Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Hata Chacha Wangwe pia anatembeaga na kifimbo chake, huwa kinampa confidence sana akikishika!

Hahaha umenichekesha kweli sijawahi kunotice hilo, nadhani hata Mkono naye anatembea na kifimbo.

Ila wakati mwingine ina kuwa kama identity au wengine inakuwa kama tabia. Kuna walimu huko vijijini hata mtaani wanatembea na fimbo hata wakistaafu wanatembea na fimbo.

Wakati mwingine inakuwa adictive mfano kama Sir Alex Fuguson anavyotafuna bazoka kila wakati. Ukishazoea inakuwa shida kuacha.

Ila mimi navyojua kwa makabila mengine fimbo ya mzee inaheshima kubwa sana Mfano kwa wachaga hiyo fimbo inaitwa "msenge". Hiyo ni kumpa mzee nguvu na sauti hata machifu walikuwa wanatumia hizo fimbo kama ishaza ya Mtawala. Ila kwa swala la Mwalimu sijui may be kwa sababu alitoka kwenye familia ya Kichifu au linauhusiano na ndumba Mama Nyerere ndie anaweza kujua.
 
Sasa wewe unamuita dikteta kwa sababu baba alinyang'anywa nyumba.. well it is personal to you. Can't argue with that. Ila kumuweka Nyerere na kundi la HItler ni jaribio dhaifu kwa sababu unachotuambia ni upande wa familia yako na hakuna mtu anayebisha. Sasa akitokea mtu mwingine ambaye aliweza kupatiwa elimu, makazi ya maana, afya n.k chini ya utawala wa Nyerere akimuita Nyerere shujaa itakuwaje? Ndiyo maana neno Dikteta lina maana yake halisi.

nimejirisha mwenyewe kuwa umekosea. mafanikio yanaanzia kwa mtu mmoja mmoja. hata kama wale watatokea sitashangaa. mbona na hitler enzi zake kulikuwa na watu wa kumfavor?a kuona anafanya kazi hadi kujitoa muanga? mbona sadamu watu wametokea kudhihirisha kuwa aliwatendea vibaya na bado wapo wengine wanaomfia kwa kumwita shujaa.? charles taylor hivyo hivyo? i repeat for the second that you are wrong per se.

pili kwamba familia yake mushobozi imekuwa muanga wa tabia yake haina maana kuwa tupuuzie. ni dhahili ndivyo anavyotafsiri udictator.
 
Tumeambiwa mara nyingi Kenya ni mfano wa nchi nzuri yenye uchumi mzuri na wenye nguvu. Tulichekwa kwa sababu tulikuwa na kiongozi kama Nyerere. Sasa ninapoangalia nchi zote zinazotuzunguka na ambazo hazikutawaliwa na Nyerere (obviously) I'm so proud to be born in a country where Nyerere was the leader!

kifo_cha_nyerere.jpg

Kumbe mamho yote siyo mambo ya uchumi yanayojenga Taifa!!

Asante Mwalimu na siasa zako za Ujamaa na Kujitegemea!!

Finally history has vindicated you!

I'm so proud and eternally grateful to be a Tanzanian. Yes I am.

Hamtaki?
 
Mwanakijiji

Ngoja waje wakandiaji hapa. Unakumbuka Kenya walivyokuwa wanatusema?

Ngoja waamke.
 
wakiamka tunanyosha kidole... kuelekeza kaskazini mwetu. Maana, tuliimbiwa nyimbo za matatizo ya uchumi ya Tanzania na jinsi gani "Kenya wako mbele, na wamesoma sana".

Sasa siyo nafurahia yanayotokea Kenya bali katika kujenga Taifa kuna mambo ya msingi. Nyerere alichagua yaliyo ya msingi.
 
Nyie ni ma-specilists wa kuboronga. Tukisema misingi ya uchumi na elimu aliyoacha Nyerere ni mibovu mnasema Nyerere aliachia madaraka zamani na matatizo ya sasa ya kiuchumi yeye hayumo.

Kama yeye aliachia ngazi zamani kwanini aendelee kuchukua credit za amani zilizopo sasa?

Katika equation ya sasa ya matatizo ya Kenya. Mzee Jomo anacheza sehemu ndogo sana hapo. Haya matatizo ni ya Kibaki na yeye akihamua kuyamaliza leo atafanya hivyo.

My two cents.
 
Nyerere alifanikiwa mno ila tatizo ni tofauti ya miono yani IQ yake ilikua kubwa mno ukilinganisha na watanzania/waafrika.

Unajua ukiwa na tofauti kubwa ya miono na watu wengi ni lazima wewe utaonekana kichaa ama mchawi.

Mfano haya madini yanayoleta zogo aliyaona na kwa miono yake akajua kabisa sasa hizi hatuna uwezo na wataalamu ngoja tuyaache tutayachiba tutakapopata uwezo lakini manyang'au wao wameiingia na kuyavamia na kuyateketeza.

Nyerere wakati anachukua madaraka alikuta ma Engineer kama sikosei ni wawili,madaktari wasiozidi watatu kwa hali hii alifanya kazi na ku produce ma prof hadi ma prof kibao.
Tanganyika baada ya mjerumani haukua chini ya koloni lolote ila ilikua chini ya uangalizi wa uingereza hivyo waingereza walichuma na hawakujishughurisha na ujengaji wowote tofauti na walivyofanya kenya.
Ktk nchi zilizokabidhiwa na mkoloni Tanganyika aliyokabidhiwa nyerere ndio nchi iliyokua hoi kuliko zote.Watu wanaobeza jitihada za Nyerere inabidi wafikirie nchi aliyokabidhiwa ilikua na wataalamu wangapi na nini alikifanya na laiti tanganyika ingekabidhiwa hawa manyangau wa leo leo hii ingekua ni stori ya kusikitisha .
 
Nyerere alifanikiwa mno ila tatizo ni tofauti ya miono yani IQ yake ilikua kubwa mno ukilinganisha na watanzania/waafrika.

Unajua ukiwa na tofauti kubwa ya miono na watu wengi ni lazima wewe utaonekana kichaa ama mchawi.

Mfano haya madini yanayoleta zogo aliyaona na kwa miono yake akajua kabisa sasa hizi hatuna uwezo na wataalamu ngoja tuyaache tutayachiba tutakapopata uwezo lakini manyang'au wao wameiingia na kuyavamia na kuyateketeza.

Nyerere wakati anachukua madaraka alikuta ma Engineer kama sikosei ni wawili,madaktari wasiozidi watatu kwa hali hii alifanya kazi na ku produce ma prof hadi ma prof kibao.
Tanganyika baada ya mjerumani haukua chini ya koloni lolote ila ilikua chini ya uangalizi wa uingereza hivyo waingereza walichuma na hawakujishughurisha na ujengaji wowote tofauti na walivyofanya kenya.
Ktk nchi zilizokabidhiwa na mkoloni Tanganyika aliyokabidhiwa nyerere ndio nchi iliyokua hoi kuliko zote.Watu wanaobeza jitihada za Nyerere inabidi wafikirie nchi aliyokabidhiwa ilikua na wataalamu wangapi na nini alikifanya na laiti tanganyika ingekabidhiwa hawa manyangau wa leo leo hii ingekua ni stori ya kusikitisha .


IQ uwa inapimwa. Je Nyerere alikuwa na IQ ngapi?
 
Zamani sana walotokea Wanafalsafa wengi na mashuhuri na walifundisha mambo mengi yakiwamo jinsi ya kushi,utu , ubunadamu etc. Mfano Mwanafalasafa kama Galileo,.Einstin, Faraday, YKristo, etc.Zamani wote hawa walikuwa wanchukuliwa kama wanfalsafa waliofundisha aina fulani ya jinsi ya kusihi na kufanikiwa kimaisha tu. Naongelea WANAFALSAFA siongelei dini. The question is, by the time hawa watu Mashuhuri walipoondoka duniani .... Walikuwa wamefanikiwa kisi gani kuifanya Jamii ya wakati huo iwe Imetekeleza na kuishi mafundisho na mfumo wa Maisha waliyofundisha? ok. Mfano YKristo, Basicaly nafikiri huyu alifundisha kuhusu kitu kimoja tu..UPENDO. Miaka imepita tagu alipotutoka huyu mwanfalsafa wa maisha ya Upendo..leo ni 2008 We question ourselves..Mafundisho yake yamefanikiwa kiasi gani? leo dunia inautekelza huo UPENDO kiasi gani? Tunaweza kusema YK for that matter hakufanikiwa? Mchukulie Mwanfalsa yeyote..Albert Einstain, Galileo g, Newton..take any; wote walifundisha basicaly the same PRINCIPAL UPENDO kila mtu kwa naman yake..tujiulize wote hao walifanikiwa au walifail completely? Ile Nembo ya serekali Ina alama ya Mwnege wa uhuru juu mlima kilimanajaro..Unasimamia alama ya UPENDO...tujiulize... Waliofundisha upendo tangu dunia kutokea Mpaka leo..Wamefeli au wamefaulu..? Tusite kujifunza na kuwapuuzia??

Look here:

Ujmbe na mafundisho ya Kifalsafa kama ya Nyerere alivyofundisha kuhusu USAWA, UTU na UPENDO wanachofundisha.... Kinahitajika muda mrefu sana kujifunzwa na watu wa kawaida. Ndio maana you can not simply put it in the category alifanikiwa au hafanikiwa ..KEEP ON PARACTISING IT!!! Mafundisho yao ni basic reference ya daily life for long time to come. Badala ya kuuliza walifanikiwa au hakufanikiwa wewe jiulize umefanikiwa au hujafanikikwa kiasi gani kupractise ...UPENDO, UTU , USAWA, UBINAADAMU na atribute nyingine za kijamii!

Kama Tanzania hatutakikujifunza kupitiakwa philosofia za Nyerere the rest of world will!!!
 
Adhaniae amesimama .......

Binafsi namsifu saaaaaaaaaaana Nyerere alifanikisha laiti Idd Amin asingefanya upuuuzi wake Leo Tanzania ingekuwa sehemu ingine kabisa.

Kumbuka ni viwanda vingapi alijenga wakati wake. Ni wasomi wangapi aliproduce, na mambo mengine.

Nadhani kwa sasa tusitukane mamba kabla hatujavuka mto 2010
 
Zamani sana walotokea Wanafalsafa wengi na mashuhuri na walifundisha mambo mengi yakiwamo jinsi ya kushi,utu , ubunadamu etc. Mfano Mwanafalasafa kama Galileo,.Einstin, Faraday, YKristo, etc.Zamani wote hawa walikuwa wanchukuliwa kama wanfalsafa waliofundisha aina fulani ya jinsi ya kusihi na kufanikiwa kimaisha tu. Naongelea WANAFALSAFA siongelei dini. The question is, by the time hawa watu Mashuhuri walipoondoka duniani .... Walikuwa wamefanikiwa kisi gani kuifanya Jamii ya wakati huo iwe Imetekeleza na kuishi mafundisho na mfumo wa Maisha waliyofundisha? ok. Mfano YKristo, Basicaly nafikiri huyu alifundisha kuhusu kitu kimoja tu..UPENDO. Miaka imepita tagu alipotutoka huyu mwanfalsafa wa maisha ya Upendo..leo ni 2008 We question ourselves..Mafundisho yake yamefanikiwa kiasi gani? leo dunia inautekelza huo UPENDO kiasi gani? Tunaweza kusema YK for that matter hakufanikiwa? Mchukulie Mwanfalsa yeyote..Albert Einstain, Galileo g, Newton..take any; wote walifundisha basicaly the same PRINCIPAL UPENDO kila mtu kwa naman yake..tujiulize wote hao walifanikiwa au walifail completely? Ile Nembo ya serekali Ina alama ya Mwnege wa uhuru juu mlima kilimanajaro..Unasimamia alama ya UPENDO...tujiulize... Waliofundisha upendo tangu dunia kutokea Mpaka leo..Wamefeli au wamefaulu..? Tusite kujifunza na kuwapuuzia??

Look here:

Ujmbe na mafundisho ya Kifalsafa kama ya Nyerere alivyofundisha kuhusu USAWA, UTU na UPENDO wanachofundisha.... Kinahitajika muda mrefu sana kujifunzwa na watu wa kawaida. Ndio maana you can not simply put it in the category alifanikiwa au hafanikiwa ..KEEP ON PARACTISING IT!!! Mafundisho yao ni basic reference ya daily life for long time to come. Badala ya kuuliza walifanikiwa au hakufanikiwa wewe jiulize umefanikiwa au hujafanikikwa kiasi gani kupractise ...UPENDO, UTU , USAWA, UBINAADAMU na atribute nyingine za kijamii!

Kama Tanzania hatutakikujifunza kupitiakwa philosofia za Nyerere the rest of world will!!!


Mwanafalsa anakuja na kipya. Kipya cha Nyerere ni Ujamaa. Nitajie mtanzania au mtu yoyote dunia anayetaka kufuata ujamaa wa Nyerere?
 
Adhaniae amesimama .......

Binafsi namsifu saaaaaaaaaaana Nyerere alifanikisha laiti Idd Amin asingefanya upuuuzi wake Leo Tanzania ingekuwa sehemu ingine kabisa.

Kumbuka ni viwanda vingapi alijenga wakati wake. Ni wasomi wangapi aliproduce, na mambo mengine.

Nadhani kwa sasa tusitukane mamba kabla hatujavuka mto 2010


Visingizio tu. Vita na Idd Amin vilikuwa chini ya miezi sita. Huo uchumi gani unashindwa kuibuka baada ya vita vifupi?

na ufunguzi wa viwanda vingi ulikuwa ni wa makosa. Vilichukua resource ambazo zilikuwa za sekta ya kilimo na kufanya kilimo kudorora.
 
Nyerere alifanikiwa mno ila tatizo ni tofauti ya miono yani IQ yake ilikua kubwa mno ukilinganisha na watanzania/waafrika.

Unajua ukiwa na tofauti kubwa ya miono na watu wengi ni lazima wewe utaonekana kichaa ama mchawi
.

Mkamap: Heshima zangu kwako.

Utafiti mkubwa scietifcaly umegundua kuwa kupima nobility ya mwanadamu ..lazima kja na kipimo tofauti kidogo amabchao kinaweza kueleza vizuri ulichotaka kutueleza hapo. Badala ya kutumia IQ inatumika EI. IQ inabakia kuw akipimo cha kiakili zaidi..Intellect na IQ= emotiona intellegent inapima UTU..look here:Kuna mwenzako Ilikuondoa ubishi usio na msingi aliandika kitabu::::http://www.danielgoleman.info/blog/purchase/

Yaani Mtu anaweza kuwa na IQ Kubwa sana yaani akawa kipanga wa kutupwa.. But Maswala ya Kibinaadamu, Kiutu, Hekima, Kimaisha na Busara akawa sifuri.Yaani GPA yako kali na EI ndogo ..unaweza usiwe wamaana sana kwnye jamiii. Nyerere ana special EI

Emotional Intelligence: Why It Can Matter More Than IQ - 1996

kwa ufupi kabisa chukulia EI kama UTU/ukomavu na IQ kama ukali wa Kiakili...Itellect na soma hapa kwa kina. Utajua jinsi ya kumtofautisha Nyerere na watu wengine.

New York Times science writer Goleman argues that our emotions play a much greater role in thought, decision making and individual success than is commonly acknowledged. He defines “emotional intelligence”?a trait not measured by IQ tests?as a set of skills, including control of one’s impulses, self-motivation, empathy and social competence in interpersonal relationships. Although his highly accessible survey of research into cognitive and emotional development may not convince readers that this grab bag of faculties comprise a clearly recognizable, well-defined aptitude, his report is nevertheless an intriguing and practical guide to emotional mastery. In marriage, emotional intelligence means listening well and being able to calm down. In the workplace, it manifests when bosses give subordinates constructive feedback regarding their performance. Goleman also looks at pilot programs in schools from New York City to Oakland, Calif., where kids are taught conflict resolution, impulse control and social skills.

Copyright 1995 Reed Business Information,

Ngoja na kuletea most important doc. Kukufanulia umhimu wa EI kwenye kuelezea watu kam nyerere na sio IQ pekee yake.. hold on!!!
 
Utafiti mkubwa scietifcaly umegundua kuwa kupima nobility ya mwanadamu ..lazima kja na kipimo tofauti kidogo amabchao kinaweza kueleza vizuri ulichotaka kutueleza hapo. Badala ya kutumia IQ inatumika EI. IQ inabakia kuw akipimo cha kiakili zaidi..Intellect na EI= emotional intellegent inapima UTU..look here:Kuna mwenzako Ilikuondoa ubishi usio na msingi aliandika kitabu::::http://www.danielgoleman.info/blog/purchase/
 
Visingizio tu. Vita na Idd Amin vilikuwa chini ya miezi sita. Huo uchumi gani unashindwa kuibuka baada ya vita vifupi?

na ufunguzi wa viwanda vingi ulikuwa ni wa makosa. Vilichukua resource ambazo zilikuwa za sekta ya kilimo na kufanya kilimo kudorora.

Bin Maryam,

Siku mbili zinatosha kufanya uchumi wako uyumbe kwa miaka 5. Mfano rahisi ni kinachoendelea Marekani kwa sasa dola imeyumba kwa miezi miwili(Ceteris paribus) recovery yake inakisiwa ni 2yrs +. Kama umefuatilia vizuri uchumi wetu ulianza kuporomoka kwa kasi miaka hiyo late 1970s and early 80s pamoja na missmanagement of the industries (kukosa wataalamu wa kutosha).

Naomba kujua kufunguliwa kwa viwanda vingi kulikua na kosa gani katika uchumi
 
IQ uwa inapimwa. Je Nyerere alikuwa na IQ ngapi?

Bin maryam
Unajua tuchukulie wewe ni mtaalamu wa uchumi na ukapewa kazi ya kuwaelezea wana kijiji kule vijijini kwamba nchi ina uhaba wa fedha na wewe ukaenda kuwaelezea wana kijiji wale kwa kutumia taalauma yako ni vyovyote vile watakuona mpumbafu,mjinga na hufai machoni kwao.
Maana utakwenda tofauti na matarajio ya majibu waliyokua wamejiandaa kuyapokea.
Ni dhahili wana kijiji wale wao watakua wametegemea majibu haya kutoka kwako nayo ni-
kwa vile nchi inakabiliwa na uhaba wa fedha basi serikali imejipanga na kuagizia mashine nyingi za kuchapisha fedha na mara tu mashine hizo zitakapofika tutachapisha fedha za kutosha.
IQ is an entity then so can be measured
 
We Mwanakijiji hii umeitoa wapi? Naona huyo dokta amekukoga kweli....
 
Tumeambiwa mara nyingi Kenya ni mfano wa nchi nzuri yenye uchumi mzuri na wenye nguvu. Tulichekwa kwa sababu tulikuwa na kiongozi kama Nyerere. Sasa ninapoangalia nchi zote zinazotuzunguka na ambazo hazikutawaliwa na Nyerere (obviously) I'm so proud to be born in a country where Nyerere was the leader!

kifo_cha_nyerere.jpg

Kumbe mamho yote siyo mambo ya uchumi yanayojenga Taifa!!

Asante Mwalimu na siasa zako za Ujamaa na Kujitegemea!!

Finally history has vindicated you!

I'm so proud and eternally grateful to be a Tanzanian. Yes I am.

Hamtaki?

Duuh, hicho kipande cha gazeti hakina jina la gazeti wala lini kimechapwa?

Kuna websites siku hizi zinakufanya utowe habari kama imetoka kwenye gazeti. Isiwe tunafungana kamba humu?
 
Mkamap: Heshima zangu kwako.

Utafiti mkubwa scietifcaly umegundua kuwa kupima nobility ya mwanadamu ..lazima kja na kipimo tofauti kidogo amabchao kinaweza kueleza vizuri ulichotaka kutueleza hapo. Badala ya kutumia IQ inatumika EI. IQ inabakia kuw akipimo cha kiakili zaidi..Intellect na IQ= emotiona intellegent inapima UTU..look here:Kuna mwenzako Ilikuondoa ubishi usio na msingi aliandika kitabu::::http://www.danielgoleman.info/blog/purchase/

Yaani Mtu anaweza kuwa na IQ Kubwa sana yaani akawa kipanga wa kutupwa.. But Maswala ya Kibinaadamu, Kiutu, Hekima, Kimaisha na Busara akawa sifuri.Yaani GPA yako kali na EI ndogo ..unaweza usiwe wamaana sana kwnye jamiii. Nyerere ana special EI

Emotional Intelligence: Why It Can Matter More Than IQ - 1996

kwa ufupi kabisa chukulia EI kama UTU/ukomavu na IQ kama ukali wa Kiakili...Itellect na soma hapa kwa kina. Utajua jinsi ya kumtofautisha Nyerere na watu wengine.



Ngoja na kuletea most important doc. Kukufanulia umhimu wa EI kwenye kuelezea watu kam nyerere na sio IQ pekee yake.. hold on!!!

Heshima mkuu.
Hiyo uliyoeleza ndio nilikua nahitaji kuileza lakini sikua na term hiyo na nzuri ya yote umenielewa na kunipa term iliyo sahihi asante kwa hilo .
 
Bin Maryam,

Siku mbili zinatosha kufanya uchumi wako uyumbe kwa miaka 5. Mfano rahisi ni kinachoendelea Marekani kwa sasa dola imeyumba kwa miezi miwili(Ceteris paribus) recovery yake inakisiwa ni 2yrs +. Kama umefuatilia vizuri uchumi wetu ulianza kuporomoka kwa kasi miaka hiyo late 1970s and early 80s pamoja na missmanagement of the industries (kukosa wataalamu wa kutosha).

Naomba kujua kufunguliwa kwa viwanda vingi kulikua na kosa gani katika uchumi

late 1970s na early 80s tulikuwa tayari tumeingia kwenye depression. Lakini recession ilianza zamani. Na kuna data zinaonyesha.

Mtaji mkubwa wa Tanzania ulitegemea masuala ya kilimo na pesa zilizotoka na kilimo hazikutumika kuendeleza kilimo kwa sehemu kubwa zilitumika katika kufungua sekta zingine (diversification) kama za viwanda ambazo hazikulipa. Ni sawa na ukiwa na duka na ukaamua kutumia pesa za duka kufungua biashara nyingine kama vile usafiri wa mabasi. Hivyo biashara ya mabasi ikikwama itakwamisha biashara ya duka vilevile kwa sababu ni mtaji uleule uliotumia. Kosa lilifanyika ni kuwa Tanzania ilikuwa bado katika ujima kuendesha viwanda.
 
Back
Top Bottom