Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Haya maneno Mzee Es..
Mawazo yasipingwe isipokuwa matusi sote tupoo!

Haya vijana akina Mswahili leteni mapungufu ya Nyerere tupo tunayasubiri...hoja kwa hoja!..Lakini usije niuliza kama alikuwa anapiga mswaki!... hiyo itakuwa kesi ya wizi wa chaki.
 
who unachekesha ,mwalimu hakupata kuwa na upendeleo wala kuwaonea waislamu,mnasahau historia,mwalimu aliwanyanganya wakatoliki,wakristo wengine na wahindi shule ili waislamu nao wasome ,leo mnakosa shukrani,serikali haikuwa na shule za kutosha,mwalimu angeweza hata kutengwa na kanisa kwa kulirudisha nyuma,kumbukeni utamaduni wa wakristo ulikuwa kuhakikisha kila kanisa linajengwa na shule ,hospitali na chekechea,,baada ya mwalimu kutaifisha shule na hospitali zao waligoma kujenga nyingine hadi mzee mwinyi alipokuja kuwaomba wasamehe.

msisahau kati ya hospitali nne za rufaa nchi hii ,tatu kutoa mohimbili ni za wakristu waliojenga,bugando [wakatoliki],kcmc[walutheri] nk hospitali hizi zingekua mbali sana kama si kutaifishwa ili tu waislamu wasikwezwe kuzitumia,nazo pia mzee mwinyi ndie alizirudisha,.

kwa hiyo hili la udini siliubali,,nyerere alitaka tofauti kati ya wananchi isiwe kubwa ,kuna msemo wake "inabidi wengine msimame kimaendeleo ili muwasubiri wengine.." kama si nyerere kuna jamii nchi hii zingebakia manamba,wakati tunapata uhuru tayari mikoa kama kilimanjaro na wakristo walikua mbali.

tena kwa hili wala tusilaumu wakoloni ,,tulaumu utamaduni wa walioleta dini zetu wengine walifundisha elimu ya dini ,kutibu na elimu wakati wengine walileta dini tu,tiba zikabaki za waganga na elimu ikabakia ya dini tu...
tuwe na shukrani,,,,
 
Katika kitabu chake cha "The life and Times of Abdulwahid Sykes (1924-1968): The untold story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika" mwandishi historian Mohamed Said anaangalia mchango wa waislam katika harakati za kuleta uhuru wa Tanganyika. Je ni kweli waislam ndio walioanzisha TAA na TANU? Je ni kweli Mwalimu Nyerere alinyakua TANU toka kwa waislam na kukifanya kuwa chombo cha kanisa? Je Kanisa Katoliki lilisaidia vipi kuwakandamiza waislam? Nani alisaidia sana kuleta uhuru wa Tanganyika kati ya Mwalimu Nyerere na Abdul Sykes? Je waislam walifanya kosa gani ambalo linawafanya waendelee kukandamizwa mpaka leo? Sikiliza.


www.RadioButiama.com
 
Radio Butiama,

Ama kweli huu ni ukumbi ambao wengi hawapendi kuingia kwa sababu nyingi za kimsingi. Na hakuna upinzani mkubwa ktk maelezo ya Mohammed Said isipokuwa upeo wa swala zima ndio umepindishwa kutokana na pale mwandishi kasimama.
Nitaeleza maelezo yangu kutokana na jinsi nilivyoelewa mimi hiki kitabu na hasa historia nzima ya UHURU wetu.
Kwanza kabisa lazima nikubali kuwa Mohaamed said kafanya kazi nzuri sana ktk kuiweka historia sawa lakini kosa kubwa ambalo limejitokeza ni pale alipowatolea mfano watu kwa rangi zao (DINI)... badala ya kuwachukulia kama Watanganyika.
Kwa nini nasema hivi:-
Kwanza ukitazama uongozi mzima wa TAA hadi TANU ulikuwa ni wakazi wa PWANI... Obvious hapa utapata waislaam wengi. Na nafasi hizo hazichaguliwi na wanachama ama viongozi wa Tanganyika nzima. Kwa mfano baraza la mawaziri wa JK hawachaguliwi na raiaama wanachama bali rais mwenyewe.
Ndugu Mohammed Said hakueleza uongozi wa TAA ama TANU mikoani ulikuwa vipi... na nakuhakikishia kila mkoa kulikuwa na aidha wakristu wengi ama waislaam wengi kutokana na wakazi wake. Lakini kilichojitokeza zaidi ni kwamba kila mkoa ulikuwa na watu wenye kabila lkubwa la hapo kuliko makabila mengine. Yaani Kilimanjaro kulikuwa na wanachama wengi wa TAA na TANU wachagga na Tabora wengi walikuwa Wanyamwezi. Je, hapa tunaweza kusema kulikuwa na Ukabila?... Sidhani!
Swala la Kupata UHURU lilikuwa very complicated toka Ukoloni na waislaam wanajua kwamba haingewezekana kuupata Uhuru wetu bila kuwatumia Wakristu. It was the fact, na Nyerere alipolia baada ya kushutumiwa kwa UDINI alikuwa akishindwa kujieleza vizuri tatizo lililopo bila kuingiza dini. Reality ni kwamba wakristu wengi ktk madaraka UHURU ulikuwa rahisi kutokana na sheria za Muingereza ambao waliwafunga Waislaam.
Muingereza alijua kuwa waislaam wanatafuta UHURU na waislaam ni karibisho la Ukommunist - kiuchumi. Sasa hapa utamwambia nini muislaam apate kukuelewa kuwa swala kubwa la nchi ni Uhuru wetu sio tofauti zetu ktk dini hali unapolianika swala zima juani (kwa Muingereza) lazima lionekane kuwa ni mahindi (Wakristu) ambao sio Wakommunist - Uhusiano wa kiuchumi na Wazungu.
Baada ya Uhuru, watu wengi wamejenga hoja ya Waislaam kutupwa nje na Nyerere lakini ukitazama kwa makini utagundua kuwa Nyerere alikuwa MBINAFSI. Mpenda madaraka kwa sababu alikuwa na dream yake. Wote ambao walikuwa tishio ktk azma yake (vision) waliondolewa bila kujali dini zao ama makabila.
UHURU kwa waafrika ulitafsirika kama kubadilisha watawala. Viongozi wengi wa Kiafrika walitegemea kuwa tukipata UHURU wetu basi wao watarithi nafasi za utajiri na Utawala wa Muingereza. Yaani hapa tunabadilisha rangi tu lakini bado wananchi watakuwa wametawaliwa na utajiri kuhama toka kwa mzungu na kushikwa na mswahili.
Nyerere was against that!.. alitaka Tanzania isiyokuwa na Wanyonyaji, Makabaila kama wazungu na pia kuondoa Ukabila na Udini. Na kukamilisha hayo lazima kuwepo na victims. Bahati mbaya msiba mkubwa uliwakuta waislaam kwa sababu ndio walikuwa ktk ngazi za juu - UONGOZI. Ukweli utasimama kuwa all politians wakati huo walikuwa na interest zao - dream ya Utajiri na madaraka na dream hii bado inaendelea hadi kesho. nani asiyependa madaraka kwa sababu ya Utajiri na madaraka ya kuwatawala watu!... That's what we have experienced for the long time.
Nyerere akawatupa Ma -chief wote nje ya nchi kuondoa influence yao ktk makabila kisha wale waislaam wenye siasa kali wakatupwa ndani BAADA ya kutumia dini kutofautisha Utawala mpya wa Nyerere.
Ni kweli Historia yetu imepindishwa sana na waandishi wetu kwa sababu ambazo sidhani kama Nyerere alitaka ziwe hivyo, kwa sababu vitabu vyote vinavyosomwa mashuleni ama University havipitishwi na Rais.
kama navyozoza siku zote kuwa ELIMU yetu waafrika imepangwa na mzungu na tunajifunza tu kile ambacho kinakubalika na mzungu hata iwe historia yetu wenyewe.
Hata mapinduzi ambayo hayakufanikiwa ya mwaka 1964 yalipangwa na waislaam na historia haisemi hivyo! - Na kama sio marehemu Sheikh Kassim Bin Jumaa kumshtua Nyerere kuhusu hayo mapinduzi leo hii Tanzania (Tanganyika) tungekuwa tunazungumza lugha tofauti. na ndio maana kuna watu wanaomchukia Marehemu Sheikh Kassim hadi alipokufa!...
Binafsi huyu Sheikh ni HERO kwangu kwa sababu azma ya Nyerere kuondoa Ukabila na UDINI ilikamilika na leo hii tunaweza kuzunguzia vitu ambavyo hakuna kati yetu anayeweza kutueleza - WHAT would happen if - Mapinduzi hayo yangefanikiwa. Ni makosa kutumia dini ya Kassim bin Jumaa badala ya kutumia Utanganyika wake kwa sababu hakuyafanya haya kwa sababu yeye ni Muislaam bali Mtanganyika.
Yes, kuna watu muhimu sana ktk kupigania Uhuru wetu wameachwa nje ya historia yetu lakini sio swala la Waislaam tu bali Watanganyika. Wapo watu mikoani ambao walishiriki kikamilifu kwa dini na kabila zao ktk mapambano yetu na tukianza kuwataja kwa kabila na dini zao utakuta mkorogano mkubwa. Kulikuwa na wanachama wengi wa TANU toka dini zote hata wahindi na waarabu walishiriki kikamilifu ktk nafasi zao kuupigania UHURU.
 
Mkandara,
Hii umetoa elimu tosha. Nisingeweza kulieleza hili vizuri kama ulivyofanya hapa. Waasisi wa TAA au TANU ingawa walikuwa waislamu walijiona ni Watanganyika kwanza. Kwao dini was secondary. Nilipata bahati ya kumfahamu hayati Abdulwahid Sykes. Mwanae was my class mate. Aliwahi kuniambia kuwa walichokiona katika Nyerere ni ile azma yake ya kulikomboa bara Afrika na ndiyo maaana alimwachia nafasi yake ya uongozi. These were nationalists, and not religious fanatics.
 
Nilisoma kitabu cha Barongo mwaka 1972 kikiwa na historia nzima ya Tanganyika kuanzia TAA hadi TANU bila kupindishwa. Baadaye historia ya Uhuru imekuwa inaanzia kwenye TANU hivyo kuna watu waliokuwa kwenye TAA huwa hawatajwi.

Mgogoro wa kura tatu niliwahi kuusoma, lakini Nyerere alipowashauri watu washiriki uchaguzi huo hakuwa na maana ya kuwaondoa waislamu bali alikuwa na nia ya kutumia hiyo opportunity ya kupata wajumbe kwenye Legco ambao wangeprove kuwa tunaweza kujitawala na hivyo kuharakisha uhuru wetu. Kumbuka kuwa wakati huo kulikuwa na imani kuwa Tanganyika ilikuwa haijawa tayari kwa uhuru labda baada ya miaka 20, yaani hakukuwa na watu wenye elimu ya kutosha kuendesha serikali. Ilikuwa ni lazima tutoe wajumbe wenye sifa hizo kuonyesha kuwa kweli walikuwapo, na hiyo ndiyo iliyoharakisha uhuru wetu na ule wa nchi jirani zetu za Kenya na Uganda.

Pili Uchaguzi wa kura tatu haukuwa Dar es salaam tu, ulikuwa ni wa nchi nzima. Hata kama masharti yale yangeondolewa, Dar es Salaam (Pwani) ilikuwa na mjumbe mmoja tu kati ya wajumbe 12 kutoka majimbo yote ya Tanganyika. Mwishoni kungekuwa na wajumbe wa dini mablimbali kutoka majimbo mengine ya bara. Kwa hiyo madia ya waislamu kuhujumiwa kwa kutumia kura tatu siyo ya kweli.
 
kutokana na maelezo ninayoyapata hapa juu ,nimegundua kuwa ni kweli mchango wa uhuru maeneo ya pwani uliongozwa na hasa na waislamu,nyerere alichofanya ni kubadilisha harakati kutoka mzizima na kukitangaza chama kikawa cha kitaifa,kwani tanzania si dar es salaama pekee,sasa ukija kwa wana TANU
 
WANA TANU wengi mikoani definately walikuwa wakristo ,dini ambayo ilishika moto zaidi bara.namkubali aby sykes ,lakini kabla ya mwalimu sijapata kuuona mahali pameandikwa mikutano waliyoifanya mikoani mfano singida ,rukwa ets.mchango wa mwalimu ulikua na sura ya kitaifa zaidi,hii tabia ya wazee wa dar es salaam kujiona ndio tanzania ipo hata kwenye mpira,hivi vilabu vina wapenzi nchi nzima lakini utakuta maamuzi yanafanywa na wazee wa dar tu
 
Kichuguu,
Hapana sii kweli kwamba Nyerere aliwachukua wakristu kwa sababu walikuwa na elimu.... Nadhani kama umesoma kitabu cha Mohammed said utakuwa waislaam kibao walikuwa naye Makelele na hata Mwapachu alikuwa Uingereza akisoma. Na ktk kuhitimu elimu za juu zaidi hawakuwepo wengi nadhani hata hawafiki wanne... kwa hiyo hapa sii mkristu wala muislaam alikuwa na elimu nzuri.
Swala la UHURU wetu kusema kweli waislaam walikuwa ni issue kwa mzungu na sababu sio dini yao bali waislaam walikuwa mbele sana na Ukommunist. hata Mahatma Ghandi alijifunza mengi ya siasa huko South Afrika kutoka kwa waislaam. Sasa huwezi kuwa against Ubepari kama huna malengo tofauti na Ubepari... kwa hiyo lazima uwe Mjamaa na hili lilikuwa tishio kubwa kwa mzungu. Muslims were communist kwa mtazamo wa mzungu.
Tukumbeni kuwa wakoloni walitawala Afrika kwa malengo ya - KIUCHUMI zaidi ya kitu chochote na hata leo hii matatizo ya nchi hizi na nchi za nje ni ya KIUCHUMI. Otherwise hakuna mtu anajali kama nchi ni ya wazungu watupu, Waafrika ama Wachina. Maslahi yao comes first!.. ndio maana hawana taabu na Saudia wala Australia ambako kuna ubaguzi kuliko nchi yeyote ile duniani.
 
Mkandara,

Sikusema kuwa Nyerere aliondoa waislamu kwa vile hawakuwa wamesoma; nilichoeleza ni kuhusu kuwashawishi wajumbe wa TANU wakubali yale masharti ya kura tatu. Sharti moja lilikuwa linahitaji mgombea awe na elimu ama ya darasa la kumi au kumi na mbili vile. Wajumbe walilipinga hili kwa nguvu sana pamoja na lile na kuhitaji wawe na mapato ya pauni kadhaa sikumbuki kiasi gani. Nyerere akawashawishi wajumbe waingie uchaguzi ule kwa vile ilikuwa ni kuonyesha kuwa kweli walikuwapo waafrika wa kutosha waliosoma wenye wana uwezo wa kuendesha serikali.

Huyu mwandishi amesema kuwa kura tatu ndiyo iliyosababisha wakristo wachukue nafasi za uongozi kutoka kwa waislamu; na hiyo ndiyo ninayopinga. Yule mtu aliyeongoza upinzani dhidi ya kura tatu hakufanya hivyo kwa msingi wa kidini, bali alikuwa akidai kuwa haikuwa halali kwa waafrika wengi wakati huo kutimiza masharti hayo ya kura tatu. Nyerere akasema kuwa kama tutapinga masharti hayo tutaoa mwanya kwa wazungu kuendeleza kisingizio cha kwambaTanganyika haikuwa tayari kwa uhuru wakati huo huku tunao watu wenye sifa hizo. Lakini sasa kuna spini kuwa Nyerere alitumia masharti hayo ya kura tatu kuwaengua waislamu.

Sasa hivi sina data za kutosha ila najua kuwa kulikuwa na majimbo kumi na mbili, na kila jimbo nadhani lilikuwa na mjumbe mmoja. TANU ilipata wajumbe waislamu na wakristo kulingana na maeneo waliyotoka. Tafuta kile kitabu cha Barongo ambacho kiliandikwa wakati nchi bado ina utaifa zaidi na hakikuwa na spin yoyote, nadhani kiliandikwa mwishoni mwa miaka ya 60 hive kwa vile mimi nilikisoma mwaka 72. Majina yote ya wazee maarufu wa Dar es Salaam yameandikwa pamoja na michango yao kwenye mapambano ya uhuru. Kitabu kile kilikuwa kinaitwa "Mikiki Mikiki ya Siasa Tanganyika"
 
Mkandara said:
Hata mapinduzi ambayo hayakufanikiwa ya mwaka 1964 yalipangwa na waislaam na historia haisemi hivyo! - Na kama sio marehemu Sheikh Kassim Bin Jumaa kumshtua Nyerere kuhusu hayo mapinduzi leo hii Tanzania (Tanganyika) tungekuwa tunazungumza lugha tofauti. na ndio maana kuna watu wanaomchukia Marehemu Sheikh Kassim hadi alipokufa!...

Mkandara,
Duuh hapa naona unaanza kutufundisha historia mpya.Ni kweli waislam ndio walifany ayale maasi mwaka 1964? Unaweza ku support hili? Kuna sehemu yoyote umesoma? Naona mjadala umekuwa mtamu.

Kichuguu,
Nashukuru kwa kutufahamisha jina la hiko kitabu cha Mzee Balongo.

Wengine,
Mie naona kuna ukweli katik ahaya malalamishi ya Waislam.Ukisoma kitabu cha Dr. John Sivalo(Kanisa Katoliki na Siasa ya Tanzania) utaona huyu Padre mkatoliki anazungumzia hili tatizo waziwazi.Hata Dr. Hamza Njozi(Mwembechai Killings and Political Future of Tanzania) nae analalamika vitu hivi hivi.Mohamed Said nae analalamika vitu hivyo hivyo. Je hatuoni hapo kama kuna tatizo?
 
Mkandara,
Duuh hapa naona unaanza kutufundisha historia mpya.Ni kweli waislam ndio walifany ayale maasi mwaka 1964? Unaweza ku support hili? Kuna sehemu yoyote umesoma? Naona mjadala umekuwa mtamu.

Kichuguu,
Nashukuru kwa kutufahamisha jina la hiko kitabu cha Mzee Balongo.

Wengine,
Mie naona kuna ukweli katik ahaya malalamishi ya Waislam.Ukisoma kitabu cha Dr. John Sivalo(Kanisa Katoliki na Siasa ya Tanzania) utaona huyu Padre mkatoliki anazungumzia hili tatizo waziwazi.Hata Dr. Hamza Njozi(Mwembechai Killings and Political Future of Tanzania) nae analalamika vitu hivi hivi.Mohamed Said nae analalamika vitu hivyo hivyo. Je hatuoni hapo kama kuna tatizo?


In fact hiyo ya mapinduzi hata mimi nimejifunzia hapa, na bado najaribu kuitafakari kwa vile najua kuwa wale askari walitulizwa na Oscar Kambona akishirikiana na John Okello, ambao walikuwa wakristo. Halafu Nyerere alisaidiwa kwenda mafichoni Kivukonina Kawawa ambaye ni mwislamu. Sasa kwa vile jambo hilo halikuwahi kuandikwa ndiyo maana nimebaki mdomo wazi.

Haya malalamishi ya waislamu yanategemea sana nia ya mwandishi mwenyewe. Wengine wakuza jambo dogo kuwa dunia nzima. Kwa mfano madai mengi yaliyoanbikwa na Dr. Njozi hayakuwa yamefanyiwa utafiti na mengi yalikuwa ni mawazo yaliyotokana na hisia za watu wachache tu. Alithibitisha hilo wakati ulipomhoji redioni. Huyu Bwana Said anasema mambo aliyoandika amesimuliwa na baba yake. Inawezekana baba yake alikuwa upande wa waliopinga kura tatu kwa hiyo ndiyo maana akachukia yote yaliyoendelea baada ya uchaguzi ule. Kwa jumla amepindisha ukweli wa kura tatu ambayo mimi binafsi naijua vizuri sana historia yake kwa vile mkutano ule ulifanyika pale kwetu Tabora na hadi leo tuna mnara wa kumbukumbu ya mkutano huo pale sokoni pembeni mwa kijumba kilichotuimiwa na mkutano huo. Kudai kuwa Nyerere alisukumizia watu kwenye uchaguzi wa kura tatu kusudi aengue waislamu na kuingiza wakatoliki kwa kweli ni uzushi wa wazi kabisa. Siamini kabisa kuwa wazee wale walioongoza mapambano ya uhuru walikuwa na udini hivyo. Sijaelewa yule padri naye alikuwa na nia gani katika kitabu chake; kwani kama ni kweli Nyerere alipendelea wakatoliki basi yeye padri alikuwa ni mmoja wa beneficiaries wakubwa.
 
Radio Butiama,
Kwanza nataka watu mfahamu ya kwamba naongea vitu kwa mpango pamoja na kwamba mimi sio mwandishi mzuri sana. jaribuni kusoma mara mbili mbili kunipata ktk lugha hii ya Kariakoo.
Niliposema kuhusu mapinduzi yaliyoshindikana mwaka 1964, nia na dhumuni langu ni kuonyesha kwamba swala lile haliwezi kuwekwa ktk Udini kwa sababu tu walioshiriki kutaka kuyafanya mapinduzi yale walikuwa waislaam. Pia nikatoa mfano wa Sheikh kassim kuonyesha kwamba ni hao hao waislaam waliomtonya Nyerere. Kwa hiyo hapa lugha inayotakiwa kutumika ni Watanganyika.. na ndio maana historia ya mapinduzi hayo haisemi kuwa ni Waislaam. Yes ndugu Butiama, hawa jamaa walioyapanga mapinduzi hayo wengi wao walikuwa Waislaam.
Kichuguu, Nadhani wewe unazungumzia yale ya mwaka 1969 ya akina Kambona. Inawezekana nimelewa mwaka lakini kulikuwepo na uvumi wa kumpindua Nyerere na yakaishia chini chini viongozi kibao wa Kiislaam walitiwa ndani, leo hii hatuna historia yake.
Pale 1969 walikuwepo kina Kambona, Kamaliza, Bibi Titi na baadhi wanajeshi.
Tukirudi ktk swala ama madai ya Mohammed said mshikaji inategemea wewe umesimama wapi kuweza kuyaona haya. Bora utoke ndani ya kabati....kama navyojaribu miye. Laa sivyo utaona kuwa suruali zote zimepangwa Upande mmoja na mashati upande wa pili bila kujua kuwa mvaaji wa hizo nguo anazihitaji zote. Ukisimama nje utaweza kulisifia hilo kabati kwa jinsi nguo zilivyopangwa. Nadhani umenipata!
kama nilivyosema problem kubwa ya kitabu hiki imemchukua Abdoul Wahid Sykes kama Muislaam na sio Mtanganyika aliye sahaulika kama akina John Okello.
Nimesoma vitabu vingi kuhusu Uhuru wetu na kila mara huwa najaribu kupima uzito wa mwandishi na kikubwa zaidi kasimama wapi!...
na hii ndio sababu kubwa hutumia neno RANGI kuonyesha kwamba mwandishi hakuzama zaidi kuona nje ya hizo rangi (Uislaam/ Ukristu).
Je, ni kweli Nyerere aliwatosa waislaam?.. jibu lake ni kweli lakini sio kwa sababu wanazodai. Kulikuwa na waislaam bado ktk Cabinet yake na wengine hapa tulipewa ELIMU na serikali yake. Ebu tazama wizarani leo hii na huko ktk makampuni kumejaa wasomi watupu (waislaam kwa wakristu) na tazama CV zao utakuta walimaliza vyuo vikuu Uingereza ktk utawala wa Nyerere. Ni hawa waislaam ambao wanasema walionewa na leo hii wameshika wadhifa kwa elimu hizo za kuonewa. Tazama mlolongo wa viongozi ktk utawala wa JK hawa waislaam walizipata elimu zao wakati gani? Fanya utafiti utakuja nambia kuwa waislaam wanazungumza bila ushahidi wa kisayansi. Yes ni kweli wakristu wengi walisoma kuliko waislaam, so were Wachagga Wahaya and Wanyakyusa ambao wengi wao ni wakristu.. They make 90% ya wasomi wetu wakati huo baada ya Uhuru. Je, Nyerere aliwapendelea hawa watu kwa makabila yao akawaacha Wakristu wengine wa Dodoma, Mwanza na hata kwao Musoma?
Noo bob, mimi hili sikubaliani nalo kwa sababu nawajua waislaam kibao tumepata elimu yetu wakati wa Nyerere na kabla ya mapinduzi ya kielemu ya mwalimu Nyerere nakumbuka sisi wengine ilibidi tubadilishe majina yaonekane ya Kikristu ili tupate hata hiyo elimu ya Msingi. baada ya mabadiliko hapakuwepo tena Muislaam wala mkristu - Wote dugu Moja.
 
Mkandara Maneno mazito unayozungumza,inataka muda kuweza kuyapitia mara kwa mara na kuyameza vilivyo!Mimi najifunza mengi humu.Kwa sababu Historia ya Nchi yetu kidogo haiko wazi!Na watunza kumbukumbu wa serikali ama kwa makusudi au kwa kutokujua hawataki kuiweka wazi kwa RAIA.Ni wajibu wetu kuutafuta UKWELI,kwani tusipofanya hivyo Historia itatusuta!
 
Nakubaliana na Mkandara kwa asilimia mia moja.

Kwa bahati nzuri nina access na baadhi ya ripoti za kabla na baada ya Uhuru zilizoandikwa na waandishi wa nje, wa ndani, wakiwepo waliokuwa kwenye harakati za uhuru.
Mojawapo ya ripoti hiyo ni ile ya mkutano wa TANU kule tabora 1958 ambao ulijulikana kama TANU,s TABORA CONFERENCE in January 1958. report inasema
This was one of the pivotal events of pre-independence period. In December 1955, Twining had sponsored the formation of multiracial United Tanganyika Party as opposition to TANU. Two years later he announced that the first elections in Tanganyika would take place in 1958, in each of the ten constituencies there would be three members of the Legislative Council, one African, one Asian and one European and each voter would vote for a candidate of each race. Most of the TANU leadership thought the party should boycott the elections but Nyerere argued them to participate. All members more than 200 said no, we should boycott election except Nyerere and a Bhoke Munanka a delegate from Tanga.

ukiendelea kusoma utakuta sehemu nyerere anasema

"But suppose we do contest it. Everybody says that TANU will elect only ten members, but that's not true. We also have Europeans and Asians who are friends of ours and will support us. We'll have 30 TANU-supported members.

...

ukisoma yote utaona swala la dini halikuwa mbele hata kidogo wakati wa harakati za uhuru.

Hivi mnafahamu Nyerere mwenyewe hakuwa Mkristu alikuwa mpagani au anafuata dini za kikabila mpaka 1942 baada ya baba yake kufariki. Na ndiyo wakati akachukua jina la Julius ambalo baadaye alikuja kujutia kuchukua kwani alisema Mtakatifu Julius hakuwa mtakatifu mzuri.

Naandika kitabu cha Historia ya Tanganyika kwa kiswahili na mpaka sasa hivi nimekusanya mafaili kutoka sehemu mbali mbali .
 
Mkandara,

Asante sana kwa maelezo yako ya kina. Nakubaliana nawe kuwa udini haukuwa na nafasi katika miaka hiyo; hii spin ya udini imeanza miaka ya hivi karibuni tu baada ya Nyerere kuondoka madarakani. Waasisi wa taifa hili wote waliofanya kazi ya kupigania uhuru walikuwa na utaifa zaidi ya udini. Mitafuruku yoyote iliyokuwa ikitokea kisiasa baina yao haikuwa na uhusiano na dini zao. Inawezekana kwa vile Nyerere alikuwa amezungukwa na waislam wengi, basi alikorofishana nao wengi kuliko kuliko wakristo kwani inajulikana kabisa kuwa Nyerere alikorofishana na watu wengi chini ya utawala wake.

Hadi anamaliza madaraka yake, siamaini kabisa kuwa Nyerere alikuwa anawachukia waislamu kiasi hicho kwani marafiki zake wakubwa walikuwa ni waislamu: Rashid Kawawa, Mzee Tabit Kombo, na in fact ni yeye binafsi aliyepiga kampeini kali ya kumpa madaraka ya Urais Ali Hassan Mwinyi ingawaje baadaye walikuja kukorofishana kutokana na uendeshaji mbaya wa serikali. Aliwahi kumpigia kampeini Salimu Ahmed Salim awe Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa. Kuna wakati baraza lake la mawaziri lilikuwa na waislamu wengi kuliko wakristo.

Kuhusu mapinduzi ya 1964, niliwahi kusoma kwenye kitabu cha John Okello, na article moja iliyoandikwa Oscar Kambona kwenye jarida la Africa Now mwanzoni mwa miaka ya 80 kuwa wale askari walipoasi, Kawawa alichukua jukumu la kwenda kumficha Nyerere huko Kivukoni; halafu Kambona binafsi alijitokeza kwenda kusikiliza madai ya askari walioasi. Kwa bahati nzuri siku hiyo, John Okello naye alikuwa mjini akiwa na nia ya kumwona Nyerere kwa jambo jambo fulaini (silikumbuki). Basi Okello naye kwa ushujaa wake, akachukua nafasi hiyo kuwa pembeni mwa Oscar Kambona kuwahutubia wale askari waliokuwa wameasi na kuwataka warudi barracks. Baada ya hotuba za Kambona na Okello, askari walikubali wakarudi kambini kwao. Ila hiyo fact kuwa wengi wao walikuwa ni waislamu ilikuwa haijulikani, na ndiyo nimeipata sasa. Inawezekana isiwe inajulikana kwa vile miaka hiyo udini haukuwa na nguvu kabisa kwa vile kila mtu alijulikana individually bila kumhusisha na dini yake.

Aljazeera,

Nitasubiri kitabu chako nikisome. Kwa muda mrefu sijasoma vitabu vya historia au siasa za Tanzania ila hii forum inanifanya nijirudi nilekebisha tabia. Unaplani kukikamilisha lini? Na je uliwahi pia kusoma kitabu cha Barongo?

Hizo data ulizomwagga hapo juu ndizo zile za Kura tatu ambayo huyo mwandishi anadai ilikuwa ni njama ya kuwaondoa waislamu madarakani.
Uamuzi wa Nyerere kushiriki uchaguzi ule ulikuwa ni strategic na wala haukuwa na ubinasi au udini wowote; ingawaje wajumbe wengi walianza wakiwa wanapinga, baada ya Nyerere kuwashwawishi walikubaliana naye ndiyo maana TANU ikashiriki. Katika uchaguzi uleTANU ilipata baadhi ya wazungu na wahindi; wanaokumbukwa zaidi ni Amil Jamal ambaye alikuwa mhindi kwenye Jimbo Morogo sikumbuki lilikuwa linaitwaje wakati huo, halafu Derick Bryceson ambaye alikuwa mzungu kwa jimbo la Dar es Salaam nalo sikumbuki lilikuwa likijulikanaje wakati huo.
 
Hakuna jambo baya kama kuandika historia kwa mwanga wa sasa (rewriting history). Tunashukuru kuwa kuna sources za tangu wakati ule hadi hii leo ambazo mtu yeyote anaweza kuziangalia. Tatizo letu sasa hivi, tunajaribu kuangalia historia yetu kufuatana na hali ya ulimwengu wa leo ambapo waislamu wanahisi kukandamizwa huko Nchi Takatifu, Afghanistan, Iraq, Chechnya n.k Hivyo, ili kujenga hali ya umoja kati ya waislamu wapo wale wanaojaribu kuonesha kila kitu kwa kutumia kurunzi hiyo!!

Alichoandika Mohammed Said na hata Dr. Njozi ni kile kile, wanaangalia matukio ya wakati wa uhuru na kuyamulika mwanga wa udini. Zaidi ya yote, lazima uangalia makusudio ya wote wawili. Ukweli ni kuwa si waandishi ambao wako neutral. Nawaambia, haiwezekani kwa hawa wawili kuandika kitabu kinachohusu Uislamu au Waislamu na wakawa neutral katika conclusions zao!

Ndo maana kati ya mapendekezo yangu ya muda mrefu ni kuwa yeyote atakayeandika historia ya Tanzania (Tanganyika na Zanzibar) ashirikiane na watu wengine ambao wako tofauti na yeye kimtazamo na kiitikadi ili kuwa na more balanced view of "Our" History.

Aljazeera, natumaini kitabu unachoandika hautakuwa peke yako. Jaribu kuwahusisha watu kama wanne hivi, na kama utakuwa tayari niko tayari kusaidia katika gharama za uchapishaji.
 
Kichuguu
Nashukuru sana, ni kwamba nimesoma kitabu ulichosema na pia nimesoma na kupitia nyaraka kibao kuanzia 1914 mpaka tulipo sasa. Kuna Nyaraka moja nimeifurahi sana ambayo inaelezea kuanzia kabla ya babu yake Nyerere mpaka Nyerere. Hivi nani anajua kwa nini Nyerere aliitwa Kambarage. Kuendana na recorded statement kutoka kwa Chief Nyerere Burito Nyerere aliitwa Kambarage kwa sababu alizaliwa wakati wa mvua nyingi (Kambarage = an ancestral spirit who live in the rain)

Historia iliyoandikwa na Padre Silvanos (sp) na yenyewe ilipindisha au iliandikwa kwa malengo ya kidini (Ukristu). Watu ambao wameweza kusema bila kuweka dini ndani ni watu kama Padre Wille, Father Richard Walsh, Oswald Marwa,Walter Wilson, chief David Makwai etc

Tatizo moja ni kwamba hata historia ya TAA imepindishwa sana. Kuendana na Nyaraka za wakati huo.

TAA ilianzishwa na Sir Donald Cameron, a highly respected British Governor as a social organisation for African civil servants.

Nyerere kwa kushirikiana na marafiki alianzisha "campus chapter ya TAA" Makerere University. Na ilitumika kama club ya kujifunza na kusomea mambo ya siasa.

Baada ya Nyerere kuhitimu masomo Makerere alirudi Nyumbani Butiama na baadaye akachukua kazi ya kufundisha St. mary's college. Akiwa anafundisha alikaa kwenye nyumba moja na Tibandebage na rafiki yake mwingine alikuwa Chief Haruni Lugusha ambao waliongea mambo ya Tanganyika. Akiwa Tabora alikuwa katibu wa TAA.

Nyerere alikuja Dar es Salaam kwa mara ya kwanza 1946 kuhudhuria mkutano mkuu wa TAA kupinga kuundwa kwa Central Assembly for East Africa. Miaka miwili baadaye ndipo Rashidi Kawawa alijiunga na Tabora Government School, na hapo urafiki wake na Nyerere ulianza baada ya Nyerere kushiriki kwenye debate ya "Wealth is Better than Education" akiwa anapinga.

Mwaka 1949 April, Nyerere aliondoka kwenda London kusoma. akiwa huko ndipo aliandika ile essay ya "The race problem in East Africa" Nyerere alirudi Tanganyika 1952 na hakukaa Dar bali alirudi Nyumbani...

Nitaendelea baadaye kwani nawahi kwenda kufundisha.
 
Aljazeera,

Aisee afadhali wewe unatupa mwanga zaidi wa haya mambo; jitahidi sana umalize kitabu hicho ili tupate ukweli wa mambo.
 
Back
Top Bottom