Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Historia mliyosoma ndiyo tuliyosoma. Nyerere hakuandika kitabu chochote cha historia. Hakuwahi kusema mahali popote kwamba alipambana peke yake katika harakati za uhuru. Tena, alipoweza alikuwa akiwasifia aliokuwa nao, wale wazee - na diyo maana alijenga utamaduni wa kulihutubia taifa kupitia wazee wa Dar es Salaam. Zaidi, hakuwandika hata historia yake mwenyewe. Hivyo, wakati tunatafuta kujenga majina yetu kwa kurekebisha historia, ni bora tukaepuka makosa ya kumsingizia kwa yale ambayo hakuyafanya.

Ninachojua ni kwamba wana historia wengi wa wakati huo, tena wengi wakiwa wageni, ndio walioandika historia yao. Walitazama matakwa ya wakati huo, wakandika kinachosomeka na kukubalika wakati huo, katika enzi za kujenga utaifa na kusifia viongozi waliokuwapo. Hawakuandika historia yote.

Walichofanya ndicho kinafanyika sasa Afrika Kusini. Kiwewe cha uhuru na umaarufu wa Mandela kinawafanya wasomi na wanahistoria kuandika kumbukumbu nyingi za mapambano kuhusu Mandela, kana kwamna aliteseka peke yake, alipambana peke yake na kuleta uhuru. Hata wazungu wengine hawakupenda manyanyaso ya waafrika. Walisaidia kupata uhuru wa Afika Kusini.

Hadi sasa wanamuimba shuleni na katika miktano kadhaa Mandela..Mandela...Lakini hakuwa peke yake. nadhani mnajua. Si haki wasomi wa baadaye wakianza kumalumu yeye kwa sehemu ya historia iliyoandikwa kumsifia Mandela. Hiyo ni sehemu tu ya historia. Wanaojua sehemu nyingine waandike. Mataifa yote ndiyo yamekua. Hakuna taifa lililoandika historia kwa vitabu vichache na kwa wakati mfupi hivyo.

Hata katika dini mambo ni yale yale. Yesu hakuandika vitabu vyote unavyosoma leo kuhusu Ukristo. Wala yeye hakuagiza viandikwe. Na havikuandikwa vyote wakati mmoja. Na havikuwa na ujumbe ule ule. Ndiyo maana historia inaendelea kufunua vingine katika karne za leo.

Kuna watu walicheza n Yesu akiwa mtoto. Kuna watu walikuwa rafiki za familia yao. Kuna watu walimsikia akifundisha. Kuna watu wanakumbuka mengi waliyoona na kusikia ambayo hayakuandikwa katika Injili. Wapo na wameandika (kwa taarifa yenu). Si vema kumlaumu Matayo, Luka, Marko au Yohana au Yesu mwenyewe kwa kila kilichoandikwa kwenye vitabu hivyo, huku baadhi ya mambo muhimu kama tarehe ta kufa kwake, alipofia Maria mama yake, alipofia Yosef na hata mitume wenyewe, yakiachwa!

Walipoandika, hilo halikuwa lengo lao. Yaani haikuwa angle ya stori waliyoandika. Wakati huo huo, huwezi kusema walichoandika ni uwongo. Ni kama waandishi wanapoandika habari kila siku. Yapo mengi wanayokuwa wameyaona siku hiyo, lakini wanayaacha na kubakiza yale tu yanayouza magazeti yao, au waliyotumwa na wakubwa wao...yale wanayoona ni habari kwa kesho yake au siku hiyo. Sasa akitokea mtu akasema 'mbonahawajaandika kile au kile' anakuwa hajui maana ya angle. na Wakati mwngine hicho walichokiacha watakitumia baadaye katika stori zijazo, iwap litatokea jambo lililo relevant au wataandika makala.

Kwa sababu hiyo, tunafanya makosa kumlaumu Nyerere kwa historia iliyoandikwa kuhusu juu yake. Kama binadamu ana mengi aliyokosea - kama mimi na wewe - lakini si hili la historia yetu. Halimhusu. Na kama sisi tunajua vinginevyo, basi tuandike. Tusiishie kulalama nakujidaidai tu kana kwamba kunajipya tumegundua. Kuandika historia ni kazi ya kila mmoja anayeweza, hasa wanahistoria. Si ya wanasiasa.
 
Aljazeera,

ukitaka proof-reader nipo mimi wa bure kusudi nipate stori yote kabla ya wengine.

Kulikoni,

Nadhani tumeelewana na kukubaliana kwa yote ila huenda tutashindwa kukubaliana kwenye udini na mapambano ya uhuru. Wazee wale walioongoza mapambano walikuwa wanatumia utaifa wao na wala udini haukuwa moyoni kabisa ama sivyo hata Azimio la Arusha lisingepita. Udini umeibuka miaka ya hivi karibuni tu. Mwanzoni mwa miaka ya themanini nilipata bahati ya kuongea na Mzee Azizi Dovya wakati nikiwa JKT pale Ruvu wakati huo nikiwa "jongolist kmkuu"; yule mzee alikuwa anazungumza utaifa tena kwa kutoka moyoni mwake akiwa na mkusanyiko wa vijitabu kadhaa vilivyokuwa na hotuba za Nyerere.

Kuna mambo ambayo hata mimi naweza kuwa ninayaelewa visivyo, kwa hiyo usikose kuwa unanikosoa kwa madai kukubali kutokukubaliana. Ukumbi huu unatufundisha mengi.

Kichwamaji,

Wewe ni kichwamaji kwelikweli. Ni kweli kuwa makosa katika historia ni ya waandishi wa historia hiyo, hata hivyo, kuna waandishi wengine wanafanya makosa hayo makusudi huku wengine wakiyafanya kwa bahati mbaya kutokana na kuwa na data finyu.
 
Yawezekana hatutakubaliana kuhusu suala hili la udini kwa kuwa kuna watu wanalivalia njuga kuliko wenzao. They rare brainwashed. Ukweli unabaki Nyerere alikuwa Mkatoliki, na Padri Mkatoliki (jina nimesahau) ndiye limtafutia scholarship Edinburg. Ukristo wake haukumzuia kubinafsisha shule za misheni ili ziwasaidie wote - wakiwamo Waislamu. Shule hizo zimeendelea kuharibikia mikononi mwa serikali, lakini nina imani historia ya elimu ingekuwa tofauti bila uamuzi huo wa kuwanyang'anya Wakristo shule zao ili ziwe za umma.

Nilimsikia Mwalimu mwaka 1995 akizungumzia sababu za kuchukuliwa kwa shule hizo. Alikuwa akimweleza Askofu mmoja mkatoliki kwamba: "Baba askofu nilipokwenda shule shule sikujua kwamba kuna shule za wakristo na zisizo za wakristo, hadi nilipokwenda Tabora...Nikachukia sana, nikasema sasa wasio wakristo warasomea wapi?...hivyo uamuzi wa kuwanyang'anya Wakristo shule....najua uliwaudhi sana...ulichukuliwa kwa ajili ya kujenga taifa, si kundi la wasomi wa dini moja tu..." Haya aliyasemea viwanja vya Uhuru, Bukoba Mjini, mkoani Kagera, siku alipokwenda kumnadi Benjamin Mkapa kuwa rais wa Tanzania. tafuteni mkanda wake mjiridhishe.

Mtu mdini hawezi kuchukua hatua za namna hii. Kumwita Nyerere mdini ni sawa na kumwita Mtanzania kuwa ni Mnigeria, na ukasisitiza, hata akijietetea yeye ni Mnigeria tu.

Kwa Nyerere, hata katika makosa mengi tunayomlaumu nayo leo, taifa lilikuwa nambati wani. Kwa hiyo, jambo lolote lililoonekana (kwa macho na akili zake) kuhatarisha utaifa, lilichukuliwa hatua. Vile vile alivyowanyang'anya Wakristo shule zao, ndivyo alivyofuta jamii ya Waislamu iliyokuwapo, wakalazimika kuanzisha BAKWATA. Dini haikuwa jambo la kutanguliza mbele ya Mwalimu. Huyu ndiye utamuita mdini? Labda kama una sababu zako.
 
Kichwamaji
Naona kuna sehemu umegusia mwalimu kwenda kusoma Edinburgh, kuna report moja iliandika hivi wakati huo, na nukuu

"Nyerere had long wanted to continue his studies abroad but had been reluctant to leave Tanganyika because his mother and young brothers needed to be cared for. He had also been the victim of some cubtle political pressure. Oswald Marwa had written the Governor advising him that Nyerere should not be allowed to study overseas because he was politically minded and might be dangerous when he returned. Finally Nyerere's friend Father Walsh helped to arranged a government scholarship as well as a grant from St. mary's for the support of Nyerere's family and his fiancee. A few months earlier, Nyerere had become formally engaged to Maria Gabriel, whom he had met in Musoma..."
 
Kichwamaji,
Asante kwa mchango wako. Ni elimu tosha. Naona hata mwanangu FD kakubali kukaa pembeni apate kusomeshwa. Sikubali kabisa kuwa lengo la Nyerere kukubali kura tatu lilikuwa ni kuwapunguzia Waislamu nafasi zao. Nyerere alipinga sana kugomea uchaguzi. Alishatizama mbali na kuona kuwa wazungu, wahindi, idadi yao haikuwa kubwa kote Tanganyika kwamba kura tatu would have made a difference. Waingereza walitaka kura tatu ku "dilute" nguvu za Waafrika. Lakini Nyerere alijua kabisa kwamba Waafrika would end up being the majority, three votes notwithstanding. Sasa huu usanii kwamba ilikuwa inawalenga Waislamu ni jambo linalosikitisha.
 
Kichuguu.
acha ubwege heading ya thread inasema nini?

Samitungo.

Nimefurahia umeingia mwenyewe mzima mzima karibu mwamba barazani na usitishike humu kuna wengine hata Dar hawakukaa na kama walikaa basi ni kota za polisi au jeshi mfano jamaa yangu wa kinyakyusa anajitia mjuaji sana Mlalahoi.

umenifurahisha hadi kiswahili unachoongea ni cha kimwinyi na kiswahili haswa nadhani kwenye interview yako akina Mlalahoi na Kichuguu wamejifunza hadi kiswahili. mie mswahili hufurahi kuona mswahili mwenzangu una mwaga vitu.

Wanabodi someni kwanza kitabu cha Mohamed Said kabla ya kuja kuropoka humu kama walokole.
 
Jasusi.
tusi lipi? kwani wewe ni wa mjini? ujalijua gogo vivu kariakoo? unamjua marehemu Abbas Mzee alikuwa anafanya nini na kuishi mtaa gani?

Nadhani Mohamed Said kuna maneno aliogopa kusema kuona kama anasimanga lakini ukweli ni kuwa Nyerere alikuja Dar na kaptula tu. na wazee wetu wakamfundisha hadi kuvaa suruali.
 
Jasusi.

Nadhani Mohamed Said kuna maneno aliogopa kusema kuona kama anasimanga lakini ukweli ni kuwa Nyerere alikuja Dar na kaptula tu. na wazee wetu wakamfundisha hadi kuvaa suruali.


What are you trying to prove here Mswahili...mbona unaelekea kutaka kuharibu somo zuri hapo juu ndugu yangu.
 
Jasusi,

Afadhali umemkumbusha ndugu yetu mswahili maana ya ustaarabu, si ajabu ndiyo maana akawa alikuwa amewekwa "kifungoni" kama alivyodai.

Mswahili,

Jifunze ustaarabu usije ukatupwa kifungoni tena; hatuko hapa kutukanana wala kushindana ujuaji, bali tunajifunza kutoka kwa wenzetu na tusipokubaliana nao tunawaambia hivyo. Post yako ilikuwa nje kabisa ya mjadala huu na ilikuwa ni combative. Pili sijadai kuwa mimi ni mtu wa Dar es Salaam. Kwetu ni Tabora Isevya ingawa nimekaa Dar es Salaama kwa muda mrefu sana na nimejenga pale Mbezi maeneo yanayojulikana kama Tangi Bovu. Sihitaji kufundishwa kiswahili pamoja na kuwa ninajua lugha nyingine kadhaa za nje ya Tanzania na zile za ndani ikiwa ni pamoja na Kinyamwezi na Kisukuma.


Nyerere alipokuja Dar es Salaama alikuwa ametokea masomoni Scotland. Kabla ya hapo alikuwa amefundisha pale kwetu Tabora kwa miaka kadhaa ambako alikuwa ameonyesha makali kiasi kuwa hata mkoloni alikuwa ameanza kumwogopa; hakuwa mshamba kama unavyodai, na ndiyo maana alipokelewa na watu wa Dar es Salaam.
 
Aljazeera, Kulikoni, Mkandara et all

Thanks kwa somo zuri hapo juu, kuna mengi sana ambayo sikupata hata kuyasikia kutokana na either kupotoshwa kwa ukweli au uhaba wa vyanzo vya historia yetu.

Suala la udini linavyolazungumzwa leo dhini ya JKN, mimi naona hamna tofauti yoyote na wale wanaosema west ina lengo la kufuta uislam duniani. Watu wanaojulikana kama wanasiasa kali na wale wenye maslahi yao binafsi wanapotosha ukweli kuhusu nia ya kweli ya west. West nia yao ni malighafi/oil n.k ambazo zimo kwa wingi katika nchi za ki-islam, katika kutimiza lengo hilo ndipo unakuta waislamu wengi wanaadhirika kwa either vita, vikwazo, njaa n.k lakisi lengo kuu sio kuwaangamiza wao kwa sababu ya dini au imani yao. Sasa hapa kama ni mvivu wa kwa neutral ni rahisi kusema West wapo agaist islam kama dini, wakati ambapo ukweli ni kuwa West wanataka malighafi zinazomilikiwa na Waislam. Kuna tofauti kubwa sana hapa...nikilinganisha hili na JKN kuitwa mdini nina imani kubwa kabisa kama wanabodi wengine waliotanguia kusema kuwa yeyote alichukiwa/kutengwa na JKN sio kwa sababu ya dini yake au udini aliokuwa nao JKN bali ni misimamo yao kisiasa kuwa tofauti.
 
Kwa kweli wazee mmeenda shule ya historia.

Aljazeera, Kulikoni, Kichuguu(Mlima kilimanjaro), Mkandara na Kichwamaji, pongezi kwa mjadala swafi kabisa.

Kulikoni
Hiyo habari ya "vikofia" ni more of a personal satisfaction than "material content"........hoja zako nyingi, na uchambuzi wako ni makini na nzito, walakini hii ya vikofia "ni very weak"
 
Mswahili,
Kwetu bara kumwita mtu bwege ni tusi. Akikupiga ngumi ya puani usishangae.
 
Kulikoni
Hiyo habari ya "vikofia" ni more of a personal satisfaction than "material content"........hoja zako nyingi, na uchambuzi wako ni makini na nzito, walakini hii ya vikofia "ni very weak"

Nimekusikia mzee Ogah.

Kwa bahati mbaya sina reference kamili on that right now, and its accompanying article. Nlikuwa natolea mfano wa baadhi ya wanahistoria kufanya makusudi kupindisha ukweli. Otherwise nimekuelewa, point noted.
 
We Jasusi ndondi unaziweza lakini au unaleta mikwara tu hapa....???
 
Kulikoni,
Mwenzangu umenielewa vizuri sana...This is what I'm talking about!
Na pia umeweza kumuelewa Mohammed Said. Ni kweli kabisa nia na dhumuni la kitabu chake ni kuonyesha - Mashujaa waliosahaulika, lakini katumia dini zao badala ya Utanganyika wao. Ukiondoa dini hakuna makosa kabisa...yeye rangi ya Blue kaichambua na kujua kuwa ni mchanganyika wa Njano na Kijani..sababu hii ndio imewachanganya wengi.
Na ndio maana mimi nadai tupewe majina ya viongozi wengine wa mikoa, wilaya na hata wanachama wliochangia UHURU kwa sababu sasa tunawapanga watu wote na sio KIONGOZI mmoja tu. Sababu zinazopingwa kwa historia kumwonyesha Nyerere peke yake (Kiongozi) ndizo hizo hizo nazotumia ili tuweke list ya wote hata wale wa mikoani - not only leader.
Mapinduzi:- Ndugu yangu hiyo issue unayotaka kuizungumzia ni nzito kwangu na siwezi kuitoa hapa wala kukuandikia kwa sababu zile zile ambazo zinawafanya waandishi wa habari na watu wasiweze kuzungumzia wazi. Kila mara nimekuwa najiuliza WHY?...na kila unaye muuliza atakwambia DON'T.
Umesema kuwa kutokana na maelezo ya wazee umeambiwa mabaya yote ya Nyerere dhidi ya Waislaam. Sasa hao hao wazee waliokupa habari hizo nakuomba waulize kisa cha - Mufti Sheikh Hassan bin Amir.
Pili, swala la Mwinyi - Sheikh Kassim na baadhi ya waislaam walikuwa na chama kinaitwa BALUKTA ambacho kilianzishwa na waislaam kwa waislaam lakini kilionekana kama chama cha magaidi (Under Mwinyi). Which was not true!...
Mwinyi alikipiga marufuku na hapo mapambano baina yake na Sheikh Kassim yalianza hadi kuna siku Sheikh Kassim mwenyewe kwa mdomo wake alisema Nyerere ni Muislaam mzuri kwa mazuri anayowafanyia watu kuliko.... malizieni wenyewe.
Yakatokea maswala ya mabucha nje kabisa ya mwongozo wa Balukta.. unajua tena...hiyo ilikuwa 9/11 tosha kwani serikali ilikuwa inasubiri hilo tu. Sheikh kassim akawa Ossama -wanted for nothing other than being himself -Sheikh.
Kinachonisikitisha mimi ni Huyo Mrema... huyu jamaa amekuwa victim wa Mwinyi kwani waislaam walimkalia siku tatu msikitini kumwomba Mungu amhukumu kwa yale aliyoyafanya.
Na trust me guys - huyo Mrema ndio kwisha kazi hata aende wapi ndio kesha ondoka Kiutawala. Nyerere mwenyewe hakuweza kumsaidia na hakuna mtu yeyote atakaye weza kuliondoa kafara hilo isipokuwa yeye mwenyewe kwa kuwaomba radhi familia ya marehemu na waislaam wa msikiti wa mtoro na kuwambia Ukweli wote. Mwisho adhuru kaburi la Kassim na kuomba radhi... labda ataweza kuanza mwanzo mpya.
Hii nzito nawapeni na nadhani wengi hamkutegemea kunisikia ktk tune hii!
Kichuguu,
Mimi nakubaliana nawe ktk kura tatu.. hapa kuna ubadilishaji wa lugha tu. Sio Nyerere aliyeweka sheria ile bali ni Muingereza. Kuna siri moja TANU ktk uchaguzi wake wa kwanza. Unajua Abdoul Wahid alishinda kura nyingi za wajumbe kuliko Nyerere. Hii wengi wenu hamfahamu na hata hao waislaam wenyewe wanaodai udini, lakini Abdoul Wahid mwenyewe aliomba jina la Nyerere lipitishwe badala yake kwa kuelewa picha ya mbele. Ni kweli walikuwepo wapinzani ambao walimshtumu kwa udini.. na hawa watu hawawezi kwisha.. Wapo hadi leo hii bado wanatumia rangi za dini zao kuonyesha mafanikio ama mapungufu.
Kibaya zaidi wengi wasichokifahamu ni kuwa TAA ya akina Abdoul Wahid na Mwapachu ilikuwa ikisisitiza sana kuondoa kabisa Udini na hii ilikuwa agenda yao kubwa ndani ya chama TAA ili kiweze kukubalika hata mikoani. Sasa nambieni utaondoa vipi udini ktk chama ambacho 100% ya viongozi wake ni waislaam? I mean come on guys waislaam nyie nambieni mngefanya nini tofauti.
Jamani hili swala si la kidini kabisa, Na kama kweli bado kuna watu wanashikiria Udini kwa Nyerere, wajibu kuhusu hoja ya Muungano!..
Pili mimi nitaongezea kitu kimoja. Leo hii Zanzibar bado wana matatizo ya huu Muungano chini ya JK muislaam. Jee, tunaweza kutumia neno waislaam badala ya Zanzibar tunapohoji jambo lolote kuhusu zanzibar?.. maanake Zanzibar asilimia zaidi ya 90 sijui 99 ni waislaam. Je, JK pia ni mdini?
Maana yangu toka huko nyuma, matatizo ya Zanzibar tuzungumze kama wao ni Wazanzibar itaeleweka zaidi kuliko kutumia dini zao. Ni sawa kabisa na mtu alete hapa madai kuwa Wazanzibar ni wadini kwa sababu viongozi wao wote ni waislaam...Hapa itakuwa kazi maanake hata India na China wanaongozwa na Wahindi na Wachina...
Nitawaleteeeni mahojiano fulani ya Nyerere kuhusu Ukoloni hapa kuna vitu vidogo vidogo tunaweza kuviunganisha na hii mada.
 
Nyani,
Kule kwetu ndondi hazifuatani na umbo la mwili. Unajua hasira inaweza kukufanya ujifikirie kuwa wewe mzito kuliko kifaru! ha!ha!ha!
 
Mkandara,
Endelea kuelimisha. Kuna mtu hapa alimtaja Abdulwahid Kleist kuwa alikuwa na udini. Nikashangaa. Kwa muda mfupi niliomjua mzee huyu sikuona kabisa mambo ya udini ndani yake. Sasa kwa sababu ujuzi wangu wa huyu mzee haukuwa mkubwa nikaona ninyamaze. Asante kuyaweka mambo sawa hapa.
 
Mkandara,

Nimekumbuka jaribio jingine la mapinduzi ambalo lilikuwa lilimemhusisha Maj Gen Sarakikya mwenyewe ingawa kweli jaribio hili halikutangazwa kabisa. Nadhani ilikuwa ni kati ya mwaka 1972 na mwaka 1974 hivi ambapo baada yake jeshi lilikagawanywa katika semi-autonomous brigades zikiongozwa na mabrigedia wapya waliopandishwa vyeo baada ya jaribio hilo akina Mayunga, Musuguri, Marwa, Walden, na wengineo. Major General Sarakikya alitolewa kabisa jeshini na kufanywa balozi huko Nigeria. Aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Kagera wakati huo Kanali Abdallah Twalipo alipandishwa moja kwa moja kuwa General na mkuu wa jeshi. Inasemekana kuwa Col Abdallah Twalipo alikuwa amehusishwa pia katika plani hiyo na ndiye aliyetoa siri hiyo nje.

Je ndilo hilo jaribio unaloongelea? nina dukuduku sana.
 
Raha kusoma mambo humu. Najifunza mengi. Ila samahani ndugu yangu Mswahili, tumia lugha za kwetu Pwani, ni lugha laini na tamu zisizo kali hivyo.

Jamani mnaongelea harakati za uhuru wa Tanzanyika, au Tanzania, mbona mnapenda kuwasahau akina Mtemi Mkwawa, Kimweri, Kinjekitile Ngwale, na wengine? Au mnadhani Uhuru wa Mtanganyika ulianzia kwa TAA, UISLAM au na akina NYERERE tu? Huyo mwandishi wa kitabu amelalia upande mmoja mno. Vugu vugu la siasa za nchi hii zilianza zamani sana, na hakukuwa na dini. Na mtakumbuka Kinjekitile alijitahidi kuwaunganisha makabila tofauti kupambana na ukoloni.
Waandishi kama akina Aljazeera mnaotaka kuandika zaidi historia ya ukombozi wa Mtanzania, naomba msiwasahau mababu hao, wasioujua Ukristo wala uislamu.
 
Back
Top Bottom