Kuna watu wenye vipaji vya njozi. Kuna watu ambao ndoto ya aina fulani ikija basi kuna mtu amefariki. Na kuna watu wanajua wakiota ndoto ya aina fulani lazima wapige simu nyumbani kuuliza kama ni wazima na wanakutana aidha na habari za furaha au na huzuni.
Tangu enzi za mababu na karibu jamii zote za wanadamu kuna watu "waotao"
Kwa vile ndoto hutumia ishara na alama mbalimbali ni vigumu mara moja kuelewa maana yake hata zile ambazo ziko wazi na dhahiri katika picha (symbolism).
Kuweza kuelewa njozi ni lazima mtu uwe na utaalam au kipaji cha kuelewa njozi na ujumbe wake. Wakati mwingine ujumbe wa njozi ni zaidi ya kile kilichootwa.
Kwenye maandiko matakatifu (Biblia na Kurani) ndoto zina nafasi ya pekee. Biblia na Kurani zote zinakubaliana kuhusu ndoto za Yusuph na japo zinatofautiana kidogo katika maana lakini zinakubaliana kuwa Yusuph alikuwa na kipaji cha kutafsiri ndoto. Kwenye Agano Jipya tunakutana na Yusuph mwingine (baba Mlishi wa Yesu) ambaye naye tunaambiwa alionywa na mungu "katika ndoto" amchukue mtoto Yesu na mamaye Misri kumlinda na mkono wa Farao.
Katika Kurani pia tunakutana na jinsi ambavyo Yusuph anamshukuru Mungu kwa kipaji cha ndoto na kuzitafsiri (Yusuph 12:101).
Abu Huraira alisema alimsikia Mtume (SAW) akisema hivi "wakati ukikaribia (yaani ule wa ufufuko) ndoto ya muumini ni kweli mara nyingi. Na ndoto ya ukweli ni ya yule ambaye ni mkweli katika maneno yake, ... na zipo ndoto za aina tatu, ndot ile yenye habari nzuri na inatoka kwa Allah, ndoto mbaya ambayo inaleta maumivu na inatoka kwa shetani, na ndoto ambayo ni mazao ya mawazo ya mtu mwenyewe."
Bila kuingia ndani sana kimsingi ndoto zinatakiwa kupambanuliwa hasa zile ambazo ni nje ya hali ya kawaida. Ni zile ambazo zinakukaa kichwani na kwa hakika unahisi kuna ujumbe.
Binafsi naamini kuwa ndoto aliyoielezea mwandishi inaweza kuwa na pande mbili. Upande mmoja ni uchungu wa mwandishi na kumbukumbu ya Mwalimu ambavyo vimeitengeneza njozi hiyo.
Hivyo, ujumbe mkubwa wa njozi ni kumtia moyo huyo mwandishi kuwa hayuko mbali na Mwalimu kimsimamo hasa anapoangalia hali inavyoendelea nchini.
Hapo ndipo picha ya "Nyerere" inapokuja. Nyerere katika ndoto hii anasimama kama alama ya ubora, kuheshimu madaraka, na kuzingatia miiko ya uongozi. Nyerere wa ndoto siyo yule aliyekufa bali ni yule aliye hai, yaani vile vitu ambavyo tunaamini havipitwi na wakati.
Lakini upande mwingine wa hili ni kuelewa pia kuwa sheria ya kutobadilika kwa nishati (law of conservation of energy) ipo pia. Kwamba energy can neither be created nor destroyed. Hivyo energy iliyoko ndani ya mwanadamu haiwezi kuharibiwa.
Je mtu anapokufa ile energy inakwenda wapi? It can not be destroyed. Sheria hiyo ya kwanza ya Thermodynamic inasema kuwa kitu ambacho kinaweza kufanyika ni kuwa nishati yaweza kubadilishwa kutoka katika hali (form) moja kwenda nyingine bila kuiharibu nishati hiyo.
Kimsingi huo basi mtu anapokufa energy yake exists in one form or another. To some this is the basis of pyschic abilities. Kuna watu ambao kwa sababu fulani wanaweza kutune hizi energies. Na wengine wana uwezo wa kutune wakiwa kwenye ndoto.
So, siwezi kushangaa kabisa kuwa mwandishi akiwa usingizini alikuwa overcame na energy ya Nyerere. It is not far fetched.
Wengi wetu ambao tumepoteza wazazi au ndugu wa karibu kuna ile ndoto moja ambayo ukimuota huyo marehemu basi lazima ufanya jambo fulani au kitu fulani kitatokea. Siyo njozi za kawaida hizo.
Natumaini nimechangia.