Naam Mwl kichuguu,
Kwanza samahani if I appeared a bit harsh when I addressed you earlier. Then katika nukta zako:
1. Katika mada ya DrWHO ya Ukweli kuhusu Nyerere, ambayo sasa hivi iko katika kabrasha, katika uchangiaji wangu nlisema udini wa nyerere umeshakuwa documented by both muslims and christians, nikatoa reference ya Mohamed Said na ya Dr. Sivalon. Ulipokuja kucomment, ukaaandika: ".. Kwanza kabisa ni vizuri kuthibitisha credibility ya kila author; hawa wote hawawezi kupasi credibility test kwa vile siyo independent: wote ni waislamu ingawa wengine wametumia pen-names za kikristo...". Kwa hiyo hapa, indirectly ulimaanisha Dr. Sivalon hata kama hukumtaja jina.. maana ndio reference niliyoitoa. [Refer post yako:
http://www.jamboforums.co.tz/showpost.php?p=5339&postcount=33 ya kwangu ilikuwa namba 26] Kwa hiyo katika point hii nahisi sina cha kusahihisha. Sana sana niseme tu kuwa hata kama kaandika Padre, si lazima kiwe 100% true, ingawa kuna dondoo na clues muhimu.
2. I was under the impression that you were statements indicates kuwa Mwandishi kaandika kitabu solely based on simulizi za babaake, which is not true. Kama hukumaanisha hivyo ni poa, chukulia hili ni sahihisho ulilotaka. Hata mimi katika hili la kura tatu bado sijalichukulia kuwa Nyerere alilikusudia kuwahujumu waislam.. ila nakubali kuwa ndipo turning point ya idadi ya waislam kushuka ghafla katika kilinge. Yaani si lazima kuwa zilikuwa ni njama.
Yap, Mkandara katuonjesha nyeti halafu hataki kutumalizia. Ni kweli kama waislamu walikula njama kumpindua Nyerere ndipo akawshughulikia, it will explain some of his actions that are perceived as udini.
3. Umeconclude kuwa mlengo wangu ni udini. What I know is that nnacknowledge kuwa tuna tatizo la udini, na kulisema wazi, na kuwaombeni mtakapokuwa na opportunity ya kulirekebisha mfanye hivyo pasi na kudhulumu wengine. Kwa hiyo kama mlengo huo ni udini basi sawa mie mdini. Lakini pia wale wanaofumbia macho ukweli huu, au kuenda extra step na kuzua uongo kuwadiscredit waandishi na wengine kuwasingizia wanatumiwa na wairani, sie tunapata hisia kuwa nao pia mlengo wao ni udini.
Kitabu cha Aljazeera, nampongeza kwa uzalendo na kumpa moyo, ila kwa dondoo alizozitoa hapa so far... binafsi naziona zimeelemea mno kurudia yale yale ya kuwa na biography ya Nyerere kuwa ndio historia ya uhuru. Especially pale alipoonyesha kuwa katika documents alizoziona, iliyomfurahisha zaidi ni ile iliyotoa sababu ya Nyerere kuitwa Kambarage! Kwa hiyo research yake siipigi vita .. bali natoa maoni yangu ili iwe bora zaidi na kukubalika na wengi.
Na pia sikitetei kitabu cha Mohamed Saidi kuwa ni infallible truth. The guy has a mission, and it is likely to slip along the way na kuweka chumvi za hapa na pale. Kwa hiyo tunaweza kuchukua data na kuuacha mtazamo wake.
4. Sipingi kuwa Nyerere alikuwa kiongozi na mwasisi wa Taifa, nnachopinga ni ile 'gape' au 'vacuum' inayowekwa katika jitihada zake na za wengine waliofanya kama yeye and possibly kumzidi. Kuna baadhi ya mambo huwa kidogo tunapata tabu kupata maelezo yake zaidi ya udini... kama vile mtu kuidoctor picha ya waanzilishi wa TANU ili kupunguza vikofia.
Mengineyo, Mh. Kichuguu, tunakubaliana ... au tunakubaliana kutokubaliana.