Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

nyerere kitu alichotujengea watanzania kujua kwamba kuna kabila zaidi ya 120,na kila mtanzania anatambua hilo bila ya kujiuliza kabila gani ni kubwa na lipi ni dogo,kitu hicho ndo ambacho watanzania tutamkumbuka nyerere,tofauti ya nchi za wenzetu kama Kenya ukizungumzia makabila tu ni lazima uwataje wajaluo na wakikuyu,na hata kwenye uchaguzi unakuta makabila makubwa haya yanatajwa sana,lakini kwa Tanzania makabila ni mengi na hakuna kuulizana wewe kabila gani katika masuala yeyote yale,hapo ndo tunapouona umuhimu wa Nyerere
 
Ukipewa uchaguzi kati ya fisadi na chungwa, utapigia kura nini?

Kwi kwi kwi!!!, ninavyowajua Watanzania, kuna wengi tu watachagua Fisadi. Huwa hatuthamini vyema.

Kikawaida usingetegemea watu wamalaumu Nyerere pamoja na makosa yake machache sana ukilinganisha na makosa ambayo wengi wetu tunayafanya kila siku.

Lakini vijana wengi ambao hata hawajui mazingira ambayo Nyerere aliishi na kufanya kazi, wanajifanya wana data za kutosha za kuweza kuwafanya waone Nyerere alikuwa hafai.

Kwa Afrika Nyerere ni Gwiji hasa, siku hizi hata Wakenya wanakubali hilo.
 
I have READ koba's comments. Lakini atambue kuwa binadamu huwezi kuwa perfect 100% ila tunaweza kujumuisha wot you have done then tukasema ulikuwa liability au la. Mwalimu aliongoza mapigano ya kuleta uhuru, akajenga amani na utulivu. akaondoka kwa amani akaacha mizizi ya kuachiana madaraka kwa amani. sijui ingekuwaje kama huo utaratibu usingekuwepo maana ufisadi ungefikia siuju daraja gani. Otherwise FREEDOM FREEDOM Here are some freedom tulipata baada ya Mwalimu Julius kutuachia mchi na kung'atuka. we achieved these freedoms na bado tunapigania zingine zije!!! watanzania bwana!

Freedom of ministers using Millions and Billions selling Government budget to the people.
Freedom of President kuwa Vasco da Gama irrespective nchi kuwa na pesa kidogo.
Freedom kuwa fisadi
Freedom ya kuuza nchi
Freedom ya kubeza maskini ingawa nchi ni moja
Freedom ya kuiba na kudanganaya watu
Freedom ya upendeleo
Freedom ya kunyanyasa wasionacho
Freedom ya matajiri kuendelea kunyonya maskini
Freedom ya kugeuza ikulu kuwa danguro na kijiwe
Freedom ya kutofuata maadili ya uongozi
Freedom ya kuuwa wanyonge na kuendelea kutanua
Freedom ya kuwa mbabe katika ofisi za serikali
Freedom ya ku exploit resources za nchi bila kujali kizazi kinachokuja
Freedom ya kunyenyekea na kuwaabudu wahisani ili hali hali ya wananchi inazidi kudorora
Freedom ya waliojuu kuendelea kuwa juu na walio chini kuendelea kuwa chini
Freedom ya kuendeleza umangi meza
Freedom ya magabacholi kuendelea kutesa ili hali wana wa nchi wakihaha na maisha
Freedom ya wa rushwa kuendesha nchi
Freedom ya kuongoza nchi kirafiki

Unaweza kundeleza hapo mwenyewe ma hizo freedom. kama unaziabudu na unazitamani basi. hongera zako. Ila mie naamini kuwa katika jamii ni pale haki usawa na amani vinapojizatiti ndiyo maendeleo mengine yatafuata. Hata leo tunajidai tuna AMANI NA UTULIVU ni wimbo wa kila mmoja lakini je tumefika hapo vipi?
Julius alikuwa Muungwana, hata kama uchumi aliona ameshindwa ndiyo akaachia ni Uungwana kwani angegomea hapo ungemtoa?? lakini alitambua hilo ndiyo akasema kazi yake ilikuwa kupigania uhuru na kujenga amani. Baada ya kutimiza hilo alituachia sasa tujenge uchumi tukiwa na amani na utulivu. sasa matokeo yake TUNAFISADI halafu tunamlaumu Mwalimu. NO NO NOT FAIR.
 
Bin Maryam ndivyo nilivyouliza.. wakati tunapewa uchaguzi wa "Ndio na Hapana" tulikuwa na uchaguzi wa kusema ndiyo au hapana. Siku hizi hata uchaguzi wa ndio au hapana hakuna, kwani tumeshachaguliwa na jukumu letu ni kusema "ndiyo".

Ndiyo maana nimeuliza ukipewa kwenye sanduku la kura uchaguzi kati ya mafisadi wawili, na kati ya mwadilifu mmoja na ndimu utachagua lipi?
 
Tusijione kuwa sisi ni watu wa amani na utulivu kwa kwa sababu ya Nyerere.Utulivu gani ambao Wazanzibari walikuwa wanapigwa risasi kama panya?Wizi wa kura wa Zanzibar na ule wa Kenya una tofauti gani?Karume na Kibaki wana tofauti gani katika suala la wizi wa kura.Kama ni mabomu yalipigwa Zanzibar kama yanavyopigwa Kenya.Tunajidai nini wakati kwenye back yard yetu kunanuka?
 
IQ ya Nyerere inajionesha kwa viwango kama vile ya wanawe Andrew na John.Au hata kama ya yule marehemu kaka yake Kiboko.Ila yeye alikuwa afadhali kidogo.
 
Bin Maryam ndivyo nilivyouliza.. wakati tunapewa uchaguzi wa "Ndio na Hapana" tulikuwa na uchaguzi wa kusema ndiyo au hapana. Siku hizi hata uchaguzi wa ndio au hapana hakuna, kwani tumeshachaguliwa na jukumu letu ni kusema "ndiyo".

Ndiyo maana nimeuliza ukipewa kwenye sanduku la kura uchaguzi kati ya mafisadi wawili, na kati ya mwadilifu mmoja na ndimu utachagua lipi?

Nikiwa boarding nilisimamia uchaguzi mkuu wa ndio na hapana. Hao mnaowaita mafisadi walikuwa ndio wakuu wa wilaya au mikoa na ndio waliokuwa na majukumu ya kupiga kampeni na kuhesabu. Kwa macho yangu nimeona kura za wabunge zikihesabiwa. Na baada ya kumaliza kutangaza matokeo ya wabunge. Mkuu wa wilaya akawaondoa wanafunzi waliofanya kazi ya kuhesabu kura na kuwaita viongozi wa wilaya kuhesabu kura za uchaguzi wa rais (ndio au hapana).

Na mkuu wa wilaya akawaambia wenzake kuwa sisi ndio tuliokuwa na jukumu la kumpigia kampeni rais na ni lazima wilaya yetu ionyeshe kuwa tulifanya kazi hiyo. Hivyo basi kura za uchaguzi wa rais hazikuhesabiwa. Na kwa muda wa siku tatu viongozi wa wilaya wakawa wanafanya party na kusubiri matokeo ya wilaya nyingine. Walipoona kuwa wilaya zingine rais amepita kwa zaidi ya asilimia 80, basi wao wakaongeza asilimia tano na wakatanga matokeo.

Hivyo naona ni afadhari uchague kati ya mafisadi wawili kuliko mfano wako wa chungwa na mtakatifu.

Tunajenga taasisi za kidemokrasi na kazi hiyo sio rais. Hata historia ya Marekani inaonyesha kulikuwa na uzandiki wa watu kuiba kura au kuzuia watu wasipige kura. Lakini miaka ilivyoendelea wameweza kuboresha vyombo vyao.

Swali lako la uadilifu na ndimu au chungwa, linatafuta instant solution lakini in long term taasisi za kidemokrasia zitashindwa kujengwa.
 
Bin Maryam;

Nimependa sana hii post ya sasa.

Iko very clear.

Mfano:

"Na vilevile kuna correlation inayoonyesha kuwa IQ bila displine haileti mafanikio yoyote. Hivyo issue nzima ya IQ is so complex na controversial"

Ni controversial hiyo iliyopelekea factor za kiutu kama displine etc amabzo haziwaklishwi kwenye IQ zilete factor hii ya EI

Personaly hakuna mahali nimesema nyerere alikuwa na IQ kubwa...etc..nimerudia mara zote kuwa alikuwa na kiwango cha juu cha utu, busara,kutokuwa binafsi, hekima ambazo hizo ndizo zinajenga what is EI.

Uniqueness ya JK Nyerere kwa watuwengine haitokani na IQ bali na EI. Kwahiyo kama unavyosema we need combination of Both kuwa productive kwenye jamii na kibinaadamu na kiutu!

unaweza kupitia!!!

[media]http://www.duniahai.com/Articles/Tumepoteza%20agano%20la%20uhuru.pdf[/media]

[media]http://www.duniahai.com/Articles/Tukapime_1.pdf[/media]


Azimio Jipya:

Niliishi mkoa wa Mara na kusoma kule. Nyerere anatoka katika ukoo wa kichifu au kifalme. Koo hizi katika mila za kiafrika
zimezungukwa na myth. Kwa watu waliotoka nje ya mkoa wa Mara wanaweza kumpenda Nyerere kwa busara na hekima zake.

Lakini kwa baadhi ya watu kutoka mkoa wa Mara, mapenzi yao ni deeper na yenye mythical nature ndani yake.

Katika mila nyingi za kiafrika, mtoto ambaye atarithi cheo cha baba yake kama chifu alizaliwa na ishara
fulani.

Kwa mfano: Baba yake Sundiata Keita (mfalme wa Mali), aliambiwa na mwindaji kuwa akioa mwanamke mbaya sana mwenye kibiongo, basi
mwanamke huyo atamzaa mtoto ambaye atakuwa mfalme mwenye nguvu na utawala mkubwa.

Mfano mwingine: Kuna chifu kule Karangwe, ilibidi mtoto ambaye atarithi utawala akalelewe Uganda na mtoto huyo atarudi Karagwe pale baba atakapokufa.
kuonana kwao uso kwa uso kungefanya mmoja wao apoteze maisha.

Na kuhusu Nyerere, kuna lundo la stori. Lakini moja niliyopewa ni kwamba mnajimu wa jadi wa kizanaki alitabiri kuwa siku
ya kuzaliwa kwa mrithi wa uchifu. Chui atatokea na kuua mbuzi. Na mtoto atayezaliwa siku hiyo atakuwa chifu mkubwa.
Na sio chifu wa wazanaki bali wa taifa kubwa. Na Nyerere alizaliwa katika siku hiyo ya chui kuua mbuzi.


Hivyo naelewa kabisa ukutaja IQ katika posti zako. Lakini kumbuka katika kundi lako, kuna watu wanaopenda kumpamba kiongozi
kwa kutumia myth ambazo haziko-supported na facts. Na moja wapo ni kutumiwa IQ.
 
Bin Maryamu, unaweza kuelezea hali ya Tanzania leo hususan umoja, utulivu na amani, bila kutaja jina la Mwalimu au vitu hivi tumeshushiwa na Mungu kwa sababu sisi ni watu wema zaidi ukilinganisha na Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Congo, Msumbiji, Nigeria, Angola n.k ?

Kwanini Mungu atupendelee sisi?
 
Bin Maryamu, unaweza kuelezea hali ya Tanzania leo hususan umoja, utulivu na amani, bila kutaja jina la Mwalimu au vitu hivi tumeshushiwa na Mungu kwa sababu sisi ni watu wema zaidi ukilinganisha na Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Congo, Msumbiji, Nigeria, Angola n.k ?

Kwanini Mungu atupendelee sisi?

Suala zima la Amani la TanzaniA ni complex issue. Na hakuna mtu anaweza kupata credit. Kwanza Tanzania ilikuwa ina njia tatu za utumwa. Na biashara hii ilifanya kuhamahama na kuchanganyikana. Ukienda Kariakoo kuna zaidi ya vizazi vitano vya wa kutoka Mwanza, Tabora au Kigoma. Na watu hawa wamechanganyika kabla mjerumani hajaja katika nchi yetu.

Vilevile wakazi wa mikoa ya kusini walishachanganyika toka miaka ya zamani sana. Na vita vya majimaji vilivyoua zaidi ya watu 300,000 katika mikoa hiyo vilifanya watu kusambaratika na kuzidi kuchanganyikana.

Vilevile utawala wa mjerumani ambao ulikuwa ni wa moja kwa moja haukuanzisha matabaka ya makabila yenye nguvu.

Tanzania ilikuwa sio koloni baada ya vita vya kwanza. Na hivyo wahamiaji wa kizungu ambao walichukua ardhi hawakuwa wengi. Mpaka tunapata uhuru kulikuwa na Wazungu kati ya 10,000 na 20,000. Wakati Kenya ilikuwa na zaidi ya wazungu 100,000. Kwa mtaji huu watanzania walibaki kwenye vipande vyao vya ardhi ambacho ni chanzo cha mahitaji yao ya kila siku na hawakuwa na sababu ya kudundana. Hiyo hali haikupatikana Kenya.

Lugha ya kiswahili ilikuwa imeenea nchi nzima. Hivyo watu tayari walikuwa na kitu kinachowaunganisha zaidi ya utaifa.

Makabila ya Tanzania ni vikundi vidogo vidogo na hakuna kabila linaloweza kubadili matokeo ya aina yoyote ya uchaguzi mkuu. Hivyo maasi au chuki ya kabila moja kwa kabila jingine, hayatingishi sehemu yoyote ya nchi. Kwa mfano kuna kabila moja dogo huko Singida lilikwenda kuiba ng'ombe na kufanya fujo huko Tabora. Na wakazi wa Tabora wakakusanya sungusungu wao na wakaenda kukomboa ng'ombe zao na mapigano makali yalitokea. Na haya yote yalifanyika kabla ya 1983. Ingekuwa mambo hayo yametokea kati ya mjaluo na mkikuyu ingekuwa ni matatizo ya nchi nzima. Kwa Tanzania ilitosha kupeleka kikosi kidogo cha FFU kutuliza ghasia.

Chanzo kikubwa cha migogoro Afrika kimekuwa EYES ON PRIZE baada ya uhuru. Prize yenyewe imekuwa kugawana mapato yanayotokana na uchimbaji wa madini. Tanzania haikuwa na prize yoyote hile ya kugombea. Amani unayoona wewe ni kwa sababu hatuna cha kugombania.

Hivyo amani ya Tanzania ipo kabla ya Tanzania kupata uhuru. Na kama unakataa lete mfano mmoja unaoonyesha watanzania walishajianda kupigana wenyewe kwa wenyewe baada ya kupata uhuru.


Na Tanzania ukilinganisha na Kenya:
Kenya kuna makabila makubwa ambayo hayakuwa na mahusiano yoyote ya karibu kabla na baada ya uhuru. Pamoja na nchi hiyo kuwa kubwa ni sehemu ndogo tu ya ardhi yafaa kwaa uzalishaji.

Na Tanzania ukilinganisha na Uganda:
Uganda kulikuwa na falme Tano za kikabila. Lakini waliopendelewa ni Baganda. Na migogor yao ina historia kabla ya kuja kwa wakoloni.

Na Tanzania ukilinganisha na Uganda:
Mgogoro wa Msumbiji ulianzia toka wao wakiwa katika vita vya mapambano ya kukomboa nchi yao. Na mgogoro huo ulianzia wakiwa Tanzania hivyo sina sababu ya kuuelezea zaidi.

Na Tanzania ukilinganisha na Nigeria, COngo:
Mgogoro wa Nigeria unafanana na wa Congo. EYES on Prize. Nchi hizi ziliachwa zikiwa tajiri kuliko nchi zozote za kiafrika ukiondoa SA. Na ufisadi uliopo Tanzania unaonyesha kabisa kuwa tungekuwa na vitu vya kugombea katika nchi hile urais wa Nyerere ungedumu kwa muda mfupi.

Na Tanzania ukilinganisha na Angola:
Pamoja na kuwa na mapigano ya kugombea mali. Mgogoro wa Angola ulitokana na ubaguzi. Moja ya tatu ya wa-Angola wanadamu ya kireno na hawa walikuwa na nafasi nzuri kuliko wasiochanganya. Hivyo mapigano kati ya walichanganya na waVimbundu yalianza.
 
Bin Maryam,
Tanzania pia kuna makabila makubwa. Hatutofautiani sana na Kenya. Ukichukua Wasukuma, Wahaya, Wanyakyusa, Wachagga kwa kutaja machache tu utaona ile picha inayojitokeza Kenya ya Wakikuyu, Wajaluo, waluhya, etc. Lakini tofauti kubwa kwetu ni kwamba nchini Kenya Kenyatta alikuwa tribalist, tofauti na Mwalimu, na sera zao kuhusu makabila zilitofautiana sana. Waingereza walipenda sana mfumo wa divide and rule na hata kule Mara kwenye makabila zaidi ya 22 walikazana kupachika machifu kwa kila kabila ili kabila moja litofautiane na jengine. Give Mwalimu his credits.
 
Bin Maryam,
Tanzania pia kuna makabila makubwa. Hatutofautiani sana na Kenya. Ukichukua Wasukuma, Wahaya, Wanyakyusa, Wachagga kwa kutaja machache tu utaona ile picha inayojitokeza Kenya ya Wakikuyu, Wajaluo, waluhya, etc. Lakini tofauti kubwa kwetu ni kwamba nchini Kenya Kenyatta alikuwa tribalist, tofauti na Mwalimu, na sera zao kuhusu makabila zilitofautiana sana. Waingereza walipenda sana mfumo wa divide and rule na hata kule Mara kwenye makabila zaidi ya 22 walikazana kupachika machifu kwa kila kabila ili kabila moja litofautiane na jengine. Give Mwalimu his credits.

Ukubwa wa kabila sio Tatizo. Tatizo ni percent yake katika nchi.
 
Azimio Jipya:
Hivyo naelewa kabisa Hukutaja IQ katika posti zako. Lakini kumbuka katika kundi lako, kuna watu wanaopenda kumpamba kiongozi kwa kutumia myth ambazo haziko-supported na facts. Na moja wapo ni kutumiwa IQ.

Bin Maryam: Thanks very much for the concern!

Ninajua Mtoto aliyemsomeshwa nyumbani.."Home school" mpaka darasa la sita. Just simple matheatics and languages! .. Ilikuwa ni kelele na kila mtu akisema that is not the procedure! alipewa Mitihani wa kupanua UTU,UBINADAMU,KUTOKUWAMBINAFSI, HEKIMA, UCHESHI,MAADILI na thamani nyingine kama hizo. Masomo mengine alikuwa ADEVELOPE INTEREST MWENYEWE kwenye computer na kwenye nature.

Alipelekwa darasa la 6 na 7 ...tu! ili kupata links tu! Na shuleni condition zilikuwa asisomeshwe kwa pressuere na kuwaforced any materials on his head kwani haikuwa muhimu darasani anakuwa wangapi! kilichotakiwa ni uwezo wake wa kujenga Creativity na JOY ya kusoma na kugundua mwenyewe anachoona ni sahihi. AND teachers just be there for him.... Now is a great man!

Utaona alikuwa anakwepeshwa swala zima la kujenga IQ na kuiabudu.

Personaly I completely regards it as a "Myth" mtu anaweza kuwa mkomavu na kumanage ustawi sahihi wa maisha bila kupitia normal programing za shule kama zinavyofahamika kwa wengi. Swala la home schooling ni very common sehemu nyingi sasahivi. Yote hii ni kuondoa myth ya IQ... kuruhusu natural growth au tuseme "EI" au shule nyingine wanaita "EQ" amabyo ni ukomavu wa kiUTU katika ustawi wa jamii!

NI kweli na ndio maana jana nilivyona wenzangu wametumia IQ na Ku_capitalise on it! Maramoja nikafanya adjustment. Its true it is very sweeping..kujaribu kuelezea what is an EI vs IQ kwenye charting bord! but that is what we have at the moment...and we shall try in our best to use it!

Ni kweli kuwa Ni Zamani sana IQ ilitumika kuonyesha uhodari fulani wa mtu kwenye jamii, ndio maana mimi sikushughulikia kabisa kujua ya JKN ni ngapi...Au Eistean, Galileo, Jesus..etc walikuwa na Ngapi kwani to me its invalid. Utaona hoja ilivyo nzito kwenye sites nilizokupa. Utaona Ni University ngapi zinafundisha the whole thing "WHY IE and not IQ.." au why we should we combine them...for any evaluation of person.. National or any System for that matter?

Naamini umefuatilia kidogo na umeona....!

Kuna mifano mingine hatuwezi kuitumia hapa..kama was JESUS, Benjamin mkapa,EL and Galeleo an EI? Unaona hatujali wana IQ kiasi gani. Wachambuzi wa hivi viwango Hawajali kuwa Nyerere alikuw ana IQ ya ngapi. Kuna bwana anafanya Phd..ya nini? Was JK Nyerere an EI? Utaona hizo links za kiswahili nilizokupa..ana task ya kuanalyse If Tanzania as a Nation is an EI na wala sio kuwa TZ is an IQ!!! alinganishe na majirani zetu etc ...Utaona amepitia alama za kitaifa/symbols/ Nyimbo etc..kwani ukizifanyia zile nyimbo uchunguzi wa kina alafu ukalinganisha nyimbo za vijana wengi wa sasa pamoa na kuwa wana IQ nzuri sana utaona kuwa EI zao ziko chini.Kwa nini kujihangaisha kote huku? ALL THIS IS BECAUSE IE/EQ NI QUATIFIBLE!!

Ndio maana hata nchi itumie mtindo gani wa kujenga uchumi..ujamaa/kijtegemea/kibepari/kikibaki/any .. bila viogozi kuwa "EI" kiasi cha kutosha...matatzo makubwa yatafuatia tu!!Utaona kunakundikubwa la wachangangiaji wengi hap JF wao in simple terms wasema Rules of law/ Utawala bora/ maadili na miko ya uogozi/..Lakini we need all this in a particular formula.

I beliave JKN was an EI and not IQ. How about BEN Mkapa and EL? sijui!!!

anyway nimalizie kwa kuseama..EI au EQ ni terms mpya tu ambazo zinatumika ku_organise scietificaly the whole concept ya UTU/MAADILI MEMA/UBINADAMU/ and the likes ili kuondoa Ambiguity kwenye mawasiliano.
 
IQ ya Nyerere inajionesha kwa viwango kama vile ya wanawe Andrew na John.Au hata kama ya yule marehemu kaka yake Kiboko.Ila yeye alikuwa afadhali kidogo.

Alnadaby;

Nafikiri umeptia mjadala mzima wa post za nyuma kuhusu IQ.
Hebu soma hii!

The Trouble with IQ

http://www.danielgoleman.info/blog/2007/03/13/the-trouble-with-iq/

The relation of IQ to exceptional performance is rather weak in many domains…For scientists, engineers, and medical doctors…the correlations between ability measures and occupational success are only around 0.2, accounting for only 4% of the variance (Baird, 1985).

More generally, prediction of occupational success from psychometric tests has not been very successful. In a review of more than one hundred studies, Ghiselli (1966) found the average correlation between success-on-the-job measurements and aptitude-test scores to be 0.19. Aptitude tests can predict performance immediately after training with an average correlation of 0.3, but the correlation between performance after training and final performance on the job is only about 0.2 (Ghiselli, 1966).

Reviews of subsequent research have reported very similar correlation estimates. When corrections were made for the restriction of range of these samples and for unreliability of performance measures, Hunter and Hunter (1984) found that only cognitive ability emerged as a useful predictor with an average adjusted correlation of 0.5 with early job performance. However, a recent review (Hulin, Henry and Noon, 1990) has shown that with increased experience on the job the predictive validities of ability tests for performance decrease over time by an average correlation of 0.6. This implies that ability tests can predict early performance on a job, whereas final performance is poorly predicted
.

Ndio maana kwa ufupi kabisa kumtathimini JKNyerere na famila yake kwa ubora wa IQ peke yake inawezakana usipte picha ya kweli na inayopimika. Kama utakuwa umefuatia utaona kuwa hawa wataalamu wanongezea nguzo niyingine hapo, waniita "EI" ili kupata ukamilimifu wa tathimni husika.

Bado ninaamini JKNYERERE alikuwa Kiumbe chenye Thamani ya juu kabisa kwenye viwango vya UTU/UPENDO/MAADILI/HEKIMA/BUSARA mambo ambayo wataalamu wanayapa formula hii ya "EI" au "EQ" na sio "IQ"
Pitia mtaa huu...http://www.eiconsortium.org/
 
Bin Mariam,
Ukubwa wa kabila sio Tatizo. Tatizo ni percent yake katika nchi.
Duh mjomba hapa umeniacha nje kabisa!... Ni ukubwa gani unaozungumzia hapo juu.
 
Ukubwa wa kabila sio Tatizo. Tatizo ni percent yake katika nchi.

Hili sioni kama ni tatizo hata kidogo. Sasa hili la kabila fulani kuchangia percent kubwa katika population ya Tanzania tutalitatua vipi? Tuwaue wale wanaotoka katika makabila yenye watu wengi? Hebu fafanua unaposema tatizo ni percent unamaanisha nini?
 
Bin Maryam wrote:

Ukubwa wa kabila sio Tatizo. Tatizo ni percent yake katika nchi.

Bin Mariam,

Duh mjomba hapa umeniacha nje kabisa!... Ni ukubwa gani unaozungumzia hapo juu.

Yaani Bob umenifanya nicheke kweli kweli..............sasa hiyo percent sijui iko low au high!!!
 
Hili sioni kama ni tatizo hata kidogo. Sasa hili la kabila fulani kuchangia percent kubwa katika population ya Tanzania tutalitatua vipi? Tuwaue wale wanaotoka katika makabila yenye watu wengi? Hebu fafanua unaposema tatizo ni percent unamaanisha nini?

Watu hawakuchagua kuwa wa kabila fulani. Wamezaliwa na kujikuta katika kabila hilo. Hivyo hilo sio tatizo. Kwa Tanzania hata kabila kubwa bado percent yake ni sehemu ndogo kwa taifa na hawawezi kujihamulia mambo yote muhimu wenyewe. Na kwa mtaji huo muundo wa makabila yetu unasaidia kudumisha AMANI.
 
Bin Mariam,'
What is true in Tanzania is or should also been true in Kenya. Kenyatta alipokuwa jela waliojenga KANU walikuwa ni Jaramogi Odinga na Tom Mboya. Lakini walikubali kumwachia nafasi ya uongozi kama vile akina Kanyama Chiume walivyomwachia Banda kule Malawi. Lakini unfortunately ule umoja uliokuwepo ndani ya KANU haukuendelezwa na Kenyatta alivyoingia Ikulu. Aligeuka kuwa a tribal chief. Ndiyo maana Kenya inaungua leo. Kwa Tanzania Nyerere alifanya kila jitihada kuhakikisha ule umoja wa TANU unaendelezwa nchi nzima hata kama makabila makubwa makubwa yalinyimwa nafasi ya kutanua misuli yao. That is the difference, and an important one, I might add.
 
Back
Top Bottom