Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

1. mabaharia waliolazimika kutoa rushwa ili wapate shule, pale wapi? Nasaco au? Yote hayo ni kwa sababu walitumwa na Nyerere, na pengine hata huko walipo leo ni rushwa hizo hizo alizowafundisha huyo mzee ndizo zimewafikisha huko.

Mkuu heshima mbele, ni mimi niliyetoa rushwa ili nisome shule ya meli, ambayo i;likuwa special kwa ajili ya Railways na Tacoshili, Mwalimu hakunituma, isipokuwa ilikuwa ni kawaida wakati wa utawala wake, na nilijifunza nikiwa shuleni Primary School plae Jamhuri, kabla ya kuingia darasani asubuhi, tulikuwa kwanza tunaenda pale kwenye Cameo Cinema, na kupewa tiketi za Cinema nzuri itakayo onyeshwa jioni ile, na kuziuza kwa bei ya kuruka, na baadaye pia wakati wa break time, that was my first leson kuhusu Rushwa, lakini sikutumwa na Mwalimu,

Nilipo sasa hivi hapana, sijafika kwa rushwa maana nilienda US nikajisomesha mwenyewe College, kutokana na hela nilizozi-save wakati wa ubaharia, Mwalimu alitufanyia mazuri as a nation, na kuna mabaya ambayo mpaka leo yanatusumbua na hatuji la kufanya zaidi ya kujaribu kufanya kejeli hapa forum, kumbe wananchi wanyonge wanaumia sana, kumbuka kwa muoga huenda kicheko na kejeli lakini sio kwa shujaaa!.


2.
Wakati Nyerere anahangaika kutafuta yanga na maharage ya funza ili wananchi wake pale Idodoma wasife njaa, mabaharia wetu hawakutaka udhia wa kunyimwa mafuta ya kuvinjari na mabenzi yao club Billicana.

Kila abiria hubeba mzigo wake, wananchi waliokufa njaa na kuliwa na simba under utawala wa Mwalimu, hawakuwa kutoka Dodoma peke yake, bali bongo nzima, Mwalimu hakupaswa kuwatafutia wananchi samaki, bali alitakiwa kuwafundisha kuvua samaki, besides ilibidi awatafutie chakula maana ni yeye ndiye aliyekuwa responsible in the first place,

Mimi sikuenda kulala baharini ili kurudi bongo niikomboe bongo nzima, hapana, kwanza niljikomboa binafsi kiuchumi, na baadaye familia yangu, then labda one day nitaweza kuwasaidia wengine wa taifa langu, so far bado sijafikia huo uwezo, lakini yes niliporudi bongo toka baharini, I had a good time kwa sababu I deserved it baada ya kazi ngumu ya baharini, hata pamoja na kunyimwa mafuta ya Mwalimu bado yalikuwepo mafuta kibao ya mwendo wa kuruka, hasa pale Agip karibu na Motel Agip, ambako mshikaji "Tall", na kina Minchum walikuwa wakiuuzia mafuta bei ya kuruka,

In the end kujaribu kuugeuza huu mjadala kuwa ni udikteta wa Mwalimu, naona ni very shallow thinking, kwa sababu that was not the ishu form the beginning the ishu, the ishu ilikuwa ni Kambona/Nyerere, Mwalimu alikuwa na uzuri wake na ubaya wake, so was Kambona, lakini haibadilishi ukweli kuwa taiufa letu limekwama kutokana na mapungufu yake Mwalimu, ambayo mpaka leo hatuna dawa yake, heshima mbele kwa wale wanaojaribu kutumia kila hila kuigeuza hii ishu kuwa tofauti na ilivyo, lakini some of us hatutakuwa moved hata siku moja, tuliuona ukweli then, tukauishi, tukau-survive, na here we go tunaendelea, tunaweza kuchagua kujifunza, kuelimishana, au kuishia kucheka tu maana ndioi kawaida yetu wabongo.

Huyu Nyerere alikuwa ni mshenzi kweli kweli kunyima watu raha.

Raha aliishia kujinyima mwenyewe, maana wabongo tuliendelea kuchacharika huku mkuu akihangaika kufuatilia restrictions zake, ambazo ukweli hazikuwa ziki-work, maan wananchi waligundua kila mbinu za kuzizunguka,

Jaribu kusoma the lesson learned kutoka kwenye kitendo cha US, na ile Alcohol Prohibit Act, ambayo ndio hasa chanzo cha utajiri wa kina Kennedy, then utagundua kuwa restrictions siku zote huwafundisha wananchi kuwa wahuni, ndio maana US waliapa kuwa hawatarudia tena mambo kama hayo, huku bongo ninajua kuwa mpaka leo bado kuna mambo ya vibali kule Investment kwa hiyo bado hatujajifunza, na here tuko kwenye kejeli!

Mungu Aibariki Nchi Yetu, na Amlaze Mahali Pema Peponi Mwalimu.
 
Mimi nina mtizamo tofauti,

1. Katika bara la Africa- kama ukisema Mwal. alikuwa dictator- je nani SSA utamwacha? Nafikiri alikuwa mkali- na hakupenda upinzani wa ndani (hata nje) in the 20 years of nation building haswa baada ya kushtuka mapinduzi ya 1964. Hii ni hali ya kawaida- remember Sadamu Hussein killed tens of 1000s Wakurdi- mara baada ya jaribio la kumwangusha kushidwa- kama kulipiza kisasi!

2. Mwalimu alikuwa na msimamo- na aliamini alichokisimamia. Mapungufu yalikuwa ya kibinadamu tu- alikufa akiwa mtu wa kawaida wala hajajilimbikizia mali kama vingozi wengine Afrika. Remember pia aling'atuka kwa hiari- 1985, na kama sii vita vya Kagera alipanga kung'atuka mapema 1980. Alisaidia sana ukombozi Southern Afrika! Tuchukue mema yake tujifunze na tusonge mbele. Hayo mapungufu yalikuwa ya kibinadamu!

Nasita kumwita diktator!
 
Hayo mapungufu yalikuwa ya kibinadamu!

Ni lazima uyajue yalikuwa ni yapi hayo, ili tuweze kujikwamua na kutoyarudia tena, kitu ambacho so far kinatusumbua sana, maana mpaka leo bado kuna vibali vya baadhi ya wawekezaji kupewa break za kutolipa kodi, I mean sasa tumejifunza nini maana hiki kibali kinatolewa na waziri kutokana na discretion yake binafsi, to me that is nonesense, hatujajifunza anything,

kibali kinatakiwa kitolewe, either na City Council ambako biashara hiyo ipo, au kamati ya bunge baada ya kuijadili ishu hiyo publicly na kusikiliza maoni ya wananchi kwanza,

Ukienda kule Investment, ndio kabisaa yaani kule watu hufanya watakavyo tu, hakuna wa kuwauliza maana wawekezaji ni muhimu sana wakiulizwa wataondoka, I mean yale yale tu sasa maendeleo yatatoka wapi? The ishu sio udikteta hapa, isipokuwa what to do ili tuondokane na ukoloni mambo leo, ambao ni lazima tujue tuliuanza lini na tumefikia nao wapi, kumbuka mkuu the first step sio ku-denie tatizo, bali ni kukubali kuwa tatizo lipo kwanza, otherwise tutaendelea kudanganyana tu!

Ndio maana nilikuwa ninamheshimu sana Ditopile, mpaka pale tu alipoua dereva mlalahoi wa dala dala, maana ninamkumbuka ile siku Mwalimu, alipotangaza kwenye kikao cha CCM Kizota, kuwa ataendelea kuwa mwenyekiti wa CCM, ingawa hatakuwa rais, as opposed na maneno aliyokuwa ameysasema mwenyewe mwanzoni, Ditopile akamwambia ukweli ulio wazi kuwa mbona unataka kutuchezea akli watu wazima? Maana kama umeamua kuacha uache vyote na ndivyo tulivyokuwa tukitegemea sasa mbona tena unabadili kauli Mwalimu? Mwalimu akajibu kuwa maswali hakuna tunaendelea, lakini Mwinyi akampa uwaziri, that was nice at least!
 
Jamani na hii mi email ya mitaperi ya Nig. nayo mnaihusianisha na Nyerere?

-Bila Nyerere uhuru tungeupata wapi?

Hili ni tusi! Yaani kama si Nyerere mpaka leo Tanzania tungekuwa chini ya wakoloni? Na huo uhuru ni uhuru gani unaouzungumzia hapa. Mimi naona uhuru kamili utapatikana TZ wakati CCM itakapoondolewa madarakani!
 
Nyerere alifanya mambo mengi sana mazuri tena kwa nia nzuri sana, hilo sikatai, lakini matokeo ya siasa zake ... mweeee, hata wanaomtetea wanajua nini kilitupata watanzania wakati wa ujamaa wake. lakini ukweli unabakia kwamba hakuwa fisadi na alikuwa na nia njema kwa kila jambo alilofanya bali kila kitu kili-back fire. Imebaki muungano tu nao siku yake ipo!
 
Utakapokuwa tayari kuyatafuta hayo mabaya ya Nyerere usisahau ya ...mabaharia waliolazimika kutoa rushwa ili wapate shule, pale wapi? Nasaco au? Yote hayo ni kwa sababu walitumwa na Nyerere, na pengine hata huko walipo leo ni rushwa hizo hizo alizowafundisha huyo mzee ndizo zimewafikisha huko.

Na usisahau 'colgate' za pale Namanga, na misururu ya foleni za mikate, kumbe ni za saruji! Wakati hizo colgate zinapatikana huko kwa majirani, wenzetu pale Turkana na Mandera walikuwa wakifa kwa njaa, huku wakubwa Nairobi wakinepa tu kwenye mabenzi. Wakati Nyerere anahangaika kutafuta yanga na maharage ya funza ili wananchi wake pale Idodoma wasife njaa, mabaharia wetu hawakutaka udhia wa kunyimwa mafuta ya kuvinjari na mabenzi yao club Billicana.
Huyu Nyerere alikuwa ni mshenzi kweli kweli kunyima watu raha.

Kalamu wewe acha tu,

Kila kitu kitawekwa hapa. Yaani huyu baba kalazimisha watu wazima eti wasome. Kanyima watu raha na udikiteta wake huu. Kaiba mabilioni hadi mtoto wake George anaomba msaada kwenye internet asaidiwe namna ya kuhamisha pesa!

Huyu Nyerere huyu, inabidi atolewe kabisa hata kwenye pesa maana historia yake ikifutika kabisaaaa ndio nchi yetu itaendelea.
 
Tufanye basi Leo kuanzia saa mbili ya usiku ya kwenu hapo yaani itakuwa ni Old School tupu na Slow Jamz. Kwa kuanzia tu kuna jamaa mmoja pale EastAfricanTube kashusha mambo ya Old School si kawaida. Check it out at Old School Jamz

Mazee Geeque,

Aminia aminia,

Uwe na weekend njema na once in a while utukumbuke wa kizazi kipya basi sio wazee tu kina Mwanakijiji.

Take care hadi jumapili ukirusha mahojiano ya Mkjj na Mark Bomani mazee.

Weekend njema everybody! Thanks
 
Kaiba mabilioni hadi mtoto wake George anaomba msaada kwenye internet asaidiwe namna ya kuhamisha pesa!

Mwalimu Nyerere, hana mtoto anayeitwa George, wakuu we can chose either kuelimishana kwa faida ya umma, au kuendelea kupotoshana, unajua the more we stay kwenye hii forum ndivyo tunavyozidi kujifunza tabia na rangi za watu,

I mean kuifuta topic ya Memba, na kuhamisha topic ya Kambona, na sasa hiii topic, it might look to be very intelligent kwa wale wanaohusika, ila kwa sisi tulioona mengi ya dunia ni childish games ambazo haziwezi ku-aaccomplish anything worthy kwa elimu ya taifa ila kuendelea kuwafanya wale wanaohusika kujisikia wana akili sana, kama vile viongozi wetu kina Karamagi,

As long as we stay na hizi mind tutaendelea tu kuchezewa na viongozi mpaka mwisho wa dunia, yaani ninashindwa kabisa kuamini kinachoendelea hapa na hasa wanaohusika, tunawatakia mafanikio mema ila tu kuna ambao tulikataa kulala usinginzi au kulalishwa na watu wengine, tulikataa enzi za Mwalimu, hatuta waive saa hizi wakati kumekucha,

Mwalimu hana mtoto anayeitwa George, never! I spend a lot of time na watoto wa Mwalimu, Joseph, na Kizurira, from Andrew, Magige, Anna, Rose, Makongoro, Madaraka, Matare, Milton, PC, Mode, I mean kuna hoja nyingi tu zinaweza kuwekwa hapa kulingana na the ishu, lakini kulazimsiha tu mpaka this kind of lies ni very low, kweli wabongo tuna safari ndefu sana!

Halafu lets say ni mtoto wake kweli, sasa vipi yeye ni kilema?
 
Mwalimu Nyerere hakuwa Mungu, alikuwa ni binadamu kama sisi hivyo alikuwa na mapungufu yake.

Umoja wetu nimatokeo ya juhudi za Mwalimu katika kuhakikisha tunakuwa na lugha ya Taifa ili kupunguza au kuondoa kabisa ukabila, hili limefanikiwa sana.

Sera za kuhakikisha uchumi wa Tanzania unakuwa mikononi mwa Watanzania na kuhakikisha nafasi za juu katika mashirika na makampuni mbali mbali ya Watanzania zinashikwa na Watanzania, hili Mwalimu alifanikiwa sana.

Ili kuhakikisha nafasi za juu katika makampuni na mashirika hayo Mwalimu aliona kuna umuhimu mkubwa wa kuhakikisha elimu kuanzia shule za msingi hadi chuo kikuu na vyuo vingine inakuwa bure ili kila Mtanzania bila kujali rangi yake, familia aliyotoka au dini yake awe na nafasi ya kupata elimu ya juu, hili pia Mwalimu alifanikiwa sana.

Sera za vijiji vya ujamaa ili kuharakisha maendeleo ya haraka kwa wananchi kwa kuwapatia huduma muhimu kama maji, umeme, shule n.k. zilikuwa ni nzuri sana ili utekelezaji wake ndio ulikuwa hafifu mafanikio hayakuwa makubwa kama ilivyotegemewa.

Miaka ile ya Mawalimu mahospitali yetu yalikuwa na hadhi ya hospitali siyo kama ilivyo sasa.Kulikuwa na madawa ya kutosha na vifaa vya kutosha na pia vitanda vya kutosha hakuna aliyekuwa analala chini, pamoja na kuwa mapato ya kodi yalikuwa ni madogo mno ukilinganisha na miaka ya karibuni na kulikuwa hakuna mapato yoyote ta kutokana na dhahabu au tanzanite.

Mwalimu pia alikutana na misukosuko kama ongezeko la bei ya mafuta duniani mwaka 1973 hili liliathiri sana Tanzania kwa sababu asilimia kubwa ya mapato ya forex ilibidi itumike kununua mafuta badala ya vifaa vingine muhimu vya kuleta maendeleo kama matrekta n.k.

Njaa iliyotukumba mwaka 1975 na hatimaye kuwa na kampeni ya 'kilimo cha kufa na kupona' nayo iliathiri sana akiba ya forex maana asilimia kubwa ilibidi ielekezwe kwenye ununuzi wa chakula toka nje.

Vita vya nduli mwaka 1978 navyo vilitumia asilimia kubwa sana ya mapato ya fedha za kigeni katika kununua silaha za kupambana na nduli.

Mwalimu hakuwa fisadi, hakuwa mpokea rushwa, hakuwa na uroho wa kujilimbikizia mali kama viongozi wa hii miaka ya karibuni akina Mkapa na wenzie. Mwalimu aliishi maisha ya kawaida kabisa.

Siku zote Mwalimu aliweka mbele maslahi ya Tanzania na Watanzania. Kwa mfano aliwahi kushinikizwa na IMF ni WB ili kupata mkopo toka WB ili kuisaidia Tanzani kutokana na hali mbaya iliyosababishwa na matatizo mbali mbali, alitakiwa ashushe thamani ya shilingi ili kupata mkopo huo. Mwalimu baada ya kutafakari akaona kuwa kufanya hivyo ni kuwaongezea gharama za maisha Watanzania hivyo hakukubali kushusha thamani ya shilingi na hatimaye kumfukuza kazi Waziri wa fedha wa wakati huo Edwin Mtei ambaye naye alikuwa anaunga mkono kushushwa thamani ya shilingi. Waliofuata baada ya Mwalimu walishusha thamani ya shilingi, lakini hadi hii leo ukiwauliza je kushusha kwa thamani ya shilingi kuliwasaidia vipi Watanzania? wanajiumauma tu bila kuwa na jibu linaloeleweka.

Kwa kumalizia nawaombeni mumwache kumsema vibaya Mwalimu ili apate mapumziko ya amani ya milele, alikuwa na mapungufu yake mengi tu, lakini mazuri aliyoyafanya kwa Tanzania siku zote yatashinda mabaya.

Kamwe hatuwezi kumlinganisha Mwalimu na fisadi Mkapa na hawa wasanii mafisadi wengine wasiowajali Watanzania bali matumbo yao na ya familia zao. Mwalimu alikuwa na mapenzi ya kweli na Tanzania na Watanzania na siku zote aliweka mbele maslahi ya Watanzania.
 
1. Those who make things happen
2. Those who complain when things happen
3. Those who watch things happen
Sijui watanzania wengi tunaangukia wapi?

Watanzania bado hatujaondoka kwenye siasa za kijamaa, viongozi wetu wanahubiri siasa nyingine, raia wengi bado wanaishi kijamaa.
Mwalimu alikuwa na mapungufu yake na alikosea kama kiongozi sasa imefikia wakati Watanzania tukayaweka yote nyuma na kusonga mbele kuendeleza Taifa, mambo ya kukaa na kusema tusingeenda vita ya Kagera or isingekuwa sera hizi na zile za Mwl tungekuwa mbali kimaendeleo.
Imeshapita miaka 22 tangu ang'atuke nadhani sasa itakuwa aibu kuendelea kulalamika wakati hatufanyi chochote kurekebisha makosa yake, muda umefika mimi, wewe na yule tupiganie taifa letu.
 
JK naye ni binadamu ana mapungufu yake, kwa nini mnamzodoa kila kukicha?. mwacheni atulie ikulu afanye vitu vyake kwani umesikia wapi kwamba JK hana uchungu na tanzania?.
 
JK naye ni binadamu ana mapungufu yake, kwa nini mnamzodoa kila kukicha?. mwacheni atulie ikulu afanye vitu vyake kwani umesikia wapi kwamba JK hana uchungu na tanzania?.

Lipi alilofanikiwa kokote alikopita katika mawizara na sasa urais? IPTL na Buzwagi tunaweza kumbebesha yeye kwa kuwa iliposainiwa IPTL alikuwa pale nishati na iliposainiwa Buzwagi alikuwa Rais na alishawaahidi Watanzania kwamba hatasaini mkataba wowote wa madini mpaka mikataba ya nyuma itakapofanyiwa marekebisho. Kwa hiyo kama angekuwa makini katika utendaji wake na ahadi zake basi leo hii kusingekuwa na IPTL na Buzwagi. Kwa sababu hizo basi, inabidi tumzodoe tu.
 
Kwa kumalizia nawaombeni mumwache kumsema vibaya Mwalimu ili apate mapumziko ya amani ya milele, alikuwa na mapungufu yake mengi tu, lakini mazuri aliyoyafanya kwa Tanzania siku zote yatashinda mabaya.

Mkuu Bubu,

Thank you kwani article yako ni educative na fair enough, kuhusiana na ishu at hand! Na sina objection kabisa na hoja zako maana ni very clear na to the point! Ingawa ninatka kusema tu kuwa hatumsemi vibaya Mwalimu, mkuu Martin Luther alipojitoa kwenye dini ya Catholic, aliyasema wazi yiliyomtoa kule, na inaaminika kwamba moja kati ya idea zake za revolution katika dini mpya aliyoianzisha, ndio kilikuwa kiini haswa cha kuzaliwa kwa Capitalism, lakini kwanza aliyaweka bayana yale aliyoyaona kuwa ni mapungufu ya kanisa la Catholic,

Kuyazungumza mapungufu ya Mwalimu, kwa ni aya kujirekebisha sio kumsema vibaya Mwalimu, wewe kuna mapungufu umeyasema hapo kwenye article yako sio kweli kwamba umemsema vibaya Mwalimu, umeyasema mapungufu ambayo tukiyakalia kitako as a nation tunaweza kujisaidia na kutoyarudia tena na ku-move forward, lakini tatizo ni pale tunapokataa, kwa mfano Mwalimu siku zote alipenda sana kuamua ishu za kisheria kwenye vikao vya CCM, I mean that was wrong na ndio mana sasa kina Kingunge bado wanajaribu kutaka ishu ya mafisadi iishie kwenye vikao vya CCM wanaposema wanataka suluhu na wapinzani, sasa hivi kweli ni kumsema vibaya Mwalimu?

Kuna tofauti ya kumsema vibaya Mwalimu, na kujifunza mapungufu ya Mwalimu kwa faida ya taifa letu, kujitawala miaka 22 baada ya Mwalimu kuondoka, haibadilishi the fact kuwa mpaka leo bado kuna trace za Mwalimu kila kona, kwa mfano Mkapa alimpa urais Muuungwana, exactly kama yeye alivyopewa na Mwalimu, sasa we need to address ishu kama hizi ili naye Muungwana asizirudie, maana Muungwana naye akifanya kama Mkapa basi taifa letu halitakuja kujinasua na haya matatizo sugu!
 
Kwa kumalizia nawaombeni mumwache kumsema vibaya Mwalimu ili apate mapumziko ya amani ya milele, alikuwa na mapungufu yake mengi tu, lakini mazuri aliyoyafanya kwa Tanzania siku zote yatashinda mabaya.

Mkuu Bubu,

Thank you kwani article yako ni educative na fair enough, kuhusiana na ishu at hand! Na sina objection kabisa na hoja zako maana ni very clear na to the point! Ingawa ninatka kusema tu kuwa hatumsemi vibaya Mwalimu, mkuu Martin Luther alipojitoa kwenye dini ya Catholic, aliyasema wazi yiliyomtoa kule, na inaaminika kwamba moja kati ya idea zake za revolution katika dini mpya aliyoianzisha, ndio kilikuwa kiini haswa cha kuzaliwa kwa Capitalism, lakini kwanza aliyaweka bayana yale aliyoyaona kuwa ni mapungufu ya kanisa la Catholic,

Kuyazungumza mapungufu ya Mwalimu, kwa ni aya kujirekebisha sio kumsema vibaya Mwalimu, wewe kuna mapungufu umeyasema hapo kwenye article yako sio kweli kwamba umemsema vibaya Mwalimu, umeyasema mapungufu ambayo tukiyakalia kitako as a nation tunaweza kujisaidia na kutoyarudia tena na ku-move forward, lakini tatizo ni pale tunapokataa, kwa mfano Mwalimu siku zote alipenda sana kuamua ishu za kisheria kwenye vikao vya CCM, I mean that was wrong na ndio mana sasa kina Kingunge bado wanajaribu kutaka ishu ya mafisadi iishie kwenye vikao vya CCM wanaposema wanataka suluhu na wapinzani, sasa hivi kweli ni kumsema vibaya Mwalimu?

Kuna tofauti ya kumsema vibaya Mwalimu, na kujifunza mapungufu ya Mwalimu kwa faida ya taifa letu, kujitawala miaka 22 baada ya Mwalimu kuondoka, haibadilishi the fact kuwa mpaka leo bado kuna trace za Mwalimu kila kona, kwa mfano Mkapa alimpa urais Muuungwana, exactly kama yeye alivyopewa na Mwalimu, sasa we need to address ishu kama hizi ili naye Muungwana asizirudie, maana Muungwana naye akifanya kama Mkapa basi taifa letu halitakuja kujinasua na haya matatizo sugu!

Sasa hapa sisi kama wananchi ndio tunatakiwa kukataa kuchaguliwa mtu na kikundi cha watu wachache, tutakataa vipi> Sasa ndio nguvu ya boksi la kura inapotumika.
 
nguvu ya boksi la kura inapotumika.

Nguvu ya box mkuu ni vigumu kutumiwa kwenye uwanja ambao either sio tambarare, au fair maana as long as tume ya uchaguzi iko mikononi mwa serikali ya CCM, na sio independent, tutaendelea kupata majibu yale yale tu,

Taifa letu kwa kushinikizwa na sisi wananchi tusipochukua hatua mathubuti za kulivalia njuga suala la elimu ya kura, pia itakuwa ni kazi ya bure tu maana CCM itashinda tu maana kuna wananchi wengi ambao mpaka leo hawajui kuwa Mwalimu hayupo tena,

Sasa umefika wakati serikali inahitaji kuvipunguza vyama vya siasa nchini ili tuwe na vichache ambavyo vitakuwa financially managable na serikali lili kuvipa nguvu za kuweza kujitosheleza kipesa, na kwa sababu vitakuwa vichache, basi ruzuku inayotumika sasa itaongezeka kwa vyama hivi na kuweza kutoa upinzani wa nguvu na wa kweli kwa CCM, hivyo kuibadili kabisa sura ya upinzani nchini,

Kuna mengi sana ya kuyaangalia kwa kupitia mapungufu ya Mwalimu, badala ya kujaribu kuuuua mjadala kwa visingizio vingi ambavyo kwa kweli havina msingi kabiisaa!
 
1. Hivi nani anakumbuka around mwaka 1979/80 nikiwa shule ya msingi kuna wakati mgambo, polisi na wanajeshi walikuwa wanapita Dar kukusanya nakala za gazeti la TIME(or was it Newsweek?) ambalo lilidaiwa kuwa limemsema vibaya Rais Nyerere, waliokutwa nalo wanajua kilichowapata... Hivi nini kilikuwa kimeandikwa mule?

2. Nani anakumbuka enzi za mashushushu kila kona, hata nyumbani watoto na wazazi mnaogopana, ukiisema vibaya serikali au chama au viongozi shauri zako...

3. Nani anakumbuka yaliyowahi kumsibu Abel Mwanga baada ya kutokuelewana fulani na Rais Nyerere akapigwa benchi kiaina?
Nafahamiana na baadhi ya wanawe(actually wa Joseph waliokuwa wanaishi kwake pale) basi tulishuhudia mtu mzima Mwanga alivyojigaragaza mbele ya Mwalimu usingeamini... he was actually groveling at his feet, a few days later kapewa ulaji.

4. Nani anakumbuka mtindo wa kulea uzembe na ubadhirifu ulianzia na utawala wa Mwalimu, mtu akiboronga sehemu moja anahamishiwa nyingine, ndipo utamaduni huu ulipoanzia, sijui ni kwa kisingizio cha "tumepigania uhuru pamoja tumetoka mbali au...". Sababu ya wasomi wachache sio issue maana wakishaharibu cha ajabu wanapatikana wasomi wa kwenda kuokoa jahazi!

5. Nani anakumbuka miezi 18 ya kufunga mkanda baada ya vita vya Kagera ilivyogeuka kuwa miaka 18. Tuliambiwa tunaisaidia Uganda kwanza hivyo mchele, sukari, unga, siagi, mabati yaani almost kila kitu kinapelekwa "mstari wa mbele", tukaitikia hewalla nani abishe...ndio tukaanzana na mambo ya foleni na kula kwa kaya, ila kwa vigogo wa chama, jeshi na serikali aaa kupeta mtindo mmoja...Personally shafukuza sana magari ya ugawaji kama alivyosema mwana JF mmoja hata hujui kuna nini we umeona gari la ugawaji kimbilia tu.

6. Kukatazwa kuendesha gari baada ya saa 8 jumapili mbona cha mtoto! Kwanza kununua gari lazima upate permit fulani hivi nakumbuka mdingi wangu ilikuwa mbinde kukubaliwa na hata baada ya kumkubalia wakamwibulia issue nyingine hakuwa amekwenda JKT(aliunganisha kusoma zaidi wakati sheria ya JKT inapitishwa) hivyo wakaja wakambeba mzobemzobe wakampeleka JKT kutoka hapo UD alipokuwa anafundisha! Yaani mdingi anarudi nyumbani kasindikizwa akafungasha vijinguo vyake huyo kabebwa kwenye Landrover kupelekwa JKT, yaani just imagine na bongo hakuna cha welfare wala nini, in short ujumbe ulikuwa: mkeo na watoto watajiju lakini wewe bwana unajifanya msomi lazima tukakusurubu JKT...

7. Nani anakumbuka Nyerere alivyokuwa mwepesi kuwapachika wasifu marais wengine waliokorofishana, mfano Jomo Kenyatta "Nyang'au", "Nduli" Idi Amin, hivi Banda alimwitaje? Nani anakumbuka. Alikuwa na viji-humour vyake mwenyewe!

Ila uongo mbaya tulivyokuwa tunaimbishwa na kukaririshwa shuleni, mbona tulikuwa tunazionea huruma nchi zingine hususan majirani zetu kwa kukosa Rais kama Nyerere...nchi zenye mabepari, wanyonyaji, mabeberu...

8. Nani anakumbuka au anafahamu yaliyomfika Ben Kiko wa RTD, alivyosema "ingawa Dodoma ni mji mkuu, unaonekana kama mji mkuu kuu"? Enzi hizo wakulu fulani fulani ndio wanafisadika na mradi wa makao makuu.
 
Umaskini chini ya Mwalimu ulisababishwa na kutegemea mazao ya biashara tu kama ndio chanzo cha mapato yetu ya kigeni. Wakati wa Mwalimu pia ukusanyaji wa kodi ulikuwa ni mdogo sana ukilinganisha na sasa.

..umasikini chini ya mwalimu ulitokana na policies zilizo build white elephants nyingi,ilihali bidhaa zilizozalishwa hazikuwa zitumike nchini na wala hazikufanyiwa marketing ya kutosha hata huko nje!

..kutokana na sera zetu za ujamaa,tuliingizwa mikenge mingi na wazungu,nia ikiwa ni kuua uchumi wetu,baada ya kuwa na miradi mikubwa tusiyoihitaji,iliyotulundikia madeni!.hii imeshajadiliwa kwenye post fulani huko nyuma!

Sasa hivi tuna rasilimali zetu kama dhahabu, tanzanite, mbao, gesi n.k. pamoja na kuwa mikataba iliyosainiwa haina maslahi kwa Tanzania, imeongeza kwa kiasi pato la fedha za kigeni, lakini wananchi hawaoni tofauti yeyote katika maisha yao ya kila siku kutokana na ongezeko hili la pato la fedha za kigeni na ongezeko kubwa la makusanyo ya kodi kupitia TRA.

..moja ya sababu ni kuongezeka kwa matumizi ya serikali!serikali ya sasa[toka enzi ya mkapa!]si masikini!ina fedha!na ndio hizo!

..hayo mapato ya dhahabu et al ni cha mtoto,kwanza ni aibu tupu!

..pato kubwa bado linatoka kwenye sekta ya kilimo na utalii!

Inakuwaje pamoja na kuongezeka pato letu la fedha za kigeni na makusanyo makubwa ya kodi, bado wananchi hawaoni kupanda kwa ubora wa maisha ukilinganisha na wakati Mwalimu Nyerere (RIP) alipokuwa madarakani? inakuwaje wengine wanaona ubora huo wa maisha unazidi kushuka?

..tatizo liko kwenye distribution ya income!kuna baadhi ya miradi au mipango ambayo hupeleka manufaa moja kwa moja kwa wananchi.mfano,hospitali na mazalio yake zilizo na gharama ndogo.elimu bora iliyo na gharama ndogo.usafiri wa umma ulio na ufanisi na wa kutegemea.nafasi za kazi zenye kukuza ujuzi na kuongeza kipato.maji,umeme,simu,na huduma kama hizo za bei nafuu!

..napoongelea bei nafuu au gharama ndogo,namaanisha ukilinganisha na kipato cha watanzania walio wengi!siongelei wale wenye uwezo wa kujaza gas kwa magari yao wiki nzima bila kutetereka kimapato!

..kama tunakumbuka enzi ya mwalimu ,shule na hospitali zilikuwa bure. usafiri hasa mijini ulikuwa mzuri,maji na umeme huduma yake ilikuwa nzuri!sasa,haya kwa sasa ni kaazi kwelikweli!

..kwa ufupi,kipato cha watu wengi hakimudu gharama za maisha ndio maana ubora wa maisha umeshuka kwa walio wengi!halafu,hata huduma za umma zimeshuka ubora!
 
Vipi....kwani nimeongopa? Jamaa anampenda Nyerere kikweli kweli. Hivi umewahi kumsikia anavyoongeaga kwenye podomatic? Yaani anasound kama Nyerere...sitashangaa na yeye kukata mitaa ya huko Detroit na kifimbo chake na kibaragashia. Hehehehehe....

Ngoja niwape stori. Kuna siku moja hivi...imekuwa kitambo kidogo. Jamaa alikuwa na podcast ya Nyerere akiongea na Watanzania....mimi nikaharakisha kusikiliza nikitegemea kumsikia Nyerere mwenyewe....sasa guess what? You guessed it....it was yours truly!! Yaani alimpatia kishenzi utadhani sijui nini....sikuwa na mbavu tena

..yawezekana ni mwanae! si unajua tena,nyerere kasingiziwa mengi!kuna mtu aliwahi kudai kuwa freeman ni mtoto wa nyerere!

..dunia kubwa hii!
 
Jamani na hii mi email ya mitaperi ya Nig. nayo mnaihusianisha na Nyerere?

Hakuwa malaika huyu mzee, kuna aliyokosea mengi, lakini mazuri aliyo yafanya kwangu mimi naona yanazidi mabaya aliyo yatenda.

-Bila Nyerere uhuru tungeupata wapi? Kumbuka alikubali kuacha kazi yake ya mshahara, akaishi kwa misaada ili atupatie uhuru wetu.
-Elimu ya bure kwetu sie walala hoi tungeipata wapi?
-Madini yetu tunayo yalilia wezi hawa wanayo kimbilia yauza na kugawana kama njugu si yangeisha isha?
-Bila Nyerere umoja na undugu wa kitanzania (ambao huwa hatubaguani kwa misingi ya dini na ukabila) alio tujengea tungeupata wapi?

Udikiteta wake ulikuwa wa maana sana ili nchi iweze kuungana, ni kama sasa hivi ili tuendelee tunamuhitaji dikiteta mwingine ambaye atatupilia mbali maamuzi ya kijinga yaliyo fanywa na walafi kina Mkapa/Yona/karama/ na wengineo ili tuanze upya!

Tunahitaji dikteta ambaye ataweza jisimamia katika maamuzi yake siyo hawa tunao waona wajasiriamali ikulu, na vascodagama kwa kodi za walala hoi!

Tunahitaji raisi amabye atakuwa na guts za kusema No, palipo na No! siyo blabla.. bila utendaji!

Misingi mizuri aliyo tuwekea ya kusomesha vijana wenye uwezo ili waje walitumikie Taifa yote tumeipiga chini, sasa hivi elimu ni kwa wateule waliobarikiwa kuwa na njuruku, kazi nzuri zinazo lipa ni kwa majina ( rejea BOT)

Tunaona misingi hiyo inavo zidi kufukiwa tunapoletewa sheria za ajira za serikalini kuwa za teuzi?? siyo za ushindani wa qualifications!

Am out of this, leave Nyerere alone, Mwacheni apumzike kwa Amani, kiumbe wa Mungu!
Mazuri mengi mno katufanyia MUNGU MPUMZISHE KWA AMANI.

Athari kubwa aliyoileta mwalimu ni colonization of our minds.Kasumba hii ilianza tangu darasa la kwanza hadi Chuo Kikuu tulipokuwa tukiiimba na kumtukuza Dikteta wetu kana kwamba amekuwa ndiye Mungu wetu.Mashuleni,vyuoni,majeshini na katika jamii nzima ilikuwa .."Nyerere kweli...kweli kweli Nyerere..."
Kasumba hiyo hadi leo hii imo ndani ya mamilioni ya vichwa vya Watanzania.Ndiyo maana ndugu Rwabugiri anaamini kuwa bila Nyerere hadi leo hii tungekuwa ni Tanganyika Territory tukiwa chini ya Mwingereza kwa niaba ya UN.Si kosa lake lakini minds zake zimejengeka kwa muda wa miaka mingi na hivyo anadhani kuwa yale yaliyokuwa yakilishwa ndani ya kichwa chake ni sahihi.Na wengi wana hiyo ninayoiita colonization of minds.Mimi nasema si Nyerere pekee aliyeleta uhuru kwani kulikuwapo na watu chungu nzima waliokuwa wameamua kudai uhuru...wakiwemo kina Sykes,Oscar Kambona(Mungu ailaze mahala pema peponi shujaa huyu),Kasela Bantu,Kina Migeyo huko Bukoba,Tewa saidi Tewa,na list ni kubwa mno ya watu waliopigania uhuru.Si sahihi kwa hiyo kusema ni Nyerere pekee aliyeleta uhuru.Hilo ni kosa na haliwatendei haki wale wote walioshiriki katika kuleta uhuru wa nchi hii.
Elimu ya bure ni sera tu.Ilijadiliwa na kukubalika na kisha ikatelelezwa.Ingeweza kufanywa na yeyote yule kwani kuna nchi nyingi duniani zenye sera hiyo.
Suala la umoja na undugu lilikuwapo hata kabla ya uhuru.Makabila yalikuwapo kama hivi leo lakini hayakuwa na uhasama.Lugha ya Kiswahili ilikuwa imeenea hadi Karagwe kwa Rumanyika na hata kuvuka mipaka ya nchi hadi Kongo n.k.Ni kwa sababu ya umoja huo uliokuwapo tangu awali na amani iliyokuwapo iliyochochea kupatikana kwa uhuru.
Ukiona mtu anashabikia udikteta hayakumkuta madhara ya kuhamishwa kwa nguvu kutoka nyumbani alikozaliwa na kukulia na kubwagwa porini bila hiari yake.Hapa tunawakumbuka kina Mazegenuka walioteswa na kufia mikononi mwa mashushushu wa usalama wa raia na kusababisha Ally Hassan Mwinyi kuachia ngazi ya uwaziri wa mambo ya ndani.Tunwakumbuka wale wote walionyanyaswa kwa kuibiwa nyumba zao wakiambiwa kuwa zimesajiliwa na kuwa mali ya umma wakati wenyewe ni sehemu ya huo umma.Na bila kusahau mashamba makubwa,mabenki na mali nyinginezo zilizoporwa kwa kutumia udikteta.Tunakumbuka wabunge walivyotishwa na kuburuzwa hadi kupitisha sheria ya kodi ya mapato kwa wafanyakazi ambao hata mishahara yao haikuwa ikitosha kuendeshea maisha.Udikteta ni mbaya....mbaya sana maana unaweza kuua watu wa maana kama Kassim Hanga ,Othman Shariff na wengineo bila kufikishwa mahakamani.Mtu aliyefumbia macho madhambi haya au kushiriki kwa namna yoyote ile si kiongozi mwadilifu.
Ni kweli tuamhitaji kiongozi anayeweza kusema NO kwa masuala yanayoipeleka nchi pabaya lakini kiongozi anayesema NO kwa IMF na akasema hawezi kugeuka jiwe na kuwafanya raia watembee uchi naye ni kingozi wa maana?Muulize mzee Mtei yupo hai hadi leo.Inaelekea vijana wa leo wamesahau adha ya Nyerere waliyoipata wazazi wao enzi zile za bidhaa adimu kwa sababu tu Mwalimu alisema NO.
Nchi hii ilikuwa na wala rushwa tangu enzi ya Nyerere na walikuwa wakifilisi mashirika ya umma kisha wakapewa idara nyingine ili waendelee kutafuna.Mimi sina haja na kiongozi aliyetupigisha mark time kwa miaka 25 wakati wenzetu walikuwa wakikimbia na kuujenga uchumi wao kama Kenya.
Kwa sasa tunaye Rais mwadilifu ambaye kachaguliwa kihalali ...(Si ile kura ya doa jeusi upande mmoja na Nyerere upande wa pili)na na anahangaika kurekebisha athari za Nyerere,,yaani anajaribu kutufanya tuondokane na ile kitu colonized minds. Tunajitahidi ku-decolonize.J4 ni sehemu mojawapo ambayo inajitahidi kukutanisha watu na kujadili mambo kwa uwazi kama hivi.Haya tujadiliane.
 
Back
Top Bottom