Mtamlaumu Mwalimu (RIP) kwa mambo ambayo yalikuwa nje ya uwezo wake. Watu wengi hawajui yaliyokuwa yanaendelea nyuma ya pazia.
Kwa kifupi tu ni kwamba Mkoloni hakuondoka Tanganyika na Afrika nzima kwa ujumla moja kwa moja. Wazungu waligundua kwamba kuitawala Afrika moja kwa moja ni gharama zaidi. Kwa hiyo wakatupa uhuru wa kisiasa lakini wakaendelea kuitawala Afika kupitia mlango wa uani.
Hii habari ya kusema "waligundua kutawala Afrika moja kwa moja ni gharama zaidi" badala ya kukubali ukweli kuwa wananchi walidai uhuru wao ni sawa na kuwatusi waliojitoa kudai uhuru, Nyerere akiwa mmoja wao. Mkoloni alijua fika kuwatawala Watanganyika wanaodai uhuru(kumbuka walishaonja joto ya Mau Mau Kenya na kupingwa vikali kwenye makoloni yao mengine wakati huo) itakuwa mbinde hivyo hawakuwa na jinsi ila kufunga virago.
Angalia nchi zote ambazo wazungu walishajiimarisha kiuchumi, hawakuondoka kirahisi, au hawakuondoka kabisa, kama vile Zimbabwe, South Africa, Mozambique na Namibia. Ila kwa nchi hizi zetu ambazo walijua kabisa wanaweza kuondoka na kuendelea kututawala kwa kutunga sera za fedha na uchumi kupitia Word Bank na IMF, waliondoka.
Kumbuka Nyerere aliwakoromea na kuwagomea hao IMF, WB (wakati Mtei waziri wa fedha in the 70's) hivyo hii nayo siyo hoja, kudai vinginevyo ni kupotosha ukweli.
Inasemekana kwamba karibu kila kitu alichokuwa anafanya Mwalimu alikuwa analetewa na Waingereza. Hii ni kuanzia siasa ya ujamaa na kujitegemea na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Kwa maneno mengine hapa unamaanisha kuwa Nyerere alikuwa kibaraka wa Waingereza, pamoja na kuwa siafikiani na baadhi ya sera zake lakini hapa mkuu
you are totally out to lunch, hakuna chembe ya ukweli hapo, hiyo ni
pure fiction maana hata sentensi yako imeanza na neno "
inasemekana".
Kumbukeni kipindi kile kulikuwa na vita baridi kati ya Magharibi na Mashariki. Waingereza walikuwa wanafuata mfumo wa kibepari. Hivyo walichofanya ni kuchagua baadhi ya yaliyokuwa makoloni yao yaliyoko Afrika kwa ajili ya kufanyia majaribio ya mfumo wa Ujamaa. Viwanda vingi vilivyojengwa wakati wa Nyerere misaada yake ilitoka Uingereza. Kwa kifupi miaka yote hiyo nchi yetu ilikuwa kama "case study" ya mfumo wa ujamaa kwa Waingereza. Who knew? Pengine Ujamaa ungeweza kufanikiwa na ubepari kufa.
Duh! Sasa naona umefikia mahali unatunga hadithi kuchangamsha baraza, yaani Uingereza wanaofuata mfumo wa kibepari leo waamue kufadhili majaribio ya mfumo wa ujamaa? Au mkono uliteleza tu pengine ulitaka kuandika Urusi? Halafu kwa kukusaidia tu, viwanda kama UFI, Urafiki n.k. vilijengwa kwa misaada toka China.
Nchi za Kiafrika ambazo viongozi wake walionekana wana kihere here cha kutaka kuleta maendeleo waliuawa katika mazingira ya kutatanisha. CIA walimuua Lumumba kule Congo na kuweka kibaraka wao Mobutu. Sasa hivi Wamarekani wamejaa huko wanafanya "mineral prospecting". Kwa kifupi Congo ilikuwa imehifadhiwa kwa ajili ya kuwa chanzo cha malighafi na madini kwa ajili ya Wamarekani. Na ndivyo ilivyokuwa kwa nchi nyingi za Kiafrika ikiwemo Tanzania.
Hapa unachanganya ndimu na maembe, viongozi kazi yao ni kuongoza wananchi wawe na maisha bora zaidi na ndio maendeleo hayo, hivyo kila kiongozi ana wajibu huo, hakuna cha kiherehere wala nini, ndio maana wanapoomba kura wanaahidi mambo ya kimaendeleo watakayoyatekeleza. Kauli yako imegubikwa na taswira ya dharau kwa viongozi wanaojitahidi kuwaletea wananchi wao maendeleo. Kuuwawa kwa Lumumba ilikuwa ni kuhusiana na vita baridi vya wakati ule ambapo nchi za magharibi (US na Ulaya Magharibi) na nchi za kikomunisti/kijamaa (Urusi, Uchina, Cuba, Ulaya Mashariki) zilikuwa zinajitahidi kushindana kuvutia nchi zinazoendelea kufuata mifumo yao. Sasa ungekuwa unataka kumtetea vizuri Nyerere basi ungekumbuka kuwa alikuwa kati ya waasisi wa
Non Aligned Movement (NAM), yaani Nchi Zisizofungamana na Upande Wowote. Ndio maana Tanzania tuliweza kuwa na uhusiano mzuri na Urusi, Marekani, Uchina, Uingereza, Cuba n.k bila kulazimika kuegemea upande mmoja tofauti na wenzetu Wakenya, kwa mfano. Kwa hili pia Nyerere alionyesha msimamo tofauti na madai yako.
Nyerere msimlaumu sana! He was being controlled by the British. Maamuzi mengi yalikuwa nje ya uwezo wake, na pia kuna mambo mengi mazuri yaliyokuwa ndani ya uwezo wake ambayo aliyafanya.
Unarudia tena kumdhalilisha Nyerere. Kwa taarifa yako Nyerere hajawahi kuwa kibaraka wa Uingereza hata siku moja, tafuta jingine.