Haujawahi kusikia? ajabu sana, ngoj nikusikilizishe kwa kifupi tuu. Nyerere aliwahamisha zaidi ya watu million kumi kutoka vijiji, miji au sehemu zao za asili na kuwapeleka sehemu mpya, ya amma kulikuwa kuna vijiji vidogo vya asili na watu wapya wakabwagwa na kuwachwa hapo bila ya kuwa na facilities zozote za kuweza kukidhi mahitaji yao kila siku au walichukuliwa na kubwagwa maporini ambapo hakuna hata kijiji wala nyumba za kuishi, wengi wao walikufa kwa kuliwa na wanyama wa kali wa porini, wengine waligongwa na nyoka, wengine walikufa kwa njaa, wengine walikufa kwa kula mizizi ya sumu kwa njaa, wengine walikufa kwa kukosa matibabu. Ni wengi sana waliokufa na ilikuwa ni marufuku kuandikwa habari mbaya yeyote, waandishi wachache waliokuwepo wakati huo, ilikuwa ni lazima waandike inavyotaka serikali.
wengine walikufia jela kwa sheria yake ya ditenshen aliyoiweka, sijui kama imefutwa hii au bado ipo, watu wengi walikuwa wakionekana kupinga tuu siasa zake, walishikwa na kuwekwa vizuizini bila kuhojiwa wala kupelekwa mahakamani aidha mpaka wafie huko au mpaka nyerere mwenyewe awakumbuke na kuwawachia, hakuna mtu mwingine yeyote kwenye serikali aliyekuwa na ubavu wa kukutowa ditenshen isipokuwa nyerere mwenyewe.
Mbali ya hayo, mahospitali yalikuwa bure lakini huduma mbovu kabisa na ndio mpaka sasa hali imebaki hivyo-hivyo. Yaani alifisadi kila kitu.
KUCHEKA na kuchekesha watu, hilo ndio moja linalonishangaza mpaka leo, kwa yote aliyokuwa akiyafanya lakini bado alikuwa na uwezo wa kucheka na kuchekesha watu na aliupata usingizi. Hiyo ni dalili ya ukatili wa hali ya juu. Kumbuka wakati huo alikuwa akiweka masharubu yake kama hitler.
Ni mengi mabaya aliyoyafanya na ndio maana unaona ufisadi uliokithiri leo hapa nchini unatokana na hawa viongozi aliowarithisha yeye. Hawana huruma hata kidogo na wananchi kama alivyo yeye. Na aliyejaribu kumpinga kidogo alikiona. Abood Jumbe ni mfano mzuri, aliwachishwa umakamu wa rais akawekwa house detention akakatiwa umeme, maji, marupupu yake ya umakamu wa rais mpaka alipotubu kwa nyerere kuwa hatosema lolote na hatoingilia tena mambo ya siasa ndio akafunguliwa. Na toka wakati huo akawa kimya mpaka wakati wa mwinyi ndio akathubutu kuandika kitabu kilichogusia kidogo siasa za kidikteta za nyerere.
Ni wengi tuu aliowauwa nyerere kwa maamuzi yake mabovu, na umasikini uliokithiri ametutakia yeye, inasemekana kuwa kuanzia mwaka 1965, mpaka anaacha urais uchumi wa tanzania ulikuwa ukishuka kwa 0.03% kila mwaka. Hatari kubwa.
Huyo nyerere ndie alikuwa fisadi mkuu wa Tanzania, au haukuwepo wakati wake na unamsoma tuu kwenye historia za uwongo? Tuulize sisi tuliokosa bahati kwa kuwepo na kuonja joto na madhila ya uongozi wake.
Haujawahi kusikia? ajabu sana, ngoj nikusikilizishe kwa kifupi tuu. Nyerere aliwahamisha zaidi ya watu million kumi kutoka vijiji, miji au sehemu zao za asili na kuwapeleka sehemu mpya, ya amma kulikuwa kuna vijiji vidogo vya asili na watu wapya wakabwagwa na kuwachwa hapo bila ya kuwa na facilities zozote za kuweza kukidhi mahitaji yao kila siku au walichukuliwa na kubwagwa maporini ambapo hakuna hata kijiji wala nyumba za kuishi, wengi wao walikufa kwa kuliwa na wanyama wa kali wa porini, wengine waligongwa na nyoka, wengine walikufa kwa njaa, wengine walikufa kwa kula mizizi ya sumu kwa njaa, wengine walikufa kwa kukosa matibabu. Ni wengi sana waliokufa na ilikuwa ni marufuku kuandikwa habari mbaya yeyote, waandishi wachache waliokuwepo wakati huo, ilikuwa ni lazima waandike inavyotaka serikali.
wengine walikufia jela kwa sheria yake ya ditenshen aliyoiweka, sijui kama imefutwa hii au bado ipo, watu wengi walikuwa wakionekana kupinga tuu siasa zake, walishikwa na kuwekwa vizuizini bila kuhojiwa wala kupelekwa mahakamani aidha mpaka wafie huko au mpaka nyerere mwenyewe awakumbuke na kuwawachia, hakuna mtu mwingine yeyote kwenye serikali aliyekuwa na ubavu wa kukutowa ditenshen isipokuwa nyerere mwenyewe.
Mbali ya hayo, mahospitali yalikuwa bure lakini huduma mbovu kabisa na ndio mpaka sasa hali imebaki hivyo-hivyo. Yaani alifisadi kila kitu.
KUCHEKA na kuchekesha watu, hilo ndio moja linalonishangaza mpaka leo, kwa yote aliyokuwa akiyafanya lakini bado alikuwa na uwezo wa kucheka na kuchekesha watu na aliupata usingizi. Hiyo ni dalili ya ukatili wa hali ya juu. Kumbuka wakati huo alikuwa akiweka masharubu yake kama hitler.
Ni mengi mabaya aliyoyafanya na ndio maana unaona ufisadi uliokithiri leo hapa nchini unatokana na hawa viongozi aliowarithisha yeye. Hawana huruma hata kidogo na wananchi kama alivyo yeye. Na aliyejaribu kumpinga kidogo alikiona. Abood Jumbe ni mfano mzuri, aliwachishwa umakamu wa rais akawekwa house detention akakatiwa umeme, maji, marupupu yake ya umakamu wa rais mpaka alipotubu kwa nyerere kuwa hatosema lolote na hatoingilia tena mambo ya siasa ndio akafunguliwa. Na toka wakati huo akawa kimya mpaka wakati wa mwinyi ndio akathubutu kuandika kitabu kilichogusia kidogo siasa za kidikteta za nyerere.
Ni wengi tuu aliowauwa nyerere kwa maamuzi yake mabovu, na umasikini uliokithiri ametutakia yeye, inasemekana kuwa kuanzia mwaka 1965, mpaka anaacha urais uchumi wa tanzania ulikuwa ukishuka kwa 0.03% kila mwaka. Hatari kubwa.
Naam, hapa kuna ukweli na ushahidi wa kutungwa(kama ukweli na ushahidi wa namna hiyo upo).
Na kwa watu waliokwishajiaminisha ukweli huo hapawezi kuwepo na ukweli mwingine.
Kwa wat wa namna hiyo,haijalishi, hata kama halaiki ya wananchi waliomuenzi Mwalimu wanapoendelea kumheshimu na kumtukuza; ni wao tu ndio wenye ukweli. Kwa maneno mengine, waTanzania walio wengi ni vichaa kwa kumwona Nyerere kuwa kiongozi aliyetukuka. Ni akina Zomba tu ndio wenye akili timamu. Sasa wanyo kazi ya kututibu ukichaa huu, nasi tufanane nao watu wenye akili timamu. But the reverse of this seems more plausible.
Hizo enzi zako unazosema, tungelikuwa na viongozi hawa tulionao kwa wakati huo, leo hii tusingeonana hapo JF. Nakuachia utafakari au ni chuki binafsi au ni nini????
Ndugu yangu Kalamu afadhali wewe umesema. Sikujua Jumbe alikatiwa umeme pale Mji Mwema mpaka Nyerere alipomsamehe. Na mbona hilo hakuliweka kwenye kitabu chake? Au naye alikuwa anaogopa adhabu kubwa zaidi?
Huo ni muono wako nami sina uwezo wa kuuingilia wala kukubadilisha mawazo. Isipokuwa, facts zijibu kama unaweza:
Jee, nyerere hakuhamisha watu takriban millioni kumi kutoka makazi yao ya asili?
Jee, nyerere hakusababisha kati ya aliowahamisha wafe kwa, kuliwa na wanyama? kugongwa na majoka? kukosa chakula? kula mizizi yenye sumu kwa njaa? kukosa matibabu?
Jee, nyerere hakuanzisha sheria ya "ditenshen" amabyo hakuna aliyeweza kukutowa isipokuwa yeye?
Jee, watu aliowa-"ditenshen" nyerere wengine hawakufia jela?
Jee, nyerere, hakuzuwia habari kuandikwa isipokuwa inazotaka serikali yake tuu?
Nadhani hizo ndio hoja na hoja si mimi wala si wewe wala si mtanzania yeyote kuwa ni mwendawazimu. Wendawazimu ni maradhi kama maradhi mengine yeyote na si tabia njema kujumuisha watu na kuwatusi kama unavyotaka ieleweke. Naomba jibu facts.
Jasusi:
Si jambo la kuficha kuwa kuna kikundi chenye mlengo na kusudio maalum la kumchafua Nyerere tokea siku nyingi. Lakini juhudi zao hazifui dafu kila wanapopambana na kivuli cha mwanamapinduzi huyu.
Zomba, mi nadhani naelewa argument yako,lakini nahisi kwamba kuna a big amount of bitterness, wakati hakuna haja. Inaeleweka kwamba Nyerere alifanya kosa kubwa na vijiji vya ujamaa, na wakati ule alitaka kujenga jamii ya kishosalisti, lakini also lazima tukubali kwamba despite it all he was honest, hakujilimbikizia mali.
Nadhani tunaweza kuanza thread nyingine kuhusu Nyerere ingawa tayari imeshajadiliwa, but katika hili la Lowassa he was right!
Angalau alifanya kama aliyosema. Hakuwa fisadi wala hakujilimbikizia mali, kama Mkapa aliyemchagua aligeuka hilo si kosa lake. Ndio tulikuwa maskini wa mwisho lakini hakukuwa na matabaka. Sasa kuna maskini wa kuzidi enzi za Mwalimu na kuna wanaoishi dunia ya kwanza.
Najua hakutufikisha mbali lakini matendo yake kama binaadamu yanaonyesha nia njema. Huwezi kufananisha na JK na wenzie wanaouza nchi.
Wewe si jasusi? ingia kazini utafute ukweli utaupata tu. Jumbe ni muungwana na muungwana "akitafunwa na mbwa hatangazi kidonda".
kama kuna kikundi hicho mimi nakuhakikishia sikijuwi, msimamo wangu ni facts zisizopingika na nilikuwepo wakati wa nyerere na nimeyaona na si ya kusikia. jee hujuwi kuwa wakati wa nyerere tulikuwa kwenye dimbwi la umasikini?
Interesting. You make the allegation and you want me to seek the evidence? Tupe ushahidi wewe, na majina ya wale waliouawa detention na walioliwa na wanyama.
BTW sheria ya detention bado ipo. Tuliirithi kwa Waingereza.
Jasusi mpe shule huyu zomba AKA.....
Labda hana taarifa kuwa hata marekani "Eminent Domain" inaruhusu serikali kuhamisha watu toka maeneo yao na kuwapeleka maeneo mengine ili kupisha uendelezi wa maeneo husika. Wamarekani wamejaribu kupingana na hii sheria lakini supreme court ya Joji Kichaka imekubaliana na serikali na watu wanahamishwa kila siku kupisha ujenzi wa mabarabara na viwanda na makampuni binafsi wakati mwingine bila hata "kulipwa fidia"!