Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Huo ni muono wako nami sina uwezo wa kuuingilia wala kukubadilisha mawazo. Isipokuwa, facts zijibu kama unaweza:

Jee, nyerere hakuhamisha watu takriban millioni kumi kutoka makazi yao ya asili?

Kasome historia vizuri na facts kuhusu Operesheni vijijini. Hivi unajua ni Watanzania wangapi leo wanaishi kwenye vijiji ambavyo ni matokeo ya kazi ile. Mwalimu alikuwa na jukumu la kujenga Taifa siyo kujenga vijiji! Anayejua mapungufu tunajua ni jinsi gani operesheni ile ilishindwa kutekelezeka jinsi ilivyopasa, lakini leo nenda uangalie ni jinsi gani nadharia yake ya "vijiji" ndio imeunda msingi wa Taifa leo hata leo hii. Ushawashi kusikia mahali kunaitwa "Geza Ulole"?

Jee, nyerere hakusababisha kati ya aliowahamisha wafe kwa, kuliwa na wanyama? kugongwa na majoka? kukosa chakula? kula mizizi yenye sumu kwa njaa? kukosa matibabu?

Yaani wewe unataka kutuambia wananchi wangeendelea kukaa nyumba moja hapa nyingine kule katika makazi ya kijima halafu wapate maendeleo? I'm glad tuliweza kuunganishwa katika vijiji. Mapungufu yake ni gharama ya maendeleo. Watu kufa n.k yote ni gharama. Tungeweza kupunguza au kuzuia vivyo na matatizo mengine ingekuwa bora zaidi, lakini ndivyo ilivyokuwa.

Jee, nyerere hakuanzisha sheria ya "ditenshen" amabyo hakuna aliyeweza kukutowa isipokuwa yeye?

wewe umewahi kuisoma hiyo sheria au unasikia "detention" tu.? Haya nimekubandikia hapa ili utuoneshe hapo mahali panaposema kuwa mtu hakuweza kuachiwa isipokuwa kwa Nyerere amuachie.

Jee, watu aliowa-"ditenshen" nyerere wengine hawakufia jela?

Hoja nyingine bwana, sasa unajua wafungwa wangapi hufia jela? Unajua wangapi huwa wanafia rumande?

Jee, nyerere, hakuzuwia habari kuandikwa isipokuwa inazotaka serikali yake tuu?

Una uhakika? alizuia lini, kwa tangazo gani, na vipi....? Nyerere alikuwa anajukumu la kujenga Taifa, baadhi ya maamuzi lazima tuyaelewe kwa mwanga wake halisi siyo kutumia darubini ya muda kuanza kuyahukumu.

Nadhani hizo ndio hoja na hoja si mimi wala si wewe wala si mtanzania yeyote kuwa ni mwendawazimu. Wendawazimu ni maradhi kama maradhi mengine yeyote na si tabia njema kujumuisha watu na kuwatusi kama unavyotaka ieleweke. Naomba jibu facts.

Nakubaliana na wewe hapo kwani hoja hujibiwa kwa hoja, siyo vioja wala vi-hoja!

kama kuna kikundi hicho mimi nakuhakikishia sikijuwi, msimamo wangu ni facts zisizopingika na nilikuwepo wakati wa nyerere na nimeyaona na si ya kusikia. jee hujuwi kuwa wakati wa nyerere tulikuwa kwenye dimbwi la umasikini?

hoja zinapingika! KUhusu dimbwi la umasikini ambalo tulikuwemo wakati wa Nyerere naomba ututangazie tulitoka lini?

Usemayo swadakta na yanaingia akilini, lakini huwezi kuwa ni chanzo cha kuuwa halaiki ya watu na si kwa ajali bali kwa maamuzi ya makusudi kabisa na ya muda mrefu, halafu ujitetee kwa kukubali nimefanya makosa lakini "nilikuwa na nia njema" Ambayo ndiyo argumente kubwa ya kutetea dhambi za nyerere. Haaa.

Hii "halaiki" ya watu waliouawa iko wapi!? Jamani naomba mtu yeyote ambaye wazazi wake, kaka zake, au ndugu zake waliuawa wakati wa Operesheni vijijini wajitokeze na tuanze kuhesabu. Kusikia "fulani aliuawa" hatukubali, tuko wengi hapa JF nina uhakika angalau mtu mmoja atakuwa amepoteza shemeji, dada, au kaka wakati wa ile Operesheni ya vijiji. Binafsi wazazi wangu walihama kule toka mabonge ya Peramiho na kusogezwa karibu na Misheni, na ingawa walitusimulia jinsi walivyoondoka kwenye makazi yao, lakini hakuna hata mtu mmoja aliyekufa au kuliwa na simba! Sasa nyinyi mliopoteza ndugu zenu mauaji ya "halaiki ya watu" naomba mnyoshe mikono.

Ukienda leo Baghdad na ukiuliza kama kuna mtu anamjua mtu yeyote aliyeuawa na vitendo vya ulipuaji kule usishangae karibu kila mmoja anajua mtu, na hata hapo nyumbani ukiuliza kama kuna mtu anamjua aliyekufa kwa Ukimwi usishangae karibu kila nyumba inamjua mtu, sasa wale walioishi miaka ya sabini (nikiwemo wenu mtiifu) nimejaribu kukumbuka ni kina nani waliuawa na Mwalimu katika operesheni vijijini.

Zomba kwa vile unasema ulikuwepo naomba tuanze na wewe, ni ndugu zako wangapi na wapi walikuwa wakihamishiwa? ili tuanze kuhesabu tuache kuandikia mate...

Kuhusu la Lowassa, argument yangu ni kuwa, si huyo tuu ni mfumo mzima wa kukubali kuwa nyerere hajafanya makosa ndio wenye tatizo na iwe kikwete, lowassa, pinda au pinduwa, kama hawa viongozi hawatakubali kosa na kulirekebisha basi tutabaki na kosa mpaka watapopatikana viongozi wataokiri kosa limeanza wapi na ndio walirekebishe. simply, kama mtu hujuwi kosa nini, utatatuwa nini? If you dont know what the problem is, how do you solve it?

point nzuri, tatizo huwezi kuumba kosa lisilokuwepo ili ulijaribu kulisolve!

Problem ni kutokukubali nyerere ndie aliyetutia kwenye ufisadi wa hali ya juu, kwa kuwa mwenyewe alikuwa fisadi.

wenzio walienda mbali zaidi walimuita nyerere Dikteta, kama Nyerere alikuwa fisadi, basi miye naupenda ufisadi wake! Kwa sababu,

> Nyerere hakuanzisha mgahawa Ikulu
> Nyerere hakuuza nchi yetu kwa wawekezaji
> Nyerere hakusujudu kwenye madhabahu ya Mataifa makubwa na kudhalilisha utu wake. n.k n.k

naomba ieleweke, ufisadi si kuiba kwenye mikataba tu, hata kutowa roho za watu wasio na makosa ni ufisadi, kudhulumu mali za watu pia ni ufisadi. jee, nyerere hakuuwa watu wasio na makosa? jee nyerere hakudhulumu mali za watu? Tukubali kulijuwa tutatizo ndio tuweze kulitatuwa bila hivyo, bure tu.

Hiyo mali aliyoidhulumu Nyerere aliipeleka wapi? Hao watu ambao Nyerere aliwaua makaburi yao yako wapi? Lazima kuna mtu anajua. Nyerere alishaondoka siku nyingi na kufa, sasa hakuna haja ya kuogopa tena, watajeni wale waliouawa na Nyerere ambao ni halaiki!! Halafu tulinganishe kama idadi yao inafikia wale waliouawa wakati wa Mkapa, au Mwinyi!
 
Nilishituka katika usingizi na kujisikia mzito kupita kiasi na ghafla nikajikuta niko katika katika nyumba moja ya kawaida kabisa mahali ambako nikaaminishwa kwamba ndipo makazi halisi ya Baba wa Taifa.

Kwa kuwa kazi yangu ni kutafuta habari, nilihitaji sana maoni ya Baba wa Taifa, mtu ambaye anaujua kwa dhati uchungu wa Tanzania, watu wake na rasilimali zake na mara moja nikamkabili mzee huyo ambaye alikuwa anaonekana kuwa mwenye mawazo mengi na hudhuni iliyomfanya kuwa na uso uliochoka.

Nilisita kumuuliza kuhusu kilichokua kikinikera kwani alianza kulia aliponiona hali iliyonifanya nami nishindwe kujizuia kububujikwa na machozi.

Nilianza kulia naye alinikumbatia na kuniambia, “nalilia Tanzania yangu, najutia yaliyotokea. Sikujua kwamba niliyemuamini amefanya yale niliyoyapinga kwa nguvu zangu zote.”

Nilipata ujasiri na kutoa kijitabu changu cha kuchukua dondoo za habari ili nianze kunukuu maneno yake. Kwa bahati mbaya nilikuta kijitabu hicho kimejaa, hakina nafasi kubwa ya kuandika.

Nikaokota vipande vya karatasi jirani na tulipokuwa tumekaa na kuanza kuandika maneno hayo. Katika mazungumzo yetu nilijiona mpumbavu kwa kutokuwa na kaseti ndogo ya kurekodi, baada ya kuona mazungumzo yananoga.

Nilitaka kujua undani wa maneno yake, na kwa kweli hakuwa na mengi ya kuzungumza na mahojiano yalikuwa mafupi mno, kasi cha kunifanya nipate maneno machache kutoka kwake.

Baada ya kusema analilia Tanzania yake, Mwalimu alisema, “zimwi la ajabu lenye mapembe ya rushwa, kulindana na matumizi mabaya ya madaraka, limeimeza Tanzania yangu. Msikate tama, pambaneni. Mwambie Jakaya (Rais Jakaya Kikwete) aangalie.”

Baada ya maneno hayo nilipoteza ujasiri maana nilipoteza mwelekeo na sikuweza kuendelea na mahojiano yake kwa kina. Katika hali ya kawaida, mimi sio mtu wa kushindwa kufanya mahojiano na mtu yeyote, hasa nikipata nafasi lakini kwa Mwalimu nilikwama.

Kabla sijaondoka aliniomba nimsindikize akapumzike kwa kuwa alikuwa amechoka. Nilimshika mkono na kumepeleka hadi chumbani kwake, ambako kulikuwa na vitanda vitatu na kabla hajalala akasema, “Nilimzuia Jakaya mwaka 1995 nikijua mwenzetu amekomaa na ni msafi kumbe amekuja kuniaibisha kabisa.”

Hayo ni maneno machache na pengine kutokana na kuguswa nayo, ndiyo niliyoweza kuyanukuu nilipozinduka huku uso wangu ukiwa umetapakaa machozi.

Nimejiuliza na kuwauliza watu wa karibu nami kuhusiana na ndoto hiyo, lakini nimepata majibu mchanganyiko ndio sababu hasa nimeamua kuwapa nafasi Watanzania wa Mwalimu Nyerere nao wapate maneno hayo. Sio lazima wayaamini, lakini wapate ujumbe.

Mara baada ya Mwalimu kufariki, nilipata kuota ndoto ambayo alinieleza huku akitembea kwamba niwaambie ‘jamaa zangu’ kwamba hajapendezwa kabisa na kuuzwa ama kubinafsishwa kwa iliyokuwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), jambo ambalo nakumbuka aliwahi kuliweka wazi wakati wa uhai wake tulipokuwa mjini Arusha.

Siku hiyo ilikuwa ni ziara ndefu ya kuanzia Dar es Salaam, Iringa mjini na hatimaye vijijini na baadaye Arusha, safari ambayo nilibaini ukakamavu wa Mwalimu katika umri wa utu uzima na hiyo ilikuwa miezi michache kabla ya kwenda nchini Uingereza kwa matibabu, safari iliyokuwa ya moja kwa moja. Hakurejea tena akiwa hai. Alipoteza maisha yake akiwa huko baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa saratani ya damu.

Lakini, hadi sasa sifahamu kinachonisukuma kuwa na hisia kali na Mwalimu Nyerere, kwani kabla hata ya kutangazwa kuugua kwake, nilipata kuwaeleza wakubwa wangu wa kazi wakati ule, Salva Rweyemamu, aliyekuwa Mhariri Mtendaji wangu ambaye tulikubaliana kuwa na subira kabla ya kuandika habari hiyo.

Ilikuwa ni gazeti moja litolewalo kwa wiki kwa lugha ya Kiingereza ndilo lililotusukuma kuanza kuandika habari za ugonjwa wa Mwalimu, kwani liliandika habari ikielezea kwamba Mwalimu amezidiwa na amesafirishwa kwenda nje ya nchi, jambo ambalo halikuwa sahihi wakati huo. Tukaandika ukweli kwamba anaumwa, lakini yupo nchini.

Tuliendelea kufuatilia habari zake hadi siku ambayo alikuwa akiondoka nchini kwa Ndege ya Shirika la Ndege la Uswisi (Swiss Air), siku ambayo ni waandishi watatu tu ndio walikuwapo uwanja wa ndege, Absalom Kibanda, ambaye sasa ni Mhariri wa Tanzania Daima na mpiga picha Emmanuel Herman, ambaye amerejea tena Habari Corporation.

Siku hiyo nakumbuka, uwanjani hapo kulikuwa na kundi la waandishi wa habari waliofika kupokea wanamichezo waliofika Dar es Salaam kwa ndege ya Swiss Air iliyomchukua Mwalimu, lakini baada ya kuwapokea wanamichezo waliondoka bila kujua Baba wa Taifa anaondoka kwa mara ya mwisho kwenda Uingereza.

Nakumbuka baada ya makosa kadhaa ya kitaaluma kutokea, nilimwambia Kibanda kwamba Mwalimu hatorudi. Sikuwa na sababu zozote za kusema maneno hayo na hakuna aliyezingatia maneno hayo na ndio maana hata mpiga picha wetu Herman hakupiga picha za kutosha katika tukio hilo. Niliumia sana.

Nakumbuka hata waliomsindikiza hawakuwa watu wazito kwani alikuwapo aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, John Chiligati na upande wa Polisi, alikuwapo aliyekuwa Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Dar es Salaam, Salum Mkwama, na pia ofisa mmoja wa Wizara ya Mambo ya Nje, ambaye alikuwa pale kusimamia itifaki.

Hata aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Andrew Chenge, alikutana na Mwalimu pale VIP akiwa katika safari zake na hakuwa katika orodha ya waliofika kumsindikiza Mwalimu na mkewe Maria, huku familia ikiwakilishwa na mabinti wawili ambao walionekana wakiipungia mkono ndege ikiwa angani.

Hisia hizo zinanipeleka siku ya kifo chake, nilipojikuta nikianguka mara baada ya kuona sura ya Baba wa Taifa pale nyumbani kwake Msasani na haikuishia hapo kwani nilitoka nyumbani kwenda kusindikiza mwili Uwanja wa Ndege kwenda Butiama, lakini nilijikita nikidandia ndege ya jeshi la Afrika Kusini kwenda Musoma na hatimaye Butiama.

Haikuwa jambo la kawaida, kwani sikuwa na chochote zaidi ya nguo nilizokuwa nimevaa hata niliponyeshewa na mvua tukiwa katika msafara wa mwili wa marehemu sikuwa na nguo za kubadili na huko nilimkuta muongoza kwaya, Ansbert Ngurumo, ambaye naye “alizamia” kufika Butiama; hakuwa ameaga ofisini. Tulivutwa na mzimu wa Nyerere.

Hata Benjamin Mkapa, akiwa Rais aliyekuwa madarakani, alisema mbele ya kaburi la Mwalimu kwamba watakaofanya mambo kinyume na wosia wa Baba wa Taifa, “jinamizi lake litawashukia,” na kwa hakika inaelekea sasa “jinamizi” linaelekea kumshukia yeye.

Hakuna ubishi kwamba mambo mengi ambayo Mwalimu aliyapinga kwa nguvu zake zote hadi anakata roho, Mkapa ameyakiuka ikiwa ni pamoja na sio tu kushindwa kabisa kupambana na rushwa, bali pia yeye binafsi kujihusisha na rushwa na ufisadi.

Mwalimu alipinga kabisa Ikulu kutumika kujinufaisha, lakini mara tu alipoaga dunia, Mkapa alianzisha kampuni akitumia rasilimali za umma, ikiwa ni pamoja na majengo, magari, wataalamu na hata kuamua kabisa bila aibu kushirikiana na waziri wake, Daniel Yona kufanya biashara wote wakiwa madarakani.

Pamoja na kufahamu wazi kwamba Baba wa Taifa alipinga kabisa kuuzwa kwa NBC, Mkapa alijenga uhusiano wenye utata mkubwa na wamiliki wa benki hiyo, uhusiano ambao ulimuwezesha kuendelea kujineemesha yeye na familia yake na kujitanua kwa kujipatia nyumba nyingine jirani na ile aliyokuwa akiishi pale Sea View, Dar es Salaam.

Ni Mkapa huyo huyo ambaye sasa tunaambiwa kwamba kwa baraka zake, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imefanya ‘madudu’ ya ajabu ambayo kwa hakika ndiyo yaliyofanya Baba wa Taifa, aniijie katika ndoto baada ya kubaini kwamba nimekuwa nikiumia sana kwa jinsi Tanzania yetu ilivyotumbukizwa katika “janga la kujitakia”.

Hakuna asiyefahamu kwamba Mkapa alitetewa kwa nguvu zote na Baba wa Taifa, wakati huo akionekana kama mtu pekee msafi katika kundi kubwa la wanasiasa walioomba kuwania urais mwaka 1995, mwalimu huko aliko sasa anajuta, lakini anamwambia Jakaya aangalie.

Mwalimu analia Jakaya angalia, Tanzania na Watanzania kwanza mambo mengine baadaye, tuko nyuma yako ukiamua.

Kuamua kwa Kikwete kutatokana na utashi wake binafsi na sio wa mashabiki wala watu waojikomba kwake.

Ni kuamua ndiko kutampa sifa na baraka tele kutoka kwa Mungu Mkuu baada ya kutovaa sura ya aibu kwa watu ambao wanamkwamisha kutekeleza azma yake.

Azma kubwa ya Kikwete ni maisha bora kwa kila Mtanzania, lakini sasa anaonekana kushindwa na wengi tunaamini kuwa anaweza, isipokuwa anaangushwa na hao wapambe wanaomzunguka.

Wapambe wake ni wengi wakiwamo marafiki zake, wasaidizi wake wa karibu serikalini ambao kila jambo wao wanaona ni hewala, wakati ukweli ni kwamba Watanzania wanateketea na kutomuamini rais wao waliyemchangua kwa kura nyingi.

Ni vyema, sasa Kikwete akaamua kabla muda haujawa mwingi, akawatosa wote wanaomuangusha na kumfanya kukosa thawabu.

Nakumbuka Simba wa Vita, Waziri Mkuu mstaafu, Rashidi Mfaume Kawawa aliwahi kukieleza kikao kimoja cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi, kwamba ni vyema mtu anayetoboa jahazi akatoswa mapema, kwani kulelewa na kushangilia huku akiendelea na hujuma zake, mwisho wake ni abiria wote, pamoja na nahodha kuzama na kupoteza maisha.

Kikwete, wakati wa kuwatosa wote wanaokuangusha ni sasa na usijali urafiki, uswahiba au undugu na watu wa aina hiyo na hapo utakuwa umeokoka na kulitendea haki taifa la Watanzania.

* Ndoto hii iliotwa na mwananchi mmoja. Mtanzania kweli.Mwenye uchungu na mzalendo wa kweli akimuasa Kikwete kuiokoa nchi inayozama mikononi mwake
 
Kama JK anaboronga kwanini watanzania msimshikee bango mpaka muote ndoto za Nyerere?
 
MESSAGE DELETED... AWAITING RESPONSE FROM THE POSTER.

Invisible
 
The title should better read "The Dark Side of Ludovick Mwijage"-which is so far the only side we know about him from this article. I have read the book too, and sincerely speaking, it has nothing whatsoever which can objectively implicate Nyerere as a man who presided over a reign of terror, as the author wants the world to believe. A man who hated Nyerere (I don't think Mwijage just opposed Nyerere, he HATED him, and this is very far from what politics should be about) is recollecting his own experiences which emanated from his hate-driven missions against Nyerere and the country which Nyerere served so faithfully, putting them in a collection of memoirs maliciously using Nyerere's name to sell his punky story! My friend, I will never buy the story! After reading Mwijage's book, I have only been able to categorically describe him as a habitual trouble-maker who was practically his own enemy!
 
Nyerere's time was the darkest for those who have eyes.
 
Nyerere's time was the darkest for those who have eyes.

They don't have eyes that's why they perceive darkness only! What do you expect a blind person to see? There are millions in Tanzania, Africa and beyond who continue to see light in Nyerere's legacy to this date, and millions more are thankful for the Nyerere's cotribution in improving the lives of the poor. Nyerere's positive role in transforming for the better lives of millions is acknowledged the world over, and the inspiration from the philosophy which he lived is so deeply and passionately upheld by people of good faith, that the likes of Mwijage can do absolutely nothing to erode Nyerere's reputation. Corrupt and selfish people who cherished retaining their priviledged positions at the expense of the poor majority hated Nyerere, and these are the likes of Mr Mwijage who shamelessly seem to possess the satanic courage to usher insults on such a dear leader and great statesman, Julius Nyerere. It is not surprising that some people want to pupularize Mwijage's book and ideas now, probably in support of the "fisadi's" in (and out of) power, preaching selfishness in opposition to patriotism.

Nyerere was a patriotic leader who did the best for his country in keeping with the prevailing circumstances at the time. Millions of people have eyes to see this, and they appreciate dearly. Selfish, greedy, and corrupt people like Mwijage (whom I equate to the chiefs who were willing to sell their kinsfolk to slavery for a piece of loin cloth) wanted to continue to amass wealth and priviledges, at any cost, even if it would include "selling" or killing their own people. Nyerere was smart, he wouldn't let them stand on his way, which makes him a hero for me.
 
were you there? at his time. Or a hero as in hero?
 
were you there? at his time. Or a hero as in hero?

what about you?If you were there what positive steps did you undertake to rectify the situation,I mean in terms of politics and general administration?If you weren't,then why do you dare criticize nyerere who at least made you see the inside of a classroom and gave you university education for free only to turn against him you together with your fellow mafisadi in the name of the doomed and cursed genge la mtandao?
 
The title should better read "The Dark Side of Ludovick Mwijage"-which is so far the only side we know about him from this article. I have read the book too, and sincerely speaking, it has nothing whatsoever which can objectively implicate Nyerere as a man who presided over a reign of terror, as the author wants the world to believe. A man who hated Nyerere (I don't think Mwijage just opposed Nyerere, he HATED him, and this is very far from what politics should be about) is recollecting his own experiences which emanated from his hate-driven missions against Nyerere and the country which Nyerere served so faithfully, putting them in a collection of memoirs maliciously using Nyerere's name to sell his punky story! My friend, I will never buy the story! After reading Mwijage's book, I have only been able to categorically describe him as a habitual trouble-maker who was practically his own enemy!

what about you?If you were there what positive steps did you undertake to rectify the situation,I mean in terms of politics and general administration?If you weren't,then why do you dare criticize nyerere who at least made you see the inside of a classroom and gave you university education for free only to turn against him you together with your fellow mafisadi in the name of the doomed and cursed genge la mtandao?

Hii ndio tunaita kumkoma nyani giladi, mbarikiwe wakuu Kithuku na Ibambasi.
 
Nyerere's time was the darkest for those who have eyes.

It depends which side your eyes were looking to. But in totality, the lighter side outweighs by far the Mwijage's rare darker side. Unlike Nyerere, the current leaders are not even ashamed of having themselves, their familly members and friends participate in the darkness acts.
 
Kuna watu wanamchokoza mwanakijiji hapa, ngoja nitafute mtemba wangu niangalie kwa mbali.....
 
Kuna watu wanamchokoza mwanakijiji hapa, ngoja nitafute mtemba wangu niangalie kwa mbali.....

Ahahahahahahahahahaaaaaa....ebwana utadhani ulikuwa kichwani mwangu....maana na mimi nilikuwa nafikiria hivyo hivyo

Let me find my recliner coz something is about to go down...
 
Kuna watu wanamchokoza mwanakijiji hapa, ngoja nitafute mtemba wangu niangalie kwa mbali.....

no.. my friend no. Ukiishi kwingi unaona mengi na mengi huwa yanajirudia. Na mimi kujirudia rudia sipendi; so kama wewe na Nyani na mimi Ijumaa nimekuja na kideo changu hapa shambani nasubiri "Reggis & Kelly". Kuna vitu vingi muhimu vya kufikiria...
 
no.. my friend no. Ukiishi kwingi unaona mengi na mengi huwa yanajirudia. Na mimi kujirudia rudia sipendi; so kama wewe na Nyani na mimi Ijumaa nimekuja na kideo changu hapa shambani nasubiri "Reggis & Kelly". Kuna vitu vingi muhimu vya kufikiria...

Nani leo yuko kwenye Regis & Kelly?
 
..You dirty old man.....lol

This is all I can say (from shaaban robert)

Nilikuwa ni waridi, furaha ya wasichana
Neno hawakunirudi, wakati wa kukutana
Sasa nanuka baridi, wanionapo waguna
Nasikitika hadumu, rafiki yangu ujana.

Walio wakinibusu, walikuwa wengi sana
Wanawake wenye busu, uzuri na usichana
Sasa sina hata nusu, ya wanitajao jina
Nasikitika hadumu, rafiki yangu ujana.

Wazuri wenye uturi, na mikono yenye hina
Kila mtu mashuhuri, alipenda kuniona
Nilifaa kwa shauri, na sasa sauti sina
Nasikitika hadumu, rafiki yangu ujana

Sasa, na uzee huo si naruhusiwa kula kuona?
 
Back
Top Bottom