Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Mwanakijiji,

..kama elimu ilidorora, ina maana tulikuwa tukielekea kwa kasi kubwa kwenye ujinga.

Nani alisema elimu ilidorora, tulipopata Uhuru tulikuwa na madaktari wazalendo 8 tu, Mwalimu alipoacha Urais unajua tulikuwa na wangapi? Shule za msingi zilikuwa ngapi wakati wa uhuru, ni wangapi na "umasikini" wetu waliweza kusoma. Unajua literacy level yetu ilikuwa over 90% under Mwalimu? Wengi unaowaona leo hii madarakani walisoma enzi za "umasikini" wa Mwalimu. Sijui hili wazo la elimu ilidorora una ushahidi gani.

..kama huduma za afya zilidorora basi maradhi yalianza kutuzingira tena.

Duh, una msingi gani wa kusema huduma za afya zilidorora? Unakumbuka kampeni ya "Mtu ni Afya" na "Chakula Bora" jinsi zilivyokuwa na mafanikio. Mara nne katika utawala wa Nyerere hatukuwahi kuishi kwa njaa kiasi kama cha 1994 na 2004. Hata njaa ya 1984 tuliposhindia Yanga na RTC watu wetu hawakufa kama ilivyotokea Ethiopia at the same time. Kwanini?


..kama viwanda viliacha kuzalisha na kilimo kilianguka ina maana umasikini nao uliongezeka.

Viwanda gani viliacha kuzalisha wakati wa Mwalimu? Mutex, Mwatex, Urafiki, Bora, n.k ?

..Mwalimu aliazimia kupigana na ujinga, maradhi, na umasikini.

Hakuazimia tu, alijitahidi kupigana navyo. Na kwa kiasi kikubwa alifanikiwa sana.

..Mwalimu alielekeza kwamba maadui hao watatu walitufanya tuwe WANYONGE, na kusababisha TUNYONYWE, TUONEWE, na KUPUUZWA.

Mwalimu alijua tatizo, na hata leo watawala wetu hawajaja na tatizo jingine. Leo hii wameongezewa tatizo la nne, Ufisadi.


..Tukubali kwamba Jemedari wetu alishindwa kutuongoza ktk vita ya kuondoa Umasikini,Ujinga, na Maradhi. Pamoja na hayo alituachia lulu nzuri ya umoja na mshikamano.

Si kweli, jemedari alipigana kwa ajili ya uwezo wake wote, alijeruhiwa vitani, na alikubali kumpa jemedari mwingine. Alifanya yote aliyoweza na aliposhindwa kuwaingiza wananchi wake kwenye ile nchi ya ahadi, akaweka manyanga chini akitumaini Mungu atamuinua Yoshua!! Bado tunasubiri Yoshua ainuke kutuongoza kupambana na Yeriko ya Ufisadi, na kuwavamia wananchi wa Kanaani na kuwanyang'anya vitu vyetu.

Kama Martin Luther kabla yake, Mwalimu alitambua bila ya shaka asingeweza kuingia kwenye ya ahadi pamoja nasi, lakini kwa mbali aliona zile tambarare za nchi ile imiminikayo "maziwa na asali"!!
 
Bin Maryam,Mwanakijiji,Mkandara

..si kwamba Nyerere hakufanya lolote jema wakati wa Utawala wake.

..Nyerere alijitihidi kueneza elimu kwa wote, kupeleka huduma za afya vijijini, na kujenga viwanda.

..then something happened which i dont know for sure.

..Nyerere akaporomosha uchumi kwa kasi ya kutisha kabisa. Hali ya maisha ikawa ngumu kwelikweli. Elimu na huduma za afya zikadorora, na viwanda vikasimama uzalishaji.

Baba wa Taifa alipoondoka madarakani, aliacha nchi ikiwa MUFILISI.

Heshima kwako Jkuu:

Analyse the whole situation by Forces and the systems on the time of action. Kuna aina mbili tu Ya Uchumi.

Wewe ni Baba Mke na watoto, wakike na wakiume. Nyumbani uchumi umeyumba. Katika hali hiyo kuna mambo mawili. Familia moja Baba anawaruhusu Mke, watoto wa kike na Wakiume..Watoke waende mtaani wauze/wasaliti UTU, UBINADAMU, MAADILI YA KIUTU..YA NDOA, WAKOPESHWE HUKU WANATUKANWA etc ilimradi tu Waje na uchumi nyumbani.... Hela ya kurahisisha maisha magumu pale nyumbani. Huo Ni uchumi unaokiuka UTU Ni uchumi usio "EI". Uchumi huu unaweza kuwa na vitu vingi na UTU kidogo!!Unaweza kuwa na vitu vingi na ufisadi mwingi, unaweza kuwa na vitu vingi na magonjwa mengi..etec..etc

Baba mwingine anafanya kinyume kabisa na huyo wa kwanza. Anaigoza familia yake kwa machungu na uvumilivu mkubwa, kujisitiri na kufanya kila kile watakachoweza hata kma ni kulala chini ilimradi tu wasihujumu na kusaliti UTU,UBINAADAMU, MAADILI YA MAHUSIANO,UONGOZI ETC. Baba anasimama imara kabisa kuhakikisha kuwa hilo linatokea. Huu ni uchumu mgumu na unaokwenda kwa Polepole na sana na wenye manunguniko hata kutoka kwa mke na watoto. Ni uchumi usio mashuhuri ni Uchumi "EI" Uchumi unaijali kila mtu, uchumi unaoheshimu kila rai, uchumi unao linnda usawa, haki..etc Ni uchumi "EI" unawezekanai uchumi unaotaguliza EI...ukawa hauna "VITU VINGI" lakini "Una UTU mwingi"

Analysisis ya WB, IMF and the like they saw what JKN was doing. WALIVUNJA HIYO PARTERN! Uchumi unaoendeshwa na WB/IMF sio na it will neve be "EI" walipofanikuwa tu..Then WATZ wakapata confusion...na.Tukapromoka...! hadithi ni ndefu lakini leo hii hiyo hadithi inaelezeka wala hakuna siri tena.

Lazima Kuwa kama mjinga fulani Kujenga uchumi "EI". Lazima upate ushirikiano wa kina toka kwa wanafamilia wote, mke, watoto..nina maana JKN apate ushiriakiano wa kina kwa Taifa lote toka moyoni na sio usoni. KANUNI KUU NI HII: Huwezi kuukana UTU na MAADILI YAKE kwa gharama ya uchumi wa Familai au Taifa. Kuukana UTU na HESHIMA YA UTU ..unaalika vita, unaalika uharibfu wote kwenye jamii, unaalika magonjwa yote sugu ...fika hapa:::[media]http://www.duniahai.com/Articles/tambua%20thamani%20ya%20utu%20kwenye%20tiba.pdf[/media]
 
Nyie ni ma-specilists wa kuboronga. Tukisema misingi ya uchumi na elimu aliyoacha Nyerere ni mibovu mnasema Nyerere aliachia madaraka zamani na matatizo ya sasa ya kiuchumi yeye hayumo.

Bin Maryam,

Misingi aliyojenga Mwalimu haikuwa mibovu. Ni uvivu wetu wa kufanya kazi na kuwa wabunifu na wenye nia ya kufanikia (ufanisi) ndio uliotufanya tulemae na kuzorota.

Aidha tumshukuru Mwalimu Nyerere kwa kusukuma Mashirika na viwanda kutoa ruzuku ya welfare kwa Watanzania ambao walichipuka kuwa tabaka la kati.

Nimelitaja hili la welfare through corporations and industries kwenye ile mada ya Money Matters http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=9328. Tulijaliwa sana kutoa ajira bwelele na huduma za jamii kwa kutumia mapato ya mashirika, ndio maana hata ingawa mishahara ilidumaa, lakini kuwepo kwa huduma bure za afya, elimuna kadhalika kulitusaidia kupata nguvu kufikia hatua fulani.

Kilichotakikwa ilikuwa kudumisha nguvu hivo na kuanza kujitegemea. Mtu anakujengea msingi bure, wewe unalalamika eti akuinulie kozi 10 za matofali?

Mentality zetu ni kuwa kila kitu tupewe bure na ndio maana tumelelea na kuzalisha tabaka la Watanzania wavivu ambao hutafuta njoa rahisi na za mkato kufanikiwa kimaisha na si kwa uchapakazi!
 
Nyerere alituletea njaa mbaya sana & umaskini wa kutupa na alikuwa dikteta wa aina yake ambaye alikuwa hauwi lakini alikuwa anaweza kuku depress na kukuweka ndani bila kosa,virtually kulikuwa hakuna freedom under his regime....wewe mambo gani ya kutuambia tupige kura ya kuchagua kati ya Nyerere na kivuli,hiyo ni akili kweli?na TZ tangu uhuru 1961 growth yetu ni negative tuu...na wanaosema Nyerere kaleta amani ni kitu gani alifanya practically which justify mnayosema,Nyerere aliachia nchi maana ilimshinda kabisa na wakati anaondoka nchi ilikuwa bankrupty na alijua akiendelea kitakachofuata ni vita tuu kwa sera zake za maduka ya kaya

Koba,

Point taken. Hakuna mmoja wetu ambaye ni mshabiki wa JKN anayesema hakuwa na mapungufu yake.

Tunajiuliza baada ya yeye kuondoka madarakani au duniani, je ni nini kimefanyika kusahihisha makosa yake ya uongozi na sera ili Mtanzania aneemeke?

It is now 22 years since he ceased to be a president and at least 8 years since he passed away, what have we done to correct his wrongs if your opinions imply that "tulikuwa tunamuogopa"?
 
Enzi za Nyerere kulikuwa na miiko ya viongozi, ambayo ilibidi ifuatwe. Kila kiongozi alifuatiliwa mienendo yake ikiwa ni pamoja na mali alizokuwa nazo kabla ya kupewa uongozi, katika uongozi na mara baada ya uongozi.

Sina maana kwamba alikuwa malaika, alikuwa na makosa yake kama binadamu. Kitu kikubwa alikuwa anawajali wananchi wake kuliko alivyokuwa akijijali yeye mwenyewe na familia yake. Hakuwa na tamaa ya kujilimbikizia mali kama viongozi wetu wa sasa hivi. Nadhani angekuwa na uroho angeliuza machimbo ya madini na mashirika, makampuni na vitu vingine vingi zamani sana. Lakini alikuwa anataka watanzania wapate elimu kwanza ili watambue nini kinawazunguka na wawe na uwezo wa kuviendesha kwa manufaa ya watanzania wote.

Mtambo,

Haya ndiyo tunayotukuza kuhusiana na Mwalimu Nyerere. Nia ya kuwa na miiko mikali ya Uongozi haikuwa kuwafanya wawe masikini kama Azimio la Zanzibar lilivyodai. Miiko hii ilihakikisha kuwa haki na usawa vinatumika katika kujipatia mali.

Hii ilikuwa ni kinga dhidi ya Viongozi kutumia ukubwa wa madaraka yao kujipatia mali kwa nguvu za kiutawala na kiunyonyaji.

Mfano, sisi Waafrika palipokuwa na Mtemi, wanakaya ilikuwa ni sharti mumpelekee zawadi iwe ng'ombe, mahindi au mtumwa wa kufanya kazi ili Mtemi anendelee kuneemeka.

Nyerere aliliona hili na ndio maana alilipiga vita. Viongozi wetu hawakutosheka na yale magunia ya mchele au mbuzi, bali walitaka pesa, pesa nyingi mpaka kukufuru na hawajui nini cha kuzifanyia kazi.

Laiti tamaa hizi za Viongozi hawa zingekuwa na matokeo bora kwa Jamii zao. Si dhambi kujipendelea kwa manufaa ya wengi kama Cleopa Msuya alivyotumia madaraka yake kuwatumikia Wabwange wa Mwanga. Mwanaga imeneemeka na ni kwa ajili ya msukumo wa mwakilishi wa mwanga.

Tamaa zenye kudhulumu za kina Karamagi, Kasungura, Mkapa na Yona ndio zinazopigiwa kelele na hizi ndizo zinaonyesha wazi kukiukwa kwa maadili ya uongozi (UTU)!
 
Bin Maryam,

Misingi aliyojenga Mwalimu haikuwa mibovu. Ni uvivu wetu wa kufanya kazi na kuwa wabunifu na wenye nia ya kufanikia (ufanisi) ndio uliotufanya tulemae na kuzorota.

Aidha tumshukuru Mwalimu Nyerere kwa kusukuma Mashirika na viwanda kutoa ruzuku ya welfare kwa Watanzania ambao walichipuka kuwa tabaka la kati.

Nimelitaja hili la welfare through corporations and industries kwenye ile mada ya Money Matters http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=9328. Tulijaliwa sana kutoa ajira bwelele na huduma za jamii kwa kutumia mapato ya mashirika, ndio maana hata ingawa mishahara ilidumaa, lakini kuwepo kwa huduma bure za afya, elimuna kadhalika kulitusaidia kupata nguvu kufikia hatua fulani.

Kilichotakikwa ilikuwa kudumisha nguvu hivo na kuanza kujitegemea. Mtu anakujengea msingi bure, wewe unalalamika eti akuinulie kozi 10 za matofali?

Mentality zetu ni kuwa kila kitu tupewe bure na ndio maana tumelelea na kuzalisha tabaka la Watanzania wavivu ambao hutafuta njoa rahisi na za mkato kufanikiwa kimaisha na si kwa uchapakazi!

Kishoka:


Tunaishi katika dunia ambayo nchi masikini zinatambulika kuwa ni nchi zisizoelewa matumizi ya pesa na maana ya ku-balance vitabu vya uhasibu. Na nchi tajiri ni zile zenye kuelewa matumizi ya pesa na maana ya ku-balance vitabu vya uhasibu.

Elimu na matibabu ya bure ni myth na ndio maana watanzania ni wavivu na sio wabunifu.
 
Nani alisema elimu ilidorora, tulipopata Uhuru tulikuwa na madaktari wazalendo 8 tu, Mwalimu alipoacha Urais unajua tulikuwa na wangapi? Shule za msingi zilikuwa ngapi wakati wa uhuru, ni wangapi na "umasikini" wetu waliweza kusoma. Unajua literacy level yetu ilikuwa over 90% under Mwalimu? Wengi unaowaona leo hii madarakani walisoma enzi za "umasikini" wa Mwalimu. Sijui hili wazo la elimu ilidorora una ushahidi gani.



Duh, una msingi gani wa kusema huduma za afya zilidorora? Unakumbuka kampeni ya "Mtu ni Afya" na "Chakula Bora" jinsi zilivyokuwa na mafanikio. Mara nne katika utawala wa Nyerere hatukuwahi kuishi kwa njaa kiasi kama cha 1994 na 2004. Hata njaa ya 1984 tuliposhindia Yanga na RTC watu wetu hawakufa kama ilivyotokea Ethiopia at the same time. Kwanini?




Viwanda gani viliacha kuzalisha wakati wa Mwalimu? Mutex, Mwatex, Urafiki, Bora, n.k ?



Hakuazimia tu, alijitahidi kupigana navyo. Na kwa kiasi kikubwa alifanikiwa sana.



Mwalimu alijua tatizo, na hata leo watawala wetu hawajaja na tatizo jingine. Leo hii wameongezewa tatizo la nne, Ufisadi.




Si kweli, jemedari alipigana kwa ajili ya uwezo wake wote, alijeruhiwa vitani, na alikubali kumpa jemedari mwingine. Alifanya yote aliyoweza na aliposhindwa kuwaingiza wananchi wake kwenye ile nchi ya ahadi, akaweka manyanga chini akitumaini Mungu atamuinua Yoshua!! Bado tunasubiri Yoshua ainuke kutuongoza kupambana na Yeriko ya Ufisadi, na kuwavamia wananchi wa Kanaani na kuwanyang'anya vitu vyetu.

Kama Martin Luther kabla yake, Mwalimu alitambua bila ya shaka asingeweza kuingia kwenye ya ahadi pamoja nasi, lakini kwa mbali aliona zile tambarare za nchi ile imiminikayo "maziwa na asali"!!


Mwanakijiji:

Njaa kubwa Tanzania ilitokea 1974. Pekua vitabu vyako.
 
Jamani mabaya ya Mwalimu, yamesemwa vya kutosha hapa JF, I mean ifike wakati tuwe wastaarabu na kusema enough is enough, kama hatuwezi kuongelea mazuri yake tu, basi tumuache mzee wa watu apumzike kwa amani mbele ya muumba wake huko alikotutangulia, wote tuko njiani kwenda.

Mzee ES, Respect Mkuu,

I will beg to differ on your stand on this. Let us have a chance to have this discussion so that Ukweli ueleweke and that is the only way to trully honor Mwalimu Nyerere.

For those who are opposing Mwalimu, they need to come out of the closet of Malalamiko and offer solutions to "mafupi" ya Mwalimu.

You Mwalimu haters, give us alternatives and workable solutions to his shortcomings that can develope our country and stop whining like sissies!
 
Mzee ES, Respect Mkuu,

I will beg to differ on your stand on this. Let us have a chance to have this discussion so that Ukweli ueleweke and that is the only way to trully honor Mwalimu Nyerere.

For those who are opposing Mwalimu, they need to come out of the closet of Malalamiko and offer solutions to "mafupi" ya Mwalimu.

You Mwalimu haters, give us alternatives and workable solutions to his shortcomings that can develope our country and stop whining like sissies!

Hakuna mtu anayemchukia Mwalimu. Kuna Mwalimu rais wa nchi mwenye sera zake. Na kuna mwalimu, baba wa watu na raia mwema.

Wengi wetu hapa hatuna chuki yoyote na Mwalimu, baba wa watu na raia mwema.

Lakini tunapokuja katika sera zake kama rais, kuna mapungufu makubwa katika sera. Na haya mapungufu yanaonyesha kati kazi mbalimbali za kitaaluma.

Huwezi ukasema watu wanamchukia Nyerere wakati twakimu za BOT, WB, IMF zinaonyesha matatizo ya kiuchumi yalikuwa makubwa wakati sera za uchumi za Mwalimu zipo kilele.

Kama ujamaa ni Imani kuna watu tumeshatafuta imani nyingine zilizo tofauti kabisa na ujamaa.
 
..OK ,its over now Mwalimu is gone and he'll never come back again,true he had his good & bad lakini does it make any difference in our lives(now),i dont think so,may be in our History books...sasa lets stand up futa vumbi and ask ourselves what now? where are we goin from here?
 
Jokakuu,

1. Kwa kweli Mwal. aliacha uchumi wetu choka mbaya- naskia wakati AHM anachukua dola ilibidi wakope 100 m USD Malaysia maana hakukuwa na akiba ya hata senti!

Is this a fact or myth? has the loan (if it exists) already repaid? Maana katika mfuatilio wa Madeni ya Taifa na kufutiwa madeni wakati wa Mkapa sijawahi kusika hili!
 
Mwanakijiji:

Njaa kubwa Tanzania ilitokea 1974. Pekua vitabu vyako.

hebu nisaidie:

a. Tumepata Uhuru 1961
b. Wakati huo huo tunakabiliwa na njaa 1962 na mapungufu makubwa ya chakula
c. Tunaungana 1964 na maasi ya 1964
d. Kujenga Taifa lililoungana
e. Inapofika 1967 watu wachache wameanza kujilimbikizia mali kwa kiasi kikubwa, weusi walioingia madarakani wameanza kujifanya miungu watu.
f. Azimio la Arusha linatangazwa kama jitihada ya kwanza na ya wazi ya kupambana na ufisadi. Mirija ikanyang'anywa.
g. 1970 upungufu wa mafuta kimataifa
h. Njaa ya 1974 (ambayo Nyerere aliileta according to Koba)
i. Hali mbaya ya kisiasa Uganda, na kutuweka katika hali ya wasiwasi
j. 1977 Kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (kisa Nyerere)
k. 1978 Vita na Uganda
j. 1979 Vita inakwisha tunabakia na jukumu la kulinda amani na kuhakikisha Uganda inanusurika.By 1981 naamini wanajeshi waliobakia wote wanarudi nyumbani
h. 1983 tunaanza kupata mapungufu mengine ya chakula (kumbuka we go through this circle every 10 or so years)
i. 1984 IMF na WB wanaendelea kutoa masharti magumu ya mikopo, Mwalimu anawatolea nje
j. KUtokana na kugongana kwake mawazo na vyombo vya fedha na kuweza kuona mgogoro wa huko mbeleni, na akiwa na haja ya kuweza kuona Mtanzania mwingine atafanya nini, Nyerere kwa hiari yake anang'atuka.

Sasa, niambie with all those odds, ambazo Kenya haikuingia, tulifanikiwa kiasi gani? Nadhani tungekuwa na hali mbaya sana kama Taifa kuliko tulivyo sasa, don't you agree?
 
..then something happened which i dont know for sure. ....Nyerere akaporomosha uchumi kwa kasi ya kutisha kabisa. Hali ya maisha ikawa ngumu kwelikweli. Elimu na huduma za afya zikadorora, na viwanda vikasimama uzalishaji.

Baba wa Taifa alipoondoka madarakani, aliacha nchi ikiwa MUFILISI.

Joka Kuu, Naomba tukae chini na kujiuliza ni vipi uchumi wetu ulianguka. Wengi wameleta Mfumuko wa Bei za mafuta 1973-74, Njaa ya 1974, Vita Uganda 1978-79. Hizi ni facts ambazo hazipingiki.

Sasa tatizo ni lile la hisia na hofu na kutokutaka kubainisha makosa yalitokea wapi. Mimi nitakuwa wa kwanza kubainisha hili kama wengine mnasitasita.

Baba yangu alikuwa akifanya kazi kwenye Shirika la Umma. Alipewa nyumba ya shirika, gari la shirika, Afya bure kwa Mke na Watoto, Dereva, na kile alicholipia ni umeme na maji pekee. Hakulipa kodi ya nyumba au kununua mafuta ya gari kwa pesa yake.

Kwenye Shirika lake watu wenye nafasi kama yake walipata marupurupu hayo hayo ingawa wengi walilalamikia mishahara (including my father) lakini walisahau kuwa walikuwa wakiishi bure.

Shirika hili, lilikuwa na nyumba na mafleti kwa wafanyakazi.

Shirikani mwake kulikuwa na wafanyakazi wataalamu na wale wa kawaida. wale wa kawaida walikuwemo madereve, mataarishi, wapishi,wakata majani, wafaguzi, seremala, fundi bomba, walinzi na upupu mwingine mwingi.

Wafanyakazi hawa, walilipiwa huduma za afya 100%, walipewa chakula cha mchana bure, walikuwa na mabasi ya kuwapeleka kazini na kuwarusisha nyumbani, walikuwa na uniform za bure na hata Duka la kaya ndani mwa shirika (co-op) ambalo liliwauzia bidhaa kwa 50% ya bei ya mtaani.

Sasa kama mashirika yote walikuwa na huduma hizi za jamii ambazo ni afya bure, nyumba za bure, usafiri wa bure na upupu mwingine, je ulitegemea ni vipi tuwe na net profits za kujiendesha?

Kutokana na kuwa na utegemezi huu wa kubebwa, ndio maana imekuwa ni vigumu kwa watanzania kuanza kujitegemea.

Mimi shule mpaka sekondari nilisoma bure, ukienda Muhimbili hata mwananyamala huduma zote zilikuwa ni bure.

What happened is this, these welfare policies created a middle class that surrendered and gave up the spirit of being hard workers when rality checked in and they were required to share the costs.

Hivo basi, mimi ni mfano mmoja wa mafanikio ya matunda ya Ujamaa. Jee njia hii ya huduma za jamii kwa mtaji wa uzalishaji ulikuwa ni sawa? jibu ni ndio na hapana.

Ndio kwa sababu kulisaidia kujenga msingi wa kujiwekea akiba na mali na ukiambatanisha na msukumo wa utaifa na kupiga vita unyonyaji na ulimbikizwaji wa mali, basi zoezi hili lilifanikiwa kwa kiasi fulani.

Hapana kwa sababu zoezi na mfumo mzima ulitupumbaza tukaegemea kutegemea vya dezo na hata kujisahau katika uzalishaji mali. Mbaya zaidi, tukaweka vyama vya wafanyakazi ambavyo vilitetea maslahi pasipo kuoanisha na uzalishaji mali.

The question becomes, what have we done after that? have we been able to acknowledge what happened and correct the shortcomings? have our leaders comeout clean and tell Wananchi that the government and mashirika can no longer continue to carry 100% of social services?

The answer is No, and what they have done is to claim everyone for himself and God for us all and they are on 100 meters dash to fill up their pockets!
 
..OK ,its over now Mwalimu is gone and he'll never come back again,true he had his good & bad lakini does it make any difference in our lives(now),i dont think so,may be in our History books...sasa lets stand up futa vumbi and ask ourselves what now? where are we goin from here?

Koba:

Mambo ya Mwalimu yalishapita. Lakini wenzetu hawachoki kuleta hizi topiki za kumtukuza Mwalimu.

Yanatokea matatizo ya ufisadi, wanasema watanzania wameacha kufuata maadili na miiko ya uongozi ya mwalimu.

Kunatokea vita Kenya. Wanasema mwalimu angekuwa rais angepeleka majeshi Kenya.

Tanzania, Afrika na Dunia sio maeneo static. Ni maeneo yanaokwenda na wakati na ufumbuzi katika haya maeneo yanategemea na wakati na jinsi gani watu wanaoishi katika wakati huo wanataka kutatua matatizo yao.

Ni lazima tuamini kuwa:
People of our generation are far ahead of previous generations. Na hiyo ni fact.
 
hebu nisaidie:

a. Tumepata Uhuru 1961
b. Wakati huo huo tunakabiliwa na njaa 1962 na mapungufu makubwa ya chakula
c. Tunaungana 1964 na maasi ya 1964
d. Kujenga Taifa lililoungana
e. Inapofika 1967 watu wachache wameanza kujilimbikizia mali kwa kiasi kikubwa, weusi walioingia madarakani wameanza kujifanya miungu watu.
f. Azimio la Arusha linatangazwa kama jitihada ya kwanza na ya wazi ya kupambana na ufisadi. Mirija ikanyang'anywa.
g. 1970 upungufu wa mafuta kimataifa
h. Njaa ya 1974 (ambayo Nyerere aliileta according to Koba)
i. Hali mbaya ya kisiasa Uganda, na kutuweka katika hali ya wasiwasi
j. 1977 Kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (kisa Nyerere)
k. 1978 Vita na Uganda
j. 1979 Vita inakwisha tunabakia na jukumu la kulinda amani na kuhakikisha Uganda inanusurika.By 1981 naamini wanajeshi waliobakia wote wanarudi nyumbani
h. 1983 tunaanza kupata mapungufu mengine ya chakula (kumbuka we go through this circle every 10 or so years)
i. 1984 IMF na WB wanaendelea kutoa masharti magumu ya mikopo, Mwalimu anawatolea nje
j. KUtokana na kugongana kwake mawazo na vyombo vya fedha na kuweza kuona mgogoro wa huko mbeleni, na akiwa na haja ya kuweza kuona Mtanzania mwingine atafanya nini, Nyerere kwa hiari yake anang'atuka.

Sasa, niambie with all those odds, ambazo Kenya haikuingia, tulifanikiwa kiasi gani? Nadhani tungekuwa na hali mbaya sana kama Taifa kuliko tulivyo sasa, don't you agree?


...whatever bro,hata uspin vipi naona unarudi pale pale tuu na hakuna mtu anamchukia mwalimu hapa ila fact lazima ziwekwe hapa watu wasije wakarudia tena,alikuwa ni dikteta wa aina yake(not necessarilly muuaji) na bad policy kiuchumi ndio hizo zilituongezea umaskini wa hali ya juu,kulikuwa na sababu gani kunyang'anya nyumba,viwanda,mashule,mashamba makubwa yaliyokuwa yakiingiza mamilioni ya dollar kama tax,biashara halali za watu just kwa jina la azimio la Arusha na kibaya zaidi kuwakabidhi cronies wake waendeshe hayo mashirika kwa sababu ni TANU tuu,kumbuka hizo shule alizonyang'anya zilikuwa hazibagui mtu na zilikuwa zinasaidia watanzania hao hao maskini,kama alikuwa anataka kuongeza elimu si angejenga zaidi kuliko kunyang'anya na kuziharibu zaidi na yote hiyo ni kwa sababu alikuwa mkuu wa nchi,wewe unaonekana unaongea theory tuu tuulize sisi ambao familia zetu zilikuwa affected moja kwa moja na policy zake za dhuluma...mimi babu yangu akikuambia jinsi alivyonyang'anywa nyumba yake na biashara zake bila sababu tena alikuwa ameajiri watu wengi tuu na kulipa tax vizuri na vitabu vya tax vipo mpaka leo....i'm done na hii topic!
 
Is this a fact or myth? has the loan (if it exists) already repaid? Maana katika mfuatilio wa Madeni ya Taifa na kufutiwa madeni wakati wa Mkapa sijawahi kusika hili!

Kishoka:

Michango ilipitishwa na nchi washikaji kuanza awamu ya pili. Mugabe pia alitupa pesa, na shukrani zetu ni kuwa kila akiwafanyia wananchi wake ubabe bado tunashindwa kumwambia ukweli.

Pesa yenyewe ilikuwa kati ya 85 Millions.
 
...na yote hiyo ni kwa sababu alikuwa mkuu wa nchi,wewe unaonekana unaongea theory tuu tuulize sisi ambao familia zetu zilikuwa affected moja kwa moja na policy zake za dhuluma...mimi babu yangu akikuambia jinsi alivyonyang'anywa nyumba yake na biashara zake bila sababu tena alikuwa ameajiri watu wengi tuu na kulipa tax vizuri na vitabu vya tax vipo mpaka leo....i'm done na hii topic!

So you issue here is more of personal and emotional.

I agree, my family lost ardhi, mifugo and property, however I benefited by going to school free and enjoy corporate welfare.

The question that still lingers is this; How in the hell after his depature from power and on earth we are still struggling? are we still intoxicated by "Umwalimu" Do we continue to blame Mwalimu todate while we have a chance to make a diffeence and prove him wrong through actions and not verbiage?
 
Bin Maryamu, anayekana historia yake hujikuta historia inamkana. Kujaribu kufuta historia kwa sababu haiependezi ni kukana one own's identity.

Hatuwezi kuiandika historia ya Tanzania bila Mwalimu hata kama tujaribu vipi.

Vizazi vya sasa vimefungamana sana na vizazi vilivyopita. Huwezi leo uzungumzie Marekani ya leo bila kuangalia 1776. Huwezi kuzungumzia uhuru wa habari na jinsi wenzetu walivyopiga hatua katika uhuru bila kuangalia Azimio lao la Uhuru.

Na hiki kizazi unachokiita ni "chetu" hakiko mbali sana na kizazi cha nyuma yake. Kama leo tuna viongozi waliokuwa kwenye serikali ya Jamhuri ya kwanza, na baadhi ya walioshirikia katika uhuru na mapinduzi bado wapo hai, ina maana hatuko mbali sana na kizazi kilichotangulia.

Ukiniuliza mimi, naamini kabisa kuwa vizazi hivi viwili ni vizazi vilivyoingiliana na viko katika kupishana.

Mgongano wa kifikra ambao ninauzungumzia mara nyingi msingi wake ni huu. Wapo wale ambao wanataka kukikana kizazi kilichotangulia wakiamini kuwa wanajua zaidi na wapo wale ambao wanakiona kizazi hiki kipya kuwa bado hakijastahili kupewa nchi.

Hivyo basi, utaona kuangalia historia yetu ni lazima tuiseme kwa usahihi wake. Baadhi ya watu wanaotaka tumpe Nyerere kwenye shimo la historia wanafanya hivyo si kwa sababu wana data zinazowathibitishia hayo bali ni hisia na machungu yao.

Vinginevyo, aje mtu atuoneshe Tanzania ilikuwaje wakati wa Mkoloni na baada ya mkoloni.

Katika Bararabara, shule, afya, n.k

Maana ni rahisi kuangalia nchi kama Zaire wakati wa ukoloni na Zaire chini ya Mabotu.

Ndugu zangu, historia ya Nyerere ni historia yetu; hatuwezi kuinyofoa na kuikana ili tujisikie vizuri.

Taifa tunaloliona leo hii ni matunda ya wale waliotutangulia. Amani, utulivu, umoja, mshikamano siyo kudra za mwenyezi Mungu. KUna watu wamevijenga vitu hivi na kuviunganisha kama kwa gundi.

Inawezekana kiuchumi na baadhi ya sera hazikwenda jinsi ambavyo zilionekana kwenye ulimwengu wa fikra au nadharia. Tutakuwa waongo tukidai kuwa mambo yalikuwa powa katika kila kitu na ya kwamba tulikuwa mbali kiuchumi. Huko kutakuwa ni kukana historia.

Hata hivyo kosa jingine ambalo siko tayari kulifanya ni la kujaribu kukataa mazuri ambayo Mwalimu aliyafanya na ambayo yamelijenga Taifa tulilo nalo leo hii.

Ukiniuliza kama ningechaguwa kuzaliwa katika nchi yenye ukabila, n.k kama ilivyo Kenya na kuzaliwa katika nchi isiyo na ukabila na vurugu za ndani na inayojitahidi kujijenga kiuchumi, nitachagua hilo la pili.
 
Nationalization of schools and quota prog ilisaidia mikoa iliyokuwa nyuma nayo kupata nafasi ktk elimu! Hii imesaidia kupunguza gap pia kati ya maskini na matajiri!

Wengi wetu hapa JF tuko hapa kutokana na sera za Mwal. ktk free na quota education.
 
Bin Maryam; Koba, Gembe, Mkandara,Mzee Mkjj na Kishoka, huu ni mmoja kati ya mijadala bora kabisa niliyopata kuisoma hapa barazani. Hongera zenu wakuu!
 
Back
Top Bottom