Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Hivi kwa nini ikitokea mtu akatoa hoja inayopingana na "Umungu mtu" wa Julius watu wanamrukia as if ni msaliti?

Mi nadhani hapa JF is where we dare talk openly, Nyerere was a human just like me and you. Hii ya kumuona kama Mungu mtu kwamba..the King can do no wrong nadhani si sawa. Watu wanatoa experience zao waliyoyapata na kuyaendure. Please give them a decent recognition hata kama hukubaliani na wanayoyaandika, lakini thats their experience. Kwamba nilisoma bure, it doesnt blind me kwamba kulikuwa na evils zinatendeka. Ni yale yale ya CCM eti chama kilikulea kwa hiyo "huwezi kupinga mzazi"

Nyerere did what any responsible leader should have done. Responsible leadership, fight corruption etc. Na haya ndo inabidi tujifunze kwamba ukipewa dhamana ya uongozi wa umma, usiibe na wala usijilimbikizie mali... lets not be apologetic...we should be bold enough to say this was wrong and this was right! I really dont buy this crap ya kumuona Mwalimu as if is our second God and if anybody says otherwise, we are on his/her nect..its unfair!! Jamaa alikuwa na mapungufu, watu walisweka ndani kwa ajiri ya kuwa na mawazo tofauti, watu walinyang`anywa mali zao walizotafuta kwa jasho simply because Julius alitaka kutekeleza sera zisizotekelezeka za ujamaa! watu walihamishwa vijiji..familia yangu ikiwemo (it was a good move,with good intentions but unplanned and heavy handed). Process haikuwa shirikishi...

Na usishangae mtu leo akiandika kitabu au memoir kuelezea what he new about Mwalimu ...people will come up na kumsulubu simply because mawazo yake hayakubaliani na indoctrination ambazo watanzania tumefundishwa. Kwamba hajawahi tokea kiongozi kama Mwalimu!! nyerere was a good leader for our country no doubt on that, he was a failure on many fronts: Mfano katiba na misingi ya chama kandamizi, poor accountability kwa watawala.... tunayopigana nayo leo..aliiweka yeye..hii mifumo ya kidekteta aliijenga yeye. Kuwa na katiba isiyokuwa na mawazo ya wengi (ya mwaka 1977) aliiweka yeye na ndo maana waliopo leo wanaona hawana haja ya kuibadili kwa sababu inawapendelea wao..on and on...).

Please for the sake of our country we should LEARN from the history and accomodate the views of those we dont agree with.

We shuld be a nation which is ready to learn from its past history na yale mabaya tuya-admit na yale mazuri tuyafanyie kazi. Na wala siyo kila hoja inayolenga kutoa upande wa pili wa shillingi wa Mwalimu tunawaona wajenga hoja kama wasaliti wa taifa. Hell no!

Nyerere was good leader. BUT HE HAD MANY FAILINGS AND WE SHOULD RESPECT AND ACCOMODATE THOSE BOLD ENOUGH TO EXPOSE THEM.

U-mungu mtu umetoka wapi; mbona mimi sijauona? Au umo akilini mwako?

The author's write-up not even fit for a work of fiction. I wouldn't recommend wasting money on it.
 
Hoja hii nadhani kuna haja ya kuwa merged (kuunganishwa) na topic kadhaa. Ilikuwa sero na sasa imerejea. I will keep a close eye on this. Kama kuna haja ya kuifunga moja kwa moja basi naomba maoni yenu

Invisible

ziunganishe tu.. labda wataelewa kwanini wengine tunapiga gumzo tu...
 
ziunganishe tu.. labda wataelewa kwanini wengine tunapiga gumzo tu...
Done buddy,

Nilikuwa naifanyia marekebisho hii hoja kuu ambayo niliiweka sero mwaka 2006 na sasa kila kitu kiko OK.

Kwa waliokuwa hawajui nini kiliwahi kujadiliwa dhidi ya Nyerere basi pata muda wa kudadavua kwa mapana ni yepi tulishaongelea ili facts zaidi ziwekwe hapa.

Invisible
 
We are two lucky men...coz I got kid sister...

Naaah,

I think I and my kid sisterz belong to the luckiest family... It aint that ize to get two of the best heads of JF (Ngabu and Mkjj) at the same time.....lol! May GOD bless us all!
 
Education Under Christian Leadership To many uninformed people, Nyerere is a public defender of secularism in the ruling Party and the government. But his secret meetings with Church leadership is quite the opposite. In his confidential conversation on August 2, 1970, with Rev. Robert Rweyemaum, the then Secretary General of Tanzania Episcopal Conference (TEC), the largest Christian denomination of Catholic Church, Nyerere is quoted in a book Development and Religion in Tanzania by J. P. van Bergen as saying that he has established in TANU a department of political education and that he deliberately appointed a Christian minister to head it not because he was a strong politician but because of his Catholic Faith. This book published by the Catholic Church stated that this reason the Rev. Mushendwa with his strong solid Christian faith, was put in charge of TANU's Development of Political Education. Nyerere continued what was left by the British educational discparity against the Muslims. He was aware of Muslim's grievance in the area of education. He wrote in his book Freedom and Unity that the disparity of educational levels could be used as a political issue
 
In his confidential conversation on August 2, 1970, with Rev. Robert Rweyemaum, the then Secretary General of Tanzania Episcopal Conference (TEC), the largest Christian denomination of Catholic Church, Nyerere is quoted in a book [/B


niliposoma kitabu hicho nikakutana na hilo nikajua wazi kuwa huyo jamaa hajui uhusiano kati ya Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC) na Kanisa Katoliki!! then I gave up. Maana kama mtu hujui uhusiano kati ya Baraza la Chuo Kikuu cha Al-Azhar Misri na Chuo Kikuu cha Al-Azhar inakuwa shida kidogo..
 
..Makala ya JENERALI ULIMWENGU ktk raia mwema. inatoa mwangaza kidogo kuhusu uongozi wa nchi na chama wakati wa Mwalimu Nyerere.

Nyerere na mgawanyiko wa dodoki lake

Jenerali Ulimwengu Machi 5, 2008



NIMEKUWA nikielezea dalili zinazoonyesha kudhoofu kwa chama kilicho madarakani, CCM, mara kwa mara nikijaribu kuonyesha ni wapi kulikotokea kudhoofu huko.

Safari ya kisiasa ya vyama vya siasa, kama ilivyo katika safari nyingine zote katika maisha, huweza kuchukua mikondo ambayo haikutazamiwa, hata na wale wanaoviongoza. Sheria ile ile ya matokeo yasiyotarajiwa inaweza kuwashangaza hata wajuzi wa mambo.

Kifupi, hebu tudurusu mambo makuu yaliyotokea katika historia ya TANU na CCM. Kwanza kilikuwa ni chama cha ukombozi wa Mtanzania na Mwafrika, kilichojengeka katika falsafa ya utu wa binadamu, upendo na mshikamano. Kisha kikawa ni chama cha uongozi wa serikali, kikakamata madaraka ya dola kikiwa na nia ya kutekeleza falsafa hiyo na kuwaletea wananchi maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Kikabuni sera madhubuti kwa lengo la kutekeleza falsafa hiyo. Kikajenga mahusiano ya karibu na wananchi kwa kusikiliza matakwa yao na kuyaandalia mikakati ya kuyatekeleza. Kikaielekeza na kuisimamia serikali ili itende yale yatakayowanufaisha wananchi.

Lakini, taratibu, katika kukua kwake, chama kikaanza kuchukua taswira ya dola, kikajichanganya na serikali, kikawa ni chama-dola. Kikaanza kujenga tabia za ki-imla. Mawazo yaliyotofautiana na mkuu wa chama (na kundi dogo lililojifanya kukubaliana naye kabisa) yakawa ni marufuku. Kikawaengua wale walioonekana kama wenye fikra zisizoendana na mkondo mkuu wa fikra zilizokubalika.

Bila kujua, na bila kupenda, chama kikajikuta kimejitenga na wananchi wa kawaida, kikajiunga na dola. Kikaacha kuongoza; kikawa ni mhimili mwingine wa dola. Hata zile sera zilizobuniwa na chama ili kumkomboa mwananchi wa chini zikatekelezwa kiimla, na matokeo yake yakawa ni kumuumiza mwananchi aliyelengwa kukombolewa. Tumekwisha kujadili matatizo ya utekelezaji wa sera za Ujamaa na ujenzi wa vile vilivyoitwa “Vijiji vya Ujamaa”.

Kimsingi, chama cha siasa ni makutano ya watu wenye fikra zinazofanana, pamoja na tofauti zao ndogo ndogo. Lengo kuu linakuwa ni moja, hata kama zitaelezwa kwa namna tofauti, kila mmoja akiongeza mbwembwe zake na kutumia lugha yake. Dira inakuwa ni moja, hata kama inabidi mara kwa mara kubadilisha mwelekeo wa chombo kufuatana na ukali wa upepo na uzito wa mawimbi baharini.

Chombo kilichoko baharini kina nahodha, na nahodha ndiye kiongozi mkuu, na kila mtu aliyemo ndani ya chombo hicho anamtarajia kuwa atafanya maamuzi yatakayokipeleka chombo hadi pwani. Lakini nahodha lazima awe na masarahangi, wasaidizi wake, wanaomsaidia kuwaongoza mabaharia walio chini yake, na sarahangi hana budi kumshauri nahodha kwa uwazi bila kumchelea.

Masarahangi nao hawana budi kuwasikiliza mabaharia, hata kama ujuzi wa mabaharia wa kawaida unaweza kuwa mdogo sana ukilinganishwa na ujuzi alio nao nahodha au masarahangi wake. Kila mmoja ndani ya chombo, kwa nafasi yake na kwa kiwango kinachokubalika katika mpangilio wa safari, anayo nafasi ya kutoa fikra zake kuhuzu mwenendo wa safari.

Mchakato wa kupeana ushauri kuhusu mwenendo wa safari haufuti madaraka ya mwisho ya nahodha, bali unamjenga, kwa sababu maamuzi yake ya mwisho (na ambayo kila baharia hana budi kuyatekeleza bila ubishi) yanakuwa yametokana na mchango wa fikra za kila mwanamaji aliyemo ndani ya chombo.

Kwa kiasi kikubwa, kama nilivyoeleza awali, TANU, na baada yake, CCM, vilipoteza mwelekeo huu, na kutokana na hilo uongozi wake ukawa unamtegemea kiongozi mkuu ambaye alikuwa habishiwi.

Hakuna shaka moyoni mwangu hata kidogo kwamba Mwalimu Julius Nyerere alikuwa nahodha mahiri na shupavu, mtu mwenye misimamo thabiti na asiyeyumbishwa na jambo lo lote, si tamaa ya mali wala nguvu za mabeberu. Lakini Mwalimu aliiruhusu hali ya kuzungukwa na akina ‘Bwana Ndiyo’ kiasi kwamba, hatimaye, akajikuta anasikiliza ushauri wake yeye mwenyewe. Ushauri wa aina hii, kama tunaweza kuuita ushauri, ni ushauri tasa, hauzai.

Watu waliomzunguka Nyerere, na ambao walilazimika kukubaliana na kila alichosema na kufanya, si kwamba wote walikuwa watu waovu, au wasiokuwa na akili nzuri. Mazingira walimokuwa yaliwafanya wakubali kukaa kimya hata pale walipoamini kwamba makosa yanafanyika. Wachache waliodiriki kubisha walikiona cha mtema kuni, na waliobaki wakajenga ‘busara’ ya kukaa kimya.

Tukumbuke, Mwalimu Nyerere, pamoja na uwezo wake mkubwa na ushawishi usio wa kawaida kwa wananchi, hakuwa katili. Hata pale alipowafanya waliompinga “kuona cha mtema kuni,” hakuna aliyepoteza maisha yake kutokana na msimamo wa kisiasa. Ni kweli, wapo walioumia, waliowekwa kizuizini, waliopelekwa uhamishoni, na wengi waliopoteza ajira. Lakini hakuna aliyekufa kutokana na shughuli hii, na hili si jambo dogo katika Afrika ya wakati huo (na hata ya leo).

Hata hivyo, hali halisi ilijenga kabila zima la wanafiki, watu waliojipendekeza kwa Mwalimu kwa kukubali kila jambo lake bila kubishi na kujitambulisha kama waumini wa dhati wa sera zake. Unafiki huo unadhihirika leo kwa wale ambao bado wamo ndani ya michakato ya kisiasa lakini hawana lo lote la kuwatambulisha na Mwalimu wala sera zake.

Viongozi waliokuja baada ya Mwalimu walirithi hali hii bila kuwa na uwezo wa kifikra wa Nyeyere. Mwalimu aliweza kuyasimamia masuala kadhaa yaliyokuwa na umuhimu mkubwa kwake na kuyafuatilia siku hadi siku, huku akitembelea vijiji na kufanya kazi za sulubu, bega kwa bega na wananchi. Nani atasahau operesheni za Kigoma na Dodoma, kwa mfano?

Wakati wa ujana wake, bado akiwa mwenye nguvu za mwili na uangavu wa akili, Nyerere alitumia muda wake mwingi kuwafundisha na kuwanasihi watu wake, huku akijibidisha kujifunza yeye mwenyewe. Nani amesahau misemo yake, kama “Jifunze kusoma, wakati ni huu”? Au “Mvua za kwanza ni za kupandia”? Nani miongoni mwetu tuliokuwapo wakati huo, amesahau maneno yake kuhusu matumizi ya marejea? Sasa tuulizane, nani anayasema maneno haya hivi leo? Ni dhahiri kwamba Mwalimu alikuwa mwalimu.

Lakini kadri alivyoongeza umri na kuanza kuchoka kimwili ( na akili yake kuelemewa na mzigo wa kufikiri kwa niaba ya wote) ndivyo tulivyoona uzee na uchovu wa chama na serikali yake. Maumbile hayaruhusu mtu mmoja kuendelea milele kufanya kazi ya kufikiri kwa niaba ya watu wote. Atachoka tu, na hatimaye atakufa. Haya tumeyaona.

Kwa sababu wakati wa umri wake wa tija alishindwa kujenga chama imara chenye misingi endelevu, kuondoka kwake, kwanza kutoka madarakani na pili duniani, kulikiacha chama kilichochoka kama alivyokuwa kachoka yeye, na tangu hapo hakijaweza tena kurejea taswira yake ya awali. Mwalimu mwenyewe, kama nilivyosema katika sura zilizotangulia, alipata wasaa wa kukichunguza chama chake na kukishangaa jinsi kilivyokuwa kimepoteza silika yake asilia.

Hivi sasa tunakiona chama ambacho hakina mwelekeo wo wote wa kifalsafa, si falsafa ya uhafidhina wala uanamapinduzi. Kwa maneno yake mwenyewe Mwalimu, kimekuwa ni kama dodoki au kokolo, kinameza kila kinachokutana nacho ziwani. Kwa maneno mengine, si chama tena bali ni utaratibu au mpangilio unaoruhusu kundi fulani la wajasiriamali wa aina mahsusi kujikusanya kila baada ya muda fulani kugawana madaraka na kufanya wapendavyo.

Kabla hajatutoka, Mwalimu alisema kwamba ili kuimarisha misingi ya demokrasia nchini, chama alichokianzisha mwenyewe, CCM, kilikuwa hakina budi kugawanyika ili kujenga upinzani wa kweli. Najua wakuu wengi ndani ya chama hicho walimwona kama msaliti, lakini ninaelewa kwamba aling’amua kwamba chama hicho kilikwisha kupoteza nguvu ya kifalsafa ya kukifanya kiendelee kuwa kitu kimoja.

Inawezekana vile vile kwamba Mwalimu alijaribu kusababisha mgawanyiko huo lakini akashindwa, jambo ambalo nitalijadili mbele ya safari.

Je, huo mgawanyiko alioutaka Mwalimu utatokea?
 
..Makala ya JENERALI ULIMWENGU ktk raia mwema. inatoa mwangaza kidogo kuhusu uongozi wa nchi na chama wakati wa Mwalimu Nyerere.

Jamani naomba mtu aniambie something new kuhusu Nyerere ambacho sijui. Kila siku ni yale yale kiasi cha kufanya hata mimi mpinzani wa ccm (ambayo Nyerere aliianzisha) nimeamua kuwa mtetezi wake.

Leta habari mpya maana the guy is dead almost ten years now!
 
Education Under Christian Leadership To many uninformed people, Nyerere is a public defender of secularism in the ruling Party and the government. But his secret meetings with Church leadership is quite the opposite. In his confidential conversation on August 2, 1970, with Rev. Robert Rweyemaum, the then Secretary General of Tanzania Episcopal Conference (TEC), the largest Christian denomination of Catholic Church, Nyerere is quoted in a book Development and Religion in Tanzania by J. P. van Bergen as saying that he has established in TANU a department of political education and that he deliberately appointed a Christian minister to head it not because he was a strong politician but because of his Catholic Faith. This book published by the Catholic Church stated that this reason the Rev. Mushendwa with his strong solid Christian faith, was put in charge of TANU's Development of Political Education. Nyerere continued what was left by the British educational discparity against the Muslims. He was aware of Muslim's grievance in the area of education. He wrote in his book Freedom and Unity that the disparity of educational levels could be used as a political issue

akbfwo.jpg


NYERERE angekuwa defender wa secularism asingekubali MUNGU atajwe kwenye nyimbo ya Taifa kwani hiyo ingewanyima haki waso na dini au wasio mwamini mungu
 
katika pitapita zangu, one time nilijikuta nakaa butiama mwezi mzima! kati ya watu niliokuwa nawaona karibu kila siku ni pamoja na fundi viatu maarufu ambaye alikuwa akishonea na kubadika gundi viatu vya mwalimu. that alone speaks volumea about mwalimu the person.

mwalimu 'the intellectual' was a different animal altogether! he had a certain intellectual arrogance that he deployed with devastating effect. mwalimu alikuwa anaweza kuwachambulia hoja nzito 'wana kisomo cha ngumbaru' mpaka wakazielewa! lakini pia ndiye mwalimu huyo huyo ambaye mara kwa mara hakusita kukunja uso na kuponda mawazo mbadala kwa kutumia maneno kama 'huu ni upumbavu, ujinga mtupu, upuuzi.'si hotuba tu bali hata makaripio kwa walio kuwa chini yake. ukikuta kapandisha mzimu wa kizanaki, basi omba dunia ipasuke ikumeze. mbe! Tabia hii iliwadhalilisha wasomi na kuwavunja moyo washauri wake ikiwa ni pamoja na kuwatia woga.

mpaka kuna wakati mwalimu akaitwa 'haambiliki'. siyo kwamba watu walikuwa wanamkejeli bali walikuwa wanaonyesha hali halisi jinsi ilivyokuwa vigumu kwa mwalimu kukubali mawazo mbadala.

tukio moja kubwa ambalo lilimlainisha mwalimu ni vita ya kagera (1978-9) ambayo ilihitimisha decade ya matatizo ukianzia na baa la njaa, kupanda kwa bei ya mafuta, na kushuka kwa bei ya mazao ya tanzania katika soko la dunia. hii yote ilipelekea uchumi wa nchi kudidimia kwa kasi ya ajabu, ghafla bin vuu tanzania ikajikuta katika kundi la nchi masikini wa kutupwa!

busara ya mwalimu ilionekana pale alipo amua 'kung'atuka' kwa hiyari yake mmwenyewe. ( that is one way of seeing it, but i would say he was forced by circumstances). mwalimu akasalimu amri kwa vijana wadogo wa IMF, nchi ikapata ahueni na ndio ikawa mwanzo wa mwananchi wa kawaida kusahaulika na serikali. Msuya summed it all 'kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe'.

wasomi wa tanzania mara nyingi wameshindwa kutoa 'objective analysis' ya mwalimu because of a 'psychological stranglehold' that he still maintains from his grave. Huyu ndiye 'baba wa taifa' na kwa mila zetu huwezi kumchambua! mwalimu alikuwa akienda mlimani kutoa speeech palikuwa panafurika..kaenda kuwafunza wasomi na maprofesa wao! akipandwa na ghadhabu wanafunzi anafukuza na chuo anafunga! wanatakiwa warudi chuo na barua ya mjumbe wa nyumba kumi! kwa udhalilishaji huo unategemea chuo kizalishe nini isipokuwa ndiyo mzee.

mwalimu had a larger than life iconic status which still strikes awe in some people. Lakini sasa kuna matumaini, kadiri kizazi kipya cha wasomi kinavyo ibuka na watu wa kawaida wanaanza kujua mambo ( zanzibar ilikuwa na tv tokea 1963 bara hadi 1992?), kizazi cha wasomi ambao hawajafanywa mazezeta na elimu ya siasa mashuleni......

will continue
 
Ukimsikiliza mtu mjinga na wewe unaweza kuwa mojawapo.
 
PrinceJafari,
Unachosema kitu gani haswa maanake hata sikuelewi. Nyerere alilazimika kujiuzuru una maana gani ikiwa kuna watu kama Mugabe wameshindwa kujiuzuru na ktk hali mbaya zaidi!..what forced him na hizo circumstances ni zipi.

Haya mara Zanzibar walikuwa na TV station toka 1963 hii ndio kitu gani haswa, yaani maendeleo ama?. Zanzibar walikuwa na taa za umeme kabla ya nchi nyingi za Ulaya na inasekana kabla hata ya vitongojio vingi vya Uingereza. So what?.. Zanzibar wako mbele ya UK?
Mkuu kuanza kuvaa nguo haina maana wewe ndio umestaarabika zaidi bali ni ishara ya umri mkubwa. Yaani wewe umetangulia kuzaliwa hivyo ni lazima uvae nguo kabla, na ndivyo Zanzibar iliweza pata mambo mengi kabla ya Bara. Hata Timbiktu huko Chad waliwahi kwa mengi sana kabla ya Marekani. Tatizo ni pale inapofikia umri bado unatembea uchi..
Tanzania ya leo, tunatembea uchi ati fashion, wengine wavaa suti jua la nyuzi 40, yet bado tunamlalamikia Nyerere kwa miaka yote iliyopita hatukuweza kuvaa suti. Je, umewahi jiuliza kipi kipya tumeweza vumbua?..HAKUNA.
Kifupi ni kusema kwamba Nyerere alichofanya ni kutukawiza sisi Kuiga tamaduni za nje... Na uhuru wote huu tuliokuwa nao leo bado tumeshindwa kutengeneza hata sindano ama kusindika matunda isipokuwa kwa mwekeshaji toka nje. Sisi wenyewe imebaki kutafuta deal la kuiba Benki Kuu, Ufisadi ambao unajenga utajiri bila hata kutoka jasho ama fedha zako.
 
PrinceJafari,
Unachosema kitu gani haswa maanake hata sikuelewi. Nyerere alilazimika kujiuzuru una maana gani ikiwa kuna watu kama Mugabe wameshindwa kujiuzuru na ktk hali mbaya zaidi!..what forced him na hizo circumstances ni zipi.

Haya mara Zanzibar walikuwa na TV station toka 1963 hii ndio kitu gani haswa, yaani maendeleo ama?. Zanzibar walikuwa na taa za umeme kabla ya nchi nyingi za Ulaya na inasekana kabla hata ya vitongojio vingi vya Uingereza. So what?.. Zanzibar wako mbele ya UK?
Mkuu kuanza kuvaa nguo haina maana wewe ndio umestaarabika zaidi bali ni ishara ya umri mkubwa. Yaani wewe umetangulia kuzaliwa hivyo ni lazima uvae nguo kabla, na ndivyo Zanzibar iliweza pata mambo mengi kabla ya Bara. Hata Timbiktu huko Chad waliwahi kwa mengi sana kabla ya Marekani. Tatizo ni pale inapofikia umri bado unatembea uchi..
Tanzania ya leo, tunatembea uchi ati fashion, wengine wavaa suti jua la nyuzi 40, yet bado tunamlalamikia Nyerere kwa miaka yote iliyopita hatukuweza kuvaa suti. Je, umewahi jiuliza kipi kipya tumeweza vumbua?..HAKUNA.
Kifupi ni kusema kwamba Nyerere alichofanya ni kutukawiza sisi Kuiga tamaduni za nje... Na uhuru wote huu tuliokuwa nao leo bado tumeshindwa kutengeneza hata sindano ama kusindika matunda isipokuwa kwa mwekeshaji toka nje. Sisi wenyewe imebaki kutafuta deal la kuiba Benki Kuu, Ufisadi ambao unajenga utajiri bila hata kutoka jasho ama fedha zako.

Komredi Mkandara:

Nyerere alikuwa Masochist. Maendeleo aliyaona yanakuja kwa kupata maumivi.
 
Mwanafunzi akimaliza muda wa shule anakwenda kufanya kazi za kujitegemea. Shida haimfundishi mtu ujanja. Ndio maana nchi imejaa wezi kila kona. Tarishi naye fisadi, anachukua nyaraka za serikali anawauzia wauza vitumbua. D@mn it nchi ile.
 
Back
Top Bottom