1. Those who make things happen
2. Those who complain when things happen
3. Those who watch things happen
Sijui watanzania wengi tunaangukia wapi?
Watanzania bado hatujaondoka kwenye siasa za kijamaa, viongozi wetu wanahubiri siasa nyingine, raia wengi bado wanaishi kijamaa.
Mwalimu alikuwa na mapungufu yake na alikosea kama kiongozi sasa imefikia wakati Watanzania tukayaweka yote nyuma na kusonga mbele kuendeleza Taifa, mambo ya kukaa na kusema tusingeenda vita ya Kagera or isingekuwa sera hizi na zile za Mwl tungekuwa mbali kimaendeleo.
Imeshapita miaka 22 tangu ang'atuke nadhani sasa itakuwa aibu kuendelea kulalamika wakati hatufanyi chochote kurekebisha makosa yake, muda umefika mimi, wewe na yule tupiganie taifa letu.