kagera ambayo inaigharimu tanzania mamilioni ya shilingi. Kwa hiyo tanzania ikawa haina pesa hata kidogo.
Kuna tetesi kuwa baada ya vita na I'd amin nyerere alitaka kung'atuka lakini intellijensia ikamshauri asubiri na akaamua kusogea hadi hiyo 1985. Alipong'atuka na kuwa nje ya uwanja ndo akaanza kuhisi madudu aliyofanya na kuwa kama mshauri wa serikali.
Mkumbuke pia kuwa uchumi ulipoanza kuyumba miaka ya 1975 mataifa mbalimbani wakiwemo IMF walikuwa wakishauri nchi yetu kujiunga na stractural adjustment programs(SAPs) kama suluhisho la uchumi lakini nyerere alikataa kabisa. Baada ya nyerere kujiuzuru, haya mataifa yaliendelea kushauri serikali kwani hali ya uchumi ilikuwa mbaya sana. Sharti mojawapo kwenye hizo SAPs ilikuwa ni kuingia kwenye vyama vingi. Ilipofika mwaka 1992 kukawa hamna jinsi na nyerere akamshauri mwinyi akubaliane na hilo sharti. Lakini kwa sababu mwamko wa vyama vingi ulikuwa mdogo miaka hiyo ikabidi nyerere amuombe mrema(usalama wa taifa) aanzishe chama kama kiini macho kwa haya mataifa ili tuweze kuendelea kupata misaada. Mantiki ikiwa sio kukifanya kiwe chama kikubwa bali kiwe kama chambo kwa haya mataifa. Hapo ndipo nccr mageuzi ikazaliwa na vyama vinginevyo. Kama mtakumbuka nccr mageuzi ilipanda chati sana 1995. Mtakumbuka pia kwenye baadhi ya mahojiano ya nyerere aliwahi kusema hatuwezi kumuachia mwizi(mchaga),mbwa(askari) kwenda ikulu na ndipo nyerere akaingilia kati kufanya kampeni chafu dhidi ya mrema hadi nccr kukosa uraisi 1995. Mkapa akaingia ndani ya mjengo kwa mgongo wa mwalimu.
Naomba kuhitimisha kwa kusema kuwa nyerere kweli hakuwa kiongozi mzuri, na hakuwa anasilikiza ushauri toka kwa mtu yeyote. Laiti kama angeshaurika tusingekuwa hapa tulipo. Kwa hiyo haya yanayotokea sasa ni matokeo ya uongozi mbovu na wakidikteta aliokuwa nao nyerere.
I stand to be corrected.
 
Niwakumbushe tu vijana wetu humu na wale ambao jamaa zao walikwaruzwa na baadhi ya maamuzi ya Mwalimu kuwa HISTORIA huwa haiandikwi upya wala haifutiki. Mazuri ya Mwalimu ni mengi mno na hasa ambao sehemu kubwa ya umri wetu tumeishi, kusoma na kufanyakazi enzi zake.
Wapo walioumizwa na baadhi ya maamuzi yake kwa sababu tu ya kutofautiana naye au kutomwelewa au Mwalimu kupewa taarifa ambazo sizo juu yao. Mmoja wa watu hao ni Christofa Kasanga Tumbo (RIP). Wapo waliomchukia kwa kuwaondoa madarakani kwa kuwa walikuwa hawafai. Wapo aloowanyima ulaji.
Pamoja na yote hayo, Mwalimu anabaki kuwa KIONGOZI wa aina yake hapa Tanzania na Afrika. Angalia akina Museveni waliomhusudu sana Mwalimu wanayoyafanya sasa. Mwalimu alistaafu Urais akiwa na umri mdogo tu wa miaka 63.
 
Ni haki yako kutomkubali Nyerere..... hatuwezi kukulazimisha kumkubali kama ambavyo huwezi kutulazimisha wengine tusimkubali Nyerere. Hata hivyo, mizania ya kipimo cha uongozi Afrika na dunia kinatambua kwamba Nyerere ni mmoja ya viongozi waliofanya jitihada za kuwakomboa wengine hata kama kuna mahali hakufanikiwa lakini nia alikuwa nayo na ndio moja ya kipimo cha uongozi bora.

Ni Rais yupi wa Tanzania unaedhani anakubalika katika medani ya kimataiafa kama Nyerere. Nyerere ameingia mpaka kwenye kitabu cha dunia cha "great thinkers". Hili ni kundi la viongozi au watu ambao wanafikiri kwa kina zaidi ya tunavyofikiri na wakati mwingine huwezi kuwaelewa mara moja fikra zao na yamkini katika mambo fulani hutuchukua muda mrefu kuelewa fikra zao.

Nafikiri ukimkuta mtu wa kabila la wabelibeji kasoma labda hadi kiwango cha PHD ni lazima atakuwa na akili sana kulingana na mazingira ya kabila lake. Katika kipindi cha Nyerere hapakuwa na wasomi na miundombinu ya elimu ilikuwa duni, kiwango cha uelewa na elimu ya mwalimu kipindi hicho inatosha kumbeba kwamba alikuwa na uwezo mkubwa ingawa hii haina maana kwamba alitakiwa kufanikiwa kwa kila jambo. Watendaji ndio wanaweza kumfanya Rais aonekane kafanya makubwa au kinyume chake.

Kuongoza wajinga ndio kazi kubwa kuliko zote katika ngazi ya uongozi, kuanzia ngazi ya familia, kata hadi taifa na ndio maana kazi ya kwanza ya mwalimu ilikuwa kuifanya elimu kuwa bure. Wajinga hawezi kumwelewa mwerevu.
 
Kwanza, Dowans ina kosa lipi?

Halafu, kumbuka kuwa Nyerere hakuweka misingi mizuri katika nyanja zote, na haya matatizo ya umeme, maji, elimu, umasikini, maradhi, yote yanatokana na Nyerere, ni lipi jema na lililofanikiwa alilifanya Nyerere? Nakuhakikishia hakuna! Mpaka haya matatizo ya katiba ni yake, katiba zake alikuwa akitunga yeye na watu wake wa karibu kwa siku mbili tatu anazi-implement kidikteta na hakuna wakukataa, na ukiuliza tu, kosa.

Sasa unachokataa nini? Mtoa mada hajaona jema kwa Nyerere nami namuunga mkono, hata mimi sijaliona jema lolote, na kumbuka, nilikuwepo wakati wa Nyerere, kabla yake na sasa awamu ya tatu baada yake.

Yaan mie hadi mnanichekesha badala ya kunisikitisha, ulimwenguni kote nani hamjui nyerere kwa sifa nzuri alizokuwa nazo? mnataka kusema huyu mndengereko mlomweka hapo kila leo kwenda kutalii nje ndo anaefaa? Mambo mnayoyaona leo ni kwa sababu ya mabadiliko ya kitechnolojia so hata nyerere angekuwa raisi leo angecope nayo.....mnan'gang'ania eti nyerere alikuwa dikteta, bila hivo si mngemkalia kichwani.... hata hivyo kiongozi yeyote aliyechaguliwa na watu ni dikteta kwa watu fulani kwani wakati wa uchaguzi huo kuna waliomkataa na waliomkubali...so kwa nyie mliomkataa nyerere mnamwita dikteta but kwa sie ambao tulimkubali....He was perfect...TUTAENDELEA KUMKUMBUKA MWALIMU
 
Nimesikitishwa na hoja mfu ambayo mtu aliyeanzisha mada hii ametoa. Kusema Nyerere hakufanya mambo ya maana katika nchi yetu ni matusi kwa wale ambao wanaelewa nchi yetu ilikuwa wapi na nini kilisababisha uchumi wetu kudorora mwaka 1979-hadi miaka ya tisini. Niliona upungufu mkubwa wa uelewa wa historia ya nchi yetu pale tulipokuwa tukijadili uamuzi wa Mwalimu kuitambua Biafra na kwa kweli wale ambao wanapima maendeleo kwa wingi wa vitu ambavyo wachache wanavyo na si jinsi ambavyo wengi wanavyo.

Je, ni nani asiyefahamu kuwa hadi mwaka 1978 nchi yetu ilikuwa na uchumi mzuri sana hadi IMF walidai kuwa Tanzania lazima itumie akiba yake ya nje na ibakie isiyozidi miezi sita hapo mwaka 1977? Najua mbumbumbu wanaotoa hoja mfu humu ndani watakuwa hawajui hilo. Je, ni nani asiyejua kuwa nchi yetu ililazimika kutumia dola milioni moja kila siku katika vita ya Uganda na kuwa vita hiyo ndiyo iliyofilisi nchi yetu? Mbumbumbu wa historia na uchumi watang'aka kama watu waliofumwa ugoni? Je, ni nani asiyejua kuwa mnamo mwaka 1979-80 bei ya mafuta ilipanda sana duniani na nchi yetu ambayo tayari ilikuwa imefilisika kwa vita haikuwa na fedha za kuweza kuendesha uchumi wake? Mazezeta wa historia na uchumi hilo halipo vichwani mwao kwani hawajui na wala hawajawahi kujishughulisha kujua hilo?
Je, ni nani asiyejua mataifa yanayotoka katika vita na ambayo uchumi wake umeyumbishwa navyo yanahitaji msaada/mikopo kutegemeza chumi zao? Watoa majibu ya kijiweni hawajui hilo kwani hawajawahi kujiuliza kuwa historia ya dunia imeonyesha hivyo kwani hata mataifa ya Ulaya yalipata msaada huo kutoka kwa Marekani katika Mpango wa Marshal. Na suala la mgawo na foleni za chakula na bidhaa baada ya vita je wamewahi kujiuliza kuwa Waingereza walikaa katika mgawo kwa miaka saba na siku waliporuhusiwa kula mayai mawili ni siku ambapo Malkia Elizabeth alisimikwa?

Ninaweza kuendelea kuuliza maswali mengi cha muhimu ni kusema kuwa Mwalimu alikuwa na makosa aliyoyafanya lakini huwezi ukaniambia kuwa eti aliporomosha uchumi kwa siasa za Ujamaa bali kukataa kwake masharti ya kijinga ya IMF na Benki ya Dunia yaliyodai eti serikali yake ilikuwa imeshindwa kuendesha uchumi vizuri ni uongo mtupu. Nilikuwepo wakati ule na nilipanga foleni ya sukari, sabuni na vitu vingine na kwa kweli kama kuna wakati serikali iliwahi kutoa sababu za ukweli kuhusiana hali ya uchumi ni wakati ule. Kama mtu aliyepata nafasi ya kusoma si tu sheria bali uchumi na siasa za taasisi za kimataifa za pesa ninathibitisha kuwa hali mbaya ya uchumi ilichangiwa kwa sehemu kubwa na sababu za nje na si za ndani. Kwa bahati mbaya watu wenye kupenda majibu mepesi na kwa kweli ya kijiweni ndio wako mstari wa mbele kupotosha ukweli na kutaka kutufanya kuwa sisi tu mazezeta wasio na uwezo wa kuchambua mambo. Chuki zao kwa Mwalimu kwa kweli huwezi ukazieleza vizuri kwani mtu ambaye alidiriki hata kutaifisha taasisi za kidini na kuzifanya za watu wote hivi sasa anaonekana kuwa alikuwa na ajenda ya kupendelea watu wa madhehebu fulani? Hivi hii kweli inaingia akilini?

Ninamalizia kusema kuwa maamuzi ya Mwalimu mengi yalilenga ustawi wa watu na si wa kutaka kujinufaisha na kama alikuwa mtu aliyependa watu wasisome je si huyu aliyetaifisha shule ili watu wa dini na makabila yote wasome? Je si huyu aliyeanzisha elimu ya watu wazima na kusababisha kiwango cha kujua kusoma na kuandika kupanda na kuwa asilimia 95? Si huyu aliyejenga miundo mbinu kama Tazara na viwanda vingi ambavyo mafisadi wamevigawa bure? Si huyu aliyeweza kushinda mbinu za benki za nje kuua NBC pale ilipotaifishwa? Si huyu ambaye hakutumia madaraka yake ya uraisi kujitarisha na hata watoto wake hali zake ni zinakaribia za Watanzania wengine.

Inanisikitisha sana kuona haya yote lakini watu wenye ajenda ovu ndivyo walivyo na hawatachoka kupotosha historia ili nia zao ovu zifanikiwe. Napenda kusema kuwa watashindwa kwani wale wenye uelewa mzuri wa mambo tutasimama imara kupangua hoja zao mfu.

Mkuu mbona unajichanganya na hizo data zako? unasema mwaka 1978 uchumi wetu ulikuwa mzuri sana hadi IMF walidai kuwa lazima itumie akiba yake yake ya nje ibakie isiozidi miezi sita hapo mwaka 1977, hapa kuna vitu viwili umechanganya miaka na umechukuwa data za IMF kama ushahidi, hapo hapo utaki tena kuzitumia data za IMF baada ya kumwambia serikali yake imeshindwa kuendesha uchumi unasema ni uongo mtupu, kuhusu vita Tanzania wamepewa misaada mingi tu kutoka China, Ujerumani,Uingereza,Malawi,Kenya,nchi za Scandnavia nazo zilitoa msaada wakati wa vita na Uganda, hivo vita vyenyewe vilichukuwa miezi minane tena vita kamili vya kupigana na vya miezi mitatu, ndio Tanzania tukafirisika?
 
Ahhha kumbe ni nyie wenye magazeti ya Alnoor! Kumbe mmeanza kuhamia jamii forum, nlisikia kipindi cha nyuma mlikuwa kwenye vijiwe vya kahawa. Na sirika lenu huwa ni wavivu sana wa kufikiria jambo lwa kina, kwa matatizo yoyote nyie huwa mnatafuta nani mwenye kosa na muanze kumtupia lawama.

Sasa ndugu yangu kwani hizi shule zote yaani elimu si zilikuwepo kipindi hicho cha Nyerere, kwa nini hukupenda kuingia darasani na kukazania masomo ili upate ufahamu mzuri wa kuchambua hoja kama hizi. Suala la rais fulani hakufanya vema huwa halipingwi kwa hoja za kahawa ulizozoea ndugu yangu. Kama umepitia shule vizuri na ulikuwa unauliza darasani maswali basi ungeweza kupata uelewa wa kutathmini kwa kina maendeleo ya nchi. Nchi na kiongozi wa nchi hupimwa na wananchi wake kwa vigezo vya kitaalam kama huduma za jamii kama elimu, afya n.k. Vile vile kiuchumi utaangalia mambo ya GDP, inflation etc.....maskini sasa sijui kama hizi misamiati iliwahi kukupitia au laah.

Labda nijaribu hili rahisi, wale babu zako kipindi kile umewahi kuwauliza kuhusu uongozi wa nyerere? walikuzaa lkn sijui kama una taarifa kuwa wale babu zetu kama walikuwa wanajifungua kitaalam au vichakani, na hizo hospitali? zilijengwa na nani na ilichukua gharama gani mpk kujengwa.

Maskini chambua hoja kwa vegezo acha porojo na unafiki, kwa hali ya sasa ni vema tukubali kuwa nyerere hakufanya yote mazuri, wala sio malaika. Lkn ndugu ni nusu karne sasa tangu ya nyerere, yani bado unaleta hoja ndani ya the great thinkers kuhusu nyerere, jadili ya sasa na toa suruhuhisho ya matatizo ya sasa, acha UJUHA!! Utalala mpk lini? AMKA KUTOKA KWENYE UJINGA MGANDO!

Wewe ndio una jipya kabisa unataka tukubali kuwa JF ni ya Wakirstu tu?
 
Nimesikitishwa na hoja mfu ambayo mtu aliyeanzisha mada hii ametoa. Kusema Nyerere hakufanya mambo ya maana katika nchi yetu ni matusi kwa wale ambao wanaelewa nchi yetu ilikuwa wapi na nini kilisababisha uchumi wetu kudorora mwaka 1979-hadi miaka ya tisini. Niliona upungufu mkubwa wa uelewa wa historia ya nchi yetu pale tulipokuwa tukijadili uamuzi wa Mwalimu kuitambua Biafra na kwa kweli wale ambao wanapima maendeleo kwa wingi wa vitu ambavyo wachache wanavyo na si jinsi ambavyo wengi wanavyo.

Je, ni nani asiyefahamu kuwa hadi mwaka 1978 nchi yetu ilikuwa na uchumi mzuri sana hadi IMF walidai kuwa Tanzania lazima itumie akiba yake ya nje na ibakie isiyozidi miezi sita hapo mwaka 1977? Najua mbumbumbu wanaotoa hoja mfu humu ndani watakuwa hawajui hilo. Je, ni nani asiyejua kuwa nchi yetu ililazimika kutumia dola milioni moja kila siku katika vita ya Uganda na kuwa vita hiyo ndiyo iliyofilisi nchi yetu? Mbumbumbu wa historia na uchumi watang'aka kama watu waliofumwa ugoni? Je, ni nani asiyejua kuwa mnamo mwaka 1979-80 bei ya mafuta ilipanda sana duniani na nchi yetu ambayo tayari ilikuwa imefilisika kwa vita haikuwa na fedha za kuweza kuendesha uchumi wake? Mazezeta wa historia na uchumi hilo halipo vichwani mwao kwani hawajui na wala hawajawahi kujishughulisha kujua hilo?
Je, ni nani asiyejua mataifa yanayotoka katika vita na ambayo uchumi wake umeyumbishwa navyo yanahitaji msaada/mikopo kutegemeza chumi zao? Watoa majibu ya kijiweni hawajui hilo kwani hawajawahi kujiuliza kuwa historia ya dunia imeonyesha hivyo kwani hata mataifa ya Ulaya yalipata msaada huo kutoka kwa Marekani katika Mpango wa Marshal. Na suala la mgawo na foleni za chakula na bidhaa baada ya vita je wamewahi kujiuliza kuwa Waingereza walikaa katika mgawo kwa miaka saba na siku waliporuhusiwa kula mayai mawili ni siku ambapo Malkia Elizabeth alisimikwa?

Ninaweza kuendelea kuuliza maswali mengi cha muhimu ni kusema kuwa Mwalimu alikuwa na makosa aliyoyafanya lakini huwezi ukaniambia kuwa eti aliporomosha uchumi kwa siasa za Ujamaa bali kukataa kwake masharti ya kijinga ya IMF na Benki ya Dunia yaliyodai eti serikali yake ilikuwa imeshindwa kuendesha uchumi vizuri ni uongo mtupu. Nilikuwepo wakati ule na nilipanga foleni ya sukari, sabuni na vitu vingine na kwa kweli kama kuna wakati serikali iliwahi kutoa sababu za ukweli kuhusiana hali ya uchumi ni wakati ule. Kama mtu aliyepata nafasi ya kusoma si tu sheria bali uchumi na siasa za taasisi za kimataifa za pesa ninathibitisha kuwa hali mbaya ya uchumi ilichangiwa kwa sehemu kubwa na sababu za nje na si za ndani. Kwa bahati mbaya watu wenye kupenda majibu mepesi na kwa kweli ya kijiweni ndio wako mstari wa mbele kupotosha ukweli na kutaka kutufanya kuwa sisi tu mazezeta wasio na uwezo wa kuchambua mambo. Chuki zao kwa Mwalimu kwa kweli huwezi ukazieleza vizuri kwani mtu ambaye alidiriki hata kutaifisha taasisi za kidini na kuzifanya za watu wote hivi sasa anaonekana kuwa alikuwa na ajenda ya kupendelea watu wa madhehebu fulani? Hivi hii kweli inaingia akilini?

Ninamalizia kusema kuwa maamuzi ya Mwalimu mengi yalilenga ustawi wa watu na si wa kutaka kujinufaisha na kama alikuwa mtu aliyependa watu wasisome je si huyu aliyetaifisha shule ili watu wa dini na makabila yote wasome? Je si huyu aliyeanzisha elimu ya watu wazima na kusababisha kiwango cha kujua kusoma na kuandika kupanda na kuwa asilimia 95? Si huyu aliyejenga miundo mbinu kama Tazara na viwanda vingi ambavyo mafisadi wamevigawa bure? Si huyu aliyeweza kushinda mbinu za benki za nje kuua NBC pale ilipotaifishwa? Si huyu ambaye hakutumia madaraka yake ya uraisi kujitarisha na hata watoto wake hali zake ni zinakaribia za Watanzania wengine.

Inanisikitisha sana kuona haya yote lakini watu wenye ajenda ovu ndivyo walivyo na hawatachoka kupotosha historia ili nia zao ovu zifanikiwe. Napenda kusema kuwa watashindwa kwani wale wenye uelewa mzuri wa mambo tutasimama imara kupangua hoja zao mfu.

Tuendelee kuwaelimisha mambo mbalimbali aliyofanya Mwalim na kutoa picha halisi ya wakati huo..naamini wengi wanaochangia mada hawakuwepo au walikuwa watoto wachanga..wanasikia kwa watu na kujenga picha tofauti ya hali halisi ilivyokuwa wakati huo na mbaya zaidi mtu anajenga chuki na Nyerere kwa sababu amesikia eti enzi hizo wananchi walikuwa wanapanga foleni dukani..bidhaa madukani hazikuwepo..alitoa elimu kwa ubaguzi..amechangia kudunisha maendeleo kwa siasa zake za ujamaa na kujitegemea..kusaidia ukombozi nchi za kusini mwa Afrika.. alikuwa dikteta...nk
Nawasikitikia wale wasiojua Nyerere na kuamini eti alikuwa kiongozi mbaya!
Mimi nakumbuka maisha kabla ya vita ya Kagera 1978-79 yalikuwa mazuri hata tulipolazimika kuingia vitani kutokana na uchokozi wa mara kwa mara wa Nduli na kisha kutangaziwa kufunga mkanda kwa miezi 18 maisha hayakuwa magumu kama tuonavyo sasa.
Alichofanya ktk kipindi hicho kigumu alihakikisha kidogo kilichopo kinagawiwa kwa kila mwananchi. Ni ktk kipindi hicho kukawa na uhaba wa bidhaa kama mchele,sukari,ngano,mahindi na viligawiwa kwa ratiba maalum kwa maduka yaliyochaguliwa kuuzia bidhaa hizo ktk kila mtaa ambapo. Shirika la umma la ugawaji, National Distributors Ltd lilipewa jukumu la kusambaza bidhaa bidhaa hizi muhimu na adimu na ndipo utaratibu wa kupanga foleni ulipofuatwa. Wanaolalamikia utaratibu huu watuambie ungetumika utaratib upi ili kila mtu apate kidogo kilichopo??..foleni ni utaratibu unaotumika sehemu nyingi tu..benki,maofisini,hospitali,visimani na hata barabarani
 
mnamlinganisha Nyerere na nani?Mkapa,Kikwete au Mwinyi? Kwa Africa ya 1960-1980 kiongozi alitakiwa kuwa mjasiri sana manake lilikuwepo wimbi la Mapinduzi lililochagizwa na WAZUNGU.
jaribuni kuwaangalia marais wa Africa kwa miaka hiyo 1960-1980 ni yupi hakuwaweka baadhi ya watu vizuizini for the sake of national security?
Nyerere alitawala kipindi nchi ikiwa na wasomi wachache mno +poor and weak mwdia coverage kwa hiyo angeweza KUFISADI kila kitu ila hakufanya hili.
Hakuianda familia yake kushika madaraka,leo hii mguse mtoto wa rais in any issue uone moto wake.
LEO KIONGOZI ANALAZIMISHA TAIFA LIKUBALI MPANGO WAKE WA UFISADI ingekuwa miaka hiyo angeuza hata barabara kwa kusingizia uboreshwaji wa huduma kwa wawekezaji uchwara.
 
Ndugu wana JF na wa TZ kwa ujumla, napenda kuwa julisha kuwa kwa sasa nchi yetu ipo kwenye tatizo kubwa la kutaka kupindua ukweli kuwa uongo mchana mchana. Nilikuwa nimeandika bango refu na kali, lakini nimeacha kulibandika kwasababu zangu tu. Hata hivyo napenda kuwa pongeza wote waliojaribu kutoa ufafanuzi kulinda ukweli halisia kuhusu uongozi na mchango mkubwa wa baba wa taifa katika nchi yetu.

Kuhusu vuguvugu la kumshutumu Nyerere, mimi naona linatokana na sababu kubwa juu ya uamuzi wake wa kuwapigania wa Afrika na hususani wa TZ wanyonge ambao walikuwa gizani, ili wasimezwe na wajanja wachache kutoka Asia, Europe na Middle East. Hawa watu ni wajanja na ni wabaya historia itakuja kuthibitisha. Kama ktk miaka ya 1950/60s wa-TZ wanyonge, kutoka makabila 122, wasingeweza kupata kiongozi kama Nyerere leo nchi yetu ingekuwa kama America, Morocco, Sudan nk ambako wazawa wanakuwa marginalized na kudhalilishwa.

Kamwe Wahindi na Waarabu hawawezi kumpenda Nyerere kwa kuwakingia wananchi wazawa wakati huo. Ndio maana alipofariki dunia wahindi walianza kutupa picture yake kwasababu walimwona ni kizingiti madhubuti dgidi ya malengo yao na hakuwanufaisha zaidi ya kupigania M-Tanganyika mweusi.

Nilikuwa Uingereza wakati Nyerere anafariki dunia, vyombo vya habari viliripoti kuwa .."aliwapenda sana watu wake, lakini amewaacha bado masikini..". Hata mataifa ya nje yalitambua mapenzi yake ya kweli kwa watu wake. Hawa wanaohoji leo uzalendo wa Nyerere wametoka wapi? Wameyatoa wapi mawazo hasi ya jinsi hiyo? Hatudanganyiki, bado tunafahamu uzri wa Nyerere na uwezo wake mkubwa katika kuongoza nchi yetu.

Najua kuna wengi wameeleza vizuri zaidi yangu, lakini bado na mimi nalazimika kusema kuwa hata JFK wa US aliwahi kusema kuwa; Nyerere angeweza kuwa kiongozi wa State mojawapo huko US. Nyerere alikuwa na akili nyingi, alikuwa na msimamo thabiti, alikuwa mwema sana, alikuwa na upeo mkubwa, na alifanikiwa kutuunganisha kuwa wamoja kama vile hatuna makabila 122 na dini mbalimbali. Haya yote yanamtofautisha sana na viongozi wa leo, wasiokuwa na hoja hadi wanataka kutugawa kwa kutumia udini. Eti hawa ndio wazuri kuliko Nyerere? Hivi tumerogwa !!!

Ujamaa wa Nyerere ulikuwa mzuri, ila tatizo hakukuwa na wajamaa wa kweli kumsaidia kuutekeleza. Hii inafanana na kule kanisani leo, kuna Ukristo mzuri lakini hakuna wakristo wa kweli kuutekeleza Ukristo. Leo tunaanza kushuhudia ubepari ukiporomoka na ujamaa wa Mchina ukileta manufaa kwa Mchina na dunia. Leo tunaona masharti ya WB na IMF yanashindwa kufanya kazi, mf nchi ya Ugiriki juzi juzi, na sehemu zingine. Haya yote Nyerere aliyaona na kuyalalamikia. Mwinyi aliyakumbatia, na Mkapa na Kikwete.. sasa yametufikisha hapa tulipo..pagumu na hatutatoboa. Nchi itavunjika, na itavunjwa na ufisadi, ubinafsi na ubebapari uchwara wa watawala wa leo na siyo Nyerere wa zamani. Nyerere ni mtakatifu na si kwa viwango vya wapinzani wake....
 
Ni kweli nyerere hakupigania uhuru bali alipewa tuu. Hata babaako kama angekuwa mstari wa mbele ktk chama angepewa huo uhuru. Kumbukeni kuwa kipindi hicho tulikuwa chini ya himaya ya waingereza baada ya mjerumani kushindwa ww2. Mkumbuke pia kuwa alikwenda UNO kwenye mkutano miaka ya 1958 akisindikizwa na baadhi ya wahindi (waliosponsor safari yake huko) . Maadhimio ya mkutano huo yalikuwa kwamba watanganyika wasubiri kidogo hadi 1961 ndo watapewa huo uhuru wanaodai. Kwa wale mtakaokumbuka, nyerere alipokuwa anarejea toka yuno akiwa eapot alikuwa ameshikilia bango lenye ujumbe wa kuwa "uhuru 1961'. Kwa hiyo ni kweli kabisa nyerere hakupigania uhuru. Kumbukeni kuwa wakati wa mkoloni kulikuwa na matabaka yaani wazungu(tabaka la juu) waasia(kati) na weusi(chini). Kwa maan hiyo waasia(wahindi) walikuwa wanaloby namna ambavyo watakuwa tabaka la juu na ndio maana walishadadia sana na kusupport move yote ya kuomba uhuru. Mtakubaliana na mimi kwamba wahindi ni wataalamu wa lobying.mtakubaliana na mimi pia kuwa katika wageni wote waliokuwapo enzi za ukoloni, ni wahindi pekee ndo hawakufukuzwa na ndo hadi sasa wako wanamiliki biashara nyingi na kuishi katika maeneo prime ya miji yetu mikubwa. Watu kama akina mtikira ndo maana walikuwa wanamchukia sana nyerere kwa kuwabeba "magabachori'
Kwa maana nyingine ni sawa na sasa ambapo matajiri (akina rostam na wengineo) wananyenyekewa kwa sababu ya kusupport chama. Hata enzi za mwalimu walikuwepo. Ninachoweza kusema ni kuwa Nyerere alikuwa na "stupidity innocense". Mkumbuke kuwa amepewa nchi akiwa a mere guy, hajui mambo ya uchumi,hana chochote yaani hakuwa na experience yoyote ya uongozi pamoja na kuwa kiongozi wa TAA na baadae Tanu. Ujinga na uppuuzi wake unakuja pale alipokuwa hataki ushauri toka kwa watu wataalamu kama akina mtei, kolimba nk. Mjue pia kuwa ndo maana uongozi wa Nyerere ulijaa viongozi ambao noi ma yes men/women. Yeyote aliyeonekana kuchallenge aliwekwa kizuizini au kupelekwa mbali mfano kuwa balozi.
Ukiangalia uchumi wa Tanganyika na baadae Tanzania utagundua kuwa wakoloni walituacha pazuri sana. Baada ya kupewa uhuru nyerere na wenzake walikuwa wakisherehekea tangu hiyo 61 hadi kuungana na zanzibar. Miaka yote hiyo no production at all. Kilichokuwa kinafanyika ni kuchukua kwenye hivyo viwanda. Kuja kutahamaki uchumi unaanza kuyumba na yeye kuja na arusha declaration(ujamaa na kujitegemea-african socialism) kama suluhisho la kurevive uchumi. Lakini kwa sababu ya mipango mibovu inashindwa. Come 1972 anakuja na villagilization anahamisha watu mahali ambapo walizoea kulima( kwa maana wanajua majira ya mwaka, udongo nk) na kupelekwa sehemu ngeni. Matokeo yake watanzania wakawa stranded. Hawajui cha kufanya. Unapita msimu wa kwanza na wapili kwani hawajui ni zao gani walime na majira hawayajui. Baati mbaya ukame unaikumba nchi miaka ya 1975 na kuleta disaster ya njaa. Kumbuka kuwa tangu 1972 uzalishaji wa chakula unayumba kwa sababu ya vilagisation, ukame unaikumba nchi, matokeo yake ni njaa. Kama mnakumbuka enzi za unga wa Yanga kama msaada toka marekani. 1978 vita ya kagera ambayo inaigharimu tanzania mamilioni ya shilingi. Kwa hiyo tanzania ikawa haina pesa hata kidogo.
Kuna tetesi kuwa baada ya vita na I'd amin nyerere alitaka kung'atuka lakini intellijensia ikamshauri asubiri na akaamua kusogea hadi hiyo 1985. Alipong'atuka na kuwa nje ya uwanja ndo akaanza kuhisi madudu aliyofanya na kuwa kama mshauri wa serikali.
Mkumbuke pia kuwa uchumi ulipoanza kuyumba miaka ya 1975 mataifa mbalimbani wakiwemo IMF walikuwa wakishauri nchi yetu kujiunga na stractural adjustment programs(SAPs) kama suluhisho la uchumi lakini nyerere alikataa kabisa. Baada ya nyerere kujiuzuru, haya mataifa yaliendelea kushauri serikali kwani hali ya uchumi ilikuwa mbaya sana. Sharti mojawapo kwenye hizo SAPs ilikuwa ni kuingia kwenye vyama vingi. Ilipofika mwaka 1992 kukawa hamna jinsi na nyerere akamshauri mwinyi akubaliane na hilo sharti. Lakini kwa sababu mwamko wa vyama vingi ulikuwa mdogo miaka hiyo ikabidi nyerere amuombe mrema(usalama wa taifa) aanzishe chama kama kiini macho kwa haya mataifa ili tuweze kuendelea kupata misaada. Mantiki ikiwa sio kukifanya kiwe chama kikubwa bali kiwe kama chambo kwa haya mataifa. Hapo ndipo nccr mageuzi ikazaliwa na vyama vinginevyo. Kama mtakumbuka nccr mageuzi ilipanda chati sana 1995. Mtakumbuka pia kwenye baadhi ya mahojiano ya nyerere aliwahi kusema hatuwezi kumuachia mwizi(mchaga),mbwa(askari) kwenda ikulu na ndipo nyerere akaingilia kati kufanya kampeni chafu dhidi ya mrema hadi nccr kukosa uraisi 1995. Mkapa akaingia ndani ya mjengo kwa mgongo wa mwalimu.
Naomba kuhitimisha kwa kusema kuwa nyerere kweli hakuwa kiongozi mzuri, na hakuwa anasilikiza ushauri toka kwa mtu yeyote. Laiti kama angeshaurika tusingekuwa hapa tulipo. Kwa hiyo haya yanayotokea sasa ni matokeo ya uongozi mbovu na wakidikteta aliokuwa nao nyerere.
I stand to be corrected.

Mkuu hizo Nondo zako ulizoshusha sio mchezo lazima nikupe thanx
 
yapo mabaya na mazuri yake,na nzuri zaidi hakukataa mapungufu yake aliyakubali,
lakini nachomkubali zaidi hakuwa JAMBAZI km hawa MAJAMBAZI tulionao sasa hivi

ila wajue lazima MUNGU wetu atamshinda Shetani wao

TANZANIA BILA MAJAMBAZI INAWEZEKANA
 
Kwa kila mwanasiasa wa Tanzania anaetaka kuungwa mkono na wananchi wengi amekuwa akijitahidi kujionesha kuwa ni mfuasi wa Rais wa kwanza wa Tzania Mwl Nyerere. Anasifiwa kwa kila kitu lakini kwangu mimi simkubali kabisa Mwl Nyerere. Siamini kama alikuwa na kipaji cha uongozi. Alikuwa ni dikteta. Alifinya uhuru wa habari, aliwafunga wapinzani wake, alileta umasikini mkubwa kwa taifa na wananchi wa Tzania. Si kwamba alikuwa anapendwa bali alikuwa anaongoza wananchi wengi wasiojua dunia inakwendaje"wajinga".

Huyo ndio Nyerere. Kwa miwani yangu namuona kuwa ana mabaya mengi kuliko mazuri kama tunavyolazimishwa kuamini. Kutojilimbikizia mali au kutoa huduma za jamii bure si kigezo cha kutokuwa dikteta maana hata Pinnochet, Hitler na Mussolin walikuwa wanatoa huduma za jamii bora na bure kabisa kwa watu wao.

ungekuwa rais enzi za cold war, bila shaka wewe ungefanya mabaya kuliko hayo unayodai nyerere alikuwa au aliyafanya. Kuwa mkuu wa nchi during cold war haikuwa kazi rahisi. bila shaka wewe umezaliwa miaka ya 1980 au 1990, na huijui historia ya dunia.
 
Ni waduni wa fikra nyie mnaosema Nyerere hakufanya jambo lolote. Ni nyie mliopigania uhuru? Walikuwa wengi ndio, lakini ilikuwa ni lazima mmoja achomoze kuwa kinara. Na huyu ni Nyerere. Wakati nchi inapata uhuru toka ukoloni ni watanganyika wangapi waliokuwa wasomi. Lazima tukiri kuwa Nyerere alikuwa na makosa yake kama mtu na kama kiongozi. Lakini Nyerere alikuwa tofauti. Alirithi nchi ikiwa katika hali ya mtafaruku. Alianza kujaribu kuboresha mambo kwa kadri alivyoweza akishirikiana na timu yake aliyoiamini. ilikuwa si lazima achukue wazo la kila mmoja

Katika zama zile udikteta ilikuwa ni lazima. Nakiri hata sasa udikteta katika nchi hii bado unahitajika kwa jinsi mambo yanavyokwenda. Nyerere aliweza kukaa na kutafakari na kisha kutamka kuwa nchi hii-Tanganyika ina maadui watatu wakuu; ujinga, maradhi na umasikini. Hakuishia hapo. Akasema ili kupambana na na maadui hawa yanahitajika mambo makuu manne; watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora. Hakuishia hapo. Ili kuhakikisha hali bora za wananchi zinawekwa katika vitendo akaja na mkakati kamambe-Azimio la Arusha. Wengi tunalijua aidha kwa kuliishi ama kwa kulisoma. Ulikuwa ni mkakati ambao naamini kama watendaji wake wangeufanya kwa umakini ungekuwa na tija kubwa.

Mbali na hapo kawapa miongozo katika maandishi kupitia vitabu vyake na hotuba kemkem zenye weledi wa hali ya juu. Mwisho wa siku alipoona kuwa amejaribu vya kutosha na hakufikia pale alipotaka akaamua mwaka 1985 kung'atuka! Alisema kuwa hata kama angekaa zaidi hakuna jipya ambalo angelileta. Mlitaka ang'ang'anie madakara kama maswahiba zake? Aliwaachia nchi walio chini yake japo aliendelea kuwapa ushauri. Mwinyi alifanya mazuri yapi? Mkapa je? Na huyu sharobaro ndio anafanya nini?

Tusipende sana kung'ang'ania historia. Tangu Nyerere kung'atuka hadi leo karibu miaka 26. Ina maana katika miaka hiyo yota waliomrithi hawakuweza japo kuboresha yale ambayo nyie mnaona yalienda harijojo? Kila mtu ana mapungufu yake lakini katika karne hii tujaribu kuyasahau hayo mnayosema ni mapungufu ya Nyerere na kufanya kazi.
 
Hapo kwenye red hebu tupe ushahidi, sio porojo

Popiexo

Mimi sina upande katika hili na pia namkubali sana nyerere .Lakini pia najua kuna makosa alifanya ! Na najua kwamba baada ya Mtei kumshauri Mwl how to hundle mashirika ya umma aliishia kukimbia nchi . Kipindi kile mashirika ya umma yalikuwa yanaendeshwa kwa hasara.Mfano halisi ni gharama za kuendesha magari ya mashirika yalikuwa ya gharama kubwa sana . Hivyo kuna mambo tunatakiwa kumuenzi Mwl kama mshikamano aliotuwekea lakini lazima tuangalie alipoteleza ili turekebishe.mwenyewe alisema kiongozi sio malaika so i wonder kwa nini unaona hakukosea
 
Comparing with other African leaders (old & current), Nyerere is too far better than most of them.
Namkubali Nyerere kuliko Kikwete
 
kwa kila mwanasiasa wa tanzania anaetaka kuungwa mkono na wananchi wengi amekuwa akijitahidi kujionesha kuwa ni mfuasi wa rais wa kwanza wa tzania mwl nyerere. Anasifiwa kwa kila kitu lakini kwangu mimi simkubali kabisa mwl nyerere. Siamini kama alikuwa na kipaji cha uongozi. Alikuwa ni dikteta. Alifinya uhuru wa habari, aliwafunga wapinzani wake, alileta umasikini mkubwa kwa taifa na wananchi wa tzania. Si kwamba alikuwa anapendwa bali alikuwa anaongoza wananchi wengi wasiojua dunia inakwendaje"wajinga".

Huyo ndio nyerere. Kwa miwani yangu namuona kuwa ana mabaya mengi kuliko mazuri kama tunavyolazimishwa kuamini. Kutojilimbikizia mali au kutoa huduma za jamii bure si kigezo cha kutokuwa dikteta maana hata pinnochet, hitler na mussolin walikuwa wanatoa huduma za jamii bora na bure kabisa kwa watu wao.

na wengi wasiokubaliana na nyerere ni wale waliokuwa wanyonyaji na walafi enzi hizo....hivyo walipoporwa mali zao walizozipata kidhuluma wakajawa na ghadhabu na mwalimu....na kama mwalimu angekuwepo leo....na akazifuata sera zake basi....wote waliotajwa epa...richmond....kagoda....vijisenti...wangekiona cha mtema kuni na watanzania tungekuwa tunazungumza mengine sasa.....!
....i love you mwalimu.....
 
Back
Top Bottom