Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Ni kweli nyerere hakupigania uhuru bali alipewa tuu. Hata babaako kama angekuwa mstari wa mbele ktk chama angepewa huo uhuru. Kumbukeni kuwa kipindi hicho tulikuwa chini ya himaya ya waingereza baada ya mjerumani kushindwa ww2. Mkumbuke pia kuwa alikwenda UNO kwenye mkutano miaka ya 1958 akisindikizwa na baadhi ya wahindi (waliosponsor safari yake huko) . Maadhimio ya mkutano huo yalikuwa kwamba watanganyika wasubiri kidogo hadi 1961 ndo watapewa huo uhuru wanaodai. Kwa wale mtakaokumbuka, nyerere alipokuwa anarejea toka yuno akiwa eapot alikuwa ameshikilia bango lenye ujumbe wa kuwa "uhuru 1961'. Kwa hiyo ni kweli kabisa nyerere hakupigania uhuru. Kumbukeni kuwa wakati wa mkoloni kulikuwa na matabaka yaani wazungu(tabaka la juu) waasia(kati) na weusi(chini). Kwa maan hiyo waasia(wahindi) walikuwa wanaloby namna ambavyo watakuwa tabaka la juu na ndio maana walishadadia sana na kusupport move yote ya kuomba uhuru. Mtakubaliana na mimi kwamba wahindi ni wataalamu wa lobying.mtakubaliana na mimi pia kuwa katika wageni wote waliokuwapo enzi za ukoloni, ni wahindi pekee ndo hawakufukuzwa na ndo hadi sasa wako wanamiliki biashara nyingi na kuishi katika maeneo prime ya miji yetu mikubwa. Watu kama akina mtikira ndo maana walikuwa wanamchukia sana nyerere kwa kuwabeba "magabachori'
Kwa maana nyingine ni sawa na sasa ambapo matajiri (akina rostam na wengineo) wananyenyekewa kwa sababu ya kusupport chama. Hata enzi za mwalimu walikuwepo. Ninachoweza kusema ni kuwa Nyerere alikuwa na "stupidity innocense". Mkumbuke kuwa amepewa nchi akiwa a mere guy, hajui mambo ya uchumi,hana chochote yaani hakuwa na experience yoyote ya uongozi pamoja na kuwa kiongozi wa TAA na baadae Tanu. Ujinga na uppuuzi wake unakuja pale alipokuwa hataki ushauri toka kwa watu wataalamu kama akina mtei, kolimba nk. Mjue pia kuwa ndo maana uongozi wa Nyerere ulijaa viongozi ambao noi ma yes men/women. Yeyote aliyeonekana kuchallenge aliwekwa kizuizini au kupelekwa mbali mfano kuwa balozi.
Ukiangalia uchumi wa Tanganyika na baadae Tanzania utagundua kuwa wakoloni walituacha pazuri sana. Baada ya kupewa uhuru nyerere na wenzake walikuwa wakisherehekea tangu hiyo 61 hadi kuungana na zanzibar. Miaka yote hiyo no production at all. Kilichokuwa kinafanyika ni kuchukua kwenye hivyo viwanda. Kuja kutahamaki uchumi unaanza kuyumba na yeye kuja na arusha declaration(ujamaa na kujitegemea-african socialism) kama suluhisho la kurevive uchumi. Lakini kwa sababu ya mipango mibovu inashindwa. Come 1972 anakuja na villagilization anahamisha watu mahali ambapo walizoea kulima( kwa maana wanajua majira ya mwaka, udongo nk) na kupelekwa sehemu ngeni. Matokeo yake watanzania wakawa stranded. Hawajui cha kufanya. Unapita msimu wa kwanza na wapili kwani hawajui ni zao gani walime na majira hawayajui. Baati mbaya ukame unaikumba nchi miaka ya 1975 na kuleta disaster ya njaa. Kumbuka kuwa tangu 1972 uzalishaji wa chakula unayumba kwa sababu ya vilagisation, ukame unaikumba nchi, matokeo yake ni njaa. Kama mnakumbuka enzi za unga wa Yanga kama msaada toka marekani. 1978 vita ya kagera ambayo inaigharimu tanzania mamilioni ya shilingi. Kwa hiyo tanzania ikawa haina pesa hata kidogo.
Kuna tetesi kuwa baada ya vita na I'd amin nyerere alitaka kung'atuka lakini intellijensia ikamshauri asubiri na akaamua kusogea hadi hiyo 1985. Alipong'atuka na kuwa nje ya uwanja ndo akaanza kuhisi madudu aliyofanya na kuwa kama mshauri wa serikali.
Mkumbuke pia kuwa uchumi ulipoanza kuyumba miaka ya 1975 mataifa mbalimbani wakiwemo IMF walikuwa wakishauri nchi yetu kujiunga na stractural adjustment programs(SAPs) kama suluhisho la uchumi lakini nyerere alikataa kabisa. Baada ya nyerere kujiuzuru, haya mataifa yaliendelea kushauri serikali kwani hali ya uchumi ilikuwa mbaya sana. Sharti mojawapo kwenye hizo SAPs ilikuwa ni kuingia kwenye vyama vingi. Ilipofika mwaka 1992 kukawa hamna jinsi na nyerere akamshauri mwinyi akubaliane na hilo sharti. Lakini kwa sababu mwamko wa vyama vingi ulikuwa mdogo miaka hiyo ikabidi nyerere amuombe mrema(usalama wa taifa) aanzishe chama kama kiini macho kwa haya mataifa ili tuweze kuendelea kupata misaada. Mantiki ikiwa sio kukifanya kiwe chama kikubwa bali kiwe kama chambo kwa haya mataifa. Hapo ndipo nccr mageuzi ikazaliwa na vyama vinginevyo. Kama mtakumbuka nccr mageuzi ilipanda chati sana 1995. Mtakumbuka pia kwenye baadhi ya mahojiano ya nyerere aliwahi kusema hatuwezi kumuachia mwizi(mchaga),mbwa(askari) kwenda ikulu na ndipo nyerere akaingilia kati kufanya kampeni chafu dhidi ya mrema hadi nccr kukosa uraisi 1995. Mkapa akaingia ndani ya mjengo kwa mgongo wa mwalimu.
Naomba kuhitimisha kwa kusema kuwa nyerere kweli hakuwa kiongozi mzuri, na hakuwa anasilikiza ushauri toka kwa mtu yeyote. Laiti kama angeshaurika tusingekuwa hapa tulipo. Kwa hiyo haya yanayotokea sasa ni matokeo ya uongozi mbovu na wakidikteta aliokuwa nao nyerere.
I stand to be corrected.

Debe tupu haliachi kupiga kelele! Lakini kelele nyingine ni za kutia aibu!
 
Mkuu mbona unajichanganya na hizo data zako? unasema mwaka 1978 uchumi wetu ulikuwa mzuri sana hadi IMF walidai kuwa lazima itumie akiba yake yake ya nje ibakie isiozidi miezi sita hapo mwaka 1977, hapa kuna vitu viwili umechanganya miaka na umechukuwa data za IMF kama ushahidi, hapo hapo utaki tena kuzitumia data za IMF baada ya kumwambia serikali yake imeshindwa kuendesha uchumi unasema ni uongo mtupu, kuhusu vita Tanzania wamepewa misaada mingi tu kutoka China, Ujerumani,Uingereza,Malawi,Kenya,nchi za Scandnavia nazo zilitoa msaada wakati wa vita na Uganda, hivo vita vyenyewe vilichukuwa miezi minane tena vita kamili vya kupigana na vya miezi mitatu, ndio Tanzania tukafirisika?

Nadhani ninazungumza na mtu ambaye hataki kuelewa au haelewi kile anachokisoma. Mnamo mwaka 1977 IMF waliitaka Tanzania itumie akiba yake ya kigeni kwani ilikuwa kubwa sana eti nchi isiwe na pesa za akiba ya zaidi ya miezi sita. Nyerere aliona ujinga wao (na ndio kama ushauri huo walioutoa kwa Malawi mwaka 2002 eti iuze akiba yake ya mahindi na pale ilipouza mwaka uliofuata ukame ukaingia na Malawi ikalazimika kuomba chakula nje. IMF na Benki ya Dunia wakaruka wakasema wao tu walitoa ushauri). Ndiyo maana nikasema mwaka 1978 hali yetu ya uchumi ilikuwa nzuri sana hata wafanyakazi wa Benki Kuu wakaambiwa watapewa bonasi ya shilingi 6,000/- nchi nzima ikapinga.Najua hilo hulijui kwani kama ungekuwa unajua usingeuliza hali yetu ya uchumi ilivyokuwa.

Sasa baada ya vita ambayo nimekuambia ilitugharimu dola milioni moja kila siku ya Mungu nchi yetu ikawa imefilisika. Na kama nilivyosema ni kuwa nchi ikitoka vitani inahitaji misaada na mikopo mataifa ya magharibi yalikataa na wakati ule ndipo Robert McNamara aliyekuwa Raisi wa Benki ya Dunia alipotangaza Structural Adjustment Programs (SAPs). Ushauri wa Benki ya Dunia ilikuwa ni kwamba Tanzania lazima iachane na sera za ujamaa na ibinafsishe mashirika yake na kushusha thamani ya sarafu yake na kutokana na "ukweli" kwamba imeendesha uchumi wake vibaya. Mtei alikubali haya Mwalimu hakuamini hayo kwani huwezi kumueleza mtu ambaye uchumi wake umeathiriwa na vita eti alikuwa anaendesha uchumi wake vibaya. Ndiyo maana nikatoa mfano wa nchi za magharibi na Uingereza jinsi zilivyosaidiwa na Marekani kufufua uchumi wao baada ya vita ya pili ya dunia. Hapakuwa na lawama zozote zile zilizoelekezwa kwao eti vita ilifanya waendeshe uchumi wao vibaya. Sasa Mwalimu alishangaa kuona watu ambao miaka miwili walikuwa wanasema una akiba kubwa ya fedha za kigeni na uzitumie, miaka miwili baadae wanakuambia eti umeendesha uchumi wako vibaya.

Kuhusu misaada kutoka Scandinavia nitakuwa muongo kama sitakiri hilo kwani ni kweli kabisa kuwa nchi hizo zilitupa misada si kwa ajili ya kupigana vita bali kulipia huduma za elimu na afya kama ambavyo walikuwa wanafanya kabla ya vita. Hawakutupa fedha za kununua silaha.Waingereza hawakutusaidia kupigana vita au kutupa msaada wa kupigana vita bali wao walitoa fedha za kujenga barabara ya Makambako-Songea kama asante yao kwa sisi kumung'oa Amini madarakani na kama kuwaenzi wapiganaji wetu 18 waliofariki katika ajali ya gari katika mlima wa Lukumburu wakitokea vitani.

Ninashangazwa na kauli eti Malawi na Kenya walitusaidia sijui unazungumzia msaada wa aina gani. Msaada wa Kenya kwetu ulikuwa ni wa kutumia anga na barabara zao na vilevile mawasiliano ya ndege na ndio hata waliwadanganya baadhi ya marubani wa Gaddafi kutua KIA badala ya Entebbe wakifikiri kuwa KIA ni Entebbe. Kama msaada wa pesa huo ni uongo. Malawi hawakutupa kitu kwani hawakuwa na cha kutupa na kwa kweli Banda aliogopa sana baada ya ushindi wetu dhidi ya Amini na alituma ujumbe kutaka suluhu kwani alifikiri kuwa baada ya Amini, yeye ndiye ambaye naye tungemshughulikia. Kuhusu China ni kweli tulipata msaada wa kununua zana za kivita si bure bali kwa mkopo. China hawakutupa fedha za kufufua uchumi wetu. Ningetegemea kuwa ungetaja Msumbiji kwani hao ni kweli walitoa askari wao kupigana nasi katika vita hivyo. Kitendo cha Msumbiji kinaeleweka kwani sisi ndio tuliowasaidia sana wao kupigania uhuru wao na tulikuwa na urafiki kama sio undugu wa "kuchanjiana damu" kwani askari na wananchi wenzetu walikufa katika vita vya uhuru wa Msumbiji.

Hivyo basi mikakati yote ya kufufua uchumi baada ya vita iliendeshwa kwa fedha zetu wenyewe na msaada wa mataifa rafiki kama ya Scandinavia kwa huduma zile zile ambazo walikuwa wanatusaidia kabla ya vita. Lakini kutokana na kuwa hali ya uchumi wa dunia iliendelea kuwa sio nzuri jitihada zetu hazikuweza kufanikiwa sana. Lakini nchi yetu haikuzama na kutolewa katika msimamo wake wa kupigania ukombozi wa Afrika. Hiyo ndiyo hali halisi. Ufufuaji wa uchumi wetu ulihitaji fedha nyingi lakini mataifa ya magharibi hayakuwa tayari kutukopesha kwani sisi tulionekana kuwa ni taifa ambalo halilambi miguu yao.

Sitaki kuendelea kuzungumzia sababu nyingine ambazo zilichangia nchi yetu kuingia katika hali ngumu ya uchumi kama vile kupanda kwa bei ya mafuta, kushuka kwa bei ya mazao yetu ghafi katika soko la dunia na hali mbaya ya hewa. Lakini kama una nia ya kuelewa na kujifunza hizo zinatosha kukufanya uelewe lakini kama ni mbishi kama mshipa hutanielewa na utaendelea na ubishi wa kijiweni.
 
Kwa kila mwanasiasa wa Tanzania anaetaka kuungwa mkono na wananchi wengi amekuwa akijitahidi kujionesha kuwa ni mfuasi wa Rais wa kwanza wa Tzania Mwl Nyerere. Anasifiwa kwa kila kitu lakini kwangu mimi simkubali kabisa Mwl Nyerere. Siamini kama alikuwa na kipaji cha uongozi. Alikuwa ni dikteta. Alifinya uhuru wa habari, aliwafunga wapinzani wake, alileta umasikini mkubwa kwa taifa na wananchi wa Tzania. Si kwamba alikuwa anapendwa bali alikuwa anaongoza wananchi wengi wasiojua dunia inakwendaje"wajinga".

Huyo ndio Nyerere. Kwa miwani yangu namuona kuwa ana mabaya mengi kuliko mazuri kama tunavyolazimishwa kuamini. Kutojilimbikizia mali au kutoa huduma za jamii bure si kigezo cha kutokuwa dikteta maana hata Pinnochet, Hitler na Mussolin walikuwa wanatoa huduma za jamii bora na bure kabisa kwa watu wao.

Thread yako ni nyepesi sana kutoa conclusion hiyo...... leta hoja za msingi zitushawishi hayo unayo sema. Inawezekana nyerere alikuwa na mapungufu yake kama mtu mwingine yeyote. Lakini dhamiri yake ilikuwa safi na hakufanya madudu kama tuyaonayo leo ambayo ni product ya unafiki na uzandiki uliokithiri. Ina wezekana sera za Nyerere zilishindwa , thats not a supprise kwasababu ujamaa umeanguka ulimwenguni kote ( USSR, China ina lega lega etc).

Nita muheshimu Nyerere kwa vitu viwili, dhamiri yake ilikuwa safi kwamba watanzania wote wafaidike na matunda ya uchumi wao ( elimu , matibabu etc bure). Tunao nduga zetu wengi wamesoma na kufika viwango vya juu kwa kusomeshwa na nchi bure. Hii yote ni juhudi za Mwalimu, lakini wameturn kuwa hostile citizens , wana tafuna wananchi wenzao na nchi kwa ujumla badala ya kuwa msaada( chenge , Lowasa na wengine wengi ). Kitu kingine ambacho Nyerere anastahili kupewa sifa, ni kwamba aliishi kile alichokiamini na kamwe hakuwa mnafiki ( neither favore to his family nor to his friends). Kurudi kuishi butiama baada ya uraisi miaka ishirini na kitu bila mali yeyote! Huyu alikuwa ni mzalendo wa hali yajuu sana , ni raisi gani leo hili ameliweza hili !!? tunaona aibu wanazozipata Arabic leaders now.

Nyerere hakuwa dictotor isipokuwa alihitraji hoja za nguvu na sio blabla..... kwa taarifa yako miongoni mwa watu ambao walikuwa wanatofautiana na kushindana sana hoja na Nyerere alikuwa Sokoine ( former prime minister), lakini hakuwahi kutiwa kizuizini na zaidi alimpenda. Hata mbunge mmoja alipojitoa katika chama wakati wa campaign na kugombea Ubunge kama independent candidate Nyerere ndie alimtetea.

Watu wengi aliowaweka kizuizini walikuwa wanaendesha vuguvugu la uhaini, and any president would have done the same following taarifa za kiusalama na kwa manuafaa ya uma.

Tchao
 
Kwa zama zake Mwalimu alikua aggressive sana,mwenye kufikiri sana mjenga hoja za nguvu na mwenye msimamo mkali kwa kile alichokiamini...Yamesemwa mengi juu yake,kwamba pamoja na mengi aliyoyafanya hakusita kutumia nguvu kubwa kuzima wale walioonekana mwiba kwake...well...kibinadamu inawezekana kafanya! Pia alikua mwasisi wa mambo mengi kimaendeleo ambayo km watendaji wake wangekua na maono yake Tanzania ya leo (Km viongozi waliomtangulia wangeishi ktk philosophy yake) ingekua mbali kimaendeleo....Binafsi namkubali sana mwalimu pamoja na madhaifu yake so far hakupata kutokea mwingine baada ya Utawala wa Mwalimu aliyefika robo ya Utendaji wake...
 
myhem,
Wanaopenda kuandikwa upya kwa historia ya Tanzania wameshaanza na wana sapoti. Kiongozi wao, Kikwete, kishaweka mguu majini kwa kudokeza kuwa Nyerere aliiacha nchi hii maskini. Wale waliokuwepo enzi zetu, anasema Kikwete, watakumbuka shida za kiuchumi tulizozipitia, niki paraphrase aliyoyasema. Kwa hiyo sitashangaa kuwa hayo ndiyo yanayozungumzwa misikitini, kwenye Al nuur na kwenye redio imani. Kwa mtu ambaye ameshindwa kuongoza, inakuwa rahisi kukumbushia udhaifu wa waliomtangulia kuliko kuonyesha kuwa hapa mimi nimefanya hiki na hiki.
 
Kwa zama zake Mwalimu alikua aggressive sana,mwenye kufikiri sana mjenga hoja za nguvu na mwenye msimamo mkali kwa kile alichokiamini...Yamesemwa mengi juu yake,kwamba pamoja na mengi aliyoyafanya hakusita kutumia nguvu kubwa kuzima wale walioonekana mwiba kwake...well...kibinadamu inawezekana kafanya! Pia alikua mwasisi wa mambo mengi kimaendeleo ambayo km watendaji wake wangekua na maono yake Tanzania ya leo (Km viongozi waliomtangulia wangeishi ktk philosophy yake) ingekua mbali kimaendeleo....Binafsi namkubali sana mwalimu pamoja na madhaifu yake so far hakupata kutokea mwingine baada ya Utawala wa Mwalimu aliyefika robo ya Utendaji wake...


Wivu tu unawasumbua huna sababu yoyote ya kusema mazuri aliyofanya .... .... ....... kibaya chajiuza.
 
There's no need for name calling,one can contribute when feels so.

Mwalimu alikuwa mmoja wa viongozi wenye kipaji
,lakini kumfanya untouchable nadhani hatujengi utamaduni mzuri kwa taifa letu.Utamaduni wa kutotofautisha critism na disrespect hautusaidia(kumbuka mapanki&Kikwete katuni).

Mimi naona viongozi wetu wanamtumia Mwl kwa maslahi yao wenyewe rather than kumuenzi baba wa taifa.Tumeona mara nyingi wakifanya hivyo,ili mtu akipinga iwe "Mwl didn't stand for that".

Tukitaka kufaidika na Mwl kikweli tujifunze kuwa wa wazi,alipokosea tuseme na alipofanikiwa hali kadhalika.Kukosoa mapungufu yake sio usaliti.

Kama yote yaliyotajwa na mtowa mada ka "fail", kipaji kipi alichokuwa nacho? labda cha kupiga porojo au "komedi"?
 
Kwa zama zake Mwalimu alikua aggressive sana,mwenye kufikiri sana mjenga hoja za nguvu na mwenye msimamo mkali kwa kile alichokiamini...Yamesemwa mengi juu yake,kwamba pamoja na mengi aliyoyafanya hakusita kutumia nguvu kubwa kuzima wale walioonekana mwiba kwake...well...kibinadamu inawezekana kafanya! Pia alikua mwasisi wa mambo mengi kimaendeleo ambayo km watendaji wake wangekua na maono yake Tanzania ya leo (Km viongozi waliomtangulia wangeishi ktk philosophy yake) ingekua mbali kimaendeleo....Binafsi namkubali sana mwalimu pamoja na madhaifu yake so far hakupata kutokea mwingine baada ya Utawala wa Mwalimu aliyefika robo ya Utendaji wake...

Kiongozi hana sababu ya kulaumu watendaji, kiongozi ndio mtendaji mkuu, alishindwa uongozi si watendaji walioshindwa. Hivyo ndivyo ilivyo.
 
myhem,
Wanaopenda kuandikwa upya kwa historia ya Tanzania wameshaanza na wana sapoti. Kiongozi wao, Kikwete, kishaweka mguu majini kwa kudokeza kuwa Nyerere aliiacha nchi hii maskini. Wale waliokuwepo enzi zetu, anasema Kikwete, watakumbuka shida za kiuchumi tulizozipitia, niki paraphrase aliyoyasema. Kwa hiyo sitashangaa kuwa hayo ndiyo yanayozungumzwa misikitini, kwenye Al nuur na kwenye redio imani. Kwa mtu ambaye ameshindwa kuongoza, inakuwa rahisi kukumbushia udhaifu wa waliomtangulia kuliko kuonyesha kuwa hapa mimi nimefanya hiki na hiki.

Tuonyeshe ni wapi nyerere alifanikiwa?
 
If I were to choose between what I have now and Nyerere...definitely I would choose Nyerere. He was a leader no matter what we want to say or no matter how he failed...what we see now is more than a failure
 
If I were to choose between what I have now and Nyerere...definitely I would choose Nyerere. He was a leader no matter what we want to say or no matter how he failed...what we see now is more than a failure

Ulikuwepo wakati wake?
 
Kiongozi hana sababu ya kulaumu watendaji, kiongozi ndio mtendaji mkuu, alishindwa uongozi si watendaji walioshindwa. Hivyo ndivyo ilivyo.
Funny you shoud say that. Today is 2011 na kila siku nasikia makosa ya Kikwete wakitupiwa lawama wasaidizi, eti, ooh, hajapewa ushauri mzuri, eti, ooh, wasaidizi wake hawajamwelekeza ipasavyo ad infinitum. Lakini naelewa uko kwenye misheni. Good luck!
 
Whatever they say about Nyerere he was a great philosopher, he believed in human values and had a strong will of doing what he believed in.
The world is full of insanes irrespective of Black or white, Moslem or Christian, poor or rich, etc and at point of time when prooved this theory AKANG'ATUKA, let him rest in peace.
 
Huyu jamaa alikuwa ni kiongozi bora na wala siyo mbabaishaji kama viongozi waliopo sasa
 
ndugu yangu unapokuwa na kiongozi anayewapigia magoti mafisadi hapo unategemea nini? unatuongezea uchungu kutukumbusha mema aliyofanya baba yetu.
 
Nyerere alifanya mengi mazuri,lakini hakufanya mabaya???nahisi alikuwa mjeuri sana na mgumu wa kufanya naye kazi!!!kwa nini hakusikiliza maoni ya kambona na wenzake mpaka wakakimbia nchi??????????ni kwa nini walikimbia nchi!labda alitaka kuwaua??mbona hakumsikilza waziri wake wa fedha mtui????anghhhhh
 
When the other fellow takes a long time to do something, he is slow. When I take a long time to do something, I am thorough.
When the other fellow does not do it, he is lazy. When I do not do it, I am busy.
When the other fellow does it without being told, he is overstepping his bounds. When I go ahead and do it without being told, that is initiative.
When the other fellow states his opinion strongly, he is bull-headed. When I state my opinion strongly, I am firm.
When the other fellow overlooks a few rules of social behaviour, he is rude. When I skip a few rules of social behaviour, I am doing my own thinking.
-Tom Knight

In the quotation above, was Mwalimu the other fellow or I?
 
Soma kitabu cha Mzee Mtei anaelezea tofauti zake na Mwalimu. Kambona hakuwa na ushauri. Alikuwa na mipango ya kisirisiri ilipogundulika akakimbia nchi. Ni kweli Nyerere alikuwa jeuri lakini jeuri yake ilikuwa ni jeuri kwamba Waafrika tunaweza. Siyo kukubali kila kitu unachoambiwa na wazungu. Mzee Bomani aliwahi kuniambia kuwa watu walikuwa wanaogopa kumpa Mwalimu ushauri kwa sababu alikuwa anauliza maswali mengi. Ukijenga hoja yako vizuri na kuweza kuitetea, utateka sikio la Mwalimu. Wale waliokuwa wanashindwa kujenga hoja ndio waliokuwa wakilalamika kuwa Mwalimu haambiliki.
 
Back
Top Bottom