Kisura
JF-Expert Member
- Jun 21, 2007
- 364
- 26
Jkikwete heshimu waliokuzidi umri!!! dont do it again!
very funny... 🙂
Jkikwete heshimu waliokuzidi umri!!! dont do it again!
Nyerere alisema Lowassa hafai kuwa Rais kwa sababu ni mla rushwa na mpenzi wa kujilimbikizia Mali.JK akaamua kukiuka maneno hayo na kumchagua kama waziri mkuu..Kumbe Mwalimu hakukosea..
Huyo nyerere ndie alikuwa fisadi mkuu wa Tanzania, au haukuwepo wakati wake na unamsoma tuu kwenye historia za uwongo? Tuulize sisi tuliokosa bahati kwa kuwepo na kuonja joto na madhila ya uongozi wake.
..nyerere alikuwa na busara na uzoefu wake katika madaraka ulimwezesha kuona baadhi ya vitu ambavyo wengine hawakuona au hawakutaka kuona!
..sasa,maneno yake yalikuwa na maana nyingi kutokana na hali halisi ,wakati na mazingira!
Busara za kuwacha watu masikini wa kutupwa?, busara za kuwacha nchi inanuka rushwa?, busara za kuwacha viongozi wasiojali wananchi? busara gani njema uionayo wewe?, hebu tuelimishe, labda ipo, mimi siijuwi!
Zomba una maneno ya chuki wewe na Mwalimu .Mwalimu kama mtu alikuwa na makosa yake lakini Mwalimu aliijali sana Tanzania na Watanzania .
Lunyungu, kweli kabisa nina mchukia sana kwa kutowa roho za watu wasio na hatia halafu anathubutu kupanda jukwaani na kujichekesha. KAUWA WATU WENGI SANA wa-Tanzania, kwa maamuzi yake mabovu, katutia kwenye umasikini mkubwa sana, Jee Lunyungu unataka nimpende mtu kama huyo?
Akina nani hao ndugu zangu ambao waliuawa na Nyerere? Mbona mimi sijawahi kuwasikia? Alipokuwa jukwaani mbona alipigiwa makofi nao hao aliowachekesha? Au kuna Tanzania mbili--moja ya Zomba na moja ya sisi wengine tunaomheshimu na kumwenzi Mwalimu?
Akina nani hao ndugu zangu ambao waliuawa na Nyerere? Mbona mimi sijawahi kuwasikia? Alipokuwa jukwaani mbona alipigiwa makofi nao hao aliowachekesha? Au kuna Tanzania mbili--moja ya Zomba na moja ya sisi wengine tunaomheshimu na kumwenzi Mwalimu?
Naam, hapa kuna ukweli na ushahidi wa kutungwa(kama ukweli na ushahidi wa namna hiyo upo).
Na kwa watu waliokwishajiaminisha ukweli huo hapawezi kuwepo na ukweli mwingine.
Kwa wat wa namna hiyo,haijalishi, hata kama halaiki ya wananchi waliomuenzi Mwalimu wanapoendelea kumheshimu na kumtukuza; ni wao tu ndio wenye ukweli. Kwa maneno mengine, waTanzania walio wengi ni vichaa kwa kumwona Nyerere kuwa kiongozi aliyetukuka. Ni akina Zomba tu ndio wenye akili timamu. Sasa wanyo kazi ya kututibu ukichaa huu, nasi tufanane nao watu wenye akili timamu. But the reverse of this seems more plausible.