Inatokea post namba 2026.
Vionjo vya Arsis 4 Kumwokoa Msukule Unguja 4.
Tukatoka bandari tukachukua taxi nje pale, kumtajia dereva wa Taxi tunapokwenda akasema napajua, hata mimi nilikua mazikoni jana. Akatufikisha. Kijana akamlipa tukashuka.
Nyumba ilikua ya kizamni lakini kubwa na safi, inapendeza, watu wawili watatu walikua nje. Tukasalimia, tukaoneshwa baba na wajomba wa marehemu nikajitambulisha, wakasema ngoja gtukuitie mama'ko ypo ndani huko kwa kina mama, njoo huku. Nikanyayuka na mwenyeji, tukainga ukumbini, aknambia kaa nikamwite, wawaletee na chai,watu wameshakunywa chai. Yule mwenzako mliokuja nae na yeye tutamwita mje kunywa nae chai, akaingia ndani akatoka mothe na wife wangu tkasalimiana nae watu wanalia kama kawaida. Wakiona wageni, yule mwenyeji akaja, njooni njooni mnywe chai, najua mmeondoka boti ya aldajiri. Kaa hapa, akatoka kwenda kumuita kijana. Mara akarudi, hayupo hapo nje, wewe endelea tu, nikaanza kunywa chai, mama akaja tena, ngoja nikuigtia mama'ke yule binyti umsalimie. Nikamwabia usimuite mama, wacha ninywe chai baadae kidogo tutamsalimia. Mama akaondoka kurudi ndani.
Nilipomaliza kunywa chai nikatoka, nikakuta yule kijana na Jini 3 wamesimama pembeni wanaongea. Nikawafata.
MImi: Mbina mnaleta vituko tuka kwenye boti?
Kijana' Vituko gani mkuu?
Mimi; Wewe umefatwa hapa tunywe chai ukawa haupo, Jini 3 katoweka bandarini, nini kinaendelea ambacho sikijui?
Kijana: Iilibidi nionane na Jini3 anifahamishe hilo unalouliza. Kwa ufupi, mambo yote mazuri sana, baada yamuda mchache sana binti atatolewa hapa nyumbani, sisi wote tuage tunaondoka hapa mpaka baadae, lakini hatuchelewi tutarudi hakuna atakae tuona hata awe jini.
Kijana: haya twendeni tukaage.
Mimi Jini 3 twende ukasalimie na kuaga.
Jini3: Twendeni tu Mkuu, mimi mnaniona nyinyi tu hakuna anaeoniona.
Nikacheka kimoyo kimoyo, nikaona najisahu kabisa kama nafatana na majini.Moyoni najisemea hata huyu anaesema binadam ni jini tu.
Mimi nikaaa, nikawaambia natoka kidogo jamani, tutaonana baadae.
Mwenyeji; Mkumbuke chkula cha mchana hapa, kija a twebde ukanywe chai, naona ulitoka kidogo.
Kijana; Ahsante, nipo vizuri, mimim nilikunywa chai kwenye biti huyu mwenzangu alilala hajawahi kunywa. Tunatoka tutaonana baadae,
Mweneyeji: Sawa jamani, msichelewe chakula cha mchana.
Nilishi anavyosisitiza kama anatamani tusirudi kabla ya mchana.
Wala hatukwenda mbali ku[pinda kona tu, kuna kichochoro tukaingia, Jini 3 akatoa kitamba cheupe kikubwa tu, akanambia hiki vaa kilemba, wedwe mwatabiu mfunge kkilemba cha kikwenu huyu. Yule kijana akachukua kilemba akaanza kunifunga kichwani, nikahisi kimekaa sawasawa.
Kijana: Sasa na wedwe huonekanai kabisa, hata aje Jini wa wapi hakuoni,Sasa sikiliz kwa makini. Tutaingia ndani ya chumba kilichooshwa na kukafiniw mgomba, Chumba kimeshgasafishwa kisafi na binti yumo humo. Sasa hivi wataingia wale wachawi na majini yao lakini wapo chini ya ulinxi, Utachokiona utachokisikia, kaa kimya kabisa.
Mimi; Sawa.
Kijana; kamanda sfaisha njia sisi tunakufata nyuma.
Jini 3; Njia safi nyeupe haina tatio kabisa, twendeni msiwe na shaka lolote.
Tukawa tunarudi tukakuta watu wengine wameondoka wemgine waamekuja, katika waliokuja wawili nikajua haw wachawi lakini ni watu, walikua wanaongea na mwenyeji wetu. Tukaingia ndani, hapo hatuongei, zinatembea ishara tu.
Kuingia ndani tukapoita mpaka chumba walichoosha. Jini 3 akafungua mlango kama kawaida, aki-aingia akatrushiria tuingie, aktuonesha pembeni kwenye kona, tukamuona binti. Dah, binti mzuri kweli kweli, kigori wa haja kabisa, kutuona sisi akawa anatabasamu tu, nikajua anatuona.
Hatujakaa sawa, jini 3 aktuita pembeni upande mmoja, mara mlangoni wakaingia majini wawili wamevaa kama jini3 lakini wao sio warefu kama yeye, mmoja akaenda mkonoi wa kulia wa binti mmoja mkono wa kushoto, mara wakaingia watu watu watatu, mmoja mtu mmoja jini, mmoja mwanamke, kijana tu.
Mwanamke; haya jamani twendeni tukamalixane njia iko nyeupe.
Yule mchawi akaenda akamshika mkono yule binti kama anamuongoza amfate, na jini waliokuja nae yupo nyuma yao.
Mchawi: haya tangulia wewe, wewe mbona umezubaa t mlangoini hapo?
Mwanamke; hapatokeki mpaka mtoe vitu vyenu, tazama tutapita wapi hapa?
Yule mmchawi kutazama, na mimi nikaangalia mlangoni nikaona kitu kama bonge la nyuka limeuxiba mlango, pembeni yake yupo Jini 1 ndio anaongea na yule mwanamke, huku macho yake mekundi sijawahi kumuona namna ile. Hana tabasamu,hatishi kasoro macho tu.
Yule mwanamke akarudi ndani, akmwambia mchawi, nendeni nyinyi, mimi sitoki mpaka waturuhusu na wanasema mpaka mtoe vyote.
Jini 3: Nawapa nusu dakika mtoe kila kitu, lasivyo na nyinyi mtazikwa humuhumu ndani bila kuoshwa.
Jini la kichawi likajua hapa kasheshe tukichelewaa wanatuua kweli. Yule mchawi ndio alikua analeta kiburi. Jini la kichawi likamtandika kofi yule mchawi.
Jini Mchawi: Toa haraka.
Huku damu za poua zinamtoka yule mchawi akaanza kumwaga unga fulani kwenye kona chumbani.
Kijana: Wewe mbwa, futa matone yote ya damu yasionekana, tena yalambe kwa ulimi wako.
Yule mwanamke hajasita, akaanza kuyayamba, yale matone yalikua yanamtoka yule mchawi puani. alikua kiainama kila pembe, pembe ya kwanza aktoa kichupa kidogo, ya pili aktoa kitambaa cheusi kama fundo hivi, ya tattu akatoa kama mizizi midogo imefungwa pamoja, pembe ya nne akatoa chupi nyeupe, imekunjwa kunjwa nikajua ya yule mtoto wa kike.
Kijana: haya wewe mwanamke nenada nao hawa na mtoto katungoje nje mlangoni hawa tunaenda nao kutoa vigtu vingine, nyie mpeni huyo uchafu wenu abebe.
Akapewa yule mwanamke vile vitu alvyochimbua aktoka nje na wale majini wawili na jini! yupo nyuma yao wote tuaktoka nao ukumbini wakaenda mlango wa uani, wakamwaga mdawa yao yule mchawi akainama kati kati ya mlango akatoa kichupa kingine. Akaanza kwenda mlango wa mbele, nakao akatoa kichupa, akasema tumemaliza. Jini 1 akase haya twendeni hawa wamemaliza, tuwahi, tuukaondoka wote wao mbele sisi nyuma, tunakatiza mitaa nawaona viumbe wengi wanapoita oita hawana hata habari na sisi. Tukaingia nyumba moja si mbali sana na pale.
Itaendelea
Simba.